STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Hapatoshi England, Liver vs Eveton, Arsenal v Spurs

http://tvnewsroom.org/wp-content/uploads/2013/09/Sky-Sports-1-NAR-Live-Ford-Super-Sunday-09-01-15-41-28-600x339.jpg




http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2008/01_03/arsenalspursccG_468x306.jpg
Nani atakayecheka kati ya Arsenal na Spurs
http://www.theevertonforum.co.uk/wp-content/uploads/2013/05/lolza.jpg
http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Clubs/Club_Home/2010/2/7/1265568899742/Tempers-flare-between-Liv-001.jpg
Presha ya pambano la mji wa Merseyside huwa hivi. Leo itaakuwaje? Tusubiri tuone
 KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea kutimka leo kwa kushuhudiwa mechi za watani wa jadi wa miji ya London Kaskazini na Merseyside wakati Arsenal itakapoumana na Tottenham Hotspur na Liverpool kuwakaribisha Everton uwanja wa Anfield.
Klabu hizo zote nne yenye upinzani wa jadi katika miji yao, zitashuka dimbani zikiwa hazina mwenendo mzuri kulinganisha na msimu uliopita na kuwafanya mashabiki wao kuwa roho juu kujua wataibuka vipi.
Mbali na mechi hiyo, pia kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo timu nyingine 12 wakiwamo Manchester United na Chelsea watakuwa dimbani kusaka pointi tatu muhimu.
Mashetani WEkundu wanaouguza kipigo cha mabao 5-3 toka kwa Leicester City itakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford kuwakaribisha West Ham United na Chelsea watakuwa darajani kuivaa Aston Villa.
Ratiba kamili ya ligi hiyo kwa leo ni kama ifuatavyo;
Liverpool    v Everton   
Chelsea        v Aston Villa       
Crystal Palace       v Leicester
Hull City    v Manchester City
Manchester United    v West Ham 
Southampton    v QPR
Sunderland    v Swansea City
Arsenal        v Tottenham

No comments:

Post a Comment