STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 19, 2015

RATIBA KAMILI YA LIGI KUU MSIMU WA 2015-2016 HII HAPA


Mabingwa watetezi Yanga

Azam
Simba
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) imeachia hadharani ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2015-2016, ikionyesha mabingwa watetezi wataanzia nyumbani katika mechi tano kaba ya kutoka kwenda Morogoro kuumana na Mtibwa Sugar.
Watetezi hao watavaana na watani zao, Simba Septemba 26, lakini ikianza mechi zake nyingi nyumbani huku wakitaabika kwa kumaliza mechi zao za mwisho mfululizo ikiwa ugenini.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ligi itaanza Septemba 12 na kumalizika Mei 7, huku pia kukiwa na michuano ya Kombe la FA ambalo limerejeshwa upya baada ya miaka mingi ya ukimya.
MICHARAZO imekuweka ratiba nzima ya Ligi hiyo kwa msimu huu ili kujua nani na nani wataanzia wapi na ligi;

Sept 12, 2015
Ndanda vs Mgambo JKT
African Sports vs Simba
Majimaji vs JKT Ruvu
Azam vs Prisons
Stand Utd vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Mwadui Fc
Mbeya City vs Kagera Sugar
 

Sept 13, 2015
Yanga vs Coastal Union
 

Sept 16, 2015
Yanga vs Prisons
Mgambo JKT vs Simba
Majimaji  vs Kagera Sugar
Mbeya City vs JKT Ruvu
Stand Utd  vs Azam
Toto Africans vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Coastal Union
 

Sept 17, 2015
Mwadui FC vs African Sports
 

Sept 19, 2015
Stand Utd vs  Africans Sports
Mgambo JKT vs Majimaji
Prisons vs Mbeya City
Yanga  vs JKT Ruvu
 

Sept 20, 2015
Mwadui Fc vs Azam
Mtibwa Sugar vs  Ndanda
Simba vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Toto Africans
 

Sept 26, 2015
Simba vs Yanga
Coastal Union vs Mwadui Fc
Prisons  vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Majimaji
Kagera Sugar vs Toto Africans
 

Sept 27, 2015
African Sports vs Ndanda
Azam vs Mbeya City
 

Sept 30, 2015
Simba vs Stand Utd
Azam vs Coastal Union
Mtibwa Sugar vs Yanga
Ndanda vs Majimaji
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
African Sports vs Mgambo JKT
Prisons vs Mwadui FC
 

Okt 01, 2015
Toto Africans vs Mbeya City


Okt 03, 2015
Mgambo JKT vs  Coasta Union
Majimaji vs Mwadui Fc
Toto Africans vs JKT Ruvu
Okt 04, 2015Stand Utd vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Prisons
Azam vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Simba
African Sports vs Yanga
 

Okt 5-13, 2015
Afcon 2017QFL/Kirafiki/WC 2018 QFL
 

Okt 17, 2015                                            Yanga vs Azam
Majimaji vs African Sports
Mbeya City vs Simba
Ndanda vs Toto Africans
Stand Utd vs Prisons
Coastal Union vs Mtibwa Sugar
 

Okt 18, 2015Mgambo JKT vs Kagera Sugar
Mwadui vs JKT Ruvu
 

Kagera Sugar
Okt 21, 2015Yanga vs Toto Africans
Stand Utd vs Majimaji
JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar
Prisons vs Simba
Coastal Union vs Kagera Sugar

 
Okt 22, 2015Mwadui vs Mgambo JKT
Mbeya City vs African Sports
Ndanda vs Azam
Okt 25, 2016

Uchaguzi Mkuu wa Taifa                                 
Okt 28, 2015                                            Toto Africans vs Mgambo JKT
Mwadui vs Yanga
Mtibwa Sugar vs  Kagera Sugar
Mbeya City vs Majimaji
Ndanda vs Stand Utd
Simba vs Coastal Union
 

Sept 29, 2015JKT Ruvu vs Azam
Prisons vs African Sports
 

Okt 31,2015Simba vs Majimaji
Kagera Sugar vs Yanga
Mtibwa Sugar vs Mwadui
Prisons vs Ndanda
Coastal Union vs Mbeya City
 

