STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Torino yashinda ugenini, Juve, Milan hapatoshi!

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Amauri+Torino+FC+v+Hellas+Verona+FC+Serie+ysKatQlJvdhl.jpgTORINO ikiwa uwanja wa ugenini hivi punde katika Ligi Kuu ya Italia, Serie A, imetoa kipigo kwa wenyeji wao Hellas Verona kwa kuikandika mabao 3-1.
Mabao ya Joseph Martinez katika dakika ya 32 , Fabio Quagliarella kwa mkwaju wa penati dakika ya 50 na bao la dakika 80 kupitia kwa El Kaddouri huku bao la kufutia machozi likifungwa na Luca Toni dakika ya 83.
Muda mchache ujao watetezi Juventus watakuwa uwanja wa nyumbani mjini Turin kuvaana na AC Milan katika pambano la kukata na shoka la ligi hiyo ya Italia.

No comments:

Post a Comment