STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 14, 2013

Ubunifu! Hata watanzania wanaweza ila basi tuu

Mwangoka akiwa ndani ya gari lake

Umeuona mlango? Mwangoka akishuka garini

Akifunga mlango

Akionyesha siti ya abiria wake

Juu tumeweka kupitisha upepo


Umeona dashboard yake ilivyo

Mbunifu Kenneth Joseph Mwangoka akiwa katika pozi

Gari hilo linaloonekana kwa mbele

Kishoka napiga hivi

Bomba la kutolea moshi ndilo hili

Watu wakilishangaa gaari hilo

Umeona vitendea kazi vyake

Usukani wake ni mbao tu kweli msimu ni mali

Muonekano wa gari hilo kwa nyuma

rivasi kama kawa

TANZANIA imejaliwa watu wenye vipaji na ujuzi mkubwa katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia ila kuna vitu vidogo vinavyowakwaza kusimama na kwenda sambamba na wataalam wa mataifa mengine ambao wapo mbali katika suala la vipaji na ubunifu.
Mifano michache ni watu wanaomudu kutengeneza magobole, mashine mbalimbali na vitu vingine na hata wabunifu wa mrusho wa matangazo ya radio, ambao badala ya kuwezeshwa hupata vikwazo ikiwamo kunaswa na vyombo vya dola na kufunguliwa mashtaka ilihali wangeweza kutumika kuitangaza Tanzania.
Hapo juu ni mmoja wa wabunifu wa Kitanzania aliyeweza kutengeneza gari ambalo alitumia muda wa miezi sita kulikamilisha kwa kuokoteza vifaa na kulipambana kiasilia kwa kutumia malighafi ya misitu.
Majina yake kamili ni Kenneth Joseph Mwangoka ambaye alikuwa moja ya vivutio katika Maonyesho ya Biashara ya Sabasaba kwa ubunifu wa gari hilo linalotumia injini ya Toyota S1na kuongeza ubunifu wao kiasi kwamba gari hilo lililomgharimu kiasi cha Sh Milioni 8.6 kutembea kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Mwangoka anayeishi Iringa, anasema lengo lake ni kuhakikisha anakuja kutengeneza vitu zaidi ya gari hilo la aina yake.

Bingwa wa RCL, zitakazopanda FDL kufahamika leo


BINGWA wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) na timu tatu zitakazopanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zinatarajiwa kufahamika leo wakati timu nne zilizofanikiwa kutinga Nusu Fainali za RCL zitakaporudiana katika viwanja viwili tofauti .
Friends Rangers ya jijini Dar es Salaam iliyodunguliwa bao 1-0 na Polisi Jamii ya Mara itakuwa dimba la nyumbani la Azam Complex, Chamazi katika pambano la marudiano ambapo kama itafanikiwa kulipa kisasi na kushinda kwa idadi kubwa itakata tiketi ya kupanda daraja la kwanza.
Mshindi yoyote wa mechi hiyo ya leo inayotarajiwa kuwa ngumu, itaungana na timu mbili zitakazokuwa nazo uwanjani leo kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga kati ya Kimondo Sc ya Mbeya na Stand United Fc ambazo zimeshajihakikisha kupanda daraja ila zinawania ubingwa wa ligi hiyo ya RCL.
Timu hizo mbili za Stand United na Kimondo zitarudiana kuwania ubingwa, huku Kimondo ikiwa mbele kwa ushindi wa bao 1-0 iliyopata katika mchezo wa kwanza uliocherzwa kwenye uwanja wa
Timu hizo sasa zitacheza Jumapili (Julai 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi. Polisi Jamii ilishinda bao 1-0 mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 6 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine ya Mbeya.

