STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 19, 2012

 DEREVA wa treni ya mizingo ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) Ali Kilumanga (57), amefariki dunia huku askari 10 wa jeshi la Polisi nchini wakinusurika kifo kwenye ajali ya treni

Na AFISA HABARI WA TAZARA
DEREVA wa treni ya mizingo ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) Ali Kilumanga (57), amefariki dunia huku  askari 10 wa jeshi la Polisi nchini wakinusurika kifo  kwenye ajali ya treni  iliyotokea karibu na stesheni ya Makambako mkoani Iringa.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TAZARA, Akashambatwa Mbikusita-Lewanika aliwaambia waandIshi wa habari  jijini Dar es Salaam jana kuwa ajali hiyo ilitokea juzi saa 11:40 jioni na kuhusisha Treni No 0755 ya shirika hilo, iliyokuwa ikiokea Dar es salaam kwenda Kapilimposhi  Zambia.
Alitaja chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu iliyojitokeza kwenye mfumo wa breki na hivyo kushindwa kufunga breki na baadae kuacha njia na kisha kupunduka, ambapo  dereva wa akiba wa treni hiyo, Mashaka Bujilima alilipata majeraha na kupelekwa Hospitali ya Ilembula iliyopo wilayani Njombe na baadae kuruhusiwa baada ya kupata matibabu.
" Tumepokea kifo cha mpedwa wetu  Kalumanga kwa masikitiko na hazuni kubwa kwa kuwa amekuwa nasi kwa muda mrefu,lakinisasa kametutoka jina la bwana lihimidiwe,’’ alisema Akashambatwa.
Alisema Treni hiyo ilikuwa imebeba shehena ya mizigo mbalimbali ikiwa ni pamoja na injini za teni mbili, magari 16 ya mbolea, magari tisa ya mafuta ya treni na mengine ni magari ya vifaa mbalimbali,ambapo tathimini ya hasara ya mali, inaendelea  kufanyiwa uchunguzi.

"Timu ya wataalamu mbalimbali  na waandamizi, mara moja imenzisha uchunguzi kwa kina sababu ya ajali hii ya  kutisha , lakini ripoti ya awali imewasilishwa kwa serikali  mbili za Tanzania na Zambia," alisema Akashambatwa.

Aidha Akashambatwa, alisema kuwa kwa  huzuni kubwa wametuma  rambirambi zao kwa familia  ya marehemu na  kuwapa  pole kwa niaba ya familia nzima ya TAZARA.
Mwisho

PICHA INAONYESHA JINSI YA MABEHEWA YALIVYOSAMBARATIKA

MABOGI YA BEHWA

BAADHI YA MIZIGO ILIYOSAMBARATIKA

Jengo la shule ya sekondari ya kata ya kiwalani liko katika hali mbaya

Jengo la shule ya sekondari ya kata ya kiwalani liko katika hali mbaya jengo hilo ambalo lina muda wa miaka ipatayo minane toka lijengwe halijaingiwa wanafunzi picha inapnyesha jinsi lilivyo milango imeibiwa silbodi imebomoka kama picha inavyonyesha hivi sasa ndio geto wanafunzi wanaonekana ni wa shule za msingi zilizopo karibu na jengo hilo wakati wanafunzi wanafanya mitihani ya darasa la saba  jee watapelekwa wapi kaama hali ni hii wanafunzi wa darasa la saba shule zilizopo katika kata hiyo ya kiwalani awanafanya mtihani jee wale ambao watakao faulu watakwenda katika shule gani  wanafuzi wanaofaulu katika shule za msingi za kiwalani hupelekwa katika shule za sekondari sehemu za chanika ,mbondole pugu ,kibada shule wananchi wa eneo hilo wanaiomba serikali kufanya kila jitihada wamalize miaka minane toka ijengwe ni mingi.

Mawaziri watatu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, wanatarajiwa kutumika kama mashahidi katika kesi ya kupinga matokeo

Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar.
Mawaziri watatu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, wanatarajiwa kutumika kama mashahidi katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mdogo wa Bububu, itakayofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa Chama hicho Issa Khamis Issa, katika Mahakama kuu ya Zanzibar.
Mawaziri hao watakaotoa ushahidi katika kesi hiyo, ni Waziri wa Katiba na Sheria, Abubakar Khamis Bakari, Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui na Waziri wa Afya, Juma Duni Haji, ambao walikuwa waangalizi wa uchaguzi kupitia Chama cha Wananchi CUF.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar, Mkurugenzi wa habari, uenezi, haki za binadamu na mawasiliano na umma wa CUF, Salim Bimani alisema kwamba Mawaziri hao walishuhudia vitendo vya ukiukwaji wa taratibu na sheria za uchaguzi.
Bimani alisema hivi sasa jopo la wanasheria wanaendelea kukusanya vielelezo muhimu, kabla ya kufungua kesi wiki hii katika mahakama Kuu ya Zanzibar, na kuiomba kutengua ushindi wa mgombea wa CCM, Hussein Ibrahim Makungu, kwa madai kuwa ushindi wake haukutokana na maamuzi ya wananchi wa jimbo la Bububu.
"Katika kesi tutakayofungua, tutawatumia Mawaziri watatu kama mashahidi, kwa vile wameshuhudia kwa macho yao, vitendo vya udanganyifu, kuruhusiwa watu wasiohusika kupiga kura, na askari wa vikosi vya SMZ kutumia nguvu na kuwatisha wananchi katika zoezi hilo la uchaguzi mdogo wa Bububu.
Aidha, Bimani aliongeza kuwa kuna watu wawili wamejeruhiwa akiwemo Abdallah Haji Mmanga, anayedaiwa kupigwa risasi katika sehemu ya paja la mguu wake wa kulia, na Shah Haji Shah ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa na vigae vya chupa, ambao walitibiwa katika hospitali ya Al Rahma.
"Safari hii tumeamua kupambana kuanzia Mahakama kuu, na kama haki haitotendeka, tutafika katika Mahakam ya Rufaa, hatuwezi kuachia misingi ya demokrasia na utawala bora ikiendelea kuvunjwa chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa" alisema Bimani.
Alisema kwamba katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, kuna viongozi bado wana dukuduku la maridhiano yaliyozaa Serikali hiyo, lakini kinyongo chao hakitofanikiwa kuzorotesha Serikali ya Umoja wa Kitaifa au kuisambaratisha.
"Kuna viongozi katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, hawaungi mkono maridhiano, lakini Wazanzibari hatutaki kurejea katika malumbano ya kisiasa, hatua iliyofikiwa imeleta amani na utulivu katika nchi" alisema bimani
Hata hivyo, alisema kwamba uchaguzi wa Bububu hautopelekea Serikali ya Umoja wa Kitaifa kuvunjika, kwa vile imekuja kutokana na maamuzi ya wananchi, ambao asilimia 66 waliunga mkono kuanzishwa kwa mfumo huo kupitia kura ya maoni iliypigwa 2010.
Alisema kwamba uchaguzi wa Bububu, Jeshi la Polisi lilishindwa kusimamia vyema majukumu yake na badala yake lilikasimu madaraka kwa vikosi vya SMZ ambavyo vilitumia vibaya majukumu yao na kushiriki katika vitendo vya kuwatisha wananchi kuweza kujitokeza na kupiga kura katika uchaguzi huo.
Bimani alisema CUF inalaani kitendo cha kupigwa kwa Mwandishi wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Munir Zakaria, kwa vile kimeingilia uhuru wake wa kikatiba wa kutekeleza majukumu yake ya kukusanya taarifa kwa ajili ya kuwahabarisha wananchi.
Alisema bahati mbaya tukio hilo limetokea siku chache tangu kuuwawa kwa Mwandishi wa Channel Ten mkoani Iringa, marehemu Daudi Mwangosi, ambapo hakuna kiongozi dhamana wa Jeshi la polisi aliyewajibika kutokana na mauaji hayo ya kikatili.
Aidha aliongeza kuwa CUF imesikitishwa na kitendo cha kupewa masharti magumu ya dhamana kwa watuhumiwa wanaodaiwa kuhusika na vurugu za uchaguzi huo, ambapo kila mmoja alitakiwa kuweka dhamana ya shilingi laki tano kama fedha taslimu na dhamana ya maandishi 500,000 kwa kila mmoja kwa watuhumiwa 10 waliofikishwa katika mahakama ya mwanzo ya Mwanakwerekwe.
Akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa jimbo la Mtoni ambaye ni mmoja kati ya watu waliopigwa katika vurugu hizo, Faki Haji Makame, alisema kwamba alipigwa mtama na kuanguka chini, wakati akiokota kiatu baada ya kumvuka alipokuwa akiwakimbia vijana waliomvamia na kumjeruhi.
"Mimi sijapigana hadharani, nimevamiwa na vijana wawili baadae akatokea mwengine, mnamhoji wa nini, wakati tumeagizwa apigwe, ndipo nilipoamua kukimbia na wakaanza kunifukuza na kunipiga" alisema Mbunge huyo wa jimbo la Mtoni.
Akielezea mukhtasari wa tukio lake, alisema kabla ya kushambuliwa wakati akitokea eneo la Kijichi, kukagua ujenzi wa nyumba yake, alipofika karibu na tawi la CCM eneo la Bububu, alimuona Naibu Katibu Mkuu wa CCm Zanzibar, Vuai Ali Vuai na kuamua kwenda kumsalimia, lakini alikataa kupokea salamu yake na kumshutumu kuwa CUF inazuia wafuasi wa CCM kwenda kupiga kura katika vituo.
"Alitahadharisha kuwa CCM haitokubali watu wake kunyimwa haki ya kupiga kura, na baada ya maneno yake, mimi nilianza safari ya kwenda kuwasalimia wakwe zangu katika eneo la Bububu, ndipo nilipokutwa na maswahiba ya kupigwa na kujeruhiwa kwa mwili wangu, kwa kunipiga kwa mipira ya mabomba ya maji na mateke na ngumi" alisema Mbunge huyo.
Alisema anakanusha taarifa ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa kuwa alikamatwa kwa madai ya kupigana hadharani, wakati Polisi ndio waliomuokoa alipokuwa akipigwa na kupelekwa katika kituo cha Bububu pamoja na watu waliokuwa wakimpiga.
Hata hivyo alisema jambo la kushangaza Polisi mpaka jana wameshindwa kumpa majina ya watu waliompiga, licha ya kuwa wamehojiwa, na vile vile wameshindwa kuwafikisha Mahakamani kutokana na makosa ya kumpiga na kumshambulia mwilini.
Kwa upande wake, aliyekuwa mgombea wa CUF, Issa Khamis Issa, alisema kwamba ameshindwa kufungua kesi yake jana kama ilivyopangwa awali, kwa vile wanasheria wake wanaendelea kukamilisha vielelezo vitalkavyotumika kama ushahidi katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo hilo.
Alisema sheria ya tume ya uchaguzi inaeleza kuwa ndani ya siku 14, mgombea yeyote ana haki ya kupinga matokeo mahakamani endapo atakuwa hajaridhika na anatarajia kufungua kesi hiyo mapema wiki hii.
Wakati huo huo Mwandishi wa Channel Ten, Munir Zakaria ambaye alipigwa katika vurugu hizo za uchaguzi, ameendelea kupata matibabu, na afya yake inaendelea vizuri, baada ya kupigwa ngumi sehemu ya mdomoni na mabegani, lakini pochi iliyopotea ikiwa na vitu muhimu bado haijapatikana.
Alisema kwamba, tayari amekamilisha taratibu za matibabu katika hospitali ya Mnazi Mmoja, na anaamini watu waliomfanyia shambulia hilo watachukuliwa hatua za kisheria kwa vile tukio hilo limeripotiwa katika kituo cha Polisi cha Mwembe Madema mjini Zanzibar.
uchaguzi mdogo wa jimbo la Bububu ulifanyika Septemba 16 mwaka huu, ambapo ulitawaliwa na vurugu, uharibifu wa mali za umma, na matumizi mabaya ya silaha, hatua ambayo wadadisi wa mambo wameitafsri kuwa ni mwanzo mbaya wa kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Monday, September 17, 2012

