STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 5, 2013

SAJUKI ALIVYOPUMZISHWA KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE 



 Waombolezaji wa Msiba wa Msanii wa Filamu hapa nchini Marehemu  Sadick Juma Kilowoko wakibeba jeneza lenye mwili wake tayari kwa taratibu za kwenda Mazikoni, wakitokea Nyumbani kwa Marehemu Tabata Bima.
Mwili wa Marehemu Sajuki ukipakiwa kwenye gari
Dua ikisomwa kabla ya kuondoka kwa Mwili wa Marehemu kwenda mazikoni.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania,Saimon Mwakifwamba akimpokea Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe alipokuwa akiwasili msibani hapo

Pamoja na mvua kubwa kunyesha haikuzuia watu kufika kwa aajili ya kuomboleza kifo cha Marehemu sajuki
Waombolezaji wakiwa wanajifunika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar
Mwili wa marehemu Sajuki ukiondoka nyumbani kuelekea makaburi ya Kisutu
 Sehemu ya waliohudhuria msiba wa Sajuki katika makaburi ya Kisutu 
Wadau mabali mbali wakisubiria mwili wa Marehemu Sajuki, huku Profesa Jay akionekana kwa mbali miongoni mwa wanaousubiri mwili.
Umati wa watu ukiwa makaburini Kisutu Dar
 Mwili wa marehemu Sajuki ukiwasili katika makaburi ya Kisutu tayari kwa mazishi
 Rais Kikwete pia alihudhuria mazishi ya marehemu Sajuki
 Jeneza liliobeba mwili wa marehemu Sajuki
Hili ndilo kaburi alilo zikiwa Maehemu Sajuki
 Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) likiwasili kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam mchana huu tayari kwa Mazishi yaliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo kwenye Kaburi la Marehemu Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) yaliyofanyika mchana huu kwenye Makaburi ya Kisutu,Jijini Dar es Salaam.
Msanii Z Anto akiswali juu ya kaburi la Marehemu Sajuki.
This is it! Hapa ndipo sajuki amelala! May his soul R.I.P

Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Raj'un

IMEHAMISHWA KUTOKA JESTINA GEORGE

Thursday, January 3, 2013

Thomas Mashali kuuanza mwaka dhidi ya Mkenya

 
Bondia Thomas Mashali
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini Thomas Mashali anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 12 katika ukumbi wa Friends Corner Manzese Jijini Dar es Salaam kutetea Ubingwa wa Afika  Mashariki.
 
Akiongea na waandishi wa habari Mratibu wa pambano hilo Aisha mbegu alisema mashali atapambana kuzipiga na Mkenya Bernard Mackoliech mpambano utakaokuwa wa raundi 10.
 
Alisema maandalizi yamekamilika ikiwa pia na kutumiwa tiketi kwa bondia huyo mkenya ambaye anatarajiwa kuwasili januari nane kwa ajili ya kupima uzito na kupanda ulingoni.
 
“tunataraji mpambano utakuwa mkali wa kukata na shoka ukizingatia mashali ameweka kambi kwa muda mrefu nje ya mkoa lakini pia Mackoliech ni bondia mahiri ambaye anasaka rekodi ya kwenda kucheza nje ya nchi”,alisema Aisha.
 
Alisema nafasi iko wazi kwa watu wanaotaka kudhamini ili kuhakikisha mpambano huo unafanikiwa ukizingatia ndio mpambano wa kwanza kwa mwaka 2013 na pia mashali anavutia mashabiki wengi.
 
Kwa upande wake rais wa TPBO amesema mapambano ya utangulizi yanatarajiwa kuwa manne na mabondi tayari wamesaini mikataba na watatangazwa hivi karibuni.
 
Bondia Thomas Mashali anatetea ubingwa huo wa Afrika mashariki na kati ambao aliupata baada ya kumpiga Mganda Medi Sebyala Jijini Dar es salaam mpambano uliohudhuriwa na mashabiki lukuki.
 
Mwisho.

