STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Jackson Chove apigwa 'stop' VPL, kisa....!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhygAN_AuPouzgtENYfVB6K9r_XT4puGs9mNJfCn6tOCsHGCVRWrpBA-fODZAj9nLzU1DQRHdz56xrsadm5UVEe7NZs7nqK16sVVLf7g2SXrk7nryIBpvpkO0zc541qNmiTEWXe83XFzXY/s640/Chove.jpg
Chove (Kulia) wakati akiichezea Coastal Union. TFF imemzuia kucheza mpaka ithibitishwe usalama wa afya yake
SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limetangaza kumpiga 'stop' kipa wa JKT Ruvu, Jackson Chove 'Mandanda' kushuka dimbani kwa usalama wake.
Mandanda aliumia na kuzimia kwa zaidi ya dakika 10 katika mechi ya kwanza kati ya JKT Ruvu ilipokuwa ikiivaa Mbeya City mjini Mbeya.
Katika mechi hiyo ya ufunguzi wa Ligi Kuu Bara, timu hizo zilimaliza kwa sare ya bila kufunga.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesema hadi Chove atakapowasilisha vipimo vyake kwa shirikisho hilo nalo kuviwasilisha kwa wataalamu ili kujiridhisha kama yuko sawa.
“Kitendo cha mtu kuzimia kwa dakika 15 si kidogo, tungependa kuhijirisha.
“Lakini tunawashauri wenzetu wa klabu kuhakikisha wanalizingatia suala la kuwapima wachezaji wao kwa kuwa mchezo wa soka si kitu lahisi,” alisema Malinzi.
Timu nyingi za Ligi Kuu Bara na hata ligi nyingine, zimekuwa hazifanyi vipimo vya uhakika kwa wachezaji wake kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment