STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 12, 2014

Aisha Bui: Nilihatarisha maisha yangu kuwapa raha mashabiki wangu

NYOTA wa kike wa filamu nchini, Aisha Fat'hi 'Aisha Bui' amevunja ukimya na kuibuka na filamu mpya iitwayo 'Mshale wa Kifo' huku akiweka bayana kwamba alijitoa na kuhatarisha maisha yake kuiandaa filamu hiyo iliyotengenezwa porini.
Aisha alisema kuwa kutokana na maoni ya mashabiki wa filamu wanaolalamika kuwa filamu  nyingi za Bongo zimekuwa za mijini tu, huku baadhi ya matukio yakirudiwa kila katika sinema hizo hali hiyo ilimfanya abadilishe na kutoka kivingine.
Alisema hivyo aliamua kuhama mji na kwenda porini kuicheza filamu hiyo ambapo chupuchupu yeye na waigizaji wenzake kung'atwa na nyoka wakati wakiitengenza filamu hiyo.
“Nilijitoa na kuhatarisha maisha yangi kwa kuingia msituni ili tu kutengeneza filamu ambayo ikakata kiu ya mashabiki wasiovutiwa na filamu za 'sebuleni'. Ninajua nina deni kwa wapenzi wa kazi zangu, wanajua mimi ni bora hivyo lazima niwe bora kila mwaka,” alisema Aisha.
Filamu hiyo ya 'Mshale wa Kifo', imetengenezwa na kampuni ya Yuneda Entertainment ikiwashirikisha wakali kama Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’, Esha Buheti, Salim Ahmed ‘Gabo Zigamba’ na wasanii wengine.

Jennifer Mgendi akaribia kumtoa Mama Mkwe

MUIMBAJI nyota wa Nyimbo za Injili nchini ambaye pia ni muigizaji wa filamu, Jennifer Mgendi anatarajia kuiachia mtaani filamu yake mpya iitwayo 'Mama Mkwe' aliowashirikisha wakali wenzake wa muziki wa injili, Bahati Bukuku na Christina Matai.
Akizungumza na MICHARAZO Jennifer alisema filamu hiyo ipo njiani kuachiwa baada ya kukamilika kuhaririwa na kuwataka mashabiki wake wajiandae kuipokea.
Jennifer anayetamba na albamu ya 'Hongera Yesu', alisema filamu hiyo inayozungumzia mkasa wa mama mkwe anayelazimisha mwanae wa kiume kumzalia mjukuu ameigiza na wasanii kama Senga,Bi Esther, Christine Matai, Husna Chobis, yeye (Jennifer)  na wengine.
"Filamu yangu mpya ya 'Mama Mkwe' bado kidogo kabla ya kuachiwa mtaani ikiwa imechezwa na mimi mwenyewe, Bahati (Bukuku) Christine Matai, Senga, Bi Esther, Mussa Banzi na wakali wengine. Siyo ya kuikosa kwa jinsi ilivyo," alisema Jennifer.
Kabla ya filamu hiyo, Jennifer amewahi kutamba na filamu kadhaa kama 'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

Van Gaal awaonyesha Chicharito, Nani mlango wa kutokea Man United

Mlango u wazi kwenu kutimka Old Traffiord
SIKU chache kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya England na kufungwa kwa pazia la usajili katikia ligi hiyo, Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amewaeleza wachezaji sita akiwamo beki wa kulia Rafael kwamba wanaweza kuchapa mwendo.
Marouane Fellaini, Wilfried Zaha, Nani, Shinji Kagawa na kinda yosso Will Keane pia wamevunja 'ndoa' na kikosi hicho cha Van Gaal na hilo limefanyika wakati United ikijifua katika Uwanja wa mazoezi wa  Carrington Jumamosi mchana.
Inaeleweka kuwa Mholanzi huyo amewaambia Fellaini, Zaha, Nani na Keane klabu hiyo itasikiliza ofa kwao baada ya kuwaweka sokoni rasmi.
Rafael, alishangaa kusikia jina lake likiwa katika orodha hiyo na kwamba pia anaweza kulazimisha kuondoka wakati huu klabu hiyo ikisaka beki wa kulia. Kagawa atatumika lakini kaelezwa ataanzia benchi nyuma ya Ander Herrera na Juan Mata.
Kiungo Anderson na mshambuliaji Javier Hernandez pia nao tayari wanajua kwamba United itasikiliza ofa endapo zitawasili mezani kwao. Southampton, Inter Milan, Tottenham, Atletico Madrid na Juventus zote zimeonyesha nia ya kumsajili Mmexico huyo, wakati Napoli itakuwa tayari kumsajili Fellaini kama dili hilo litakubalika na United.
Newcastle inaongoza katika vita ya kumsajili Zaha, huku Crystal Palace, West Ham na Nottingham Forest nazo zikihitaji huduma yake.
Cardiff City imeulizia uwezekano wa kumsajili kwa mkopo Keane ambaye ni pacha wa beki Michael, lakini United inahitaji kumtazama zaidi kabla ya kukamilisha dili hilo.
Kwa sasa United ipo sokoni ikisaka mabeki wapya wawili baada ya kushindwa kumsajili beki wa kati wa Arsenal, Thomas Vermaelen ambaye juzi alijiunga rasmi na Barcelona
Mabingwa hao wa zamani wamejipanga kufanya vyema katika msimu huu baada ya msimu uliopita kuboronga na kumaliza kwenye nafasi ya katikati tofauti na mazoea yao.

Monday, August 4, 2014

Mcongo wa Azam atimka kwao, Ghana, Mhaiti bado majaribuni

Kiungo Lofo Serge aliyetimkia kwao
Kiungo Joseph Peterson wa Haiti anayeendelea kujaribiwa
MABINGWA wa soka nchini, Azam wanaendelea kuwapima kwa mara ya mwisho wachezaji wawili wa kimataifa kutoka Haiti na Ghana, huku nyota mwingine wa DR Congo Lofo Serge akitimka kwao baada ya majaribio yake.
Wachezaji wanaoendelea kujaribiwa kabla ya kuamuliwa hatma yao ni kiungo Joseph Peterson wa Haiti na beki Ben Achaw kutoka Ghana, wakati Serge ambaye ni mshambuliaji akimaliza majaribio yake na kutimka.
Akizungumza na MICHARAZO, Meneja wa Azam, Jemedari Said alisema wachezaji wote wameonyesha viwango vya hali ya juu katika kusaka soka, ila hatma yao itaamuliwa na kocha Joseph Omog mwenye maamuzi ya mwisho.
Jemedari alisema Serge alitua nchini baada ya kutumiwa tiketi na uongozi wao na muda wake ulikuwa wa wiki moja, wakati wenzake walitua wenyewe nchini na watamalizia wiki yao ya pili kabla ya kuondoka.
"Serge alijaribiwa kwa wiki moja na kwa uzoefu na umaarufu wake siyo jambo la ajabu kumaliza mapema na hao wengine waliokuja wenyewe wanamalizia wiki yao ya mwisho kabla ya kocha kuamua hatma yao," alisema Jemedari.
Meneja huyo alisema kwa waliowashuhudia wachezaji hao wakati na kikosi cha Azam watakubaliana naye kwamba ni wachezaji wazuri, ila kocha ndiye atakayeamua iwapo kama watafaa uitumikia timu yao.
"Kama wataonekana wanavitu vya kuisaidia timu basi watafahamishwa hata wakiwa makwao, lakini kwa hakika karibu wote wanaonekana wazuri," alisema Jemedari nyota wa zamani wa kandanda nchini aliyetamba Majimaji-Songea.
Kabla ya kujaribiwa Azam Serge anayeichezea pia timu ya taifa ya nchi yake, aliwahi kutamba na timu za AS Paulino Kinshasa, TP Mazembe, AS Aviacao, Sagrada Esperança, AS Vita, FC Brussels na Maccabi Netanya.

