STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 15, 2013

Ngumi kuipamba Ghana Mei 3


Nchi ya Ghana ambayo ni moja ya nchi zenye vipaji vingi vya wanamichezo mahiri na majina makubwa hususan mchezo wa ngumi, itawaka moto tarehe 3, Mei wakati mabondia mahiri sita watakapogombania mataji ya IBF katika ubingwa mbalimbali.

Bondia atakayeanza kupanda ulingoni kufukisha moto huo ni “Mtoto wa Kijiweni” Albert Mensah ambaye amejizolea sifa kemkem za kupambana na mabondia mahiri duniani. Mensah yuko kwenye viwango vya IBF vya dunia na amewekwa namba 7 kwa ubora duniani katika uzito wa Welter.
 
                 Helen Joseph
Mbabe huyu atakumbana na bondia mwenye maringo na “Mtoto wa Mjini” Ben Odamettey ambaye amekulia katika viunga vya Jamestown katika kata ya Bukom jijini Accra, ambayo ni maarufu kwa kutoa mabingwa wengi wa dunia kama kina Azumah Nelson, Ike Quartey, Joseph Agbeko na Poison Kotey. Wawili hawa watapambana kugombania ubingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa Junior Middleweight.
               Marriana Gulyas (kushoto)
 
Mpambano wa pili na unaongojewa kwa hamu kubwa ni ule wa mwanadada na mrembo kutoka Nigeria ambaye anaishi nchini Ghaba, Helen Joseph atakapombana na binti Mfalme kutoka Himaya ya Austrohungrian (Hungary) bi. Marianna Gulyas. Warembo hawa wanagombania mkanda wa IBF wa Mabara wa wanawake katika uzito wa unyoya (Featherweight) na moto mkubwa unategemewa kuwaka kutokana na umahiri wa warembo hawa wa kurusha makonde ulingoni.

Helen atakuwa anarudisha heshina yake baada ya kupoteza pambano la ubingwa wa dunia kwa mwanadada Dahianna Santana wa Dominican Republic mwezi wa Desemba mwaka jana. Hii ni heshima pekee kwa kina mama kutoka bara la Afrika wa kuonyesha umahiri wao kwa binti huyo wa Kifalme kutoka Hungary.
 
                                                          Albert Mensah (kulia)
Ndipo litakapokuja pambano la kukata na shoka kati ya mbabe kijana anayeinukia katika ulimwengu wa masumbwi nchini Ghaha na Afrika kwa ujumla bondia Issa Samir kutoka Ghana atakapopambana na mbabe kutoka kwenye jangwa la barafu la Siberia, bondia Robison Omsarashvili kutoka katika nchi ya Georgia ambayo ni moja ya nchi zilizokuwa kwenye Muungano wa Kishoshalisti wa Sovieti ya Urusi (USSR).

Ni nderemo na vifijo kwa Waghana na watu wote wa Afrika wakati mabondia hawa watakapo pambana kugombea mataji haya makubwa kabisa ya IBF na kuliwakilisha bara la Afrika katika ramani ya dunia.

Mapambano haya yanaandaliwa na kampuni ya GoldenMike Boxing Syndicate ya Accra, Ghana chini ya Henry Many-Spain na Michael Tetteh na yatafanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Accra (Accra International Conference Center) na yatasimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi.

Simba, Azam wafunika mapto ya Yanga Oljoro




Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 66,855,000 kutokana na watazamaji 11,458.
 Kiwnago hicho ni kikubwa kuliko pambano lililochezwa Jumamosi kati ya Yanga na JKT Oljoro ambapo mchezo huo uliingiza kiasi cha Sh Milioni 63.
Kwa pambano la jana, viingilio katika mechi hiyo namba 155 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,587,177.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,198,220.34.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,925,683.45, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 4,755,410.07, Kamati ya Ligi sh. 4,755,410.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,377,705.03 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,849,326.14.
Katika pambano la Yanga na Oljoro jumla ya Watazamaji 11,021 walikata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Oljoro JKT iliyochezwa juzi (Aprili 13 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuingiza sh. 63,170,000.