AVB azuga, eti hakuwa na presha yoyote Spurs

Tottenham manager Andre Villas-Boas has insisted he did not feel under any pressure before recording his first Spurs win at Reading.
The Portuguese was the subject of speculation about his future, having not won any of his first three games.
But Villas-Boas dismissed such talk after his team's impressive 3-1 Premier League success at the Madejski Stadium.
"I talk to the chairman Daniel Levy every day. I didn't feel under any pressure at all," he said.
He also refused to react to comments by his predecessor Harry Redknapp,  appearing to criticise modern managers in the mould of Villas-Boas who present players with "70-page dossiers".
Play media
Cannot play media. You do not have the correct version of the flash player. Download the correct version
Reading 'will learn from mistakes'
Villas-Boas said: "It is not about the manager, it is about the players. It is the players that take us to success. Different managers have different leadership styles and the way they go about their business.
"I don't know if Harry was mentioning that about Jose Mourinho but it seems strange. I don't use those situations but in the end the most important thing is for your team and your players to reach a level that is needed for success.
"It doesn't matter if a manager is modern, old-fashioned or old school. The most important thing is you have to feel what is right, feel your convictions. Then you can sell your ideas better and take your players to success."
Villas-Boas admitted there had been anxiety in the Spurs dressing room after a defeat and two draws in their opening three games, but he insisted: "I am extremely happy because the players showed tremendous responsibility, commitment and concentration.
"They have been working so hard and deserve to get this first win. We managed to mix the result and the performance and come out of Reading very satisfied."

Kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanza rasmi kesho

KINYANG'ANYIRO cha Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kinatarajiwa kuanza rasmi hatua ya makundi kesho kwa mechi kadhaa ambapo Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England wataanzia ugenini mjini Madrid, Hispania kuumana na mabingwa wa nchini, Real Madrid katika mechi ya kundi D.
Tayari timu hizo zimeanza kutoleana tambo kuhusiana na mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandandfa duniani kote kutaka kuona kikosi cha Manchester City itavuna nini mbele ya vijana wa Jose Mourinho ambayo timu yao imeanza na 'mwaka wa tabu' katika ligi ya nchini mwao.
Mechi nyingine zinazotarajiwa kuchezwa kesho itazikutanisha timu za Ac Milan inayoyumba ligi ya Seria A kwa kupokea vipigo mfululizo kama Real Madrid kwa kuumana na Anderlecht, mjini MIlan.
Vijana wa Arsene Wenger ambao imetoka kupata ushindi wa kishidno katika ligi ya nchini mwao kwa kuialaza Southampton kwa mabao 6-0, yenyewe nayo itakuwa ugenini kuumana na Montpellier ya Ufaransa.
Mechi nyingine kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo hatua ya makundi ni kama ifuatavyo:

Tuesday, 18 September 2012
AC Milan v Anderlecht, GpC, 19:45
Borussia Dortmund v Ajax, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v FC Porto, GpA, 19:45
Malaga v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Montpellier v Arsenal, GpB, 19:45
Olympiakos v Schalke 04, GpB, 19:45
Paris SG v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Real Madrid v Man City, GpD, 19:45

Wednesday, 19 September 2012
Barcelona v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Bayern Munich v Valencia, GpF, 19:45
Braga v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Celtic v Benfica, GpG, 19:45
Chelsea v Juventus, GpE, 19:45
Lille v BATE Borisov, GpF, 19:45
Man Utd v Galatasaray, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45

Tuesday, 2 October 2012
Spartak Moscow v Celtic, GpG, 17:00
BATE Borisov v Bayern Munich, GpF, 19:45
Benfica v Barcelona, GpG, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Man Utd, GpH, 19:45
FC Nordsjaelland v Chelsea, GpE, 19:45
Galatasaray v Braga, GpH, 19:45
Juventus v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Valencia v Lille, GpF, 19:45

Wednesday, 3 October 2012
Zenit St Petersburg v AC Milan, GpC, 17:00
Ajax v Real Madrid, GpD, 19:45
Anderlecht v Malaga, GpC, 19:45
Arsenal v Olympiakos, GpB, 19:45
Dynamo Kiev v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
FC Porto v Paris SG, GpA, 19:45
Man City v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Schalke 04 v Montpellier, GpB, 19:45

Tuesday, 23 October 2012
Spartak Moscow v Benfica, GpG, 17:00
BATE Borisov v Valencia, GpF, 19:45
Barcelona v Celtic, GpG, 19:45
FC Nordsjaelland v Juventus, GpE, 19:45
Galatasaray v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Lille v Bayern Munich, GpF, 19:45
Man Utd v Braga, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v Chelsea, GpE, 19:45

Wednesday, 24 October 2012
Zenit St Petersburg v Anderlecht, GpC, 17:00
Ajax v Man City, GpD, 19:45
Arsenal v Schalke 04, GpB, 19:45
Borussia Dortmund v Real Madrid, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v Paris SG, GpA, 19:45
FC Porto v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Malaga v AC Milan, GpC, 19:45
Montpellier v Olympiakos, GpB, 19:45

Tuesday, 6 November 2012
AC Milan v Malaga, GpC, 19:45
Anderlecht v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Dynamo Kiev v FC Porto, GpA, 19:45
Man City v Ajax, GpD, 19:45
Olympiakos v Montpellier, GpB, 19:45
Paris SG v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
Real Madrid v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Schalke 04 v Arsenal, GpB, 19:45

Wednesday, 7 November 2012
Bayern Munich v Lille, GpF, 19:45
Benfica v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Braga v Man Utd, GpH, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Galatasaray, GpH, 19:45
Celtic v Barcelona, GpG, 19:45
Chelsea v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Juventus v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45
Valencia v BATE Borisov, GpF, 19:45

Tuesday, 20 November 2012
Spartak Moscow v Barcelona, GpG, 17:00
BATE Borisov v Lille, GpF, 19:45
Benfica v Celtic, GpG, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Braga, GpH, 19:45
FC Nordsjaelland v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Galatasaray v Man Utd, GpH, 19:45
Juventus v Chelsea, GpE, 19:45
Valencia v Bayern Munich, GpF, 19:45

Wednesday, 21 November 2012
Zenit St Petersburg v Malaga, GpC, 17:00
Ajax v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Anderlecht v AC Milan, GpC, 19:45
Arsenal v Montpellier, GpB, 19:45
Dynamo Kiev v Paris SG, GpA, 19:45
FC Porto v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
Man City v Real Madrid, GpD, 19:45
Schalke 04 v Olympiakos, GpB, 19:45