MKAZI MWANZA AJIFUNGUA WATOTO WANNE

Watoto wa Tecra waliozaliwa wakiwa ni wanne huku mmojawapo ambaye hakufunuliwa uso akiwa amefariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa-Picha na Antony Sollo-Malunde1 blog-Mwanza 

 Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi Proscovia Leopod akimhudumia bi Tecra baada ya kujifungua Picha na Antony Sollo-Malunde1 blog-Mwanza


Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Tecra Kazimili(24) mkazi wa Lubili katika wilaya ya Misungwi Mkoa wa Mwanza amjefungua watoto (4) kwa wakati mmoja huku mtoto mmoja wa kiume akifariki muda mfupi baada ya mama huyo kujifungua.
Akizungumza na waandishi wa habari waliofika kushuhudia tukio hilo ambalo si la kawaida mama Tecra alisema hii ni mara yake ya nne kujifungua lakini ni mara yake ya kwanza kujifungua watoto wanne kwa wakati mmoja. 

Tecra ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi katika Hospitari ya wilaya ya misungwi Mkoani Mwanza alisema anamshukuru Mungu kwa kumjalia Afya njema na kumuwezesha kujifungua watoto (4) pamoja na kwamba mmoja wa watoto hao amepoteza maisha muda mfupi baada ya kuzaliwa. 

“yote ni mipango ya mungu.”alisema Tecra

Tecra  aliongeza kuwa hiyo ni uzao wake wa nne lakini hana mtoto hata mmoja kutokana na watoto wake wote (3) kufariki wanapofikisha mwaka moja hadi mwaka mmoja na nusu kitendo kilichosababisha kufukuzwa na mume wake Mussa Masalu aliyekuwa anaishi naye baada ya kuona watoto wanafariki na kudaiwa kuwaua yeye mwenyewe jambo ambalo halina ukweli,alisema Tecra.

Pamoja na hayo Tecra  anawaomba Watanzania wasamalia wema watakaoguswa wamsaidie kwa kuwa huyu aliyempa mimba hiyo si mumewe hivyo hana msaada wowote atakaopata wakati atakapokuwa anaendelea kuwalea watoto wake hao.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi Marco Mwita aliwaambia waandishi wa Habari kuwa tukio hili ni si la kawaida kutokea mara nyingi wakina mama wamekuwa wakijifungua watoto watatu na si wanne kama ilivyotokea kwa Tecra.

Wauguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi wameonyesha utendaji uliotukuka kwa namna ya kipekee jinsi waandishi walivyofika na kushuhudia namna walivyokuwa wakimhudumia Tecra ambapo mmoja wa wauguzi hao Proscovia Leopod 36 alikutwa akitoa huduma kwa upendo wa aina yake kwa kumsaidia Tecra mambo mbalimbali aliyopaswa kuyafahamu ili kuhakikisha watoto hao wanakaa salama.

Akifafanua Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi  Proscovia Leopod alibainisha baadhi ya mambo aliyokuwa akimfundisha Tecra kuwa ni namna ya kuwanyonyesha watoto,kuwahudumia na kuwafunika shuka,na kumshauri ale chakula cha kutosha na bora ili aweze kupata maziwa mengi kwa ajili ya kuwanyonyesha watoto wake.

Pamoja na kufanya kazi katika mazingira magumu,wauguzi wa Hospitali hiyo wamesema kuwa,

“Tumefurahishwa na jinsi Mungu alivyotujalia moyo wa kujituma kufuatana na mazingira magumu ya utendaji wa kazi zetu,jambo hili siyo la mchezo tumehangaika na kutumia uwezo wetu wote tulio nao kuhakikisha Tecra anajifungua salama,tunaahidi kwa,tutamsaidia mama huyu kwa hali na mali mpaka hapo hali yake itakapotengemaa na kuruhusu arudi kwao.” Walisema wauguzi hao.

Bi Tecra hana msaada,na kama unaguswa basi piga simu namba 0768102438


Na Valence Robert

Huu ndiyo usajili wa timu za Ligi Kuu za England

Luke Shaw ametua Manchester United toka Southampton
Kipa David Ospina ametua Arsenal
Didier Drogba amerejea Chelsea
Fillipe Luis (mbele) amehamia Chelsea
http://static.goal.com/434100/434187_heroa.jpg
Alexis Sanchez ametua Arsenal toka Barcelona
Romelu Lukaku amehamia jumla Everton toka Chelsea
ARSENAL
WALIOSAJILIWA
Alexis Sanchez (Barcelona, £30m),
Calum Chambers (Southampton, £12m),
Mathieu Debuchy (Newcastle, £10m),
David Ospina (Nice, £3m)

WALIOONDOKA

Thomas Eisfeld (Fulham, ada haikutajwa),
Bacary Sagna (Manchester City, huru),
Lukasz Fabianski (Swansea, huru),
Nicklas Bendtner (ameruhusiwa),
Park Chu-young (ameruhusiwa),
Chuks Aneke (ameruhusiwa),
Daniel Boateng (ameruhusiwa),
Wellington Silva (Almeria, mkopo),
Carl Jenkinson (West Ham, mkopo)

ASTON VILLA

WALIOSAJILIWA
Philippe Senderos (Fulham, huru),
Joe Cole (West Ham, huru),
Tom Leggett (Southampton, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Southampton, ada haikutajwa)
Kieran Richardson (Fulham, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA

Marc Albrighton (Leicester City, huru),
Nathan Delfouneso (Blackpool, huru),
Jordan Bowery (Rotherham, ada haikutajwa),
Nicklas Helenius (Aalborg, mkopo),
Yacouba Sylla (Kayseri Erciyesspor, mkopo)

BURNLEY

WALIOSAJILIWA
Lukas Jutkiewicz (Middlesbrough, £2.5m),
Michael Kightly (Stoke, ada haikutajwa),
Marvin Sordell (Bolton, huru),
Matt Gilks (Blackpool, huru),
Matt Taylor (West Ham, huru),
Steven Reid (West Brom, huru)

WALIOONDOKA

Chirs Baird (West Brom, huru),
Junior Stanislas (Bournemouth, huru),
David Edgar (Birmingham, huru),
Keith Treacy (ameruhusiwa),
Brian Stock (ameruhusiwa),
Nick Liversedge (ameruhusiwa)

CHELSEA

WALIOSAJILIWA
Cesc Fabregas (Barcelona, £30m),
Diego Costa (Atletico Mdrid, £32m),
Mario Pasalic (Hadjuk Split, ada haikutajwa),
Filipe Luis (Atletico, £16m),
Didier Drogba (Galatasaray, huru)

WALIOONDOKA

David Luiz (Paris Saint-Germain, £50m),
Romelu Lukaku (Everton, £28million),
Samuel Eto'o (ameruhusiwa),
Frank Lampard (New York City, huru),
Sam Hutchinson (Sheffield Wednesday, huru),
Mark Schwarzer (ameruhusiwa),
Henrique Hilario (ameruhusiwa),
Wallace (Vitesse Arnhem, mkopo),
Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, mkopo)
Thorgan Hazard (Borussia Monchengladbach, mkopo),
Ashley Cole (Roma, £1.5m),
Demba Ba (Besiktas, £8m),
Mario Pasalic (Elche, mkopo)
Patrick van Aanholt (Sunderland, ada haikutajwa),
Ryan Bertrand (Southampton, mkopo),
Gael Kakuta (Rayo Vallecano, mkopo)

CRYSTAL PALACE

WALIOSAJILIWA
Chris Kettings (Blackpool, huru)
Fraizer Campbell (Cardiff, £800k)

WALIOONDOKA

Jonathan Parr (Ipswich, huru),
Dean Moxey (Bolton, huru),
Aaron Wilbraham (Bristol City, huru),
Kagisho Dikgacoi (Cardiff, huru),
Danny Gabbidon (ameruhusiwa),
Neil Alexander (ameruhusiwa),
Ibra Sekajja (ameruhusiwa),
Alex Wynter (Portsmouth, mkopo),
Kwesi Appiah (Cambridge, mkopo),
Jose Campana (Sampdoria, ada haikutajwa),
Jack Hunt (Nottingham Forest, mkopo)

EVERTON

WALIOSAJILIWA
Romelu Lukaku (Chelsea, £28m),
Gareth Barry (Manchester City, free)
Muhamed Besic (Ferencvaros, £4m)

WALIOONDOKA

Apostolos Vellios, (Lierse, huru)
Mason Springthorpe (ameruhusiwa)
Magaye Gueye (Millwall, huru)

HULL

WALIOSAJILIWA
Robert Snodgrass (Norwich, £8m),
Jake Livermore (Tottenham, £6m),
Tom Ince (Blackpool, free),
Harry Maguire (Sheffield United, £2.5m),
Andrew Robertson (Dundee United, £2.85m)

WALIOONDOKA

Matty Fryatt (Nottingham Forest, huru),
Cameron Stewart (Ipswich, huru),
Robert Koren (ameruhusiwa),
Abdoulaye Faye (ameruhusiwa),
Conor Henderson (Crawley, huru),
Dougie Wilson (released),
Conor Townsend (Dundee United, mkopo),
Joe Dudgeon (Barnsley, mkopo)

LEICESTER CITY

WALIOSAJILIWA
Matthew Upson (Brighton, huru),
Marc Albrighton (Aston Villa, huru),
Leonardo Ulloa (Brighton, £7m),
Ben Hamer (Charlton, huru),
Jack Barmby (Manchester United, huru),
Louis Rowley (Manchester United, huru)

WALIOONDOKA

Lloyd Dyer (Watford, huru),
Neil Danns (Bolton, huru),
Sean St Ledger (ameruhusiwa),
Zak Whitbread (Derby, huru),
Paul Gallagher (Preston, mkopo),
Marko Futacs (ameruhusiwa),
George Taft (Burton Albion, huru)

LIVERPOOL

WALIOSAJILIWA
Adam Lallana (Southampton, £23m),
Lazar Markovic (Benfica, £20m),
Emre Can (Bayer Leverkusen, £9.8m),
Rickie Lambert (Southampton, £4m)
Dejan Lovren (Southampton, £20m),
Divock Origi (Lille, £10m)

WALIOONDOKA

Luis Suarez (Barcelona, £75m),
Luis Alberto (Malaga, mkopo),
Iago Aspas (Sevilla, mkopo),
Andre Wisdom (West Brom, mkopo),
Divock Origi (Lille, mkopo)

MANCHESTER CITY

WALIOSAJILIWA
Fernando (Porto, £12m),
Bacary Sagna (Arsenal, free),
Willy Caballero (Malaga, £6m),
Bruno Zuculini (Racing Club, £1.5m)

WALIOONDOKA

Costel Pantilimon (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (West Brom, huru)
Gareth Barry (Everton, huru),
Alex Nimely (ameruhusiwa),
Rony Lopes (Lille, mkopo),
Emyr Huws (Wigan, mkopo)

MANCHESTER UNITED

WALIOSAJILIWA
Luke Shaw (Southampton, £31.5m),
Ander Herrera (Athletic Bilbao, £29m),
Vanja Milinkovic (FK Vojvodina, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA

Alexander Buttner (Dinamo Moscow, £5.6m),
Rio Ferdinand (QPR, huru),
Nemanja Vidic (Inter Milan, huru),
Federico Macheda (Cardiff City, huru),
Jack Barmby (Leicester, huru),
Louis Rowley (Leicester, huru)
Ryan Giggs (amestaafu),
Patrice Evra (Juventus, £2.5m)
Bebe (Benfica, £2.4m)

NEWCASTLE

WALIOSAJILIWA
Remy Cabella (Montpellier, £12m),
Emmanuel Riviere (Monaco, £6m),
Siem de Jong (Ajax, £6m),
Daryl Janmaat (Feyenoord, £5m),
Ayoze Perez (Tenerife, £1.5m),
Jack Colback (Sunderland, huru)

WALIOONDOKA

Mathieu Debuchy (Arsenal, £10m),
James Tavernier (Wigan, ada haikutajwa,
Dan Gosling (Bournemouth, huru),
Shola Ameobi (ameruhusiwa),
Conor Newton (Rotherham, huru),
Michael Richardson (ameruhusiwa),
Sylvain Marveaux (Guingamp, mkopo)

QUEENS PARK RANGERS

WALIOSAJILIWA
Rio Ferdinand (Manchester United, huru),
Steven Caukler (Cardiff, £8m)

WALIOONDOKA

Tom Hitchcock (Mk Dons, huru),
Aaron Hughes (Brighton, huru)
Stephane Mbia (ameruhusiwa),
Andrew Johnson (ameruhusiwa),
Luke Young (ameruhusiwa),
Hogan Ephraim (ameruhusiwa),
Angelo Balanta (ameruhusiwa),
Yossi Benayoun (Maccabi Haifa, ada haikutajwa),
Esteban Granero (Real Sociedad, ada haikutajwa)

SOUTHAMPTON

WALIOSAJILIWA
Dusan Tadic (Twente, £10.3m),
Graziano Pelle (Feyenoord, £8m),
Ryan Bertrand (Chelsea, loan)

WALIOONDOKA

Luke Shaw (Manchester United, £31.5m),
Rickie Lambert (Liverpool, £4m),
Adam Lallana (Liverpool, £23m)
Guly do Prado (released),
Lee Barnard (Southend, huru),
Jonathan Forte (released),
Danny Fox (Nottingham Forest, huru),
Andy Robinson (Bolton, huru),
Tom Leggett (Aston Villa, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Aston Villa, ada haikutajwa)
Dejan Lovren (Liverpool, £20m)
Calum Chambers (Arsenal, £12m)

STOKE CITY

WALIOSAJILIWA
Mame Biram Diouf (Hannover, huru),
Dionatan Teixeira (Banska Bystrica, ada haikutajwa),
Phil Bardsley (Sunderland, huru),
Steve Sidwell (Fulham, huru),
Bojan Krkic (Barcelona, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA

Michael Kightly (Burnley, ada haikutajwa),
Matthew Etherington (ada haikutajwa),
Juan Agudelo (ada haikutajwa)

SUNDERLAND

WALIOSAJILIWA
Billy Jones (West Brom, huru),
Jordi Gomez (Wigan, huru),
Costel Pantilimon (Manchester City, huru)
Patrick van Aanholt (Chelsea, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA

Jack Colback (Newcastle, huru),
Craig Gardner (West Brom, huru),
Phil Bardsley (Stoke, huru),
Billy Knott (Bradford, huru)
Keiren Westwood (Sheffield Wednesday, huru),
Carlos Cuellar (ameruhusiwa),
Andrea Dossena (ameruhusiwa),
Louis Laing (ameruhusiwa),
Oscar Ustari (Newell's, huru),
David Vaughan (Nottingham Forest, huru),
John Egan (Gillingham, huru),
Ignacio Scocco (Newell's, £800,000)

SWANSEA

WALIOSAJILIWA
Marvin Emnes (Middlesbrough, £1.5m),
Bafetimbi Gomis (Lyon, huru),
Lukasz Fabianski (Arsenal, huru),
Stephen Kingsley (Falkirk, ada haikutajwa),
Gylfi Sigurdsson (Tottenham, ada haikutajwa)
Jefferson Montero (Monarcas Morelia, £4m)

WALIOONDOKA

Leroy Lita (ameruhusiwa),
David Ngog (ameruhusiwa),
Daniel Alfei (Northampton, mkopo),
Jernade Meade (ameruhusiwa),
Darnel Situ (ameruhusiwa),
Michu (Napoli, mkopo),
Ben Davies (Tottenham, £10m)
Michel Vorm (Tottenham, £5m)
Alejandro Pozuelo (Rayo Vallecano, ada haikutajwa)

TOTTENHAM

WALIOSAJILIWA
Ben Davies (Swansea, ada haikutajwa)
Michel Vorm (Swansea, £5m)

WALIOONDOKA

Jake Livermore (Hull, £6m),
Heurelho Gomes (Watford, huru),
Cameron Lancaster (ameruhusiwa),
Alex Pritchard (Brentford, mkopo),
Gylfi Sigurdsson (Swansea, mkopo)

WEST BROMWICH ALBION

WALIOSAJILIWA
Brown Ideye (Dynamo Kiev, £10m),
Craig Gardner (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (Manchester City, huru),
Chris Baird (Burnley, huru),
Sebastien Pocognoli (Hannover 96, ada haikutajwa),
Andre Wisdom (Liverpool, mkopo)

WALIOONDOKA

Liam Ridgewell (Portland Timbers, huru),
Billy Jones (Sunderland, huru),
Steven Reid (Burnley, huru),
Cameron Gayle (Shrewsbury, huru),
Diego Lugano (ameruhusiwa),
Zoltan Gera (ameruhusiwa),
Scott Allan (ameruhusiwa),
Nicolas Anelka (ameruhusiwa),
George Thorne (Derby County, ada haikutajwa)

WEST HAM

WALIOSAJILIWA
Enner Valencia (Pachuca, £12m),
Cheikhou Kouyate (Anderlecht, £7m),
Mauro Zarate (Velez Sarsfield, ada haikutajwa),
Aaron Cresswell (Ipswich, ada haikutajwa),
Diego Poyet (Charlton, ada haikutajwa),
Carl Jenkinson (Arsenal, huru)

WALIOONDOKA

Joe Cole (Aston Villa, huru),
Matt Taylor (Burnley, huru),
Stephen Henderson (Charlton, huru),
Jack Collison (ameruhusiwa),
George McCartney (ameruhusiwa),
Callum Driver (ameruhusiwa),
Jordan Spence (ameruhusiwa),

Isike Samuel: Wasanii tuache wivu wa kijinga tusonge mbele

MUIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu nchini, Isike Samwel amesema tabia za wivu, utengano na kutopendana miongoni mwa wasanii ndiko kunakofanya waendelee kulizwa na maharamia kwa kuwaibia kazi zao na kushindwa kusonga mbele.
Hivyo akawataka wasanii kubadilika na kupendana, kushirikiana na kusaidiana bila kujali uzoefu, umaarufu au uwezo wa kiuchumi walionao kwa vile wote wanasafiri katika 'jahazi' moja.
Akizungumza na MICHARAZO, Isike alisema gurudumu la fani ya sanaa hasa ya uigizaji imekuwa ikishindwa kusonga mbele kutokana na wasanii kutopendana na kuoneana kijicho pale mwenzao anapofanya vyema.
Isike alisema hivyo ni wajibu wasanii kubadilika kwani umoja, mshikamano na upendo itasaidia kuwafanya wawe kitu kimoja na kusaidia kupambana na watu wanaowanyonya na kuwaibia kazi zao wanazozitolea jasho kuziandaa.
"Bila umoja, upendo na ushirikiano ni vigumu fani yetu kusonga mbele, wasanii tumekuwa hatupendani wenyewe kwa wenyewe na watu wanaoneana wivu wa kijinga ambao unazorotesha maendeleo ya fani hiyo kwa ujumla," alisema.
Mkali huyo anayejiandaa kutoa filamu yake mpya iitwayo 'Naiogopa Kesho' kupitia kampuni binafsi ya Classic Vision alisema pia wasanii wazoefu wasiogope kuwapiga tafu chipukizi kwa hofu ya kufunikwa kwani hata wao waklisaidia na kupewa nafasi ndiyo maana wapo hapo walipo.

Cheki picha za ajali ya basi la iliyoua watu Arusha



 Muonekano wa basi la Hood kwenda Mbeya baada ya kugongana na Hiace eneo la Kilala, Arusha asubuhi ya leo.


 Wananchi wakiwa wamekusanyika baada ya basi la Hood kwenda Mbeya baada ya kugongana na Hiace eneo la Kilala, Arusha.


 Muonekano wa Hiace hiyo kwa mbele baada ya ajali.







Watu 5 wamekufa baada ya basi la Hood kwenda Mbeya kugongana na Hiace eneo la Kilala, Arusha asubuhi ya leo, wengi wajeruhiwa.

Lampard atua Manchester City kwa mkopo, Pellegrini athibitisha

KOCHA wa Mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa kiungo wa zamani wa Chelsea, Frank Lampard keshokutwa ataanza mazoezi na wachezaji wa Manchester City kwenye uwanja wa Carrington kwa ajili ya msimu mpya wa ligi hiyo.
Pellegrini alisema kuwa Lampard atakuwa mchezaji muhimu kwenye mechi za ligi kuu na ligi ya mabingwa mpaka atakapoondoka kwenda Marekani mwezi Januari mwakani.
City imewasili nyumbani kutoka Marekani ilipokuwa katika maandalizi ya ligi na kucheza mechi kadhaa za kimataifa maalum kabla ya jana jumapili kupoteza nafasi ya kucheza fainali ya michuano hiyo kwa kufungwa kwa penati ikiwa ni mecxhi yao ya pili katika siku nne kupoteza kwa mikwaju ya penati.
Baada ya mechi, Pellegrini kwa mara ya kwanza alizungumzia kumsajili Frank kwa mkopo na kusema maamuzi ya kumchukua kiungo huyo wa kimataifa wa England mwenye miaka 36 ni kumfanya awe fiti kabla ya kuanza kuichezea klabu yake ya New York City mwakani.
Lampard alijiunga na New York City akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Chelsea.
Pellegrini alisema: "Kuanzia jumatano ijayo ataanza kufanya kazi na timu na atacheza mpaka januari na tutaona baada ya hapo".
"‘Kwa wakati huu atafanya kazi na kikosi na atakuwa mmoja wa wachezaji wa kikosi. Atapambana kusaka nafasi"
"Anajua tuna timu nzuri, tuna wachezaji wengi katika nafasi yake na yeye ameongezeka. Tuna mechi nyingi sana hususani za ligi ya mabingwa, kwahiyo ni mtu muhimu sana kwa timu".