Viingilio katika mechi hiyo namba 156 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,853,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,636,101.69.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,552,501.25, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,531,500.75, Kamati ya Ligi sh. 4,531,500.75, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,265,750.37 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,762,250.29.


Sunday, April 14, 2013

Man City yainyoa Chelsea na kuifuata Wigan fainali FA Cup

Kun Aguero aliyeifungia Man City bao la pili

Vincent Kampany akichuana na Torres

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City muda mfupi uliopita imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la FA baada ya kuinyuka Chelsea kwa mabao 2-1 na kuifuata Wigan Athletic iliyotangulia katika hatua hiyoi tangu jana.
Chelsea ilijikuta ikienda mapumziko katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Londoni ikiwa nyuma kwa bao 1-0, lililofungwa na Samir Nasir katika dakika ya 35.
Sergio kun Aguero aliiandikia Manchester City bao la pili dakika mbili baada ya kuanza kipindi cha pili na kuifanya timu yake katika mchezo huo wa nusu fainali kucheza kwa kujiamini zaidi.
Demba Ba, alifutia machozi Chelsea kwa kutumbukiza bao pekee ambalo halikuwasaidia kitu katika dakika ya 66 na kufanya hjadi dakika ya mwisho Manchester City kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na hivyo kusubiri pambano la fainali dhidi yake na Wigan iliyoing'oa Milwall jana kwa mabao 2-0.

SIMBA, AZAM HAKUNA MBABE, YANGA YAPUMUA KILELENI

 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akichuana na beki wa Azam FC, John David katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilifunga mabao 2-2 (Picha na Habari Mseto Blog)  
 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akimtoka beki wa Azam FC, Joockins Atudo wakati wa mchezo wa Ligi Kuu  Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
 Wachezaji wa Simba wakishangilia baada ya kuapata bao la pili.
Kiungo wa timu ya Simba, Abdallah Seseme akiwatoka wachezaji wa Azam FC, Himid Mao (kulia) na Salum Abubakar wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2.

LICHA ya tambo nyingi kabla ya pambano lao timu za Simba na Azam jioni ya leo zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na kuwafanya vinawa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga kupumua.
Yanga mabo mashabiki wake leo walionyesha kioja kwa kuwashangilia watani zao Simba dhidi ya Azam, wanapumua kwa vile Azam inayowafukuza kwenye mbio za ubingwa imepunguza pengo la pointi moja tu na kuipa nafasi Yanga kuhitaji pointi tano tu kati ya mechi zake nne zilizosalia kutangaza ubingwa msimu huu.
Yanga yenyewe ina pointi 52 wakati Azam waliopo nafasi ya pili wana pointi 47, huku kjwa sare hiyo ya leo Simba imeendelea kusalia kwenye nafasi ya nne akiwa na pointi 36.
Ramadhani Singano 'Messi' ndiye aliyeipa Simba uongozi wa mabao katika pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Oden Mbaga kwa kufunga mabao mawili katika dakika ya 10 na 14 akimalizia kazi murua iliyofanywa kwa ushirikiano wa Mrisho Ngassa na Haruna Changono.
Dakika ya 29 Kipre Tchetche aliifungia Azam bao la kwanza baada ya Khamis Mcha kuangushwa akielekea kumsalimia kipa Abel Dhaira na kumfanya afikishe bao la 15 msimu huu.
Dakika mbili baadaye kocha wa Azam, Stewart Hall alionyeshwa kadi nyekundu kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi kutokana na maamuzi yake na hadi mapumziko matokeo yalikuwa mabo 2-1.
Kipindi cha pili Azam walionyesha uhai zaidi kwa kushambulia lango la Simba na kufanikiwa kupata bao la pili na la kusawazisha dakika ya 72 kupitia kwa Humphrey Mieno.
Kwa matokeo ya pambano hilo lililokuwa likisubiriwa kwa hamu kutokana na tambo zilizokuwa zikitolewa na pande zote mbili na mkasa ulioibuka baada ya mechi yao ya kwanza ambapo Simba walishinda mabao 3-1 na kupelekea Azam kusimamisha wachezaji wake wanne kwa tuhuma za rushwa, msimamo upo hivi;


