STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 21, 2013

Masogange, Melisa waachiwa huru hatimaye

http://api.ning.com/files/It3-odgnrfRW80PWalq53lRwVSPptJtp*DOsLRl-yTPt24Tlnfb-fOv0Dzh6ppWTIjHud9Q--mi-9R3wu5ArUT7KY4Lt9FlD/MASOGANGE.jpg?width=450
Masogange
WATANZANIA wawili Agness Gerard ‘Masogange’ na Melissa Edward wameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg baada ya kutakiwa kulipa faini ya Sh 4.8 milioni (Randi 30,000) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumiwa kutengeneza dawa za kulevya.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini (hawk) Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo mahakama ilibaini kuwa Melissa hana hatia kwa kuwa ilionekana amemsindikiza Masogange, aliyemuomba amsaidie kubeba mzigo huo.
Mosagange alilipa faini ya Shilingi 2.5 milioni (R15, 000), huku akiahidi kumaliza nusu yake ambayo juhudi zilikuwa zinafanyika amalize kulipa jana Ijumaa.
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu kusaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini haikuwa mizigo yake. Mizigo yote iliandikwa jina la Agness Masogange na si Melissa,” alisema Kapteni Ramaloko.
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa amesafiri na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na Masogange alimuomba amsaidie mizigo hiyo kwani ilikuwa mikubwa.
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba kemikali zozote ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria hivyo mahakama iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela miezi 30 (miaka miwili na miezi sita) au alipe faini ya R30, 000(Sh 4.8 milioni).
Hata hivyo alilipa faini na nusu ya fedha hizo ilishalipwa na nyingine ilikuwa inakaribia kulipwa.
Ingawa Kamishana Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa juzi Alhamisi alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni dawa za kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS) Marika Muller, alieleza kuwa timu ya SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5, mwaka huu ni methamphetamine.

MWANASPOTI

Amani Simba aanza tambo Ashanti United

Amani Simba
KIPA mpya wa Ashanti United, Amani Simba ametamba kwamba bado muda mfupi tu kabla ya mashabiki wa soka kuikubali timu yao ambayo imeanza vibaya Ligi Kuu Tanzania Bara kiasi cha kuruza mkia katika msimamo wa ligi hiyo.
Aidha kipa huyo alisema ni mapema mno kuanza kuitabiria ligi ya msimu huu kwa sababu anaamini lolote linaweza kubadilika kwa sasa kutpkana na ukweli ligi ndivyo kwanza ipo raundi ya nne kwa sasa.
Simba aliyeidhinishwa hivi karibuni na TFF kuidakia timu hiyo baada ya kuitema timu aliyoipandisha daraja ya Mbeya City, alisema Ashanti inasumbuliwa na ugeni wa ligi, ila kadri siku zinavyosonga mbele wachezaji wataizoea na kutisha.
Kipa huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Moro United, Simba na Taifa Stars alisema ni mapema mno kuanza kuihukumu Ashanti na matokeo iliyopata kwa sasa kwa sababu ligi bado mbichi na wachezaji wao wanaendelea kuizoea ligi hiyo.
"Ni mapema mno kuijadili Ashanti, naamini muda mfupi ujao wanayoibeza wataikubali baada ya kuanza kupata matokeo mazuri, unajua ugeni wa ligi ndiyo tatizo lakini kadri siku zinavyoenda mbele wachezaji wanaondoa woga," alisema.
Simba, aliyewahi pia kuzidakia Lipuli Iringa, Prisons Mbeya na JKT Ruvu, alisema akishirikiana na wenzake watahakikisha Ashanti inafanya vyema katika mechi zilizopo mbele yake.
Ashanti United inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa pointi moja ni kati ya timu tatu zilizopanda Ligi Kuu msimu huu, nyingine zikiwa ni Mbeya City na Rhino Rangers ya Tabora.

Gaucho bado aliota soka la kulipwa

http://api.ning.com/files/Z311HW*8BLsTaHW*p4y9dVjDgbR8cx2tskdyBtk0ZluRwicT9*Nf2fkCQ3unhX6sg*ce5TuwMHaY4TPmDCzkUwHTqR41EqDZ/GLOBALHUMUD.jpg?width=351
Gaucho
KIUNGO nyota wa klabu ya Simba, Abduhalim Humud 'Gaucho' amesema bado hajakata tamaa na mipango ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi hata baada ya mipango ya kwenda nchini Afrika Kusini kukwama.
Akizungumza na MICHARAZO, Gaucho, aliyerejea tena Simba akitokea Azam aliyoichezea msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema japo ametuliza akili zake kuitumia kikamilifu Simba, bado analiwaza soka la kulipwa.
Gaucho, alisema bado ana kiu kubwa ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi na imani yake siku yoyote ataenda nje ksa kuamini ana kipaji na uwezo wa kucheza soka kokote akipata fursa hiyo.
"Sijakata tamaa na soka la kulipwa, bado naamini ipo siku nitaenda nje kwa uwezo wa Muingu kwani yeye ni Muweza na Mpangaji wa kila jambo," alisema Gaucho nyota wa zamani wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars.
Hata hivyo Gaucho aliwataka viongozi swa soka nchini kuepukana hali ya kibabaishaji na tabia za kuwawekea kauzibe wachezaji wanapopata nafasi ya kwenda nje ya nchi kusakata kandanda akidai ni faifa kwa taifa.
Mapema mwaka huu Gaucho alifaulu majaribio yake ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Jomo Cosmos ya Afrika Kusini, lakini wakati akiwa katika maandalizi ya kuondoka alitangaza ghafla kutua klabu ya Simba.
Hata hivyo alinukuliwa katika mahojiano na kituo kimoja cha redio kwamba klabu yake ya zamani ya Azam ndiyo iliyomwekea vikwazo kabla ya uongozi wa Azam kukanusha taarifa hizo na kutangaza kuachana naye.

