STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 8, 2013

Hivi ndivyo Extra Bongo ilivyowatambulisha wanenguaji wao wapya Leaders

Wanenguaji wapya wa Extra Bongo, Jolie na Grace wakionyesha makeke yao

Tunatomboka namuna hii ...ayaa ayaaa hiiiiii
Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki (mwenye kofia) akiwatambulisha wanenguaji wao wao huku Super Nyamwela akiwa makini kumsikiliza pembeni kulia. Kushoto ni Papii Catalogue
Mi naitwa Jolie Kindu au Muringo Ngassa nimekuya Kutanzanie kwa ajili ya kufunika madancers wote mutaona
Msiniangushe jamani, nimeshawafagilia kwa mapaparazi kuwa nyie ni nouma sawasawaaa?
Ally Choki akitoa ufafanuzi kwa wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa waneguaji wao wawili kutoka Kongo.
Choki alikuwa na kazi kubwa ya kufafanua baadhi ya mambo juu ya madansa hao wanaojiita Mrisho Ngassa na John Bocco ambao watatambuilishwa rasmi kesho kwenye onyesho la Idd Mosi Meeda Club bna Idd Pili itakuwa zamu wa wakazi wa Mbagala kwani Extra Bongo watakuwa Dar Live

Mwanafunzi wa darasa la kwanza afa kwa kugongwa na gari Mbeya

 [ DIWANI ATHUMANI  - ACP ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


WILAYA YA  KYELA - AJALI YA  GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA        
                                            KUSABABISHA KIFO.
MNAMO TAREHE 07.08.2013 MAJIRA YA  SAA 08:30 HRS HUKO KATIKA ENEO LA KALUMBULU  WILAYA YA  KYELA  MKOA WA MBEYA. GARI  T.932 BUF AINA YA  T/IPSUM IKIENDESHWA NA KAIMU S/O HENDE, MIAKA 33, MBONDEI, MKULIMA  MKAZI WA KYELA-KATI  ILIMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU MTOTO HAWA D/O GIBSON,MIAKA 6,MSAFWA,MWANAFUNZI DARASA LA KWANZA S/MSINGI MBUGANI  MKAZI KALUMBULU NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO.  MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA. CHANZO NI MWENDO KASI, DEREVA AMEKAMATWA. TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
Signed by:
 [ DIWANI ATHUMANI  - ACP ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Huyu ndiye jambazi wa kwenye ATM, lanaswa kilaini Dar baada ya mtego

Mtu anayedaiwa kuwa mwizi wa kwenye ATM rais wa Bulgaria akiwa chini ya ulinzi baada ya kunaswa akiiba jijini Dar es Salaam kutokana na kuwekewa mtego kumnasa


MSAKO wa wezi wa kwenye Mashine za Kutolea Fedha (ATM), umeanza kuzaa matunda baada ya raia wa Bulgaria kukamatwa akiiba kwenye ATM ya Bank of Africa (BOA), Tawi la Afrikana, Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za benki, mtuhumiwa huyo ambaye
hakutajwa jina lake alikamatwa baada ya kamera maalumu zilizowekwa kwenye ATM za BOA, kumtambua kuwa ni mwizi sugu wa benki hiyo anayetafutwa.

Mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa si msemaji, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 12 asubuhi baada ya mtuhumiwa huyo kuwekewa mitambo maalumu ya kumnasa.

Alisema benki hiyo ilipelekewa malalamiko na baadhi ya wateja kwamba wakienda kutoa fedha kwenye ATM wanakuta akaunti zao hazina salio wakati wanaamini zilikuwa na fedha.

Chanzo hicho cha habari kilidai kuwa baada ya kupelekewa malalamiko hayo, waliweka mitambo maalumu ya kuwawezesha walinzi wa maeneo ya ATM za BOA kumbaini mtu atakayetoa fedha kwa njia ya wizi.

“Kama Benki tuliweka mtambo maalumu na mtuhumiwa huyo alionekana kwenye mtambo wetu, hivyo tuliwaagiza walinzi wetu watakapomwona mtu huyo wamkamate haraka 
sana,”alisema.
Alisema mtuhumiwa huyo alianza mchezo huo kwa muda mrefu ambapo kwa kutumia kadi za ATM zisizojulikana idadi yake, alikuwa anakwenda kwenye ATM mbalimbali za benki hiyo na kutoa fedha hadi Sh10 milioni.

Kuhusu tukio la jana, mmoja wa walinzi wa BOA aliyejitambulisha kwa jina moja la Frank alisema mtuhumiwa huyo alipofika kwenye ATM hiyo aliingia na kuchukua fedha ambazo alizipeleka kwenye gari lake.
Frank alisema baada ya kupeleka fedha hizo, alirudi kwa mara ya pili ili achukue fedha nyingine ndipo walinzi hao walimkamata na kumfunga pingu.

