STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 9, 2013

PFA yamshushua Luis Suarez


LONDON, Uingereza
LIVERPOOL haifungwi kimkataba kumuuza Luis Suarez, kwa mujibu wa mwenyekiti wa chama cha wachezaji wa kulipwa (PFA), Gordon Taylor.
Suarez anaamini kwamba ana makubaliano na klabu hiyo ambayo yatamruhusu kujiunga na klabu inayoshiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, kama wataletewa ofa inayozidi paundi milioni 40.
Klabu hiyo ya Anfield imekataa ofa ya paundi milioni 40 na ziada ya paundi 1 kutoka kwa Arsenal, na Taylor amesema Liverpool walichoafiki ni kwamba watafanya tu mazungumzo na klabu husika kama ofa hiyo italetwa.
Taylor aliiambia Press Association: "Kama una kipengele cha kuvunjia mkataba ni lazima kieleze wazi, lakini hapa (kwa Suarez) ni tofauti kwa sababu kinasema kama Liverpool itashindwa kufuzu Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na kama kuna ofa ya angalau paundi milioni 40 pande husika zitakaa mezani kujadili mambo lakini hakisemi kama klabu ni lazima imuuze.
"Iko wazi kwamba ofa ya paundi milioni 40 ndiyo kiwango awali cha kuanza mazungumzo, lakini inakuwa ngumu sana kwenye vipengele kama hivyo.
"Kuna kipengele cha 'maelewano ya kiungwana' katika suala 'siriasi' la mazungumzo ya uhamisho lakini siwezi kusema kinaibana Liverpool kwamba ni lazima imuuze.
"Luis ni mmoja wa memba wetu na tunataka kutoa sapoti yetu, hata hivyo, huenda anadhani kwamba ofa kama hiyo inaweza kulazimisha uhamisho."
Taylor pia alisema kwamba PFA itazungumza na Suarez na Liverpool katika jaribio la kulimaliza tatizo hilo.
Aliongeza: "Kwa sasa mambo hayako poa na sidhani kama ni hali nzuri kwa kila upande mchezaji au klabu zinazohusika.
"Hamna manufaa na ndiyo maana naona kwamba ni lazima tufanya kila tuwezalo tukae mezani na kuona kama kuna mazingira ya kufikiria uhamisho lakini kipengele kilichopo hakielezi wazi kwa asilimia 100.
"Tunawasiliana na pande zote kujaribu kuona kama suluhu itapatikana ambayo itazinufaisha pande zote."

Thursday, August 8, 2013

Javu aendeleza makali, Yanga wakiwagonga Wanigeria Taifa


MSHAMBULIAJI Mpya wa Yanga kutoka Mtibwa Sugar, Husseni Javu ameendelea kuonyesha makali yake baada ya jioni hii kuisaidia Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya 3 Pillars ya Nigeria.
Javu alijiunga hivi karibuni na mabingwa hao wa soka nchini hilo ni bao lake la pili baada ya Jumapili kuisaidia Yanga kuilaza timu yake ya zamani wakati walipoishindilia mabao 3-1 katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja waTaifa ilishuhudia karibu nyota wote wa Yanga akiwemo Mrisho Ngassa akishuka dimbani.

Ikiwa tumia washambuliaji wake wapya Hussein Javu na Mrisho Ngassa waliojiunga na kikosi msimu huu, Yanga ilikosa nafasi za wazi za kufungua kupitia kwa washambuliaji hao ambao hawakuonekana kuwa makini makini katika umaliziaji wa mipira iliyokuwa ikiwafikia.

David Luhende alikosa bao dakika ya 34 kufuatia mpira alioupiga kuokelewa na mlinda mlango wa 3Pillars FC na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda, huku awali Said Bahanuzi akikosa nafasi pia kama hiyo dakika ya 17 ya mchezo.

Hussein Javu aliipatia Young Africans bao kwanza dakika ya 40 ya mchezo kwa ustadi akiitumia vizuri nafasi hiyo aliyopewa na kuingo Athuman Idd 'Chuji' aliyewazidi ujanja walinzi wa 3Pillars FC na kumpasia Javu aliyeukwamisha mpira wavuni na kuhesabu bao kwa watoto wa Jangwani.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans -0 3Pillars FC.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ambapo Yanga iliwaingiza Didier Kavumbagu, Kelvin Yondani, Oscar Joshua, na Salum Telela kuchukua nafasi za Nadir Haroub, Jerson Tegete, Juma Abdul na Said Bahanuzi mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mchezo.