Ile Ile atoa Wazazi akijipanga upya

Msani Ile Ile katika pozi
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya, Maishani Ndee 'Ile Ile' ameachia kibao kipya kiitwacho 'Wazazi' ukiwa ni wimbo wake wa tatu tangu atumbukie kwenye fani hiyo miaka minne iliyopita.
Wimbo huo na video yake umeanza kuwa gumzo kwenye vituo vya redio na runinga kutokana na maudhui wake na Ile Ile alisema amefarijika na anajipanga kuandaa kazi nyinginje mbili kwa mpigo.
Ile Ile aliyewahi kukimbiza na nyimbo za 'Ileile' alioutoa mwaka 2010 na 'Bora Twende' wa mwaka jana alisema nyimbo ambazo zitafuata baada ya 'Wazazi' ni 'Amani na Upendo' na 'Sheila'.
"Hizi zimeshakamilika kila kitu na wakati wowote naziingiza studio kuzirekodi ili kuendelea kuwapa burudani mashabiki wangu na muziki kwa ujumla," alisema Ileile anayejishughulisha na biashara za nguo na hasa lebo yake ya Ile Ile Wears.
Msanii huyo mwenyeji wa Kondoa, alisema angetamani kutoa albamu yake ya kwanza, lakini soko la muziki kwa sasa nchini linamtisha na hivyo anaona bora aendelee kurtoa 'singo' moja moja na video zake ili kujitengenezea mazingira mazuri ya kupata shoo zitakazomuingiza pato la kutosha.

Steve Nyerere 'ala shavu' kifo cha Baba wa Taifa


MSANII wa filamu nchini, Steve Mangendela 'Steve Nyerere' amepata shavu la kutangaza kwa kutoa hotuba mbalimbali za baba wa taifa zitakazokuwa zikirushwa hewani na  Luninga ya TBC mpaka siku ya kilele cha kifo cha hayati Baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Hotuba hizo ambazo zilikuwa zikitolewa na baba wa Taifa sasa Steve Nyerere atakuwa akizitoa kwa kuiga sauti hile hile
Msanii huyo aliyejizolea umaarufu kwa kuiga sauti za viongozi mbalimbali nchini na Duniani kwa ujumla amekuwa akipendwa na wengi kutokana na kuiga sauti ya hayati Baba wa Taifa na kufanya kuchukua jina lake moja kwa moja ambapo kwa sasa popote uendapo uwezi kumwita kwa jina la Steve bali lazima useme Steve Nyerere
Kwa sasa ameingiza kazi yake mpya mtaani inayojulikana kwa jina la Before Wedding ambayo ipo mtaani ikisambazwa na kampuni ya Steps Entatainment ya jijini Dae rs salaam

Bendera 'akiuma' sikio' chama cha Pool kuhusu TBL



 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera(wa pili kushoto), Meneja wa wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa(TAPA), Fred Mushi na Katibu wa chama cha Pool Taifa , Amos Kafwinga wakiwa katika maandamano ya ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari National Pool Championships.
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera (wa tatu kushoto) akipigiwa makofi mara baada kufungua rasmi fainali za mashindano ya Safari National Pool Championship 2013 Mkoani Morogoro. Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Chama cha Pool Taifa(TAPA), Amos Kafwinga, Makamu Mwenyekiti wa chama cha Pool, Fred Mushin a Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.