“Huyu mtuhumiwa mwenye asili ya Kiarabu alifika na gari lake saa 12 asubuhi, aliingia kwenye ATM na kutoa fedha ambazo hazikujulikana ni shilingi ngapi na kuzipeleka kwenye gari lake, baadaye alirejea tena kwa ajili ya kutoa fedha zingine, wakati anaingia ndipo alipokamatwa na mlinzi aliyekuwa analinda hapo,” alisema Frank.

Kamanda wa Polisi Kinondoni, Camilius Wambura alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi hilo huku uchunguzi dhidi yake ukiendelea.

“Ni kweli taarifa nimezipata, mtuhumiwa amekamatwa, bado hatujajua ni kiasi gani ambacho ameiba kwa kutumia mtandao, tunaendelea na uchunguzi,” alisema Wambura.

Tukio kama hili lilishawahi kutokea mkoani Mwanza Februari 19 mwaka huu na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na maofisa ya Benki ya NMB liliwatia mbaroni watu watatu ambao walidaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti.

MWANANCHI

Real Madrid yaichakaza Chelsea 3-1, Mourinho

KIUNGO Frank Lampard alicheza kwa mara ya kwanza majira haya ya joto, lakini alishindwa kumzuia Cristiano Ronaldo kuinyanyasa Chelsea jana.
Kabla ya mechi hiyo na Real Madrid mjini Miami, kiungo huyo mkongwe alikosa mechi zote za kujiandaa na msimu za klabu, Stamford Bridge kutokana na kuwa majeruhi.
Lakini Lampard ameimarika na kuanza kazi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu dhidi ya Hull City, Agosti 18 baada ya kumaliza dakika 45 za kwanza katika Fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
Katika mechi hiyo, mabao mawili ya Ronaldo na moja Marcelo, yalitosha kuitotesha timu ya Jose Mourinho 3-1 dhidi ya timu yake ya zamani ambayo kwa sasa inafundishwa na Carlo Ancelotii.
Chelsea ilipata bao lake pekee kupitia kwa Ramires.  
Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Khedira, Isco, Ozil, Ronaldo na Benzema.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Lampard, Van Ginkel, Ramires, Oscar, Hazard na Lukaku.
On target: Cristiano Ronaldo scored a brace as Chelsea went down to the La Liga giants
Kiboko yao: Cristiano Ronaldo amefunga mabao mawili dhidi ya Chelsea jana
Party time: Real Madrid stars celebrate with the International Champions Cup after beating Chelsea
Kujiachia: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea na taji lao la Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness
Lethal: Ronaldo blasted home a free-kick and later added a header to help Madrid secure the game
Kitu hichoo: Ronaldo akifunga kwa mpira wa adhabu
Unloved: A Real Madrid fan holds up a banner showing he doesn't care that Mourinho left the club
Mapenzi yameisha: Shabiki la Real Madrid likiwa limebeba bango kuonyesha kutojali kuondoka kwa Mourinho katika klabu hiyo
Chinwag: Mourinho and former Chelsea boss, and current Madrid manager, Carlo Ancelotti, have a chat
Mazungumzo baada ya tukio: Mourinho na kocha wa zamani wa Chelsea, ambaye kwa sasa ni kocha wa Madrid, Carlo Ancelotti wakizungumza baada ya mechi
Triumphant: Real Madrid stars celebrate after beating Chelsea in the final of the Champions Cup
Mabingwa: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea kuifunga Chelsea katika fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
 BI ZUBEIRY BLOG

Answar Sunnah wala Eid yao leo sawa wa wengine duniani


WAISLAM WA AN-SUNA WAMEJUMUIKA  NA WAISLAM WENZAO DUNIANI KUSHEREHEKEA SIKU  HIYO BAADA YA KUMALIZIKA KWA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANIPICHA WAKIWA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI LEO

WAKISALI KWENYE VIWANJA VYA JANGWANI LEO

Waumini wa Kiislam wakisujudu wakati wa swala ya Eid iliyoswaliwa leo na sehemu kubwa ya waumini duniani wanaofuata kalenda ya Kiislam

Wednesday, August 7, 2013

Wanafunzi wafa maji Tabora kisa Bata Mzinga


WANAFUNZI wawili wa shule ya msingi Itobo wilaya ya Nzega mkoani wa Tabora wamekufa maji katika bwawa wakati wakiwinda bata mzinga. 

