STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 11, 2013

Hatma ya Milovan Simba leo

Kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic


HATMA ya aliyekuwa kocha wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic, kulipwa fidia yake ya kusitisha mkataba wa kuifundisha timu hiyo huenda ikajulikana leo wakati atakapokutana na viongozi wa klabu hiyo kabla ya kurejea kwao baada ya kupata haki yake.
Hata hivyo, Milovan ambaye ameumizwa na sare ambazo Simba imeendelea kuzipata, alisema jana kwamba yuko tayari kurejea kwenye timu hiyo endapo uongozi utamrejesha.
Milovan anaidai Simba dola za Marekani 24,000 (Sh. milioni 36), ambazo ni malimbikizo ya mishahara yake ya miezi mitatu.
Akizungumza jana, Milovan, alisema kwamba  hadi sasa anafahamu kuwa yeye bado ni kocha halali wa timu hiyo kwani mkataba wake unamalizika Julai Mosi mwaka huu.
Mserbia huyo alisema kwamba ndiyo maana, baada ya kuona viongozi wa klabu hiyo wakikaa kimya, aliamua kuja nchini kufuatilia haki yake na kwamba, hata hoteli anayoishi jijini Dar es Salaam gharama zake zitalipwa na Simba.
"Mimi najua bado ni kocha wa Simba kwa sababu mkataba wangu haujamalizika. Na kama watakuwa tayari kuzungumza na mimi, naweza kurejea kazini. Bila shaka mnajua uwezo wangu na nini nilikifanya katika ligi na mshindano ya kimataifa mwaka jana," alisema kocha huyo.
Aliongeza kwamba kabla ya kukutana leo na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alitarajiwa kukutana jana na katibu mkuu wa timu hiyo, Evodius Mtawala; ambaye ndiye huwasiliana naye mara kwa mara.
"Hata hivyo, naye aliahidi tutakutana leo (jana) asubuhi, lakini sijamuona na alisema kwamba anamsubiri Rage na Kaburu,"  aliongeza Milovan.
Akihojiwa juzi katika kipindi cha michezo cha Radio One, Rage alikiri kocha huyo kuidai Simba lakini akashangazwa na maamuzi yake (Milovan) kufuata malipo yake jijini Dar es Salaam wakati wao walimueleza kuwa watamtumia kwa njia salama za kibenki.
Milovan alitua jijini Jumatano wiki iliyopita na kulieleza gazeti hili kwamba amechukua maamuzi ya kufuata haki yake baada ya kuona ahadi alizopewa kwa njia ya simu hazitekelezwi na kwamba sasa, anafahamu kuwa klabu hiyo inazo fedha baada ya kumuuza kwa klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia aliyekuwa mshambuliaji wao wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi.
 

CHANZO:NIPASHE

MAN UNITED YAZIDI KUPAA ENGLAND, MAN CITY WAKATA TAMAA


VINARA wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Manchester United imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo baada ya kuendeleza wimbo lake la ushindi kwa kuilaza Everton mabao 2-0, huku wakishuhudiwa na kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho ambao watakutana na kikosi chake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Timu hizo mbili zitakutana Jumatano katika mechi hizo za kuwania kutinga robo fainali za Ulaya, ambapo Mourinho ambao vijana wao jana walipata ushindi mnono wa mabao 4-1 dhidi ya Sevilla 
ipashia vema misuli Real Madrid na Cristiano Ronaldo wao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Everton na kuzidi kupaa kileleni mwa Ligi Kuu England kwa pointi 12 zaidi.
Pamoja na Jose Mourinho kuushuhudia mchezo huo, Real Madrid inaonekana haitakuwa na kazi nyepesi mbele ya United ambayo leo ushindi wake umetokana na mabao ya Ryan Giggs na Robin van Persie.
Gap: Manchester United moved 12 points clear of rivals City at the top of the table
Wachezaji wa Manchester United wakishangilia

AZAM YAIKAMATA YANGA, WAISHINDILIA MTIBWA 4-1




Kikosi cha Azam  ambacho jana kiliendelea kushinda mechi zake kwa asilimia 100

TIMU ya soka ya Azam jana ilifanikiwa kuikamata Yanga kileleni baada ya kuizabua Mtibwa Sugar kwa mabao 4-1 katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, huku mshambuliaji wake wa kimataifa, Kipre Tchetche akirejea dimbani kwa kishindo akifua mabao mawili kati ya hayo.
Azam ilipata ushindi huo katika mechi pekee iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro na kurejea rekodi kama hiyo waliyoipata mbele ya Mtibwa katika uwanja huo misimu miwili iliyopita.
Kipre Tchetche aliyekuwa majeruihi alirejea kwa kishindo katika kiosi cha Azam kwa kufunga mabao mawili, baada ya kushuhudiwa dakika 45 za kwanza zikiisha kwa sare ya baoa 1-1.
Bao la Azam la kwanza lilifungwa na Humphrey Aturdo kabla ya Vincent Barnabas wa Mtibwa kusawazisha na walipoanza kipindi cha pili, Mganda Brian Umony  alifunga bao la pili kabla ya Tchetche kutupia mengine mawili moja dakika za lala salama.
Kwa ushindi huo, Azam sasa wameikamta Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ya Bara baada ya kufikisha pointi 33, lakini wakiendelea kukamata nafasi ya pili kwa tofauti ya magoli. Yanga imefunga mabao 29 na kufungwa 12 wakati Azam wamefunga goli 27 na kufungwa 14.
Wenyewe Yanga watashuika dimbani siku ya Jumatano kuvaana na African Lyon katika pambano litakalochezwa uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo tayari wachezaji wa Yanga jana usiku waliingia kambini tayari kwa mchezo huo wakipania kupata ushindi.
Kwa mabao mawili ya jana Kipre Tchetche amefikisha jumla ya mabao 10 na kumzidi Mrundi wa Yanga, Didier Kavumbangu aliyesaliwa na mabao yake nane tangu duru lililopita.
Ligi hiyo itaendelea Jumatano kwa michezo mingine kadhaa mbali na huo wa Yanga na Lyon ambayo imeendelea kugawa pointi kwa wapinzani wao tangu duru la pili lianze.

NIGERIA BINGWA MPYA WA AFRIKA YAIZIMA BURKINA FASO


Cup of joy: A jubilant Nigeria squad hoist the Africa Cup of Nations trophy aloft for the third time
Wachezaji wa Nigeria wakishangilia Kombe lao la Mataifa ya Afrika baada ya kuifunga Burkina Faso kwenye Fainali nchini Afrika Kusini jana.Fancy seeing you again: Nigeria coach Stephen Keshi grabs the Africa Cup of Nations trophy after winning the competition as a player in 1994
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi akiwa ameshika Kombe ambalo awali alitwaa akiwa mchezaji mwaka 1994Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in Johannesburg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter wa pili kutoka kulia alikuwepo Johannesbug jana, chini mashabiki wakiwa na bango na kuonyesha upendo wa Waafrika kwake
Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in South Africa
Winner: Sunday Mba is congratulated by Nigeria team-mates after firing the only goal of the game
Sunday Mba akipongezwa na wenzake kwa kufunga bao la ubingwa
No holds barred: Burkina Faso's Mady Panandetiguiri clashes with Nigeria keeper Vincent Enyeama
Mchezaji wa Burkina Faso, Mady Panandetiguiri akivaana na kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama
Outnumbered: Nigeria's Victor Moses scraps for possession with Burkina Faso's Bakary Kone (centre), Mohamed Koffi (back) and Djakaridja Kone (right)
Mchezaji wa Nigeria, Victor Moses akipambana na ukuta Burkina Faso, Bakary Kone (katikati), Mohamed Koffi (nyuma) na Djakaridja Kone (kulia)