 Baadhi ya wachezaji wa Pool kutoka mikoa 17 ikiwakilisha na vilabu 17 nchini wakiwa katika maandamano kuelekea katika Ukumbi wa Tanzanite Morogoro wakati wa ufinguzi wa fainali za kitaifa za Safari National Pool Championships.
 Top Land- Mkoa wa kimichezo wa Kinondoni Dar es Salaam






 Mdhamini Mkuu wa mashindano ya Safari National Pool Championships, Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo(wa tatu kushoto), Mwakilishi wa TBL Morogoro, Julius Ngaga(wa nne kushoto), Mwenyekiti wa chama cha Pool Mkoa wa Iringa, Salum Kisaku (wa pili kushoto) na Mwamuzi wa kike pekee, Vaileth Mrema (kushoto)  na baadhi ya wachezaji wakiwa katika maandamano ya ufunguzi wa fainali za Pool Taifa Mkoani Morogoro.
 Na Mwandishi Wetu.
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, amewaasa chama cha Pool Taifa(TAPA), kumkumbatia mdhamini mkuu  wa mhezo wa Pool Taifa, “Safari Lager” kupitia Kampuni kubwa nchini Tanzania Breweries(TBL).
Bendera aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa fainali za mashindano hayo yanayoyofanyika kitaifa Mkoani Morogoro ambapo yeye alialikwa kuwa mgeni rasmi.
Alisema Bendera, vipo vyama vya michezo vingi vinashindwa hata kufanya mashindano kwa mwaka lakini Pool ni mwaka wa sita sasa mnafanya, vipo vyama vingi vya michezo vinalia kwanini mpira wa miguu peke yake ndio unapata udhamini lakini Pool ni mwaka wa sita sasa mnaye mdhamini na bado mnaendelea nae na baada ya hapa anaipeleka timu ya Taifa kwenye mashindano ya Afrika ya mchezo wa Pool.
Mchezo wowote  ili ukue na kutambulika nchini na Duniani unaanza na mchezaji mwenyewe kuupenda na kuufanya kutoka moyoni kwa kujiheshimu kwanza mwenyewe na kuuheshimu mchezo ndipo hata jamii huudhamini (Self displine and Tactical displine).
Alisema Bendera yeye kama mdao na mzoefu kwenye tasnia ya michezo na mpaka sasa anashikiria sifa kemkem ambazo hazijawahi kutolewa kwenye rekori anauzoefu wa kutosha na maswala ya michezo, siri ya maendeleo katika michezo ni nidhamu pekee na si vinginevyo.
Mtazamo wa mchezo wa Pool katika jamii siku kadhaa hapo nyuma ulionekana kama mchezo wa kihuni lakini leo mmebadilisha taswira hiyo na sasa mko kwenye mikoa 17 ikiwakilisha na vilabu 17 mkiunganisha na mchezo wa Pool mkiwa mkoani Morogoro katika fainali za kitaifa, hongereni sana TAPA.
Mkuu wa Mkoa pia aliipongeza TBL kupita bia ya Safari Lager kwa kuendelea kudhamini mchezo wa Pool na sasa ni mwaka wa sita ambapo aliomba waendelee kudhamini kwani mchezo huu unaunganisha vijana wengi Tanzania kwa hapo walipofikia kwenye mikoa 17,unaepusha mambo mengi maovu ambayo wangekumbana nayo hawa vijana ni zaidi ya vijana 300 wamekutana Mkoa wa Morogoro na kilicho wakutanisha ni mchezo wa Pool.Endeleeni kudhmini mchezo wa Pool kwani kwa sasa michezo ni afya, michezo ni upendo,michezo ni urafiki,michezo ni matangazo na michezo ni afya.
Bendela aliwakaribisha wote Mkoani Morogoro na kuwaomba wawe na amani kwani Morogoro ni shwari kabisa hewa nzuri baridi kiasi.
Nae Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kujitokeza kufungua fainali hizo na kuahidi lengo la Safari Lager na kuufanya mchezo wa Pool kuwa mchezo namba moja kama ilivyo Safari Lager bia namba moja Afrika hivyo wataenelea kudhamini mashindano ya Pool daima.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa, Fred Mushi alimsukuru mdhamini Safari Lager kuendelea kuwadhamini na pia kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa changamoto alizozieleza za kumlinda mdhamini na kuahidi wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wao kuwaweka sawa vijana kuhakikisha mchezo wa Pool unakuwa chezo namba moja nchini na Afrika kama bia ya Safari Lager.


 Katibu wa Chama cha Pool Taifa, Amos Kafwinga akizungumza.
 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo. akizungumza
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool, Fred Mushi akizungumza
 Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akizungumza

Friday, September 20, 2013

Shafii Dauda achimba mkwara mzito, kisa...!