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Peter Ouma alisema Massanja Shija (42) ambaye ni baba wa mmoja wa watoto hao waliokufa, amenusurika katika tukio hilo baada ya kunasa kwenye tope.

Kamanda alitaja watoto waliokufa ni Elias Massanja (13) na Shabani Ramadhan (15) wote wanafunzi wa darasa la sita shule ya Msingi Itobo. Tukio hilo ni la Julai 30 mwaka huu, saa 12:30 jioni katika Kijiji cha Chamwabo, Kata Itobo.

Ouma alisema walikuwa wakiwinda bata mzinga ambaye aliruka na kwenda kwenye bwawa na katika kumfuata, walizama katika kina kirefu cha maji.

Alisema baada ya kuzama, jitihada za kuokoa miili yao ilikuwa ngumu kutokana na kukosa waokoaji. Hata hivyo baadaye iliopolewa.

Mbunge wa Jimbo la Bukene, Selemani Zedi alisema tukio hilo ni la kusikitisha kwa jamii. Aliwataka wananchi kuwa makini na mabwawa.

Shindano la BSS sasa TBC1 siyo ITV tena, kisa....!

 
Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 

Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.

“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1. 

Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.

Extra Bongo yanasa wawili toka Congo kuwatambulisha siku ya Eid

 KATIKA kujiimarisha zaidi na kutaka kuendelea kufunika nchini bendi ya Extra Bongo 'Wana Next Level' maarufu kama Wazee wa Kizigo, wamewanyakua wanenguaji wapya wawili wa kike kutoka DR Congo watakaotambulishwa rasmi kwa mashabiki katika maonyesho ya sikukuu ya Eid el Fitri.
Wanenguaji hao walitambulishwa mchana wa leo kwa wanahabari ni Jolie Moncotina Kindu 'Mrinsho Ngassa' na Grace Messu Kamba (Fatuma) au maarufu kama John Bocco waliodai wanatoka katika makundi ya wanamuziki Werrason Ngiama Makanda na Ferre Golla.
Utambulisho huo ulifanyika kwenye viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade' alisema wanenguaji hao tayari walioshaanza mazoezi na wasanii wenzao ila walikuwa wakisubiri vibali vya kufanya kazi nchini.
"Tumekuwa nao kwa muda wakiendelea na mazoezi wakati tukihangaikia vibali vyao na tunashukuru vibali vimepataika ana hivyo watawatambulishwa rasmi katika maonyesho yetu ya sikukuu ya Eid katika kumbi za Meeda Club-Sinza Mori na Dar Live," alisema Choki.
Aidha Choki alisema bendi yao pia itatambulisha siku hiyo kwa mashabiki wao nyimbo mbili mpya za 'Hafidh' uliotungwa na Michael Athanas 'Montanabe' na 'Mwanamke Hapigwi' Papii Catalogue.
"Pia kutakuwa na nyimbo mbili zitakazotambulishwa sambamba na zile mbili za Mgeni wa Khadija Kimobitel na Sagna nilioutunga mimi lakini anaimba sehemu kubwa Kimobitel," alisema.
Nao wanenguaji hao walioonyesha manjonjo yao kwa wanahabari, walisema wamekuja nchini kuonyesha namna ya kunengua, huku wakisema wanajiita majina ya washambuliaji hao nyota wa soka wa Taifa Stars kutokana na kukunwa na umahiri wao dimbani.
"Tangu niko kule Kin, namuonaga Murisho Ngassa namna anavyochezaga nami navutiwa na yeye ndiyo najipa hii jina yake, na nitafunika kama Ngassa," alisema Jolie ambaye angalau anakifahamu kiswahili kuliko mwenzake aliishia kusema yeye ni John Bocco tu.
Naye Rapa Catalogue alisema wimbo wake mpya una lengo la kuleta mabadiliko na utetezi kwa wanawake kutokana na mikstari yake inayoasa wanaume kutowapiga wanawake wala kuwanyanyasa badala yake iwatunze vyema ili wasije wakawaacha na kupata wanaojua kubembeleza.
"Pia kuna rapu mpya nitatitambulisha siku hiyo inayosema tutaishie Dar bila ya kazi, tutaishije Dar es Salaama bila ya kazi wakati taka, maji umeme na kila kitu lazima pesa..." alisema rapa huyo mahiri.
Kiongozi na mwalimu wa uenguaji wa bendi hiyo, Super Nyamwela alisema kutua kwa wasanii hao wawili kumeongeza chachu na kuboresha safu yao na kwamba hataki kusema mengi ila kuwataka mashabiki wajitokeze katika maonyesho yao waone kazi.
"Sitaki kusema sana kwa sababu hakuna asiyemjua Nyamwela na kazi yake, mimi ni mwalimu na mashabiki waje waone kwa nini anaitwa mwalimu, wenzetu wamezoea kuongea sasa ila mimi na bendi yangu ni watu wa vitendo zaidi," alisema Nyamwela.

Majambazi wamuua kwa risasi Mfanyabiashara wa madini Arusha

 
Mwili wa Erasto Msuya ukiwa chini baada ya kupigwa risasi.
 
MFANYABIASHA maarufu wa madini aina ya Tanzanite ambeye pia ni mmiliki wa hotel ya kitali ya S.G Resort ya jijini Arusha anayefahamika kwa jina la Erasto Msuya amefariki dunia leo majira ya alasiri baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wakati alipokuwa akitokea Mirerani akielekea jijini Arusha.
Taarifa kutoka kwa shuhuda wa tukio hilo zinaeleza kuwa Bwana Erasto Msuya alisimamishwa na watu hao karibu na njia panda ya KIA (Kilimanjaro International Airport) na aliposimama walimtishia kwa kutumia bastola na kumtaka afate matakwa ya watu hao ndipo Erasto alipotoa bastola ili aweze kujitetea ndipo majambazi hao walipo amua kumpiga risia ambazo idadi yake haikuweza kufahamika kwa haraka.

NMB YASHIRIKI FUTARI NA WATEJA WAKE


 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akishukuru uongozi wa NMB kwa kuandaa wasaa mzuri na kushiriki katika kukamilisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.Hii ilikua katika futari iliyoandaliwa na Benki ya NMB tawi la Zanzibar  kwenye hoteli ya Zanzibar Ocean view Zanzibar mwishon mwa wiki.
  Mkuu wa kitengo cha akaunti binafsi wa NMB, Abdulmagid Nsekela akiongoza wageni waalikwa katika kupata futari.
  Meneja Mawasiliano NMB, Josephine Kulwa nae hakubakia nyuma kushiriki futari na wateja wa NMB
Maofisa wa NMB wakiwa wameambatana  kuingia ukumbini na mgeni rasmi (katikati) katika hafla hii ya kushiriki futari na wateja wa NMB mjini Zanzibar.

MKUTANO WA DHARURA WA WANACHAMA WA YANGA AGOST 18



1.   Hivi karibuni tumepata uhakika kuwa Tanzania Premier League (TPL) na Azam Media wanayo nia ya kuingia mkataba wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu (Premier League) kwa msimu wa 2013/2014, 2014/2015 na 2015/2016


2.   Baada ya Kamati ya Utendaji ya YANGA kufanya uchambuzi wa kina juu ya taarifa ya makubaliano ya kibiashara ya TPL / Azam Media ilihitimisha kuwamkataba huu hauna maslahi kwa YANGA, na kwa hivyo, Kamati ya Utendaji ya YANGA ilifikia uamuzi kuwa mechi za YANGAzisirushwe hewani na Azam Media.


Kwa kuwa wawazi, Kamati ya Utendaji ya YANGA ilitoa taarifa kwa wanachama wa YANGA kupitia vyombo vya habari tarehe 29 Julai, 2013 ambapo iliweka bayana sababu zake na kueleza kuwa YANGAhaina tatizo na vilabu vingine vya mpira wa miguu ikiruhusu mechi zao kurushwa na Azam Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mechi zake za Vodacom Premier League katika Azam Television.


3.   Sote tumeona baada ya hapo kuwa “nguvu ya ziada” inatumika kupotosha msimamo wa Kamati ya Utendaji ya YANGA na kuidhalilisha Klabu ya YANGA hadharani


Juu ya hayo Na Kwa kushangaza Sana, baadhi ya vilabu vya mpira WA miguu ambavyo vina sifa kuwa havijawahi kushinda Ligi Kuu, vimeundwa hivi juzi tu, havina uzoefu wowote WA kucheza soka kimataifa n.k. vina kuja kuyapanga Kamati ya Utendaji ya YANGA jinsi ya kuendesha shughuli za Klabu ya Yanga, vikiwa vinasahau vilabu vyao wenyewe na badala yake kuiingilia YANGA kwa sababu zinazojionyesha wazi.


Inadhihirika wazi kwamba kuna ushirikiano usio mzuri unaoashiria kula njama kuilazimisha YANGA iruhusu mechi zake zirushwe na Azam Television.


Kwa kuwa YANGA ni Klabu ya Wanachama yenye kupata nguvu kutokana na misingi yake ya kidemokrasia iliyojijengea na uamuzi wake wa mwisho unatokana na Wanachama wake mwenyewe, umeamua kuliweka suala hili zima kwa Wanachama wa Yanga ili waamue ni njia gani ya kufuata kwa maslahi ya Klabu yetu.