NCHI ya Nigeria jana usiku ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu miaka 19 na taji la tatu kwa nchi hiyo baada ya kuifunga Burkina Faso bao 1-0 katika fainali kali iliyopigwa kwenye Uwanja wa FNB(Soccer City), Johannesburg, Afrika Kusini.
Shujaa wa Nigeria kwa mechi ya jana alikuwa ni Sunday Mba aliyefunga bao hilo pekee la ushindi dakika ya 40, baada ya kutokea purukushani kwenye lango la Burkina Faso.
Burkina Faso ambayo hiyo ndiyo fainali yake ya kwanza kucheza tangu ilipoanza kushiriki michuano hiyo, ilipigana kutaka kurudisha bao hilo, lakini bahati haikuwa yao na hivyo kujikuta wakijifuta machozi kwa kushika nafasi ya pili.
Nigeria ilitwaa taji la michuano hiyo mwaka 1980 na 1994 na baada ya hapo ilikuwa ikishuhudia mataifa mengine yakinyakua kabla ya mwaka huu ikiwa chini ya kocha mzawa Stephen Keshi aliyenyakua taji la mwisho mwaka 1994, kuibebesha taji hilo akiweka rekodi ya kuwa kocha wa 15 mzawa kubebea taji hilo dhidi ya 14 ya makocha wa kigeni wa nchi mbalimbali katika michuano hiyo ya Afrika.

NJIKU KUWANIA TAJI LA PST SIKU YA WAPENDANAO



Mabondia Omary Ramadhani kushoto na Deo Njiku wakitunishiana misuri baada ya kusaini mkataba kupigania ubingwa wa Tanzania PST siku ya February 14 katika ukumbi wa Friends Corner Hotel Manzese picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
MABONDIA Deo Njiku wa Morogoro na Omary Ramadhani wataingia uringoni  February 14 katika ukumbi wa Friends Corner Hotel Manzese 14 kuwania Ubingwa wa Tanzania PST 


Mpambano huo wa aina yake unatarajiwa kuwa wa kusisimua kutokana kila mtu kuwa na rekodi nzuri mpambano uho utakaosindikizwa na mpambano mwingine wa ubingwa kati ya  Godfrey Silver na Adam Yahya ambapo mipambano hiyo itakuwa ya raundi kumi
Huku kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Nchini, Rajabu Mhamila 'Super D' atampandisha kwa mara ya kwanza bondia wake mpya Iddy Mnyeke kuvaana na Sadiki Momba mpambano utakaopigwa kwa raundi nne

Mgeni rasmi siku hiyo anatsrahjiwa kuwa ni Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa kinondoni Charles Kenyela atakaewafisha mikanda ya ubingwa

Super D, alisema katika mpambano huo atasambaza DVD zake mpya tofauti na kanda yake ya awali iliyokwenda kwa SUPER D BOXING COACH, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa ‘clips’ za michezo ya nyota wa Dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa Dunia akiwemo Manny Pacquio,Juan Emanuel Marquez, Floyd Maywether, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo zina.  michezo
ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha mkongwe Habibi Kinyogoli.”katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na CD nyingine tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundition ” alisema.
 Super D ambae ni kocha wa timu ya ngumi ya Ashanti pamoja na timu ya mkoa wa Ilala kimichezo alisema anamini kupitia njia  hii watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo.   
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado wanaitajika vijana wenye vipaji kujitokeza kuja kushiriki katika mazoezi ya ngumi ili wajiunge na wenzao wa
timu ya Ashanti na Amana kujifunza ‘live’ chini ya makocha Habibu Kinyogoli, Kondo Nassoro, na yeye mwenyewe Super D na wengine wanaowanoa vijana

