STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

BALAA TUPU LEO LIGI KUU YA ENGLAND

http://www.independent.co.uk/incoming/article9756138.ece/alternates/w620/Liverpool%20v%20Everton,%20Arsenal%20v%20Tottenham:%20The%20major%20talking%20points%20this%20weekend%20in%20the%20Premier%20League.jpghttp://news.bbcimg.co.uk/media/images/80827000/jpg/_80827370_newsplit.jpgWAKATI nahodha wa Manchester City Vincent Kompany akidai anaamini kuwa uzoefu wa sasa wa mabingwa hao unaweza kuwasaidia kukwea kileleni katika kiti walichokalia Chelsea katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, leo ni kama vita katika ligi hiyo.
Arsenal watavaana na wapinzani wa jadi wa London ya Kaskazini, Tottenham, wakati Liverpool watawafuata wapinzani wao wa jadi Everton.
City iliyopo katika nafasi ya pili leo itacheza mchezo wake wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Hull City kwenye uwanja wa Etihad ikiwa pointi tano nyuma ya vinara Chelsea, ambao watakuwa ugenini leo dhidi ya Aston Villa.
Kikosi hicho cha kocha Manuel Pellegrini kilikuwa pointi moja nyuma ya Liverpool wakati zimebaki mechi mbili kabla ya kumalizika kwa msimu uliopita lakini iliweza kutwaa taji la Ligi Kuu.
Na Man City ilikuwa pointi nane nyuma ya Manchester United wakati zimebaki mechi sita kabla hawajatwaa taji la Ligi Kuu siku ya mwisho ya msimu wa mwaka 2011/12 wakiwa chini ya kocha wazamani wa timu hiyo Roberto Mancini.
"Hii ndio hali ya kawaida kwetu, alisema Kompany beki wa kati kutoka Ubelgiji, ambaye alikuwa mchezaji muhimu wakati timu hiyo ilipotwaa taji hilo mara zote.
"Kuwa pointi tano nyuma Januari au Februari ni jambo kubwa.
"Tunajisikia vizuri kuwa katika nafasi hiyo. Tumekuwa katika nafasi hiyo mara nyingi."
Huku Man United wakitawala misimu miwili iliyopita, Chelsea waliweza kufanya mambo kama Man City kama wapinzani wakubwa katika mbio za kuwania taji.
Man United wamekuwa wakipambana tangu kuondoka kwa Alex Ferguson mwaka 2013 na sio ama mbadala wake, David Moyes na Louis van Gaal, aliweza kuiweka timu hiyo katika mbio za ubingwa.
Ukiacha tambo hizo za Kompany, ligi hiyo leo itakuwa kama vita wakati viwanja kadhaa vitakavyotimua vumbi huku gumzo likiwa mechi za watani wa miji ya London na Liverpool.
Liverpool watakuwa ugenini kuvaana na Everton, kama itakavyokuwa kwa Arsenal watakaowafuata Tottenham Hotspur uwanja wa White Hart Lane.
Ratiba kamili EPL ipo hivi wikiendi hii:
Leo Jumamosi:
Tottenham     v    Arsenal   (Saa 9:45 alasiri)
Man City  v    Hull City (Saa 12:00 jioni)
Villa     v    Chelsea   (Saa 12:00 jioni)
Swansea  v    Sunderland  (Saa 12:00 jioni)
QPR  v    Southampton (Saa 12:00 jioni)
Leicester     v    Palace (Saa 12:00 jioni)
Everton   v    Liverpool (Saa 2:30 usiku)
Kesho Jumapili:
Burnley   v    West Bromwich (Saa 9:00 alasiri) 
Newcastle v   Stoke City (Saa 11:05).
West Ham  v   Man United

No comments:

Post a Comment