David Luhende ambaye leo alikuwa mwiba kwa timu ya 3Pillars FC nusura aipatie Yanga bao la pili lakini mpira alioupiga ulikokolewa na walinzi wa timu hiyo ya Nigeria na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Yanga iliendelea kulishambulia lango la 3Pillars dakika zote za mchezo lakini kutokua makini kwa mshambuliaji Didier Kavumbagu na Hussein Javu kuliendelea kuufanya ubao wa mabao uendelee kusomeka 1-0.

Mpaka dakika 90 za mwamuzi Oden Mbaga zinamalizika, Young Africans 1-0 3Pillars FC .

Kesho kikosi cha Yanga hakitakua na mazoezi na wachezaji wote watakua na mapumziko kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Eid na waterejea tena mazoezini siku ya jumamosi asubuhi katika uwanja wa Loyola kuendelea kujifua na maandalizi ya Ligi Kuu.

Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul/Salum Telela, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro'/Kelvin Yondani, 5.Rajab Zahir, 6.Athuman Idd 'Chuji/Issa Ngao, 7.Said Bahanuzi/Abdallah Mguhi 'Messi'/Shaban Kondo, 8.Haruna Niyonzima/Bakari Masoud, 9.Jerson Tegete/Didier kavumbagu, 10.Hussein Javu, 11.Mrisho Ngassa

Maskin Mhadhiri huyo wa UDSM auwawa kwa risasi Dar



Picture: Patrick Rweyongeza

Mhadhiri wa College of Engeneering katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM, Patrick Rweyongeza, ameuawa jana kwa kupigwa na risasi.

Tukio limetokea jana mchana katika maeneo Magomeni-TANESCO wakati marehemu akielekea mjini ambapo watu waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki walimfuata na kumfyatulia risasi na kisha kutokomea.

Inatisha! Tindikali zahamia kwa wageni

RAIA wawili wa kigeni kutoka katika nchi ya Uingereza ambao wanafanya kazi ya kujitolea katika upande wa ualimu  wamemwagiwa tindi kali mjini Zanzibar jana jioni katika mitaa ya Shangani Mji Mkongwe  visiwani Zanzibar.
Habari kutoka katika chanzo chetu cha habari  kinasema Jeshi la Polisi Zanzibar limeanza msako na kuwatafuta watu waliofanya kitendo hicho dhidi ya walimu hao wa kike waliofika Zanzibar kwa kujitolea kufundisha walitambulika kwa majina ya Kate Gee (18) na Kirsiwer Trup (18) na walikuwa na wiki mbili tu.
Walimu hao waliokutwa na janga hilo walikuwa wanafanya kazi katika shule  moja ya msingi inayojulikana kama Mtakatifu Monika iliyopo chini ya kanisa la Aglicana. habari tulizozipata hivi punde  Raia hao hivi sasa wamehamishiwa katika Hospitali ya Aghakani jijini Dar es salaam kwa matibabu zaid tutazidi kuwaleta habari zaidi.
Tukio hilo limetokea wakati hakuna taarifa zozote za matukio ya nyuma ya kumwagiwa watu tindikali visiwani humo akiwamo Katibu wa Mufti visiwani humo na yale yanayotokea Tanzania Bara maeno ya Dar na Arusha hivi karibuni.