Wanajeshi 7 wa Tanzania wauwawa Darfur

WANAJESHI saba wa Tanzania, ambao ni miongoni mwa kikosi cha Umoja wa Mataifa, cha kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan, wanadaiwa kuwa wameuawa.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zilisema kwamba wanajeshi hao wa Tanzania, wamekufa kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, miili yao wanajeshi hao bado ipo nchini Sudan ikisubiri taratibu za kusafirishwa kuletwa nchini.
Hii ni mara ya kwanza kuripotiwa kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kufa kwa wakati mmoja.
Agosti mwaka jana wanajeshi watatu wa Tanzania huko Darfur waliripotiwa kuuawa kwenye tukio kama hilo.
Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) , Kanali Kapambala Mgawe alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu vifo vya wanajeshi wa Tanzania huko Darfur, alisema kuwa naye amesikia, lakini hana taarifa rasmi kwa mujibu wa taratibu za kiofisi.
Hii ni mara ya pili kwa wanajeshi wa Tanzania kuuawa katika Jimbo la Darfur, ambapo Agosti mwaka jana, Kanali Mgawe alinukuliwa na vyombo vya habari akithibitisha kutokea kwa vifo vya askari watatu ambao gari lao lilizolewa na maji walipokuwa wakivuka mto uliokuwa umefurika maji.
Kanali Mgawe aliwataja askari hao kuwa ni Sajini Julius Chacha, Sajini Anthony Daniel na Koplo Yusuph Said na kwamba askari wengine walinusurika baada ya kuogolea.
Tanzania ina askari 850 kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani jimbo la Darfur, ambao ni sehemu ya askari 1,081 wa kulinda amani katika jimbo la Darfur.
Wanajeshi hao wa Tanzania wametawanywa kwenye miji ya Khor Abeche na Muhajeria kusini mwa Darfur.
Aprili mwaka huu Tanzania ilipeleka wanajeshi wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kupambana na kikundi cha waasi wa nchi hiyo M23 kinachopigana kuiangusha serikali ya DRC.
Majeshi ya Tanzania yalipelekwa kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa. Tanzania inaungana na nchi za Afrika Kusini na Malawi kukamilisha kikosi cha wanajeshi 3,000. Tanzania imepeleka wanajeshi 850.

MWANANCHI 

NB: Taarifa ambazo MICHARAZO imezipata asubuhi zinasema kuwa Jeshi linatarajiwa kutoa taarifa rasmi juu ya tukio hilo la Darfur saa 3 asubuhi katika Makao Makuu ya Jeshi hilo Upanga, Dar es Salaam.

Rais Kikwete awatunuku Maafisa wa JWTZ

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiingia katika uwanja wa gwaride wa Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, tayari kwa kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ jana Julai 13. Pamoja naye ni Mkuu wa Chuo hicho Meja Jenerali V.K. Mritaba. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.
 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua  gwaride katika  Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  jana Julai 13.
 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akitunuku kamisheni kwa maafisa katika Chuo cha  Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  jana Julai 13. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na
Visiwa vya Shelisheli.
Meza kuu wakati wa sherehe za  kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  jana Julai 13. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akimpa zawadi  Ofisa Kadet  Ngodoke kwa kuibuka mwanafunzi bora wa jumla mwaka huu katika Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  jana Julai 13. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akimpa zawadi Ofisa Kadet  D.G.L. Wong- Pool toka Visiwa vya Ushelisheli kwa kuibuka mwanafunzi bora wa kigeni wa jumla mwaka huu katika Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ jana Julai 13. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiongea na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange baada ya sherehe za kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  jana Julai 13. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.

Kim akiri Stars imefungwa kizembe

Kocha Kim Poulsen (Kati)
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Kim Poulsen amesema uzembe uliofanywa na wachezaji wake katika pambano lao la jana dhidi ya Uganda The Cranes ndiyo iliyowaponza kupoteza mchezo huo wa awali wa kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).Stars ilipoteza mchezo huo kwa kulala bao 1-0 lililofungwa katika kipindi cha pili na nyota wa the Cranes anayeichezea SC Villa, Dennis Iguma na kuzima tambo za Stars kwamba wangeishikisha adabu wapinzani wao hao kutokana na asilimia kubwa ya kikosi chao ni kile kile kilichokuwa kikiwania fainali za Dunia 2014.
kiri kwamba vijana wake hawakustahili kupoteza mechi
Akizungumzia matokeo hayo baada ya mchezo huo, Kocha wa Stars, Kim Poulsen amesema mpira wa miguu ni mchezo wa kufunga mabao ambapo timu ilipata nafasi nzuri katika dakika ya kwanza tu lakini ilishindwa kuibadili kuwa bao.
“Uganda walitengeneza nafasi moja tu katika kipindi cha kwanza wakati sisi tulikuwa nazo kadhaa. Kipindi cha pili tuliwapa nafasi wakafunga bao lao. Lakini kwa kifupi kama wao wameweza kufunga hapa (Dar es Salaam), hata sisi tunaweza kufunga Kampala,” amesema Kim akizungumzia nafasi ya timu yake kusonga mbele.
Timu hizo zitarudiana jijini Kampala kati ya Julai 26 na 27 mwaka huu ambapo mshindi ndiye atakayepata tiketi ya kwenda kwenye fainali za tatu za CHAN zitakazofanyika Afrika Kusini. Stars ilicheza fainali za kwanza za CHAN zilizofanyika mwaka 2009 nchini Ivory Coast.
Katika hatua nyingine baadhi ya wadau wa kandanda walikiponda kikosi cha Stars kwa mchezo wa jana kwa kudai ni kama hawakujua walikuwa wanatakiwa kufanya nini uwanjani.
Kipa wa zamani wa kimataifa wa Simba ambaye kwa sasa ni kocha, Spear Mbwembwe alisema hajawahi kuona Stars ikicheza kichovu kama mechi ya jana, akisema kwa mtazamo wake ni wachezaji wawili tu waliokuwa wakitimiza wajibu ambao ni winga Mrisho Ngassa na beki Aggrey Morris.
"Wengine hawakuwa mchezoni kabisa na kibaya zaidi mabadiliko yaliyofanywa ya kutolewa kwa Nyoni na kuingiwa Luhende wakati nilidhani Kapombe na Nyoni wangebadilishana nafasi tu na tumeona kilichotokea," alisema.
Mbwembwe alisema ni lazima Stars ifanye kazi ya ziada kwa mechi ya marudiano aliyoikatia tamaa kwa madai haoni kitakachobadilisha matokeo ikizingatiwa wachezaji ni wale wale na kocha yule yule tena ugenini.
"Mie nadhani kuna haja TFF ikafanya jambo moja la muhimu, lazima Poulsen apewe kocha ambaye yupo 'active', sidhani kama Sylveter Marsh anamfaa kocha wakati kwa miaka miwili sasa hana timu yoyote anayofundisha," alisema Mbwembe.
Kocha huyo alisema tatizo la kubebana ndilo linalogharimu ska la Tanzania kusonga mbele licha ya mikakati mizuri na kocha bora iliyonayo Tanzania, yaani Kim Poulsen kutoka Denmark.
Kipigo cha jana ni cha tatu mfululizo kwa Tanzania baada ya vipigo viwili vya awali toka Morocco na Ivory Coast walioumna nao katika mechi za marudiano ya kuwania Fainali za Kombe la Dunia za Brazili.