                                       P     W     D     L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans       22    16     4     2    40    12    28    52
    2. Azam                      23    14     5     4    41    19    22    47    
    3 . Kagera Sugar         22    10     7     5    25    18    7      37     
    4.  Simba                     22     9     9     4     32    21    11    36
    5.  Mtibwa Sugar         23     8     9     6     26    24     2     33   
    6. Coastal Union          22     8     8     6     23    20     3     32    
    7.  Ruvu Shooting         23     8     6     9     21    22    -1    30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27    -5    28     
    9. Tanzania Prisons       24     6     8    10    14     21    -7    26    
    10.JKT Mgambo         22     7     3     12    14     22    -8    24
    11.Ruvu Stars              21     6     4     11     19     34   -15   22
    12. Toto Africans         24     4    10    10     22     32   -10   22
    13. Polisi Morogoro     23     3    10    10     11     21    -10  19    
    14.  African Lyon         23     5     4     14     16     35    -19  19

WAWILI WAFA KATIKA AJALI KAGERA


 

Magari yaliyohusika na ajali hiyo iliyotokea jana jioni huko Ngara, Kagera

Watu wawili wamefariki dunia  papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mercedec benz lenye namba ya usajili T 908 ABZ semitrailer lililokuwa ikitokea nchini Burundi, kuacha njia leo(April 13,2013) muda wa saa 12 jioni na kupinduka katika eneo la Kumuyange nje kidogo ya mji wa Ngara mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi wilaya ya Ngara  Abel Mtagwa amewataja watu hao waliofarki katika ajali hiyo kuwa ni Edward Filimon alie kuwa akiendesha pikipiki yake yenye namba za usajiri T 756 BZJ na abiria wake ambae hadi sasa haja fahamika jina lake.
Kamanda Mtagwa amewataja majeruhi wa ajari hiyo kuwa ni Dereva wa gari hilo Hajji Omary Ibrahim(29) mkazi wa gongolamboto jijini Dar es salaam na tingo wake aliyejulikana kwa jina la Kambi simba(40).
Kamanda Mtagwa ameongeza kuwa katika ajal i hiyo nyumba moja mali ya Bi.Bibiana John (58) imegongwa na gari hilo na kuharibika.
Aidha Kamanda Mtagwa amesema kuwa chanzo cha ajari hiyo ni  gari hilo kufeli  mfumo wa Breki  jambo ambalo Dereva wake alishindwa kulimudu kuliendesha ndipo lilipanda mtaro na kubomoa nyumba hiyo. 
 