Tangulia Sajuki, kweli wewe ulikuwa mpiganaji

Sajuki enzi za uhai wake nilipomtwanga picha nyumbani kwake Magomeni kwa Macheni


KWA kipindi cha miaka miwili mfululizo, Juma Juma Kilowoko maarufu kama Sajuki, aliweza kupigana na kupambana na maradhi yaliyokuwa yakimsumbua tangu mwaka 2010.
Pamoja na kwamba alianza kuugua tangu mwaka 2010, hakuna aliyekuwa anafahamu kutokana na kufanya usiri mkubwa akijiuguza mwenyewe na familia yake, lakini mambo yalipomzidi ndipo mapema mwaka jana alijitokeza hadharani na kuweka bayana kabla ya Mei kupelekwa India kufanyiwa upasuaji.
Tangu alipotoka India, kila aliyemuona kwa siku za karibuni aliamini amefanikiwa kuyashinda mauti, kwa vile alijichanganya na kuendelea na shughuli zake, lakini kumbe Mungu alikuwa na siri kubwa nyuma ya matukio yake kwani alimpa fursa ya kuuaga salama mwaka 2012 na kuuona mwaka mpya wa 2013 kabla ya saa chache akamchukua na kutuachia majonzi watanzania walio wengi.
Sajuki, mmoja wa waigizaji, watunzi, waongozaji na wazalishaji wa filamu nchini aliyekuwa mtu wa watu amesaliwa saa chache kabla ya kupelekwa kwenye makazi yake ya milele katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar er Salaam baada ya kuaga dunia jana asubuhi hospitalini Muhimbili.
Binafsi nilipata taarifa hizo nikiwa nyumbani kwangu, KImara King'ongo nikijiuguza Malaria na mafua makali yaliyonishika tangu Desemba 31 mwaka jana.
Nilishtuka kwa vile zilikuja ghafla mno, japo nilikuwa nafahamu Sajuki, alikuwa kalazwa Muhimbili baada ya kuzidiwa alipokuwa kwenye ziara ya kuwashukuru Watanzania na kuchangisha fedha za kupelekwa tena India jijini Arusha.
Sikuwa na kitu kingine cha kusema zaidi ya Alhamdulillah kulingana na mafundisho ya dini yetu na kumalizia kwa Innalillah Wainaillah Rajiun, kama Mtume Muhammad SAW aliyotuelekeza kila tunapokumbwa na Msiba tuseme hivyo kwa maana kwamba 'Sisi ni waja wa Mwenyezi Mungu na kwake hakika tutarejea'.
Pamoja na kwamba Sajuki ametutoka tungali tukimuhitaji katika fani yake na namna alivyokuwa akionyesha anavyothamini kazi kuliko hata afya yake, lakini Mungu ana mapenzi zaidi na tunapaswa kumshukuru.
Namkumbuka Sajuki, aliyenidokeza jina hilo lilitokana na muunganiko wa majina ya kaka yake aitwae Salum na lake la Juma na lile la ukoo yaani Kilowoko na kuzaa SAJUKI, kwa ucheshi, utani na kujiamini kupita kiasi alikojaliwa na maanani.
Mara ya kwanza kukutana naye nakumbuka ilikuwa mwaka 2009 nyumbani kwake Magomeni Mapipa nilipoenda kufanya mahojiano naye ambapo aliweza kuweka bayana ndoto aliyokuwa nayo tangu utotoni ya kuja kuwa muigizaji mchekeshaji kama Amri Athuman maarufu kama King Majuto.
"Nilitamani sana kuwa mchekeshaji kama King Majuto, lakini filamu za Sylvester Stallone 'Rambo' na ubabe wake zilibadilisha upepo na kujikuta kwenye filamu za kawaida na hasa zile za mapugano na ubabe," aliniambia nilipozungumza naye huku jirani yake akiwepo Soud Ally maarufu kama Chomba au Akuhi.
Sajuki, ambaye majina yake kamili ni Juma Juma Issa Kilowoko, alisema hamu yake ya kufika mbali katika sanaa ya uigizaji ndiyo iliyomfanya apite kundi moja hadi jingine hadi kuangukia Kaole Sanaa, lililomtangaza vema kupitia michezo iliyokuwa ikirushwa na kituo cha runinga cha ITV.