Simba wam-delete Wambura na wenzake jumla Msimbazi

Michael Wambura
Mwenyekiti wa Simba, Evance Aveva
ALIYEKUWA mgombea wa nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Soka ya Simba uliofanyika mwezi Juni mwaka huu, Michael Wambura, pamoja na wanachama wengine 70 jana walifutwa rasmi uanachama wa klabu hiyo kutokana na hatua ya kufungua kesi kwenye mahakama za kawaida jambo ambalo ni kinyume na katiba.
Maamuzi ya kumfuta uanachama Wambura pamoja na wanachama wengine yalifikiwa kwa pamoja jana katika Mkutano Mkuu wa mwaka uliofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Wanachama 860 waliokutana jana hawakutaka agenda hiyo ya 12 ijadiliwe na badala yake wakisema kwa sauti kwamba wanachama hao wafutwe mara moja.
Agenda hiyo ya kuwajadili wanachama hao ambao awali walisimamishwa na Kamati ya Utendaji ilianza kujadiliwa saa 6:33 mchana na ilipofika saa 6:49 mchana Aveva alitangaza kwamba wanachama hao 71 wamefutwa uanachama wao kutokana na kwenda kinyume na ibara ya 55 ya Katiba ya Simba.
Kabla ya kutoa maamuzi hayo, Aveva alisema alipokea maoni mbalimbali kutoka kwa wanachama na aliamua kumtumia mmoja wa wadhamini wa klabu hiyo, Ramesh Patel, ili akutane na wanachama hao kwa ajili ya kupata suluhu.
Aveva alisema wanachama hao walielezwa na Patel kwamba wanatakiwa kwanza wafute kesi waliyoifungua Juni 23, mwaka huu katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam na kwamba walikataa na hakuna kati yao ambaye alijitokeza kukanusha kuhusika na uvunjwaji huo wa katiba.
"Natangaza rasmi watu wote 71 sio wanachama wa Simba Sports Club kuanzia leo (jana)", alisema Aveva na kumaliza agenda hiyo iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na wanachama waliohudhuria mkutano huo.
Rais huyo alisema kwamba wanachama walikosea kwa kupinga bila kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba ya Simba, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Fifa.
NIPASHE lilipomtafuta Wambura jana ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa FAT sasa TFF,  kuelezea maamuzi hayo yaliyochukuliwa na mkutano mkuu wa wanachama, alisema "siwezi kuzungumza lolote kwa sasa hadi nitakapopewa barua ya kufahamishwa kufutwa uanachama."

MABADILIKO YA KATIBA
Wanachama wa klabu hiyo pia walifanya mabadiliko kadhaa katika baadhi ya vipengele vya katiba ikiwamo ibara ya 5 inayoainisha aina ya wanachama kwa kuteua wanachama wa heshima ambao waliitumikia Simba kwa muda mrefu na kutoa mchango mkubwa.
Ibara ya 18 sasa inasomeka kuwa wadhamini wa klabu watakuwa wanne na ndiyo wamiliki na wadhibiti wa mali zote za klabu zinazohamishika na zisizohamishika. Pia mkutano mkuu ndiyo utakuwa na mamlaka ya kumuondoa mdhamini kutoka kwenye wadhifa huo baada ya kupata taarifa kutoka katika Kamati ya Utendaji.
Kipengele kingine kilichofanyiwa marekebisho ni cha ibara ya 22 ambacho kinaelezea Mkutano Mkuu wa dharura sasa kinasema kuwa wanachama wasiopungua 1000 waliojiorodhesha ndiyo wanaweza kuomba mkutano huo kwa maandishi na Kamati ya Utendaji itatakiwa kuitisha mkutano ndani ya siku 30 baada ya kuwasilisha ombi.
Ibara ya 25 (8) (111) inayompa nguvu rais wa klabu kuteua wajumbe wengine watano wa Kamati ya Utendaji ambao anaweza kuwabadilisha kwa kadri anavyoona inafaa ilipitishwa lakini baadhi ya wanachama walikuwa wakiipinga kwa madai kwamba itafanya kiongozi huyo wa juu kuwa dikteta.
Wanachama hao pi walitoa ridhaa ya kuundwa kwa Kamati ya Maadili (ibara ya 40) huku ibara ya 42 ikieleza kwamba kutaundwa Kamati ya Nidhamu ya Simba ambayo Mwenyekiti na Makamu wake lazima wawe na taaluma ya sheria.
Mkutano huo uliamua kwamba kila tawi litaendelea kuwa na wanachama kuanzia 50 na wasiozidi 250 na kukataa idadi ya tawi moja kuundwa na wanachama 500 kwa kuhofia 'mapinduzi'.

SITTA, MO WAULA SIMBA
Rais huyo aliyechaguliwa katika uchaguzi uliofanyika Juni 29, mwaka huu pia aliwatangaza wadhamini wapya wa klabu hiyo kuwa ni pamoja na Samwel Sitta, Patel, Hassan Dalali na Adam Mgoyi.
Aveva pia aliwatangaza wanachama wengine wanne ambao watakuwa ni walezi wa Simba kuwa ni aliyekuwa mfadhili wa klabu hiyo, Mohammed Dewji 'Mo', Naibu Waziri Wizara ya Maji, Amos Makalla , Jaji, Thomas Mihayo na Zacharia Hanspoppe.
Wadhamini na walezi hao walithibitishwa na mkutano huo na watatambuliwa kwa muda wa miaka minne.

NIPASHE

Ligi ya wanawake Dar kuanza Agosti 28

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi18rX9xD35fNe7sEatYXVlGC5N3kSwbk9mXkU2mRjmrbN47__02bzOL9rdGPuJ38cYQFWp_mNmtz0P5wM3cy1brDiJZh5qAZscl9N3Ld9QlevvNQlROe21kwK6qmSoSplekcOY7eXmxfQ/s1600/MADEM.JPG 
LIGI ya Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam inatarajiwa kuanza Agosti 28 mwaka huu katika viwanja vya  Benjamin Mkapa, Bandari na Makurumla.

Ofisa Habari wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Mohamed Mharizo alisema kuwa ligi hiyo ni moja ya mkakati wao wa kuimarisha mchezo ili uweze kuwa na hamasa kwa wanawake.

Alizitaja timu zitakazoshiriki ligi hiyo kuwa ni Mburahati Queens, Evergreen Queens, Sayari, Real Tanzanite, Uzuri Queens,  Simba Queens,  BYC Queens, JKT Queens,  Lulu Queens,  Mchangani Sisters, TMK Queens, Msimamo Queens na Mikocheni Queens.