Tuesday, 4 December 2012
AC Milan v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Borussia Dortmund v Man City, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Malaga v Anderlecht, GpC, 19:45
Montpellier v Schalke 04, GpB, 19:45
Olympiakos v Arsenal, GpB, 19:45
Paris SG v FC Porto, GpA, 19:45
Real Madrid v Ajax, GpD, 19:45

Wednesday, 5 December 2012
Barcelona v Benfica, GpG, 19:45
Bayern Munich v BATE Borisov, GpF, 19:45
Braga v Galatasaray, GpH, 19:45
Celtic v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Chelsea v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45
Lille v Valencia, GpF, 19:45
Man Utd v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v Juventus, GpE, 19:45


Orodha ya makundi:
Kundi A: Porto, Dynamo Kiev, Paris St Germain, Dinamo Zagreb
Kundi B: Arsenal, Schalke, Olympiakos, Montpellier
Kundi C: AC Milan, Zenit St Petersburg, Anderlecht, Malaga
Kundi D: Real Madrid, Manchester City, Ajax, Borussia Dortmund
Kundi E: Chelsea, Shakhtar Donetsk, Juventus, FC Nordsjaelland
Kundi F: Bayern Munich, Valencia, Lille, BATE Borisov
Kundi G: Barcelona, Benfica, Spartak Moscow, Celtic
Kundi H: Manchester United, Braga, Galatasaray, CFR Cluj

Cheka kucheza mara ya mwisho na Nyilawila, kisa...!

Francis Cheka (kulia) alipokuwa 'akimsulubu' Karama Nyilawila katika pambano lao lililofanyika mapema mwaka huu na mjini Morogoro na Cheka kuibuka mshindi wa pointi dhidi ya mpinzani wake.

BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Cheka 'SMG' amesema huenda pambano lake dhidi ya Karama Nyilawila 'Captain' ndilo likawa la mwisho kwake kupigana na mabondia wa Tanzania.
Cheka anatarajiwa kuzipigana na Nyilawila katika pambano la kuwania ubingwa wa UBO litakalofanyika Septemba 29 kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya tatu kwa mabondia hao kukutana.
Katika michezo yao ya awali, wawili hao walitoka sare mechi moja na nyingine iliyochezwa mapema mwaka huu, Cheka aliibuka kidedea kwa kumpiga mpinzani wake kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Cheka alisema anaamini pambano hilo alilodai ana hakika ya kuibuka na ushindi mbele ya Nyilawila, huenda likawa la mwisho kwake kuzipiga na mabondia wa Tanzania.
Alisema, awali alishasema asingecheza tena nchini kwa kukosa mpinzani wa kweli kufuatia kuwachakaza karibu mabondia wote wakali akiwemo Rashid Matumla, Mada Maugo, Japhet Kaseba na hata Nyilawila mwenyewe.
"Iwapo nitaendeleza mkong'oto kwa Nyilawila, japo nina hakika kwa hilo kutokana na ubora nilionao na uwezo mkubwa katika ngumi, sitacheza tena na mabondia wa nchini, nitaelekeza nguvu zangu kwa mabondia wa nje ili kujenga zaidi jina," alisema.
Alisema kwa sasa anaendelea vema na maandalizi yake dhidi ya pambano hilo lililoandaliwa na Robert Ekerege na litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi na kutamba ataendelea kuwapa raha mashabiki wake.
"Naendelea vema kujifua chini ya kocha wangu Abdallah Saleh 'Komando', sitawangusha mashabiki wangu kwa namna nitakavyomchapa Nyilawila," alisema.
Pambano hilo la uzani wa Super Middle raundi 12, litaamuliwa na mwamuzi wa kimataifa wa Malawi Jerome Waluza na litasindikizwa na michezo ya utangulizi ambapo Juma Kihiyo dhidi ya Ibrahim Maokola, Seba Temba wa Morogoro dhidi ya Stam Kesi.
Michezo mingine ni kati ya Sadik Momba dhidi ya Amos Mwamakula, huku Anthon Mathias wa Morogoro atacheza na Shaban Kilumbelumbe na Deo Samwel akipambana na Hassan Kidebe.
          
Mwisho

Mbio za Uchaguzi Mkuu SPUTANZA zaanza rasmi


MBIO za kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu wa Chama cha Umoja wa Wacheza Soka Tanzania, SPUTANZA, zimeanza rasmi kwa fomu za uchaguzi huo kuanza kutolewa jijini Dar.
Uchaguzi huo wa SPUTANZA unatarajiwa kufanyika Oktoba 20 na fomu hizo zimeanza kutolewa leo ambapo wanamichezo wanaotaka kugombea nafasi za juu watapaswa kulipia kiasi cha Sh 100,000 na zile za ujumbe kwa sh 50,000.
Katibu Msaidizi wa chama hicho, Abeid Kasabalala aliiambia MICHARAZO nafasi zitazowaniwa kwenye uchaguzi huo ni Uenyekiti, Umakamu Mwenyekiti, Ukatibu Mkuu na Msaidizi wake, Mhazini na Msaidizi wake ambao gharama za fomu ni Sh 100,000.
Kasabalala aliyewahi kutamba zamani na timu za Plisners na Mecco ya Mbeya, alisema nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni Ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na nafasi saba za Kamati ya Utendaji ambazo gharama zake ni sh. 50,000.
"Zoezi la uchukuaji na urudishaji wa fomu za uchaguzi mkuu wa SPUTANZA linaanza rasmi leo (jana) fomu zinapatikana eneo la Magomeni, " alisema.
Kasabalala alisema mwisho wa zoezi hilo la kuchukua na kurudisha fomu ni siku ya Ijumaa kabla ya zoezi la kuyapitia majina, pingamizi na usaili kufanyika takati kwa uchaguzi huo utakaoiwezesha SPUTANZA kupata viongozi wapya.
Katibu huyo alisema wakati zoezi hilo la uchaguzi wa taifa ukianza rasmi, chaguzi za vyama vya mikoa inaendelea kufanyika na kusema mikoa yote imetakiwa iwe imaliza chaguzi zao kabla ya Oktoba 10.
"SPUTANZA Taifa tumewashawaeleza vyama vyote vya mikoa iwe imeshafanya chaguzi zao kabla ya Oktoba 10 ili kuwawezesha viongozi wao kushiriki uchaguzi wa taifa utakaofanyika siku kumi baadae," alisema.

Mwisho

MKURANGA wapata viongozi wapya wa soka

CHAMA cha Soka Wilaya ya Mkuranga, MDFA, kimefanikiwa kupata viongozi wake wapya baada ya chama hicho kufanya uchaguzi wake mkuu jana Jumapili.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Mkoa wa Pwani, COREFA, iliyosimamia uchaguzi huo wa Mkuranga, Masau Bwire, uchaguzi huo wa MDFA ulifanyika wilayani humo juzi Jumapili, ambapo Sudi Baisi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa chama hicho.
Bwire, alisema Baisi alipata jumla ya kura 41 kati ya wajumbe 46 kutoka klabu 19 walioshiriki kinyang'anyiro cha uchaguzi huo ambao baadhi ya nafasi zilikosa wagombea wenye sifa za kuziwania.
Mwenyekiti huyo alisem, aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu ni Issa Kivyele aliyezoa kura 42, huku John Malata alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA na Mwakilishi wa Klabu nafasi hiyo ilitetewa vema na Rashid Selungwi.
Bwire, alisema nafasi nyingine katika uchaguzi huo hazikuwa na wagombea na hivyo chama hicho kitalazimika kuitisha uchaguzi mdogo kwa ajili ya kuziba mapengo hayo.
MDFA kimekuwa chama cha pili kufanya uchaguzi wake mkuu baada ya awali Chama cha soka Kisarawe, KIDAFA kuchaguana wiki mbili zilizopita, huku vyama vingine viwili vya Rufiji na Mafia vyenyewe zikitarajiwa kufanya Septemba 29 sambamba na kile cha Soka la wanawake mkoa wa Pwani, TWFA.
Chama cha soka Bagamoyo chenyewe kitaitisha uchaguzi wake Oktoba 8, siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa COREFA utakaofanyika Oktoba 14 wilayani Mafia.