Nov 01, 2015African Sports vs JKT Ruvu
Azam vs Toto Africans
 

Nov 02, 2015
Mgambo JKT vs Stand Utd
 

Nov 07, 2015Mgambo JKT vs Yanga
Kagera Sugar vs Ndanda
Stand Utd vs Mwadui
Mbeya City vs Mtibwa Sugar
Azam vs Simba
Majimaji vs Toto Africans
 

Nov 08, 2015JKT Ruvu vs Prisons
Coastal Union vs African Sports
Nov 9-17, 2015
Kirafiki/ WC 2018 QFL/Challenge/Mini Window (Nov 15-Dec 15)/ Nani Mtani Jembe (Dec 12)
 

Mtibwa Sugar
Dec 19, 2015Yanga vs  Stand Utd
Mwadui vs Ndanda
Kagera Sugar vs African Sports
Prisons vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Simba
Majimaji vs Azam

 
Dec 20, 2015JKT Ruvu vs Coastal Union
Mbeya City vs Mgambo JKT
 

Dec 26, 2015Ndanda vs JKT Ruvu
Yanga vs Mbeya City
Majimaji vs Prisons
Mwadui vs Simba
Mtibwa Sugar vs  Mgambo JKT
Coastal Union vs Stand Utd
 

Dec 27, 2015Azam vs Kagera Sugar
Toto Africans vs African Sports
Jan 01-13, 2016
Mapinduzi Cup                                           
 

Jan 16, 2016JKT Ruvu vs Mgambo JKT
Toto Africans vs Prisons
Simba vs Mtibwa Sugar
Stand Utd vs Kagera Sugar
Mbeya City vs Mwadui
Coastal Union vs Majimaji
Azam vs  African Sports
 

Jan 17, 2016Yanga vs Ndanda
 

Jan 20, 2015Ndanda vs Mbeya City
Prisons vs Coastal Union
JKT Ruvu vs Simba
Stand Utd vs Toto Africans
Mgambo JKT vs Azam
 

Jan 21, 2016Mwadui vs Kagera Sugar
African Sports vs Mtibwa Sugar
Yanga vs Majimaji
 

Jan 23-24
FA CUP
 

Jan 30, 2016    Coastal Union vs Yanga
Simba vs African Sports
JKT Ruvu vs Majimaji
Prisons vs Azam
Mtibwa Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Toto Africans
Kagera Sugar vs Mbeya City
 

Jan 31, 2016Mgambo JKT vs Ndanda
 

Feb 03, 2016                                            Prisons vs Yanga
Simba vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs  Majimaji
JKT Ruvu vs Mbeya City
African Sports vs     Mwadui
Mtibwa Sugar vs Toto Africans
Azam vs Stand Utd
 

Feb 04, 2016Coastal Union vs Ndanda

Feb 06, 2016Kagera Sugar vs  Simba
Mbeya City vs  Prisons
JKT Ruvu vs Yanga
African Sports vs Stand Utd
Ndanda vs Mtibwa Sugar
 

Feb 07, 2016Azam vs Mwadui
Toto Africans vs  Coastal Union
Majimaji vs Mgambo JKT
Feb 12-14, 2016 CAF-CC&CL 

Feb 13, 2016Stand Utd vs Simba
Mgambo JKT vs African Sports
Yanga vs Mtibwa Sugar
Mbeya City vs Toto Africans
Ndanda vs Majimaji
JKT Ruvu vs Kagera Sugar
Mwadui vs Prisons
Coastal Union vs azam
 

Feb 20, 2016Yanga vs Simba
Mgambo JKT vs Prisons
Stand Utd vs JKT Ruvu
Mbeya City vs Azam
Majimaji vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Kagera Sugar
Feb 21, 2016Ndanda vs  African Sports
Mwadui vs Coastal Union
 

Feb 26-28, 2016 CAF-CC& CL
 

Mar 05, 2016Azam vs Yanga
African Sports vs Majimaji
Toto Africans vs Ndanda
Kagera Sugar vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Mwadui
Prisons vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Coastal Union
 

Mar 06, 2016Simba vs Mbeya City
Yanga vs African Sports
Mtibwa Sugar vs Azam
 

Mar 09, 2016Prisons vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Mgambo JKT
Mwadui vs Majimaji
JKT Ruvu vs Toto Africans
 