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA


VIPIGO vinne mfululizo ilivyopata timu ya taifa 'Taifa Stars' imezidi kuiporomosha Tanzania katika orodha ya viwango vya soka duniani ambapo orodha mpya iliyotolewa inaoonyesha ipo nafasi ya 128 toka 121 kwa mwezi uliopita.
Moja wa timu ilizozikwanyua Tanzania katika mbio za kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia, Ivory Coast yenyewe nayo imeporomoka kwa nafasi tano kutoka namba 13 iliyokuwa katika orodha iliyopita hadi kwenye nafasi ya 18 japo inaendelea kutamba barani Afrika ikishika nafasi ya 1.
 ikifuatiwa na Ghana ambao wamesalia nafasi yao ya 24 duniani.
Nchi za Cape Verde imeendelea kupanda chati safari hii kwa nafasi 13 duniani ikikamata namba 36 toka 49 za mwezi uliopita huku barani Afrika ikishika nafasi ya 6 toka ya nane iliyokamata orodha ya awali, huku Cameroon iliyoonekana kuyumba akwa siku za karibu ikipanda kwa nafasi 20 ikishika nafasi ya 51 toka 71 ya awali na Afrika ikishika nafasi ya 8.
Orodha ya jumla ya dunia kwa nafasi za 12 Bora zimesalia kama zilivyo kwa Hispania kuendelea kuongoza ikifuatiwa na Ujerumani, kisha Colombia, Argentina, Uholanzi,  Italia, Ureno, Croatia, Brazili na Belgium, kisha Ugiriki na kumalizwa na Uruguay, huku Marekani wakirejea tena kwwenye Top 20 ya Dunia safari hii.
Orodha kamili mpya ya FIFA unaweza kuipata katika:FIFA World Ranking

Hivi ndivyo Extra Bongo ilivyowatambulisha wanenguaji wao wapya Leaders

Wanenguaji wapya wa Extra Bongo, Jolie na Grace wakionyesha makeke yao

Tunatomboka namuna hii ...ayaa ayaaa hiiiiii
Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki (mwenye kofia) akiwatambulisha wanenguaji wao wao huku Super Nyamwela akiwa makini kumsikiliza pembeni kulia. Kushoto ni Papii Catalogue
Mi naitwa Jolie Kindu au Muringo Ngassa nimekuya Kutanzanie kwa ajili ya kufunika madancers wote mutaona
Msiniangushe jamani, nimeshawafagilia kwa mapaparazi kuwa nyie ni nouma sawasawaaa?
Ally Choki akitoa ufafanuzi kwa wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa waneguaji wao wawili kutoka Kongo.
Choki alikuwa na kazi kubwa ya kufafanua baadhi ya mambo juu ya madansa hao wanaojiita Mrisho Ngassa na John Bocco ambao watatambuilishwa rasmi kesho kwenye onyesho la Idd Mosi Meeda Club bna Idd Pili itakuwa zamu wa wakazi wa Mbagala kwani Extra Bongo watakuwa Dar Live

Mwanafunzi wa darasa la kwanza afa kwa kugongwa na gari Mbeya

 [ DIWANI ATHUMANI  - ACP ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


WILAYA YA  KYELA - AJALI YA  GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA        
                                            KUSABABISHA KIFO.
MNAMO TAREHE 07.08.2013 MAJIRA YA  SAA 08:30 HRS HUKO KATIKA ENEO LA KALUMBULU  WILAYA YA  KYELA  MKOA WA MBEYA. GARI  T.932 BUF AINA YA  T/IPSUM IKIENDESHWA NA KAIMU S/O HENDE, MIAKA 33, MBONDEI, MKULIMA  MKAZI WA KYELA-KATI  ILIMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU MTOTO HAWA D/O GIBSON,MIAKA 6,MSAFWA,MWANAFUNZI DARASA LA KWANZA S/MSINGI MBUGANI  MKAZI KALUMBULU NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO.  MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA. CHANZO NI MWENDO KASI, DEREVA AMEKAMATWA. TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
Signed by:
 [ DIWANI ATHUMANI  - ACP ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Huyu ndiye jambazi wa kwenye ATM, lanaswa kilaini Dar baada ya mtego

Mtu anayedaiwa kuwa mwizi wa kwenye ATM rais wa Bulgaria akiwa chini ya ulinzi baada ya kunaswa akiiba jijini Dar es Salaam kutokana na kuwekewa mtego kumnasa


MSAKO wa wezi wa kwenye Mashine za Kutolea Fedha (ATM), umeanza kuzaa matunda baada ya raia wa Bulgaria kukamatwa akiiba kwenye ATM ya Bank of Africa (BOA), Tawi la Afrikana, Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za benki, mtuhumiwa huyo ambaye
hakutajwa jina lake alikamatwa baada ya kamera maalumu zilizowekwa kwenye ATM za BOA, kumtambua kuwa ni mwizi sugu wa benki hiyo anayetafutwa.

Mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa si msemaji, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 12 asubuhi baada ya mtuhumiwa huyo kuwekewa mitambo maalumu ya kumnasa.

Alisema benki hiyo ilipelekewa malalamiko na baadhi ya wateja kwamba wakienda kutoa fedha kwenye ATM wanakuta akaunti zao hazina salio wakati wanaamini zilikuwa na fedha.

Chanzo hicho cha habari kilidai kuwa baada ya kupelekewa malalamiko hayo, waliweka mitambo maalumu ya kuwawezesha walinzi wa maeneo ya ATM za BOA kumbaini mtu atakayetoa fedha kwa njia ya wizi.

“Kama Benki tuliweka mtambo maalumu na mtuhumiwa huyo alionekana kwenye mtambo wetu, hivyo tuliwaagiza walinzi wetu watakapomwona mtu huyo wamkamate haraka 
sana,”alisema.
Alisema mtuhumiwa huyo alianza mchezo huo kwa muda mrefu ambapo kwa kutumia kadi za ATM zisizojulikana idadi yake, alikuwa anakwenda kwenye ATM mbalimbali za benki hiyo na kutoa fedha hadi Sh10 milioni.

Kuhusu tukio la jana, mmoja wa walinzi wa BOA aliyejitambulisha kwa jina moja la Frank alisema mtuhumiwa huyo alipofika kwenye ATM hiyo aliingia na kuchukua fedha ambazo alizipeleka kwenye gari lake.
Frank alisema baada ya kupeleka fedha hizo, alirudi kwa mara ya pili ili achukue fedha nyingine ndipo walinzi hao walimkamata na kumfunga pingu.

“Huyu mtuhumiwa mwenye asili ya Kiarabu alifika na gari lake saa 12 asubuhi, aliingia kwenye ATM na kutoa fedha ambazo hazikujulikana ni shilingi ngapi na kuzipeleka kwenye gari lake, baadaye alirejea tena kwa ajili ya kutoa fedha zingine, wakati anaingia ndipo alipokamatwa na mlinzi aliyekuwa analinda hapo,” alisema Frank.

Kamanda wa Polisi Kinondoni, Camilius Wambura alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi hilo huku uchunguzi dhidi yake ukiendelea.

“Ni kweli taarifa nimezipata, mtuhumiwa amekamatwa, bado hatujajua ni kiasi gani ambacho ameiba kwa kutumia mtandao, tunaendelea na uchunguzi,” alisema Wambura.

Tukio kama hili lilishawahi kutokea mkoani Mwanza Februari 19 mwaka huu na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na maofisa ya Benki ya NMB liliwatia mbaroni watu watatu ambao walidaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti.

MWANANCHI

Real Madrid yaichakaza Chelsea 3-1, Mourinho

KIUNGO Frank Lampard alicheza kwa mara ya kwanza majira haya ya joto, lakini alishindwa kumzuia Cristiano Ronaldo kuinyanyasa Chelsea jana.
Kabla ya mechi hiyo na Real Madrid mjini Miami, kiungo huyo mkongwe alikosa mechi zote za kujiandaa na msimu za klabu, Stamford Bridge kutokana na kuwa majeruhi.
Lakini Lampard ameimarika na kuanza kazi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu dhidi ya Hull City, Agosti 18 baada ya kumaliza dakika 45 za kwanza katika Fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
Katika mechi hiyo, mabao mawili ya Ronaldo na moja Marcelo, yalitosha kuitotesha timu ya Jose Mourinho 3-1 dhidi ya timu yake ya zamani ambayo kwa sasa inafundishwa na Carlo Ancelotii.
Chelsea ilipata bao lake pekee kupitia kwa Ramires.  
Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Khedira, Isco, Ozil, Ronaldo na Benzema.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Lampard, Van Ginkel, Ramires, Oscar, Hazard na Lukaku.
On target: Cristiano Ronaldo scored a brace as Chelsea went down to the La Liga giants
Kiboko yao: Cristiano Ronaldo amefunga mabao mawili dhidi ya Chelsea jana
Party time: Real Madrid stars celebrate with the International Champions Cup after beating Chelsea
Kujiachia: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea na taji lao la Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness
Lethal: Ronaldo blasted home a free-kick and later added a header to help Madrid secure the game
Kitu hichoo: Ronaldo akifunga kwa mpira wa adhabu
Unloved: A Real Madrid fan holds up a banner showing he doesn't care that Mourinho left the club
Mapenzi yameisha: Shabiki la Real Madrid likiwa limebeba bango kuonyesha kutojali kuondoka kwa Mourinho katika klabu hiyo
Chinwag: Mourinho and former Chelsea boss, and current Madrid manager, Carlo Ancelotti, have a chat
Mazungumzo baada ya tukio: Mourinho na kocha wa zamani wa Chelsea, ambaye kwa sasa ni kocha wa Madrid, Carlo Ancelotti wakizungumza baada ya mechi
Triumphant: Real Madrid stars celebrate after beating Chelsea in the final of the Champions Cup
Mabingwa: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea kuifunga Chelsea katika fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
 BI ZUBEIRY BLOG

