STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 16, 2013

Baby Madaha kupasua anga la kimataifa


NYOTA wa filamu ambaye pia ni mwanamitindo na muimbaji wa muziki wa kizazi kipya nchini, Baby Madaha anatarajiwa kufanya ziara ya maonyesho katika nchi nne tofauti za Afrika.
Ziara hiyo itakayoanza mapema mwezi ujao na itakayochukua muda wa mwezi mzima itamshirikisha msanii huyo na wakali wengine ambao watapangwa katika ratiba hiyo kutoka nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, Madaha alisema ziara hiyo itahusisha nchi za DR Congo, Zimbabwe, Angola na Msumbiji na itaratibiwa na 'super market' moja kubwa nchini inayomilikiwa na Jumanne Kishimba.
"Kaka yangu natarajia kufanya ziara ndefu ya kujitangaza kimataifa nje ya nchi ambayo itakuwa ya maonyesho ya muziki na filamu katika nchi nne za Afrika, ziara itakayochukua muda wa zaidi ya wiki tatu," alisema Baby Madaha.
Mkali huyo alisema katika ziara hiyo mratibu mkuu atakuwa muigizaji mwingine nchini Mariam Mndeme 'Mamuu'.
Alisema kwa sasa anaendelea na maonyesho ya ndani ambapo wiki hii anatarajiwa kuwa jijini Mwanza kabla ya kuanza maandalizi ya safari hiyo ambayo amedai itamsaidia kujitangaza na kuitangaza Tanzania kimuziki na filamu nje ya mipaka.
"Kwa sasa naelekea Mwanza kwa ajili ya maonyesho kadhaa kabla ya kujiandaa na safari hiyo," alisema Baby aliyeibuliwa na shindano la Bongo Star Search (BSS) la mwaka 2008.

Golden Bush Veterani yaitafuna Moro Veterani x3

Kikosi cha Golden Bush Veterani

MABAO mawili kutoka kwa Athuman Machuppa na moja la Abuu Ntiro jumamosi yalitosha kuipa ushindi wakali wa soka la maveterani jijini Dar, Golden Bush Veterani kuitambia Morogoro Veterani nyumbani kwao kwa kucharaza mabao 3-1 katika pambano la kirafiki lililochezwa kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Kwa mujibu wa msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema katika pambano lao walionyesha kiwango kikubwa kama kawaida yao na kuwapeleka puta wapinzani wao na kuibuka na ushindi huo wa mabao 3-1, ikiwa wanajiandaa kuvaana na wapinzani wao Wahenga.
Timu hizo mbili 'mahasimu' zilipokutana mara ya mwisho hivi karibuni kwenye uwanja wa Kinesi na Wahenga kulala mabao 2-1, huku wachezaji na aliyekuwa mgeni rasmi Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye wakinyeshewa na mvua iliyonyesha siku hiyo.
Pambano la safari hii kwa wapinzani hao wa jadi linatarajiwa kuchezwa siku ya maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wa Tanzania, ambapo tayari pande hizo mbili zimeshaanza kutambiana kila moja ikitamba kuibuka na ushindi ili kulinda heshima kwa wenzake.

Coastal Union, kuvuna nini leo kwa JKT Ruvu Mkwakwani?


Kikosi cha Coastal Union watakaoikaribisha JKT Ruvu
MICHUANO ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayoelekea ukingoni, inatarajiwa kuendelea leo kwa pambano moja la kukata na shoka kati ya Coastal Union ya Tanga dhidi ya wageni wao maafande wa JKT Ruvu ya Pwani.
Pambano hilo litachezwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Mkwakwani-Tanga, ambapo kila timu itakuwa ikihitaji ushindi ili kufikia malengo tofauti waliyonayo, Coastal ikiwania kuingia kwenye Tatu Bora na JKT kujinasua toka kwenye mstari wa hatari wa kushuka daraja.
Coastal ambayo katika mechi yake ya mwisho ilikumbana na kipigo cha kushtukiza toka kwa wanaoburuza mkia, African Lyon, ina pointi 32 na ushindi katika pambano la leo itawafanya wakwee nafasi moja hadi ya tano na kuiengua Mtibwa Sugar itakayoshuka dimbani kesho.
Hata hivyo maafande wa JKT ambo wamekuwa na msimu mbaya safari hii, wanapigana kuondoka katika janga la kuteremka daraja kutokana na ukweli mpaka sasa ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 22 tu sawa na Toto African, wakizizidi pointi mbili timu zilizozopo mkiani Lyon na Polisi Moro ambazo zina pointi 19 kila moja.
Kwa mazingira ilizonazo timu hizo ni wazi pambano la leo litakuwa gumu na lenye ushindani mkubwa ikizingatiwa kuwa, mashabiki wa Coastal wamekosa furha kitambo na timu yao kiasi cha kupost maoni yenye kukera dhidi ya uongozi na wachezaji wao.
Ligi hito inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa michezo kadhaa likiwamo pambano la Yanga dhidi ya JKT Mgambo ambao kupitia kocha wao mkuu, Mohammed Kampira wameapa kuwazuia vinara wa ligi hiyo wasiwafanye daraja la kutwaa ubingwa msimu huu.
Yanga inaoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 52 na inahitaji pointi sita tu kutawazwa mabingwa wapya baada ya waliokuwa wakilishikilia Simba kutemeshwa mapema wakati ligi ikiwa bado inaendelea kwa vile itawafanya wafikishe pointi 58 ambazo hazitaweza kufikiwa na Azam wanashika nafasi ya pili ambao wakishinda mechi zake nne tatu zilizosalia itafikisha pointi 56 tu.
Mechi zitakazopigwa kesho kwa mujibu wa ratian ya ligi hiyo ni kama ifuatavyo;
Mgambo JKT vs Yanga,
Kagera Sugar v Toto Africans (japo Toto imetishia kutoicheza mechi hiyo ya leo, ikihofia upangaji matokeo)
Mtibwa Sugar v JKT Oljoro

Hatari!