Aidha Majeruhi wa Ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
 
CHANZO:MWANA AFRIKA

Simba, Azam. ni vita ya kisasi leo taifa

Simba

Azam

SIMBA na Azam jioni ya leo wanatarajiwa kushuka dimbani kumenyana katika pambano pekee la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoelekea ukingoni huku, ambalo limetabiriwa na wengi kama vita ya kisasi baina ya timu hizo.
Timu hizo zitakutana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kila moja ikiwa na malengo tofauti, Azam kulipa kisasi ya kipigo cha mabao 3-1 ilichopewa kwenye pambano lao la kwanza lililosababisha iwasimamishe wachezaji wake wanne kwa tuhuma za kuihujumu kupitia rushwa.
Simba wenyewe wakaikabilia Azam wakiwa na hasira za kutuhumia na rushwa sakata ambalo lilimalizwa nna Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kabla ya kuibuka ikitaka kulipwa fidia ya Bilioni 1 kwa tuhuma hizo nzzito.
Pia Simba inashuka uwanja wa Taifa ikiwa inataka kulinda heshima yake katika ligi ya msimu huu kutokana nna ukweli imeshatemeshwa ubingwa na ipo hatua chachee kukosa hata nafasi ya uwakilishi wa nchi katika michuano ya Kimataifa mwakani.
Tayari kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' ametamka wazi kwamba wanashuka dimbani leo kwa lengo moja tu la kutaka kulinda heshima yao mbele ya Azam na pia kuhakikisha wanamaliza ligi wakiwa katika nafasi nzuri baada ya kutemeshwa taji.
Azam mbali na kuhitaji kulipa kisasi kwa Simba ikiamini kwamba mechi ya kwanza walifungwa kwa hila, lakini pia inasaka ushindi ili kuifukuzia Yanga kileleni ambayo jana ilitakata kwa kupata ushindi wa mabao 3-0 mbele ya maafande wa JKT Oljoro na kuzidi kujichimbia kwenye nafasi ya kwanza.
Yanga mbali na kuendelea kuongoza na kuongeza pendo la pointi dhidi yake na Azam, pia imejihakikisha nafasi ya kushiriki michuano ya Afrika mwakani mpaka sasa kati ya nafasi mbili za uwakilishi wa nchi.
Kwa kuangalia mazingira hayo, huku Azam wakijinafasi kwamba kiu yao ni kutwaa ubingwa msimu huu na kuweka rekodi, ni wazi pambano la jioni litakuwa ni patashika nguo kuchanika.
Wachezaji wanne waliohusishwa na tuhuma za rushwa baada ya pambano hilo la duru la kwanza, nahodha wa zamani Aggrey Morris, Said Morad, Erasto Nyoni na kipa Deo Munishi 'Dida' tayari wameripoti kambini katika kikosi cha timu hiyo wakielezwa wanaweza kushuka dimbani leo kuwakabili 'Mnyama'.
Hata hivyo kwa mazingira yalivyo huenda ikawa vigumu kwa wachezaji hao kucheza pambano hilo ikizingatiwa kwamba ni Simba hao hao waliowaponza hata kuingia matatani kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Mashabiki wa soka watakuwa na hamu kubwa ya kuona kipi kitakachotokea katika mechi hiyo baada ya dakika 90 huku macho na masikio yakielekezwa kwa washambuliaji nyota wa Azam, Kipre Tchetche na John Bocco 'Adebayor'.
Tchetche anaangaliwa kutokana na kasi yake ya ufungaji mabao akifunga karibu kila mechi tangu arejee dimbani katika duru la pili, huku Adebayor kwa bahati yake ya kuitungia Simba kila timu hizo zinapokutana.
Bila shaka kujua nani atakayecheza ua kulia leo taifa ni suala la kusubiri kuona baada ya dakika 90 za pambano hilo la kusisimua.

MIUJIZA:ABIRIA ZAIDI YA 100 WANUSURIKA KIFO AJALI YA NDEGE

































  
ZAIDI ya abiria 100 wamenusurika kimiujiza katika ajali ya ndege iliyoanguka muda mfupi baada ya kuruka hewani kando ya pwani ya bali, nchini Indonesia.
Mashuhuda wa tukio hilo lililoikumba ndege ya Lion Jet iliyoanguka ikitoka kuruka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Ngurah Rai nje kidogo ya mji wa Denparsar walisema walisema manusura wa ajali hiyo walionekana kuhamanika wakati wakiokolewa kutoka kwenye ndege hiyo iliyozama baharini kwa futi kadhaa.
Inaelezwa ndege hiyo ilikuwa imebebea jumla ya abiria 101 na watumishi wapatao saba wakati ikianguka majini kutoka umbalio wa Mita 50 juu.

Saturday, April 13, 2013

Prisons yazidi kukimbia janga la kushuka daraja


MAAFANDE wa Prisons Mbeya wamezidi kupigana kuepa janga la kushuka daraja baada ya kuinyoa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika pambano lililochezwa jioni ya leo mjini Mbeya.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo baada ya Jumatano iliyopita kuicharaza Mgambo JKT, ulipatikana kwenye uwanja wa Sokoine na kuifanya Prisons kuchupa kwa nafasi moja toka nafasi ya 10 haid ya 9.
Hata hivyo bado Prisons ina kibarua cha kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia dhidi ya JKT Ruvu na Kagera Sugar kujihakikishia kusalia Ligi Kuu msimu ujao.
Habari kutoka Mbeya zinasema kuwa Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania walipata ushindi huo kwa magoli ya kipindi cha pili yaliyowekwa yote kimiani na mchezaji wake aliyekuw shujaa leo, Elias Maguli.Maguli alifunga bao la kwanza kwa shuti akiunganisha pasi murua ya mchezaji mwenzake katika dakika ya 53 kabla ya kuongeza jingine dakika tano baadaye kwa mkwaju wa penati baada ya beki mmoja wa Ruvu kuunawa mpira langoni mwake.
Kwa matokleo hayop Prisons imefikisha pointi 26 na kuishuka Mgambo katika nafasi ya tisa na kukalia wao nafasi hiyo.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano kati ya Azam na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

 Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za leo jioni;

                                        P     W     D    L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans     22     16    4     2    40   12    +28     52
    2.  Azam                     22     14    4     4    39   17    +22     46    
    3.  Kagera Sugar         22     10    7     5    25   18    +7       37     
    4.  Simba                     21     9     8     4     30   19   +11      35
    5.  Mtibwa Sugar        23      8     9     6     26   24    +2      33   
    6. Coastal Union         22     8     8     6     23    20    +3      32    
    7.  Ruvu Shooting       23     8     6     9     21     22     -1     30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27     -5     28     
    9. Tanzania Prisons     24     6     8    10    14     21     -7     26    
   10.JKT Mgambo          22     7     3    12    14     22     -8     24
   11.Ruvu Stars              21     6     4     11    19     34     -15   22
   12. Toto Africans        24     4     10    10    22    32     -10    22
   13.  African Lyon       23     5      4     14    16     35     -19   19
   14. Polisi Morogoro    23     3     10    10    11     21     -10   19    
             

Yanga yaitemesha Simba ubingwa, yaikwangua JKT Oljoro 3-0

Vinara wa ligi kuu Yanga walioivua Simba taji jioni ya leo
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeendelea kudhihirisha wamepania kutwaa taji la msimu huu baada ya jioni hii kuikwangua JKT Oljoro ya Arusha mabao 3-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo uliopatikana kwa mabao ya kipindi cha kwanza yameifanya Yanga kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 52 na kuivua rasmi Simba ubingwa kutokana na kufikisha pointi 52 ambazo haziwezi kufikiwa na Wana Msimbazi.
Simba ambayo itashula kesho dimbani kuumana na Azam yenyewe ina pointi 35 na kama itashinda mechi zake zote itafikisha pointi 50 tu.
Mabao yalioifanya Yanga kulishika taji la ubingwa kwa mkono mmoja na kusubiri mwingine iwapo Azam wanaowafukuzia watateleza katika mechi zake yaliwekwa kimiani na beki Nadir Haroub 'Cannavaro' katika dakika ya 5 tu ya mchezo kabla ya Simon Msuva kufunga la pili dakika ya 19 na Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza la tatu dakika mbili kabla ya mapumziko.
Pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Amon Paul wa Mara lilihuhudia kadi kadhaa za njano zikitolewa kwenye mchezo huo na mpaka dakika 90 zinamalizika Yanga walikuwa wababe mbele ya maafande hao kwa ushindi huo wa mabao 3-0.

Supersport yakwama kurusha live mechi za VPL

PRESS RELEASE



Na Boniface Wambura
MECHI tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.

Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.