Answar Sunnah wala Eid yao leo sawa wa wengine duniani


WAISLAM WA AN-SUNA WAMEJUMUIKA  NA WAISLAM WENZAO DUNIANI KUSHEREHEKEA SIKU  HIYO BAADA YA KUMALIZIKA KWA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANIPICHA WAKIWA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI LEO

WAKISALI KWENYE VIWANJA VYA JANGWANI LEO

Waumini wa Kiislam wakisujudu wakati wa swala ya Eid iliyoswaliwa leo na sehemu kubwa ya waumini duniani wanaofuata kalenda ya Kiislam

Wednesday, August 7, 2013

Wanafunzi wafa maji Tabora kisa Bata Mzinga


WANAFUNZI wawili wa shule ya msingi Itobo wilaya ya Nzega mkoani wa Tabora wamekufa maji katika bwawa wakati wakiwinda bata mzinga. 

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Peter Ouma alisema Massanja Shija (42) ambaye ni baba wa mmoja wa watoto hao waliokufa, amenusurika katika tukio hilo baada ya kunasa kwenye tope.

Kamanda alitaja watoto waliokufa ni Elias Massanja (13) na Shabani Ramadhan (15) wote wanafunzi wa darasa la sita shule ya Msingi Itobo. Tukio hilo ni la Julai 30 mwaka huu, saa 12:30 jioni katika Kijiji cha Chamwabo, Kata Itobo.

Ouma alisema walikuwa wakiwinda bata mzinga ambaye aliruka na kwenda kwenye bwawa na katika kumfuata, walizama katika kina kirefu cha maji.

Alisema baada ya kuzama, jitihada za kuokoa miili yao ilikuwa ngumu kutokana na kukosa waokoaji. Hata hivyo baadaye iliopolewa.

Mbunge wa Jimbo la Bukene, Selemani Zedi alisema tukio hilo ni la kusikitisha kwa jamii. Aliwataka wananchi kuwa makini na mabwawa.

Shindano la BSS sasa TBC1 siyo ITV tena, kisa....!

 
Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 

Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.

“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1. 

Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.