  Fedha za serikali zabebwa bila ulinzi TFF
  Ni mamilioni yatokanayo na makato U/Taifa
 
Viongozi wakuu wa TFF, Rais Leodger Tenga (kulia) na Angetile Osiah (kushoto)
 
WIZARA inayoshughulikia michezo nchini imekuwa ikifanya kitendo hatari cha kutuma maafisa wake kwenda kubeba mamilioni ya fedha zitokanazo na mgawo wake utokanao na makato ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam bila ya ulinzi wowote ule kama taratibu za usafirisha fedha zinavyoelekeza, imefahamika.
 
Aidha, malipo ya mamilioni hayo ya fedha za serikali kutoka katika ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) hufanywa kwa fedha taslim na wala siyo kwa njia nyingine salama kama ya hundi, huku anayehusika kuzibeba ni afisa mmoja tu ambaye ni wazi kwamba anahatarisha usalama wake binafsi na pia wa fedha za umma.
 
Uchunguzi uliofanywa kwa siku kadhaa na NIPASHE umebaini kuwa utaratibu huo unaopingana pia kwa kiasi kikubwa na taratibu za malipo ya fedha za umma umekuwa ukifanyika kwa muda mrefu, hata kabla ya kuanza kutumika kwa Uwanja wa Taifa.
 
 
MAMILIONI YANGA v OLJORO
Juzi (Jumapili), mwandishi alishuhudia mmoja wa maafisa wa Wizara ya Michezo akifika katika ofisi za TFF na kubeba kienyeji (bila ya kusindikizwa na askari yeyote mwenye silaha) kiasi cha Sh. 7,552,500 zilizotokana na asilimia 15 ya uwanja katika mapato ya mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Yanga na Oljoro JKT iliyochezwa Jumamosi na kuingiza Sh. milioni 63.17.
 
Afisa huyo alionekana akitinga kwenye ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam saa 4:38 asubuhi, akiwa peke yake kwenye gari aina ya Suzuki Vitara (namba tunazihifadhi) na kuondoka peke yake pia kwenye gari hilo mishale ya saa 5:22 asubuhi.
 
Kibaya zaidi, afisa huyo aliyekuwa amevaa shati la mikono mifupi lenye rangi nyeupe, kaptula yenye mifuko mingi na viatu vya raba vyenye mchanganyiko wa rangi nyeupe na nyeusi, hakuwa na ulinzi wowote wakati akiingia na kutoka kwenye ofisi ya fedha ya TFF.
 
"Ofisi imefunguliwa leo Jumapili kwa sababu kuna mechi ya Simba dhidi ya Azam. Ni kweli afisa wa wizara amechukua fedha za mgawo wa uwanja. Mtafute afisa habari (Boniface Wambura) au katibu mkuu (Angetile Osiah)... wao wanaweza kuzungumzia kwa kina sababu za uchukuaji fedha kwa mtindo huu wa malipo ya fedha taslim," alisema mmoja wa watu waliokutwa katika maeneo ya ofisi za TFF kwa sharti la kutotajwa jina lake. 
 
MAMILIONI SIMBA v AZAM
Kwa kutambua kuwa juzi kulikuwa na mechi kali ya ligi kati ya Simba na Azam, NIPASHE ilipiga tena kambi jana asubuhi kwenye ofisi za TFF ili kuona kama utaratibu wa kuchukua mamilioni hayo ya serikali kwa malipo taslim utaendelea, na tena bila ya mbebaji kuambatana na askari wa kumlinda.
 
Ilipofika saa 3:11 asubuhi, afisa yule yule aliyejihatarisha Jumapili ndiye aliyetinga tena kwenye ofisi za TFF akiwa peke yake kwenye gari lilelile aina ya Suzuki Vitara.
 
Mwandishi alifuatilia kwa karibu nyendo za afisa huyo. Ni kwamba, baada ya kupaki gari lake, alionekana akisalimiana na maafisa kadhaa wa TFF, akiwamo kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars), Mdenmark Kim Poulsen. IIimchukua takriban dakika 26 afisa huyo kukamilisha zoezi hilo maana saa 3:57 asubuhi ndipo alipoingia ndani na kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha malipo na kubeba mamilioni yanayokadiriwa kuwa ni Sh.
 7,925,600, kiasi ambacho ni sawa na asilimia 15 ya mgawo wa uwanja kwani mechi hiyo ya Simba dhidi ya Azam iliyochezwa juzi iliingiza Sh. milioni 66.855.
 
Baada ya kubeba fedha hizo, afisa huyo alionekana akifungua mlango wa nyuma wa gari alilokuwa nalo na kuweka begi linalodhaniwa kuwa na fedha hizo kabla ya kuondoka. 
 