Saturday, February 9, 2013

Ramadhani Shauri kuwania taji la Dunia

Ramadhani Shauri


BINGWA wa Afrika anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Ngumi za Kulipwa la IBF, Ramadhani Shauri ameteuliwa kuwania ubingwa wa vijana wa dunia wa IBF.
Kwa mujibu wa taarifa ya IBF/USBA, inasema kuwa bingwa huyo wa uzito wa Feather atawania taji hilo la dunia katika uzito wa light kwa vijana chini ya umri wa miaka 25.
Shauri alitwaa taji hilo la Afrika kwa kumchapa Mganda, Sunday Kizito katika pambano laio lililofanyika mwishoni mwa mwaka jana jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo ya IBF/USBA iliyotolewa na rais wa shirikisho hilo, Onesmo Ngowi ni kwamba hiyo ni fursa nzuri kwa Mtanzania huyo kuweza kujitangaza kimataifa iwapo atafanikiwa kutwaa taji hilo la dunia la vijana.
Inaelezwa IBF iliamua kumpatia Shauri nafasi ya kugombea ubingwa huo wa vijana baada ya kuangalia mkanda wa video wa pambano lake la ubingwa wa Afrika na kuridhika kuwa anaweza kushindania ubingwa huo wa vijana,
Mabondia wengi wa Marekani waliokuja kuwa mabingwa wa dunia na kuweza kupata pesa nyingi walianza kuwa mabingwa wa dunia kwa vijana hivyo kuweza kupanda chati kwenye viwango vya IBF.
Mifano wa mabondia hao ni akina Bernard Hopkins, Floyd Maywealther na Oscar De la Hoya.
Iwapo Shauri atashinda na kuwa bingwa wa dunia upande wa vijana atakuwa kwenye macho ya mapromota wakubwa duniani kama kina Don King, Bob Arum na wengine wengi.
Pia itakuwa ni mara ya kwanza kwa historia ya ngumi nchini kwa Mtanzania kutwaa taji kubwa kati ya manne duniani ya IBF, WBA, WBO na WBC.
Kadhalika inaeleza kushinda kwa Mtanzania huyo kutatoa fursa kwa nchi ya anzania kujitangaza kibiashara na utalii duniani.

Kikosi cha Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu, Simba

SIMBA, OLJORO HAPATOSHI LEO ARUSHA, AZAM ZAMU YAO KESHO


LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 16 leo kwa mechi kadhaa ambapo jijini Arusha, mabingwa watetezi Simba itavaana na wenyeji wao JKT Oljoro.
Mechi hiyo namba 129 itafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, huku Simba ikiingia na kumbukumbu ya sare katika mechi yake iliyopita dhidi ya JKT Ruvu wakati wenyeji wao wakiwa wameshinda 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Simba italazimika kupata ushindi ili kufufua mbio zao za kuwania taji hilo kwa mara ya pili mfululizo ambalo linawindwa na timu za Yanga iliyopo kileleni na Azam wanaoshika nafasi ya pili ambao kesho watakuwa wageni wa Mtibwa Sugar mjini Manungu, Morogoro.

Mechi nyingine zinazochezwa leo Jumamosi ni pamoja na kivumbi kitakachowaka uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, wakati wenyeji  Kagera Sugar na Mgambo Shooting zitaonyeshana kazi katika pambano litakaloamuliwa na mwamuzi Amon Paul kutoka Musoma, Mara.
Toto Africans baada ya kufanya vibaya katika mechi tatu zilizopita ugenini imerejea nyumbaji jijini Mwanza itakapoumana na Coastal Union ya Tanga katika mchezo utaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Mchezaji wa kimataifa wa Coastal Union kutoka Brazil, Gabriel  Barbosa

Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor BinSlum, aliweka wazi kwamba huenda mchezaji wao wa kimataifa kutoka Brazil, Gabriel Barbosa, ambaye ITC yake imeshapatikana atashuka dimbani katika pambano hilo.
Mchezaji huyo alikwama karibu duru zima la msimu huu kuichezea Coastal kwa kukosa hati hiyo, lakini Binslum kaithibitishia MICHARAZO kwamba kila kitu sasa kipo shwari na wapo tayari kumtumia mchezaji wao huyo.
Mwamuzi Simon Mberwa kutoka mkoani Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya wenyeji Tanzania Prisons na African Lyon ambayo imepata huduma za kocha mpya Salum Bausi kutoka Zanzibar. Hiyo itakuwa mechi ya kwanza kwa Bausi kuiongoza timu katika VPL.
Maofisa wengine wa mechi hiyo ni mwamuzi msaidizi namba moja Abdallah Rashid, mwamuzi msaidizi namba mbili Abdallah Mkomwa wote kutoka Pwani wakati mwamuzi wa mezani ni John Kanyenye wa Mbeya. Kamishna wa mechi hiyo ni Rashid Rwena kutoka Ruvuma.
Mechi kati ya Mtibwa Sugar na Azam iliyokuwa ichezwe kesho imesogezwa mbele kwa siku moja ambapo sasa itafanyika Jumapili katika Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro.