Extra Bongo yanasa wawili toka Congo kuwatambulisha siku ya Eid

 KATIKA kujiimarisha zaidi na kutaka kuendelea kufunika nchini bendi ya Extra Bongo 'Wana Next Level' maarufu kama Wazee wa Kizigo, wamewanyakua wanenguaji wapya wawili wa kike kutoka DR Congo watakaotambulishwa rasmi kwa mashabiki katika maonyesho ya sikukuu ya Eid el Fitri.
Wanenguaji hao walitambulishwa mchana wa leo kwa wanahabari ni Jolie Moncotina Kindu 'Mrinsho Ngassa' na Grace Messu Kamba (Fatuma) au maarufu kama John Bocco waliodai wanatoka katika makundi ya wanamuziki Werrason Ngiama Makanda na Ferre Golla.
Utambulisho huo ulifanyika kwenye viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade' alisema wanenguaji hao tayari walioshaanza mazoezi na wasanii wenzao ila walikuwa wakisubiri vibali vya kufanya kazi nchini.
"Tumekuwa nao kwa muda wakiendelea na mazoezi wakati tukihangaikia vibali vyao na tunashukuru vibali vimepataika ana hivyo watawatambulishwa rasmi katika maonyesho yetu ya sikukuu ya Eid katika kumbi za Meeda Club-Sinza Mori na Dar Live," alisema Choki.
Aidha Choki alisema bendi yao pia itatambulisha siku hiyo kwa mashabiki wao nyimbo mbili mpya za 'Hafidh' uliotungwa na Michael Athanas 'Montanabe' na 'Mwanamke Hapigwi' Papii Catalogue.
"Pia kutakuwa na nyimbo mbili zitakazotambulishwa sambamba na zile mbili za Mgeni wa Khadija Kimobitel na Sagna nilioutunga mimi lakini anaimba sehemu kubwa Kimobitel," alisema.
Nao wanenguaji hao walioonyesha manjonjo yao kwa wanahabari, walisema wamekuja nchini kuonyesha namna ya kunengua, huku wakisema wanajiita majina ya washambuliaji hao nyota wa soka wa Taifa Stars kutokana na kukunwa na umahiri wao dimbani.
"Tangu niko kule Kin, namuonaga Murisho Ngassa namna anavyochezaga nami navutiwa na yeye ndiyo najipa hii jina yake, na nitafunika kama Ngassa," alisema Jolie ambaye angalau anakifahamu kiswahili kuliko mwenzake aliishia kusema yeye ni John Bocco tu.
Naye Rapa Catalogue alisema wimbo wake mpya una lengo la kuleta mabadiliko na utetezi kwa wanawake kutokana na mikstari yake inayoasa wanaume kutowapiga wanawake wala kuwanyanyasa badala yake iwatunze vyema ili wasije wakawaacha na kupata wanaojua kubembeleza.
"Pia kuna rapu mpya nitatitambulisha siku hiyo inayosema tutaishie Dar bila ya kazi, tutaishije Dar es Salaama bila ya kazi wakati taka, maji umeme na kila kitu lazima pesa..." alisema rapa huyo mahiri.
Kiongozi na mwalimu wa uenguaji wa bendi hiyo, Super Nyamwela alisema kutua kwa wasanii hao wawili kumeongeza chachu na kuboresha safu yao na kwamba hataki kusema mengi ila kuwataka mashabiki wajitokeze katika maonyesho yao waone kazi.
"Sitaki kusema sana kwa sababu hakuna asiyemjua Nyamwela na kazi yake, mimi ni mwalimu na mashabiki waje waone kwa nini anaitwa mwalimu, wenzetu wamezoea kuongea sasa ila mimi na bendi yangu ni watu wa vitendo zaidi," alisema Nyamwela.

Majambazi wamuua kwa risasi Mfanyabiashara wa madini Arusha

 
Mwili wa Erasto Msuya ukiwa chini baada ya kupigwa risasi.
 
MFANYABIASHA maarufu wa madini aina ya Tanzanite ambeye pia ni mmiliki wa hotel ya kitali ya S.G Resort ya jijini Arusha anayefahamika kwa jina la Erasto Msuya amefariki dunia leo majira ya alasiri baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wakati alipokuwa akitokea Mirerani akielekea jijini Arusha.
Taarifa kutoka kwa shuhuda wa tukio hilo zinaeleza kuwa Bwana Erasto Msuya alisimamishwa na watu hao karibu na njia panda ya KIA (Kilimanjaro International Airport) na aliposimama walimtishia kwa kutumia bastola na kumtaka afate matakwa ya watu hao ndipo Erasto alipotoa bastola ili aweze kujitetea ndipo majambazi hao walipo amua kumpiga risia ambazo idadi yake haikuweza kufahamika kwa haraka.

NMB YASHIRIKI FUTARI NA WATEJA WAKE


 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akishukuru uongozi wa NMB kwa kuandaa wasaa mzuri na kushiriki katika kukamilisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.Hii ilikua katika futari iliyoandaliwa na Benki ya NMB tawi la Zanzibar  kwenye hoteli ya Zanzibar Ocean view Zanzibar mwishon mwa wiki.
  Mkuu wa kitengo cha akaunti binafsi wa NMB, Abdulmagid Nsekela akiongoza wageni waalikwa katika kupata futari.
  Meneja Mawasiliano NMB, Josephine Kulwa nae hakubakia nyuma kushiriki futari na wateja wa NMB
Maofisa wa NMB wakiwa wameambatana  kuingia ukumbini na mgeni rasmi (katikati) katika hafla hii ya kushiriki futari na wateja wa NMB mjini Zanzibar.