Kwa kuzingatia hali hiyo basi, na kulingana na mamlaka niliyonayo kama Mwenyekiti wa YANGA, natangaza mkutano wa dharura wa Wanachama wa YANGA tarehe 18 Agosti, 2013 utakaofanyika uwanja wa Sabasaba kwenye ukumbi wa PTA saa 3.30 asubuhi waje tujadiliane na kuamua suala la Azam Television kurusha mechi za YANGA.

AIRTEL YATOA CHAKULA CHA FUTARI NA IDDI KWA YATIMA DAR

 Afisa mauzo wa Airtel,  Bw Salehe Safi  akimkabidhi  Bibi  Saada Omary
moja ya zawadi zilizotolewa na kampuni za simu za mkononi  ya Airtel
kwenye kituo cha watoto yatima kinachofahamika kwa jina la Mwana
Orphanage Center kilichopo Vingunguti jijini Dar es salaam.   AIRTEL
ilitoa sukari, mchele, mafuta, sabuni, maziwa na Unga wa ngano
kwaajili ya kumalizia mwezi wa Ramadhani na kusheherekea sikukuu ya
IDDI.


Baadhi ya watoto yatima katika kituo cha Mwana Orphanage kilichopo
maeneo ya Vingunguti jijini Dar es salaam, wakiwa wameshikilia baadhi
ya zawadi walizokabidhiwa na kampuni ya simu za mkoni Airtel Tanzania.
AIRTEL ilitoa sukari, mchele, mafuta, sabuni, maziwa na Unga wa ngano
kwaajili ya kumalizia mwezi wa Ramadhani na kusheherekea sikukuu ya
IDDI.

Tuesday, August 6, 2013

Mussa Mgosi atua Mtibwa Sugar kumrithi Javu

Mussa Hassain Mgosi
MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Simba Mussa Hassan Mgosi amejiunga rasmi na klabu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Morogoro.

Mgosi ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia klabu ya JKT Ruvu amejiunga na Mtibwa kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Akiongea na mtandao huu, kocha wa Mtibwa Sugar  Mecky Mexime amethibitisha kwamba klabu yake imemsajili mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.
 
"Mgosi anakidhi vigezo vya mshambuliaji tunayemhitaji baada ya kuondoka wa Javu aliyejiunga na Yanga. Ameshaini mkataba wa mwaka mmoja na atajiunga na kambi ya maandalizi ya msimu mpya hivi karibuni."
 
Shafih Dauda

Kumekucha Tamasha la Idd Mosi Dar Live


Meneja wa Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kulia) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu burudani mbalimbali zitakazokuwepo Dar Live sikukuu ya Idd Mosi.
WASANII wa muziki watakaopanda katika jukwaa la kisasa la Dar Live sikukuu ya Idd Mosi pamoja na mabondia leo wamelonga na wanahabari kwenye mkutano uliowakutanisha ambao umefanyika katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wasanii wametambiana kila mmoja akitamba kuwa atamfunika mwenzake. Vilevile mabondia nao wametunishiana misuli hali inayoonyesha kuwa kutakuwa na bonge la burudani katika sikukuu hiyo ya Idd Mosi.
Katika sikukuu hiyo wasanii Ali Kiba, H-Baba, Chegge, Temba, Dogo Aslay, Bi. Cheka na Bendi ya Mapacha Watatu watashusha bonge la burudani na kuwapa raha mashabiki watakaohudhuria shoo hiyo. Kwa Upande wa masumbwi bondia Francis Miyeyusho atazipiga na Darius Lupupa kutoka nchini Zambia, Chupaki Chipindi atapigana na Ramadhan Kido. Vilevile mabondia wa kike Ester Kimbe na Irene Kimaro wataonyeshana moto siku hiyo.
(PICHA: SHAKOOR JONGO /GPL)
Mwanamuziki H – Baba akitamba mbele ya wanahabari (hawapo pichani) kuwa atafunika mbovu siku hiyo.

Mratibu wa mapambano ya ndondi, Abdallah Yasin ‘Ustaadh’ (kulia) akiongea na wanahabari. Kushoto ni Abdallah Mrisho.

Mwanamuziki Ali Kiba (kulia) akipeana ‘hi’ na Ustaadh wakati wa mkutano huo.
Bondia Francis Miyeyusho akitunisha misuli. Bondia huyu atapigana na Mzambia Darius Lupupa.

Bondia Chupaki Chipindi atakayezipiga na Ramadhan Kido.
Ramadhan Kido atakayepambana na Chupaki Chipindi siku hiyo.
Mabondia wa kike Ester Kimbe (kushoto) na Irene Kimaro wakijaribu kuzipiga.

