STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Bayern Munich, Dortmund zazinduka Bundesliga

David Alaba scores a free-kick for Bayern Munich's second goal against Stuttgart
David Alaba akishangilia bao lake
BAADA ya kuyumba katika mechi zao mbili zilizopita za Bundesliga, Bayern Munich leo imezinduka wakiwa ugenini baada ya kuicharaza Stuttgart kwa mabao 2-0 na kujiimarisha kileleni, lichja ya wapinzani wao wa karibu Wolfsburg wakipata ushindi wa mabao 3-0 nyumbani dhidi ya Hoffenheim.
Arjen Robbin alifunga bao la kuongoza dakika ya 41 kabla ya David Alaba kuongeza la pili dakika ya 51 na kuwafanya Bayern kufikisha pointi 49 na kujichimbia kileleni.
Wapinzani wao Wolfsburg wanawapumulia Bayern baada ya kupata ushindi mnono nyumbani wa mabao 3-0 dhidi ya Hoffeinheim.
Mabingwa wa zamani wa ligi hiyo Borussia Dortmund walizinduka katika hali mbaya waliyonayo baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 ugeninmi dhidi ya Freiburg, ilhali Mainz 05 ilikubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Hertha Berlin, na timu za Fc Koln na Paderborn zilishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu na hivi sasa  Hamburger SV ipo mbele kwa mabao 2-0 dhidi ya Hannover 96.

No comments:

Post a Comment