STRIKA
USILIKOSE
Friday, January 5, 2018
Dk 70 Yanga bado ipo mbele ya kwa mabao 2-0
AJIB anakosa bao la wazi dakika ya 70, matokeo bado ni yale yale, Yanga inaongoza mabao 2-0. Pambano ni kali kwelikweli Uwanja wa Amaan.
Mkomola anaiandikia Yanga bao la pili
Dakika ya 60 matokeo bao 1-0 Yanga inaongoza
Simba kazi wanayo kwa Azam
![]() |
| Kocha Masudi Djuma akimkumbatia nahodha msaidizi, Mohammed Hussein 'Tshabalala', huku aliyekuwa Kocha Mkuu Joseph Omog na Mratibu, Abbas Ali wakishuhudia |
![]() |
| Wachezaji wa Simba wakijifua mazoezini |
RAHIM JUNIOR
HAKUNA namna ila kushinda tu. Ndivyo ambavyo Simba inapaswa kufanya wakati kesho Jumamosi itakaposhuka Uwanja wa Amaan, mjini Unguja kupepetana na Azam katika mechi ya kisasi itakayoamua hatma yao ya kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani hapa.
Simba ambayo ilipata ushindi wa kishindo usiku wa jana kwa kuikandika Jamhuri Pemba kwa mabao 3-1, itavaana na Azam usiku wa kesho na timu yoyote ikishinda itajihakikishia nafasi ya kutinga nusu fainali na kusubiri kujua itaungana na nani.
Azam inayotetea taji hilo ililolipata mwaka jana kwa kuichapa Simba kwa baoa 1-0 katika fainali, huo utakuwa ni mchezo wao wa mwisho na kwa sasa ikiwa na alama sita baada ya mechi tatu, kutokana na kupigwa 1-0 jioni ya leo na URA ya Uganda.
Simba yenyewe ipo nafasi ya tatu katika Kundi B ikiwa na alama nne baada ya mechi mbili, huku URA wakiongoza msimamo na pointi zao saba baada ya mechi tatu. Pambano la mwisho la Waganda hao litakuwa ni dhidi ya Simba litakalopigwa Jumatatu jioni.
Hata hivyo Simba chini ya Kocha, Masudi Djuma imeonyesha kuwa na mabadiliko makubwa kulinganisha na ilipokuwa chini ya Mcameroon, Joseph Omog aliyetimuliwa na kama itacheza kama ilivyocheza mechi yao iliyopita, Azam ni lazima ijipange kwa Vijana hao wa Msimbazi.
Mrundi huyo aliyewapa taji Rayon Sports ya Rwanda, anatarajiwa kuendelea kumtegemea nahodha wake, John Bocco 'Adebayor' kuongoza mashambulizi akisaidiana wa nyota wengine, huku beki kiraka, Asante Kwasi aliyetupia kambani jana katika mechi yake ya kwanza akiwa na uzi wa Simba akitarajiwa kufanya yake.
Kwasi alisajiliwa na Simba hivi karibuni akitokea Lipuli na ameanza kuonyesha makeke yake na kuwafanya mashabiki wa Simba kutabasamu kwa kuamini kuwa timu yao inazidi kunoga, ikiwa siku chache tangu watolewa na kutemeshwa taji la Kombe la FA kwa kufungwa na timu ya Daraja la Pili, Green Warriors.
Azam iliyokuwa haijafungwa bao lolote katika michuano hiyo tangu mwaka jana walipobeba taji bila kupoteza, sio ya kubeza kwanui ukuta wake unaoongozwa na Mghana, Yakubu Mohammed na safu kali ya ushambuliaji chini ya Mghana mwingine, Bernard Arthur na chipukizi Paul Peter na Zayd na Shaaban Idd huenda isikubali kirahisi kupoteza mchezo huo na kutemeshwa taji la michuano hiyo.
Mbali na mchezo huo mapema jioni Singida United itakuwa uwanjani kupepetana na JKU katika mechi nyingine.
Ajibu atupia kambani, Yanga 1-0 Taifa Jang'ombe
RAHIM JUNIOR
IBRAHIM Ajib ameitanguliza Yanga mguu mmoja kwenye nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika chache kabla ya kwenda mapumziko akimalizia mpira wa shuti kali ha Yohana Nkomola kuokolewa na kipa wa Jang'ombe.
Kwa sasa pambano hilo lipo mapumziko na kama matokeo yatasalia hivyo, basi Yanga itaifuata Singida United iliyotangulia mapema leo mchana kwa kuilaza Mlandege.
Katika mchezo wa leo unaochezwa Uwanja wa Amaan usiku huu, Yanga imechezesha kikosi cha vijana zaidi, huku wakongwe kama kina Youthe Rostand, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amissi Tambwe, Papy Kabamba Tshishimbi wakiwa jukwaani.
IBRAHIM Ajib ameitanguliza Yanga mguu mmoja kwenye nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika chache kabla ya kwenda mapumziko akimalizia mpira wa shuti kali ha Yohana Nkomola kuokolewa na kipa wa Jang'ombe.
Kwa sasa pambano hilo lipo mapumziko na kama matokeo yatasalia hivyo, basi Yanga itaifuata Singida United iliyotangulia mapema leo mchana kwa kuilaza Mlandege.
Katika mchezo wa leo unaochezwa Uwanja wa Amaan usiku huu, Yanga imechezesha kikosi cha vijana zaidi, huku wakongwe kama kina Youthe Rostand, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amissi Tambwe, Papy Kabamba Tshishimbi wakiwa jukwaani.
Chirwa apigwa stop, Kocha Mbao ala kibano
![]() |
| Obrey Chirwa |
![]() |
| Kocha wa Mbao, Etienne Ndayiragije |
MZAMBIA Obrey Chirwa ambaye ameididia klabu ya Yanga kucheza na kutimkia kwao Zambia, amesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuitimulia timu yake kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.
Chirwa ameasimamiwa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi maarufu kama Kamati ya Saa 72 iliyokutana jana Alhamisi na kujadili mechi mbalimbali za Ligi Kuu (VPL) Daraja la Kwanza (FDL) na Daraja la Pili (SDL).
Soma maamuzi ya kamati hiyo na adhabu zake katika ligi hizo;
LIGI KUU YA VODACOMMechi namba 72 (Mbeya City 0 vs Simba 1).Kamishna wa mechi hiyo Billy Mwilima amepewa Onyo Kali kwa kuruhusu mchezaji Hamisi Msabila wa Mbeya City kucheza mechi bila kuonyesha leseni, hivyo kukiuka Kanuni ya 14(16 na 17) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.
Mechi namba 81 (Ndanda 1 vs Njombe Mji 1). Klabu ya Ndanda imepigwa faini ya sh 500,000 (laki tano) kwa kutowasilisha orodha ya wachezaji wake (team match list) kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre- match meeting) kama ilivyoainishwa katika Kanuni ya 14(2k) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu dhidi ya Ndanda katika mechi hiyo iliyofanyika Novemba 24, 2017 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Pia Kamati imeiomba Sekretarieti ya Bodi ya Ligi kutoa Waraka mwingine kwa klabu kuzikumbusha kuhusu kutoa orodha ya wachezaji kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting).
