STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 15, 2014

Hivi ndivyo Iraq Hudu 'Kimbunga' alivyopumzishwa makaburi ya Kisutu jana

Jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu Iraq Hudu 'Mkumwena' wakipeleka mwili kuzika katika makaburi ya Kisutu Dar es salaam kwa ajili ya kumuhifadhi
Baadhi ya waombelezaji wakitia udongo katika kaburi la marehemu Iraq Hudu wakati wa maziko yaliyofanyika leo katika makaburi ya Kisutu Dar es salaam
Baadhi ya waombelezaji na mabondia wakiwa nyumbani kwa marehemu Iraq Hudu kutoka kushoto ni bondia Adwer George, Rashidi Matumla, Rais wa Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini Yasini Abdallah na Mwenyekiti wa Shiwata Cassim Twalibu 
Mtoto wa Marehemu Iraq Hudu, Daniel Hudu  kushoto akisalimiana mabondia Adrwe George,Rashidi Matumla na Rais wa TPBO Yassin Abdallah
Mtoto wa Marehemu Iraq Hudu, Daniel Hudu  kushoto akisalimiana mabondia Adrwe George,Rashidi Matumla na Rais wa TPBO Yassin Abdallah
Mashekhe wakisoma duwa kabla ya kwenda kuzika
Meneja wa bendi ya msondo ngoma Said Kibiriti akisalimiana na mabondia
Baadhi ya waombelezaji waliojitokeza
Mtangazaji Maulid Baraka Kitenge akizungumza na mabondia mbalimbali wakati wa msiba wa bondia Iraq Hudu
Mtangazaji wa kipindi cha Michezo Maulid Baraka Kitenge akisalimiana na bondia mkongwe ambaye kwa sasa ni kocha wa MKoa wa Tanga katika wilaya ya Muheza Charles Mhillu 'Spinks'
Bondia Marehemu Iraq Hudu 'Kimbunga' kulia enzi za uhai wake katikati ni marehemu bondia Papa Upanga
Bondia Iraq Hudu' Kimbunga kulia akipambana na Stanley Mabesi katika mpambano wao
IRAQ HUDU
WAOMBWELEZAJI WAKIWA WAMEBEBA JENEZA LA MAREHEMU IRAQ HUDU
WAOMBWELEZAJI WAKIWA WAMEBEBA JENEZA LA MAREHEMU IRAQ HUDU
Mmoja wa waombelezaji kulia akimpa pole bondia Chuku Duso katika msiba wa bondia Iraq Hudu
Ibrahimu Kamwe na Said Chaku
wadau mbalimbali wa mchezo wa ngumi
WAOMBWELEZAJI WAKIWA WAMEBEBA JENEZA LA MAREHEMU IRAQ HUDU

WAOMBELEZAJI WAKITIA UDONGO KWENYE KABURI LA MAREHEMU IRAQ HUDU
WAOMBELEZAJI WAKITIA UDONGO KATIKA KABURI LA IRAQ HUDU
WAOMBELEZAJI WAKITIA UDONGO KATIKA KABURI LA IRAQ HUDU

Ivory Coast yaizima Japan, Balotelli aiua England

Balotelli akiiangamiza England

Andre Pirlo akonyesha ujuzi wake

Kitu


Danile Sturridge akishangilia bao lake aliloifungia England


Kitu jamaniii



Gervinho akishangilia bao lake la ushindi na wachezaji wenzake wa Ivory Coast

Yaya Toure akiwatesa wachezaji wa Japan alfajiri ya leo wakati wakiibuka na ushindi wa 2-1

