STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 4, 2013

Cheki ajali ya lori la mafuta lililoanguka jana Mbalizi-Mbeya na watu walivyokuwa wakijizolea mafuta bila kuhofia kitu

 Lori lenye namba za usajili  T97 AJL lenye tela namba T746 BKF lilipo acha njia na kupinduka na kuziba njia

Lori  likishindwa kupita baada ya Mafuta kumwagika Barabarani na kusababisha barabara kushindwa kupitika
Magari yakipita kwa shida baada ya Lori kudondoka
Askari wakijitahidi kukabiliana na watu waliokuwa wanachota mafuta
Shughuli za uokoaji zikiendelea kulia ni Dereva wa Lori hilo baada ya kunusurika
Dereva wa gari hilo Hassan Abdi (35) akiwa haamini kilicho tokea baada ya Kunusurika kifo


YALE YALE!!! Wananchi  wenye ndooo Haya.... Wenye Madumu haya .... wenye Masefuria haya... wote walikuwepo kuchota Mafuta kama inavyo onekana ... bila kujali kama yaweza kulipuka 
Wananchi Mbalimbali wakiwa wanapata shida kupita baada ya Lori kudondoka

Askari wa zima moto wakiwa wanaendelea na Juhudi za kuondoa mafuta barabarani kwa maji 
Wananchi mbalimbali wakiwa wanaondoka na Mafuta... huku wengine wakiendelea kuchota
Wakina mama... Watoto... Vijana na wazee wakiwa wanapata shida jinsi ya kupita baada ya ajali

Kushoto ni Tingo Saimoni Msovela (23) na dereva wake Hassan Abdi wakijitahidi kuziba mafuta yasiendelee kuvuja
 
veta
Tingo wa Lori hilo la mafuta baada ya kuokolewa kutoka kwenye Gari.


Ezekiel Kamanga
WATU wawili wamenusurika kifo baada ya lori la mafuta lenye namba za usajili T 978 AJL lenye tela namba T 746 BKE Aina ya SCANIA walilokuwa wakisafiria kutoka DAR ES SALAAM kwenda ZAMBIA kuacha njia na kupinduka katika mteremko wa MBALIZI barabara MBEYA TUNDUMA.
Dereva ametambuliwa kwa jina la HASSAN ABDI 35 na msaidizi wake SAIMON SOVELA 23 ambao walikuwa wametokea DAR ES SALAAM kuelekea ZAMBIA likiwa limejaa shehena ya mafuta
Kwa mujibu wa Dereva amesema kuwa gari hilo ghafla lilipoanza kuteremka mteremko liliharibika mfumo wa breki na mbele yake kukiwa na magari matano baada ya kuona kuwa angesababisha maafa makubwa aliamua kulichepusha pembeni ndipo lilipoacha njia na kupinduka na kumwaga shehena ya mafuta.
Kikosi cha zimamoto kilifika eneo la tukio na kuhakikisha usalama wa eneo hilo kuhofia mlipuko wa moto ambao ungeweza kutokea kutokana na baadhi ya wananchi kuanza kuchota mafuta yaliyokuwa yanatiririka.
Pamoja na juhudi za Jeshi la Polisi kudhibiti wananchi kutochota mafuta lakini wananchi walikaidi na kuendelea kuchota mafuta.
Ajali hiyo ilisababisha adha kubwa kwa wasafiri waliokuwa wana pita barabara hiyo wakiwemo wagonjwa na waliokuwa wanawahi usafiri wa ndege majira ya saa saba mchana.

WABUNGE WACHAPANA NGUMI ZA KAVU KAVU BUNGENI


Uuuh aaaah!
PICHANI ni baadhi ya  wabunge wa Taiwan 'walivyokuwa wakiadabishana' jana baada ya kupishana lugha kufuatia mpango wa kupiga kura ya maoni iliyoazimia kuidhinisha umaliziwaji wa mradi wa nne wa Nyuklia katika kisiwa ambacho kinakaliwa na watu wapatao milioni 23. Wabunge wa Tanzania ambao wamekuwa wakichimbana mkwara bungeni...wakifikia huku sijui itakuwaje? 
Acha mshikaji mnaharibu! Ngoja nimfunze adabu
Kuja hapa weweee!