Mar 10, 2016Simba vs Ndanda
Mbeya City vs  Stand Utd
Mar 11-13, 2016 CAF-CC&CLToto vs Yanga
Azam vs  Ndanda
 

Mar 12, 2016African Sports vs Mbeya City
Mtibwa Sugar vs JKT Ruvu
 

Mar 13, 2016Majimaji vs Stand Utd
Kagera Sugar vs  Coastal Union
Simba vs Prisons
Mgambo JKT vs Mwadui 

Mar 18-20, 2016 CAF-CC&CL                               
 

Mar 19, 2016                                    Coastal Union vs Simba
Yanga vs Mwadui
Azam vs JKT Ruvu
Kagera Sugar vs Mtibwa Sugar
Majimaji vs Mbeya City
Stand Utd vs Ndanda
 

Mar 20, 2016African Sports vs Prisons
 

Mar 21, 2016Mgambo JKT vs Toto Africas
 

Mar 21-29, 2016 Kirafiki/FA Cup
 

Apr 02, 2016Majimaji vs Simba
Yanga vs Kagera Sugar
Toto Africans vs Azam
Stand Utd vs Mgambo JKT
Ndanda vs Prisons
Mbeya City vs Coastal Union
 

Apr 03, 2016JKT Ruvu vs African Sports
Mwadui vs Mtibwa Sugar
 

Apr 08-10, 2016 CAF-CC&CLStand Utd vs Yanga
 

Apr 09, 2016Ndanda vs Mwadui                                   
African Sports vs Kagera Sugar
Mtibwa Sugar vs Prisons
Azam vs Majimaji
 

Apr 10, 2016Coastal Union vs JKT Ruvu
 

Apr 11, 2016Mgambo JKT vs Mbeya City
 

Apr 16, 2016Simba vs Azam
Ndanda vs Kagera Sugar
African Sports vs Coastal Union
Mwadui vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Mbeya City
Prisons vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Majimaji
 

Apr 17, 2016Yanga vs Mgambo JKT
 

Apr 18-20, 2016 CAF-CC&CL
 

Apr 23-24, 2016 FA Cup                                           
Apr 26, 2016JKT Ruvu vs Ndanda
 

Apr 27, 2016Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs Azama
Simba vs Mwadui
Stand Utd vs Coastal Union
African Sports vs Toto Africans
 

Apr 28, 2016Prisons vs Majimaji
Mgambo JKT vs Mtibwa Sugar
 

Apr 30, 2016Mtibwa Sugar vs Simba
Mgambo JKT vs JKT Ruvu
 

Mei 01, 2016Ndanda vs Yanga
Kagera Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Mbeya City
Majimaji vs Coastal Union
African Sports vs Azam
Prisons vs Toto Africans
 

Mei 07, 2016                            Mbeya City vs Ndanda
Coastal Union vs  Prisons
Simba vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Stand Utd
Azam vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs Mwadui
Mtibwa Sugar vs African Sports
Majimaji vs Yanga
 

Mei 14, 2016 FA Cup

Tuesday, August 18, 2015

Christian Bentekeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

Benteke, signed in a £32.5million deal this summer, jumps for joy and is congratulated by Dejan Lovren after scoring on his Anfield debut
Chistian Benteke akishangilia bao lake aliyoisaidia Liverpool kushinda usiku wa jana
Benteke lets out a roar and clenches his fist as he looks towards the fans after scoring in front of the Kop midway through the first halfBenteke embraces captain Henderson after the England international assisted the former Aston Villa man with his first Liverpool goalBAO pekee la straika mpya wa Liverpool, Christian Benteke usiku wa kuamkia leo limeiwezesha Majogoo hao wa Anfield kubuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu iliyopanda daraja ya Bournemouth.
Pambano hilo pekee la Ligi Kuu ya England lililochezwa usiku wa jana lilipigwa kwenye Uwanja wa Anfield na iliwachukua wenyeji dakika 27 kuandika bao hilo tamu baada ya Benteke kuunganisha pasi ya nahodha wake, Jordan Henderson.
Ushindi huo umeifanya Liverpool kukwea hadi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 6 sawa na vinara, Manchester City na Manchester United,huku wageni hao wa EPL wakikamata nafasi ya 19 wakiwa hawana pointi hata moja kama ilivyo kwa Sunderland wanaoburuza mkia.
Kipute hicho cha Ligi ya England kitandelea wikiendi hii na Jumatatu ijayo.