“Kwa kweli ligi ya wanawake nayo ni muhimu kama ilivyo kwa wanaume, lengo letu ni kuona wanawake wanakuwa na ligi yao na sisi tunaona hili ni jambo zuri ambalo litasaidia kupata wachezaji wa timu ya taifa (Twiga Stars).

Mharizo aliyaomba makampuni na taasisi mbalimbali kujitokeza kudhamini ligi hiyo ili iweze kuleta ushindani kwa timu shiriki.

Stars si Riziki AFCON, kama kawa yanyukwa na Msumbiji

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/taifa.jpgUTEJA wa timu ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) mbele ya Msumbiji umeendelea baada ya kutolewa katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa wenyeji Msumbiji (Mambas) katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Zimpeto mjini Maputo.
Kwa ushindi huo, Mambas wamesonga mbele katika mashindano hayo kwa kutinga hatua ya makundi baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-3 baada ya awali kutoka sare ya 2-2 katika mechi iliyochezwa Julai 20, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mambas walimaliza kipindi cha kwanza wakiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na Josemar sekunde chache kabla timu hizo hazijaenda mapumziko.
Mshambuliaji wa Taifa Stars na klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mbwana Samata, aliisawazishia timu yake bao la kwanza katika dakika ya 77 na kuufanya mchezo huo uzidi kuwa mgumu kwa pande zote mbili.
Dakika sita kabla ya filimbi ya mwisho kupulizwa na mwamuzi, Dennis Batte kutoka Uganda, Domingues alizima ndoto za Taifa Stars kutinga hatua ya makundi baada ya kuipatia Mambas bao la pili na la ushindi.
Stars ilikuwa hivi; Deogratius Munishi ‘Dida’, Said Mourad, Shomary Kapombe, Kelvin Yondani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Erasto Nyoni, Thomas Ulimwengu, Mwinyi Kazimoto, John Bocco, Mbwana Samata na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Katika benchi waliwapo Aishi Manula, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Haroun Chanongo, Mrisho Ngassa, Simon Msuva na Amri Kiemba.
Baada ya kushindwa kutinga hatua ya makundi, Tanzania ikiwa chini ya kocha huyo, Mholanzi Mart Nooij, itasubiri kucheza mashindano ya Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki huku ikiwa watazamaji kwenye fainali zijazo za Afcon zitakazochezwa nchini Morocco mwakani.
Wakati huo huo mjini Kigali juzi timu ya soka ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) juzi Jumamosi ilifanikiwa kusonga mbele katika mashindano hayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuiondoa Congo kwa njia ya penalti 4-3 baada ya matokeo ya jumla kuwa 4-4.
Amavubi juzi ilipata ushindi wa mabao 2-0 ikiwa nyumbani wakati Congo nayo ilipata ushindi wa aina hiyo ilipokuwa nyumbani na kusababisha mechi hiyo kutinga hatua ya matuta.
Nyota wa mechi ya juzi mjini Kigali alikuwa ni kipa wa Amavubi, Jean Luc ‘Bakame’ Ndayishimiye, ambaye alidaka penalti tatu za Congo zilizopigwa na Ferebory Dore, Mael Francis Lepicier na Herman Lakolop wakati Delvin Chansel Ndinga, Silver Mbousi Ganvoula na Thierry Koulossa Bifouma walifunga.
Kwa upande wa Amavubi waliopata ni Jimmy Mbaraga, James Tubane, Emery Bayisenge na Patrick Sibomana wakati Haruna Niyonzima aligongesha mwamba na ile ya Meddy Kagere ilidakwa na kipa wa Congo, Chasel Mohikola Massa.
Amavubi sasa itaungana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo Nigeria, Afrika Kusini na Sudan kwenye Kundi A.
Harambee Stars ya Kenya jana ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu na Lesotho hivyo kuyaaga mashindano hayo kufuatia kichapo cha bao 1-0 ilichopata ugenini wiki mbili zilizopita.

Sunday, August 3, 2014

'Hii ndiyo dawa ya kuiepushia TZ aibu michezo ya kimataifa'

Mkurugenzi wa Joyland International School, Fredrick Otieno akihutubia wageni katika hafla iliyofanyika jana shuleni kwao Kigamboni.

Mkurugenzi wa Joyland International School, Fredrick Otieno akicheza muziki na wanafunzi wake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYgRiCanZ-Y6lvhLQ4z0iq94PjDAuEDm0QhQwQJR4BVvyW7w2320pVTf2t08XuLpgwdt99gOtVe0kcASsKme3CzX4uY2nGiLEQQ8qlTuPTM2Nd496XEPZ0ES-4PiJWbuHo_id6_0A-2Vou/s1600/Joy12.JPG
Fredrick Otieno (kulia) akionyesha kipajo chake cha kucheza muziki akichuana na mmoja wa walimu wake
WAKATI mabondia wa Tanzania waliokuwa wakishiriki michezo ya Jumuiya ya Madola nchini Scotaland wakitarajiwa kuanza kurejea kesho kwa mafungu, imefichuliwa dawa ya kuiondolea aibu Tanzania katika michezo ya kimataifa.
Imeelezwa dawa pekee ya Tanzania kufanya vizuri michezo ya kimataifa ni kuwaandaa wachezaji tangu wangali wadogo wakiwa wamejengwa moyo wa kizalendo na ufahamu wa mchezo husika badala ya kukurupuka.
Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Joyland na nyota wa zamani wa soka wa nchini Kenya, Fredrick Otieno, ndiye aliyefichua hayo wakati wa mahafali ya kwanza ya wanafunzi wa Chekechea shuleni kwao, Kigamboni jijini Dar.
Otieno aliyewahi kuichezea Gor Mahia, alisema ili Tanzania iweze kuja kutamba katika michuano ya kimataifa ni lazima ikubali kuwekeza michezo mashuleni na kuwaandaa vijana na siyo kutegemea miujiza.
Alisema amekuwa akijisikia aibu kila mara timu na wanamichezo wa Tanzania wakichemsha kwenye michuano ya kimataifa licha ya ahadi na mbwembwe nyingi na kuamini siasa zikiondolewa michezoni Tanzania itang'ara kimataifa.
"Hakluna njia ya mkato kuyaendea mafanikio katika michezo zaidi ya kuwekeza na kuwajengea misingi imara wenye vipaji tangu utotoni, na katika kuliunga hilo shule yetu inatarajia kuanzisha mtaala wa kimataifa ambao utahusisha poa masuala ya michezo," alisema Otieno.
Otieno alisema kama kila shule itakuwa na programu za michezo kama moja ya somo la darasani na wanafunzi wenye vipaji wakaanza kupikwa mapema ni wazi miaka michache ijayo Tanzania itakuwa na wanamichezo wenye kutisha.
"Zamani michezo ilipewa kipaumbele na kushuhudia Tanzania ikitoa nyota mbalimbali, siasa zilikuja kuua suala hilo. Sasa ni lazima tuamke na Joyland inataka kuonyesha mfano wa kuja kutoa nyota mbalimbali wa michezo watakaokuja kulisaidia taifa na nawahimiza wengine wafanye hivyo," alisema.
Alisema anajisikia aibu kusikia Tanzania imeenda Scotland na kuambulia patupu katika michezo ya Jumuiya ya Madola na kudai ni wakati wa serikali na wadau wa michezo kwa ujumla kujipanga kuifuta aibu hiyo siku za baadae.