Alisema mchezo wake wa kwanza ndani ya kundi hilo lililotoa nyota kibao wa filamu nchini ni Baragumu wa mwaka 2005 na kufuatia na michezo mingine hadi mwaka 2008 alipojitoa kundini na kujikita zaidi katika filamu, kazi yake ya kwanza ikiwa ni Revenge.
"Baada ya kupita makundi kadhaa tangu nikiwa mjini Songea nilipozaliwa, hatimaye nilitua Kaole Sanaa, lililoniivisha kabla ya kuachana nao kusaka masilahi zaidi na kujikita katika filamu," alisema.
Mbali na Revenge filamu zingine alizocheza Sajuki ni pamoja na Dhambi, Mboni Yangu, Two Brothers, Behind the Scene, Round, Shetani wa Pesa, Hero of the Church na nyinginezo.
Wakati nilipokuwa nazungumza naye alikuwa akijiandaa kutoa filamu mbili binafsi za Vita na Briefcase zilizowashirikisha nyota kadhaa nchini akiwemo mshindi wa pili wa BBA, Mwisho Mwampamba.
Sajuki alisema fani ya filamu imemnufaisha kwa mambo mengi ikiwemo kimaisha, lakini kubwa ni kufanikiwa kumuoa mke mrembo na muigizaji mwenzake, Wastara Issa Juma 'Stara'.
"Kufanikiwa kumpata Wastara na kumuoa kwangu ni jambo kubwa na la kuvutia mno kati ya mafanikio kibao niliyoyapata katika fani hii ya filamu nchini," alisema.
Mkali huyo, aliyekuwa akipenda kucheza na watoto na shabiki wa muziki wa 'Quito', alisema kama kuna kitu kinachomkera katika sanaa hiyo ni tabia za 'Wauza Sura' wanaojiingiza kwenye skendo chafu zinazowachafua wasanii wote wa tasnia hiyo mbele ya jamii.
Alisema wasanii wenye kusaka umaarufu kwa lazima wanamnyima raha kwa vile jamii inadhani wasanii wote wana silka na tabia kama za wauza sura hao wanaojirahisi na kujidhalilisha.
Kuhusu rushwa ya ngono, Sajuki mtoto wa nne kati ya watano wa Mzee Juma Issa Kilowoko, alisema wanaojihusisha nao wanafanya hivyo kwa kujitakia kwa sababu hakuna anayelazimishwa kutoa mwili wake iwapo ana uwezo na kipaji kikubwa katika sanaa hiyo.
"Rushwa ya ngono kwa watoto wakike ni kujitakia kwa vile wana akili na ufahamu wa kujua athari za kufanya hivyo na watayarishaji wanaolazimisha hawafai na wanapaswa kuchukuliwa hatua kali za kisheria," alisema Sajuki.
Sajuki, alinidokeza kuwa hakuna kitu kilichomtia simanzi na kumsikitisha kama tukio la ajali ya pikipiki iliyompata akiwa na mkewe, Wastara Juma enzi wakiwa wachumba.
Nyota huyo ambaye ameacha mjane na mtoto mmoja wa kike, aliishukuru familia yake na Vincent Kigosi 'Ray' kwa kumfikisha alipokuwapo alisema ajali hiyo sio inayomuuma, ila kitendo cha kulazimika kuidhinisha fomu hospitalini ili Wastara akatwe mguu wake uliokuwa umeharibika kwa ajali hiyo.
"Kwa kweli kile kitendo cha kuidhinisha kukatwa kwa mguu kwa Wastara kinaniuma hadi leo, lakini sikuwa na jinsi ila kufanya hivyo ili kumuokoa," Sajuki aliniambia kwa masikitiko katika mahojiano hayo.
Hata hivyo alidai alikuwa akijisikia fahari mno kuoana na kisura huyo ambaye kwa sasa anao mguu wa bandia, kwa vile wamesaidiana kuanzisha kampuni yao binafsi ya Wajey Films Production.
Sajuki alizaliwa miaka 27 iliyopita huko Songea na kusoma hadi elimu ya sekondari katika shule za Songea na Luwiko, alikoanza kuonyesha kipaji chake cha sanaa katika matamasha mbalimbali ya shule kabla ya kujitosa kwenye makundi.
Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu Sajuki anayezikwa kesho katia makaburi ya Kisutu.