WAWAKILISHI wa Afrika kwenye Kombe la Dunia, Tembo ya Ivory Coast wamewatoa kimasomaso Waafrika baada ya alfajiri ya leo kuifumua Japan mabao 2-1 huku England wakiendelea kuwa wateja kwa Italia kwa kuzabuliwa idadi katika hiyo katika mfululizo wa fainali hizo zinazofanyika nchini Brazil.
Ushindi wa Ivory umewapoza waafrika ambao waliishuhudia timu yao nyingine Cameroon ikianza vibaya kwa kichapo cha bao 1-0 toka kwa Mexico katika mechi ya kundi A.
Mabao ya Wilfried Bony na Gervinho katika kipindi cha pili kimeifanya timu hiyo kutoka nyuma ilipotanuliwa kufungwa na Japasn na kuvuna pointi tatu zao za kwanza katika michuano hiyo ya Dunia ikiwa nyuma ya Colombia inayoongoza kundi C baada ya kuitandika Ugiriki mabao 3-0.
Japan waliwashtua Tembo hao wa Ivory Coast walipojipatia bao la kuongoza katika dakika ya 16 Keisuke Honda na kudumu hadi mapumziko.
Hata hivyo kipindi cha pili Ivory Coast walijipanga na kurejesha bao hilo dakika ya 64 kupitia Bony na dakika mbili baadaye Gervinho alimalizia udhia kwa kufunga bao la ushindi.
Katika mechi nyingine iliyochezwa usiku wa manane, Italia iliendelea kuitesa England kwa kuicharaza mabao 2-1 katika pambano lililokuwa kali na la kusisimua.
Mario Balotelli ndiye aliyekuwa mwiba wa England baada ya kufunga bao la pili na la ushindi dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili na kuzima ndoto za vijana wa Hodgsons kulipa kisasi cha kung'olewa kwenye robo fainali ya Kombe la Ulaya.
Italia walionyesha dalili za kuibuka na ushindi mapema baada ya Claudio Marchiso kufunga bao dakika ya 34 kabla ya Daniel Sturridge kusawazisha dakika tatu baadaye na kuzifanya timu hizo zienda mapumziko zikiwa nguvu sawa ya kufunga bao 1-1.
Ndipo katika kipindi cha pili Mario Balotelli alipodhihirisha kuwa yeye ni mchezaji muhimu katika kikosi cha Azzurri alipofunga bao la pili lililoiweka Italia katika nafasi ya pili katika kundi D nyuma ya Costa Rica iliyoifumua Uruguay kwa mabao 3-1 mapema jana.
Michuano hiyo itaendelea tena siku ya leo kwa michezo ya kundi E ambapo itaumana na  Ecuador kabla ya Ufaransa kushuka dimbani kupepetana na Hondurus na pambano jingine la usiku wa manane litazikutanisha timu za kundi F Argentina dhifi ya Bosnia-Herzegovina.

Friday, June 13, 2014

Steve Nyerere atema cheche Bongo Movie

Steve Nyerere (kushoto) akiwa na Mkwere kwenye msiba wa Mzee Small
MWENYEKITI wa Bongo Movie, Steve Nyerere amesema umefika wakati wasanii wa filamu nchini na waigizaji kwa ujumla kujenga utamaduni wa kupenda kusaidiana wakati wanapokuwa na shida badala ya kuonyesha umoja na mshikamano kwenye misiba tu.
Steve alisema wasanii wamekuwa wepesi kujitokeza na kuonyesha umoja na mshikamano kwenye mazishi ya wenzao, lakini wamekuwa wazito wakati wasanii wenzao wanapokuwa na matatizo ikiwamo kuugua au janga lolotge linalowapata kitu ambacho alidai siyo kizuri.
Akizungumza na MICHARAZO kwenye msiba wa Mzee Small, Steve Nyerere ambaye majina yake kamili ni Steven Mengele alisema ni aibu wasanii na wadau wa sanaa kuchangishana fedha wakati wa misiba ya wenzao wakati wanapokuwa wagonjwa wanashindwa kutoa fedha kuwasaidia kuokoa uhai wao.
Muigizaji huyo na muigaji wa sauti za watu mashuhuri duniani, alisema anajisikia aibu na kujifunza mambo mengi kupitia msiba wa Mzee Small ambaye amekufa huku akisononeka kutengwa na waigizaji wenzake wakati akihitaji msaada wa matibabu.
"Ifike wakati wasanii sasa tukajenga utamaduni wa kusaidiana wakati wa matatizo, Mzee Small alikuwa anaugua naamini fedha ambazo zinatumika leo kugharamia mazishi yake ingetosha kusogeza uhai wake hata kama kifio kimeumbwa kwa kila mtu na hakuna wa kuweza kuzuia kisimfikie yeyote," alisema.
Alisema tayari chini ya uongozi wake wameunda mfuko wa kusaidia wasanii wenye matatizo na wapo katika mchakato wa kufanya mazungumzo na taasisi za kijamii na fedha kama NSSF, PSPF na GPRF na Bima ya Afya ili kuwezesha wasanii kujiunga nayo na kujiwekea akiba inayoweza kuwasaisdia wanapokuwa wamekwama.
"Pia kama wazo alililotoa Mkuu wa Mkoa, Meck Sadick wakati wa kuagwa marehemui George 'Tyson' Otieno juu ya kuanzisha Saccos au benki tunalifanyia kazi na Inshallah mambo yakikaa vyema tutaanika kila kitu hadharani, kwa sababu hali inatosha na wasanii wamekuwa wakiumia wanapokumbwa na matatizo kama haya," alisema