Maxime kutumia kasi ile ile iliyopita kufunika VPL

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/03/Mecky-Mexime1.jpg
KOCHA Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime amesema kuwa ile kasi waliyoanza nayo msimu uliopita ndiyo watakayoitumia msimu ujao kuweza kurejesha heshima ya mabingwa hao wa zamani.
Mtibwa iliianza ligi ya msimu uliopita kwa mkwara ikishinda mfululizo na kuongoza msimamo hadi ligi iliposimama Novemba 9, kisha kwenda kwenye Kombe la Mapinduzi na kufika fainali dhidi ya Simba.
Baada ya kichapo cha Simba cha mikwaju ya penalti, Mtibwa ilirudi katika ligi kuu kichovu na kupoteza mechi mfululizo, kiasi cha kuwa hatarini kushuka daraja kabla ya kuzinduka mwishoni.
Hata hivyo Maxime, alisema kwa namna anavyowaandaa vijana wake ana hakika mambo yatakuwa bambam katika msimu ujao ili kurejesha heshima ya klabu yao.
Maxime anasema ingawa hana maproo waka kufanya usajili mkubwa, lakini kurejesha baadhi ya majembe yake kama Issa Rashid 'Baba Ubaya', Said Bahanuzi na kipa Hussein Sharif 'Casillas' ni vitu vinavyompa jeuri kuamini msimu ujao wapinzani wao lazima wakae.
Mtibwa iliwahi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mwaka 1999 na 2000 na kuweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kutwaa mataji mengi nje ya Simba na Yanga ambazo zimekuwa zikipokezana miaka nenda rudi.
Pili ilikuwa ni klabu ya kwanza nje ya Dar kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara mbili mfululizo.

Machuppa azitonya klabu Ligu Kuu ya Bara

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJWTA2TDV-ACUgQUZnSVhXXx6q9XrzSkWHIGwVk3H8X5tXnNCbSDYpiePUQsBjJ762-WY4XYfjl-R17BO613mKaOTCP4LMuAaA93Vr9NQEXFvBxhc1DQJZOGs6IGyU6nw6c5IRtMc5240/s1600/MACHUPA%5B1%5D.jpg
STRAIKA wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Athuman Machuppa 'Smilling Killer' amezitaka klabu za Tanzania kuachana na ulimbukeni wa kuwapapatikia wachezaji wa kigeni na badala yake kutumia vipaji vilivyojazana nchini kuzijenga timu zao.
Machuppa alisema ni kweli wachezaji wa kigeni ni muhimu katika klabu, lakini sio wanaokuja nchini ambao wengi wao huwa ni wazee na walio na viwango vizivyotisha au kupitwa hata na wazawa.
"Nadhani klabu ziwekeze kwenye vipaji vya nyumbani, kuna wachezaji wengi wazuri Tanzania kama watatengenezwa na kuaminiwa, wageni waje lakini wenye viwango kama vya akina Emmanuel Okwi, Kipre Tchetche au wengine siyo kuletwa ilimradi tu na kulipwa fedha nyingi bila sababu," alisema Machuppa.
Mshambuliaji huyo aliyeweka maskani yake nchini Sweden kwa sasa akijiandaa kuwa raia wa nchi hiyo panapo majaliwa Mei mwakani, alisema hata idadi ya mapro katika vikosi vya klabu za Ligi kuu kutoka watano mpaka saba hakukuwa na sababu yoyote ya maana.
"Watano wangetosha tu, watatu wacheze na wawili wakae benchi, saba ni wengi na ninavyojua viongozi wa soka wa Tanzania walivyo na mzuka na wageni watalazimisha wote wacheze kama ruksa ilivyo, je wazawa wataonekana wapi, tutapata timu nzuri ya taifa vipi?"
"Watu wawekeze kwa vijana, Simba ilipata mafanikio ikiwa na wazawa waliojituma na kutumia vyema vipaji vyao, ila tusiwakatae wageni wanongeza chachu kama wakiwa ni wakali," alisema.