Bahanuzi, Javu waizamisha Mtibwa Sugar Taifa

 Beki wa Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe akichuana na mshambuliaji wa Yanga wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga imeshinda 3-1. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Beki wa Mtibwa Sugar, Ally Lundega akimiliki mpira huku akizongwa na mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
 Mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima akimtoka beki wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhan wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 


 Kikosi cha Mtgibwa Sugar.
Kikosi cha Yanga.
 Mashabiki wa Yanga waklifuatilia mtanange huo.

Young Africans leo imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wakata miwa kutoka Morogoro timu ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu uliofanyika katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Ikiwatumia wachezaji wake wapya iliyowasajili kwa ajili ya msimu huu kikosi cha mholanzi kiliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha wanapata ushindi na kuendeleza heshima kwa timu wanazokutana nazo.
Dakika ya sita ya mchezo mshambuliaji mpya Shaban Kondo almanusura aipatie Young Africans bao baada ya kupokea krosi safi ya Said Bahanuzi kutoka upande wa kulia lakini kutokua makini kwa mshambuliaji huyo kulimfanya mlinda mlango wa Mtibwa Sugar Hussein Sharrif kuokoa hatari hiyo.
Said Bahanuzi aliwainua washabiki, wapenzi na wanachama wa klabu ya Yanga dakika ya 24 ya mchezo baada ya kuukwamisha mpira wavuni kufuatia mlinzi wa mtibwa kuokoa kwa kichwa mpira wa Jerson Tegete ulikokuwa ukielekea wavuni.
Mara baada ya bao hilo Mtibwa Sugar waliongeza kasi ya mashambulizi kwa lango la Yanga ili waweze kupata bao la kusawazisha laikini harakatia zao zilishia mikononi mwa mlinda mlango Deogratius Munishi 'Dida' 
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 1 - 0 Mtibwa Sugar.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ambapo Yanga iliwaingiza golikipa Ally Mustapha 'Barthez, Rajab Zahir, David Luhende, Bakari Masoud, Hussein Javu, na Abdallah Mguhi 'Messi, mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mchezo.
Dakika ya 57 ya mchezo Shaban Kisiga aliipatia Mtibwa Sugar bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penati kufuatia mlinzi Rajab Zahir kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari na Kisiga kufunga penati hiyo na kupata bao la kusawazisha.
Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 80 ya mchezo kufuatia mlinzi wa kati wa Mtibwa Sugar Salvatory Ntebe kumkwatua Tegete na mwamuzi kuamuru penati ambayo aliipiga Tegete na kuukwamisha mpira wavuni.
Huku washabiki wa soka wakianza kutoka nje na wengine wakiwahi kufuturu Hussein Javu aliifungia Yanga bao la tatu na la ushindi dakika ya 87 ya mchezo kufuatia mpira aliorudhishiwa golikpa Said Mohamed kushindwa kuuondoa na Javu kuuwahi na kuhesabu bao la tatu kwa watoto jangwani.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 1 Mtibwa Sugar.
Mara baada ya mchezo kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amesema kikosi chake kinaendelea kuimarika na wachezaji wanaonekana kushika vizuri mafunzo yake, anaendelea na mazoezi kwa hizi wiki mbili kabla ya kucheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya timu ya Azam FC Agosti 17 2013.
Young Africans: 1.Deogratius Munishi 'Dida'/Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua/David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro'/Rajab Zahir, 5.Issa Ngao, 6.Athuman Idd 'Chuji/Bakari Masoud, 7.Said Bahanuzi/Abdallah Mguhi 'Messi', 8.Salum Telela, 9.Jerson Tegete, 10.Shaban Kondo/Hussein Javu, 11.Haruna Niyonzima.