Mwisho

Kado azivuruga Yanga, Mtibwa

Kado akitambulishwa na viongozi wa Coastal Union hivi karibuni

KLABU za Yanga na Mtibwa Sugar zimeendelea kuzozana kuhusiana na mchezaji Shaaban Kado baada ya kipa huyo kusaini mkataba wa kuichezea Coastal  Union ya Tanga kwa mwaka mmoja.
Kipa huyo ambaye aliichezea Mtibwa kwa mkopo katika mzunguko wa kwanza wa msimu akitokea Yanga, amekuwa chanzo cha malumbano baina ya klabu hizo; ambapo ‘Wanajangwani’ wanadai kuwa wana haki ya kumuuza kokote kwavile ni mchezaji wao halali huku ‘wakata miwa’ wa Mtibwa wakisisitiza kuwa anapaswa kuendelea kubaki kwao kwavile walimtwaa kwa mkataba wa kuichezea hadi mwisho wa msimu.
Hata hivyo, akizungumza jana, Kado alisema kuwa tayari ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Coastal iliyowahi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mwaka 1988.
“Ni kweli nimesaini mkataba wa mwaka mmoja katika klabu ya Coastal… na nimeshaanza kufanya nao mazoezi,” alisema Kado.
Akieleza zaidi, kipa huyo alisema: “Kulikuwa na mvutano kati ya Yanga na Mtibwa juu yangu, lakini kila kitu kuhusiana na hilo nimewaachia wao. Naamini watamalizana,” alisema Kado.
Mratibu wa Mtibwa, Jamal Bayser, alisema jana kuwa wameshangazwa na kitendo cha Yanga kumuuza mchezaji huyo il-hali walikubaliana kuichezea timu yao (Mtibwa) hadi mwishoni mwa msimu huu wa ligi kuu ya Tanzania Bara.
Bayser alisema kuwa tayari klabu yake imewasilisha malalamiko katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusiana na suala la kipa huyo ambaye aliwahi kuichezea Mtibwa kabla ya kuuzwa Yanga na baadaye kurejea tena klabuni hapo kwa mkopo.
“Inashangaza sana kuona klabu zinasajili wachezaji kinyume na utaratibu. Kulingana na makubaliano yetu na Yanga, Kado anatakiwa kuitumikia Mtibwa hadi mwishoni mwa msimu huu,” alisema Bayser.
“Tumeshaandika barua TFF, maana tulikubaliana na na Yanga, tena tukaweka mkataba kimaandishi. Sasa tunasubiri TFF watoe maamuzi,” aliongeza mratibu huyo.
Alipotafutwa na gazeti hili jana kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema kuwa kwa sasa hawana muda wa kuzungumzia suala hilo kwavile Kado si mali yao tena kwa sasa.
“Kado ni mali ya Coastal Union kwa sasa, siwezi kuzungumzia suala la mchezaji huyo maana siyo mali yetu tena (Yanga),” alisema Mwalusako.
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kuwa sakata la mchezaji huyo limepelekwa kwenye Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF ili lipatiwe ufumbuzi.


Chanzo:NIPASHE

Golden Bush Veterani, Wahenga Fc kurudiana Januari 12

Kikosi cha Golden Bush Veterani ambacho kinatarajiwa kurudiana na Wahenga Fc Januari 12

BAADA ya kukaribisha mwaka kwa kipigo cha aibu cha mabao 4-3 kutoka kwa wapinzani wao, timu ya soka ya Golden Bush Veterani, imekata rufaa na sasa watarudiana na wapinzani wao Wahenga Fc Januari 12.
Tayari pande zote zimekuwa zikitoleana tambo mbalimbali Wahenga wakisisitiza kuwa waliamua kutoa zawadi ya mwaka mpya kwa watani zao kwa kuwapa kipigo hicho, huku Golden Bush kikisisitiza kuwa waliotewa na kwamba mechi hiyo ya kisasi wataifumua Wahenga mabao 7-0.
Golden Bush tayari kimeweka hadhaarani kikosi kitakachoshuka dimbani siku ya mechi hiyo ambapo golini atakuwepo Hamza, kipa wa timu yao ya vijana huku kulia atasimama Chidi Rasta, kushoto Abuu Ntiro, Mmalawi Wisdom Ndhlovu atacheza kama beki namba nne na mkoba atakuwa Majaliwa.
Kiungo nama sita atacheza Yahya Issa, wingi ya kulia atasimama mlezi wao, Onesmo Wazir 'Ticotico' na Katina Shija atazungusha dimba la juu, Herry Morris atacheza kama mshambuliaji wa kati na Kapeta atacheza namba 10 na Said Swedi Panucci atacheza wingi ya kushoto.
Pamoja na Golden Bush kujinasibu kushinda mchezo huo wa marudiano, Wahenga wamekejeli wakieleza kuwa wao hawana hofu yoyote kwa sababu soka wanalijua japo wachezaji wao hawana majina makubwa kama ya wapinzani wao ambao katika mechi zao mbili za awali walitoka sare ya 1-1 na kisha kuwanyuka mabao 4-2 kabla ya kuwazima wiki mwishoni mwa wiki kwa mabao hayop 4-3 mechi zote zikichezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Dar es Salaam.