Mwisho

Kipemba achezwa shere 'trela' la Injinia

Msanii Issa Kipemba
KATIKA hali ya kushangaza kabla filamu yenyewe haijaingizwa sokoni wala kutangazwa itatoka lini, tayari wajanja wachache wameanza kusambaziana 'trela' la filamu ya 'Injinia', kupitia simu za mikononi, huku mwenye filamu hiyo, Issa Kipemba akiwa hana taarifa zozote.
Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kuwaona baadhi ya abiria ndani ya daladala wakirushiana trela la filamu hiyo kupitia simu zao za mikononi na yeye kuomba arushiwe kwa nia ya kuwa na ushahidi wa kutosha kwa kile alichokishuhudia.
Walipododoswa walipoipata 'trela' hilo ambayo filamu yake inahaririwa kwa sasa, abiria hao walidai wamerushiwa na jamaa yao.
MICHARAZO liliwasiliana na Issa Kipemba ambaye ndiye mtunzi na mmoja wa waigizaji wa filamu hiyo kutaka kujua juu ya jambo hilo, alidai hata yeye ameshangazwa na taarifa hizo akidai amekuwa akipokea simu tangu wiki iliyopita juu ya kuonekana kwa trela la filamu hiyo.
Kipemba alisema japo ni kweli alitengeneza 'trela' la filamu hiyo ya Injinia kwa ajili yake mwenyewe na kumpa mmoja wa rafiki yake aliyoiona, cha ajabu limesambaa hata kwa watu ambao hawakuwa na habari juu ya filamu hiyo.
"Kwa kweli wewe ni mtu wa 10 kama sikosei kunipigia simu kuniuliza juu ya jambo hilo, sijajua nani anayesambaza hilo trela, ingawa nililitengeneza kwa ajili yangu binafsi na nikampa mmoja wa watu wangu wa karibu japo sijui kama ndiye aliyesambaza au imevujia wapi," alisema Kipemba.
Mchekeshaji huyo aliyevuma na kundi la Kaole kabla ya kutoweka katika fani miaka nane iliyopita, alisema atachunguza ajue aliyevujisha 'trela' hilo, ili kuweza kumchukulia hatua zinazostahili kwa kuhofia isije 'akaumizwa', hata kabla filamu hiyo haijatoka.
Filamu hiyo ya 'Injinia', iliyoongozwa na Leah Richard 'Lamata' imeshirikisha wakali kama Kipemba, Jacklyne Wolper, Lumole Matovolwa na 'stelingi' Castro Dickson.

Tuesday, September 11, 2012

Omari Matuta: Wanchope wa Mtibwa aliyeamua kutundika daluga kwa muda

Omar Matuta 'Wanchope'



Omar Matuta 'Wanchope' (kati) akishangilia bao lililoipa Mtibwa Ubingwa wa Kombe la Tusker lililofungwa na Rashid Gumbo (kulia), Kushoto yao ni Uhuru Seleman alipokuwa wakiichezea Mtibwa Sugar

UMAHIRI wake wa kuwasumbua mabeki na kuwatungua makipa hodari uwanjani, ilimfanya Omar Matuta abatizwe jina la 'Wanchope' akifananishwa na nyota wa zamani wa Costa Rica aliyetamba timu za West Ham na Manchester City, Paulo Wanchope.
Kwa wanaomkumbuka Wanchope aliyezichezea pia Derby County na Malaga alikuwa na kipaji kikubwa cha ufungaji kilichomfanya ashikilie nafasi ya pili ya wafungaji bora wa timu yake ya taifa akiifungia mabao 45 katika mechi 73 alizoichezea.
Kama ilivyokuwa kwa Wanchope, ndivyo ilivyokuwa kwa Matuta, ambaye katika timu zote alizozichezea kuanzia zile za Ligi daraja la nne mpaka za Ligi Kuu Tanzania  amekuwa akifungia mabao muhimu na kuwa tegemeo.
Nyota huyo aliyewahi kutamba na timu za Ndanda Republic, Vijana Ilala, AFC Arusha kabla ya kudakwa na Mtibwa Sugar tangu mwaka 2004 anakumbukwa na mashabiki nchini kwa mabao yake mawili yaliyoipa nafasi timu ya vijana 'Serengeti Boys' tiketi ya kucheza Fainali za Vijana Afrika za mwaka 2005.
Matuta alifunga katika ushindi wa 3-1 dhidi ya vijana wa Zimbabwe yaliyoifanya ifuzu kwa jumla ya mabao 4-1 baada ya kwenda kushinda 1-0 Harare kwa bao la Nizar Khalfan, hata hivyo waliondolewa fainali na kufungiwa na CAF kwa udanganyifu.
Bao lake la pili katika mechi hiyo, Matuta analitaja kama bao bora kwake kwa namna alivyolifunga, ingawa mechi isiyofutika kichwani mwake ilikuwa ni dhidi ya Ethiopia mwaka 2005 kwa namna walivyofanyiwa vimbwanga na kufungwa kwa hila.
Matuta, ameamua kupumzika soka msimu huu baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Mtibwa klabu anayoitaja kuwa bora kwake na anayeishabikia.
"Nimeamua kupumzika ili nifanye mambo yangu binafsi, ila  nikiwahi kumaliza huenda  nikarejea tena dimbani kwenye duru la pili la ligi kuu, ingawa sijui itakuwa timu ipi."
Mkali huyo anayefurahia soka kumpa mafanikio kimaisha ikiwamo kujenga nyumba Kigamboni na kumiliki miradi kadhaa ya biashara, anasema hajawahi kuona klabu iliyo makini na inayojali wachezaji wake kama Mtibwa Sugar.
Anasema kama mfumo wa klabu hiyo wa kujali na kuwathamini wachezaji wake ndio unaomfanya aiheshimu Mtibwa iliyomuuguza goti lake kwa miaka miwili kitu alichodai kwa klabu nyingine nchini ni vigumu kufanya jambo hilo hata kama umeisaidia vipi.

OWINO
Matuta asiyekumbuka idadi ya mabao aliyoyafunga kwa kutoweka kumbukumbu,  anasema licha ya umahiri wake dimbani, kwa beki wa kimataifa wa Azam, Mganda Joseph Owino ndiye ananayemnyima raha kwa uwezo wake mkubwa kisoka.
"Ni bonge la beki, anacheza kwa akili na ndiye anayenisumbua dimbani tangu nianze kukutana nae katika mechi za kimataifa na zile za Ligi Kuu Tanzania Bara."
Matuta anayependa kula ugali kwa samaki au nyama choma na kunywa vinywaji laini, anasema uwezo wake uwanjani na mwili na nguvu alizojaliwa huwa hapati shida kwa  mabeki wenye papara na wanaotumia nguvu, tofauti akutanapo na Owino.
Matuta, ambaye hajaoa ila ana mtoto mmoja aitwae Zuma, anayesoma darasa la tatu katika Shule ya msingi Bunge, anasema soka la Tanzania licha ya kusifiwa kukua ukweli  limedumaa kwa muda mrefu kutokana na sababu kadhaa.
Anadai moja ya sababu hizo ni u-Simba na u-Yanga uliowaathiri karibu wadau wote wa soka, kufutwa kwa mfumo wa ligi ya madaraja kama ilivyokuwa zamani na kupewa kisogo kwa michezo ya Yosso.
"Usimba na uyanga na kubadilishwa kwa mfumo wa ligi ya madaraja kama ilivyokuwa zamani ni sababu ya kukwama kwetu sawa na kupuuzwa kwa soka la vijana wenzetu wamekuwa wakilitegemea kupatia mafanikio yao," anasema.
Anasema ni muda wa wadau wa soka kubadilika japo anakiri huenda ikawa ngumu kwa namna ushabiki huo ulivyowathiri watu, pia akiwaomba viongozi wa FA na klabu kuwekeza nguvu kwa vijana sawia na kuwaruhusu kucheza soka nje ya nchi.

MIKWAJU
Matuta, mwenye ndoto za kufika mbali kisoka na kuwa mfanyabiashara mkubwa hapo baadae, anasema wakati akiibukia kwenye soka alipata wakati mgumu kwa baba yake ambaye ni marehemu kwa sasa aliyekuwa hapendi acheze soka badala yake asome.
Anadai baba'ke alilazimika wakati mwingine kumcharaza bakora ili kumzuia kucheza soka na kukazinia masomo, lakini haikusaidia kitu kwani alijikuta akikacha hata masomo ya sekondari ili ajikite kwenye soka.
"Nilikacha masomo ya sekondari pale JItegemee kwa ajili ya soka, wakati mwingine huwa najuta, lakini nafarijika kwa mafanikio niliyonayo," anasema.
Matuta aliyemudu pia nafasi za kiungo, anawashukuru makocha Mussa Stopper, Mzee Panju na Abdallah Kibadeni waliogundua na kukikiendeleza kipaji chake, pia akiwataja wazazi wake na uongozi mzima wa Mtibwa kumsaidia kufika hapo alipo.
Mkali huyo, aliyezaliwa mwaka 1988, akiwa mtoto wa nne kati ya watano wa Mzee Othman Matuta, anadai alivutiwa kisoka na nyota wa zamani wa RTC Kagera, Msabah Salum, licha ya kukiri kukunwa na soka la Ronaldo de Lima na Romario wa Brazil.
Matuta alianza safari yake kisoka tangu akisoma Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, akiichezea timu ya yosso ya Vijana Ilala na baadae kupandishwa timu B na baadae kutua Ndanda kuichezea Ligi Daraja la Nne wilayani Ilala kabla ya kurudishwa Vijana Ilala alioisaidia kuipandisha Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka 2002.
Bao pekee aliloifungia Vijana dhidi ya Pallsons ya Arusha ndilo lililoipandisha daraja timu hiyo jambo ambalo anadai anajivunia mpaka sasa kabla ya kuichezea AFC Arusha katika michuano ya Nane Bora ya Ligi Kuu na mwaka 2004 kutua Mtibwa aliyoichezea mpaka msimu uliopita akiisaidia kuiwezesha kushika nafasi ya nne katika Ligi Kuu.
Akiwa Mtibwa, Matuta anayechizishwa na rangi zote isipokuwa zenye mng'ao mkali,

alitwaa nao ubingwa wa Kombe la Tusker- 2008, akiwa mmoja wa walioifungia mabao akishirikiana na Uhuru Seleman, Monja Liseki na Rashid Gumbo.
Kuhusu timu ya taifa aliyoichezea kuanzia timu za vijana tangu mwaka 2004, anasema inaweza kufuzu fainali za kimataifa iwapo TFF na wadau wote wataipa maandalizi ya kutosha.
Anasema chini ya kocha Kim Poulsen anamatumaini makubwa licha ya kutaka wadau kumpa nafasi kocha huyo na kuepukwa kubadilishwa kila mara kwa kikosi cha timu hiyo ili kuwafanya wachezaji wazoeane.
Pia anataka timu za taifa za vijana zipewe kipaumbele zikitafutiwa wadhamini wake ili kuwa na maandalizi mazuri, huku akiitaka TFF irejeshe mfumo wa ligi ya madaraja na kuwa wakali kwa wavunjaji wa kanuni za sheria za soka.