Mechi namba 83 (Yanga 1 vs Tanzania Prisons 1). Tanzania Prisons imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi ya Tanzania Prisons katika mechi hiyo iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa Azam Complex ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Wachezaji Lambart Sabiyanka wa Tanzania Prisons na Obrey Chirwa wa Yanga wamesimamishwa kwa kuzingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kutokana na kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu, wakisubiri malalamiko dhidi yao kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.
Pia Kamati imeiomba TFF iipatie Bodi ya Ligi uamuzi (ruling) wa Kamati ya Nidhamu juu ya mchezaji wa Yanga kusimamishwa baada ya mechi dhidi ya Mbao FC wakati akisubiri mashtaka yake ili kuufanyia kazi kwa ajili ya mapendekezo ya marekebisho ya Kanuni.
Mechi namba 84 (Mbao 1 vs Mwadui 0). Klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuruka uzio wa ndani na kwenda kushangilia katika eneo lisiloruhusiwa katika mechi iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Adhabu dhidi ya Mbao FC ni uzingativu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 90 (Lipuli 0 vs Tanzania Prisons 1).Mtunza Vifaa wa Lipuli FC, George Mketo amesimamishwa akisubiri suala lake la kuwatukana waamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Samora mjini Iringa kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Mechi namba 94 (Mbao 2 vs Yanga 0). Kocha wa Mbao FC, Etiene Ndayiragije amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kushindwa kuheshimu taratibu na kuonywa mara tatu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Ndayiragije katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(11) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Pia klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 96 (Mwadui 2 vs Ruvu Shooting 1).Klabu ya Mwadui imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyochezwa Januari 1, 2018 Uwanja wa Mwadui Complex. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 42(10) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu
LIGI DARAJA LA KWANZAMechi namba 37 Kundi B (JKT Mlale 1 v Mufindi United 0). Klabu ya Mufindi United imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na Kiongozi wake Hussein Turuka kutoa lugha chafu kwa Mwamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 mjini Songea. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 40 Kundi B (Mawenzi Market 1 v Polisi Dar 0). Klabu ya Mawenzi Market imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kutaka kuwapiga waamuzi na kuwashawishi ball boys kuchukua mipira iliyotoka nje na kuwapelekea jukwaani. Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 31, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Pia Kocha Mkuu wa Mawenzi Market amepewa Onyo Kali kwa kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-macth meeting) kwa dakika saba. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.
Mechi namba 39 Kundi C (Dodoma FC 3 v Alliance Schools 2). Klabu ya Alliance Schools imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa timu yake kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 mjini Dodoma. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mchezaji Shaban William wa Alliance Schools amesimamishwa, hadi suala lake la kumpiga Mwamuzi litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Waamuzi wote wanne; Andrew Shamba, Abdallah Mkomwa, Athuman Athuman na Omari Juma wamefungiwa miaka mitatu kila mmoja kwa kuchezesha mechi hiyo chini ya kiwango. Adhabu dhidi ya waamuzi hao imezingatia Kanuni ya 38(1a) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.
Pia Kamishna wa mechi hiyo Mackshem T. Nzunda amefungiwa miaka mitatu kwa kushindwa kutoa taarifa ya mchezo kwa usahihi. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 39(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Kamishna.
Kamati imeomba suala la waamuzi hao ambao baadhi yao ni wa Ligi Kuu, kupitia TFF liwasilishwe kwenye chombo chenye dhamana ya kisheria ya rushwa kufanyiwa uchunguzi zaidi.
LIGI DARAJA LA PILIMechi namba 18 Kundi B (Africans Sports 1 v Kitayosce 2). Kitayosce imepigwa faini ya sh. 50,000 (elfu hamsini) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi yao katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 jijini Tanga imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu taratibu za Mchezo.
Mechi namba 16 Kundi C (Mighty Elephant 1 v Green Warriors 3). Kocha wa Green Warriors, Azish Kondo amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kutumia lugha chafu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Kondo katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 mjini Songea imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(10) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Mechi namba 18 Kundi C (Mkamba Rangers 0 v Boma 1). Klabu ya Mkamba Rangers imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuingia uwanjani (pitch). Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 29, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 16 Kundi D (Area C v Nyanza). Timu ya Nyanza FC imeshushwa madaraja mawili na matokeo ya michezo yako yote imefutwa kwa kutofika uwanjani bila kutoa sababu yoyote na kusababisha mechi yao dhidi ya Area C iliyokuwa ichezwe Desemba 29, 2017 mjini Dodoma isifanyike.
Uamuzi huo dhidi ya Nyanza FC umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani. Pia kwa mujibu wa Kanuni ya 28(2) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani, imepigwa faini ya sh. 2,000,000 (milioni mbili) ambapo sh. 1,000,000 (milioni moja) itachukuliwa na Bodi ya Ligi, na sh. 1,000,000 (milioni moja) italipwa timu pinzani.
Vilevile Kamati imeiomba Sekretarieti kukiandikia barua Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Manyara (MARFA) ili kujua tatizo la timu hiyo.
MVUVUMWA VS FRIENDS Kamati imeipa Friends Rangers ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Mvuvumwa kuchezesha wachezaji ambao hawajasajiliwa (non qualified) katika mechi ya Kundi A Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya timu hizo iliyochezwa Oktoba 29, 2017. Mvuvumwa ilishinda mechi hiyo mabao 4-1.
Uamuzi huo dhidi ya Mvuvumwa umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(18) na 42(20) za Ligi Daraja la Kwanza. Nayo Friends Rangers imepewa ushindi kwa kuzingatia Kanuni ya 14(37) na ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.
Vilevile viongozi wa Mvuvumwa waliohusika kughushi leseni zilizotumiwa na wachezaji hao ambao hawakusajiliwa watafikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya TFF kwa ajili ya hatua zaidi.
ALLIANCE SCHOOLSKamati imepitia malalamiko ya Alliance Schools kupinga uchezeshaji wa Mwamuzi wa mechi yao dhidi ya Dodoma FC iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Baada ya kupitia hoja zote, Kamati haikukubaliana na malalamiko hayo kwa vile hayakuwa na vielelezo wala kanuni za kuyathibitisha. Pia kwa suala la muda, Kamati imejiridhisha kuwa kazi ya kutunza muda ni ya Mwamuzi.
Yanga, Azam, Singida wasipojipanga wamekwisha Kombe la FA
![]() |
| Kikosi cha Yanga |
| Azam FC |
VIGOGO wa Ligi Kuu Bara, Yanga, Azam na Singida United, lazima zijipange baada ya kupewa wababe katika mechi za Raundi ya Tatu ya michuano ya Kombe la FA.