Mabondia Francis Miyeyusho (kulia) na Ramadhan Kido (kushoto) wakifuatilia mkutano huo.
Chupaki Chipindi kutoka mkoani Iringa akiwa kwenye pozi.

Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.
Bondia Ester katika pozi.
Bondia Irene naye akiwa kwenye picha ya pozi.
H – Baba katika pozi la kusimama.
Ester ndani ya gloves.

Rufaa 84 zakatwa Baraza la Ushidani

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/08/IMG_1843.jpg
Na Suleiman Msuya
KWA kipindi cha zaidi ya miaka sita tangu kuanzishwa kwa Baraza la Ushindani (FCT) jumla ya rufaa 84 zimesajiliwa 36 zimesikilizwa na kutolewa uamuzi na jopo la wajumbe waa Baraza hilo.
Hayo yamebainishwa Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa FCT Nzinyangwa Mchany wakati akijibu swali la mwandishi wqa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema katika rufaa hizo 29 zilisitishwa kutokana na wahusika kuamua kuziondoa baada ya kufikia maamuzi ambayo baraza hilo halina mamlaka yakuingilia ambapo kwa sasa rufaa zinazoendelea kusikilizwa ni 19.
Mchany alisema Baraza la Ushindani limejipangia kusikiliza rufaa 24 kwa mwaka iwapo zitakuwepo lakini bado mwitikio ni mdogo hali ambayo inatajwa kuwa inachangiwa na uelewa mdogo kutoka katika jamii juu ya FCT.
“Baraza la Ushindani FCT limeanza kazi rasmi mwaka 2007 ambapo huwa tunapokea rufaa kutoka katika kwa watu na taasisi mbalimbali ambazo zinakuwa hazijaridhika na maamuzi ambayo yanatolewa na  mamlaka za udhibiti hapa nchini,” alisema.
Kwa upande wake Mwanasheria Mwandamizi Hafsa Said  alisema pamoja na mafanikio hayo madogo ambayo wameweza kuyapata tangu kuanza kwa FCT bado wana changamoto chache ambazo zinawakabili.
Alizitaja baadhi ya changamoto kuwa ni uchache wa majaji wa kusikiliza rufaa ambapo wamekuwa wakifanya kazi kwa muda maalumu (party time) kutokana na ukweli kuwa ni watumishi wa Mahakama ya Kuu nay a Rufaa.
Said alitaja changamoto nyingine ni ufahamu mdogo kwa jamii juu ya FCT ambapo wanajipanga kwa kushirikiana na mamlaka za udhibiti kutoa elimu hiyo ili wananchi na jamii kwa ujumla kutopoteza haki zao pale wanapoona kuna dalili za kuzikosa.
Pia alisema pamoja na changamoto hizo kupitia maamuzi yao wanayotoa ubora wa mamlaka za udhibiti umeongezeka jambo ambalo linaleta tija kwa jamii.
Alisema tangu waanze kupokea rufaa zinazotoka kwa taasisi na watu binafsi asilimia kubwa ya maamuzi yamekubalika ambapo ni maamuzi mawili tu ndio yaliendelea katika ngazi zingine za kimaamuzi.
Mwanasheria huyo Mwandamizi alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali ambazo zinasimamiwa na mamlaka kama TCRA, SUMATRA, EWURA, FCC na TCAA kujitokeza kukata rufaa iwapo watakuwa hawajaridhika na maamuzi yao.