Omar Matuta 'Wanchope' akiwa ameshikilia kombe la Tusker la mwaka 2008 alilotwaa na Mtibwa Sugar

Vazi la taifa miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika

Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Dk Fenella Mukangara

VAZI rasmi la Taifa linatarajia kuanza kuvaliwa siku ya kilele cha sherehe za miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania zitakazofanyika Desemba 9, mwaka huu imeelezwa.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema vazi hilo litavaliwa baada ya mchakato mzima wa kulipata vazi hilo utakapokamilika ambapo umepitia hatua mbalimbali.
Waziri Fenella alisema wizara yake inatarajia kuchukua michoro minne kati ya tisa iliyopitishwa na Kamati ya Vazi la Taifa iliyoundwa ambapo pia mchakato huo unahusisha kupata aina ya kitambaa kitakachotumika kutengenezea vazi hilo.
Waziri huyo alisema kuwa michoro hiyo minne (miwili ya vazi la kitenge na mingine ya khanga) itachukuliwa na kuwasilisha kwa sekretariati ya Baraza la Mawaziri ambalo litatakiwa kufanya maamuzi kabla ya Oktoba 31 mwaka huu.
"Baada ya kupata vazi hilo,kila mtu atakuwa na uhuru wa kuvaa mtandio, kushona gauni, shati au kuvaa kitambaa cha kichwani ambacho kitakuwa kinaonyesha vazi la taifa," alisema Fenella.
Katibu wa Kamati ya Vazi la Taifa, Angella Ngowi alisema kuwa kamati yake ilipokea maoni kutoka katika sehemu mbalimbali nchini na kuongeza kwamba mchakato wa kupata vazi hilo ulianza mwaka 2003.
Alisema kuwa michoro yote iliyopo katika mchakato huo ina rangi za bendera ya taifa na alama mbalimbali kama picha ya mlima Kilimanjaro, mwenge wa Uhuru, ala za muziki na picha za wanyama (Twiga na Pundamilia).


Hosea Mgohachi: Mpiga besi wa Extra afurahie muziki kumwezesha kimaisha

Hosea Mgohachi akiwa kwenye pozi kwenye ukumbi wa White House, Kimara

Moja ya nyumba za mwanamuziki Hosea Mgohachi
Hosea Mgohachi akicharaza gitaa kwenye mazoezi ya bendi yake ya Extra Bongo
Hosea akionyesha manjonjo yake kwenye moja ya maonyesho ya Extra Bongo nchini Finland hivi karibuni ilipoenda kwa ziara maalum nchi za Scandinavia
WAKATI wasanii na wanamuziki wengine wakilia kwamba fani zao zimekuwa zikishindwa kuwanufaisha kimaisha kwa sababu hizi na zile, kwa mkung'uta gitaa la besi wa Extra Bongo, Hosea Mgohachi 'Fukuafuku' kwake ni tofauti. Mgohachi, anasema anashukuru Mungu muziki aliouanza tangu akiwa kinda akiimba na kupiga ala shuleni na kanisa la Anglican-Kurasini, umemsaidia kwa mengi kiasi hajutii kujitosa kwke kuifanya fani hiyo. "Sio siri muziki umenisaidia mengi kiasi najivunia fani hii kwani, imeniwesha kumiliki nyumba mbili zilizopo Mbagala Kilungule na Mbagala Kuu, pia nina mradi wa 'Bodaboda' wenye pikipiki kadhaa," anasema. Mbali na hayo, Mgohachi anasema muziki umemwezesha pia kutembea nchi kadhaa duniani, kupata rafiki na kuitunza familia yake kwa pato la fani hiyo. Mgohachi, mwenye ndoto za kuja kuwa mfanyabiashara mkubwa, anasema siri ya mafanikio yake imetokana na nidhamu yake katika matumizi ya fedha na kiu kubwa aliyonayo ya kuwa mfanyabiashara atakapostaafu muziki. "Mtu hupata mafanikiokwa kujituma kwa bidii, ila kubwa ni suala la nidhamu hasa kwa matumizi ya fedha, kitu ambacho nimekuwa nikizingatia kwa muda mrefu hadi kufika hapa nilipo," anasema. Anasema hata kwa wasanii na wanamuziki wenzake ni vema wakazingatia hilo iwapo wanataka kufika mbali licha ya ukweli pato litokanalo na sanaa kukiri kuwa dogo kulinganisha na ukubwa wa kazi. MDUDU Mpiga gitaa huyo aliyesoma darasa moja na nyota wa muziki wa kizazi kipya anayetamba kundi la Wanaume Halisi, Sir Juma Nature, anasema wakati akichipukia kwenye muziki alivutiwa na kwaya za St James na Kristo Mfalme. Ila kwa sasa anadai anakunwa na wapiga gitaa Minicha na Kapaya waliopo pamoja na nyota wa DR Congo, Werrason Ngiama Makanda na mpiga solo nyota wa Extra Bongo, aliyewahi kutamba na bendi kadhaa nchini Ephrem Joshua 'Kanyaga Twende'. "Hawa jamaa nawazimia sana kwa ucharazaji wao wa magitaa, hasa Joshua, yaani tukiwa kundi moja utashangaa vitu tunavyotoa," anasema. Mkali huyo, anayeitaja Extra Bongo kama bendi bomba kwake kwa namna inavyomtunza na kumlipa dau kubwa kuliko bendi zote alizowahi kuifanyia kazi, anasema hakuna chakula anachopenda kula nyama ya nguruwe maarufu kama 'Kitimoto' au 'Mdudu'. "Aisee katika vyakula ninavyopenda kula hakuna kama 'mdudu' yaani ukitaka kunifurahisha we nipe nyama hii kwa ndizi za kuchoma ," anasema. Mgohachi, ambaye hajaoa kwa sasa ingawa yu mbioni kufanya hivyo kwa mwanamke anayeishi naye, anasema pia anapenda kunywa soda na siku moja moja kusuuza roho yake kwa kugida bia. OKWI Akiwa na watoto watatu, Wilson, 7 anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Mwananyamala, Mery, 7, anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Mtoni na Junior, 3, Mgohachi anasema japo soka halicheza sana utotoni mwake, lakini ni shabiki mkubwa wa mchezo huo. Anasema yeye ni shabiki mkubwa wa Simba na Manchester United akimtaja Emmanuel Okwi anayichezea Simba kama anayemkuna kwa umahiri wake wa kufumania nyavu uwanjani. "Kati ya nyota wanaonipa raha katika soka Emmanuel Okwi ndiye kinara wao, huyu jamaa ana akili ya kufunga, mjanja na ana kipaji cha kipekee hata Yanga wanamjua," anasema kwa utani huku akicheka. Mgohachi anayepiga magitaa yote na kupapasa kinanda, anasema hakuna tukio la furaha maishani mwake kama alipomaliza kujenga nyumba yake ya Mbagala Kuu na kusitikishwa na kifo cha dada yake kilichotokea mwaka 1999. Juu ya muziki wa Tanzania, Mgohachi anayeiomba serikali iitupie macho fani ya sanaa ili kuwainua wasanii, anasema umepiga hatua kubwa tofauti na miaka ya nyuma, ingawa anataka wanamuziki kubadilika na kuwa wabunifu zaidi./ Anasema ubunifu utaweza kuutangaza muziki huo kimataifa kama ilivyokuwa ikifanywa na makundi kama Tatu Nane, InAfrica Band na wengine. "Lazima tuwe wabunifu tuweze kutamba kimataifa, tuachane na kasumba na kupenda kuwaiga wakongo tunawatangaza zaidi wao badala ya muziki wetu," anasema. ALIPOTOKA Hosea Simon Mgohachi, alizaliwa Aprili 14, 1978 jijini Dar es Salaam akiwa mtoto wa nne kati ya watano wa familia yao, alisoma Shule ya Msingi Kurasini alipoanza kuonyesha kipaji chake cha sanaa akiimba kwaya na kupiga ala. Mbali na shuleni, Mgohachi pia alikuwa akiimbia kwaya ya kanisa lao la Anglican chini ya walimu Charles na Yaredi Disanura kabla ya kupitia makundi ya Chikoike Sound na Mwenge Jazz. Bendi yake ya kwanza kuifanyia kazi kama mwanamuziki kamili ni African Beat mnamo mwaka 1998 kabla ya kutua Mchinga Sound 'Wana Kipepeo' akiwa na rafikie Ibrahim Kandaya 'Profesa' aliyepo Msondo Band kwa sasa. Bendi nyingine alizofanyia kazi mwanamuziki huyo anayewaasa wasanii wenzake na watanzania kwa ujumla kujiepusha na Ukimwi kwa kujenga utamaduni wa kuwa waaminifu na kupima afya zao sawia na kutumia kondomu inaposhikana ni Double M Sound, Double Extra, Chipolopolo na African Vibration. Pia amewahi kufanya kazi za muziki Umangani kwa zaidi ya mara mbili wakati akiipigia bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' kabla ya mwaka jana kuhamia Extra Bongo alionao mpaka sasa akiwa amerejea nao kutokea nchi za Skandinavia. Mgohachi anayependa kutumia muda wake kuangalia vipindi vya runinga na kusikiliza muziki wa Bongofleva akimzimia Sir Juma Nature anasema atakuwa mchoyo wa fadhila kama hatawashukuru wazazi wake, Mama Shuu, Mudhihir Mudhihir na Ally Choki kwa namna walivyomfikisha hapo alipo.