Je, nani atakayeiobuka na ushindi? Tusubiri kuona hiyo Januari 12.

HALI HALISI ILIVYO NYUMBANI KWA MAREHEMU SAJUKI


Mke wa marehemu, Juma Kilowoko 'Sajuki', Wastara Juma (aliyejifunika nguo) akiwa na simanzi nzito kwa kumpoteza mumewe.
Mzee Kilowoko ambaye ni baba mzazi  wa marehemu 'Sajuki' akiwasiliana na ndugu na jamaa msibani hapo.
Mama  mzazi  wa marehemu Sajuki (wa kwanza kushoto) akiwa na majonzi.
Dada wa Wastara aitwaye Marian (aliyesujudu) akilia kwa uchungu.
 
Bibi wa marehemu Sajuki akiwasili msibani.
Pichani juu ni baadhi ya taswira za waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Juma Kilowoko 'Sajuki', Tabata- Bima jijini Dar es Salaam. Sajuki amefariki dunia jana asubuhi akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo alikuwa akitibiwa.
(PICHA NA HAMIDA HASSAN / GPL)

Chelsea hoi wa QPR, Liverpool yazidi kupeta

Wachezaji wa QPR wakimpongeza Shaun Wright Phillips aliyefunga bao pekee lililoiangusha Chelsea jana usiku.

WAKATI Liverpool ikiendeleza wimbi la ushindi kwa kuisambatarisha timu ya Sunderland kwa mabao 3-0, Chelsea walijikuta wakiteleza nyumbani kwao uwanja wa Stanford Bridge kwa kudunguliwa bao 1-0 na 'vibonde' wa Ligi Kuu ya England, QPR inayonolewa na kocha Harry Redknapp.
Chelsea ilikumbana na kipigo hicho kutokana na bao la nyota wake wa zamani Shaun Wright-Phillips aliyefunga katika dakika ya 78 kutokana na kazi nzuri ya Mmorocco Adel Taarabt.
Kipigo hicho kimeiacha Chalsea kwenye nafasi ya nne ikiwa na pointi 38 ikishindwa kuipiku Tottenham waliowazidi pointi moja wanaokamata nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City na Manchester United.
Liverpool wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumba waliinyoa Sunderland kwa mabao 3-0, mabao wawili yakitupiwa kambani na Luis Suarez, huku bao la awali likifungwa na Raheem Sterling akimalizia kazi ya Suarez.
Katika mechi nyingine ya mfululizo wa ligi hiyo Newcastle United imeendeleza wimbi la vipigo kwa kulala nyumbani kwao mabao 2-1 toka kwa Everton.

SAJUKI  KUZIKWA KESHO MAKABURI YA KISUTU

Sajuki akichapa mzigo enzi za uhai wake
Sajuki na mkewe Wastara enzi za uhai wake
Baba yake Sajuki... Mzee Kilowoko akiwasiliana na ndugu na jamaa kwa simu wakati akiwa kwenye msiba wa mwanawe, Tabata jijini Dar es Salaam jana. Familia imeamua Sajuki azikwe makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam kesho Ijumaa.

Wasanii wa vichekesho, Mtanga (kushoto) na Kiwewe (aliyejishika goti) wakiwa na waombolezaji wengine katika msiba wa Sajuk.

Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Sajuki
Tutakukumbuka milele Sajuki... msanii nyota wa filamu za Kibongo, Suzan Lewis 'Natasha' akiwa kwenye msiba wa Sajuki mapema leo kushiriki maandalizi ya shughuli za mazishi, eneo la Tabata jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya waombolezaji wa msiba wa Sajuki waliofika mapema Tabta

Piga pale...! Sajuki (kulia) akiwa katika maandalizi ya filamu yake ya Vita wakati wa enzi za uhai wake.


