STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

TCAA yatumia Mil. 200 kuboresha ya Mawasiliano Mnyusi Tanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgp92-UaJEj1Q0BjT_TDJlnGpzbAF6zP5KT-cZH_G44BNiUmbX0m6g_APf_eQrmnpcrKGydWuifPpvWnpx42jPfxzImYnUADbpageNtG_fXTkJGadqNeUsvun0rVvuBDXPKuHc4fzxRf0/s1600/1.jpgNa Kipimo Abdallah
ZAIDI ya shilingi milioni 200 zimetumika katika maboresho ya kituo cha mawasiliano cha Mnyusi mkoani Tanga kinachotumika kupokea na kutuma mawasiliano ya radio zinazo tumika katika usafiri wa anga.
Hayo yamebainishwa na Afisa habari wa TCAA  Bestina Magutu wakati akizungumza na mwandishi wahabari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema maboresho hayo yametokana na ukweli kuwa kituo hicho kilikuwa hakifanyi kazi kwa muda mrefu hali ambayo ilikuwa inaasababisha kukosekana kwa mawasiliano katika ukanda wa mashariki kutoka usawa wa bahari.
Kabla ya kukamilika kwa maboresho haya baadhi ya maeneo mchini yalikuwa hayapati mawasiliano ya kitekonologia kutoka nchini na badala yake walikuwa wanapata huduma hiyo kutoka nchi jirani,"alisema.
"Mradi huo umekamilika na kukabithiwa kwenye mamlaka ya usafiri wa anga mwezi agost mwaka huu na kukabithiwa kwenye kituo cha Mnyusi jijini Tanga,umegharimu shilingi za kitanzania milioni 292,887,921," alisma.
Magutu aliongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo kumeongeza ufanisi wa usafirishaji wa anga kwa kurahisisha huduma ya kuongoza ndege,utaongeza mapato kwa mamlaka hiyo.
"Nimategemeo yangu kwamba kupitia maboresho haya mamlaka itajiongezea mapato kupitia tozo ya huduma ya uongozaji ndege,
Kwa upande wake Mkaguzi Mwandamizi,Redemptus Rugombe alisema mamlaka inandelea kupanua miondombinu ya kuongeza ndege sanjari na mabadiliko ya teknolojia ili kumudu ukuaji wa sekta ya usafirirshaji wa anga.
"Takwimu za mwaka 2031 zinaonyesha ongezeko la miruko ya ndege (flight movement) imeongezeka hadi kufikia miruko 230,458 sawa na ongezeko la asilimia3.6 kotoka miruko 222,430 mwaka 2012,
Kadharika katika kipindi hicho idadi ya abilia imeongezeka kutoka 4,056,925 hadi kufikia 4,626,016 sawa na ongezekola asilimia 14,kwa sasa idadi ya abilia inatarajiwa kuongezeka zaidi kufikia mwishoni mwa mwaka huu," alifafanua.
Mkaguzi Mwandamizi huyo aliongeza kuwa katika kuhakikisha watanzania wanapata uelewa wa elimu ya mamlaka ya anga mamlaka inaendelea kuwapatia wanafunzi mafunzo kwa njia ya udhamini na hadi sasa kuna wamnafunzi watano wanaendelea ma mafunzo ya urubani.
"Kwa tarifa za wanafunzi wetu ambao wako Afrika ya kusini kwa masomo ya urubani chini ya udhamini wa mamlaka wanaendelea vizuri,huu mpango kwa mamlaka ni endelevu ili kusaidia kuwawezesha watanzania kpambana katika soko la ajira, "alisema.

No comments:

Post a Comment