Katika droo ya michuano hiyo iliyofanyika asubuhi ya leo ikihusisha timu 32 zilizopenya hatua hiyo, Yanga imepewa wababe wa Mbeya City, Ihefu FC ya Mbalali, huku Singida wakikabidhiwa watemi wea Simba, Green Warriors.
Azam yenyewe imepangwa kupepetana na Shujaa FC katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Mkamba CCM, mjini Morogoro ili kusaka tiketi ya kuingia Robo fainali.
Katika raundi hiyo ya imehusisha timu nne za Mabingwa wa Mikoa (RCL), tatu za Ligi Daraja la Pili (SDL), 12 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na klabu 13 za Ligi Kuu zilizopenya kwenye mechi zao za raundi ya pili zilizochezwa mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mechi za raundi hiyo zitachezwa kati ya Januari 31 na Febaruari Mosi kwenye miji tofauti kulingana na ratiba ilivyo.
Kabla ya mechi hizo za raundi ya tatu kuchezwa tayari zimechezwa mechi 59 na magoli 137 yamefungwa.
Cheki ratiba kamili ilivyo na viwanja vyake:
Kagera Sugar v Buseresere FC- Kaitaba, Bukoba
Shupavu FC v Azam FC- Mkamba CCM, Morogoro
Majimaji Rangersv Mtibwa Sugar - Ilulu, Lindi
Kariakoo Lindi v Mbao FC- Ilulu, Lindi
Prisons v Burkina Fc- Sokoine, Mbeya
Green Warriors v Singida FC-Azam Complec, Dar
Mwadui FC v Dodoma FC- Mwadui, Shinyanga
Ihefu FC v Yanga SC-Sokoine, Mbeya
JKT Tanzania v Polisi Dar- Uhuru, Dar
Polisi Tanzania v Friends- Ushirika, Moshi
Pamba SC v Stand United-Kirumba, Mwanza
Ndanda FC v Biashara United-Nangwanda Kiluvya United v JKT Oljoro-Mabatini, Pwani
Njombe Mji v Rhino Rangers-Sabasaba Njombe
Majimaji Fc v Ruvu Shooting -Majimaji, Songea
KMC v Toto Africans- Uhuru, Dar
Singida United yatangulia nusu fainali, Azam yatibuliwa Mapinduzi Cup
![]() |
| Kikosi cha Azam ambacho jioni hii kimelala mbele ya URA |
![]() |
| Wachezaji wa Singida wakipongezana katika mechi yao ya Kombe la Mapinduzi |
![]() |
| Danny Usengimana akijiandaa kupioga penalti iliyoiandikia Singida bao la kuonmgoza jioni ya leo |
Singida imefikisha pointi 9 ikiwa imecheza mechi tatu na kukata tiketi moja ya Kundi A ambalo lina timu ya Yanga inayoshuka dimbani usiku huu kuumana na Taifa Jang'ombe katika mechi nyingine kali ya michuano hiyo.
Walima Alizeti hao wamejihakikishia nafasi hiyo kutokana na ukweli timu zilizopo nyuma yake ni Yanga pekee inayoweza kuzipiku pointi ilizonazo, huku pia ikiwa na michezo miwili mkononi ya kufungia makundi.
Mabao ya Danny Usengimana aliyefungwa kwa penalti dakika ya 29 na mengine Kenny Ally la dakia ya 37 na lile la Lubinda Mundia la dakika ya 56 yalitosha kuipa ushindi Singida inayoshiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza mwaka huu.
Wakati Singida ikichekelea kutangulia nusu fainali, watetezi wa taji hilo, Azam ilinyooshwa na URA ya Uganda kwa bao 1-0 na kutenguliwa rekodi yao iliyokuwa ikishikilia kwa kutoruhusu bao lolote tangu michuano ya 2017.
Azam ilibeba taji hilo Januari mwaka jana kwa kucheza mechi zake zote bila kuruhusu bao lolote achilia mbali kupoteza mchezo, lakini URA wakiwa na utulivu mkubwa waliwaotea Matajiri nao na kuwatengua 'udhu' kwa bao la dakika ya 32 lililofungwa na Nicholaus Kabaga akipiga tobo kipa Razak Abalora.
Hata hivyo Azam bado ina nafasi ya kupenya hatua ya nusu fainali kama itapata matokeo mazuri katika mechi yao ya mwisho kesho dhidi ya Simba ambayo inafuatia nyuma yao kwa alama zao nne baada ya kucheza mechi mbili.
URA imefikisha pointi saba na kuongoza msimamo wa kundi hilo la B, kisha Azam ikifuata na alama zao 6. Timu zote tatu zina nafasi sawa ya kutinga nusu fainali kupitia kundi hilo na zinatarajiwa kukutana zenyewe kuamua hatma yao.
Cheki matokeo ma msimamo mzima wa michuano hiyo inayoingia mwaka wa 11 tangu kuasisiwa kwake mnamo Mwaka 2007;
Kombe la Mapinduzi 2018
Kundi A
Mlandege, JKU, Zimamoto, Yanga, Taifa Jang'ombe, Singida United
Kundi B
Jamhuri, Mwenge, Simba, Azam, URA
Des 29, 2017
Mlandege 2-1 JKU
Jamhuri 0-1 Mwenge
Zimamoto 2-1 Taifa Jang’ombe
Des 30, 2017
Zimamoto 0-1 JKU
Taifa Jang’ombe 1-0 Mlandege
Des 31, 2017
Azam 2-0 Mwenge
Jamhuri 1-1 URA
Jan 01, 2018
Mlandege 2-1 Zimamoto
JKU 0-0 Taifa Jang’ombe
Jan 02, 2018
Singida United 3-2 Zimamoto
Simba 1-1 Mwenge
Yanga 2-1 Mlandege
Jan 03, 2018
URA 1-0 Mwenge
Azam 4-0 Jamhuri
Taifa Jang’ombe 1-3 Singida United
Jan 04, 2018
JKU 0-1 Yanga
Simba 3-1 Jamhuri
Jan 05, 2018
Mlandege 0-3 Singida United
URA 1-0 Azam
Yanga v Taifa Jang’ombe
Jan 06, 2018JKU v Singida United
Simba v Azam
Jan 07, 2018Zimamoto v Yanga
Jan 08, 2018Simba v URA
Yanga v Singida United
Nusu FainaliJan 10, 2018Kinara Kundi A v
Mshindi wa Pili Kundi B
Kinara Kundi B v
Mshindi wa Pili Kundi A
Saa 2:15 usiku
FAINALIJan 13, 2018Saa 2:15 usiku
Msimamo:
Kundi A
P W D L F A Pts
1.Singida 3 3 0 0 9 3 9
2.Yanga 2 2 0 0 3 1 6
3.M'ndege5 2 0 3 5 7 6
4.Taifa 4 1 1 2 3 5 4
5.JKU 4 1 1 2 2 3 4
6. Z'moto 3 1 0 2 3 4 3
Kundi B
P W D L F A Pts
1.URA 3 2 1 0 3 1 7
2.Azam 3 2 0 1 6 1 6
3.Simba 2 1 1 0 4 1 4
4.Mwenge4 1 1 2 2 4 4
5.Jamhuri4 0 1 3 2 9 1
Tuesday, September 12, 2017
Dude linaamshwa Champion League, nani kucheka?