KUMEKUCHA TAMASHA LA FILAMU LA DFF 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYuv6bNsqeC15tcE96cfTvXKQZxzGNk4eoEXss_qMYflQhuHglyh0FVFKL3exd6g7HAVgHCUxMXt4ZUmXD8FeTfRaqDyKN4GqIL4FSAS-pd6rFPdAyndp6wzQMGP-4VUpv9C0aEIq7xKU/s640/lulu+1.jpg
Mabalozi wa mwaka jana wa DFF, Ray na Lulu katika pozi
TAMASHA kubwa la Filamu la Dar es Salaam maarufu kama Dar Filamu Festival (DFF) 2014 lipo njiani kufanyika likiwa na kauli mbiu isemayo "Filamu Zetu, Maisha Yetu".
Mratibu Mkuu wa tamasha hilo, Staford Kihore aliiambia MICHARAZO kuwa kila kitu kwa ajili ya tamasha hilo kipo tayari na kuanzia sasa utaratibu utatangazwa.
Kihore alisema tamasha lao limejikita katika kuhakikisha kazi za ndani ambazo zinazalishwa kwa wingi nchi zinapata fursa ya kutangazwa na kuingia katika majumba ya sinema sehemu ambayo ni biashara mpya na inayolipa haraka zaidi tofauti na Dvd na liliasisiwa mwaka jana na kufana.
"Dar Filamu Festival ni mkombozi wa mtayarishaji wa filamu Tanzania, lakini kitu kingine muhimu sana ni ukuzaji na kuitangaza Lugha ya Kiswahili ambayo ni biashara nyingine na alama ya filamu zetu," alisema.
Alisema ni fursa kwa watayarishaji kuwa tayari kupeleka filamu zao kwa ajili ya ushiriki wa tamasha hilo kubwa na la kimataifa, na ni sehemu ya kupata soko jipya kwani tamasha la mwaka huu litahusisha pia wageni kutoka nchi mbalimbali.
“Tamasha la mwaka jana lilifanikiwa sana kwani kwa mara ya kwanza tuliweza kuona filamu katika ubora mkubwa kuanzia sauti, picha na mambo mengine, mwaka huu tunakuja na kauli mbiu "Filamu Zetu, Maisha Yetu'" alisema Kihore.
Aliongeza kuwa, pia tamasha la DFF 2014 litaambatana na semina za utengenezaji wa filamu utoaji wa tuzo kwa filamu zilizofanya vizuri kwa mwaka wa 2013/2014 ikiwa ni katika hali ya kuwatia motisha watengenezaji wa filamu Bongo.
Alidokeza kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kutangaza mabalozi wa DFF 2014 baada ya mwaka kamati yao kuwateua  Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Vincent Kigosi 'Ray'.

Tip Top Connection, TMK Wanaume wakumbushia Chama Kubwa

http://www.timesfm.co.tz/content/uploads/2014/7/10/cache/ww_full.JPG
Wakurugenzi wa makundi ya Top Top na TMK Wanaume Family, Said Fella na Babu Tale
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEji03SsvzTETvUSLX83T9Hg7KAhg3k3Q-EnQ9WOjWg-mhWbbEtjsrKzinlaFzWotAvkq_qOaxwJiGHuOv2i6p1BVJf7AKY7CUUrESwrzZK4bnTQZW_GWhAYo2rBp02Mnw0GKOigVxglqtg/s400/19.JPG
Baadhi ya vichwa vya Tip Top
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqIjwnLbpME9u1DjM5-e6u8k893BW186Gkejj3lQqLtuoBZp7DINoSYUtldaQIK7pgzbyKZuQQ5m3iFQ8Iqd4kBZq6_BUF4IeAXoSW3up9yRvGKVkXU8dvhrL5WNcTpSsbAS5WAw7IxvQ/s640/b2b31624f03011e29c2822000a1fbe4c_7.jpg
Majembe ya TMK Wanaume Family
MAKUNDI maarufu ya muziki wa kizazi kipya nchini, Tip Top Connection na TMK Wanaume Family wameungana tena na kurekodi kati ya pamoja wakikumbushia enzi za kibao chao cha 'Chama Kubwa'.
Makundi hayo yanayoongozwa na wadau wakubwa wa muziki nchini Said Fella 'Mkubwa' na Hamis Tale 'Babu Tale' yamerekodi wimbo huo katika studio za Barning Records, japo mpaka sasa bado hawajaupa jina mpaka kwanza wajadiliane kuutafuta jina muafaka.
Akizungumza na MICHARAZO, mmoja wa wasanii wanaounda makundi hayo, Madee alisema wimbo huo unatarajiwa kuachiwa hewani mara baada ya kutungiwa jina na ni moja ya wimbo bomba.
"Baada ya kitamboi kirefu tangu tutoe Chama Kubwa, Tip Top Connection na TMK Wanaume Family tumeungana tena na kufyatua wimbo wa pamoja ambao bado hatujaupa jina mpaka sasa," alisema Madee.
Madee alisema wimbo huo umewashirikisha wasanii wa makundi hayo yote akiwamo yeye mwenyewe (Madee), Tundaman, Dogo Janja, Chege, Mheshimiwa Temba.
Msanii huyo aliongeza mara baada ya wimbo huo kuanza kurushwa hewani wataanza mchakato wa kurekodi video ya wimbo huo.

Madee kuweka shida zake videoni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjQ4vjrMKRzzb0ZkNWac2z2qZhcVySxPvwckgE1ntwoUPIkAMY62tPhffhV_lbRmQUiLRZR1a98qDlDby0L_97A_F5rsEovrJo4tKMp3OhS-d0VCM2XeJ6YRR2siJzlXomJPUD_WdZ2H0pX/s1600/Mtu+mzima+Madee.jpg
Madee katika pozi
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya, Hamad Ally 'Madee' a.k.a Rais wa Manzese, anajianda kuanza kurekodi video ya wimbo wake mpya unaoendelea kutamba katika vituo vya redio uitwao Ni Sheeda'.
Akizungumza na MICHARAZO, Madee alisema ndani ya wiki mbili zijazo video ya wimbo huo itakuwa hewani kwani ameanza maandalizi ya kuirekodi.
Madee alisema video hiyo itarekodiwa na kampuni ya Next Level Production chini ya mtaalam Adam Juma na itafanyiwa katika maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam.,
"Nipo katika maandalizi ya kurekodi video ya wimbo wangu mpya wa 'Ni Sheeda' (Ni Shida) kazi hiyo itafanywa na Adam Juma na huenda ikakamilika ndani ya wiki mbili kabla ya kuiachia hewani," alisema.
Madee alisema anaharakisha kutoa video hiyo kutokana na maombi ya mashabiki wengi wa muziki ambao wanataka kuona uhalisia wa wimbo huo ambao umekuwa gumzo kwa sasa nchini.
"Mashabiki wamekuwa wakiulizia mno juu ya video yake ndiyo maana nataka kuitoa mapema kabla ya kufanya mambo mengine," alisema Madee.
Mkali huyo anayeliongoza kundi la Tip Top Connection, kabla ya wimbo huo wa 'Ni Sheeda' Madee alitamba na nyimbo kama 'Pesa', 'Kazi yake Mola', 'Tema Mate', 'Pombe Yangu', Hip Hop Haiuzi na 'Yote Maisha'.