Newz Alert! Bondia Iraq Hudu 'Kimbunga' afariki, kuzikwa kesho

MISIBA imeendelea kuiandama fani ya michezo na burudani baada ya alfajiri ya leo bondia nyota wa zamani wa ngumi za kulipwa, Iraq Hudu 'Kimbunga' kufariki akiwa amelazwa kwenye hiospitali ya  Hindu Mandal, Dar es Salam.
Kwa mujibu wa mpwa wa bondia huyo aliyetisha kwa ngumi nzito na kutwaa ubingwa katika ngumi za ridhaa kabla ya kuingia zile za kulimwa miaka ya 1990, Rajab Mhamila 'Super D', Kimbunga alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Figo na kwamba anatarajiwa kuzikwa kesho majira ya saaa saba mchana.
Super D alisema msiba wa biondia huyo upo nyumbani kwake  Buguruni Kisiwani na mazishi yatafanyika kwenye makaburi ya Kisutu.
Msiba huo wa Kimbunga umekuja wakati wadau wa michezo na burudani wakiwa bado wanaendelea kuomboleza vifo vya wasanii na wanamichezo kadhaa waliokumbwa na mauti ndani ya kipindi cha mwezi mmoja sasa.
Baadhi ya waliokumbwa na mauti kwa siku za karibuni ni wanamuziki Muhidini Mwalimu Gurumo, Amina Ngaluma 'Janapese', Recho Haule, Adam Kuambiana, George Tyson, Mzee Small, Abdallah Sumbwa, Ally Mwanakatwe na nahodha wa zamani wa KMKM ya Zanzibar.

Balotelli kutua Arsenal kwa msaada wa Puma

KAMPUNI ya usambazaji wa vifaa vya michezo, Puma itaisaida Arsenal kufanikisha mpango wa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli kutoka AC Milan.

Mpachika mabao huyo anadhaminiwa na Puma, ambao pia mapema Januari walitangaza kuidhamini Arsenal.

Mustakabali wa Balotelli ndani ya Milan uko shakani baada ya Rais Silvio Berlusconi kusema bado hajaamua lolote kuhusu mchezaji huyo na mchambuzi wa Sky Sport nchini Italia, Mario Giunta akaandika: "Arsenal inamtaka sana Balotelli na Arsene Wenger atafanya kitu chochote kumhamishia London. 
Kutua kwa mshambuiliaji kwa Wapiga Mitutu hao wa Londo kutakuwa msaada mkubwa katika safu ya ushambiuliaji inayomtegemea Oliver Giroud.

Fabregas atua rasmi Chelsea kama utani

CHELSEA wamekamilisha usajili wa kiungo wa zamani wa Arsenal, Cesc Fabregas kutoka Barcelona kwa ada ya uhamisho inayoaminika ya paundi milioni 30 na amesaini mkataba wa miaka mitano.
Fabregas aliiambia tovuti rasmi ya klabu hiyo: "Kwanza napenda kumshukuru kila mmoja klabuni FC Barcelona ambako nimefurahia miaka mitatu mizuri. Ilikuwa ni klabu yangu ya utotoni na daima nitajivunia kwamba nilikuwa na fursa ya kuchezea timu kubwa kiasi hicho.
"Najiona bado nina kazi ambayo sijaimaliza katika Ligi Kuu ya England na sasa ni wakati mwafaka kurejea.
"Nilitafakari ofa nyingine zote kwa umakini na nikaona kwamba Chelsea ni chaguo bora. Wanalingana na malengo yangu ya soka kutokana na njaa yao ya kutwaa makombe. Wana kikosi cha wachezaji wazuri na kocha babkubwa. Nimeingia kikamilifu katika timu hii na nashindwa kuendelea kusubiri kuanza kazi."
Fabregas alifunga magoli nane katika La Liga akiwa na Barcelona na kutoa pasi za mwisho zilizozaa magoli 19 katika mechi 36 msimu uliopita.

Neymar aiongoza vyema Brazil, yaitungua Croatia 3-1

20140613-010343-3823241.jpg












WENYEJI wa michuano ya Fainali za Kombe la Dunia, Brazili imeanza vyema fainali hizo kwa kuicharaza Croati kwa mabao 3-1, huku nyota wa timu hiyo na blabu ya Barcelona, Neymer akifunga mabao mawili moja likiwa la penati iliyolalamikiwa na wageni.
Goli jingine la Brazili lilifungwa na Oscar dakika za lala salama, baada ya awali kutanguliwa na bao la kujifunga la Marcelo dakika ya 11 ya mcvhezo huo ulioptanguliwa na sherehe za ufungizi zilizofana.
Ushindi huio umeiweka Brazil katika nafasi nzuri ya kuwatuliza mashabiki wao ambao wamekuwa hawana amani na timu yao na hasa kutawaliwa na vurugu za watu wanaopinga michuano hiyo kufanyika nchini kwao kwa madai ni gharaa kubwa ambazo fedha zilizotumika kuandaa zingewasaidia katika huduma za kimaendeleo.
Michuano hiyo itaendelea tena leo saa 1 usiku kwa saa za Afrika Mashariki kati ya Mexico dhidi ya wawakilishi wa Afrika Cameroon kabla ya timu za Uholanzi kuvaana na mabingwa watetezi Hispania baadaye.

Thursday, June 12, 2014

Rais TAFF amwagiwa sifa kwa kujitolea


RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba amemwagiwa sifa kwa kuwa mwepesi wa kujitolea kuwasaidia wasanii wenye matatizo, huku wasanii wengine wakiombwa kuiga mfano wake bila kujali uwezo wa mtu wa kifedha.
Pongezi hizo zimetolewa kwenye msiba wa Mzee Small kutokana na namna Rais huyo wa TAFF alivyokuwa akihaha kuweka mambo sawa huku wasanii wa Bongo Movie wakiwa hawapo kwenye eneo hilo mpaka walipokuja baadaye majira ya mchana.
"Kwa kweli Rais wa TAFF, ni mtu wa watu anajitolea na amekuwa mwepesi kila wasanii wanapopatwa na shida ni mfano wa kuigwa na kufahamu wajibu wake kama kiongozi, wasanii wote wangekuwa hivi mambo yangekuwa mazuri sana," alisema mmoja wa wasanii wakiongwe aliyeomba kuhifadhiwa jina lake aliyekuwa msibani hapo mapema.
Mdau mwingine wa sanaa, alisema tofauti na wasanii wa Bongo Movie ambao huchagua aina ya misiba au wasanii wa kuwasaidia hali ni tofauti kwa uongozi wa TAFF na hasa Rais wake na baadhi ya waigizaji
wakongwe wakitajwa kwa majina, Dk Cheni, Chiki Mchoma, Monalisa na mama yake.