Yanga warudi Dar, wakitamba kuiva tarari kuiua Azam

MABINGWA wa Soka Tanzania Yanga inatarajiwa kutua jijini Dar es Salaam leo Jumanne ikitokea Mbeya ilipoenda kupiga kambi ya siku kama 10 na kucheza mechi tatu za kirafiki na timu za jijini humo.
Yanga ilianza kuumana na Kimondo Fc na kuishinda kwa mabao 4-1 kabla ya kuicharaza Prisons-Mbeya kwa mabao 2-0 na kumaliza kazi kwa Mbeya City ikiichapa mabao 3-2.
Kikosi hicho kilinatarajiwa kutua leo na kuingia kambini moja kwa moja kusubiri pambano lao dhidi ya Azam ambao walijichimbia Zanzibar na leo nao watarudi jijini Dar es Salaam kusubiri pambano hilo la Ngao ya Jamii liatakalopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa.
Kocha wa Yanga Hans Pluijm amenukuliwa kwamba kikosi chake kimeiva na kazi waliyoenda kuifanya Mbeya imemalizika na sasa ni kuonyesha makali yao hasa kuimarika kwa safu yao ya ushambuliaji.
Pluijm anasema washambuliaji wake wameonekana kukamilika kwa michezo hiyo mitatu na ana tumaini kubwa la kuilaza Azam ambayo ina rekodi ya kucheza mechi 11  mfululizo bila kuruhusu nyavu zake kuguswa, kati ya michezo 12 iliyocheza chini ya kocha Stewart Hall.
Mechi pekee iliyoruhusu wavu wao kuguswa kabla ya kukaza buti ni ile ya kirafiki dhidi ya Friends Rangers ambapo walishinda kwa mabao 4-2.
Baada ya hapo imekuwa ikiendelea kugawa dozi, lakini bila kuruhusu bao langoni mwake kuanzia kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyotwaa msimu huu kwa mara ya kwanza na hata mechi nyingine za kirafiki.
Azam licha ya kushiriki mechi za Ngao ya Hisani mara tatu haijawahi kushinda hata mara moja, mwaka 2012 ilipoteza mchezo kwa Simba kwa kupigwa mabao 3-2, kabla ya kulazwa bao 1-0 na Yanga mwaka uliofuata na mwaka jana ilipigwa mabao 3-0.
Redodi za Azam chini ya Hall baada ya kurudishwa kwa mara ya tatu;

Azam 4-2 Friends Rangers (kirafiki-Dar)
Azam 1-0 JKT Ruvu (kirafiki-Dar)
African Sports 0-1 Azam (kirafiki-Tanga)
Coastal Union 0-1 Azam (kirafiki-Tanga)
Azam 1-0 KCCA Uganda (Kagame-Dar)
Azam 2-0 Al Malakia Sudan Kusini (Kagame-Dar)
Azam 0-0 (pen 5-3) Yanga (Kagame-Dar)
Azam 1-0 KCCA-Uganda (Kagame-Dar)
Azam 2-0 Gor Mahia Kenya (Kagame-Dar)
KMKM 0-1 Azam (Kirafiki-Zanzibar)
Mafunzo 0-3 Azam (Kirafiki-Zanzibar)

Saturday, August 15, 2015

Azam wazidi kunoa makali Zanzibar

11846696_1009621735744849_7161429854397873130_n
Kikosi cha Azam kilipopelekea Kombe lao la Kagame Ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete
BAADA ya kuikong'ota KMKM ya Zanzibar katika pambano lao la kirafiki, mabingwa wa Kombe la Kagame, Azam jioni ya leo inatarajiwa kushuka Uwanja wa Amaan kucheza mchezo wake wa pili visiwani humo wakiwa wamepiga kambi kujiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga wikiendi ijayo.
Azam chini ya kocha Stewart Hall imejichimbia humo ikiwa na kikosi chake chote isipokuwa Allan Wanga aliyepo Kenya alipoenda kwa matatizo, huku Mganda Brian Majwega akiwa ametemwa rasmi kikosini.
Mabingwa hao wanajaribu kusaka ushindi kwa mara ya kwanza kwenye mechi ya Ngao ya Hisani kwani tangu mwaka 2012 haijawahi kushinda mbele ya Simba na Yanga waliowatungua mara mbili mfululizo ikiwamo mwaka 2013 walipowafunga bao 1-0 na mwaka jana kuwafumua mabao 3-0.
Azam inatarajiwa kurejea jijini Dar es Salaam Jumanne baada ya kuwepo kwa taarifa ya ziara ya TP Mazembe kufutwa rasmi, na kabla ya kutimka visiwani inaelezwa kuwa huenda ikaiita URA ambayo leo inashuka Uwanja wa Taifa kucheza na Simba katika pambano la kirafiki la kimataifa, ili angalau kuwapa makali ya kuikabili Yanga ambayo ina hasira ya kung'olewa kwenye Kombe la Kagame kwa matuta.

