STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Pascal Ndomba ampania Francis Cheka Morogoro

http://www.thisday.co.tz/media/picture/large/Boxing.jpg
Pascal Ndomba
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjw8LmdtQarvRbtu2no4R1hcuEdxu1zGNK2lAmGpagaOyI3Bem_cLLA8XVo2JKPzaMdMNNrg2OsGmQMtC2kmvwmYr1HmUYcu_syCvVzxmyX3BqGqcSwGzWebz-wvcCmNPi2kU9q7-oNcQ5y/s1600/Bondia-Francis-Cheka.jpg
Francis Cheka
 BONDIA Pascal Ndomba anayetarajiwa kupanda ulingoni Novemba Mosi kupigana na aliyekuwa Bingwa wa Dunia wa WBF, Francis Cheka wiki ijayo anatarajiwa kuingia kambini kujiwinda na pambano lisilo la ubingwa.
Aidha bondia huyo ametamba kumsambaratisha Cheka ili kuvunja mwiko wa kutopigwa na bondia yeyote katika ardhi ya Tanzania tangu mwaka 2008.
Mabondia hao watapambana kwenye uwanja wa Sabasaba mjini Morogoro katika uzito wa Light Heavy raundi 8.
Akizungumza na MICHARAZO, Ndomba alisema ataingia kambini wiki ijayo kujiandaa na pambano hilo akiwa na nia moja tu ya kumtandika Cheka na kuziba ubabe kwa mabondia wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment