STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Arsenal yafa kwa Spurs, Man City yabanwa Itihad

Tottenham striker Harry Kane
Harry Kane aliyewaangamiza Arsenal leo
Harry Kane scores his first goal against Arsenal
Harry Kane akifunga bao la pili na la ushindi la  Spurs
Chelsea
Hazard na wachezaji wenzake wakishangilia bao la kwanza la Chelsea
Aston Villa
Jores Okore wa Aston Villa akishangilia bao la kufutia machozi la timu yake
James Milner scores Man City's equaliser against Hull
James Milner akiisawazishia Manchester CIty waliokuwa wakielekea kuzama nyumbani mbele ya Hull City leo
WAKATI Arsenal wakiduwazwa ugenini kwa kucharazwa mabao 2-1 na wapinzani wao wa jadi wa London ya Kaskazini, Tottenham Hotspur, mabingwa watetezi Manchester City imeng'ang'aniwa nyumbani  na Hull City na kutpoka sare ya 1-1, huku Chelsea ikizidi kujichimbia kileleni kwa kuilaza Asron Villa mabao 2-1.
Arsenal ikienda kwenye uwanja wa White Hart Lane wakiwa na kumbukumbu ya kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Aston Villa walitangulia kupata bao dakika ya 11 kupitia Mesut Ozil bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Wenyeji walirejea kipindi cha pili na hasira na kufanikiwa kuyarejesha mabao hayo kupitia kwa kinda linalotisha kwa sasa England, Harry Kane aliyefunga katika dakika ya 56 na 86 na kuipa ushindi muhimu Vijogoo vya London na kufikisha pointu 43 na kuingia kwenye Nne Bora wakiishusha Arsenal.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mabingwa watetezi walilazimishwa sare ya 1-1 na Hull City, huku Chelsea wakishinda mabao 2-1 ugenini dhidi ya timu isiyofunga mabao ya Aston Villa,.
Mechi nyingine Southampton ikiwa ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya QPR,  Swansea City ililazimishwa sare ya 1-1 na Sunderland, huku Leicester City ilikubali kipigo cha bao 1-0 nyumbani dhidi ya Crystal Palace.
Hivi sasa Everton na wapinzani wao wa jadi wa Merseyside, Liverpool zinajiandaa kupepetana kwenye uwanja wa Goodson Park.

No comments:

Post a Comment