Kikosi cha Azam




SIMBA, OLJORO HAPATOSHI LEO ARUSHA, AZAM ZAMU YAO KESHO


LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 16 leo kwa mechi kadhaa ambapo jijini Arusha, mabingwa watetezi Simba itavaana na wenyeji wao JKT Oljoro.
Mechi hiyo namba 129 itafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, huku Simba ikiingia na kumbukumbu ya sare katika mechi yake iliyopita dhidi ya JKT Ruvu wakati wenyeji wao wakiwa wameshinda 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Simba italazimika kupata ushindi ili kufufua mbio zao za kuwania taji hilo kwa mara ya pili mfululizo ambalo linawindwa na timu za Yanga iliyopo kileleni na Azam wanaoshika nafasi ya pili ambao kesho watakuwa wageni wa Mtibwa Sugar mjini Manungu, Morogoro.

Mechi nyingine zinazochezwa leo Jumamosi ni pamoja na kivumbi kitakachowaka uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, wakati wenyeji  Kagera Sugar na Mgambo Shooting zitaonyeshana kazi katika pambano litakaloamuliwa na mwamuzi Amon Paul kutoka Musoma, Mara.
Toto Africans baada ya kufanya vibaya katika mechi tatu zilizopita ugenini imerejea nyumbaji jijini Mwanza itakapoumana na Coastal Union ya Tanga katika mchezo utaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor BinSlum, aliweka wazi kwamba huenda mchezaji wao wa kimataifa kutoka Brazil, Gabriel Barbosa, ambaye ITC yake imeshapatikana atashuka dimbani katika pambano hilo.
Mchezaji huyo alikwama karibu duru zima la msimu huu kuichezea Coastal kwa kukosa hati hiyo, lakini Binslum kaithibitishia MICHARAZO kwamba kila kitu sasa kipo shwari na wapo tayari kumtumia mchezaji wao huyo.
Mwamuzi Simon Mberwa kutoka mkoani Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya wenyeji Tanzania Prisons na African Lyon ambayo imepata huduma za kocha mpya Salum Bausi kutoka Zanzibar. Hiyo itakuwa mechi ya kwanza kwa Bausi kuiongoza timu katika VPL.
Maofisa wengine wa mechi hiyo ni mwamuzi msaidizi namba moja Abdallah Rashid, mwamuzi msaidizi namba mbili Abdallah Mkomwa wote kutoka Pwani wakati mwamuzi wa mezani ni John Kanyenye wa Mbeya. Kamishna wa mechi hiyo ni Rashid Rwena kutoka Ruvuma.
Mechi kati ya Mtibwa Sugar na Azam iliyokuwa ichezwe kesho imesogezwa mbele kwa siku moja ambapo sasa itafanyika Jumapili katika Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro.

Kikosi cha Azam

Polisi Tabora wajipa moyo

Mwinyimadi Tambaza (aliyesimama)


LICHA ya kuanza vibaya mechi za Ligi Daraja la Kwanza kwa kupokea kipigo cha bao 1-0 toka kwa Rhino Rangers, Kocha Mkuu wa timu ya Polisi Tabora, Mwinyimadi Tambaza ametamba hajakatishwa tamaa katika mikakati yake ya kuinusuru timu hiyo.
Kocha huyo alinyakuliwa na Polisi Tabora hivi karibuni kwa ajili ya duru la pili la ligi hiyo iliyoanza wiki iliyopita na kuisaidia kuiongoza kufanya vema katika mechi zao za kirafiki ikiwemo kuibana Kagera Sugar na kuzinyuka timu za Tabora Combain na Reli.
Hata hivyo katika mechi yake ya kwanza walilazwa na Rhino na juzi alitarajiwa kuiongoza tena katika pambano lao la pili dhidi ya Polisi Dodoma mechi linalotarajiwa kupigwa uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.
Tambaza alisema licha ya kwamba kipigo hicho kimetibua mipango yao ya kuvuna pointi za kutosha katika duru hilo, lakini bado wanaamini Polisi Tabora itasalia ligi hiyo kwa kushinda mechi zinazofuatia mbele yao.
"Hatujakatishwa tamaa na kipigo cha Rhino, ilitokea kama bahati mbaya kutokana na vijana wangu kujisahau lakini tumejipanga kufanya vema kwa mechi zetu zijazo, naomba mashabiki wa Polisi Tabora wasikate tamaa kwani kazi ndiyo kwanza imeanza," alisema.
Kocha huyo alisema wamerekebisha makosa yaliyowaponza mbele yua Rhino na kwamba wamepania kuanzia mechi yao ya leo kutopoteza pointi yoyote ili wamalize duru hilo katika nafasi nzuri hata kama hawatapanda Ligi Kuu msimu ujao.

