STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Ancelotti awakosa Rodriguez, Ronaldo Madrid Derby

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/James+Rodriguez+Club+Atletico+de+Madrid+v+xwEg2Ahj4GDl.jpg
Ameikosa Derby ya Madrid baada ya kuumia mguu
http://www.realmadridfootballblog.com/wp-content/uploads/2013/05/1530-cristiano-ronaldo-real-madrid.jpg
Ronaldo karudi
KOCHA klabu ya ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amethibitisha kuwa James Rodriguez na Sergio Ramos watakosa mchezo wa La Liga dhidi ya mahasimu wao jiji Atletico Madrid leo Jumamosi, lakini cha kufurahisha ni kwamba nyota wake Cristiano Ronaldo atakuwepo katika mchezo huo.
Ronaldo alikosa mechi iliyopita kutokana na adhabu iliyotokana na kadi nyekundu na leoi atarejea kwenye mechi hiyo ya watani wa jadi wa jiji la Madrid litakalochezwa kwenye uwanja wa Estadio Vincente Calderon nyumbani kwa mabingwa watetezi wa La Liga, Atletico Madrid.
Ancelotti atawakosa wachezaji wake wawili Rodriguez na Ramos baada ya wawili hao walipata majeruhi katika mchezo wa majuzi wakiiitandika Sevilla kwa mabao 2-1, ambapo Ramos alipata majeruhi ya msuli wa paja huku Rodriguez akielezwa kuvunjika mguu wa  kulia baada ya kufunga bao la kuongoza.
Ancelotti sasa anakabiliwa na uhaba wa mabeki kutokana na beki wake wa kati Pepe naye kuwa nje kutokana na majeruhi ya mbavu.
Hata hivyo, Ancelotti ana matumaini chipukizi Raphael Varane na Nacho wataweza kumudu changamoto za Atletico iliyo chini Diego Simeone.
Akihojiwa Ancelotti amesema pamoja na kuwakosa mabeki wake kutegemea lakini bado ana imani na waliopo akiwemo Nacho na Varane kwamba wataweza kuhimilia mikikimikiki ya wapinzano wao hao.

No comments:

Post a Comment