STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Kocha Liverpool akiri Balotelli bado sana, japo amemsifu Anfield

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhz4XqJAAKnprDJap4_tn1QZtE-90nE7JVa1KXPPSo34ulgKddta1D1UPbRVLDhilRX1FxRY0gMqnVBAMwH97o56EtYPXHAVmH_AE1iGygVEZivYIp7SRNaIE-ui9fyJ4BEMaiUxyiG8m5u/s1600/baloooooooooo.jpgMENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amekiri kuwa Mario Balotelli bado hajafikia hadhi ya kiwango cha dunia lakini amemuunga mkono kuwa anaweza kuvaa viatu vya Luis Suarez na kufanya vitu vikubwa Anfield. 
Suarez aliuzwa Barcelona kwa kitita cha euro milioni 88 katika usajili wa kiangazi huku nafasi yake ikizibwa na Balotelli aliyesajiliwa akitokea AC Milan kwa kitita cha euro milioni 20. 
Rodgers anaamini kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Italia anapswa kufuata nyayo za Suarez akiwa hapo na kuonyesha thamani yake akiwa kama mshambuliaji. 
Rodegrs amesema pamoja na kwamba Balotelli hajafikia hadhi ya kiwango cha dunia lakini hana shaka na kipaji chake kwani ana uwezo wa kufikia huko kama akitilia maanani kazi yake hiyo.

No comments:

Post a Comment