Shafii Dauda
MCHAMBUZI maarufu wa soka nchini, Shafii Dauda ameuchimba mkwara uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unaodaiwa kutaka kuendelea kumwekea mizengwe katika kuwania uongozi ndani ya shirikisho hilo.
Dauda, ambaye ni miongoni mwa wagombea waliokuwa wameondolewa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa TFF utakaofanyika mwezi ujao na kurudishwa na kamati ya Maadili ametema cheche hizo kupitia akaunti ya Facebook.
Mwanamichezo na mtangazaji huyo, amelazimika kuchimba mkwara huo baada ya kusisikia fununu za kutaka kuwekewa zengwe kama ilivyowahi kusikia awali na kujikuta kweli jina lake likitupwa kwa madai ambayo hayakuonekana kama ana hatia.
Dauda ameomba kugombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, ambapo jina lake la wenzake kadhaa yalitemwa kabla ya Kamati ya Maadili ya TFF chini ya Jaji Jesse Mguto kuwarejesha tena kuendelea na mchakato wa uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba 27.
Ebu isome mwenyewe ujumbe huo, ingawa kuna baadhi ya sarufi tumezirekebisha ili ziende sawia la lugha fasaha ya kiswahili;
"Siku chache za nyuma nilizisikia njama za baadhi ya viongozi wa TFF kutaka kuondoa jina langu kwenye mchakato wa uchaguzi wa TFF na kulipeleka kwenye kamati ya Maadili eti nili-publish barua ya FIFA kwenye blog yangu bila idhini yao, nikazipuuzia nikidhani ni stori tu za mitaani,muda ulipofika Taarifa ya TFF ikatoka kweli jina langu likapelekwa kwenye kamati ya Maadili kwasababu zile zile nilizozisikia kabla kwa watu,Kamati ya MAADILI ikaniita nikayasikiliza mashitaka ya Secretarieti ya TFF ambayo iliwakilishwa na Afisa Habari ndugu yangu Boniface Wambura ikanihoji namimi nikatoa utetezi wangu na hatimaye kamati ikaonelea sina kesi ya kujibu hivyo basi jina langu likarudishwa kwenye mchakato wa uchaguzi. Kutoka kwenye vyanzo vyangu mbali mbali ndani ya TFF eti sasa wanajipanga kesho kutoa PRESS ya kuliondoa tena jina langu eti kwa kigezo sina UZOEFU,sasa ninachowambia kama ni kweli yanayozungumzwa WASITHUBUTU kufanya hivyo kwani kwa mara nyingine tena watanipa pointi 3 za mezani.IJUMAA KAREEM!

Simba, Mbeya City uso kwa uso, Mtibwa yaifuata Prisons Mbeya, kivumbi za FDL nacho mmh!

Mbeya City
Simba
Na Boniface Wambura

BAADA ya kuifanyia mauaji ya kutisha Mgambo JKT, vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara,Simba kesho itaikaribisha Mbeya City ambayo iliyozidindia Yanga na Mtibwa Sugar katika mechi zake mbili zilizopita.
Simba itaialika Mbeya City iliyopanda daraja msimu huu kwenye dimba la Taifa ikiwa ni muendelezo ya michezo ya ligi kuu (VPL) inayopingia raundi yake ya tano ambapo pia itashuhudiwa michezo mingine mitatu tofauti.

Uwanja wa Mkwakwani, Tanga utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting Stars na Rhino Rangers ya Tabora. Mtibwa Sugar itakuwa mgeni wa Tanzania Prisons katika pambano litakalochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.


Nayo Kagera Sugar itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake wa Kaitaba mjini Bukoba kuvaana na Ashanti United ya Dar es Salaam katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo kutoka Mara.


Ligi hiyo itakamilisha mzunguko wa tano keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) kwa mechi tatu ambapo Azam na Yanga zitacheza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku JKT Ruvu ikikwaruzana na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Azam Complex.


Ruvu Shooting inayokamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi itakuwa mgeni wa Coastal Union katika mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Wakati huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaendelea wikiendi hii kwa mechi kumi na moja. Kundi A kesho (Septemba 21 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Transit Camp na Green Warriors (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam), Tessema na African Lyon (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi).


Ndanda itacheza na Villa Squad kwenye Nangwanda Sijaona mjini Mtwara wakati keshokutwa (Septembe 22 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Polisi Dar es Salaam na Friends Rangers katika Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.


Kundi B kesho (Septemba 21 mwaka huu) ni Mkamba Rangers dhidi ya Burkina Faso kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, na Mlale JKT itakuwa mwenyeji wa Kurugenzi Mafinga kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea. 
Keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) ni Majimaji na Kimondo katika Uwanja wa Majimaji.


Mechi za kundi C kesho (Septemba 21 mwaka huu) ni Pamba dhidi ya Polisi Dodoma (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Stand United na Polisi Tabora (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) na Kanembwa JKT itacheza na Mwadui kwenye Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji. 
Keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) Polisi Mara na Toto Africans zitacheza Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

NSSF YAIPIGA JEKI' ROCKY CITY MARATHON 2013

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini BMT, Dioniz Malinzi akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa mbio za Rocky Marathon.  
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky City Marathon uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo NSSF imedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Suleima Nyambui.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky Marathon 2013 Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, akizindua rasmi mbio za Rocky City Marathon 2013 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu ambao wamedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
 Baadhi ya wadau.
Picha ya pamoja.
MSIMU wa tano wa mbio za Rock City Marathon umezinduliwa, ambapo mdhamini mkuu Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetaka kuwepo kwa mgawanyo wa majukumu kwa mbio za umbali tofauti ili kuharakisha uendelezaji wa vipaji vya wanariadha nchini.

Rock City Marathon zinaratibiwa na Kampuni ya Capital Plus International (CPI), ambapo Ofisa Uhusiano wa NSSF inayodhamini mbio hizo kwa mwaka wa nne sasa, Juma Kintu aliliomba Shirikisho la Riadha Tanzania RT kugawana majukumu na wadau.