Hosea Mgohachi akiwa katika pozi
Hosea Mgohachi akiwa na mwanae Junior

Wednesday, September 5, 2012

Eddo Boy: Kinda la Simba achekeleaye kuitungua Mtibwa Sugar

LICHA ya kuibuka mfungaji bora wa michuano ya Super8, mshambuliaji kinda wa Simba, Edward Christopher Shija 'Eddo Boy' a.k.a Teko Modise, amedai hajafurahishwa kama alivyoibebesha timu yake ubingwa wa michuano hiyo. Eddo, alisema tuzo ya ufungaji bora kwake isingekuwa na maana kama Simba isingekuwa mabingwa kwa jinsi walivyojituma na kuipigania timu yao. "Ingawa mechi ya fainali dhidi ya Mtibwa Sugar kwangu ni mechi ngumu kuwahi kuicheza kwa jinsi ilivyokuwa na funga nikufunge, ila sijivunii tuzo ya ufungaji bora wala kung'ara kwangu zaidi ya kuipa Simba ubingwa," alisema. Alisema, mara pambano lilipoisha akiifungia bao la ushindi katika matokeo ya mabao 4-3, alijisikia faraja kwa kutwaa taji jingine akiwa na Simba. "Mechi na Mtibwa sintoisahau kwa walivyocheza na kurejesha mabao yetu kila tulipofunga kabla ya kuwazidi ujanja kwa bao la nne lililotupa ubingwa, hakika najisikia fahari kwa kuilaza Mtibwa na kuipa Simba taji jingine," alisema. Kabla ya taji hilo, Eddo alishatwaa na Simba mataji ya Rolling Stone 2011, Kinesi 2011, Uhai 2011 na Ujirani Mwema lililochezwa mwaka huu. Pamoja na mafanikio yote, Eddo anayeichezea pia timu ya taifa, akipandishwa mwaka huu na kocha Kim Poulsen toka timu ya U20, alisema habweteki wala kulewa sifa. "Siwezi kulewa sifa kwa mafanikio niliyonayo kwa kipindi kifupi, ndoto zangu nije kucheza soka la kulipwa Ulaya na kutamba kimataifa," alisema. LUNYAMILA Eddo, alizaliwa Septemba 10, 1992 mjini Tabora akiwa mtoto wa pili kati ya watatu kwa familia iliyolelewa na mama pekee. Elimu ya Msingi aliisoma Shule za Choma Chankola,Tabora na Mwele ya Morogoro, kabla ya kujiunga na Sekondari za St Francis na baadae Makongo. Kisoka alianza kutamba tangu akiwa darasa la tatu akiwa Morogoro, timu yake ya chandimu ikiwa ni Jamhuri Ball Boys na baadae Moro Kids iliyowakusanya baadhi ya nyota wanaotamba kwa sasa nchini. Alisema wakati akichipukia alivutiwa na baadhi ya nyota wa zamani wa Simba na Yanga kama Edibily Lunyamila, Salvatory Edward, Mark Sirengo na Nteze John wa Simba, huku akimtaja kocha Yahya Belini kama mtu aliyekigundua na kukiendeleza kipaji chake. Eddo alisema safari yake kisoka ilipata vikwazo vingi toka kwa mama yake aliyekuwa hapendi kabisa acheze, kiasi cha kumchapa, kumnyima chakula na hata kumfungia na kulala nje pale alipomkaidi na kujihusisha na soka. "Mama yangu aliyekwishafariki hakupenda nicheze soka, ila nilikuwa nunda na kuishia kulambwa bakora, kunyimwa chakula na hata kufungiwa mlango na kulala nje, ingawa sikukata tamaa," alisema. Alisema jambo zuri ni kwamba kabla mama yake hajafariki mwaka 2005 alishaanza kusikia sifa zake kisoka toka kwa shoga zake na kumuacha acheze hasa alipohamia Makongo jijini Dar es Salaam. Eddo, aliyedai hajaonana na baba yake mzazi tangu mwaka 1998 baada ya kutengana na marehemu mama yao, alisema roho inamuuma kuona mamaye akifa bila kula jasho lake kisoka. YANGA B Eddo, anayependa kula vyakula vyote na kunywa vinywaji laini, alisema safari yake kisoka alipohamia Dar aliwahi kuichezea Yanga B aliyokuja kuachana nayo baada ya kuona hawana muelekeo wowote wa kimaendeleo.maendeleo. Alisema alienda Yanga baada ya kuisaidia Kinondoni kutwaa ubingwa wa Copa Coca Cola mwaka 2007 na kisha kuifikisha timu ya Kinondoni katika fainali za Taifa na kulazwa na Ilala mabao 5-0. Alisema alipoachana na Yanga alirejea darasani katika Shule ya Lord Baden Powell kabla ya kutimkia Moro United B aliyoichezea kabla ya kutua Miundo Mbinu ya Lindi aliyoipandisha daraja la kwanza na kuichezea timu ya mkoa wa Lindi katika michuano ya Kombe la Taifa 2009. Alisema mara baada ya fainali hizo na Lindi kufungwa na Singida, ndipo aliponyakuliwa na Simba kung'ara nao akinyakua mataji na tuzo mbalimbali hadi kupandishwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo msimu uliopita. Eddo anayezishabikia Arsenal, Barcelona, Orlando Pirates na Brazil akiwazimia Neymar, Samuel Etoo na Ronaldo de Lima, alisema soka limempa mafanikio mengi kisoka na maisha ingawa hakupenda mambo yake yaanikwe. "Soka limenisaidia mengi, ila sipendi kila mtu ajue, najivunia na kiu yangu ni kung'ara zaidi nicheze soka la kulipwa Ulaya, safari yangu bado kabisa Simba sio mwisho wangu," alisema. Eddo ambaye hajaoa wala kuwa na mtoto, ingawa angependa kuwa na watoto watatu atakapooa, alitoa wito kwa wachezaji wenzake kujituma, kujiamini na kuwa na nidhamu waweze kufika mbali. Pia aliwakumbusha viongozi wa soka nchini kubadilika na kuachana na tabia ya kutumia nguvu na fedha nyingi kuwapapatikia 'mapro' wa kigeni na badala yake kuwekeza katika soka la vijana ili kulisaidia taifa hapo baadae. "Mafanikio ya kikosi cha Simba B ni funzo kwa viongozi na wadau wa soka nchini wawekeze katika soka la vijana badala ya kupigana kumbo kugombea mapro wa nje, fedha wazitumiapo kwao zisaidie soka la vijana," alisema. Eddo anayetamani kuwa mfanyabiashara mkubwa atakapostaafu soka na anayependa muziki wa reggae akimzimia J Booge, Biggy Signal na P Square, aliwashukuru mama yake, makocha wote waliomnoa na rafiki na wachezaji wenzake kwa kufika hapo alipo. Nyota huyo asiyeamini mambo ya uchawi katika soka akiamini mazoezi ndio kila kitu, alisema angekutana na Rais au waziri wa michezo angewaomba zijengwe na kuanzishwa shule maalum za michezo. pia kutaka soka la vijana lipewe kipaumbele zaidi. Mwisho

KIMOBITEL ALIVYOREJEA 'NYUMBANI' EXTRA BONGO

PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UTAMBULISHO WA KHADIJA MNOGA KIMOBITEL ALIPOREA BENDI YA EXTRA BONGO JANA JIJINI DAR ES SALAAM.