Wajumbe TFF wapitisha Katiba Mpya


Mwakilishi wa FIFA katika mkutano huo wa TFF, James Johnson akihutubia

Rais Leodger Tenga na Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah wakiwa na Mwakilishi wa FIFA, James Johnson,


 

Baadhi ya Wajumbe wa TFF katika mkutano huo

Na Boniface Wambura
WAJUMBE wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) uliofanyika jana (Julai 13 mwaka huu) wamepitisha marekebisho ya Katiba yake, hivyo mchakato wa uchaguzi unatarajia kuanza wakati wowote.

Wajumbe zaidi ya 100 walihudhuria Mkutano huo uliofanyika ukumbi wa NSSF Waterfron, Dar es Salaam na kufunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera aliyewataka wajumbe kuhakikisha kiwango cha mpira wa miguu nchini kinakuwa.

Mkutano huo uliokuwa chini ya uenyekiti wa Rais wa TFF, Leodegar Tenga umefanya marekebisho ya Katiba kutokana na maelekezo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA). James Johnson kutoka Idara ya Wanachama ndiye aliyeiwakilisha FIFA katika mkutano huo.

Aprili mwaka huu FIFA ilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa TFF, na kuagiza kwanza yafanyike marekebisho ya Katiba ili kuingiza Kamati ya Maadili, na Kamati ya Rufani ya Maadili ambavyo ndivyo watashughulikia matatizo ya kimaadili kwa familia ya mpira wa miguu nchini.

Mbali ya kamati hizo, mabadiliko hayo pia yametengeneza ngazi mbili za kushughulikia masuala ya kinidhamu ambazo ni; Kamati ya Nidhamu na Kamati ya Rufani ya Nidhamu.

Kamati ya Utendaji ya TFF chini ya Rais Tenga itakutana kesho (Julai 14 mwaka huu) kwa ajili ya kuteua wajumbe watakaounda Kamati hizo ili kuruhusu kuanza mchakato wa uchaguzi ambao FIFA iliusimamisha hadi vitakapoundwa vyombo hivyo.

Saturday, July 13, 2013

Taifa Stars bado sana, yapigwa na The Cranes




LICHA ya ahadi tamu toka kwa kocha Kim Poulsen na kauli ya Rais wa TFF, Leodger Tenga kwamba timu ya taifa, Taifa Stars imeiva kwa mashindano, hali imekuwa tofauti jioni hii baada ya Stars kukubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Uganda the Cranes katika mechi ya mkondo wa kwanza ya kuwania kucheza CHAN.
Stars ikiwa na nyota wake karibu wote ukiondoa wawili tu wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi ambao haruhusiwi kuitumikia timu hiyo, ilikubali kipigo hicho kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao lililoizamisha Stars na kuwa na wakati mgumu kwenda kuiondosha The Cranes nyumbani kwao wiki ijayo liliwekwa kimiani na Iguma Dennis dakika moja tangu kuanza kwa kipindi cha kwanza.
Stars inaweza kujilaumu kwa kukosa mabao mengi ya wazi kutokana na nafasi zilizopotezwa na washambuliaji wake huku ikionekana kupwaya katika kiungo kusiko kawaida.
Kwa kipigo hicho Stars italazimisha kupata ushindi usiopungua mabao 2-0 iwapo inataka kuing'oa Uganda na kwenda Afrika Kusini mwakani kwenye Fainali hizo za timu za taifa zinazohusisha wachezaji wa ndani tu.
Pia ni kipigo cha tatu mfululizo kwa Stars baada ya vile ilivyopata katika michezo yake miwili ya kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za mwakani zitakazochezwa Brazili kwa kulala mbele ya Morocco kisha kucharazwa na Ivory Coast katika mechi zao za kundi C.