Hiyo ilikuwa ni saa 4:03 asubuhi. Mwandishi alijaribu kumfuatilia kwa nyuma. Saa 4:07, afisa huyo aliingia ndani ya Shule ya Sekondari Benjamin William Mkapa iliyopo umbali mfupi kutoka TFF.
 
Saa 4:12, afisa huyo aliondoka kwenye shule hiyo na kurejea tena TFF na kuingia ndani ambapo akiwa na begi lake dogo lenye fedha, bila kuwapo na ulinzi wowote, alikaa kwa dakika 23, baadaye alitoka na kuingia kwenye gari na kuondoka saa 4:35.
 
TFF wanena
Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TFF, Osiah alikiri kuwa serikali hutuma maafisa wake kubeba fedha hizo kwa malipo taslim kila siku moja baada ya mechi na utaratibu huo umekuwapo kwa muda mrefu.
 
"Ni kweli kwamba hata sisi tunatambua kuwa si vizuri kuwalipa pesa taslimu, tena ni kinyume cha sheria... lakini utaratibu huo umekuwapo kwa miaka mingi na sasa imekuwa kama desturi yetu," alisema Osiah.
 
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kuwa hata fedha za klabu zinachukua mgawo wake kwa njia hiyo, licha ya kuwapo kwa taarifa za tukio la kuporwa kwa Sh. milioni 10 za Simba katika eneo la Sinza Makaburini.
 
MICHAEL WAMBURA
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT sasa TFF), Michael Wambura alisema jana kuwa utaratibu wa TFF kutoa fedha taslimu badala ya hundi kwa serikali ni kosa, lakini akasema kuwa imezoeleka hivyo na kwamba hata wakati wa uongozi wao (FAT), walikuwa na mfumo huo ambao anaamini kwamba siyo sahihi.
 
"Wakati tukiwa madarakani, tuliwahi kuamua kutumia utaratibu wa hundi lakini ulileta matatizo. Kuna watu hawakutaka kabisa utaratibu huo. Nafikiri kuna haja ya kufanya uchunguzi kujua ni kwanini hawataki utaratibu huo," alisema Wambura.

KAMANDA WA POLISI 
Alipotafutwa na NIPASHE jijini Dar es Salaam kuzungumzia taratibu za usafirishaji wa fedha, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, alisema ni kosa kwa mtu yeyote kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha za umma bila kuwa na ulinzi.
 
"Ni kosa kusafirisha fedha za umma na hata za watu binafsi pasipokuwa na ulinzi wa polisi ama vyombo vingine vya usalama vya serikali au kampuni za ulinzi za watu binafisi zinazotambuliwa kisheria," alisema Kenyela.
 
"Inashangaza kuona TFF na wizara hawatumii utaratibu wa benki (hundi) kulipana. Kulipana fedha taslimu, tena mamilioni ya fedha ni kuhatarisha usalama wa fedha na watu wanaozisafirisha," aliongeza Kenyela.
 
Wakati wa tukio la kudaiwa kuporwa kwa fedha za Simba baada ya mechi yao dhidi ya Black Leopards ya Afrika Kusini iliyochezwa Desemba 29, 2012, aliwahi kuonya kuwa hivi sasa, likitokea tukio lolote la kuporwa fedha huku wahusika wakiwa hawajaomba ulinzi, watakuwa wakianza kwa kuwakamata watu hao
waliobeba fedha hizo kiholela.
 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema jana kuwa hawezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu hakuwa katika mazingira mazuri ya kuzungumza kupitia simu kwa kuwa alikuwa safarini kuelekea jijini Dar es Salaam.
 
Hivi karibuni, watu kadhaa waliuawa katika tukio la uporaji wa Sh. milioni 150 
zilizokuwa zikisafirishwa bila ulinzi wa askari rasmi katika eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam.
 
 
CHANZO: NIPASHE

MASHINE ZA UMRI ZAWAUMBUA 'VIJEBA' VYA MICHUANO YA AFRIKA


UDANGANYIFU wa umri wa wachezaji kutoka barani Afrika umekuwa ni jambo la kawaida, lakini teknolojia mpya iliyobuniwa ya kutumia mashine kupima umri sahihi wa wachezaji umeanza kuwaumbua wachezaji 'vijeba' wanaochjachakachua umri ili kujifanya wadogo.
Teknokojia hiyo imewaumbua wachezaji tisa na kuondolewa kwenye michuano ya mataifa  ya Africa chini ya umri wa miaka 17 yanayofanyika nchini Morocco baada kipimo cha kugundua umri kupitia kiganja cha mkono kuonyesha kwamba wana umri mkubwa zaidi kuliko inavyopaswa.
Miongoni mwa wachezaji watatu wanatoka Congo-Brazzaville, Ivory Coast na Nigeria wamefungiwa kabisa kushiriki kwenye mashindano yoyote.
Mashine ya Magnetic Resonance Imaging (MRI) ilitumika kupima viganja vya wachezaji ili kujua ukweli wa umri wao.
Wachezaji ambao wameondolewa kwenye michuano hiyo ni kutoka Congo Cherlevy-Diabala Carim, Hardy Binguila na Bermagin Kangou, kutoka Ivory Coast  ni Dagou Britto, Abdul Diarrassouba na Siriki Dembele, na kutoka Nigeria ni Onyinye Ndidi, Ibrahim Abdullahi and Emmanuel Asadu.
Vikosi vya timu zote tatu vimepunguzwa mpaka kufikia wachezaji 18.
FIFA walianza kufanya utafiti wa umri wa wachezaji kwa kutumia technolojia ya MRI mwaka 2003 lakini wakaanza kuifanyia majaribio machine hiyo kwenye michuano ya U-19 World Cup in Nigeria.
Matokeo ya vipimo kwenye michuano ya kombe la dunia U-17 kuanzia 2003, 2005 na 2007 yalionyesha kwamba asilimia 35 ya wachezaji walikuwa wamezidisha umri unaoruhusiwa.
Wadau wa soka wanatamani kipimo hicho kianze kutumika pia hapa nchini ili kubaini baadhi ya wachezaji 'vibabu' lakini wakijitambulisha wakiwa na umri mdogo, jambo ambalo hata wenyewe wanajishangaa wanavyoongopa.
Credit to shaffihdauda.com