MSD yatataka uwekezaji zaidi sekta ya dawa

BOHARI ya Dawa nchini (MSD) imetoa rai kwa wawekezaji kuwekeza katika sekta ya viwanda vya kuzalisha dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ili kuhakikischa kuwa nchi inapiga hatua kiuchumi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD Isaya Mzoro wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema kutokana na ukweli kuwa asilimia 80 ya dawa, asilimia 95 ya vifaa tiba na vitendanishi vya maabara asilimia 100 huagizwa kutoka nje hali ambayo inachangia fedha nyingi kufaidisha nchi zingine.
Mzoro alisema ni vema wawekezaji wan je na ndani wakajitokeza kuwekeza katika viwanda ambavyo vitajihusisha na uzalishaji wa mahitaji yote ambayo yanahusu afya ya binadamu hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema kabla ya kuanzishwa MSD hapa nchini kulikuwa na viwanda vya kutengeneza dawa zaidi ya saba lakini hadi sasa ni viwanda viwili ambavyo vinafanyan kazi hivyo kusababisha Serikali kuagiza dawa kutoka nje.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba watu kutoka nje au ndani ya nchi kuwekeza katika sekta hii ya uzalishaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwani ni fedha nyingi ambazo zinaenda nje kwa lengo hilo,” alisema.
Aidha alisema pamoja na changamoto hiyo kubwa ya ukosefu wa viwanda MSD imefanikiwa kufikisha huduma za ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa huduma zao kwa asilimia 75 jambo ambalo linawapa matumaini kwa siku za karibuni.
Mzoro alisema MSD kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali ina mpango wa kupanua maghala kwa kukamilisha ujenzi wa awamu ya pili ili kuongeza nafasi za kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
Alisema MSD inatumia mfumo wa EPICOR 9 tangu mwezi Agosti 2012 ambapo wanatoa mafunzo endelevu kwa watumishi wao ili waweze kutoa huduma kwa haraka na kwa ufanisi.
Kwa upande mwingine Kaimu Mkurugenzi huyo alisema MSD inakabiliwa na changamoto nyingi kama ongezeko kubwa la mahitaji ya dawa ukilinganisha na uwezo serekali, ucheleweshaji wa kufikishwa pesa MSD kutoka hazina, Halmashauri kutotumia vyanzo vingine vya fedha, uhaba wa viwanda vya dawa nchini.
Changamoto nyingine taratibu za ununuzi kuchukua muda mrefu na baadhi ya zahanati na vituo vya afya kutopeleka maombi ya dawa na vifaa tiba katika kanda za MSD kama utaratibu unavyohitaji.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema matarajio yao ni kushirikisha sekta binafsi katika kusambaza dawa na vifaa tiba, kubandika orodha ya dawa na vifaa tiba vilivyokabidhiwa vituoni, kuendelea kuweka nembo ya serikali kwenye vidonge, kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma ya dawa na vifaa tiba na waganga kuwasilisha maombi mapema.

Shilole kukomaa na jiji videoni hivi karibuni

Zuwena Mohammed 'Shilole'
MUIGIZAJI nyota wa filamu anayejishughulisha pia na muziki, Zuwena Mohammed 'Shilole' yupo mbioni kuachia video ya wimbo wake unaoendelea kutamba wa 'Nakomaa na Jiji'.
Akizungumza na MICHARAZO leo, Shilole alisema video hiyo iliyorekodiwa nchini Marekani alipoenda ziarani hivi karibuni kwa sasa inahaririwa kabla ya kuachiwa hewani mashabiki waone namna anavyokomaa na jiji.
Shilole alisema tofauti na nyimbo za nyuma kama 'Lawama', ' Dada Dume', 'Dudu' au 'Paka la Baa' ambazo zipo katika miondoko ya 'Chakacha' safari hii ametoka kivingine katika Bongofleva kuonyesha uwezo alionao katika fani hiyo ya muziki.
"Wakati wimbo wangu wa 'Nakomaa na Jiji' ukiendelea kuwa gumzo kwa sasa, nakamilisha mipango ya kuachia video yake hivi karibuni ili kuwapa raha mashabiki wangu," alisema Shilole.
Mkali huyo, alisema video hiyo aliipiga katika jiji la New York alipoenda Marekani na kwamba kila kitu kimekamilisha kwa ajili ya kuhakikisha anaiachia mapema iwezekanavyo.
Pia alisema kutoka hadharani kwa video ya 'Nakomaa na Jiji' itakuwa fursa yake nyingine ya kujiandaa kutoa kazi nyingine katika mtindo wa 'bandika bandua'  ili kuwapa raha mashabiki wake.
Shilole alisema ana hazina kubwa ya muziki katika stoo yake na ndiyo maana kila mara anawaangushia mashabiki wake nyimbo mpya kali kama alivyofanya katika kazi zilizopita ambapo kabla ya 'Nakomaa na Jiji' alikuwa gumzo na wimbo wa 'Paka wa Baa'.