Maskini mwanachuo huyu, afa maji akiogelea

MSOMI wa mwaka wa kwanza Uhandisi wa Kompyuta wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Wendy Habakuki Lwendo amepoteza maisha yake jana jioni wakati akiogelea na wenzake katika bahari ya Hindi eneo la Kipepeo Kigamboni, jijini Dar.
Akisimulia tukio hilo, kaka wa Marehemu, Sammy Lwendo amesema mdogo wao alipatwa na maswahibu hayo akiwa na rafiki zake hao watatu wakiogelea baharini na wakati wanaogelea walikuwa katika eneo la kina kifupi cha maji yaliyokupwa na mara maji hayo yaka jaa na walipokuwa wakijaribu kutoka ndipo Wendy akazidiwa na maji.
Lwendo amesema kuwa wenzake walifanikiwa kumtoa majini lakini hali yake tayari ilikuwa mbaya na kwakuwa hawakuwa na ujuzi wa kutosha wa kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyezama majini walihangaika kwa zaidi ya dakika 40 kumsaidia ndipo wakapata msaada wa Polisi kumkimbiza kituo cha afya Kibaoni huko Kigamboni lakini jitihada za kuokoa maisha yake ziligonga mwamba.
Aidha alisema kuwa mwili wa Marehemu ulihamishiwa katika Hospitali ya Wilaya Vijibweni na sasa ndugu wamefika na kuhamishia mwili huo Hospitali ya jeshi Lugalo.
Msiba kwa sasa upo Kinondoni nyuma ya Vijana, huku wakisubiriwa wazazi wa marehemu pamoja na ndugu wengine ili kujua taratibu kamili za maziko.
Wazazi wa Wendy, Mchungaji Habakuki Lwendo ni mwalimu wa Chuo cha Uchungaji Makumira mkoani Arusha.
Father Kidevu

TPBO YATAHADHARISHA KUHUSU FRANCIS CHEKA

Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh'
NINAWAPA TAARIFA RASMI KWAMBA TAREHE 30-08-2013 KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JIJINI DAR--ES-SALAAM KUTAFNYIKA PAMBANO KUBWA LA NGUMI ZA KULIPWA KATI YA MTANZANIA FRANCIS CHEKA  NA MMAREKANI DERRICK FINDLEY , PAMBANO LA KUGOMBEA UBINGWA UNAOTAMBULIWA NA SHIRIKISHO LA NGUMI LA DUNIA [WBF].

HILI NI PAMBANO LA RAUNDI KUMI NA MBILI ZA DAKIKA 3 KILA RAUNDI NA MAPUMZIKO YA DAKIKA MOJA  KWA KILA RAUNDI. KATIKA UZITO WA SUPER MIDDLE [75 KGS]

PIA NINATUMIA FURSA HII KUWAFAHAMISHA RASMI KWAMBA BONDIA FRANCIS CHEKA ALISHASAINI MKATABA WA PAMBANO HILI TANGU MWEZI WA TANO .NA MASHARTI YA MKATABA HUO NI KWAMBA HARUHUSIWI KUCHEZA PAMBANO LOLOTE KWA SIKU 30 KABLA YA PAMBANO HILO NA MMAREKNI [FINDLEY] NA TAYARI AMELIPWA MALIPO YA AWALI[ADVANCE]

PAMBANO HILI LINAANDALIWA NA KAMPUNI YA HALL OF FAME BOXING &PROMOTION[USA] KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA NAI INCORPORATION COMPANY-LTD YA TANZANIA NA LITAKUWA CHINI YA USIMAMIZI WA NDANI WA TPBO-LTD.

WAAMUZI WA PAMBANO HILI WATATOKA AFRIKA KUSINI NA RAIS WA WBF MR HOWARD GOLDBEIG ATAKUWA KAMISHNA WA PAMBANO HILI KUBWA.

PIA SIKU HIYO HIYO MABONDIA MADA MAUGO NA THOMAS MASHALI WATAPANDA ULINGONI KUGOMBEA UBINGWA WA WBF -AFRIKA ,PAMBANO LA RAUNDI 12 LA UZITO WA SUPER MIDDLE PIA ALPHONSE MCHUMIA TUMBO ATAPAMBANA NA BONDIA KUTOKA MAREKANI DE-ANDRE MAC'COLL KATIKA PAMBANO LA RAUNDI 10 UZITO.