Waombolezaji wakiwa na majozni tele katika msiba wa Sajuki, Tabata jijini Dar es Salaam.
HATIMAYE ule utata kuhusiana na mahala pa kumzika msanii Juma Kilowoko 'Sajuki' umepatiwa jibu baada ya baba yake kukubali kuwa azikwe jijini Dar es Salaam.

Kutokana na uamuzi huo, sasa msanii huyo aliyekuwa nyota na kipenzi cha wengi enzi za uhai wake atazikwa kesho 
saa 7:00 mchana baada ya swala ya Ijumaa kwenye makaburi ya Kisutu.

Awali, baba wa msanii huyo alitaka mwanawe akazikwe kwao mkoani Songea. Hata hivyo, baada ya kuketi na kujadili kwa kina na familia yake, akaamua kutangaza kuwa mwanawe huyo kipenzi atazikwa jijini Dar es Salaam ili kutoa nafasi kwa rafiki zake wengi aliokuwa akishirikiana nao katika kazi zake za kila siku za kisanii kupata nafasi ya kushiriki mazishi yake.

Mzee Kilowoko ametoa msimamo huo mpya leo hoo hii, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kutangaza awali kuwa mwanawe atakwenda kuzikwa Songea.

Sajuki amefariki leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa katika wodi ya wagonjwa mahututi na kupumua kwa msaada wa mashine kabla ya kuaga dunia mishale ya saa 1:00 asubuhi.



Mashabiki wa filamu za Kibongo nchini watamkumbuka marehemu kwa filamu zake kama 'Round', 'Shetani wa Pesa', 'Hero of the Church', 'Vita' na 'Briefcase, 'Revenge', 'Dhambi', 'Mboni Yangu', 'Two Brothers', na'Behind the Scene'.
Sajuki alizaliwa mwaka 1986 Songea mkoani Ruvuma, ameacha mke na mtoto mmoja.

Tuesday, January 1, 2013

KABURU, WENZAKE WAHOJIWA UPORAJI FEDHA ZA SIMBA

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu'

MAKAMU Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ na katibu mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala ni miongoni mwa watu waliohojiwa na Jeshi la Polisi jana kusaidia uchunguzi mkali kuhusiana na ujambazi uliosababaisha kuporwa kwa Sh. milioni 10.59 za klabu hiyo zilizotokana na mgawo walioupata katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Tusker ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi.
Akizungumza na jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, alisema kuwa wameshawahoji Kaburu, Mtawala na watu wengine kadhaa ili kupata maelezo muhimu yatakayosaidia kupatikana kwa ukweli kuhusiana na kilichotokea.
"Tumewahoji viongozi hao wawili wa Simba (Kaburu na Mtawala) ili kujua taratibu za uhifadhi na utunzwaji wa fedha na mali za klabu yao... maana inastusha kusikia mtu mmoja anakwenda nyumbani kwake na mali ya klabu, tena buila ulinzi wowote ule," alisema Kenyela.
"Tumeamua pia kuwahoji ili kujua hasa ni nini kilichotokea kuanzia Uwanja wa Taifa maana tulibaini kuwa wao (Kaburu na Mtawala) ndiyo waliosaini na kupokea mgawo wa Simba kule uwanjani (Taifa),"  aliongeza.
Kataka hatua nyingine, Kenyela alisema kuwa Mhasibu wa Klabu hiyo, Erick Sekiete na watu wengine wawili, Said Pamba na Stanley Phillipo (23) waliokuwa wakishikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo waliachiwa kwa dhamana jana.
Sekiete na wenzake hao, walivamiwa wakati wakiwa katika eneo la Sinza kwa Remmy baada ya kuteremka katika gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T869 BKS iliyokuwa ikiendeshwa na Pamba.
Katika tukio hilo, ilidaiwa kuwa Sh. milioni 7.59 na dola za Marekani 2,000 (Sh. milioni tatu) zilizotokana na mgawo wa klabu hiyo katika mechi yao dhidi ya Tusker FC ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ziliporwa baada ya Sekiete (28) kuvamiwa na majambazi sita katika eneo la  Sinza kwa Remmy jijini Dar es Salaam ambapo risasi kadhaa zilipigwa hewani. Tukio hilo lilitokea saa 3:20 usiku.
Kamanda Kenyela alieleza kuwa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alimdhamini Sekiete huku Phillipo akidhaminiwa na ndugu yake aitwaye Julius Kiwale.
Kamanda Kenyela alisema kuwa Pamba, ambaye alikuwa dereva wa gari lililowabeba Sekiete na Phillipo, alidhaminiwa na Kasim Pamba.
“Wanatakiwa waripoti katika Kituo cha Polisi Magomeni Jumatano (kesho),” aliongeza Kenyela.