Twanga Pepeta kumtambulisha Ige Moyaba na wengine Mango Garden siku ya Idd Pili

Ige Moyaba aliyerejea tena Twanga atatambulishwa Idd Pili
BENDI ya African Stars “Twanga Pepeta” itatambulisha wanamuziki wapya pamoja na warembo watakaoshiriki Miss Ilala siku ya Iddi Pili Katika ukumbi wao wa Mango Garden, Kinondoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo Asha Baraka alisema jana kuwa onyesho hilo limeandaliwa na Bob Entertainment na kudhaminiwa na Konyagi, Freddito Entertainment, Saluti5 na Twitter Pub.
Alisema wanamuziki watakaotambulishwa siku hiyo maalum ni wanenguaji wapya, muimbaji Ige Moyaba ambaye alikuwa mwanamuziki wa bendi hiyo kabla kwenda Ufaransa kuendeleza kipaji chake.
 “Tumeamua kuleta wanenguaji wapya kabisa, wenye damu changa ili kuleta mapinduzi kwenye muziki wa dansi. Madansa wetu ni mabinti warembo, pia tuna  wanenguaji watanashati,” alisema Asha na kuongeza kuwa awameamua kubadilisha wanenguaji ili kuenda na wakati pamoja na soko la muziki.
Kwa upande wa Ige Moyaba aliyetamba kwenye albamu ya ‘Mtu Pesa’ katika mwaka wa 2004,  Asha alisema ameanda vitu vipya kuwapa mashabiki wa bendi hiyo inayotamba kwa staili ya Kisigino.
“Kwa kweli hi siyo onyesho la kukosa kwani itakuwa ni zawadi yetu ya Idd kwa mashabiki wetu,” mkurugenzi huyo alisema.
Mwezi uliyopita Twanga Pepeta walizindua albamu yao ya 10 lijulikanayo kana “Nyumbani ni Nyumbani”.
Albamu zingine ambazo zitapigiwa siku hiyo ni Jirani, Fainali Uzeeni, Chuki Binafsi, Ukubwa Jiwe, Mtu Pesa, Safari, Password, Mtaa Wa Kwanza, Mwana Dar es Salaam na Dunia Daraja.
Naye mratibu wa onyesho hilo Joseph Kapinga alisema kuwa warembo watakoshiriki kwenye shindano la kumtafuta Redds Miss Ilala pia watatambulishwa siku hiyo.
BENDI ya African Stars “Twanga Pepeta” itatambulisha wanamuziki wapya pamoja na warembo watakaoshiriki Miss Ilala siku ya Iddi Pili Katika ukumbi wao wa Mango Garden, Kinondoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo Asha Baraka alisema jana kuwa onyesho hilo limeandaliwa na Bob Entertainment na kudhaminiwa na Konyagi, Freddito Entertainment, Saluti5 na Twitter Pub.
Alisema wanamuziki watakaotambulishwa siku hiyo maalum ni wanenguaji wapya, muimbaji Ige Moyaba ambaye alikuwa mwanamuziki wa bendi hiyo kabla kwenda Ufaransa kuendeleza kipaji chake.
 “Tumeamua kuleta wanenguaji wapya kabisa, wenye damu changa ili kuleta mapinduzi kwenye muziki wa dansi. Madansa wetu ni mabinti warembo, pia tuna  wanenguaji watanashati,” alisema Asha na kuongeza kuwa awameamua kubadilisha wanenguaji ili kuenda na wakati pamoja na soko la muziki.
Kwa upande wa Ige Moyaba aliyetamba kwenye albamu ya ‘Mtu Pesa’ katika mwaka wa 2004,  Asha alisema ameanda vitu vipya kuwapa mashabiki wa bendi hiyo inayotamba kwa staili ya Kisigino.
“Kwa kweli hi siyo onyesho la kukosa kwani itakuwa ni zawadi yetu ya Idd kwa mashabiki wetu,” mkurugenzi huyo alisema.
Mwezi uliyopita Twanga Pepeta walizindua albamu yao ya 10 lijulikanayo kana “Nyumbani ni Nyumbani”.
Albamu zingine ambazo zitapigiwa siku hiyo ni Jirani, Fainali Uzeeni, Chuki Binafsi, Ukubwa Jiwe, Mtu Pesa, Safari, Password, Mtaa Wa Kwanza, Mwana Dar es Salaam na Dunia Daraja.
Naye mratibu wa onyesho hilo Joseph Kapinga alisema kuwa warembo watakoshiriki kwenye shindano la kumtafuta Redds Miss Ilala pia watatambulishwa siku hiyo.