Baby Madaha ala 'shavu' Kenya

NYOTA wa filamu na muziki wa Tanzania anayefanya kazi zake nchini Kenya, Baby Madaha amelamba 'shavu' nono kupitia kampuni ya simu ya Safaricom.
Akizungumza na MICHARAZO toka nchini humo, Baby Madaha aliyeachia wimbo mpya uitwao 'Nawaponda' alisema karibu mwezi mmoja sasa anafanya 'tour' chini ya Safaricom, jambo alilofichua limempa ulaji mkubwa na kujitambulisha zaidi nchini humo.
"Nipo kwenye 'tour' ya Safaricom, ambapo napiga shoo sambamba na kuitangaza kampuni kwa kweli nashukuru sana kufanya kazi chini ya Candy n Candy', " alisema Baby.
Msanii huyo hata hivyo hakuweka bayana mkataba alioingia na kampuni hiyo maarufu ya simu za mkononi nchini humo, ila alidai ni mnono na kwamba umemfanya kujivunia kuwa msanii anayefanya kazi nchini Kenya.

Kipute cha Kombe la Dunia kuanza leo Brazil

Wenyeji Brazil watakaoanza mtihani wao leo dhidi ya Croatia
FAINALI za Kombe la Dunia zinatarajiwa kuanza kutimka rasmi kuanzia usiku wa leo kwa wenyeji wa michuano hiyo Brazil itakapou
mana na Croatia. 
Brazil chini ya kocha Luis Fillipe Scolari na itakayokuwa ikimtegemea Neymar kulibakisha kombe hilo itakuwa na mtihani mbele ya Croatia.
Michuano hiyo itakayodumu kwa muda wa mwezi mmoja, itashuhudia mataifa 32 yakichuana katika kugombea nafasi ya kucheza fainali itakayofanyika Julai 13 jijini Rio de Janeiro. 
Mchezo huo wa ufunguzi utakaochezwa katika Uwanja wa Corinthians uliopo jijini Sao Paulo utatanguliwa na sherehe fupi ambazo zitakuwa na maonesho mbalimbali kuelezea uhalisia wa watu wa nchi hiyo na soka. 
Akihojiwa jana kocha wa timu ya taifa ya Brazil, Luis Felipe Scolari aliwaambia wapenzi wote wa soka kwamba muda umefika, wanatakiwa kwenda pamoja kwasababu hilo ni Kombe lao la Dunia. 
Pamoja na shamrashamra za kuanza michuano hiyo, mwaka jana zaidi ya watu milioni moja waliingia mtaani katika miji mikubwa kwa ajili ya kuandamana kupinga kile walichokiita gharama kubwa za maandalizi ya michuano hiyo. 
Hata hivyo safari hii, rais wa Brazil Dilma Rousseff amesema hataruhusu maandamano kwa ajili ya kufuruga michuano hiyo ambapo maelfu ya polisi na wanajeshi wamepangwa ili kuhakikisha michuano hiyo inakwenda vyema.

Kajala aibuka na laana kivyake

Lamata aliyeiongoza filamu ya Kajala iitwayo Laana
BAADA ya kuzitumikia filamu za wenzake, hatimaye msanii Kajala Masanja amevunja ukimya akijiandaa kutoa kazi yake mwenyewe iitwayo 'Laana' kupitia kampuni yake ya Kay Entertainment.
Muongozaji wa filamu hiyo, Leah Richard 'Lamata' alisema filamu hiyo ipo ambayo Kajala ameiigiza akishirikiana na wasanii wengine nyota ipo hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa mtaani, ikiwa ni kazi yake ya kwanza binafsi.
Lamata alisema mkasa wa filamu hiyo ni simulizi linaloelekea kweli juu ya mambo yanayowapata baadhi ya wanajamii kiasi cha kushindwa kuamini.
Baadhi ya wasanii walioshirikishwa katika filamu hiyo ni Salim Ahmed 'Gabo', Farida Sabu 'Mama Sonia' na wengine.
"Tupo katika maandalizi ya mwisho kutoa filamu mpya na ya kwanza binafsi ya Kajala iitwayo 'Laana' imeshirikisha wakali kadhaa na ni bonge la filamu," alisema Lamata mmoja wa waongozaji bora nchini wa filamu kwa sasa.
Kabla ya kutoa kazi binafsi, Kajala alitamba na filamu za watu wengine alizoshirikishwa zikiwamo, Jeraha la Moyo, House Boy, Vita Baridi, House Girl & Boy, Dhuluma, Shortcut, Basilisa, You Me and Him na Devil's Kingdom ya marehemu Steve Kanumba iliyomshirikisha nyota wa kimataifa, Ramsey Nouah.