'Magaidi' walipua mabom na kuua watatu, zaidi ya 140 wajeruhiwa Boston Marathon



Baadhi ya picha za tukio hilo ambalo limesababisha kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka 8 miongoni mwa waliofariki

Boston Marathon bombing kills 3, injures over 140

BOSTON (AP) — Two bombs exploded in the crowded streets near the finish line of the Boston Marathon on Monday, killing at least three people and injuring more than 140 in a bloody scene of shattered glass and severed limbs that raised alarms that terrorists might have struck again in the U.S.
A White House official speaking on condition of anonymity because the investigation was still unfolding said the attack was being treated as an act of terrorism.
President Barack Obama vowed that those responsible will "feel the full weight of justice."
As many as two unexploded bombs were also found near the end of the 26.2-mile course as part of what appeared to be a well-coordinated attack, but they were safely disarmed, according to a senior U.S. intelligence official, who also spoke on condition of anonymity because of the continuing investigation.
The fiery twin blasts took place about 10 seconds and about 100 yards apart, knocking spectators and at least one runner off their feet, shattering windows and sending dense plumes of smoke rising over the street and through the fluttering national flags lining the route. Blood stained the pavement, and huge shards were missing from window panes as high as three stories.
"They just started bringing people in with no limbs," said runner Tim Davey of Richmond, Va. He said he and his wife, Lisa, tried to shield their children's eyes from the gruesome scene inside a medical tent that had been set up to care for fatigued runners, but "they saw a lot."

"They just kept filling up with more and more casualties," Lisa Davey said. "Most everybody was conscious. They were very dazed." As the FBI took charge of the investigation, authorities shed no light on a motive or who may have carried out the bombings, and police said they had no suspects in custody. Officials in Washington said there was no immediate claim of responsibility.
WBZ-TV reported late Monday that law enforcement officers were searching an apartment in the Boston suburb of Revere. Massachusetts State Police confirmed that a search warrant related to the investigation into the explosions was served Monday night in Revere but provided no further details.
Some investigators were seen leaving the Revere house early Tuesday carrying brown paper bags, plastic trash bags and a duffel bag.
Police said three people were killed. An 8-year-old boy was among the dead, according to a person who talked to a friend of the family and spoke on condition of anonymity. The person said the boy's mother and sister were also injured as they waited for his father to finish the race.
Hospitals reported at least 144 people injured, at least 17 of them critically. The victims' injuries included broken bones, shrapnel wounds and ruptured eardrums.
At Massachusetts General Hospital, Alasdair Conn, chief of emergency services, said: "This is something I've never seen in my 25 years here ... this amount of carnage in the civilian population. This is what we expect from war."
Some 23,000 runners took part in the race, one of the world's oldest and most prestigious marathons.
One of Boston's biggest annual events, the race winds up near Copley Square, not far from the landmark Prudential Center and the Boston Public Library. It is held on Patriots Day, which commemorates the first battles of the American Revolution, at Concord and Lexington in 1775.
Boston Police Commissioner Edward Davis asked people to stay indoors or go back to their hotel rooms and avoid crowds as bomb squads methodically checked parcels and bags left along the race route. He said investigators didn't know whether the bombs were hidden in mailboxes or trash cans.
He said authorities had received "no specific intelligence that anything was going to happen" at the race.
The Federal Aviation Administration barred low-flying aircraft within 3.5 miles of the site.
"We still don't know who did this or why," Obama said at the White House, adding, "Make no mistake: We will get to the bottom of this."