Ratiba ya Ligi Kuu ya England wikiendi hii ipo hivi

optimized-premier-league-2015-2016-700x400

BAADA ya Mashetani Wekundu, Manchester United jana kupata ushindi na kukwea kileleni mwa Msimamo, Ligi ya England itaendelea leo na kesho kwa michezo kadhaa na ratiba kamili tunakuwekea kama ifuatavyo:

Jumamosi Agosti 15
14:45 Southampton vs Everton
17:00 Sunderland vs Norwich
17:00 Swansea vs Newcastle
17:00 Tottenham vs Stoke
17:00 Watford vs West Brom
17:00 West Ham vs Leicester
Jumapili Agosti 16
15:30 Crystal Palace vs Arsenal
18:00 Man City vs Chelsea

Jumatatu Agosti 17
22:00 Liverpool vs Bournemouth
 

Huku Simba, kule Yanga Utamu Ulioje!

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2015/08/KIKOSI.jpg
Kikosi cha timu ya Simba
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhgBANjTf-2fkrx3RLm5RPaUrUbyBwYcFEdzPN7vo1to9_q2hUECoRKM5sjZMEd6wKlYjM72Itb9JeMgpbevjrJZAmBeXrbFiVN2ohR7iP20AWcyQ7rwfR__s4p6_Gx2dc7gmy0Ivy3BZ6R/s640/DSC_6726.JPG
Mabingwa wa Tanzania Yanga
WAKATI kocha Dylan Kerr akiwa na mtihani mwingine mgumu wa kutaka kuwathibitishia mashabiki wa Simba kwamba kikosi chake kimeiva wakati jioni ya leo Jumamosi watakabiliana na URA ya Uganda, watani zao Yanga wenyewe wataendeleza libeneke lao jijini Mbeya kesho kuwa kuumana na Mbeya City.
Mechi hizo za kirafiki ni maalum kwa maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu, ambapo Simba yenyewe baada ya kuweka kambi ya mwezi mmoja na ushei katika wilaya ya Lusohoto, Tanga na Zanzibar imerudi jijini Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini na leo itaumana na URA Uwanja wa Taifa.
Mechi hiyo ni ya sita kwa Kerr tangu apewe jukumu la kuinoa timu hiyo akimpokea Goran Kopunovic, akiwa na rekodi ya kushinda mechi zote, zikiwemo tano na timu za visiwani Zanzibar na moja ya kimataifa walipoumana na SC Villa ya Uganda kwenye tamasha la Simba Day Jumamosi iliyopita.
Simba inatarajiwa kuwatumia nyota wake wale wale iliyowatumia katika mchezo wao na Villa, huku ikiwa imeshamalizana na nyota wao wa kimataifa, Vincent Agban na Justice Majabvi.
Yanga wenyewe ambao wamekimbilia Tukuyu Mbeya baada ya kutolewa Kombe la Kagame, kesho Jumapili itaumana na Mbeya City katika mechi yao ya tatu jijini humo, awali ilianza kwa mkwara kwa kuitandika Kimondo Fc ya Mbozi kwa mabao 4-1 kabla ya bkuizabua Prisons Mbeya kwa mabao 2-0 na baada ya mchezo hio wa kesho itawasubiri Zesco ya Zambia na Bata Bullets ya Malawi kumaliza kazi kabla ya kurudi Dar kuisubiri Azam kwenye pambano la Ngao ya Hisani litakalochezwa Jumamosi ijayo.
Mechi hiyo ya Ngao ya Hisani itakayopigwa Uwanja wa Taifa ni maalum katika kuzindua msimu mpoya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara amabyo itaanza kutimua vumbi lake, Septemba 22.