Soko la Karume lateketea



Pichani ni namna moto ulivyokuwa ukiteketeza soko la mitumba la Mchikichikini

Duh! Waganga wanaotibu wagionjwa kwa ngono wanaswa na Ch**i za kike



POLISI Mkoa wa Temeke, imewakamata vijana wawili wanaodaiwa kujifanya waganga wanaotoa tiba kwa wanawake, ambao masharti yake ni kushiriki nao ngono bila kinga na kuacha nguo za ndani, ili zifanyiwe dawa zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englibert Kiondo, alidai vijana hao Juma Hemedi (32) na Abrahman Mulsin, wote wakazi wa Tandika, baada ya kushiriki ngono na wagonjwa wao huwaambia waache nguo za ndani.
Kamanda Kiondo alidai baada ya kupata malalamiko, Jeshi la Polisi ilianzisha msako na kuwapekua waganga hao, ambapo walikutwa na nguo za ndani za kike 22, ambazo alisema zitakuwa ushahidi wa kuingiliwa kimwili kwa wanawake hao. Vitu vingine wanavyodaiwa kukutwa navyo ni pembe, tunguli, makopo ya dawa na vibuyu.
 “Sheria iko wazi, inasema mganga anapofanya ngono kama uganga anakuwa amebaka, na hii ni kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni ya Adhabu 130 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,”alisema Kamanda Kiondo.
Kwa mujibu wa madai ya Kamanda Kiondo, vijana hao wamekuwa wakijifanya waganga wa tiba asili, husambaza vipeperushi sehemu mbalimbali za jiji kutafuta wateja.
Mbali na tiba hiyo ya kupata watoto, inayotolewa kwa kushiriki ngono na mganga, Kamanda Kiondo alidai watuhumiwa hao wamekuwa wakidai kutibu magonjwa mengine kama kisukari, vidonda vya tumbo, nguvu za kiume, kukuza maumbile, kupata kazi, kufaulu mtihani, mvuto wa biashara, kumilikishwa jini na kupewa pete ya bahati.

Katika tukio lingine, Polisi inamshikilia kijana mwingine mkazi wa Tandika Devis Corner, Maalim Kimti  Rita au kwa jina lingine, Joseph Rita  anayedaiwa kutapeli Sh milioni 11 akijidai kumfanyia dua mfanyabiashara aweze kukuza biashara yake.

Alidai kuna mfanyabiashara mwanamke ambaye alitoa Sh milioni 11 kwa Maalim Rita, akidanganywa kuwa atafanyiwa uganga ili afanikiwe katika biashara yake, lakini alipoona hakuna alichopata, akaamua kutoa taarifa Polisi.

Kamanda Kiondo alisema jamii inapaswa kuelimishwa kuachana na mambo hayo, kwa sababu  tiba yake haipo kwa waganga wa jadi na kwamba hakuna uhusiano kati ya kufaulu na kwenda kwa waganga isipokuwa bidii ya kazi.

“Watu wengi wamelalamikia matukio ya namna hiyo, sasa tumeamua kuweka wazi kwa umma kwa kuwa watu wanateketea kwa kukosa elimu… watu wanauza nyumba magari na mali zao, kwa ajili ya kupata fedha za kupeleka kwa waganga wakiamini kuna tiba, huu ni utapeli vijana kama hawa hawawezi kukupa utajiri wala mtoto,” alisema Kamanda Kiondo.

Alisema waganga hao wamepata vyeti vya kufanyia kazi hiyo ya uganga wa jadi, lakini wanachofanya ni kinyume na kazi hiyo ambapo aliahidi vyeti vyao kuchunguzwa, kuona  wamevipataje na kuwasiliana na Wizara ya Maliasili na Utalii, ili watambue pembe wanazotumia ni za mnyama gani. 



via Habari leo.