NDG WAANDISHI NINATOA TAARIFA HII KWENU PAMOJA NA VIONGOZI WA NGUMI ZA KULIPWA TANZANIA, KWA SABABU MOJA KUBWA, KUNA BAADHI YA WATU BILA KUFUATA TARATIBU ZA NGUMI KULIPWA WAMEKUWA WAKITUMIA VYOMBO VYENU VYA HABARI KUTANGAZA PAMBANO LINGINE LA FRANCIS CHEKA KWAMBA ATAPAMBANA NA MMALAWI CHIMWEMWE CHIOTCHA HALI WAKIJUA WAZI KABISA UTARATIBU WA MAPAMBANO  KAMA BONDIA AMESHASAINI MKATABA SEHEMU NYINGINE UKOJE. TPBO ILISHATOWA KIBALI KWA HALL OF FAME NA WASHIRIKA WAKE  CHA KURUHUSU PAMBANO HILO TANGU TAREHE 28 MAY 2013  MARA TU MAKUBALIANO YA FRANCIS CHEKA NA MAPROMOTA YALIPOFANYIKA ,KWA MASHARTI HAYO YA KUTOKUPIGANA PAMBANO LOLOTE SIKU 30 KABLA YA PAMBANO  NA MMAREKANI HUYO. NAKALA ZA MIKATABA TUNAYO [kama mtahitaji]

NA MAANDALIZI YA PAMBANO YANAENDELEA VYEMA ,NA MIPANGO YA USAFIRI KWA WAAMUZI NA MABONDIA KUTOKA MAREKANI INAKWENDA VYEMA.

NDG ZANGU KAMA MTAKUMBUKA VYEMA KUHUSU BONDIA KARAMA NYILAWILA ALIVYOPOTEZA UBINGWA WA DUNIA KWA KUSHINDWA KUTETEA BAADA YA BAADHI YA VIONGOZI WENZETU WALITOWA KIBALI KWA KARAMA KUPAMBANA NA CHEKA. .MJINI MOROGORO NA KUACHA KUTETEA UBINGWA WAKE WA DUNIA.

NDG ZANGU KATIKA KUTETEA KWAO KUTAKA CHEKA APAMBANE NA CHIMWEMWE ETI WANADAI WANAMUANDAA BONDIA FRANCIS CHEKA KWA PAMBANO LAKE NA MMAREKANI ,HII MBALI NA MASHARTI YA MKATABA KIUFUNDI  TU HAIKUBALIKI.

KWA SABABU KWA MASHARTI YA MKATABA HUO ,KAMA KWELI WANATAKA KUMUANDAA CHEKA HAWAPASWI KUTANGAZA PAMBANO BALI WAMUITE CHIMWEMWE AMSAIDIE MAZOEZI YAKE NDANI YA GYM KAMA SPARRING PATNER WAKE .

CHIMWEMWE NI BONDIA HATARI SANA NA TUNAZO  CD ZAKE NI LAZIMA ATAMUUMIZA CHEKA NIVYO KUVURUGA PAMBANO HILI KUBWA.

TUNAOMBA TUUNGANE WATANZANIA WOTE KATIKA KUFANIKISHA PAMBANO HILI KWA MANUFAA YA MABONDIA WETU KIMATAIFA.
 
IMELETWA KWENU NAMI;-
YASSIN ABDALLAH MWAIPAYA -USTAADH
RAIS - TPBO-LIMITED

Bint Mfalme wa Saudia akamatwa kwa unyanyasaji

 
MWANAMKE mmoja anayetajwa kuwa Binti wa Mfalme wa Saudi Arabia, Meshael Alayban, 42, amekamatwa katika jimbo la Carlifonia nchini Marekani na kutuhumiwa kuhusika na biashara ya watu.
Bi Alayban anakabiliwa na mashtaka ya kumlazimisha mama mmoja kutoka Kenya kufanya kazi kwa zaidi ya saa kumi na sita kila siku, na kumlipa kiasi kidogo cha pesa kuliko walivyokuwa wameafikiana.
Utawala wa eneo hilo, umesema kuwa bint mfalme huyo alichukua pasi ya kusafiria ya mama huyo, hatua iliyomfanya atoroke.
Mawakili wa mtuhumiwa huyo wametaja kesi hiyo kuwa mzozo kuhusu hali ya utendaji kazi.
Novemba mwaka uliopita, wapiga kura katika jimbo la Carlifonia, waliidhinisha sheria kali dhidi ya watu watakaopatikana na hatia ya kuhusika na ulanguzi wa watu.
Ikiwa atapatikana na hatia, Bi Alayban, huenda akahukumiwa kifungo cha miaka kumi na miwili gerezani, adhabu ambayo ni asilimia mia moja zaidi kuliko ilivyokuwa kabla ya wapiga kura kuidhinisha mageuzi sheria hiyo mpya.
Waendesha mashtaka wanasema Bi Alayban, ni mmoja wa wake sita wa Mwana Mfalme Abdulrahman bin Nasser bin Abdulaziz al-Saud, mmoja wa wanawe wa kiume wa familia moja ya kifalme nchini Saudi Arabia.