Jennifer Mgendi ajianda kumtoa Mama Mkwe

http://www.jennifermgendi.com/images/gallery/1361202026.JPG
Jennifer Mgendi katika pozi
MUIMBAJI nyota wa Nyimbo za Injili nchini ambaye pia ni muigizaji wa filamu, Jennifer Mgendi amekamilisha filamu yake mpya iitwayo 'Mama Mkwe' ambayo amewashirikisha wasanii kadhaa nyota wa filamu na miondoko ya Injili akiwamo Mussa Banzi na Bahati Bukuku.
Filamu hiyop inatarajiwa kuachiwa hadharani wakati wowote ndani ya mwezi huu na Jennifer amewataka mashabiki wa filamu wasiikose filamu hiyo kutokana na kubeba ujumbe mwanana wenye mafunzo makubwa kwa jamii.
Akizungumza na MICHARAZO, Jennifer alisema filamu hiyo iliyoongozwa na Mgeni Khamis na Chrissant Mhega wa Mega  Video Production imekamilika wiki iliyopita na sasa ipo katika maandalizi ya kuachiwa kwa sasa.
Jennifer anayetamba na albamu ya Hongera Yesu, alisema ndani ya filamu hiyo inayozungumzia mkasa wa mama mkwe anayemlilia mwanae wa kiume kumletea mjukuu na kuzua kizaazawa wamo pia Senga,Bi Bi Esther, Christine Matai, Husna Chobis. yeye (Mgendi)  na wengine ambao wameinoigesha vilivyo.
"Nimekamilisha filamu yangu mpya ya 'Mama Mkwe' ambayo nimeigiza mimi, Bahati (Bukuku) Christine Matai, Senga, Bi Esther, Mussa Banzi na wengine. Ni filamu yenye mafunzo makubwa kwa jamii na hasa mama wakwe wanaoingilia ndoa za watoto wao," alisema.
Kabla ya filamu hiyo, Jennifer amewahi kutamba na filamu kadhaa kama 'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

Hivi ndivyo mahafali ya kwanza ya Pre Primary Joyland yalivyofana

Mgeni Rasmi wa Mahafali hayo Bi Bushra Malik Regional Development Manager wa Edexcel akizungumza kwenye shughuli hiyo zilizofanyika jana Kigamboni, Dar es Salaam
Mmoja wa wahitimu wa kozi ya Kiingereza inayotolewa bure shuleni Joyland akipokea cheti chake toka kwa Bi Bushra Malik

Mmoja ya wanafunzi waliofanya vyema katika mitihani akipewa zawadi yake na mmoja wa wageni waalikwa wa hafla hizo
Mwanafuzi Ansilath Kwariko akilia kwa furaha wakati akijiandaa kupokea zawadi yake
Madogo kwa kuimba hawajambo
Wahitimu wa Pre Primary wakiongozwa na mwalimu wao kuingia eneo la tukio
Sisi tunajua kuimba
Mkurugenzi wa Joyland International School, Fredrick Otieno akisaini mkataba wa kurushwa kwa vipindi vya shule yake na kituo cha Channel Ten huku akishuhudiwa na mwakilishi wa Idara ya Masoko ya kituo hicho

Saini hapa.....Tutakurusha hewani mpaka basi! Mwakilishi wa Channel Ten akimuangalia Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Joyland akisaini mkataba walioingia baina yao kwa mujibu wa taarifa zilizotangazwa kwenye hafla hiyo jana.
Wanafunzi wa Grade 5 wakitumbuiza

Siyo kuhitimu tu hata kuimba nasi tunajua
Mkurugenzi wa Joyland, Fredrick Otieno  akionyesha ufundi wa kucheza akichuana na wanafunzi wake

Yebhaa! Mnacheza hivi bhana!
Full Vipaji Joyland International School
Hongera kwa kumaliza kozi!
Msosi nao ulikuwapo kuwafariji wahitimu

Kadhalika vinjwaji navyo viliburudisha makoo ya watoto

Tupo makini na watoto wenu, tunawaangalia vya kutosha kuhakikisha wapo salama
Mkurugenzi wa Joyland International School, Fredrick Otieno akizungumza kwenye hafla hiyo
WAZAZI na walezi nchini wamehimizwa kuwapatia elimu watoto wao ili kuwajengea msingi imara wa maisha yao kwa kuwa, elimu ni hazina isiyoweza kuharibika au kuibwa na yeyote.
Aidha wazazi na walezi pia wamekumbushwa kujenga utamaduni wa kuwa na mahusiano mazuri baina yao na walimu wanaosoma watoto wao sambamba na kufuatilia nyendo za watoto wao ili kulinda wasiharibike.
Wito huo ulitolewa juzi na Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Joyland, Fredrick Otieno wakati akizungumza na wazazi na walezi waliohudhuria mahafali ya kwanza ya wahitimu wa Chekechea wa shule hiyo.
Otieno alisema elimu ndiyo msingi wa kila kitu kwa maisha ya binadamu, hivyo wazazi wajenge utamaduni wa kuwa wepesi kuwasomesha watoto wao ili kuwajengea msingi mzuri wa mustakabali wa maisha yao ya ukubwani.
Alisema wapo baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa wepesi kuwanunulia watoto wao vitu vyenye thamani, lakini wanakuwa wagumu kuwalipia watoto ada au kuwapatia elimu bora bila kujua kama wanawaharibia maisha yao ya ukubwani ambayo hujengwa na elimu bora ya utotoni.
"Dunia ya sasa imebadilika, bila elimu ni kazi bure hivyo wazazi na walezi wakubali kujinyima mradi kuwapatia watoto wao elimu bora itakayowasaidia maisha yao ya ukubwani," alisema.
Alidokeza katika kuhakikisha shule yao inaendelea kuwapatia watoto elimu bora wanatarajia kuanzisha mtaala wa kimataifa utakaoenda sambamba na ule wa taifa ambao kwa sasa unafundishwa katika shule hiyo.
Nao wageni rasmi wa mahafali hayo, Bushra Maliki na Mchungaji Albert Okanga katika hotuba zao waliwaasa wazazi kujenga uhusiano mzuri na walimu ili kuhakikisha watoto wanapata elimu bora na malezi mazuri kwa maisha yao ya baadae.
Bushra ambaye ni Meneja Maendeleo wa Edexcel tawi la Tanzania, alisema amejitolea kushirikiana na uongozi wa shule hiyo ya Joyland ili kuhakikisha wanatoa elimu bora kwa ngazi ya kimataifa kwa lengo la kuinua elimu nchini na kusaidia watoto wa Tanzania kupata elimu inayostahiki katika dunia ya sasa.
Mchungaji Okanga kwa upande wake alisisitiza kwa kusema ni wazazi wanakijita katika kuwapa watoto huduma vipaumbele kwa ajili ya kuwajengea msingi imara wa maisha kuliko kuwastarehesha, sambamba na kuwa karibu na watoto wao kuwasikiliza kujua matatizo waliyonayo na kuwasaidia kwa haraka.
Katika mahafali hayo wanafunzi waliofanya vizuri mbali na wale wahitimu wa Pre Primary walizawadiwa sambamba na wahitimu wa mafunzo ya lugha ya Kiingereza yanayotolewa bure shuleni hapo kwa lengo la kusaidia ufahamu wa lugha hiyo ya kigeni.