STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Liverpool wapewa Swansea, Man City v Newcastle Capital One


Suso wa Liverpool akishangilia bao lililosaidia kuivusha timu yao katika michuano ya Kombe la Ligi (Capital One)


Frank Lampard akishangilia goli lake la tatu katika mechi mbili dhidi ya Sheffield jana

SHREWSBURY Town, timu pekee ya daraja la chini zaidi iliyosalia katika michuano ya kombe la ligi 'Capital One Cup' amepangwa kukutana na timu ngumu ya ligi kuu ya England, Chelsea kwenye mechi ya raundi ya nne.
Raundi iliyopita Shrews inayocheza daraja la pili iliwaondoa mabingwa wa Championship, Norwich na sasa itawakaribisha Chelsea walioshinda 2-1 dhidi ya Bolton jana usiku.
Mabingwa watetezi, Manchester City, walioitoa Sheffield jana kwa kuifunga mabao 7-0 katika dimba la Etihad watachuana na Newcastle inayocheza ligi kuu.
Liverpool waliosonga mbele kwa penati 14-13 dhidi ya Middlesbrough jumanne usiku, watachuana na Swansea City, zote zinacheza ligi kuu.
Stoke wataikaribisha Southampton , wakati Tottenham watakuwa nyumbani dhidi ya Brighton.
Mechi nyingine za raundi ya nne zitawakutanisha Sheffield United watakaosafiri kuifuata MK Dons na Fulham watakabiliana na Derby.


Ratiba kamili hii hapa:
Tottenham Hotspur vs Brighton
Stoke City vs Southampton
Bournemouth vs West Brom
Shrewsbury vs Chelsea
Liverpool vs Swansea City
MK Dons vs Sheffield United
Manchester City vs Newcastle United

No comments:

Post a Comment