Mama huyo kutoka Kenya ambaye jina lake halijatolewa, aliajiriwa na Bi Alayban miaka miwili iliyopita, baada ya kusaini mkataba na shirika moja la kutoa uajiri nchini Saudia.
Mkenya huyo aliahidiwa kulipwa dola 1,600 kila mwezi na kuwa atafanya kazi kwa saa nane kila siku kwa siku tano.
Hata hivyo, Bi Alayban amekuwa akimlipa dola 220 kwa  mwezi na kulazimishwa kufanya kazi kwa zaidi ya saa 16 kila siku.
Mama huyo amedai, kupokonywa pasi yake ya kusafiria na alikabidhiwa muda mfupi tu kabla ya wao kusafiri kwenda Carlifonia na Bi Alayban.
Akiwa Carlifonia, alilazimishwa kufanya majukumu mengi zaidi ya nyumbani kwa familia ya watu wanane waliokuwa katika vyumba vinne tofauti, ambako amedai alizuiliwa mateka.
Wakati alifanikiwa kutoroka, alisimamisha basi moja na kwenda moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
Bi Alayban alikamatwa siku ya Jumatano na kufikishwa mahakamani juzi Alhamisi.
Aliachiliwa huru kwa dhamani ya dola milioni tano na kuamriwa kurejesha pasi ya kusafiria ya amama huyo kutoka Kenya.
Aidha Bi Alayban sasa atavalia chombo maalum ambacho kitatoa maelezo ya mahala aliko na hataruhusiwa kuondoka Marekani hadi kesi hiyo itakapokamilika.
Viongozi wa Mashtaka walitaka jaji kumuachilia kwa dhamani ya dola milioni 20 au anyimwe dhamana kwa kuwa yeye ni tajiri mkubwa na aweza kutoweka.

Emirates hosts Iftar celebrations in Tanzania



Emirates Country Manager for Tanzania Abdulaziz Al Hai speaking to the Media during the Iftar dinner last evening in honour of its trade partners and the Media at the Hyatt Regency Dar es Salaam, the Kilimanjaro.
Emirates, one of the world’s fastest growing airlines, hosted Iftardinner last evening in honour of its trade partners and the media at the Marquee Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kiimanjaro.

Speaking at the event, Emirates Country Manager for Tanzania Abdulaziz Al Hai thanked the Government of Tanzania, trade partners and the media for their outstanding and continuous support to the airline.

“Ramadan is a period of sharing and we are pleased that each one of you found time to join us as we celebrate Iftar,” said Al Hai. 
Our services in Tanzania have gone from strength to strength over the last 15 years and we owe our success to the very important partnerships we have with our trade partners, our loyal customers, as well as the media. This event is an amicable opportunity for us to show our appreciation for your vital role in the growth of Emirates in Tanzania. I am confident we can always count on your assistance going forward.”

He noted that the provision of excellent in-flight service and entertainment, ongoing network expansion and focus on developing innovative ways to improve customer comfort and convenience have been key in driving  success for Emirates in Tanzania.

“Our modern and convenient Dubai hub enables our customers to seamlessly connect to our ever-expanding global network,” Al Hai said. 

Emirates established operations in Tanzania in 1997. Currently, the airline flies daily from Julius Nyerere International Airport (JNIA) to Dubai, connecting passengers to 134 destinations in 77 countries across six continents.

EK 725 departs Dubai International Airport every day at 1015hrs and arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam at 1455hrs. The return flight leaves JNIA at 1645hrs and lands in Dubai at 2320hrs every day.  
More information on offering conditions and bookings can be obtained fromwww.emirates.com/tz

'TAIFA STARS SASA YAIVA KWA MAPAMBANO'

Rais wa TFF, Leodger Tenga
Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema kikosi cha Taifa Stars sasa kina uwezo wa kushindana katika mashindano yoyote, kwani tayari kimeiva.

Akizungumza na wachezaji wa timu hiyo kambini kwao hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam, Rais Tenga aliwaambia kuwa kiwango walichoonesha kwenye mechi zilizopita za mchujo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast kimethibitisha hilo.

“Kiwango mlichoonyesha katika mechi hizo kila Mtanzania anayewafuatilia amekiona, hivyo hatuna shaka kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya kesho (leo) dhidi ya Uganda,” amesema Rais Tenga na kuwataka kupigana kwa ajili ya Tanzania.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager leo (Julai 13 mwaka huu) saa 9 kamili alasiri Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itacheza na Uganda (The Cranes) katika mechi ya kwanza ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Rais Tenga amesema TFF, mdhamini Kilimanjaro Premium Lager, Kamati ya Ushindi na Watanzania kwa ujumla wanawaunga mkono kwani wamekuwa wakiboresha kiwango chao kila wanavyozidi kucheza mechi tangu wake chini ya Kocha Kim Poulsen, Mei mwaka jana.