With scant official information to guide them, members of Congress said there was little or no doubt it was an act of terrorism. "We just don't know whether it's foreign or domestic," said Rep. Michael McCaul, R-Texas, chairman of the House Committee on Homeland Security.
A few miles away from the finish line and around the same time, a fire broke out at the John F. Kennedy Library. The police commissioner said that it may have been caused by an incendiary device but that it was not clear whether it was related to the bombings.
The first explosion occurred on the north side of Boylston Street, just before the finish line, and some people initially thought it was a celebratory cannon blast.
When the second bomb went off, spectators' cheers turned to screams. As sirens blared, emergency workers and National Guardsmen who had been assigned to the race for crowd control began climbing over and tearing down temporary fences to get to the blast site.
The bombings occurred about four hours into the race and two hours after the men's winner crossed the finish line. By that point, more than 17,000 of the athletes had finished the marathon, but thousands more were still running.
The attack may have been timed for maximum carnage: The four-hour mark is typically a crowded time near the finish line because of the slow-but-steady recreational runners completing the race and because of all the friends and relatives clustered around to cheer them on.
Runners in the medical tent for treatment of dehydration or other race-related ills were pushed out to make room for victims of the bombing.
A woman who was a few feet from the second bomb, Brighid Wall, 35, of Duxbury, said that when it exploded, runners and spectators froze, unsure of what to do. Her husband threw their children to the ground, lay on top of them and another man lay on top of them and said, "Don't get up, don't get up."
After a minute or so without another explosion, Wall said, she and her family headed to a Starbucks and out the back door through an alley. Around them, the windows of the bars and restaurants were blown out.
She said she saw six to eight people bleeding profusely, including one man who was kneeling, dazed, with blood trickling down his head. Another person was on the ground covered in blood and not moving.
"My ears are zinging. Their ears are zinging," Wall said. "It was so forceful. It knocked us to the ground."
Competitors and race volunteers were crying as they fled the chaos. Authorities went onto the course to carry away the injured, while race stragglers were rerouted away from the smoking site.
Roupen Bastajian, a state trooper from Smithfield, R.I., had just finished the race when he heard the blasts.
"I started running toward the blast. And there were people all over the floor," he said. "We started grabbing tourniquets and started tying legs. A lot of people amputated. ... At least 25 to 30 people have at least one leg missing, or an ankle missing, or two legs missing."
The race honored the victims of the Newtown, Conn., shooting with a special mile marker in Monday's race.
Boston Athletic Association president Joanne Flaminio previously said there was "special significance" to the fact that the race is 26.2 miles long and 26 people died at Sandy Hook Elementary School.
___
Associated Press writers Jay Lindsay, Steve LeBlanc, Bridget Murphy, Rodrique Ngowi and Meghan Barr in Boston; Julie Pace, Lara Jakes and Eileen Sullivan in Washington; and Marilynn Marchione in Milwaukee contributed to this report.

Monday, April 15, 2013

Ngumi kuipamba Ghana Mei 3


Nchi ya Ghana ambayo ni moja ya nchi zenye vipaji vingi vya wanamichezo mahiri na majina makubwa hususan mchezo wa ngumi, itawaka moto tarehe 3, Mei wakati mabondia mahiri sita watakapogombania mataji ya IBF katika ubingwa mbalimbali.

Bondia atakayeanza kupanda ulingoni kufukisha moto huo ni “Mtoto wa Kijiweni” Albert Mensah ambaye amejizolea sifa kemkem za kupambana na mabondia mahiri duniani. Mensah yuko kwenye viwango vya IBF vya dunia na amewekwa namba 7 kwa ubora duniani katika uzito wa Welter.
 
                 Helen Joseph
Mbabe huyu atakumbana na bondia mwenye maringo na “Mtoto wa Mjini” Ben Odamettey ambaye amekulia katika viunga vya Jamestown katika kata ya Bukom jijini Accra, ambayo ni maarufu kwa kutoa mabingwa wengi wa dunia kama kina Azumah Nelson, Ike Quartey, Joseph Agbeko na Poison Kotey. Wawili hawa watapambana kugombania ubingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa Junior Middleweight.
               Marriana Gulyas (kushoto)
 
Mpambano wa pili na unaongojewa kwa hamu kubwa ni ule wa mwanadada na mrembo kutoka Nigeria ambaye anaishi nchini Ghaba, Helen Joseph atakapombana na binti Mfalme kutoka Himaya ya Austrohungrian (Hungary) bi. Marianna Gulyas. Warembo hawa wanagombania mkanda wa IBF wa Mabara wa wanawake katika uzito wa unyoya (Featherweight) na moto mkubwa unategemewa kuwaka kutokana na umahiri wa warembo hawa wa kurusha makonde ulingoni.

Helen atakuwa anarudisha heshina yake baada ya kupoteza pambano la ubingwa wa dunia kwa mwanadada Dahianna Santana wa Dominican Republic mwezi wa Desemba mwaka jana. Hii ni heshima pekee kwa kina mama kutoka bara la Afrika wa kuonyesha umahiri wao kwa binti huyo wa Kifalme kutoka Hungary.
 
                                                          Albert Mensah (kulia)
Ndipo litakapokuja pambano la kukata na shoka kati ya mbabe kijana anayeinukia katika ulimwengu wa masumbwi nchini Ghaha na Afrika kwa ujumla bondia Issa Samir kutoka Ghana atakapopambana na mbabe kutoka kwenye jangwa la barafu la Siberia, bondia Robison Omsarashvili kutoka katika nchi ya Georgia ambayo ni moja ya nchi zilizokuwa kwenye Muungano wa Kishoshalisti wa Sovieti ya Urusi (USSR).

Ni nderemo na vifijo kwa Waghana na watu wote wa Afrika wakati mabondia hawa watakapo pambana kugombea mataji haya makubwa kabisa ya IBF na kuliwakilisha bara la Afrika katika ramani ya dunia.

Mapambano haya yanaandaliwa na kampuni ya GoldenMike Boxing Syndicate ya Accra, Ghana chini ya Henry Many-Spain na Michael Tetteh na yatafanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Accra (Accra International Conference Center) na yatasimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi.