ZA LEO LEO

Friday, April 12, 2013

Ni vita vya Barca na Bavarian, Chelsea waangukia kwa Basel


MABINGWA wapya wa Ujerumani, Bayern Munich imeangukia mikononi mwa Barcelona katika mechi za hatua na Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku wapinzani wao Borussia Dortmund wakipangiwa Real Madrid.
Aidha Chelsea ya Uingereza timu pekee inayoiwakilisha Uingereza imepangwa kukwaruzana na Basel ya Uswiss katika mechi za Nusu Fainali ya UEFA Ndogo, huku Benfica ya Ureno na Fenarbeche ya Uturuki zikipangwa pamoja.
Kupangwa kwa droo hiyo iliyozitenganisha timu hasimu kutoka nchi moja inamaanisha kwamba fainali za mwaka huu ya Ligi ya Ulaya itazikutanisha timu za taifa moja baada ya kipindi kirefu.
Mechi za mkondo wa kwanza zinatarajiwa kucheza kati ya Aprili 23 na 24 na zile za marudiano zitachezwa Aprili 30 na Mei Mosi kabla ya fainali kupigwa uwanja wa Wembley Uingereza Mei 25.
Kwa mechi za UEFA Ndogo mkondo wa kwanza utaanza Aprili 25 na za mkondo wa pili Mei 2 kabla ya fainali Mei 15.
Barcelona watakuwa wageni wa wana fainali za mwaka jana katia mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana wiki moja baadaye kwenye dimba lake la Camp Nou, kadhalika Wahispania wengine Real Madrid watasafiri pia Ujerumani kuvaana na wenyeji wao Dortmund kabla ya kurejea nyumbani katika mechi ya mkondo wa pili.
Kwenye mechi za UEFA Ndogo Chelsea wataanzia ugenini sawa na itakavyokuwa kwa Benfica na kurudiana na wapinzani wao kwenye viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya Basel na Fenerbeche.

Kivumbi cha VPL kuendelea wikiendi, Simba, Yanga, Azam kuvuna nini?




Na Boniface Wambura
Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea kesho (Aprili 13 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Yanga itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa wakati Uwanja wa Sokoine utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons na Ruvu Shooting.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 14 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Simba. Mechi hiyo namba 155 itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Shelisheli kuchezesha mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam na AS FAR ya Morocco itakayofanyika Aprili 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao ni Emile Fred atakayepuliza filimbi akisaidiwa na Steve Maire na Jean Ernesta. Mwamuzi wa mezani (fourth official) atakuwa Jean Claude Labrossa. Kamishna wa mechi hiyo ni Abbas Sendyowa kutoka Uganda.

Wakati huo huo, CAF imemteua Mtanzania Alfred Lwiza kuwa Kamishna wa mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Liga Muculmana ya Msumbiji na Wydad Casablanca ya Morocco.

Mechi hiyo itakayochezwa kati ya Aprili 19,20 au 21 mwaka huu nchini Msumbiji itachezeshwa na waamuzi kutoka Zimbabwe wakiongozwa na Ruzive Ruzive.


UJUMBE WA FIFA KUWASILI APRILI 15




Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwatangazia wadau wa mpira wa miguu kuwa ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utawasili nchini Jumatatu (Aprili 15 mwaka huu) kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, ujumbe huo utaongozwa na Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro na utafanya kazi kwa siku tatu kuanzia siku ya ujio na kuondoka Aprili 18 mwaka huu.

Ukiwa nchini, ujumbe huo utakutana na wagombea uongozi walioathiriwa na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambao waliomba mashauri yao yaangaliwe upya, wagombea ambao walikata rufani FIFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya Rufani na Sekretarieti ya TFF.

Wajumbe hao wangependa kukutana na waziri anayehusika na michezo, hivyo TFF imeiandikia Wizara ikipendekeza kuwa ujumbe huo ukutane na Waziri na wakuu wengine wa michezo Aprili 16 mwaka huu 2013 kabla ya kuanza kazi zao.

Wagombea watakaosikilizwa na ujumbe huo wa FIFA ni:
1.   Farid Salim Mbaraka Nahdi: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.

2.   Elliud Peter Mvella: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kukata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kabla ya maombi yake ya kutaka shauri lake kuangaliwa upya, kukataliwa.


3.   Mbasha Matutu: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi na kukata rufani ambayo pia ilitupwa kabla ya kuomba shauri lake liangaliwe upya, ombi ambalo lilikataliwa.

4.   Hamad Yahya: Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.

5.   Jamal Emily Malinzi: Mgombea wa nafasi ya urais wa TFF ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kuondolewa kwenye mchakato. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini likakataliwa. Hata hivyo, alikuwa ameshakata rufani FIFA.

6.   Michael Wambura: Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. Hakuomba shauri lake liangaliwe upya, lakini alikata rufani FIFA.

Shirikisho linawaomba wote waliotajwa hapo juu kujiandaa kwa utetezi na maelezo ya kutosha na kwamba barua za kuwaita zinafuata. (Orodha ya waathiriwa na programu ya ujumbe wa FIFA imeambatanishwa)

Kigogo Yanga matatani, kisa...!