Wakati huo huo, Rais Tenga ameahidi kumpatia tiketi ya kwenda Uganda kwenye mechi ya marudiano mshabiki Wiseman Mwakyusa Luvanda anayetembea kwa miguu kutoka Mbeya kuja Dar es Salaam kushuhudia mechi ya leo.

“Kama ni kweli anakuja kwa kutembea, huyu ameonyesha kiwango kikubwa cha uzalendo kwa timu ya Taifa, nitampatia tiketi ya kwenda Kampala kuishangilia Taifa Stars kwenye mechi ya marudiano,” amesema Rais Tenga.

…POULSEN, MICHO WATABIRI MECHI KALI

Makocha wa timu hizo Kim Poulsen wa Taifa Stars na Sredojvic Micho wa The Cranes wamesema mechi ya leo itakuwa ngumu kwa vile kila mmoja amejiandaa kuhakikisha anafanya vizuri.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari jana, makocha wote waliezea ubora wa wapinzani wao, lakini wakasisitiza kuwa wanaingia uwanjani kuhakikisha wanashinda ili kujiweka katika mazingira mazuri kwa ajili ya mechi ya marudiano itakayochezwa Kampala wiki mbili zijazo.

Kim alisema Uganda ndiyo inayoongoza kwa ubora wa viwango vya FIFA katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, hivyo ni changamoto kwao ingawa wachezaji wake tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo.

Naye Micho aliyefuatana na nahodha wake Hassan Wasswa alisema Taifa Stars imekuwa ikifanya vizuri tangu iwe chini ya Kim, na itakuwa na wachezaji tisa wa kikosi cha kwanza kinachocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia wakati kwa upande wake atakuwa na wachezaji wawili tu.

WAKAZI WA TABORA WACHANGAMKIA MCHEZO WA POOL

Mchezaji wa Omari Azizi wa timu ya Pool ya Texas- Tabora akijiiweka tayari kupiga mpira wakati wa mazoezi ya klabu yao iliyofanyika mkoani hapo jana.

Mchezaji wa Texas Pool Mkoa wa Tabora Salum Kazuga akijitayarisha kupiga mpira wakati wa mazoezi ya klabu yao.

Mchezaji wa klabu ya Pool ya Texas-Tabora Shabani Ramadhani akijiandaa kupiga mpira wakati wa mazoezi ya timu yao iliyofanyika mkoani hapo jana.

Mchezaji wa Klabu ya Pool ya Texas ya Mkoa wa Tabora Hassani Sasi akijitayarisha kupiga mpira wakati wa mazoezi ya klabu yao iliyofanyika mkoani hapo.

Friday, July 12, 2013

Hussein Javu sasa njia panda

Hussein Javu akiwa katika pozi
MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Mtibwa Sugar, Hussein Javu amekiri kwamba amewahi kufuatwa na klabu za Simba na Yanga kwa nia ya kumsajili, lakini hadi sasa hajui kinachoendelea kuhusu majaliwa yake msimu ujao.
Javu alisema hata taarifa kwamba amesajiliwa Yanga kwa mkataba wa miaka mitatu anazisikia tu hewani, ila ukweli suala hilo sio kweli kwa vile hajasaini mkataba wowote na mabingwa hao wa soka nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, mshambuliaji huyo aliyekuwa kinara wa mabao ndani ya Mtibwa Sugar na mmoja wa wachezaji wanaounda timu ya pili ya taifa 'Young Taifa Stars' alisema Simba na Yanga kwa nyakati tofauti walimfuata kwa nia ya kumshawishi kujiunga na timu zao, lakini  aliwaelekeza wamalizane na 'mabosi' wake.
"Unajua mimi bado nina mkataba na Mtibwa, pia klabu hii nimetoka nayo mbali hivyo sikuwa na maamuzi zaidi ya kuwataka Simba na Yanga wazungumze na uongozi wa klabu yangu na kwa msingi huo yaliyoendelea au yanayoendelea siyajui," alisema.
Kuhusu kwamba tayari keshasaini mkataba wa miaka mitatu Yanga, Javu alisema hilo halina ukweli kwa sababu hakuna fomu zozote alizosaini mpaka sasa na kushangaa habari hizo kusambazwa kwenye vyombo vya habari.
"Ningekuwa nimesaini ndugu yangu ningekuambia ukweli, hilo halijafanyika na wala sijajua kinachoendelea au kujua kama msimu ujao nitacheza Mtibwa, Yanga au Simba," alisema.
Aliongeza kuwa, yeye kama mchezaji anasubiri kusikia maelekezo ya viongozi wake kama wameafikiana na Yanga au Simba na wangetaka kumuuza hatakuwa na tatizo na kama wataamua kumbakisha Mtibwa Sugar kwa msimu mwingine pia kwake ni sawa tu kwani anafurahia maisha katika klabu hiyo ya Manungu.
"Nikibakishwa Mtibwa Sugar au kuuzwa Yanga au Simba poa mradi masilahi yawepo kwani soka ndiyo ajira yangu na siwezi kuchagua mahali pa kwenda," alisema.
Dai la kwamba yeye ni majeruhi wa kudumu wa goti, Javu alisema taarifa hizi zinalengo la kumharibia kwani hajawahi kuumia kwa siku za karibuni na kushangaa wanaompakazia uzushi huo.
Alisema anadhani wanaomzushia wanafanya hivyo kwa minajili ya kukomoana baina ya Simba na Yanga ambao wamekuwa na mvutano wa kumwania mara baada ya ligi kuu msimu uliopita kumalizika.

