STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 17, 2014

Mbwana Samatta aihofia Mambaz Jumapili

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,  Mbwana Samata, amesema mechi ya Jumapili dhidi ya Msumbiji (Mambas) itakuwa na ushindani kwa pande zote mbili lakini amewataka Watanzania wasiwe na wasiwasi.
Samata na mshambuliaji mwenzake wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu, waliwasili jijini Dar es Salaam jana asubuhi wakitokea Tunisia ambako klabu yao imeweka kambi kujiandaa na mechi za Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.
Akizungumza na gazeti hili juzi usiku kabla ya kupanda ndege kuja nchini, Samatta, alisema kuwa anaamini Taifa Stars ina nafasi nzuri ya kushinda mechi hiyo licha ya kwamba itakuwa ni ngumu na ni lazima wacheze kwa kujihadhari.
Samata alisema watahakikisha wanapata matokeo mazuri Jumapili na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.
"Kwa upande wangu nimetoka katika maandalizi ya Ligi ya Klabu Bingwa, niko fiti kulipigania taifa langu, Inshaallah Allah atatia wepesi," alisema mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba na African Lyon (zamani Mbagala Market).
Jana mchana Samatta aliliambia gazeti hili wamefika nchini salama lakini wataungana na wachezaji wenzao wa Stars Ijumaa baada ya kurejea wakitokea Mbeya.
“Ndiyo tumeshafika Dar, niko pamoja na Tom," alisema mshambuliaji huyo anayependwa na mashabiki wa TP Mazembe.
Aliongeza kuwa wanaahidi watapambana na akawataka Watanzania wajitokeze kwa wingi Jumapili kuishangilia timu hiyo.
Kabla ya kwenda Mbeya, Stars iliweka kambi ya wiki mbili jijini Gaborobe, Botswana kwa ajili ya kujiandaa na mechi hiyo ya Jumapili kabla ya kurudiana Agosti 3 mwaka huu mjini Maputo.
Nyota mwingine wa Stars kiungo, Mwinyi Kazimoto, anatarajiwa kuwasili leo mchana akitokea Qatar kujiunga na timu hiyo.
NIPASHE

STEVE NYERERE AHIMIZA JAMII KUSAIDIA WALEMAVU

Steve Nyerere aliyesimama kulia akizungumza huku wanafunzi wa Shule ya Sinza Maalum wakimsikiliza walipowatembea shuleni hapo katika maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa mtoto wa Kajala Masanja aitwaye Paula
Steve Nyerere alipokuwa akiwasilia shule ya Sinza Maalum
MWENYEKITI wa Bongo Movie, Steven Mengele 'Steve Nyerere' ameitaka jamii pamoja na wasanii wenzake nchini kubadili mtazamo wao katika kuisaidia jamii kwa kuwakumbuka pia watoto wenye ulemavu.
Steve Nyerere alitoa wito huo juzi wakati wa sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa mtoto wa Kajala Masanja aitwaye Paula iliyofanyika katika Shule Maalum Sinza inayofundisha watoto wenye ulemavu wa akili, ambako alisema pamoja na umuhimu wa kuwasaidia yatima, lakini pia makundi mengine ya watoto kama walemavu wa akili yanapaswa kuangaliwa kwa jicho la ziada.
"Unajua jamii na hata sisi wasanii tumezoea kila tukitaka kutoa misaada tunakimbilia kwenye vituo vya kulelea yatima, lakini kumbe wapo watoto wengine wahitaji kama watoto hawa ambao wameonyesha furaha na uwezo wa hali ya juu wa utambuzi tofauti na hali zao," alisema.
Nyota huyo wa kuigiza sauti za watu mashuhuri, aliwapongeza walimu wa shule hiyo ya Sinza Maalum kwa kazi kubwa na ngumu waliyonayo katika kuwatunza na kuwalea wanafunzi hao ambao walimtambua kwa haraka Steve Nyerere walipoulizwa kama kuna mtu yeyote katika msafara uliotembelea shuleni hapo na kumtaja yeye kwa kwenda kumshika mkono na kuamsha vicheko.

