STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Simba, Yanga sasa kutifuana Oktoba 18

PAMBANO la watani wa jadi wa soka nchini, Simba na Yanga ambalo lilikuwa lichezwe Oktoba 12, sasa litafanyika Oktoba 18 baada ya mabadiliko ya ratiba.
Mabadiliko hayo yamekuja kutokana na kuwepo kwa pambano la kirafiki la kimataifa linalotambulishwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA kati ya Taifa Stars dhidi ya Benin litakalochezwa Oktoba 12 jijini Dar.
Kwa mujibu wa marekebisho madogo yaliyofanywa na Shirikisho la Soka nchini, TFF, ni kwamba mechi zote zilizokuwa zichezwe Oktoba 12 na 13 sasa zitachezwa Oktoba 18 na 19 sambamba na pambano la watani wa Jadi.

No comments:

Post a Comment