“Sisi kama NSSF tuko tayari kudhamini na kuchangia maendeleo ya riadha nchini, ndio maana tunasisitiza mgao wa majukumu kwa wakimbiaji wa umbali fulani kusimamiwa na taasisi au kampuni moja, ili kusaidia maendeleo ya haraka na makuzi sahihi ya vipaji,” alisema Kintu.

Pamoja na NSSF, wadhamini wengine wa Rock City Marathon 2013 zitakazofanyika jijini Mwanza Oktoba 27 ni pamoja na PPF, Airtel, African Barrick, Nyanza Bottlers, Sahara Media, Precission Air, Bank M, New Mwanza Hotel na Umoja.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, aliyekuwa mgeni rasmi, alisema mchezo wa riadha nchini unaelekea kuangamia na jitihada za kuunusuru zinahitajika.

“Ni aibu kuwa mchezo wa riadha nchini unaelekea kufa wakati viongozi waliopewa mamlaka ya kuhakikisha unaendelea wanashuhudia. Ni wakati wa kuamka kuunusuru mchezo huu ambao katika miaka ya 1970 mpaka 1980 uliiletea nchi yetu heshima kubwa.

Kwa upande wake, Rais wa RT, Suleiman Nyambui aliwataka waratibu wa marathon kote chini kuhakikisha wanakuwa na mbio fupi za vijana ili kupanua wigo wa kuzalisha vipaji vipya, vitakavyoliletea sifa taifa na kushinda mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Naye Mgurugenzi Mtendaji wa Capital Plus, Ellen Otaru Okoedion, aliishukuru Serikali kwa ahadi ya ushirikiano, lakini akaitaka kuhakikisha inakaa mezani na (kina Nyambui) RT, ili kujadili njia sahihi zitakazofanikisha kupatikana kwa kina ‘Nyambui wapya.’

Aidha, Mratibu wa tukio hilo, Mathew Kasonta alisema kuwa mbio hizo zitajumuisha  kilometa tano kwa wakimbiaji kutoka katika makampuni, kilometa tatu kwa wenye ulemavu, kilometa tatu kwa watu wazima (zaidi ya miaka 55) na kilometa mbili kwa watoto wenye umri kati ya miaka 7 mpaka 10.

Msiba tena! Mwanajeshi mwingine wa Tanzania afariki Congo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdNJZZWb0uOyOr0xkZ4jESmQ2W9lpQ7JqPz7eO55Re1lTPE9x_VB50rB3ip7BdIvmzMXuzfPSrEPHFiXk3c58fxJmXG4R96K8IghFM_XbKsy5ZG0DVK8q3OsuweCkJUla56q1Cf65TPP5V/s640/mwamnyange.jpg
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamnyange

MSIBA tena! Hizi ni habari za kusikitisha kusikia, ila ni kwamba  shujaa mwingine wa Tanzania amefariki dunia katika harakati za kulinda amani ya waafrika wenzetu. 
Habari zilizotolewa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) zinasema mwanajeshi anayetambulika kwa jina la Private Hugo Munga, ambaye alijeruhiwa kwenye shambulio lilisababisha Meja Khatibu kufariki dunia, naye amefariki.
Mwanajeshi huyo alikuwa nchini South Africa kwa ajili ya matibabu, lakini kwa bahati mbaya Tanzania imempoteza shujaa huyu. 
Mwili wake unatarajiwa kufikishwa hapa nyumbani kesho ukitokea nchini South Africa.
1j
2j

Polisi Dar wapiga marufuku maandamano ya Wapinzani, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTqetlsLeH_ScYXsPtt6WO1C0fCX-TowGb2uhPjHn6Tr5y1FeOFQlW2IKA6Gvj_SbkIxEdBwIkNjl_C_wq6S1VMWROlSa0pU8X4P2JHsx_PisWpU2abyDZBphoYSSGa0JX6_sKaf-j_NY/s1600/Kova1%252814%2529.jpg
Kamanda Suleiman Kova
JESHI la Polisi Jijini Dar es Salaam limeyapiga marufuku maandamano ya umoja wa vyama vya CUF, NCCR na CHADEMA yaliyopangwa kufanyika kesho Jumamosi.
Maandamano hayo yaliyokuwa  yamepangwa  kuanzia Tazara hadi Jangwani kisha Mwenge hadi Jangwani na sehemu mbalimbali .

Taarifa  iliyotolewa  na Kamanda Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova kupitia ITV   imeeleza kuwa Polisi wamechunguza na kugundua kwamba  maandamano  hayo  yataleta usumbufu kwa watu wengine na kwamba kwa kuwa lengo ni kufika Jangwani basi Viongozi wa vyama hivyo wawaambie wafuasi wao waende Jangwani bila Maandamano. 

Masogange aanza kufurahia 'uhuru' wa dhamana aliyopewa 'Kwa Mabida'

Mcheki katika picha hizi alizotupia leo mtandaoni



Picha hizi Amezipiga akiwa Gym leo asubuhi zinazidi kutoa ushahidi kuwa yupo Mtaani ...au jela za South Mambo ndio hivi ? We unasemaje?

Waziri Mukangara mgeni rasmi Redd's Miss Tanzania

Vimwana wanaotarajiwa kuchuana kesho kwenye shindano la Redd's Miss Tanzania 2013
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika shindano la urembo la taifa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2013' litakalofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar se Salaam.
Gazeti la kila siku la NIPASHE linalochapishwa na Kampuni ya The Guardian Ltd ni miongoni mwa wadhamini wa shindano hilo litakalotoa mwakilishi wa nchi katika fainali za Urembo za Dunia (Miss World).
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga, alisema jana wanatarajia  kiongozi huyo wa serikali kushuhudia shindano hilo na kwamba amesharidhia kuwa mgeni rasmi.
Lundenga alisema kila kitu kimekamilika na kuwataka wadau wa sanaa ya urembo kusubiri kushuhudia shindano lililo bora zaidi ya miaka iliyopita.
"Maandalizi yamekamilika na kama ni chakula, sasa kinachosubiriwa ni kukila tu," alisema kwa kifupi mratibu huyo ambaye kampuni yake imekuwa ikiandaa shindano hilo tangu 1994.
Alisema shindano hilo litapambwa na burudani kutoka kwa mshindi wa tuzo ya mwanamuziki bora wa kike nchini, Judith Wambura 'Lady Jay Dee' ambaye kwa sasa anatamba na vibao vyake vya Yahaya na Joto Hasira, Mike Rose wa Uganda na kikundi cha ngoma za asili cha Mama Afrika.
Shindano hilo linatarajiwa kushirikisha warembo 30 kutoka sehemu mbalimbali nchini watakaowania taji linaloshikiliwa na Brigitte Alfred, kutoka Kanda ya Kinondoni jijini ambaye kwa sasa yuko Indonea akijiandaa kupanda jukwaani kuwania taji la dunia ifikapo Septemba 28, mwaka huu.
Hata hivyo, warembo watano wameshatinga hatua ya 15 bora baada ya kutwaa mataji madogo yaliyoshindanishwa wakiwa kambini.
Warembo hao ni Severina Lwinga, kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam ambaye ni Redd's Miss Personality, Prisca Clement (Redd's Miss Tanzania Talent), Clara Bayo (Redd's Miss Sports Woman ), Happiness Watimanywa (Redd's Miss Photogenic) na Narietha Boniface ambaye ni Redd's Miss Tanzania Top Model.
Mshindi wa taji hilo mwaka huu atabeba dhamana ya kuiwakilisha nchi katika shindano la urembo la dunia mwakani na zawadi ya Sh. milioni nane pamoja na gari lenye thamani ya Sh. milioni 15.

Homa ya pambano la Man Utd, City yaanza

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01507/kompany_1507398a.jpg
Vincent Kompany
http://www.independent.co.uk/incoming/article8668976.ece/BINARY/original/wayne-rooney.jpg
Wayne Rooney


KATIKA kile kinachoonekena kama ni kuanza kupanda kwa 'homa ya pambano' baina ya wapinzani wa mji wa Manchester, Manchester United na Manchester City waachezaji wa timu hizo wameanza kutambiana.
Beki nmahiri wa Manchester City, Vincent Kompany amesema anasubiri kwa hamu kucheza dhidi ya Wayne Rooney keshokutwa Jumapili na anatumai kwamba mshambuliaji huyo wa Manchester United atakuwa katika kiwango chake cha juu.
Rooney amefunga magoli matatu katika mechi mbili tangu aliporejea katika kikosi kwa kwanza baada ya kupata jeraha la katika paji la uso lililomweka nje ya uwanja lakini nahodha huyo Man City alipuuza mitazamo kwamba anatamani kuona kiwango cha mshambuliaji huyo kinakuwa chini katika mechi yao ya mahasimu wa mji wa Manchester Jumapili.
"Hapana. Unahitaji kucheza dhidi ya wachezaji walio katika kiwango chao cha juu kabisa," aliwaambia waandishi wa habari. "Hivyo ndivyo ninavyoona. Daima nataka kucheza dhidi ya wachezaji wanaokuwa katika kiwango chao bora kabisa.
"Nina furaha sana kwa Wayne kwamba yuko katika kiwango cha juu. Huu ndiyo utamu wa Ligi kuu ya England, unacheza dhidi ya washambuliaji wakubwa wakati wote, lakini kuna wachezaji wengi wa kuchunga katika timu zote."
David Moyes na Manuel Pellegrini wanaelekea katika mechi yao ya kwanza ya watani wa jadi wa mji wa Manchester wakiwa kama makocha wa timu hizo, ingawa Mscotland huyo alishinda mechi nne mfululizo kwenye Uwanja wa Etihad baina ya mwaka 2008 na 2010 wakati akiifundisha Everton.
Lakini Kompany haamini kama matokeo hayo ya zamani yana mchango wowote katika kitakachotokea Jumapili.
"Ni timu tofauti, ni msimu tofauti na naweza kusema kwamba huwezi kutabiri matokeo ya mechi hii ya watani wa jadi," aliongeza. "Hakuna mtu aliyetabiri kwamba tungeshinda 6-1 kwenye Uwanja wa Old Trafford (katika msimu wa 2011-12), kwamba wangetufunga kwenye Uwanja wa Etihad au kwamba tungeshinda Old Trafford (msimu uliopita). Nadhani hicho ndicho mashabiki wanachopenda. Mechi isiyotabirika.
"Ni mechi ambayo daima unaisubiri. Sidhani kama watu wa mjini Manchester tu bali duniani kote wanajiandaa kufurahia mechi hiyo.
"Ni mechi ambayo inavutia kwa mengi. Sijawahi kuichukulia poa na najiona kubarikiwa kucheza katika mechi hizo. Unafanya kila uwezalo kuhakikisha unacheza vyema katika mechi hizi."
 





Tottenham, Swansea, Fiorentina 'zaua' Ulaya

Goal king: Jermain Defoe scored twice in the first half as Spurs cruised to victory
Defoe akishangilia moja ya mabao yake ya jana
Up and running: Swansea celebrate after Wilfried Bony scored the club's first European goal
Swansea City wakishangia moja ya mabao yao yalioizamisha Valencia
WAKATI Swansea wakishinda ugenini dhidi ya wenyeji wao Valencia ya Hispania, 'Vijogoo' vya Londo ya Kaskazini, Tottenham Hotspur wenyewe wameikandika Tromso kwa mabao 3-0 ikiwa nyumbani katika mechi za Ligi ndogo ya UEFA.
Valencia iliyomaliza mchezo huo ikiwa pungufu baada ya mchezaji wake Adil Rami kutolewa dakika 10 kabla ya pambano kuisha ilijikuta ikilala nyumbani kwa mabao ya Wilfried Bony, Michu na Jonathan de Guzman.
Katika mchezo wa Spurs dhidi ya Tromso, washindi walipata mabao yake kupitia Jermain Defoe aliyefunga mara mbili na jingine la Christian Eriksen.
Mechi nyingine  timu ya St. Gallen iliishinda 2 - 0 dhidi ya Kuban' Krasnodar,        Dinamo Zagreb ikalala nyumbani 2-1 mbele ya Chornomorets kama ilivyokuwa kwa PSV iliyonyukwa mabao 2-0 nyumbani na Ludogorets.
Nayo timu ya Salzburg iliisasambua Elfsborg kwa mabao 4-0, Standard Liège ikalala 2-1 kwa Esbjerg, Zulte-Waregem na Wigan zikatoka suluhu, Maribor ikalala 5-2 kwa Rubin Kazan' na Fiorentina ikashinda nyumbani 3-0 djhidi ya Paços de Ferreira.
Mechi nyingine matokeo yake ni kama ifuatavyo;
Pandurii Târgu Jiu  0-1 Dnipro Dniprop…    
Eintracht Fran…    3-0  Bordeaux    
Maccabi Tel Aviv    0-0  APOEL    
Dynamo Kyiv     0-1  Genk    
Thun     1-0  Rapid Wien    
Freiburg    2-2  Slovan Liberec    
Estoril     1-2  Sevilla    
Real Betis    0-0  Olympique Lyonnais
Vitória Guimarães   4-0  Rijeka    
Apollon     1-2 Trabzonspor    
Lazio     1-0  Legia Warszawa
Sheriff    0-0  Anzhi    
PAOK     2-1  Shakhter Karagandy    
Maccabi Haifa   0-1 AZ      

Thursday, September 19, 2013

Maskini! Watoto wa3 wa familia moja wateketea kwa moto



WATOTO watatu wa familia moja wenye umri kati ya miaka miwili na sita, mmoja wao mwanafunzi wa shule ya awali, wamekufa baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuungua moto.

Tukio hilo lililozua simanzi kubwa, lilitokea katika Kijiji cha Lushamba, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza, saa 5:00 usiku wa kuamkia Septemba 16, mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Careen Yunus, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, ingawa hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi.

Mama mzazi wa watoto hao anadaiwa kuwaacha watoto hao na kwenda kwa rafiki yake, ambaye mahusiano yao hayakutajwa.

Kitendo hicho ambacho kiliwaudhi wanakijiji na kutaka kumvamia, kumshambulia na kumuua mama huyo.

Hata hivyo, mama huyo alinusurika baada ya uongozi wa kata hiyo chini ya Afisa Mtendaji wake, Amos Mabula, kuingilia kati na kutuliza hasira za wananchi hao.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bulyaheke, Mabula, aliwataja watoto waliofariki dunia katika ajali hiyo kuwa ni Joseph Alfonce (6),  mwanafunzi wa Shule ya Awali Kanyala; sofia Alfonce (4) na Ndeva Alfonce (2).