Simba, Azam wafunika mapto ya Yanga Oljoro




Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 66,855,000 kutokana na watazamaji 11,458.
 Kiwnago hicho ni kikubwa kuliko pambano lililochezwa Jumamosi kati ya Yanga na JKT Oljoro ambapo mchezo huo uliingiza kiasi cha Sh Milioni 63.
Kwa pambano la jana, viingilio katika mechi hiyo namba 155 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,587,177.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,198,220.34.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,925,683.45, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 4,755,410.07, Kamati ya Ligi sh. 4,755,410.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,377,705.03 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,849,326.14.
Katika pambano la Yanga na Oljoro jumla ya Watazamaji 11,021 walikata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Oljoro JKT iliyochezwa juzi (Aprili 13 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuingiza sh. 63,170,000.

Viingilio katika mechi hiyo namba 156 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,853,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,636,101.69.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,552,501.25, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,531,500.75, Kamati ya Ligi sh. 4,531,500.75, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,265,750.37 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,762,250.29.


Sunday, April 14, 2013

Man City yainyoa Chelsea na kuifuata Wigan fainali FA Cup

Kun Aguero aliyeifungia Man City bao la pili

Vincent Kampany akichuana na Torres

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City muda mfupi uliopita imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la FA baada ya kuinyuka Chelsea kwa mabao 2-1 na kuifuata Wigan Athletic iliyotangulia katika hatua hiyoi tangu jana.
Chelsea ilijikuta ikienda mapumziko katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Londoni ikiwa nyuma kwa bao 1-0, lililofungwa na Samir Nasir katika dakika ya 35.
Sergio kun Aguero aliiandikia Manchester City bao la pili dakika mbili baada ya kuanza kipindi cha pili na kuifanya timu yake katika mchezo huo wa nusu fainali kucheza kwa kujiamini zaidi.
Demba Ba, alifutia machozi Chelsea kwa kutumbukiza bao pekee ambalo halikuwasaidia kitu katika dakika ya 66 na kufanya hjadi dakika ya mwisho Manchester City kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na hivyo kusubiri pambano la fainali dhidi yake na Wigan iliyoing'oa Milwall jana kwa mabao 2-0.

SIMBA, AZAM HAKUNA MBABE, YANGA YAPUMUA KILELENI

 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akichuana na beki wa Azam FC, John David katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilifunga mabao 2-2 (Picha na Habari Mseto Blog)  
 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akimtoka beki wa Azam FC, Joockins Atudo wakati wa mchezo wa Ligi Kuu  Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
 Wachezaji wa Simba wakishangilia baada ya kuapata bao la pili.
Kiungo wa timu ya Simba, Abdallah Seseme akiwatoka wachezaji wa Azam FC, Himid Mao (kulia) na Salum Abubakar wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2.

LICHA ya tambo nyingi kabla ya pambano lao timu za Simba na Azam jioni ya leo zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na kuwafanya vinawa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga kupumua.
Yanga mabo mashabiki wake leo walionyesha kioja kwa kuwashangilia watani zao Simba dhidi ya Azam, wanapumua kwa vile Azam inayowafukuza kwenye mbio za ubingwa imepunguza pengo la pointi moja tu na kuipa nafasi Yanga kuhitaji pointi tano tu kati ya mechi zake nne zilizosalia kutangaza ubingwa msimu huu.
Yanga yenyewe ina pointi 52 wakati Azam waliopo nafasi ya pili wana pointi 47, huku kjwa sare hiyo ya leo Simba imeendelea kusalia kwenye nafasi ya nne akiwa na pointi 36.
Ramadhani Singano 'Messi' ndiye aliyeipa Simba uongozi wa mabao katika pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Oden Mbaga kwa kufunga mabao mawili katika dakika ya 10 na 14 akimalizia kazi murua iliyofanywa kwa ushirikiano wa Mrisho Ngassa na Haruna Changono.
Dakika ya 29 Kipre Tchetche aliifungia Azam bao la kwanza baada ya Khamis Mcha kuangushwa akielekea kumsalimia kipa Abel Dhaira na kumfanya afikishe bao la 15 msimu huu.
Dakika mbili baadaye kocha wa Azam, Stewart Hall alionyeshwa kadi nyekundu kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi kutokana na maamuzi yake na hadi mapumziko matokeo yalikuwa mabo 2-1.
Kipindi cha pili Azam walionyesha uhai zaidi kwa kushambulia lango la Simba na kufanikiwa kupata bao la pili na la kusawazisha dakika ya 72 kupitia kwa Humphrey Mieno.
Kwa matokeo ya pambano hilo lililokuwa likisubiriwa kwa hamu kutokana na tambo zilizokuwa zikitolewa na pande zote mbili na mkasa ulioibuka baada ya mechi yao ya kwanza ambapo Simba walishinda mabao 3-1 na kupelekea Azam kusimamisha wachezaji wake wanne kwa tuhuma za rushwa, msimamo upo hivi;


                                       P     W     D     L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans       22    16     4     2    40    12    28    52
    2. Azam                      23    14     5     4    41    19    22    47    
    3 . Kagera Sugar         22    10     7     5    25    18    7      37     
    4.  Simba                     22     9     9     4     32    21    11    36
    5.  Mtibwa Sugar         23     8     9     6     26    24     2     33   
    6. Coastal Union          22     8     8     6     23    20     3     32    
    7.  Ruvu Shooting         23     8     6     9     21    22    -1    30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27    -5    28     
    9. Tanzania Prisons       24     6     8    10    14     21    -7    26    
    10.JKT Mgambo         22     7     3     12    14     22    -8    24
    11.Ruvu Stars              21     6     4     11     19     34   -15   22
    12. Toto Africans         24     4    10    10     22     32   -10   22
    13. Polisi Morogoro     23     3    10    10     11     21    -10  19    
    14.  African Lyon         23     5     4     14     16     35    -19  19