Chanzo;NIPASHE
----------

KALA JEREMIAH KUTOKA NA ALBUM YAKE MPYA


Baada ya kufanya vizuri katika baadhi ya redio na televisheni kwa ngoma yake ya Dear GodKala Jeremiah sasa ameweka wazi kwamba siku ya tarehe 20 mwezi huu anatarajia kutoka na album yake mpya inayokwenda kwa jina la Pasaka.

GOlden Bush yaaga mwaka 2012 kwa aibu yanyukwa na Wahenga

LICHA ya kuwatumia nyota wa zamani wa klabu kubwa za soka nchini za Simba, Yanga na Mtibwa, timu ya soka ya Golden Bush Veterani jana uliuaga mwaka 2012 na kuukaribisha kinyonge mwaka 2013 baada ya kutandikwa mabao 4-3 na wapinzani wao wakubwa, Wahenga Fc katika pambano maalum la kirafiki.
Pambano la timu hizo lilifanyika jana jioni kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Dar es Salaam ambapo Golden Bush, ilijikuta ikipelekwa puta na Wahenga iliyokuwa aikiongozwa na kipa wa zamani wa Yanga na Mtibwa, Mengi Matunda.
Japo Golden Bush, iliyowatumia nyota kama Yahya Issa, Athuman Machuppa, Abuu Ntiro, Waziri Mahadhi, Said Swedi na nduguye Salum Swedi 'Kussi', Nico Nyagawa, Heri Morris, Katina Shija na wengineo iliweza kuongoza kwa mabao 2-1 hadi wakati wa mapumziko, lakini ilishindwa kuepuka kipigio katika mchezo huo.
Golden Bush ilianza kujipatia bao la kuongoza katika dakika ya 18 baada ya Heri Morris kufumua shuti kali lililomshinda kipa wa Wahenga, David 'Seaman' kabla ya Said Swedi kuifungia timu hiyo bao la pili kwa kichwa akiuynganisha krosi pasi ya Nico Nyagawa.
Hata hivyo katika dakika ya 31 Wahenga walipata bao lao la kwanza kupitia kwa mchezaji wao aitwae God aliyeusukumia mpira wavuni kwa shuti karibu na lango lwa Golden Bush.
Kipindi cha pili kilishuhudiwa kwa Golden Bush ikifanya mabadiliko makubwa katika kikosi chao ikiwamo kumtoa Onesmo Waziri 'Ticotico' aliyekuwa akisumbua mbele licha ya kucheza akiwa majeruhi, lakini mabadiliko hayo hayakuwasaidia baada ya Wahenga kutumbukiza wavuni bao la kusawazisha katika dakika ya 65 kupitia Frank 'Super Et'oo'.
Wakati Golden Bush wakitafarakari jinsi walivyofungwa bao hilo, Wahenga walipata bao jingine la tatu lililofungwa kwa njia ya penati na kipa David Seaman katika dakika ya 78 baada ya mmoja wa wachezaji wa timu hiyo kuchezewa rafu ndani ya lango la Golden Bush.
Jahazi la Golden Bush lilizidi kuzama katika dakika ya 82 wakati Wahenga walipojipatia bao lao la nne lililofungwa na beki aliyepanda mbele kusaidia mashambulizi Shomar aliyewatoroka mabeki wa Golden Bush ambao katika mechi ya jana walionekana kuyumba kusiko kawaida.
Hata hivyo zikiwa zimesalia dakika nne, Golden Bush ilijipatia bao lao tatu la kujifutia machozi, lililofungwa kwa ,mpira wa adhabu ndogo na Salum Swedi 'Kussi' baada ya Machota kuchezewa vibaya na mabeki wa Wahenga nje ya eneo la hatari.
Mara baada ya pambano hilo, Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema wamekikuibali kipigo cha wapinzani wao, licha ya kwamba alimtupia lawama mwamuzi wa pambano hilo, Ally Mayay kwamba 'aliwauma' na kuahidi kuomba pambano la marudiano na wapinzani wao hao ili kukata mzizi wa fitina.
"TUmekubali kipigo, lakini tutaomba mechi ya marudiano, tunaamini leo tumefungwa kwa sababu mwamuzi alikuwa 'wao', hatuamini kama hawa jamaa wana uwezo wa kuwafunga wakati hivi karibuni tuliwanyuka mabao 4-2 baada ya awali kutokana nao sare ya 1-1," alisema Ticotico.
Hata hivyo baadhi ya watazamaji wa mchezio huo wakieleza kipigo walichopewa Golden Bush kilikuwa halali kutokana na kuzidiwa ujanja na Wahenga, huku wakiwapoingeza walioandaa pambano hilo kwa kuwapa burudani ya kuagia mwaka na kuwashuhudia nyota waliotamba zamani katika klabu mbalimbali nchini ambao walikuwa hawajui wapo wapi kwa sasa baada ya kutoweka kwenye ligi kuu.