Mama wa watoto hao, Naomi Kilembi (25), anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.

Mumewe, Alfonce Budanda, ambaye walijaliwa kuzaa watoto wanne, akiwamo mwenye umri wa miezi mitano aliyekuwa ametoka na mama yake usiku huo, wakati tukio hilo linatokea alikuwa safarini.

Mabula alisema akiwa mlinzi wa amani katika kata hiyo, baada ya wananchi kukusanyika eneo la tukio wakiwa na hasira, mama wa watoto hao alitokea, huku watoto wakiwa wameshateketea kwa moto.

Alisema kuwa alichukua hatua baada ya mama huyo kukiri mbele yake kuwa alikuwa ametoka usiku na kuwaacha watoto hao.

Awali, Diwani wa Kata hiyo, Bagesi Ngele, akizungumzia tukio hilo, alisema tabia hiyo haiwezi kuruhusiwa kuendelea.

Alisema tukio hilo lingeweza kuzuilika kama hatua zingechukuliwa kunzia kwa familia yenyewe kwani kitendo cha kuwaacha watoto peke yao huku kukiwa moto ni cha hatari ikizingatiwa ilikuwa nyumba

TFF yatoa siku 14 kuiona mikataba ya makocha VPL, FDL


Kocha wa Azam na wasaidizi wake inatakiwa mikataba yao TFF

Brandts wa Yanga na Minziro nao wanatakiwa mikataba yao itue TFF
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.


Simba, Mgambo wavuna Sh. Mil 58


Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

Baby Madaha alamba 'bingo' Kenya

Baby Madaha
Bosi Mpya wa Madaha, Joe Kariuki
MSHIRIKI wa zamani wa BSS, Baby Madaha amelamba 'bingo' baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi na kampuni na Candy n Candy Records ya nchini Kenya wenye thamani ya Sh. Mil 20 za Kenya ambazo ni sawa na Sh. Mil 50 za kitanzania.
Mbali na donge hilo, pia kampuni hiyo inayoongozwa na Mkurugenzi wake, Joe Kariuki imepa msanii huyo anayetamba kwenye fani ya muziki na filamu nchini, gari aina ya Audi TT.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema mkataba huo aliingia hivi karibuni na kampuni hiyo na tayari ameshafyatua kazi mpya kupitia kampuni hiyo iitwao 'Summer Holiday' ambao anatarajia kuizindua rasmi Oktoba 6 jijini Dar es Salaam.
Baby alisema uzinduzi huo utakaoambatana na 'party' ya kusherehekea mafanikio yake kisanii itafanyika kwenye ukumbi wa Dar Live na kusindikizwa na burudani za wasanii mbalimbali.
"Nimeingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi nchini Kenya kupitia kampuni ya Candy n Candy ambayo mbali na fedha pia wamenipa usafiri na tayari nimeshatoa kazi chini yao  iitwayo Summer Holiday iliyoanza kutamba kwenye vituo vya Channel O na MTV," alisema.
Msanii huyo aliyeibuliwa na shindano la BSS 2008, alisema anajisikia fahari kuwa msanii wa kwanza wa kike nchini kupata mkataba mnono kama huo nchini Kenya na imani yake ni mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye kilele cha mafanikio kimuziki.

Barafu, Mzee Majuto waja na Daladala pamoja na Monalisa

Kava la filamu mpya ya msanii Barafu
Barafu
BAADA ya kuwatumikia wenzake kwa muda mrefu, hatimaye msanii mahiri wa filamu, Seleman Abdallah 'Barafu' ameibuka na kazi yake binafsi iitwayo 'Daladala' inayozungumzia mikasa, vituko na kero zote zilizopo ndani ya usafiri huo wa umma.
Ndani ya filamu hiyo, mkali huyo ameigiza na wasanii wakongwe nchini kama Amri Athuman 'King Majuto', Yvonne Cherly 'Monalisa' na wengine.
Akizungumza na MICHARAZO Barafu anayefahamika pia kama 'Mzee wa Land Rover', alisema hiyo ni kazi ya kwanza kwake kuuitoa kupitia kampuni yake iitwayo 'Mtafuna Films Production' na ni 'serious comedy'.
Barafu alisema, anatarajiwa kuitoa hadharani filamu hiyo wiki mbili zijazo, na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata burudani na 'kuvunjika mbavu' kwa namna walivyoiigiza filamu hiyo na hasa vimbwanga vya Mzee Majuto.
"Kwa wale ambao wavijua vituko vya Mzee Majuto wajiandae kuumia zaidi kwa namna mzee huyo, mimi na Monalisa tulivyofanya mambo makubwa katika filamu hii ya 'Daladala'," alisema.
Barafu alisema baada ya kutoka kwa 'Daladala' ataanza maandalizi ya kazi zake nyingine kupitia kampuni yake mbali na zile za kushirikishwa na wenzake ambazo alidai hawezi kuziacha.