WAWILI WAFA KATIKA AJALI KAGERA


 

Magari yaliyohusika na ajali hiyo iliyotokea jana jioni huko Ngara, Kagera

Watu wawili wamefariki dunia  papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mercedec benz lenye namba ya usajili T 908 ABZ semitrailer lililokuwa ikitokea nchini Burundi, kuacha njia leo(April 13,2013) muda wa saa 12 jioni na kupinduka katika eneo la Kumuyange nje kidogo ya mji wa Ngara mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi wilaya ya Ngara  Abel Mtagwa amewataja watu hao waliofarki katika ajali hiyo kuwa ni Edward Filimon alie kuwa akiendesha pikipiki yake yenye namba za usajiri T 756 BZJ na abiria wake ambae hadi sasa haja fahamika jina lake.
Kamanda Mtagwa amewataja majeruhi wa ajari hiyo kuwa ni Dereva wa gari hilo Hajji Omary Ibrahim(29) mkazi wa gongolamboto jijini Dar es salaam na tingo wake aliyejulikana kwa jina la Kambi simba(40).
Kamanda Mtagwa ameongeza kuwa katika ajal i hiyo nyumba moja mali ya Bi.Bibiana John (58) imegongwa na gari hilo na kuharibika.
Aidha Kamanda Mtagwa amesema kuwa chanzo cha ajari hiyo ni  gari hilo kufeli  mfumo wa Breki  jambo ambalo Dereva wake alishindwa kulimudu kuliendesha ndipo lilipanda mtaro na kubomoa nyumba hiyo. 
 
Aidha Majeruhi wa Ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
 
CHANZO:MWANA AFRIKA

Simba, Azam. ni vita ya kisasi leo taifa

Simba

Azam

SIMBA na Azam jioni ya leo wanatarajiwa kushuka dimbani kumenyana katika pambano pekee la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoelekea ukingoni huku, ambalo limetabiriwa na wengi kama vita ya kisasi baina ya timu hizo.
Timu hizo zitakutana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kila moja ikiwa na malengo tofauti, Azam kulipa kisasi ya kipigo cha mabao 3-1 ilichopewa kwenye pambano lao la kwanza lililosababisha iwasimamishe wachezaji wake wanne kwa tuhuma za kuihujumu kupitia rushwa.
Simba wenyewe wakaikabilia Azam wakiwa na hasira za kutuhumia na rushwa sakata ambalo lilimalizwa nna Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kabla ya kuibuka ikitaka kulipwa fidia ya Bilioni 1 kwa tuhuma hizo nzzito.
Pia Simba inashuka uwanja wa Taifa ikiwa inataka kulinda heshima yake katika ligi ya msimu huu kutokana nna ukweli imeshatemeshwa ubingwa na ipo hatua chachee kukosa hata nafasi ya uwakilishi wa nchi katika michuano ya Kimataifa mwakani.
Tayari kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' ametamka wazi kwamba wanashuka dimbani leo kwa lengo moja tu la kutaka kulinda heshima yao mbele ya Azam na pia kuhakikisha wanamaliza ligi wakiwa katika nafasi nzuri baada ya kutemeshwa taji.
Azam mbali na kuhitaji kulipa kisasi kwa Simba ikiamini kwamba mechi ya kwanza walifungwa kwa hila, lakini pia inasaka ushindi ili kuifukuzia Yanga kileleni ambayo jana ilitakata kwa kupata ushindi wa mabao 3-0 mbele ya maafande wa JKT Oljoro na kuzidi kujichimbia kwenye nafasi ya kwanza.
Yanga mbali na kuendelea kuongoza na kuongeza pendo la pointi dhidi yake na Azam, pia imejihakikisha nafasi ya kushiriki michuano ya Afrika mwakani mpaka sasa kati ya nafasi mbili za uwakilishi wa nchi.
Kwa kuangalia mazingira hayo, huku Azam wakijinafasi kwamba kiu yao ni kutwaa ubingwa msimu huu na kuweka rekodi, ni wazi pambano la jioni litakuwa ni patashika nguo kuchanika.
Wachezaji wanne waliohusishwa na tuhuma za rushwa baada ya pambano hilo la duru la kwanza, nahodha wa zamani Aggrey Morris, Said Morad, Erasto Nyoni na kipa Deo Munishi 'Dida' tayari wameripoti kambini katika kikosi cha timu hiyo wakielezwa wanaweza kushuka dimbani leo kuwakabili 'Mnyama'.
Hata hivyo kwa mazingira yalivyo huenda ikawa vigumu kwa wachezaji hao kucheza pambano hilo ikizingatiwa kwamba ni Simba hao hao waliowaponza hata kuingia matatani kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Mashabiki wa soka watakuwa na hamu kubwa ya kuona kipi kitakachotokea katika mechi hiyo baada ya dakika 90 huku macho na masikio yakielekezwa kwa washambuliaji nyota wa Azam, Kipre Tchetche na John Bocco 'Adebayor'.
Tchetche anaangaliwa kutokana na kasi yake ya ufungaji mabao akifunga karibu kila mechi tangu arejee dimbani katika duru la pili, huku Adebayor kwa bahati yake ya kuitungia Simba kila timu hizo zinapokutana.
Bila shaka kujua nani atakayecheza ua kulia leo taifa ni suala la kusubiri kuona baada ya dakika 90 za pambano hilo la kusisimua.