![]() |
| Picha tofauti zikionyesha Juventus wakipasha kwenye Uwanja wa Nou Camp kabla ya leo usiku uliamsha dude dhidi ya Barcelona |
KAZI imeanza kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati mechi za makundi kwa msimu huu wa 2017-2018 ukianza rasmi usiku wa leo kwa kushuhudiwa mechi nane, lakini macho na masikio yakielekezwa Nou Camp, wakati Kibibi Kizee cha Turin, Juventus itakapoifuata Barcelona katika mechi iliyovuta mashabiki wengi wa michuano hiyo.
Juventus imeenda Hispania ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa fainali zilizopita dhidi ya mahasimu wa Barcelona, Real Madrid, lakini wakijivunia rekodi ya kuanza Ligi Kuu ya Italia Serie A ikishinda mechi zao tatu zote na kufunga mabao 10 na kukaa kileleni ikizizidi ujanja Napoli na Inter Milan kwa tofauti na uwiano wa mabao.
Kikosi hicho cha Juve kilifanya mazoezi jana kwenye Uwanja wa Nou Camp kikiwa na nyota wake wote wakiwamo wakali kinara wa mabao Paul Dyabala, Gonzalo Higuain na Mario Mandzukic.
Wenyeji wataendelea kumtegemea zaidi nyota wao Lionel Messi na Luis Suarez kuweza kulinda heshima yao katika michuano hiyo baada ya msimu uliopita kukwamia njiani kwa aibu.
Mbali na mechi hiyo, pia leo kuna gemu kali yenye mvuto Manchester United waliorejea kwenye michuano hiyo kwa mlango wa uwani itakuwa nyumbani kukabiliana na Basel, huku Chelsea wakicheza na Qarabag, PSG ikiwa na wachezaji ngali zaidi kwa sasa duniani Neymar na Kylian Mbappe watakuwa ugenini nchini Scotland kuvaana na Celtic.
RATIBA KAMILI LIGI YA MABINGWA ULAYA
Leo, Jumanne
Celtic v PSG (Saa 3:45 usiku)
Benfica v CSKA Moskva (Saa 3:45 usiku)
Man United v Basel (Saa 3:45 usiku)
Olympiakos v Sporting CP (Saa 3:45 usiku)
Bayern Munichv Anderlecht (Saa 3:45 usiku)
Roma v At.Madrid (Saa 3:45 usiku)
Chelsea v Qarabag (Saa 3:45 usiku)
Barcelona v Juventus (Saa 3:45 usiku)
Kesho Jumatano
Maribor v Spartak Moskva (Saa 3:45 usiku)
Tottenham v B.Dortmund (Saa 3:45 usiku)
RB Leipzig v Monaco (Saa 3:45 usiku)
Feyenoord v Man City (Saa 3:45 usiku)
Shakhtar v Napoli (Saa 3:45 usiku)
Liverpool v Sevilla (Saa 3:45 usiku)
Porto v Besiktas (Saa 3:45 usiku)
Real Madrid v APOEL (Saa 3:45 usiku)
EUROPA LEAGUE
Alhamis, Septemba 14, 2017
Young Boys v Partizan (Saa 2:00 usiku)
Atalanta v Everton (Saa 2:00 usiku)
Slavia Praha v Maccabi Tel Aviv(Saa 2:00 usiku)
Dynamo Kyiv v Skënderbeu Korçë(Saa 2:00 usiku)0
Hoffenheim v Sporting Braga (Saa 2:00 usiku)
Apollon v Lyon (Saa 2:00 usiku)
ZlÃn v Sheriff (Saa 2:00 usiku)
Rijeka v AEK Athens (Saa 2:00 usiku)
Istanbul Basaksehir v Ludogorets (Saa 2:00 usiku)
København v L'tiv Moskva (Saa 2:00 usiku)
Austria Wien v Milan (Saa 2:00 usiku)
Villarreal v Astana (Saa 2:00 usiku)
Hapoel B.Sheva v Lugano (Saa 4:05 usiku)
Zorya v Östersunds FK (Saa 4:05 usiku)
Real Sociedad v Rosenborg (Saa 4:05 usiku)
Vitesse v Lazio (Saa 4:05 usiku)
Zulte-Waregemv Nice (Saa 4:05 usiku)
Arsenal v Koöln (Saa 4:05 usiku)
Marseille v Konyaspor (Saa 4:05 usiku)
Vitoria Guimarães v Salzburg (Saa 4:05 usiku)
Crvena Zvezda v BATE (Saa 4:05 usiku)
Hertha BSC v At.Bilbao (Saa 4:05 usiku)
Vardar v Zenit (Saa 4:05 usiku)
FCSB v Viktoria Plzen (Saa 4:05 usiku)
Andre Ayew aitibulia Huddersfield akiibeba West Ham
![]() |
| Andre Ayew akiifungia West Ham bao la pili |

![]() |
| Andre Ayew akishangilia bao lake |
![]() |
| Obiang akishangilia bao lake |
WEST Ham United usiku wa kuamkia leo walipata ushindi muhimu nyumbani baada ya kuichapa Huddersfield na kuitibulia rekodi yao ya kupototeza mchezo wowote tangu msimu huu wa Ligi Kuu England kuanza.
Straika Andre Ayew aliyetokea benchi alihusika na mabao yote mawili ya Wagonga Nyundo hao baada ya awali kumtengenezea bao Pedro Obiang katika ya 72 kabla ya mwenyewe kutumbukiza wavuni bao la pili dakika tano baadaye kwenye mchezo mkali uliopigwa Uwanja wa London.
Nyota huyo wa Ghana na mtoto wa Mwanasoka Bora wa zamani Afrika, Abedi Ayew Pele aliingia uwanjani dakika ya 64 kuchukua nafasi ya nyota wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez 'Chicharito' kabla ya kuibeba West iliyotoka kupoteza mechi yao dhidi ya NewCastle United waliowafumua mabao 3-0 ugenini.
Okwi awazidi ujanja Ngoma na Ajibu, Mtibwa yatikisa
![]() |
| Emmanuel Okwi akiwa na mpira wake baada ya kupiga hat trick dhidi ya Ruvu Shooting |
![]() |
| Ibrahim Ajibu katika mazoezi ya Yanga |
![]() |
| Donald Ngoma |
![]() |
| Mtibwa Sugar |
STRAIKA wa Simba, Emmanuel Okwi anayeichezea Simba amewazidi ujanja mastraika wa Yanga, Donald Ngoma na Ibrahim Ajibu, baada ya kusalia kileleni mwa orodha ya wafungaji akiwa na mabao manne, licha ya nyota hao wa Jangwani kushuka dimbani kwa dakika nyingi zaidi ya Mganda huyo.
