STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Nahodha Coastal Union awaponda akina Jaja

NAHODHA wa timu ya Coastal Union, Mbwana Kibacha amewaponda washambuliaji wa kulipwa wa klabu za Simba na Yanga akiwamo Genilson Santana 'Jaja' akidai hawa lolote zaidi ya kubebwa na vyombo vya habari.
Kibacha alisema viwango vya Jaja na wengine wanaoichezea Yanga na wale wa Simba ni wa kawaida mno tofauti na waliopo Azam aliowafagilia akidai ni moto wa kuotea mbali.
Akizungumza katika mahojiano maalum na MICHARAZO, Kibacha aliyepewa mikoba ya unahodha baada ya kuwa msaidizi wa Juma Nyosso msimu uliopita ambaye kwa hayupo kikosini humo..
"Mapro wa Simba na Yanga ni wa kawaida sana, hawana viwango vya kutisha ila wanafagiliwa na kupambwa sana na magazeti kiasi cha kuwafanya waonekane kama akina Cristiano Ronaldo au Angel di Maria.
Beki huyo alikiri kuwa, wachezaji wanaostahili kuendelea kuwepo nchini kwa viwango vyoa vya soka ni wale waliopo Azam na pengine wenzake anaocheza nao Coastal Union.
"Mapro wa Azam ni wa ukweli, lakini waliopo Simba na Yanga wanapambwa tu kwenye magazeti, hawana lolote, wanazidiwa hata na wakali wetu wa Coastal Union," alisema Kibacha.

No comments:

Post a Comment