STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Wenyeji Guinea ya Ikweta watozwa faini


256137B200000578-2941812-image-a-28_1423209530874
WENYEJI wa fainali za kombe la Mataifa ya Africa, Afcon 2015, Guinea ya Ikweta wametozwa faini ya dola laki moja kwa mtafaruku wa juzi usiku katika mechi ya nusu fainali dhidi ya Ghana ‘Black Stars’.
Hata hivyo CAF imesema Guinea ya Ikweta wataucheza mpambano wao wa kusaka Msindi wa Tatu dhidi ya DR Congo mchezo unaochezwa leo.
Plastic bottles and other debris litter the running track at the Malabo Stadium following the crowd disturbances
Mashabiki wa timu mwenyeji walifanya vurugu na kuwarushia chupa za maji wachezaji wa Ghana, Viongozi pamoja na mashabiki.
Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki hao, huku wachezaji wa Ghana wakitolewa uwanjani chini ya ulinzi mkali.
Vurugu hizo zilisababisha mechi kusimama kwa dakika 35, lakini Ghana walifuzu fainali kutokana na ushindi wa mabao 3-0.
Ghana wanasema katika vurugu zile watu wangeweza kufa, ingawa inaelezwa watu 14 walijeruhiwa akiwa raia wa Mali aliyeumia vibaya.

No comments:

Post a Comment