Okwi ametumia dakika 90 tu kufunga mabao yake akicheza mchezo mmoja tu na kuukosa mchezao mmoja, lakini Ngoma na Ajibu kila mmoja amecheza mechi mbili na kufunga bao moja kila mmojam, jambo lililowapa kiburi mashabiki wa Msimbazi kuwatambia wenzao wa Jangwani.
Mganda huyo aliyewahi kuichezea Yanga misimu mitatu iliyopita, aliukosa mchezo wa timu yake dhidi ya Azam Jumamosi iliyopita ulioisha kwa suluhu, lakini hilo halikumfanya ashindwe kukalia kiti cha uongozi wa wafungaji.
Okwi ambaye jana asubuhi alishindwa kuhudhuria mazoezi ya timu yake yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam ili kujiandaa na mchezo wao ujao dhidi ya Mwadui Jumapili hii, alishindwa kuwahi mechi ya Azam kutokana na kuwa na timu yake ya taifa ya Uganda The Cranes iliyoenda kuvaana na Misri katika mechi ya makundi ya kuwania Fainali za Kombe la Dunia 2018.
Ngoma aliyeifungia Yanga bao la kusawazisha katika mchezo wa kwanza dhidi ya Lipuli na kutolewa katika kipindi cha pili kwenye mchezo dhidi ya Njombe Mji, bado hajarudi kwenye ubora wake tangu atoke kwenye majeraha ya muda mrefu yaliyomfanya ashindwe kuitumikia timu hiyo kwenye mechi za nusu wa msimu uliopita aliomaliza na mabao nane.
Ajibu aliyecheza dakika 180 za mechi mbili za Yanga za msimu huu, naye alifunga bao moja lililokuwa la pekee katika mchezo wao na Njombe Mji na kuzidi kuwapa kiburi Simba kuamini kuwa, licha ya Yanga kuwa na safu kali ya washambuliaji lakini jeshi la mtu mmoja, yaani Okwi ni funika bovu.
Okwi alifunga mabao manne katika mechi ya ufunguzi wa ligi dhidi yas Ruvu Shooting ambapo Simba walishinda mabao 7-0 na timu yake kushindwa kupata matokeo kwenye Uwanja wa Azam Complex dhidi ya Azam.
Mpaka sasa wachezaji 27 wamefanikiwa kufunga jumla ya mabao 32, huku Mohammed Rashid wa Prisons na Marcel Bonventure wa Majimaji wenye mabao mawili kila mmoja wakionekana kumkimbiza Okwi.
Mpaka sasa Ligi ikiwa imeshacheza mechi 16, Ruvu Shooting ndio klabu yenye ukuta mlaini baada ya kuruhusu mabao tisa na yenyewe kufunga bao moja tu, huku Chama la Wana Stand United ikiwa ndiyo timu pekee ambayo haijafanikiwa kufunga bao hata moja, licha ya yenyewe kuruhusu mabao mawili nyavuni mwao.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo nane, Ijumaa Azam itaikaribisha Kagera Sugar kabla ya Simba na Yanga kucheza katika miji ya Dar es Salaam na Ruvuma dhidi ya Mwadui na Majimaji, wakati vinara wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar wenyewe wataendelea kuwa nyumbani kuwakaribisha Mbao FC iliyotoka kujeruhiwa mjini Dodoma na Singida United Jumapili iliyopita.
Msimamo Ligi Kuu Tanzania Bara 2017-2018 ulivyo kwa sasa
P W D L F A PTS
1.Mtibwa 2 2 0 0 2 0 6
2.Simba 2 1 1 0 7 0 4
3.Prisons 2 1 1 0 4 3 4
4.Lipuli 2 1 1 0 2 1 4
5.Yanga 2 1 1 0 2 1 4
6.Azam 2 1 1 0 1 0 4
7.Singida 2 1 0 1 3 3 3
8.Mwadui 2 1 0 1 2 2 3
9.Mbao 2 1 0 1 2 2 3
10.Mbeya 2 1 0 1 1 1 3
11.Ndanda2 1 0 1 1 1 3
12.Majimaji2 0 1 1 2 3 1
13.Kagera2 0 1 1 1 2 1
14.Ruvu 2 0 1 1 1 8 1
15.Njombe2 0 0 2 1 3 0
16.Stand 2 0 0 2 0 2 0
WAFUNGAJI:
4 Emmanuel Okwi (Simba)
2 Marcel Boniventure (Majimaji)
Mohammed Rashid (Prisons)
1 Ibrahim Ajibu (Yanga)
Erasto Nyoni (Simba)
Juma Liuzio (Simba)
Shiza Kichuya (Simba)
Donald Ngoma (Yanga)
Paul Nonga (Mwadui)
Yahaya Mohammed (Azam)
Salim Khamis (Mwadui)
Kenny Ally (Singida United)
Boniface Maganga (Mbao FC)
Hussein Javu (Mtibwa Sugar)
Eliud Ambukile (Mbeya City)
Kassim Khamis (Prisons)
Nurdin Chona (Prisons)
Hassan Kapalata (Njombe Mji)
Seif Karihe (Lipuli)
Jerome Lambele (Lipuli)
Mudathir Yahya (Singida)
Michelle Katsvairo (Singida)
Seleman Kihimbwa (Mtibwa)
Habib Kayombo (Mbao)
Majid Bakar (Ndanda)
Raphael Kyara (Ruvu Shooting)
RATIBA WIKIENDI HII:
Ijumaa Sept 15, 2017
Azam v Kagera Sugar
Jumamosi Sept 16, 2017
Mtibwa Sugar v Mbao FC
Majimaji v Yanga
Prisons v Ndanda
Stand United v Singida United
Lipuli v Ruvu Shooting
Jumapili Sept 17, 2017
Simba v Mwadui
Mbeya City v Njombe Mji
Thursday, April 13, 2017
Sanchez, Lukaku, Zlatan kuonyeshana kazi tuzo za PFA 2017
![]() |
| Lukaku |
NYOTA wa Arsenal, Alexix Sanchez na yule wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, watachuana kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Chama cha Soka cha Wachezaji wa Kulipwa nchini England, (PFA)
Mbali na wakali hao wanaochuana kwa kufumania nyavu katika Ligi Kuu ya England (EPL), pia watakula sahani moja na nyota wengine akiwamo kinara wa mabao wa sasa wa ligi hiyo, Romelu Lukaku wa Everton.