Makamui Mwenyekiti wa Yanga, Clement  Sanga
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Clement Sanga, anatarajiwa kufikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu kufuatia kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa timu yao inayoongoza kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwamba inahujumiwa na ndiyo maana mechi yao dhidi ya JKT Oljoro imesogezwa mbele na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Awali, mechi hiyo ya Yanga dhidi ya Oljoro ilipangwa kufanyika juzi (Jumatano ya Aprili 10) lakini sasa itachezwa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kuwa kauli kama za Sanga zinachangia kujenga chuki  zisizokuwa na sababu kati ya shirikisho hilo na mashabiki wa soka nchini.
Kwa sababu hiyo, Osiah alisema kuwa Sanga atatakiwa athibitishe ni kwa namna gani Yanga inahujumiwa baada ya kuwapo kwa mabadiliko hayo ya ratiba ambayo yalizihusu pia timu nyingine zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, zikiwamo za Simba na Azam ambazo sasa zitacheza Jumapili.
Osiah alisema kuwa anashangaa kusikia madai ya Sanga kuwa klabu hazijashirikishwa katika kufanya marekebisho hayo wakati ukweli ni kwamba klabu hizo ziliwakilishwa na viongozi wao walioko kwenye kamati ya ligi na timu yao ina mjumbe kwenye kamati hiyo.
Katibu huyo wa TFF alisema kuwa viongozi wa klabu walielezwa katika kikao kilichofanyika mapema kabla ya ligi kuanza kwamba kutakuwa na 'Super Week' katika hatua ya mwisho wa ligi ambayo itatekelezwa kupitia nafasi itakayopatikana katika kituo cha televisheni ya kulipia cha Afrika Kusini cha  Super Sport.
"Mnapotafuta wadhamini kuna wakati ni lazima mjitoe mhanga... na kuonekana kwetu kupitia Super Sport kumesaidia kuleta wadhamini wengi ambao tayari wamevutiwa na ligi yetu," alisema Osiah.
Katika mahojiano yake na vyombo vya habari hivi karibuni, Sanga alisema kuwa wao walikuwa tayari wameshaiandaa timu yao na kwa mabadiliko hayo ambayo hawaoni faida yake zaidi ya kuwapunguzia mashabiki viwanjani yamewapa hasara kubwa itokanayo na kuendelea kuiweka timu kambini.
Aliyewahi kuwa Afisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage waliwahi kuadhibiwa na TFF baada ya kukutwa na hatia ya kutoa kauli ambazo baadaye walishindwa kuzithibitisha.


Chanzo:NIPASHE

Matapeli wamhujumu rais wa IBF nchini

Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi
MATAPELI wa kimataifa wanaoingilia barua pepe na akaunti nyingine za watu mbalimbali wamemvamia rais wa hapa nchini wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF/USBA), Onesmo Ngowi na kutumia jina lake kwa nia ya kuwatapeli fedha watu mbalimbali anaojuana nao.
Jina la Ngowi ambaye pia ni Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, (TPBC), limetumiwa na matapeli hao kutuma ujumbe wa barua pepe kwa watu mbalimbali anaowasiliana nao, wahusika wakijifanya ni Ngowi na kuomba msaada wa fedha.
Katika barua pepe mojawapo iliyotumwa kwa mwandishi, inaeleza Ngowi alikuwa akiomba msaada wa Euro 2,950 (Sh. milioni 6.2) ili kumuwezesha kujinasua na tatizo lililomkumba akiwa nchini Ugiriki; jambo ambalo Ngowi amelilaani na kuwatahadharisha watu anaojuana nao kuwa wawe macho na matapeli hao.
"Matapeli wanatuma akaunti yangu (ya email) na kuomba pesa kwa watu mbalimbali... mimi siko Ugiriki na wala sijamuomba mtu fedha. Tafadhali naomba usijibu meseji hizo," alisema Ngowi kuelezea utapeli huo ambao umeshawakuta pia watu wengi.

TFF ipo tayari kukutana na Nsa Job utetezi wa Rushwa

Nsa Job (kulia)
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema liko tayari wakati wowote kukutana na mchezaji wa Coastal Union ya jijini Tanga, Nsa Job, ambaye alikiri hadharani kuwa aliwahi kupokea rushwa ya Sh.milioni mbili kutoka kwa kiongozi mmoja wa timu vigogo nchini ili asifunge magoli.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema katika barua yao waliyomuandikia mshambuliaji huyo hawakumpa siku maalumu lakini endapo nyota huyo atachelewa kujisalimisha atakumbushwa kabla ya kuchukuliwa hatua kupitia kamati husika.
"Tuliiweka wazi lakini tutamuandikia barua nyingine ya kumkumbusha na itakayofuata itakuwa imetoa muda fulani, ila tunaamini atatoa ushirikiano kama alivyokaririwa na gazeti (la NIPASHE)," alisema Katibu mkuu huyo.
Osiah alisema TFF inaamini mchezaji huyo atatoa ushirikiano kama alivyolieleza gazeti la NIPASHE lilipozungumza naye mapema wiki hii.
Aliongeza kwamba wanaamini akiwa wazi mhusika wa tuhuma hizo atajulikana na hatimaye adhabu itatolewa na kukomesha suala la rushwa katika soka la nchini.
Osiah alisema pia tayari Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo cha redio cha Clouds ameahidi kuwapa ushirikiano katika kupata nakala ya kipindi kilichorushwa mahojiano na Nsa ambacho kilifanyika Aprili 3 mwaka huu.
Nsa alizungumza katika mahojiano na kituo cha redio hiyo akisema aliwahi kupokea rushwa lakini aliifungia timu yake goli pekee la ushindi.
Hata hivyo, hadharani, hakuitaja timu aliyokuwa anaichezea wakati huo wala timu aliyoifunga na wala jina la kiongozi aliyemhonga, ambaye alisema alianza kumsumbua kudai fedha zake pale “alipowatungua”.
Nyota huyo ambaye kwa sasa anafanya mazoezi binafsi baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti nchini India aliwahi kuchezea timu za Simba, Yanga, Moro United, Azam, Villa Squad na sasa Coastal Union zote zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Nsa aliiambia NIPASHE kwamba atatoa ushirikiano kwa TFF kama alivyotakiwa na kwa sasa anajiandaa kwenda kukutana nao.
Alisema pia alipokea barua hiyo tangu wiki iliyopita na atafanya kila linalowezekana ili kutekeleza kile atakachoambiwa na wajumbe wa kamati hiyo.


CHANZO:NIPASHE.

Azam yamalizana na wachezaji wake iliyowasimamia kwa rushwa

 
Add caption



KLABU ya soka ya Azam ambayo Jumapili inatarajiwa kuvaana na Simba, imemalizana na wachezaji wake wanne iliyokuwa imewasimamisha kwa tuhuma za Rushwa kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa klabu ya Azam, imesema wachezaji wote wanne waliosimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi yao wameripoti kambini tayari kuikabili Simba SC siku ya jumapili

Kurejea kwa wachezaji hao kunamaliza mgogoro uliokuwepo na kudumu kwa takribani miezi mitano kufuatia shutuma za rushwa ambazo zilipelekwa takukuru kuchunguzwa ili kujua ukweli na uongozi wa Azam FC unaishukuru takukuru kwa kazi nzuri ambapo imegundulika kuwa wachezaji hao hawakuhusika na hivyo kusafishwa na chombo hicho chenye mamlaka ya kuchunguza tuhuma za rushwa.
Wachezaji hao wote wanatarajiwa kuwemo kwenye mchezo wa Jumapili dhidi ya Simba SC ikiwa mwalimu ataona inafaa na wapo katika hali nzuri kuweza kucheza.
Mchezo huo wa jumapili ni muhimu sana kwa Azam FC kwani ikishinda itaizidi Simba SC pointi 14 huku simba ikisaliwa na michezo minne na hivyo kumaanisha kuwa Kagera Sugar atabaki kuwa mpinzani pekee wa Azam FC katika kuwania nafasi ya pili.