Manchester United yafanya kweli Ligi Kuu ya England

Luke Shaw grabs Januzaj after his opening goal put Manchester United on course for their second consecutive victory
Januzaj akishangilia bao lake la wachezaji wenzake wa Man United
MASHETANI Wekundu, Manchester United usiku wa jana walifanikiwa kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kushinda baoa 1-0 ugenini dhidi ya Aston Villa.
Baoa pekee la dakika ya 29 lililofungwa na Adnan Januzaj limewawezesha vijana wa Louis Van Gaal kushinda mechi ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya England na kukaa kileleni ikiwa na pointi 6.
Pambano hilo lililochezwa Uwanja wa Villa Park, liliwahishwa kuchezwa kutokana na muingiliano wa masuala ya kijamii karibu na mji huo na Mashetani WEkundu wakaona wafanye yao mapema kabla ya kuelekea kwenye pambano lao la mchujo la Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Warusi.
Januzaj alifunga bao hilo akimalizia pasi murua ya Juan Mata. Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini kivumbi kitakuwa kesho kati ya Manchester City dhidi ya mabingwa watetezi Chelsea kwenye Uwanja wa Etihad, mjini Manchester. Tayari makocha wa timu hizo wametoa tambo zaom lakini Manuel Pellegrin amesisitiza ni lazima safari hii ampe mkono Jose Mourinho.

Hapana! Hii ni Barcelona kweli? Yapigwa 4-0 na Bilbao

Athletic Bilbao's defender Mikel San Jose points to the heavens after scoring an incredible goal to put the underdogs ahead
Wachezaji wa Bilbao wakishangilia mabao yao dhidi ya Barcelona
Gorka Iraizoz comes out to deny Luis Suarez as the former Liverpool man tries to round the home keeper and bring his side level
Suarez akijitahidi kuipiugania Barcelona, lakini wapi walilala 4-0
Mikel Balenziaga ushers the ball away from Messi as the home defence looked to minimise the impact of Barcelona's best player
Messi hakufurukuta kabisa
SIKU chache baada ya kufanikiwa kushinda UEFA Super Cup kwa mbinde kwa kushinda mabao 5-4 dhidi ya Sevilla, mabingwa wa Hispania, Barcelona imetoa ishara mbaya ya kwamba msimu huu huenda ikawa urojo baada ya usiku wa jana kupigwa 4-0.
Barca wamekumbana na kipigo hicho kwenye pambano la Super Cup la Hispania kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa La Liga na klabu ya Athletico Bilbao waliokuwa uwanja wa nyumbani.
Mabao matatu ya Aritz Aduriz na jingine la Mikel San Jose kwenye Uwnaja wa wa San Mames Barria, yalitosha kuizima Barcelona licha ya kuwa na nyota wake kadhaa akiwamo Messi na Luis Suarez.
San Jose alianza kumtungua kipa Marc-Andre ter Stegen dakika ya 13 kabla ya Aduriz kufunga mabao mawili ya haraka haraka dakika za 53 na 62.
Aduriz akakamilisha hat-trick yake kwa bao la mkwaju wa penalti, baada ya beki Dani Alves kumchezea rafu. 

Bayern Munich yatoa onyo mapema Bundesliga

Benatia (left) races away to celebrate following his 27th opener at the Allianz Arena
Wachezaji wa Bayern Munich wakipongezana baada ya kufunga moja ya mabao yao jana katika Bundesliga
Bayern striker Robert Lewandowski jumps for joy after the Poland striker made it 2-0 after the break
Robert Lewandowski akishangilia bao alililoifungia Bavarian usiku wa jana
MTAISOMA namba! Hivyo ndivyo Bayern Munich ilivyojitambulisha baada ya usiku wa jana kuanza vema Ligi Kuu ya Ujerumani wao kama mabingwa watetezi kwa kuikandika Hamberger kwa mabao 5-0.
Bavarians hao walipata ushindi huo kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo katika Uwanja was nyumabi wa Allianz Arena kwa mabao ya Robert Lewandowski, Mehdi Benatia, Thomas Muller aliyefunga mawili na Douglas Costa.