NYota wa zamani wa soka wataka 2013 uwe wa mapinduzi katika kandanda

Mecky Mexime


NYOTA wa zamani wa soka nchini wamewataka wadau wa mchezo huo kujipanga ili kuhakikisha mwaka 2013 unakuwa wenye tija na mafanikio kwa mchezo wa kandanda baada ya mwaka uliopita wa 2012 kutokuwa na cha kujivunia.
Wakizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa pambano maalum la kuuaga 2012 na kuukaribisha 2013 wachezaji hao wakiongozwa na nahodha wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mecky Mexime, walisema mwaka uliopita ujlikuwa na matukio ya kuumiza katika soka kwa timu za Tanzania kushindwa kung'ara.
Hivyo wakataka mwaka 2013 uwe wa mapinduzi ili Tanzania iweze kurejesha makali yake ya miaka ya nyuma ilipotikisa soka la Afrika.
"Awali ya yote tunashukuru kuweza kukutana wachezaji wa zamani ambao tulipoteana kitambo, lakini kubwa ni kutaka kuona mwaka 2013 unakuwa wa mapinduzi katika soka ili Tanznaia itambe kimataifa," alisema Mexime ambaye kwa sasa ni kocha wa timu ya Mtibwa Sugar.


Katina Shija

Madaraka Seleman
Wengine waliotoa  maoni yao kutaka mwaka 2013 uwe na mabadiliko katika michezo hususani soka ni Yahya Issa, Nico Nyagawa, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio', Katina Shija, Wazir Mahadhi, Zubeir Katwila, kipa Steven Marashi, Onesmo Waziri 'Ticotico', Abuu Ntiro na wengine ambao walikuwa wakiichezea timu ya Golden Bush Veterani waliokuwa wakiumana na Wahenga Fc na kukubali kipigio cha aibu cha mabao 4-3.

KOCHA MFARANSA ATUA SIMBA AAHIDI MAKUBWA

Kocha wa Simba, Mfaransa Liewig akizungumza na waandishi baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana
HATIMAYE kocha mpya wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig ametua nchini  na kuahidi kuiletea mafanikio makubwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Liewig aliyekuja kutwaa nafasi iliyoachwa wazi na Mserbia Milovan Cirkovic, amesema 'Wanamsimbazi' watarajie mambo mazuri kutoka kwake, lakini kwa sharti la kumpa ushirikiano katika kila hatua wakati atakaposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo na kuanza kibarua chake.
"Nimefurahishwa sana na mapokezi haya... najihisi kuwa nina deni kubwa. Naamini nitapata ushirikiano wa kutosha na baada ya kuzoeana na wachezaji, naamini Simba itafika mbali katika kila michuano," alisema kocha huyo.
Miongoni mwa watu waliofika uwanjani kumpokea kocha huyo ni Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, ambaye aliwaongoza mamia ya mashabiki wa Simba kumpokea kwa maandamano ya magari na pikipiki za bodaboda na bajaji.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza kuwa kocha huyo atasaini mkataba wa kuifundisha klabu hiyo kwa miezi 18 na tukio hilo litakamilishwa leo asubuhi.