Orodha kamili ya wawania tuzo hiyo ipo hivi;
Mchezaji Bora
Eden Hazard - Chelsea Zlatan Ibrahimovic - Manchester United
Harry Kane - Tottenham Hotspur
N'Golo Kante - Chelsea
Romelu Lukaku - Everton
Alexis Sanchez - Arsenal
Wachezaji Chipukizi
Dele Alli - Tottenham Hotspur
Harry Kane - Tottenham Hotspur
Michael Keane - Burnley
Romelu Lukaku - Everton
Jordan Pickford - Sunderland
Leroy Sane - Manchester City
Mchezaji Bora Wanawake
Lucy Bronze - Manchester City
Karen Carney - Chelsea
Jane Ross - Manchester City
Jill Scott - Manchester City
Caroline Weir - Liverpool
Ellen White - Birmingham City
Mchezaji Bora Chipukizi wa KikeMillie Bright - Chelsea
Jess Carter - Birmingham City
Nikita Parris - Manchester City
Georgia Stanway - Manchester City
Keira Walsh - Manchester City
Caroline Weir - Liverpool
Viongozi DRFA warejea tena DRFA
| Almas Kasongo aliyetetea kiti cha Uenyekiti wa DRFA |
SEHEMU kubwa ya uongozi uliokuwepo kwenye Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), akiwamo Mwenyekiti Almas Kasongo na Katibu Mkuu wake, Msanifu Kondo wamerejea madarakani baada ya kushinda kwenye uchaguzi uliofanyika leo.
Uchaguzi huo uliofanyika Hoteli ya Lamada, Ilala ilishuhudia Kasongo akitetea kiti chake mbele ya Peter Mhinzi na Emmanuel Kazimoto kwa kupata kura 12 dhidi ya 9 za Mhinzi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Temeke (TEFA).
Kondo akitetea kiti cha ukatibu Mkuu akimbwaga Frank Mchaki na Ramadhani Nassib, huku Mhazini aliyeongoza kiti hicho kwa muda mrefu, Ally Hassan akibwaga na Ally Masoud, huku Mtanganzaji na mchambuzi mahiri wa soka nchini, Shafii Dauda akitwaa Ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF.
Wengine waliochaguliwa ni Salum Mwaking'inda aliyeshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti, huku Michale Lupiana akishinda Uwakilishi wa Klabu na Amour Amour na Chichi Mwidege wakitwaa Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya chama hicho.
Yanga wawafuata Waalgeria kwa mafungu
MABINGWA wa Soka nchini, Yanga wameondoka nchini kwa mafungu kundi la kwanza likitimka jioni hii na jingine linatarajiwa kuondoka usiku huu ili kuwahi pambano lao la Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya MC Alger ya Algeria.
Kundi la kwanza lilitimka saa 10 likitumia ndege ya Shirika la Emirates Air likiwa na wakuu wa benchi la ufundi chini ya Kocha George Lwandamina sambamba na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Hassan Kessy, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva, Geoffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi na straika Amissi Tambwe ambao watapitia Dubai.
Mbali na Lwandamina wengine wa benchi la ufundi waliopo kwenye kundi hilo ni Wasaidizi wake, Juma Mwambusi, Kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili, Noel Mwandila kutoka zambia na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Pia kundi hilo lina Meneja Hafidh Ally, Daktari Edward Bavu na Mchua Misuli, Jacob Onyango.
Kundi la pili litafuatia muda mchache ujao litaondoka kwa Ndege ya Shirika la Uturuki likiwa na wachezaji 13 na baadhi ya Maofisa wa timu hiyo likipitia Istanbul ambao ni makipa; Deogratius Munishi ‘Dida’ na Beno Kakolanya; mabeki; Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’ na Kevin Yondan.
Pia wamo viungo ni Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Emmanuel Martin wakati mshambuliaji ni Donald ngoma.
Wawakilishi hao walishinda mchezo wa awali jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwa bao 1-0 hivyo inahitaji sare ama kutofungwa zaidi ya mabao 2-1 ili kutinga makundi na kuwang;oa wenyeji wao MC Alger.
Yanga haijawahi kuitoa timu yoyote ya Afrika Kaskazini wala kupata ushindi ugenini katika nchi hizo, zaidi ya sare mbili ilizopata mwaka 1992 dhidi ya Ismailia ya Misri waliotoka nao 1-1 sawa na ile ya 2008 dhidi ya Al Alkhdar ya Libya.
Kama Yanga itapenya hapo itafuzu makundi ya michuano hiyo na kuweka rekodi kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana ilipenya, ikiwa chini ya Kocha Hans Pluijm ambaye alitimuliwa na kutua Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao.
Kundi la kwanza lilitimka saa 10 likitumia ndege ya Shirika la Emirates Air likiwa na wakuu wa benchi la ufundi chini ya Kocha George Lwandamina sambamba na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Hassan Kessy, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva, Geoffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi na straika Amissi Tambwe ambao watapitia Dubai.
Mbali na Lwandamina wengine wa benchi la ufundi waliopo kwenye kundi hilo ni Wasaidizi wake, Juma Mwambusi, Kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili, Noel Mwandila kutoka zambia na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Pia kundi hilo lina Meneja Hafidh Ally, Daktari Edward Bavu na Mchua Misuli, Jacob Onyango.
Kundi la pili litafuatia muda mchache ujao litaondoka kwa Ndege ya Shirika la Uturuki likiwa na wachezaji 13 na baadhi ya Maofisa wa timu hiyo likipitia Istanbul ambao ni makipa; Deogratius Munishi ‘Dida’ na Beno Kakolanya; mabeki; Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’ na Kevin Yondan.
Pia wamo viungo ni Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Emmanuel Martin wakati mshambuliaji ni Donald ngoma.
Wawakilishi hao walishinda mchezo wa awali jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwa bao 1-0 hivyo inahitaji sare ama kutofungwa zaidi ya mabao 2-1 ili kutinga makundi na kuwang;oa wenyeji wao MC Alger.
Yanga haijawahi kuitoa timu yoyote ya Afrika Kaskazini wala kupata ushindi ugenini katika nchi hizo, zaidi ya sare mbili ilizopata mwaka 1992 dhidi ya Ismailia ya Misri waliotoka nao 1-1 sawa na ile ya 2008 dhidi ya Al Alkhdar ya Libya.
Kama Yanga itapenya hapo itafuzu makundi ya michuano hiyo na kuweka rekodi kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana ilipenya, ikiwa chini ya Kocha Hans Pluijm ambaye alitimuliwa na kutua Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao.
Algeria yamteua Kocha Mkuu Mpya
CHAMA cha Soka cha Algeria, kimemteua Lucas Alcaraz kuwa Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo maarufu kama Mbweha wa Jangwani, ikiwa ni mara ya nne kufanya hivyo katika kipindi cha miezi 13 iliyopita.
Alcaraz raia wa Hispania alitimuliwa Jumatatu iliyopita kama kocha wa Granada kufuatia klabu hiyo kusuasua kwenye La Liga ikiwa mkiani kwenye msimamo. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 anachukua nafasi ya Georges Leekens wa Ubelgiji ambaye alijiuzulu baada ya Algeria kuenguliwa katika hatua ya makundi ya michuano ya Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu.