BADO KIDOGO UMSIKIE THEA KWENYE INJILI

MUIGIZAJI nyota nchini, Ndimbangwe Misayo 'Thea' amesema yupo hatua ya mwisho kabla ya kuibukia studio kurekodi wimbo wake wa kwanza wa muziki wa Injili, fani anayopanga kujitosa jumla kwa lengo la kumtumia bwana.
Akizungumza na MICHARAZO, Thea alisema kuwa mpango wake wa kuhamia kwenye muziki wa Injili unaendelea kwa kuanza kutunga nyimbo kabla ya kuingia studio kwa ajili ya kurekodi ili mashabiki wa miondoko hiyo washuhudie kipaji kingine alichonacho.
"Nipo kwenye maandalizi ya kuanza kuimba nyimbo za Injili, kuna kazi nimeanza kuziandika na muda ukifika nitaingia studio na kuanza kutoa kazi moja baada ya nyingine, mashabiki wa muziki huo wavute subira," alisema.
Thea ambaye aling'ara kwenye michezo ya kuigiza ya kwenye luninga akiwa na kundi la Kaole Sanaa kabla ya kuhamia kwenye filamu alisema kiu yake ni kumtumikia Mungu kama alivyokuwa akiutumikia ulimwengu na hatanii katika hilo. Alisema uimbaji ni fani aliyokuwa nayo tangu udogoni kwa kuimba kanisani na kwenye kwaya ya kanisa lake kabla ya kuzamia kwenye filamu.

KAJALA: SASA NIMEZALIWA UPYA BONGO MOVIE


NYOTA wa filamu nchini, Kajala Masanja amesema filamu yake mpya anayojiandaa kuingiza sokoni iitwayo 'Laana' inakuja kuthibitisha kuwa kwa sasa amezaliwa upya na yupo kikazi zaidi kuwapa burudani.
Kajala ambaye alinusurika kwenda jela katika kesi iliyokuwa ikimkabili kabla ya kusaidiwa na Wema Sepetu kwa kumlipia faini ya Sh. milioni 13, alisema filamu hiyo mpya itatoka hivi karibuni kwani tayari ameishaikabidhi kwa wasambazaji.
Akizungumza na MICHARAZO, Kajala anayemiliki kampuni ya Kay Entertainment alisema baada ya misukosuko aliyokumbana nayo kwa sasa ametuliza akili kwa ajili ya kufanya kazi akianza na filamu ya 'Laana' ambayo amewashirikisha wasanii nyota nchini.
Kajala aliwataja baadhi ya wasanii walioicheza filamu hiyo ni Ahmed Salim 'Gabo', Philemon Lutwazi 'Uncle D', Mama Kawele, Mama Sonia, yeye (Kajala) na wakali wengine.
"Kwa sasa nipo kikazi zaidi na naanza hesabu na 'Laana' iliyotengenezwa na kampuni yangu ya Kay Entertainment chini ya muongozaji Leah Richard 'Lamata' na bada ya hapo natarajia kutoa 'Pishi' wakati 'Heart Attack' niliyoiandaa kabla ya misukosuko ikisubiri kwanza," alisema Kajala.
Msanii huyo alisema anaamini kazi hizo zitathibitisha kuwa anachokisema hatanii, bali ni kweli amezaliwa upya chini ya kampuni yake.

MATOKEO KIDATO CHA SITA YATOKA EBU YACHUNGILIE HAPA

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA
ACSEE 2014 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES

  P0101 AZANIA CENTRE   P0104 BWIRU BOYS CENTRE   P0110 ILBORU CENTRE
  P0112 IYUNGA CENTRE   P0116 KANTALAMBA CENTRE   P0119 KIBAHA CENTRE
  P0123 KWIRO CENTRE   P0129 MARA CENTRE   P0132 MILAMBO CENTRE
  P0133 MINAKI CENTRE   P0134 MOSHI CENTRE   P0136 MUSOMA CENTRE
  P0140 MZUMBE CENTRE   P0143 NJOMBE CENTRE   P0144 NSUMBA CENTRE
  P0145 NYAKATO CENTRE   P0147 PUGU CENTRE   P0150 SAME CENTRE
  P0151 SENGEREMA CENTRE   P0152 SHINYANGA CENTRE   P0156 TANGA TECH. CENTRE
  P0158 TOSAMAGANGA CENTRE   P0167 KIDUGALA SEMINARY CENTRE   P0184 AGAPE LUTH JUNIOR SEMINARY CENTRE
  P0203 IRINGA GIRLS CENTRE   P0209 KOROGWE CENTRE   P0211 LOLEZA CENTRE
  P0218 RUGAMBWA CENTRE   P0219 SONGEA GIRLS CENTRE   P0220 TABORA GIRLS CENTRE
  P0228 MPANDA GIRLS CENTRE   P0301 AIRWING J.W.T.Z. CENTRE   P0302 ARUSHA CENTRE
  P0303 ARUSHA-MERU CENTRE   P0305 BULUBA CENTRE   P0306 DODOMA CENTRE
  P0309 FIDEL CASTRO CENTRE   P0313 IKIZU CENTRE   P0316 KIBASILA SEC.SCHOOL CENTRE
  P0320 KIGOMA CENTRE   P0321 KINONDONI CENTRE   P0324 LINDI CENTRE
  P0326 LUMUMBA CENTRE   P0327 MINJA TECH. CENTRE   P0328 MAWENZI CENTRE
  P0329 MAKUMIRA CENTRE   P0330 MBEYA CENTRE   P0333 MWANZA CENTRE
  P0334 MWENGE CENTRE   P0336 HUDUMA J.W.T.Z. CENTRE   P0338 NDANDA CENTRE
  P0341 SANGU CENTRE   P0345 USAGARA CENTRE   P0351 BAGAMOYO CENTRE
  P0352 TARIME CENTRE   P0353 PARANE CENTRE   P0359 KIGURUNYEMBE CENTRE
  P0360 KISHOJU CENTRE   P0361 SINGE CENTRE   P0364 KARATU CENTRE
  P0368 IMBORU CENTRE   P0370 IFAKARA CENTRE   P0377 LUGALO J.W.T.Z. CENTRE
  P0379 MGULANI J.K.T. CENTRE   P0380 UCHAMA CENTRE   P0381 UTAANI CENTRE
  P0383 BEN BELLA CENTRE   P0385 UJIJI   P0386 GEITA CENTRE
  P0387 KARAGWE CENTRE   P0389 SHAURITANGA CENTRE   P0391 HAILE SELASSIE CENTRE
  P0400 SHAMIANI CENTRE   P0402 MKWAJUNI CENTRE   P0404 TUNDURU CENTRE
  P0413 KIBITI CENTRE   P0418 LUTENGANO CENTRE   P0427 MAKAMBAKO CENTRE
  P0431 MTWANGO CENTRE   P0432 JABAL-HIRA CENTRE   P0438 MASJID QUBAH MUSLIM SEM. CENTRE
  P0440 SONGEA TEACHERS’ COLLEGE CENTRE   P0443 META CENTRE   P0445 MWEMBETOGWA CENTRE
  P0457 IGAWILO CENTRE   P0458 KASULU TEACHERS’ COLLEGE CENTRE   P0461 JOHN PAUL II KAHAMA CENTRE
  P0465 JAMHURI CENTRE   P0467 NYUKI J.W.T.Z. CENTRE   P0476 MWANGAZA CENTRE
  P0493 AL-HARAMAIN CENTRE   P0501 UWELENI CENTRE   P0516 MOMBO CENTRE
  P0531 RUAHA CENTRE   P0538 VWAWA   P0546 PAMBA (I A E) CENTRE