Sikinde yapeleka Jinamizi lake Sauti za Busara

Waimbaji wa Mlimani Park, Hassan Kunyata, Abdallah Hemba na Hassan Bichuka wakiwajibika

BENDI kongwe ya muziki wa dansi, Mlimani Park 'Sikinde' inatarajiwa kuondoka jijini Dar keshokutwa kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kushiriki tamasha la kimataifa la muziki la Sauti za Busara litakalofanyika visiwani humo kuanzia Alhamisi.
Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo aliiambia MICHARAZO kuwa, bendi yao ni miongoni mwa makundi ya muziki na wasanii walioalikwa kushiriki tamasha hilo linalofanyika kila mwaka visiwani Zanzibar.
Alisema bendi yao imejiandaa kwenda kutoa burudani kabambe sambamba na kujitangaza kupoitia tamasha hilo ambalo hushirikisha wasanii na makundi ya muziki kutoka nchi mbalimbali za Kiafrika.
"Bendi yetu imeteuliwa kushiriki tamasha la kimataifa la muziki la Sauti za Busara na tunatarajiwa kuondoka Jumanne kuelekea Zanzibar tukiwa tumekamilika na kutaka kuwaonyesha makundi mengine kwamba sisi ndiyo Mabingwa wa dansi," alisema.
Sikinde itaungana na wasanii wengine wa Tanzania katika tamasha hilo litakalofanyikia eneo la Ngome Kongwe, akiwamo Peter Msechu, Msafiri Zawose & Sauti Band, Super Maya Baikoko, Lumumba Theatre Group na Culture Musical Club.
Makundi mengine yatakayoshiriki tamasha hilo litakalomalizika Februari 17 ni Cheikh Lo (Senegal), Khaira Arby (Mali), Comrade Fatso na Chabvondoka (Zimbabwe), Atongo Zimba (Ghana), N'Faly Kouyaté (Guinea), Nathalie Natiembe (Reunion), Nawal & Les Femmes de la Lune na (Comoros/Mayotte).
Pia wamo Wazimbo (Msumbiji), The Moreira Project (Msumbiji/Afrika Kusini), Owiny Sigoma Band (Kenya/UK), Mokoomba (Zimbabwe), Mani Martin (Rwanda), Burkina Electric (Burkina Faso/USA) na Sousou & Maher Cissoko (Senegal/Sweden).
Kwa mujibu wa waandaaji wa tamasha hilo pia litajumuisha filamu za muziki wa Kiafrika, kumbukumbu, video za muziki na maonesho ya moja kwa moja, yote yakilenga kukuza utajiri na utofauti wa muziki wa Kiafrika.

Sadikina kuuza sura mara mbili



Msanii Sadikina Mussa 'Vicky'



MUIGIZAJI wa filamu anayekuja juu nchini, Sadikina Mussa 'Vicky' anatarajiwa kuuza sura katika filamu mbili tofauti za 'Hiari Yangu' na 'My Heart'.
Akizungumza na MICHARAZO, Sadikina alisema filamu hizo zilizowashirikisha wasanii mbalimbali wakiwemo nyota zimeshakamilika na zitaingizwa sokoni hivi karibuni.
Mwanadada huyo, alisema filamu zote zinahusisha masuala ya mapenzi lakini katika mitazamo tofauti na kwamba amezitendea haki kutokana na kiu aliyonayo ya kujitangaza zaidi.
Alisema katika filamu ya Hiari Yangu amecheza kama nyumba ndogo ya Kobra ambaye ndiye mhusika mkuu bila kujua kama ni mume wa shoga yake kipenzi na kuibua ugomvi uliosababisha uhasama baina yake na shogaye huyo.
"Ni moja ya kazi murua, inasisimua na ipo katika kiwango cha hali juu kama ilivyo 'My Heart'," alisema Sadikina shabiki mkubwa wa Yanga na Manchester United.