Mechi ya kwanza ya mashindano kwa Alcaraz itakuwa dhidi ya Togo wakati Algeria watakapoanza kampeni zao za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2019.
Alcaraz raia wa Hispania alitimuliwa Jumatatu iliyopita kama kocha wa Granada kufuatia klabu hiyo kusuasua kwenye La Liga ikiwa mkiani kwenye msimamo. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 anachukua nafasi ya Georges Leekens wa Ubelgiji ambaye alijiuzulu baada ya Algeria kuenguliwa katika hatua ya makundi ya michuano ya Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu.
Mechi ya kwanza ya mashindano kwa Alcaraz itakuwa dhidi ya Togo wakati Algeria watakapoanza kampeni zao za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2019.
Mbeya City ikiibana Lyon, Pazi kama kawa
BAO la kipindi cha pili lililofungwa na Thomas Morris limeisaidia African Lyon kuepuka kipigo mbele ya Wakali wa Green Town, Mbeya City baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye pambano la Ligi Kuu Bara lililochezwa jioni ya leo Alhamisi.
Katika pambano hilo lililopigwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, Mbeya City itabidi ijilaumu kwa kushindwa kuibuka na ushindio baada ya kupoteza mkwaju wa penalti dakika ya 37 kabla ya zahoro Pazi kusahihisha makosa dakika tano baadaye kwa kuifungia timu hiyo bao la kuongoza.
Bao hilo lilikuwa la tano kwa winga huyo teleza ndani ya timu hiyo iliyomrejesha uwanjani baada ya kuwa nje ya karibu misimu miwili kwa tatizo la ITC iliyokuwa imenasa FC Lupopo ya DR Congo.
Uzembe uliofanywa na mabeki wa Mbeya City ulisaidia mkongwe Thomas Morris aliyewahi kutamba na Yanga na Moro United kufunga bao la kusawazisha na kuifanya Lyon kufikisha pointi 31 baada ya mechi 27.
City kwa sare hiyo imeifanya ifikishe pointi 32 sawa na Mwadui ila imebebwa kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, ikishika nafasi ya saba ikiwatoa wachimba madini hao wa Shinyanga ambao wanarudi nafasi ya 8.
Ligi hiyo itaendelea tena wikiendi hii kwa mechi sita ambapo nne zitachezwa Jumamosi ikiwamo ile inayosubiwa kwa hamu kubwa kati ya Toto Africans itakayoikaribisha Simba wanaoongoza msimamo wa ligi kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza na Jumapili zitapigwa mechi mbili tu.
Katika pambano hilo lililopigwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, Mbeya City itabidi ijilaumu kwa kushindwa kuibuka na ushindio baada ya kupoteza mkwaju wa penalti dakika ya 37 kabla ya zahoro Pazi kusahihisha makosa dakika tano baadaye kwa kuifungia timu hiyo bao la kuongoza.
Bao hilo lilikuwa la tano kwa winga huyo teleza ndani ya timu hiyo iliyomrejesha uwanjani baada ya kuwa nje ya karibu misimu miwili kwa tatizo la ITC iliyokuwa imenasa FC Lupopo ya DR Congo.
Uzembe uliofanywa na mabeki wa Mbeya City ulisaidia mkongwe Thomas Morris aliyewahi kutamba na Yanga na Moro United kufunga bao la kusawazisha na kuifanya Lyon kufikisha pointi 31 baada ya mechi 27.
City kwa sare hiyo imeifanya ifikishe pointi 32 sawa na Mwadui ila imebebwa kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, ikishika nafasi ya saba ikiwatoa wachimba madini hao wa Shinyanga ambao wanarudi nafasi ya 8.
Ligi hiyo itaendelea tena wikiendi hii kwa mechi sita ambapo nne zitachezwa Jumamosi ikiwamo ile inayosubiwa kwa hamu kubwa kati ya Toto Africans itakayoikaribisha Simba wanaoongoza msimamo wa ligi kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza na Jumapili zitapigwa mechi mbili tu.
Messi aichanganya Argentina adhabu ya FIFA
WAMEPAGAWA. Kitendo cha nyota wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limewatia wazimu Waargentina kiasi Chama cha Soka nchini humo (AFA) kuamua kujitosa kumtetea.
Rais wa AFA, Claudio Tapia amefunga safari mpaka Hispania ili kujadili kesi inayuomkabili Messi, ambaye ndiye tegemeo na tumaini la nchini hiyo katika mbio zake za kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2018.
Tapia alisisitiza safari ya kwenda nchini Hispania ni mahsusi kwa ajili ya kwenda kujadili kesi ya Lionel Messi ya kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA na sio kwenda kuzungumza na Jorge Sampaoli au Diego Simeone kuhusiana na kibarua cha kuinoa nchi hiyo.
Messi alilimwa adhabu hiyo na FIFA baada ya kumtolea kauli chafu mwamuzi wakati wa ushindi wa bao 1-0 Argentina iliyopata dhidi ya Chile mwezi uliopita na kumfanya kukosa mchezo waliofungwa na Bolivia mabao 2-0 na nyingine tatu zijazo za kufuzu Kombe la Dunia.
Nyota huyo wa Barcelona anayo nafasi ya kukata rufani ya kutaka kupunguzwa kwa adhabu hiyo mwezi ujao kitu ambacho Tapia alitaka kwenda kujadili naye ana kwa ana.
Tapia alisema FIFA imemtaka Messi kupeleka shauri lake hilo la kufungiwa mechi nne baada ya mchezo wao dhidi ya Chile Alhamisi Mei 4 mwaka huu hivyo ilikuwa muhimu kwenda kujadiliana naye kuhusiana na hilo.
Mchezo ujao wa Argentina utakuwa ni ule wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Brazil utakaofanyika nchini Australia Juni mwaka huu huku mechi za kufuzu Kombe la Dunia zikitarajiwa kuendelea Agosti.
Mabao ya Barcelona yampa ulaji Dyabala Juventus
SAA chache baada ya kuitia aibu Barcelona katika mechi ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Straika wa Juventus, Paulo Dybala amesaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Italia ambao utamalizika mwaka 2022.
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 23 ameifungia Juventus mabao 16 msimu huu na kulikuwa na tetesi zikimuhusisha na kuondoka. Dybala alijiunga Juventus kwa kitita cha Pauni 23 milioni kutoka Palermo na kupewa mkataba wa miaka mitano Juni 2015 na kufanikiwa kushinda mataji mawili mwaka jana.
Dybala alisema siku zote amekuwa akitaka kufanikiwa kwenye kila kitu na anafahamu Juventus ndio mahali sahihi kuwepo kama anataka kushinda mataji. Dybala amefunga mabao 39 na kusaidia mengine 16 kwenye mechi 82 toka ajiunge na Juventus, ikiwa ni dadi kubwa zaidi ya mchezaji yeyote katika klabu kwa muda aliojiunga.