Mzee Yusuf aanzisha kampuni kusambaza kazi ili kudhibiti wezi

NYOTA wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yusuf 'Mfalme' amefungua kampuni yake binafsi ya usambazaji wa kazi zake na wasanii wengine iitwayo MY Collection. Akizungumza na MICHARAZO, mkurugenzi huyo wa kundi la Jahazi Modern Taaran alisema ameamua kufungua kampuni hiyo ili kusaidia kuthibiti uchakachuaji na wizi wa kazi zake ambao umekuwa ukimkomesha mapato mengi. Alisema kampuni hiyo ambayo imeshafungua duka la kuuzia cd na dvd katika mitaa ya Likoma na Mhonda itakuwa ikihusika na usambazaji na uuzaji wa kazi za Jahazi Modern na zile za wasanii wengine iwapo watapenda kufanya hivyo kwake. "Katika kukabiliana na vitendo vya wizi wa kazi zangu, nimeamua kufungua kampuni ya usambazaji na uuzaji wa cd na dvd ambayo itahusika na kazi zote za Jahazi Modern, ila kama kutakuwa na watakaotaka kuwasaidia kusambaza kazi zao sitakuwa na noma," alisema. Naye Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Mussa Msuba duka walillofungua litakuwa likihusika na kuuza kazi za taarab kwa jumla na rejereja ili kuwarahisishia mashabiki wa muziki huo eneo la kupata burudani hiyo. "Hili ni duka la awali tu, pnago ni kufungua karibu kila kona ya nchi kuwarahisishia mashabiki mahali pa kupata burudani za taarab kwa matumizi yao ya majumbani na ya kibiashara kwa ujumla na hasa kazi za Jahazi ambao wanatarajia kutoa albamu mpya ya tisa," alisema Msuba. Uamuzi wa Mzee Yusuf kufungua kampuni na duka hilo, imekuja mwezi mmoja baada ya kunasa baadhi ya albamu zake zilizochakachuliwa walipoendesha msako wakishirikiana na wadau wengine wa sanaa wakiwemo Shirikisho la Filamu Tanzania, TAFF na Bongo Movie.

Erick Mawalla: Kinda anayeililia ligi ya vijana, kombe la Taifa

KUTOKUWEPO kwa ligi ya muda mrefu na ya kudumu kwa timu za vijana na kutopewa kipaumbele kwa michuano ya Kombe la Taifa, kunamfanya beki kinda anayepanda chati nchini, Erick Mawalla 'Sekana' aamini ni sababu ya kudidimia kwa soka la Tanzania. Beki huyo aliyetua African Lyon akitokea timu iliyoshuka daraja ya Moro United anasema michuano ya timu za vijana na Kombe la Taifa kwa mtazamo wake ndio ukombozi wa soka la Tanzania na kurejesha makali yake katika anga la kimataifa. "Hatuwezi kufanya vema kwenye michuano ya kimataifa iwapo hatuna ligi ya vijana, lazima iwepo mipango ya kuanzisha ligi hiyo na kuipa kipaumbele michuano ya Kombe la Taifa, ambayo siku za nyuma ilitumika kuibua nyota waliotamba nchini," anasema. Anasema hata klabu na mataifa yanayofanya vema katika soka la kimataifa, zilipoteza fedha zao kuwekeza kwa vijana na mavuno yao yanavutia kila mtu, kitu ambacho ametaka Tanzania nayo kufuata nyayo hizo ili ifanikiwe. "Bila kuwepo kwa ligi ya kudumu ya vijana, au shule maalum za kukuzia vipaji tangu utotoni na kutopewa kipaumbele kwa michuano muhimu kama Kombe la Taifa ni vigumu kuwa na timu imara kuanzia ngazi za klabu mpaka timu za taifa," anasema. Erick aliyeanza kucheza soka tangu shuleni kama winga kabla ya kubadilishwa na kuwa beki, anasema kuanzia serikali, wafadhili, viongozi na mashabiki watambue hakuna njia ya mkato ya mafanikio katika michezo bila watu kuwekeza fedha zao katika sekta hiyo. NYOTA NJEMA Kinda hilo, linalopenda kula chakula cha aina yoyote mradi akimdhuru na kunywa Juisi, anasema anashukuru soka kumsaidia kwa mengi ikiwamo kutwaa mataji na tuzo kadhaa tangu akiwa kinda ukiacha mafanikio binafsi ya kimaisha. "Siwezi kusema nimefanikiwa sana, ila nashukuru kwa muda mfupi niliopo katika soka nafarajika nimeweza kupata mafanikio ya kujivunia ikiwamo kutwaa vikombe, tuzo na kupata fedha zinazosaidia kuendesha maisha yangu," anasema. Erick, 'swahiba' mkubwa wa Mfungaji Bora wa michuano ya Super 8 anayeichezea Simba, Edward Christopher 'Eddo Boy', anasema moja ya mataji ambayo hawezi kusahau maishani mwake ni Kombe la Copa Coca Cola 2007 akiwa na timu ya vijana ya Kinondoni. "Hili ndilo lilikuwa taji langu la kwanza kubwa katika maisha ya soka, kwa hakika nilifurahi mno kuipa Kinondoni taji hilo, ingawa nimeshatwaa pia ubingwa wa Kombe la Taifa nikiwa na Ilala na mwaka jana tulishika nafasi ya tatu katika michuano kama hiyo," anasema. Erick, aliyeingia kwenye soka kwa kuvutiwa na 'mapacha' wa zamani wa klabu anayoishabikia ya Manchester United, Dwight Yorke na Andy Cole, anasema kabla ya kuibukia kwenye Coca Cola, kipaji chake kilianza kuonekana Kijitonyama Stars aliyoichezea tangu akiwa darasa la sita. "Baadae nilitua Yanga B nikiwa na swahiba wangu Eddo Boy na wengine, lakini kutokana na klabu hiyo kuonekana haikuwa na mipango endelevu ya soka la vijana, nilihamia Moro Utd B na kuichezea kwa misimu kadhaa akishuka na kupanda nayo Ligi Kuu," anasema. Chipukizi huyo anasema alikuwa katika kikosi cha Moro kilichoshuka daraja msimu wa 2009-2010 na kuirejesha tena Ligi Kuu msimu uliopita kabla ya kuzama tena na yeye kukimbilia African Lyon. Matarajio ya Erick anayeishabikia pia Real Madrid na aliyewataja makocha Juma Matokeo na Seleman Kiiza kama watu waliosaidia kukuza kipaji chake, ni kucheza soka la kulipwa nje ya nchi akidai tayari ameanza kipango ya jambo hilo. "Kiu yangu kubwa ni kucheza soka la kulipwa hasa Ulaya, naamini ni kipaji na uwezo wa kufanya hivyo, ingawa napenda kabla ya hapo nipate fursa ya kulitumikia taifa langu," anasema. Mchezaji huyo anasema licha ya kuitwa mara kadhaa katika vikosi vya timu za vijana U17 na U20, kiu yake kubwa ni kuichezea Taifa Stars. NSAJIGWA Erick anayehuzunishwa na kifo cha baba yake kilichotokea mwaka 2006, anasema licha ya kucheza mechi nyingi, pambano gumu kwake ni lile la Moro United dhidi ya Yanga lililochezwa msimu uliopita na lililoisha kwa sare ya mabao 2-2. Anasema anaikumbuka mechi hiyo hasa kwa tukio lililofanywa na aliyekuwa nahodha wa Taifa Stars, Shadrack Nsajigwa cha kumpiga 'kiwiko' winga wao Benedict Ngassa na kutolewa nje kwa kadi nyekundu na jinsi Yanga iliyosawazisha bao la pili. "Ni mechi hiyo na ile ya nusu fainali dhidi ya Mwanza katika michuano ya Kombe la Taifa 2011 tuliyopoteza ndizo ninazozikumbuka kwa ugumu na namna zilivyojaa upinzani," anasema. Erick Lawrance Mawalla alizaliwa Julai 5, 1993 jijini Dar es Salaam akiwa mtoto wa kwanza kati ya wanne wa familia yao, alisoma Shule ya Msingi Bunge kabla ya kutua Makongo Sekondari kutokana na kipaji chake cha soka. Akiwa Makongo ndiko alikoitwa timu ya vijana ya Kinondoni na baadae timu ya taifa ya U17 kabla ya kupandishwa ile ya U20 chini ya kocha Kim Poulsen. Anasema kama kuna watu anaowashukuru kumsaidia kufanikiwa kisoka na maisha basi si wengine zaidi ya wazazi, makocha wake na wachezaji wenzake bila kuusahau uongozi wa Moro United. Erick anayependa kusikiliza muziki na kuangalia filamu, anasema kama angekutana na Rais wau Waziri wa Michezo kilio chake kingekuwa juu ya kujengwa shule maalum za michezo.