MIUJIZA:ABIRIA ZAIDI YA 100 WANUSURIKA KIFO AJALI YA NDEGE

































  
ZAIDI ya abiria 100 wamenusurika kimiujiza katika ajali ya ndege iliyoanguka muda mfupi baada ya kuruka hewani kando ya pwani ya bali, nchini Indonesia.
Mashuhuda wa tukio hilo lililoikumba ndege ya Lion Jet iliyoanguka ikitoka kuruka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Ngurah Rai nje kidogo ya mji wa Denparsar walisema walisema manusura wa ajali hiyo walionekana kuhamanika wakati wakiokolewa kutoka kwenye ndege hiyo iliyozama baharini kwa futi kadhaa.
Inaelezwa ndege hiyo ilikuwa imebebea jumla ya abiria 101 na watumishi wapatao saba wakati ikianguka majini kutoka umbalio wa Mita 50 juu.

Saturday, April 13, 2013

Prisons yazidi kukimbia janga la kushuka daraja


MAAFANDE wa Prisons Mbeya wamezidi kupigana kuepa janga la kushuka daraja baada ya kuinyoa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika pambano lililochezwa jioni ya leo mjini Mbeya.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo baada ya Jumatano iliyopita kuicharaza Mgambo JKT, ulipatikana kwenye uwanja wa Sokoine na kuifanya Prisons kuchupa kwa nafasi moja toka nafasi ya 10 haid ya 9.
Hata hivyo bado Prisons ina kibarua cha kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia dhidi ya JKT Ruvu na Kagera Sugar kujihakikishia kusalia Ligi Kuu msimu ujao.
Habari kutoka Mbeya zinasema kuwa Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania walipata ushindi huo kwa magoli ya kipindi cha pili yaliyowekwa yote kimiani na mchezaji wake aliyekuw shujaa leo, Elias Maguli.Maguli alifunga bao la kwanza kwa shuti akiunganisha pasi murua ya mchezaji mwenzake katika dakika ya 53 kabla ya kuongeza jingine dakika tano baadaye kwa mkwaju wa penati baada ya beki mmoja wa Ruvu kuunawa mpira langoni mwake.
Kwa matokleo hayop Prisons imefikisha pointi 26 na kuishuka Mgambo katika nafasi ya tisa na kukalia wao nafasi hiyo.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano kati ya Azam na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

 Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za leo jioni;

                                        P     W     D    L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans     22     16    4     2    40   12    +28     52
    2.  Azam                     22     14    4     4    39   17    +22     46    
    3.  Kagera Sugar         22     10    7     5    25   18    +7       37     
    4.  Simba                     21     9     8     4     30   19   +11      35
    5.  Mtibwa Sugar        23      8     9     6     26   24    +2      33   
    6. Coastal Union         22     8     8     6     23    20    +3      32    
    7.  Ruvu Shooting       23     8     6     9     21     22     -1     30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27     -5     28     
    9. Tanzania Prisons     24     6     8    10    14     21     -7     26    
   10.JKT Mgambo          22     7     3    12    14     22     -8     24
   11.Ruvu Stars              21     6     4     11    19     34     -15   22
   12. Toto Africans        24     4     10    10    22    32     -10    22
   13.  African Lyon       23     5      4     14    16     35     -19   19
   14. Polisi Morogoro    23     3     10    10    11     21     -10   19    
             

Yanga yaitemesha Simba ubingwa, yaikwangua JKT Oljoro 3-0

Vinara wa ligi kuu Yanga walioivua Simba taji jioni ya leo
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeendelea kudhihirisha wamepania kutwaa taji la msimu huu baada ya jioni hii kuikwangua JKT Oljoro ya Arusha mabao 3-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo uliopatikana kwa mabao ya kipindi cha kwanza yameifanya Yanga kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 52 na kuivua rasmi Simba ubingwa kutokana na kufikisha pointi 52 ambazo haziwezi kufikiwa na Wana Msimbazi.
Simba ambayo itashula kesho dimbani kuumana na Azam yenyewe ina pointi 35 na kama itashinda mechi zake zote itafikisha pointi 50 tu.
Mabao yalioifanya Yanga kulishika taji la ubingwa kwa mkono mmoja na kusubiri mwingine iwapo Azam wanaowafukuzia watateleza katika mechi zake yaliwekwa kimiani na beki Nadir Haroub 'Cannavaro' katika dakika ya 5 tu ya mchezo kabla ya Simon Msuva kufunga la pili dakika ya 19 na Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza la tatu dakika mbili kabla ya mapumziko.
Pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Amon Paul wa Mara lilihuhudia kadi kadhaa za njano zikitolewa kwenye mchezo huo na mpaka dakika 90 zinamalizika Yanga walikuwa wababe mbele ya maafande hao kwa ushindi huo wa mabao 3-0.

Supersport yakwama kurusha live mechi za VPL

PRESS RELEASE



Na Boniface Wambura
MECHI tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.

Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.

ZA LEO LEO