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 23 ameifungia Juventus mabao 16 msimu huu na kulikuwa na tetesi zikimuhusisha na kuondoka. Dybala alijiunga Juventus kwa kitita cha Pauni 23 milioni kutoka Palermo na kupewa mkataba wa miaka mitano Juni 2015 na kufanikiwa kushinda mataji mawili mwaka jana.
Dybala alisema siku zote amekuwa akitaka kufanikiwa kwenye kila kitu na anafahamu Juventus ndio mahali sahihi kuwepo kama anataka kushinda mataji. Dybala amefunga mabao 39 na kusaidia mengine 16 kwenye mechi 82 toka ajiunge na Juventus, ikiwa ni dadi kubwa zaidi ya mchezaji yeyote katika klabu kwa muda aliojiunga.
Sunday, January 15, 2017
Manchester City aibu tupu, wapigwa 4-0
![]() |
![]() |
| Picha zote kwa hisani ya Mirror |
City inayonolewa na Kocha Pep Guardioala kwa kipigo hicho imesalia nafasi ya tano ya msimamo na ikiwa katika hati hati ya kuzidiwa maarifa na watani zao wa Jiji la Manchester, Man United iwapo itafanikiwa kuifunga Liverpool kwa idadi kubwa ya mabao, kwani zinaweza kulingana na kuzidiana uwiano wa mabao.
United ina pointi 39 na mabao 31 ya kufunga na kufungwa 19 wakati City kwa kipigo cha jioni hii imesaliwa na pointi 42 na mabao 41 ya kufunga na kufungwa 26, ikiwa na maana wana uwiano tofauti na mabao matatu tu mpaka sasa.
Mabao yaliyoiangamiza City leo ikiwa kiigo chao cha tano msimu huu yalitumbukizwa na Romelu Lukaku dakika ya 34, Kevin Mirallas dakika 47', Tom Davies dakia ya 79 na chipukizi Ademola Lookman aliyefunga dakika za nyingeza za mpambano huo mkali ambao umemfanya Guardiola kujikuta kwenye simanzi kubwa.
Muda mchache ujao Man United itakuwa wenyeji wa Liverpool kwenye Uwanja wa Old Trafford, kwenye mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutofungana. Mechi ilichezwa Oktoba 17, 2016.
Mbao, Lyon zashindwa kutambiana kesho zamu ya Toto v Prisons
| Mbao FC |
![]() |
| Lyon |
KLABU za Mbao FC na wageni wao African Lyon zimeshindwa kutambia kwenye mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Bara baada ya kutoka suluhu.
Timu hizo zimeshindwa kufunga kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kuzifanya zigawane pointi moja moja.
Kwa matokeo hayo zimezifanya timu hizo kuendelea kusalia katika nafasi zao walizokuwa kabla ya mchezo huo uliomalizika hivi punde.
Lyon imefikisha pointi 21 na Mbao imekusanya alama 20, lakini zimeshindwa kusogea katika maeneo waliyokuwapo.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumatatu kwa mchezo mmoja kati ya Toto African na Prisons jijini Mwanza na Jumanne Yanga itakuwa wageni wa Majimaji Songea na Jumatano Simba na Azam zitashuka viwanja tofauti vya mjini Morogoro na Dar es Salaam.
Simba itakuwa mgeni wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakati usiku wa saa 1 jioni, Azam itakuwa wenyeji wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Simba ndio vinara wa Ligi Kuu mpaka sasa ikiwa na pointi 44 baada ya kushuka uwanjani mara 18, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 40 na Kagera Sugar kushika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 ikiiengua Azam iliyoshuka nafasi ya nne na pointi zao 30.
Msimamo wa Ligi Kuu Bara
P W D L F A Pts
1. Simba 18 14 2 2 30 6 44
2. Yanga 18 12 4 2 39 9 40
3. Kagera Sugar 19 9 4 6 21 18 31
4. Azam 18 8 6 4 23 15 30
5. Mtibwa Sugar 18 8 6 4 22 19 30
6. Stand Utd 19 6 7 6 18 16 25
7. Mbeya City 18 6 6 6 16 16 24
8. Ruvu 19 5 9 5 18 20 24
9. Prisons 18 5 7 6 10 13 22
10.Mwadui 19 6 4 9 16 24 22
11.African Lyon 19 4 9 6 11 16 21
12.Mbao 19 5 5 9 17 24 20
13.Ndanda 19 5 4 10 15 26 19
14.Majimaji 18 5 2 11 13 26 17
15.Toto Africans 18 4 4 10 11 20 16
16.JKT Ruvu 19 3 9 7 7 17 15
Wafungaji:
9- Shiza Kichuya (Simba)
Simon Msuva (Yanga)
Amissi Tambwe (Yanga)
8- Abdulrahman Mussa (Ruvu Shooting)
Mbaraka Yusuf (Kagera Sugar)
7- Rashid Mandawa (Mtibwa Sugar)
Donald Ngoma (Yanga)
John Bocco (Azam)
6- Mzamiru Yasin (Simba)
Haruna Chanongo (Mtibwa Sugar)
5- Omar Mponda (Ndanda)
Obrey Chirwa (Yanga)
Riffat Khamis (Ndanda)
Victor Hangaya (Prisons)
Rafael Daud (Mbeya City)
Venance Joseph (African Lyon)
4-Peter Mapunda (Majimaji)
Kelvin Sabato (Stand United)
Laudit Mavugo (Simba)
Marcel Boniventure (Majimaji)
Boniface Maganga (Mbao)
Deus Kaseke (Yanga)
Shaaban Kisiga (Ruvu Shooting)
Mohammed Ibrahim 'MO' (Simba)
Tito Okello (Mbeya City)
3- Hood Mayanja (African Lyon)
Ibrahim Ajib (Simba)
Abdalla Mfuko (Mwadui)
Subianka Lambert (Prisons)
Ditram Nchimbi (Mbeya City)
Wazir Junior (Toto African)
Issa Kanduru (Ruvu Shooting)
Ally Nassor 'Ufudu' (Kagera Sugar)
Kelvin Friday (Mtibwa Sugar)
Mfanyeje (Majimaji)
Francisco Zukumbawira (Azam)
Shaaban Idd (Azam)
Jamal Mnyate (Simba)
Jamal Soud (Toto Africans)
Adeyum Saleh (Stand United)
Jacob Massawe (Stand United)
2- Adam Kingwande (Stand United)
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)
Vincent Philipo (Mbao)
Mcha Khamis (Azam)
Danny Mrwanda (Kagera Sugar)
Pastory Athanas (Stand United)
Paul Nonga (Mwadui)
Fully Maganga (Ruvu Shooting)
Themi Felix (Kagera Sugar)
Mudathir Yahya (Azam)
Atupele Green (JKT Ruvu)
Jerry Tegete (Mwadui)
Jamal Mwambeleko (Mbao)
Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar)
Adam Salamba (Stand United)
Jaffar Salum (Mtibwa Sugar)
Subscribe to:
Posts (Atom)






