Kimobiteli arejea Extra Bongo, atua na moja mpya

BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo imemrejesha kundini aliyekuwa muimbaji wao Khadija Mnoga 'Kimobitel' aliyekuwa ametimkia African Stars 'Twanga Pepeta'. Uongozi wa Extra Bongo ulisema umemrejesha kundini mwanamuziki huyo baada ya mwenyewe kuridhia kurudi huku bendi yao ikiwa ina upungufu mkubwa katika safu ya uimbaji kwa sauti ya kike. Mkurugenzi wa Extra, Ally Choki, alisema wakati wa kumtambulisha muimbaji huyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa kurejea kwa Kimobitel kutasaidia kuimarisha safu yao ya uimbaji. Choki alisema Kimobitel aliyeikacha Extra Bongo miezi kadhaa iliyopita amerejea kundini akiwa na 'zawadi' kwa mashabiki kwa kuja na wimbo mpya uitwao 'Mgeni'. Mkurugenzi huyo alisema Extra Bongo inatarajiwa kumtambulisha rasmi Kimobiteli kwa mashabiki wiki ijayo baada ya kufanya mazoezi ya kutosha na wenzake. Kimobitel alisema amerejea Extra Bongo bila kulazimishwa na mtu huku akidai bendi aliyotoka hakuwa na mkataba wowote na hivyo anawaomba mashabiki wa bendi hiyo wampokee na watarajie mambo mazuri kutoka kwao. "Nimeamua mwenyewe kurejea Extra Bongo, na yale yaliyopita yamepita tuangalie mapya ninachoomba mashabiki wetu wasubiri vitu adimu toka kwangu," alisema. Mwanadada huyo aliyewahi kutamba na bendi mbalimbali ikiwemo African Revolution na Double M Sound, alisema anaamini aliwakwaza watu alipoondoka Extra Bongo, lakini ni suala la kusameheana kwani ametambua alipotoka na amerejea nyumbani akihitaji kupokelewa vema. Naye kiongozi wa bendi hiyo, Rogart Hegga 'Katapila' alisema wana Extra Bongo wamefurahishwa na ujio wa Kimobitel akidai bendi yao sasa imekamilika vya kutosha hasa baada ya kushindwa kuziba pengo la mwanamuziki huyo tangu alipoondoka. Alisema licha ya kwamba mwanamuziki huyo atatambulishwa rasmi wiki ijayo, lakini bendi yao itaendelea na maonyesho yao kama kawaida wiki hii kwa siku za Ijumaa na Jumapili kufanya vitu vyao White House-Kimara na Jumamosi Meeda Club, Sinza. Mara baada ya utambulisho wa mwanamuziki huyo kwa waandishi, alitambulishwa pia kwa wanamuziki wote wa Extra Bongo ambapo kwa kauli moja wanamuziki hao walimpokea na kumkaribisha nyumbani wakimuahidi ushirikiano ili bendi yao izidi kupaa.

Monday, August 13, 2012

Simba, Azam, Mtibwa zafuzu semi fainali Super8

TIMU za soka za Simba na Azam zinatarajiwa kukumbushia mechi yao ya robo fainali za Kombe la Kagame 2012 zitakapokutana katika nusu fainali ya Super 8 baada ya zote kufuzu hatua hiyo ya michuano hiyo maalum inayodhaminiwa na BancABC. Simba imetinga hatua hiyo baada ya kuifunga Zimamoto ya Zanzibar mabao 2-0 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. Simba walioingiza kikosi chao cha pili kwenye michuano hiyo, kinachonolewa na Kocha Suleiman Abdallah Matola, ilipata mabao yote yote kupitia kwa kiungo chipukizi anayeinukia vema katika soka ya Tanzania, Christopher Edward kipindi cha pili. Christopher ambaye hukomazwa pia kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na kikosi cha kwanza cha Simba, alifunga bao la kwanza penalti dakika ya 50, baada ya beki Miraj Adam kuangushwa kwenye eneo la hatari. Edward ambaye ni kipenzi cha kocha Mserbia wa Simba, Profesa Milovan Cirkovick, alifunga bao la pili dakika ya 55 baada ya kuwapiga chenga mabeki watatu wa Zimamoto kabla ya kumchambua kipa wa timu hiyo ya Zanzibar. Pamoja na Simba SC kuwania ubingwa wa michuano hiyo, lakini sasa Christopher ameingia kwenye mbio za kiatu cha dhahabu cha michuano hiyo, kwa kufikisha mabao manne, akiwa anaongoza. Katika michezo mingine ya kuhitimisha hatua ya makundi ya michuano hiyo, Uwanja wa Chamazi, Jamhuri FC iliichapa 4-0 Mtende, zote za Zanzibar mabao ya washindi yakifungwa na Sadik Rajab dakika ya 20, 44, Issa Achimwene aliyejifunga dakika ya 82 na Suleiman Khatib dakika ya 88. Kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi, Azam FC ilitoka nyuma kwa bao 1-0 na kuifunga Polisi Moro FC mabao 2-1, mabao yake yakitiwa kimiani na beki Said Mourad dakika ya 20 na Abdi Kassim ‘Babbi’ dakika ya 70, wakati la Maafande wa Morogoro lilitiwa kimiani na Mokili Rambo dakika ya kwanza. Polisi ilimpoteza mchezaji wake, Abdallah Rajab dakika ya 88 aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu. Uwanja wa Amaan, Zanzibar, Kocha Mecky Mexime ataiongoza Mtibwa Sugar katika mchezo wa mwisho wa makundi dhidi ya wenyeji Super Falcon FC. Katika Kundi A, Simba SC inaongoza kwa pointi zake nne, baada ya kutoa sare moja na kushinda moja, ikifuatiwa na Zimamoto na Mtende zinazofungana kwa pointi tatu kila moja, wakati Jamhuri inashika mkia kwa pointi yake moja. Kundi B, Mtibwa inaongoza kwa pointi zake sita ikifuatiwa na Azam FC na Polisi Moro, zenye pointi tatu kila moja, wakati Falcon inashika mkia, ikiwa haina pointi hata moja. Kwa kufuzu hatua hiyo, Simba inatarajiwa kuvaana na Azam, ambao katika mechi yao ya Kagame waliishindilia 'Mnyama' mabao 3-1 yote yakiwekwa kimiani na John Bocco aliyepo Afrika kwa sasa kifanya majaribio katika klabu ya Super Sports. Mechi nyingine itakayochezwa mapema saa 8 siku hiyo ya Jumamosi itazikutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya jamhuri ya Pemba. Mechi zote za Nusu fainali na fainali zote zitachezwa Dar es Salaam. Mdhamini wa michuano hiyo, Banc ABC anagharamia usafiri wa ndege kwa timu zote kutoka kituo kimoja hadi kingine, malazi na jezi. Kanuni za mashindano haya ni kushirikisha timu zilizoshika nafasi tatu za juu katika Ligi Kuu za Bara na visiwani na mbili zilioongoza katika kupanda Ligi Kuu zote mbili, lakini kwa Bara, Yanga waliokuwa washindi wa tatu msimu uliopita, walijitokea na nafasi yao ikachukuliwa na Mtibwa Sugar ambayo ilishika nafasi ya nne kwenye Ligi Kuu. Bingwa wa michuano hiyo mipya itakayokuwa ikifanyika kila mwaka, ataondoka na Sh. Milioni 40, mshindi wa pili Sh. Milioni 20, wa tatu Sh. Milioni 15 sawa na wa nne, wakati washiriki wengine wataondoka na Sh. Milioni 5 kila moja. NUSU FAINALI Agosti 15, 2012 Mtibwa Sugar Vs Jamhuri (Saa 8:00 mchana) Simba SC Vs Azam FC (Saa 10:00 jioni) (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam)

Sunday, August 12, 2012

Chelsea, Man City kufungua pazia la msimu mpya EPL leo

PAZIA la msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL)kwa mwaka 2012/13 linatarajiwa kufunguliwa rasmi leo Jumapili kwa mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kati ya Mabingwa wa Ligi Kuu England, Manchester City, na Mabingwa wa FA Cup, Chelsea, ambao pia ni Mabingwa wa Ulaya. Pambano la timu hizo mbili zitakazoshuka dimbani leo zikiwa na mabadiliko yanayotofautiana katika vikosi vyao unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Villa Park, kuanzia saa 9 Alasiri kwa saa za Afrika Mashariki na Kati. Wakati Chelsea ikiwa na nyota wapya walionunuliwa hivi karibuni kwa ajili ya msimu mpya, Man City wao hawana mabadiliko yoyote. Chelsea itashuka dimbani leo ikiwa haina kinara aliyewapa mataji hayo mawili inayoyashikilia kwa sasa Didier Drogba, kutoka Ivory Coast aliyehamia katika klabu ya Shanghai Shenhua ya China akiungana na Nicolas Anelka. Vifaa vipya vilivyosajiliwa na ambavyo vimeanza kuonyesha makeke katika mechi za kujipima nguvu kujiandaa na msimu mpya utakaoanza mwishoni mwa wiki ijayo ni Eden Hazard, Marko Marin na Oscar lakini ni Hazard na Marin ambao wanaweza kucheza Mechi hii na Man City kwa vile Oscar atakuwa bado yuko na nchi yake Brazil kwenye Olimpiki. Msimu uliopita, Timu hizi ziligawana ushindi kwa Chelsea kuifunga Man City 2-1 Mwezi Desemba na Man City kuifunga Chelsea 2-1 Mwezi Machi. Katika Mechi zao za hivi karibuni, Mechi za kujipasha kwa ajili ya Msimu mpya, Chelsea imekuwa na matokeo yasiyoridhisha kwa kushinda Mechi moja tu kati ya 4 walizocheza na kufungwa zilizobaki wakati Man City wamecheza Mechi 5 na kushinda 3 na kufungwa mbili. Chelsea hawana majeruhi yeyote lakini Man City watamkosa Nahodha wao Vincent Kompany na Micah Richards ambao wameumia. Vikosi vinatarajiwa kupangwa kwa siku ya leo ni kama ifuatavyo: Chelsea [Mfumo 4-3-3]: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Mikel, Meireles, Lampard, Ramires, Torres, Hazard Man City [Mfumo 4-4-2]: Hart, Zabaleta, Savic, Lescott, Clichy, Yaya Toure, De Jong, Nasri, Johnson, Tevez, Aguero