Wanahabari wa Habari Group watoa msaada kwa yatima


Diwani wa Viti Maalumu na Mwenyekiti Mtendaji wa Aisha Sururu Foundition, Bi. Aisha Sururu kulia akiwakabidhi sehemu ya msaada alioutoa kwa ajili ya kuchangia yatima kwa wanachama wa kikundi cha Habari Group, Rabia Bakari (kushoto) na Asha Bani kwa ajili ya kupeleka kwa yatima katika vituo mbalimbali  Misaada mingine ilitolewa na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia, January Makamba, Mmiliki wa Maduka ya Silva Botique, Madam Nora, Katibu wa Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa kiislam Sheikh  Khamisi Mataka, na Mkurugenzi wa Kampuni ya QUALITY Printers And Stationers Amani Soko

Diwani wa Viti Maalumu na Mwenyekiti Mtendaji wa Aisha Sururu Foundition, Bi Aisha Sururu (kushoto) akiwakabidhi sehemu ya msaada alioutoa kwa ajili ya kuchangia yatima kwa wanachama wa kikundi cha Habari Group Rabia Bakari na Asha Bani kwa ajili ya kupeleaka kwa yatima wa vituo mbalimbali.

Wanachama wa kikundi cha Habari Group, Rabia Bakari (kulia) na Asha Bani wakiangalia baadhi ya vyakula na vitu mbalimbali walivyokabidhiwa kwa ajili ya kwenda kugawa kwa  yatima.
Sehemu ya misaada hiyo

Wanachama wa Habari Group wakia katika picha ya pamoja na na mwenyekiti mtendaji wa Aisha Sururu Foundition Bi. Aisha Sururu
Moja ya kituo cha kilichopewa misaada na Habari Group Leo

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada  walioutoa kwa  Katibu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni Bw. Abubakari Simba jijini Dar es salaam leo.

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha habari Group wakiwa katika picha ya pamoja na  yatima wanaolelewa katika Kituo cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni baada ya kutoa misaada mbalimbali leo

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani kulia akikabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa  Katibu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni Bw. Abubakari Simba Dar es salaam leo.

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada  walioutoa kwa  Msimamizi Mkuu wa kituo cha kulelea yatima cha Al Furqan Islamic Center cha Chanika Bw. Hamisi Omari  Dar es salaam leo
Baadhi ya wanachama wa kikundi cha habari Group wakiwa katika picha ya pamoja na  yatima wanaolelewa katika kituo cha Al Furqan Islamic Center cha Chanika baada ya kutoa misaada mbalimbali leo.

Meshack Abel kwenda Ulaya akiizitabiria Ashanti, Coastal kufanya maajabu Ligi Kuu 2013-2014


Meshack Abel (kulia) akiwa na wachezaji wenzake wa Kitanzania wanaoichezea Bandari-Kenya, Mohammed Banka, Thomas Mourice na David Naftar
BEKI wa kimataifa zamani wa Simba anayecheza soka la kulipwa nchini Kenya katika timu ya Bandari, Meshack Abel, anajiandaa kuitema timu hiyo na kwenda Ulaya kusaka timu ya kuichezea.
Aidha Abel amezitabiria timu za Ashanti United na Coastal Union ya Tanga kufanya vyema kwenye msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza rasmi Agosti 24, akiamini itazipiku vigogo Simba na Yanga zinazopokezana taji kila msimu.
Akizungumza na MICHARAZO toka Kenya, beki huyo wa kati alisema anatarajiwa kuachana na timu hiyo na kutimka Ulaya mara baada ya mkataba wa kuitumikia klabu hiyo ya Ligi Kuu nchini humo utakapomalizika Desemba mwaka huu.
Abel, aliyewahi kuzichezea pia timu za Ashanti United na African Lyon, alisema tayari mipango ya safari ya kwenda Ulaya inafanywa na meneja wake.
Beki huyo aliyejaliwa mwili mkubwa, alisema ingawa bado hajadokezwa anatafutiwa timu katika nchi gani barani huko, lakini mipango ya awali ilikuwa kati ya nchi za Sweden, Norway au Uswisi.
"Mkataba wangu unakaribia kuisha na tayari sina mpango wa kuongeza kwa vile najiandaa kwenda kusaka timu ya kucheza soka la kulipwa barani Ulaya, wakati wowote natimkia huko," alisema.
Alipoulizwa kama alikuwa na mipango ya kurejea nchini kucheza soka baada ya kutamba na timu kadhaa ikiwamo Simba, Abel alisema kwa sasa hafikirii kabisa jambo hilo zaidi ya kusonga mbele kwa madai soka la Bongo limejaa mizengwe tofauti na hali aliyokutana nayo nchini Kenya ambapo klabu zinawathamini na kuwajali wachezaji huku mashabiki wakiwaunga mkono.
"Sifikirii kurudi nyumbani kwa sasa, mawazo yangu ni kusonga mbele zaidi ndiyo maana najiandaa kuondoka Kenya," alisema.
Kuhusu Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013-2014 inayoanza Agosti 24, Abel alisema kwa namna anavyozifuatilia timu shiriki anaweka turufu yake kwa klabu za Coastal Union na Ashanti United kuzifunika Simba na Yanga katika mbio za kuwania ubingwa.
"Simba na Yanga zilikuwa zamani, kama siyo mizengwe Azam ilishazifunika na msimu huu naamini Coastal Union na Ashanti United itaongeza ushindani kwa klabu hizo na kufanya vyema katika ligi ijayo," alisema.
Alisema hata hivyo klabu hizo hazipaswi kujiamini kupita kiasi na badala yake wachezaji wake wajitume na kuhakikisha kila mechi wanapata ushindi na kusaidia kutimiza utabiri wake kwa klabu hizo msimu huu.

Zahoro Pazi hahofii chochote Simba

Zahoro Pazi
 MSHAMBULIAJI mpya wa Simba, Zahoro Pazi amesema hahofii ushindani wa namba katika kikosi cha timu hiyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Pazi, mtoto wa kipa wa zamani wa 'Wekundu wa Msimbazi', Idd Pazi 'Father' alisema licha ya kutambua ametua Msimbazi wakati kikosi hicho kikiimarishwa kwa kusajiliwa wachezaji wapya wakiwemo wa ndani na wale wa kigeni bado anajiamini kupata nafasi kwa kipaji na uwezo mkubwa alionao katika soka.
Pazi, alisema kitu cha muhimu kwake atakachozingatia ni kujituma mazoezi, kucheza kwa bidii akipata nafasi kama ilivyotokea katika mechi za kirafiki ambazo Simba imeshacheza hivi sasa zikiwemo mbili zilizopita dhidi ya URA na Coastal Union ambapo timu hiyo ilipoteza mechi zote.
"Ni kweli kuna ushindani mkubwa katika kikosi cha Simba, tumekutana wachezaji wapya wenye uwezo mkubwa, lakini sihofii chochote kwa vile najiamini na nitajitahidi kumridhisha kocha Abdallah Kibadeni kisha kuliacha jukumu mikononi mwake kuamua nani wa kumpanga katika mechi za Ligi zinazotarajiwa kuanza karibuni," alisema.
Pazi alisema katika mechi zote za kujipima nguvu anashukuru alipewa nafasi ya kucheza na kuonyesha uwezo wake, ingawa bado hajafunga bao lolote, akiamini anaendelea kuzoea mazingira ya klabu hiyo iliyowahi kuchezwa na baba yake.
Mshambuliaji huyo alisema kwa namna kikosi chao kilivyo chini ya kocha anayemzimia aliyewahi kumnoa alipokuwa Mtibwa Sugar, anaamini Simba itatamba katika msimu ujao, ingawa alikiri huenda ikakamiwa na kupata wakati mgumu kutimiza ndoto za kurejesha ubingwa baada ya msimu uliopita kuupoteza kwa watani zao Yanga.
Simba inatarajiwa kufungua dimba la pazia la ligi kuu msimu huu kwa kuumana ugenini na timu 'ngeni' ya JWTZ, Rhino Rangers ya Tabora iliyopanda toka daraja la kwanza sambamba na timu za Ashanti United na Mbeya City.

Golden Bush wagawa msaada kwa yatima, Kaseja kivutio

Juma kaseja akiwa kando yawatoto yatima

'Tanzania One' Juma Kaseja akiwa amekaa na  yatima wanaolelewa katika kituo cha New Life Orphans Home wakati timu ya Golden Bush ilipopeleka msaada katika kituo hicho. Kipa huyo alikuwa kivutio kwa watoto hao.
Wachezaji wa Golden Bush wakiwa pamoja na yatima hao

Mmoja wa wachezaji wa Golden Bush akiwa amebeba mmoja wa yatima hao

Watoto wakifurahia kujumuika na wachezaji wa Golden Bush

Naondoka na wewe! Yatima akiwa mikononi mwa mmoja wa wachezaji wa Golden Bush

Salum Swedi akizungumza jambo, kushoto  KR Mulla na kulia kwake ni Herri Morris
Yatima wa kituo cha New Life Orphans Home wakiimba wakati wachezaji wa Golden Bush walipowatemebelea leo

Katibu wa kituo cha Kulelea Yatima cha New Life Orphans Home, Hamad Kombo (kushoto) akisoma risala fupi mbele ya uongozi wa Golden Bush

Yahya Issa kati akiwa amempakata mtoto kando ya Mkuu wa Nidhamu wa kituo cha kulelea Yatima Mbwana Said huku Herry Morris akiwa kando yake kushoto
Rashid Ziada 'KR Mullah' naye alikuwa mmoja wa wana Golden Bush waliotembelea kituo cha yatima na kuwaonyesha namna ya kucheza Mapanga Shaa'
TIMU ya soka ya Golden Bush Fc kimewatembelea yatima wanaolelewa katika kituo cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo, jijini Dar es Salaam na kuwafariji kwa kuwapa msaada wa vitu mbalimbali ikiwamo chakula kwa ajili ya sikukuu ya Eid.
Msaada huo Golden Bush ulitolewa leo asubuhi na wachezaji hao wakiongozwa na mlezi wao, Onesmo Waziri 'Ticotico', viongozi na nyota kama Juma Kaseja, Salum Swedi 'Kussi' , Yahya Issa, Amani Simba, Waziri Madhi na wengine una thamani ya Sh. 3.5.
Baadhi ya msaada huo ni sabuni, juisi, mchele, sukari, mafuta ambavyo vilikabidhiwa na timu hiyo kwa uongozi wa kituo hicho ukiongozwa na Katibu Mkuu wake, Hamad Kondo na Mkuu wa Nidhamu, Mbwana Said.
Yatima hao wakiwa na bashasha na hasa baada ya kuwaona wachezaji hao mastaa waliwaimbia Golden Bush na kuchezewa miondoko ya Mapanga Shaa na msanii Rashid Ziada 'KR Mullah' ambaye naye ni mchezaji wa timu hiyo kabla ya Katibu wa kituo kusoma risala fupi.
Hamad akieleza kwa ufupi kwamba historia ya kituo hicho kilichoanzishwa mwaka 2001......kikiwa na watoto 17 tu tofauti na sasa wanafikia 103 wasichana wakiwa 38 na waliosalia wakiwa ni wavulana.
Katibu huyo alieleza kuwa kituo chao kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo ada za kuwalipia wanafunzi wanaosemeshwa na kituo hicho ambapo baadhi wapo Shule ya Msingi na wengine wa Sekondari.
Pia Hamad aliweka bayana kuwa kituo chao kimefanikiwa kupata eneo huko Boko-Dawasa na wamejenga jengo la ghorofa moja ambalo walisaidiwa kiwanja na mlezi wao na mpaka sasa jengo hilo limesimama isipokuwa bado halijamalizika kutengenezwa sakafu.
Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' akizungumza kabla ya kuupisha uongozi wa juu wa timu hiyo, alisema wanafahamu walichokitoa ni kidogo, lakini waliuomba uongozi upokee kwa mikono  miwili na kuahidi kutoa msaada wa kifedha kupitia akaunti ya kituo hicho.
"Nimesikia kilio chenu, ninachoomba nipeni namba yenu ya akaunti nami nilichojaliwa nitakituma huko, ila kwa sasa tunaomba mpokee japo hiki kidogo kwa ajili ya kuwafariji watoto katika kuelekea sikukuu ya Eid," alisema Ticotico.
Nao Mwenyekiti wa timu hiyo, Salum Swedi na Katibu wake, Herry Morris waliwataka watoto hao kuwa watiifu na kuishi kwa wema na Mungu akiwajalia waje kuwa nyota kama walivyokuwa wao katika soka, huku wakijinadi wapo wanaodaka kama Kaseja ambaye walimshangilia zaidi na kuonyesha kumjua na kutaka kupiga naye picha kila mara.
Naye Kaseja alipata nafasi ya kuzungumza na watoto hao na kuwataka kujibidiidha katika masomo, kumcha Mungu na kuwa watiifu kwa kila mtu na kwa wale wenye vipaji waviendeleze ili vije kuwasaidia ukubwani kama ilivyokuwa kwake na wenzake waliowatembelea.