Mwanafunzi atekwa, azirai saa 14 Mbeya

 Kijana Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba mkazi wa Mama John kata ya Ilomba Jijini Mbeya ambaye alitekwa  akiwa akiwa anapelekwa uwani
 Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba  akiwa ameshikiliwa
 Majirani wakiwa wanasubiri kusikia kutoka kwa Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba
 Mama mzazi wa Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba Vumilia Komba akiwa anatoka kumtazama mtoto wake
 Vumilia Komba mama mzazi wa mtoto akiwa anataka kuulizwa maswali
 Mama mzazi wa kijana huyo Vumilia Komba  akihojiwa na waandishi wa Habari
 Ndugu jamaa na Marafiki pamoja na mzazi wa mtoto wakiwa wanatoa vitu vya mwanafunzi huyo
 Shati hili lilikuwa limechanwa ambalo ndilo lilitumika kuchanwa  na kumfunga mikono na kumziba mdomo


 Nguo pamoja na Viatu alivyokuwa amevivaa muhanga   wa tukio



Mjomba wa muhanga Kasian Mwezi Komba

Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba akifanya mazoezi baada ya kufikishwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya

Emanuel Komba umri wa miaka (15)  kidato cha kwanza Shule ya sekondari Ilomba  akiwa amepata fahamu na kuelezea kisa kizima



Wakiondoka katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya baada ya matibabu 

PICHA NA MBEYA YETU

Man City yapania kumnasa Ronaldo

http://i2.mirror.co.uk/incoming/article1867031.ece/ALTERNATES/s615/Cristiano-Ronaldo-1867031.jpg
Ronaldo
MANCHESTER, England
MANCHESTER City wameamua kuvunja benki kwa nia ya kumshawishi mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo atue katika uwanja wa Etihad katika kipindi hiki cha usajili.
Na wameiambia kambi ya Ronaldo kwamba wamejiandaa kuipiku ofa kutoka kwa Manchester United, jambo linalomaanisha kwamba wako tayari kumlipa mshahara wa zaidi ya paundi 300,000 (Sh. milioni 709) kwa wiki.
Man U wametumia miezi mitano iliyopita kujaribu kuandaa dili la kumrejesha Old Trafford nyota huyo mwenye umri wa miaka 28, na Ronaldo mwenyewe ameshaonyesha kwamba bado timu hiyo iko moyoni mwake.
Man City wanatambua kuwa jambo hilo ni kiunzi kigumu kuruka, lakini mkurugenzi mtendaji wao Ferran Soriano na mkurugenzi wa soka Txiki Begiristain wote wamewaambia mawakala wa mchezaji huyo kwamba wako 'siriasi' sana na uhamisho huo.
Na wameweka wazi kwamba kama Real watakuwa tayari kumuachia Mreno huyo aondoke, watafanya kila liwezekanalo kuwapiku mahasimu wao Man U.
Mwenyekiti wa Man City, Sheik Mansur ameweka wazi kwa Soriano kwamba kama Ronaldo ataingia sokoni, City ni lazima wafanye chochote kinachowezekana kuhakikisha wanamsajili.
Ronaldo amebakisha miaka miwili katika mkataba wake Hispania, lakini licha ya kusema hadharani kwamba anakaribia kusaini mkataba mpya, Real bado hawajampa ofa yoyote ya mkataba mpya.
Jambo hilo linawaongezea matumaini Man U kwamba wanaweza kumnasa, ingawa mipango hiyo mipya ya Man City inaleta presha mpya Old Trafford.
PSG ndiyo klabu pekee ambaye kufikia sasa iliwasilisha ofa ya paundi milioni 55 ambayo Real waliikataa.
Klabu hiyo ya Ufaransa inajiandaa kumlipa pesa nyingi zaidi, lakini Ronaldo anafahamika kwamba anavutiwa zaidi kurejea Uingereza kama ataondoka Bernabeu.