Side Boy Usimdharau Usiyemjua

Msanii Side Boy katika pozi
MSANII wa miondoko ya Bongofleva anayejishughulisha na ujasiriamali, Said Salim 'Side Boy Mnyamwezi', anayetamba na wimbo wa 'Hujafa Hujaumbika' yupo mbioni kuachia kazi mpya iitwayo 'Usimdharau Usiyemjua'.
Akizungumza na MICHARAZO, Side Boy alisema wimbo huo aliorekodi katika studio za Pamoja Records, ni utangiulizi wa nyimbo za albamu yake ya tatu anayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Side Boy aliyewahi kutamba na nyimbo kama 'Kua Uone', 'Jifungue Salama' na 'Pongezi wa Kikwete', alisema wimbo huo mpya ameuimba peke yake yake tofauti na kazi yake iliyopita ya Hujafa Hujaumbika alioimba na wasanii Best Naso na Aunty Ezekiel 'Gwantwa'.
"Baada ya kutamba na 'Hujafa Hujaumbika' kwa sasa najiandaa kuachia wimbo wa 'Usimdharau Usiyemjua' ambao nimeimba pekee yangu na ni utambulisho wa albamu yangu ya tatu inayokuja," alisema.
Side Boy alisema albamu hiyo ijayo inayofuata baada ya zile za 'Kua Uone' na 'Acha Waseme' itatoka ikiwa na cd mbili kwa moja ikijumuisha video na audio, ili kuwapa raha mashabiki wake na wale wa muziki wa ujumla.
"Albamu yangu ijayo ambayo bado sijaipa jina itatoka ikiwa na CD mbili,. moja video na nyingine au audio ili mashabiki wasisumbuke," alisema.,
Msanii huyo aliyewahi kufanya kazi pamoja na kundi la TMK Wanaume Family, japo hakuwa 'membaz' wa kundi hilo, alisema mashabiki wake wajiandae kupata ladha mpya toka kwake kutokana na albamu hiyo ya tatu anavyoiandaa kwa sasa itakayokuw ana nyimbo nane.

Kibudu cha Msechu kuandaliwa Kenya

Peter Msechu
 Na Elizabeth John

HATIMAYE ngoma inayokwenda kwa jina la ‘Kibudu’ liyoimbwa na mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Peter Msechu, imeanza kutamba katika vituo mbalimbali vya redio kutokana na ujumbe wa mashairi yaliyomo ndani yake.

Mbali ya kutamba na kibao hicho, mkali huyo alishawahi kutamba na kibao chake cha ‘Relax’, ‘Kumbe’ ambavyo vilifanya vizuri zaidi mbali na kuwa na vibao vingi ambavyo vilimtambulisha katika tasnia ya muziki huo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Msechu alisema katika kazi hiyo kamshirikisha mkali wa muziki huo, Ally Nipishe na kwamba tayari imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Alisema kibao hicho kakitengeneza katika studio ya Ufundi Production chini ya mtayarishaji wake mahiri, Fundi Samuel.
“Naomba mashabiki wangu wakipokee vizuri kibao hicho ambacho natarajia kukifanyia video yake Nairobi, Kenya,” alisema.

Msechu aliwataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa ajili ya video hiyo ambayo anatarajia kuitoa mwinzoni mwa mwezi ujao ikiwa ni pamoja na nyimbo nyingine nyingi zinazofuata.

Awamu ya kwanza usajili wa wachezaji wakamilika



Na Boniface Wambura
HATUA ya kwanza ya usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2013/2014 imefungwa rasmi jana (Agosti 5 mwaka huu) ambapo klabu zote za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zimewasilisha usajili wa vikosi vyao ndani ya wakati.

Baadhi ya klabu zimefanya makosa madogo madogo katika usajili ambapo zimepewa siku ya leo (Agosti 6 mwaka huu) kufanyia marekebisho kasoro hizo. 

Hivyo kesho (Agosti 7 mwaka huu) majina ya vikosi vyote yatabandikwa kwenye mbao za matangazo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa ajili ya kipindi cha pingamizi kitakachomalizika Agosti 12 mwaka huu.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa itakutana Agosti 13 na 14 mwaka huu kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.

Hatua ya pili ya usajili itaanza tena Agosti 14 mwaka huu ikihusisha wachezaji ambao watakuwa hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje ya Tanzania. 

Hivyo, dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29 mwaka huu.

TFF yaridhia 3 Pillars ya Nigeria kucheza Bongo



Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa baraka zote kwa timu ya 3Pillars Football Club ya Nigeria kucheza mechi za kirafiki nchini baada ya kupata idhini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Nigeria (NFF).

Awali tuliikatalia timu hiyo kucheza mechi za kirafiki nchini kwa vile haikuwa na barua kutoka NFF, lakini sasa Shirikisho hilo limetoa idhini hiyo. Pia ziara yake haikuwa inaratibiwa na wakala wa mechi anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) au mwanachama wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Klabu hiyo kutoka Jimbo la Lagos ilipanga ziara hiyo kwa kuwasiliana na chama cha mpira wa miguu cha jimbo hilo ambacho nacho kilitakiwa kuomba idhini NFF kwa niaba ya 3Pillars.

Hivyo timu hiyo inaweza kucheza mechi, kwani ziara hiyo sasa inaratibiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) ambaye ni mwanachama wetu.

Tunapenda kukumbusha kuwa watu pekee wanaotakiwa kuandaa mechi za kirafiki za kimataifa ni mawakala wa mechi wanaotambuliwa na FIFA au wanachama wa TFF.