Sadikina Mussa 'Vicky'



























Baby Madaha afyatua mpya akijiandaa kwenda kuwania tuzo Nigeria



Baby Madaha katika pozi

WAKATI filamu yake ya 'Ray of Hope' ikiteuliwa kwenda kuwania tuzo ya kimaataifa za African Magic nchini Nigeria, msanii nyota nchini wa filamu na muziki, Baby Madaha anajiandaa kupakua filamu mpya   iitwayo 'Tatakoa'.
Akizungumza na MICHARAZO, Madaha alisema filamu hiyo imekamilika na ipo katika hatua za kuingizwa sokoni ikiwa imeshirikiana na wasanii kadhaa nyota nchini akiwamo Jumanne Kihangale 'Mr Tues'.
Madaha aliwataja wasanii wengine walioshiriki filamu hiyo inayozungumzia masuala ya mapenzi, uchawi na mauaji ni Salma Jabu 'Nisha', Frola Mvungi, Mariam Mndeme na wengineo.
"'Tatakoa' ni filamu ya aina yake imesheheni uchawi, mapenzi na mauaji ndani yake, yaani nimekuja kama Angelina Jolie," Baby Madaha alitamba.
Alisema wakati filamu hiyo ikiwa njiani, kazi yake iliyonyakua tuzo za ZIFF-2012 ya 'Ray of Hope' imeteuliwa kuwania tuzo za filamu za kimataifa za African Magic ambazo zitafanyika mwezi ujao nchini Nigeria.
Madaha alisema amefurahi kuona filamu hiyo ikiziangusha nyingine za wasanii wakongwe nchini na Afrika Mashariki katika mchujo wa kupenya kuwania tuzo hizo maarufu Afrika na duniani kwa ujumla.
Msanii alisema kwa sasa anajiandaa kwa ajili ya safari hiyo ya kwenda Nigeria, akiwaomba Watanzania wamuombee aweze kuibuka kidedea katika tuzo hizo.

Baby Madaha katika pozi jingine matata

Warembo wa Utalii 'kutalii' mikoa sita

Baadhi ya warembo wa Miss Utalii Tanzania wakiwa katika pozi

Warembo wa Miss Utalii Tanzania katika pozi

WAREMBO wanaojiandaa na kinyang'anyiro cha Miss Utalii Tanzania, wanatarajiwa kuanza ziara ndefu ya kutalii katika Hifadhi na vivutio vingine vya utalii katika miji mitano tofauti.
Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo 'Chipps' alisema warembo hao wanaanza ziara hiyo wiki ijayo kwa kuitembelea mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Pwani na Mtwara.
Chipungahelo alisema warembo hao watatalii na kujifunza mambo mbalimbali kabla ya kinyang'anyiro chao katika hifadhi za taifa za Mikumi, Udzungwa, Saadan na Selous, pia wakitembele vivutio vya kitalii kama maeneo ya kihistoria ya Bagamoyo, Amboni, Kijiji cha Makumbusho, Makumbusho ya Taifa na Pugu Sekondari.
"Pia watatembelea maeneo ya fukwe ya Kigamboni, Soko la Kimataifa la Magogoni, Uwanja wa Taifa,  Uwanja wa Ndege wa J.K.Nyerere, Soko la Kariakoo, mashule kadhaa za Sekondari na Msingi na kutembelea Manispaa zote za mkoa wa Dar es Salaam kukutana na viongozi wakuu wa wilaya, mikoa na wabunge wake," alisema.
Warembo hao wanatarajiwa kuchuana katika shindano la kusaka kisura wa mwaka 2012-2013 litakalofanyika jijini Dar es Salam mwishoni mwa mwezi huu.