MKUTANO WA DHARURA WA WANACHAMA WA YANGA AGOST 18



1.   Hivi karibuni tumepata uhakika kuwa Tanzania Premier League (TPL) na Azam Media wanayo nia ya kuingia mkataba wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu (Premier League) kwa msimu wa 2013/2014, 2014/2015 na 2015/2016


2.   Baada ya Kamati ya Utendaji ya YANGA kufanya uchambuzi wa kina juu ya taarifa ya makubaliano ya kibiashara ya TPL / Azam Media ilihitimisha kuwamkataba huu hauna maslahi kwa YANGA, na kwa hivyo, Kamati ya Utendaji ya YANGA ilifikia uamuzi kuwa mechi za YANGAzisirushwe hewani na Azam Media.


Kwa kuwa wawazi, Kamati ya Utendaji ya YANGA ilitoa taarifa kwa wanachama wa YANGA kupitia vyombo vya habari tarehe 29 Julai, 2013 ambapo iliweka bayana sababu zake na kueleza kuwa YANGAhaina tatizo na vilabu vingine vya mpira wa miguu ikiruhusu mechi zao kurushwa na Azam Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mechi zake za Vodacom Premier League katika Azam Television.


3.   Sote tumeona baada ya hapo kuwa “nguvu ya ziada” inatumika kupotosha msimamo wa Kamati ya Utendaji ya YANGA na kuidhalilisha Klabu ya YANGA hadharani


Juu ya hayo Na Kwa kushangaza Sana, baadhi ya vilabu vya mpira WA miguu ambavyo vina sifa kuwa havijawahi kushinda Ligi Kuu, vimeundwa hivi juzi tu, havina uzoefu wowote WA kucheza soka kimataifa n.k. vina kuja kuyapanga Kamati ya Utendaji ya YANGA jinsi ya kuendesha shughuli za Klabu ya Yanga, vikiwa vinasahau vilabu vyao wenyewe na badala yake kuiingilia YANGA kwa sababu zinazojionyesha wazi.


Inadhihirika wazi kwamba kuna ushirikiano usio mzuri unaoashiria kula njama kuilazimisha YANGA iruhusu mechi zake zirushwe na Azam Television.


Kwa kuwa YANGA ni Klabu ya Wanachama yenye kupata nguvu kutokana na misingi yake ya kidemokrasia iliyojijengea na uamuzi wake wa mwisho unatokana na Wanachama wake mwenyewe, umeamua kuliweka suala hili zima kwa Wanachama wa Yanga ili waamue ni njia gani ya kufuata kwa maslahi ya Klabu yetu.


Kwa kuzingatia hali hiyo basi, na kulingana na mamlaka niliyonayo kama Mwenyekiti wa YANGA, natangaza mkutano wa dharura wa Wanachama wa YANGA tarehe 18 Agosti, 2013 utakaofanyika uwanja wa Sabasaba kwenye ukumbi wa PTA saa 3.30 asubuhi waje tujadiliane na kuamua suala la Azam Television kurusha mechi za YANGA.

AIRTEL YATOA CHAKULA CHA FUTARI NA IDDI KWA YATIMA DAR

 Afisa mauzo wa Airtel,  Bw Salehe Safi  akimkabidhi  Bibi  Saada Omary
moja ya zawadi zilizotolewa na kampuni za simu za mkononi  ya Airtel
kwenye kituo cha watoto yatima kinachofahamika kwa jina la Mwana
Orphanage Center kilichopo Vingunguti jijini Dar es salaam.   AIRTEL
ilitoa sukari, mchele, mafuta, sabuni, maziwa na Unga wa ngano
kwaajili ya kumalizia mwezi wa Ramadhani na kusheherekea sikukuu ya
IDDI.


Baadhi ya watoto yatima katika kituo cha Mwana Orphanage kilichopo
maeneo ya Vingunguti jijini Dar es salaam, wakiwa wameshikilia baadhi
ya zawadi walizokabidhiwa na kampuni ya simu za mkoni Airtel Tanzania.
AIRTEL ilitoa sukari, mchele, mafuta, sabuni, maziwa na Unga wa ngano
kwaajili ya kumalizia mwezi wa Ramadhani na kusheherekea sikukuu ya
IDDI.