  P0549 LUGOBA CENTRE   P0554 NGUDU CENTRE   P0560 KASULU CENTRE
  P0563 TABORA TEACHERS’ COLLEGE CENTRE   P0566 BUTIMBA TEACHERS’ COLLEGE CENTRE   P0586 KAISHO CENTRE
  P0611 KABANGA CENTRE   P0620 TEGETA CENTRE   P0640 MBALIZI CENTRE
  P0641 MEATU CENTRE   P0652 POMERINI CENTRE   P0660 MOROGORO TEACHERS’ COLLEGE CENTRE
  P0673 NANGWA CENTRE   P0681 IVUMWE CENTRE   P0685 NAMABENGO CENTRE
  P0686 CHATO CENTRE   P0688 MSAKILA   P0706 KALANGALALA CENTRE
  P0710 BINZA CENTRE   P0716 MALECELA CENTRE   P0725 NEWMAN
  P0738 RIDHWAA SEMINARY CENTRE   P0770 SUMVE HIGH SCHOOL CENTRE   P0796 MCHANGA MDOGO CENTRE
  P0797 BUNDA TEACHER’S COLLEGE CENTRE   P0798 KOROGWE TEACHERS COLLEGE CENTRE   P0832 KIPONDA CENTRE
  P0841 HUMURA CENTRE   P0904 KONGWA CENTRE   P0936 KALIUA CENTRE
  P0938 MBEZI BEACH CENTRE   P0947 DR OLSEN CENTRE   P0967 MLOLE CENTRE
  P1043 TUKUYU CENTRE   P1072 KAMENE CENTRE   P1077 OCEAN CENTRE
  P1119 ZANZIBAR COMMERCIAL   P1141 SWILLA CENTRE   P1156 TEMEKE TEACHER’S RESOURCE CENTRE
  P1246 MIDLAND CENTRE   P1278 MBEZI HIGH SCHOOL CENTER   P1291 PEMBA ISLAMIC COLLEGE CENTRE
  P1298 KIEMBESAMAKI SEC SCHOOL CENTRE   P1377 NATIONAL CORRESPONDENCE INSTITUTE   P1378 KLERRUU TEACHERS COLLEGE CENTRE
  P1379 MTWARA TEACHERS COLLEGE CENTRE   P1383 MZINGA CENTRE   P1475 PERFECT-VISION SEC SCHOOL CENTRE
  P1495 GENESIS HIGH SCHOOL CENTRE   P1556 DUNGA   P1584 KIWANJA CENTRE
  P1587 MUFINDI T.R.C. CENTRE   P1600 BISHOP DURNING CENTRE   P1612 ARUSHA SCHOOL CENTRE
  P1740 BISHOP MPANGO   P1817 SENGEREMA T.R.C. CENTRE   P1918 AL-FALAAH MUSLIM CENTRE
  P2211 MWILAMVYA CENTRE   P2341 MLIMA MBEYA HIGH SCHOOL   P2454 SPLENDID SECRETARIAL COLLEGE CENTRE
  P2500 CHUO CHA UFUNDI – VETA CENTRE   P2517 ALFA CENTRE   P2673 RAIDA HIGH SCHOOL CENTRE
  P3000 MAZIZINI ISLAMIC CENTRE   P3240 LUDEWA TRC CENTRE   P3601 ILASI CENTRE
  P3634 MUGUMU CENTRE   P3722 FPCT SHINYANGA VIJANA CENTRE   P3733 MAHENJE CENTRE
  P4002 MWANAKWEREKWE C CENTRE   P4007 AGUSTIVO CENTRE   P4036 EBONITE TC CENTRE
  P4236 DINOBB CENTRE   P4348 T.E.W.W TABORA CENTRE   P4351 GENDA CENTRE
  P4624 PREMIER GIRLS CENTRE   S0101 AZANIA   S0103 BIHAWANA
  S0104 BWIRU BOYS   S0106 DUNG’UNYI SEMINARY   S0107 LUTHERAN JUNIOR SEMINARY
  S0108 IFUNDA TECHNICAL   S0109 IHUNGO   S0110 ILBORU
  S0111 ITAGA SEMINARY   S0112 IYUNGA TECHNICAL   S0113 MAFINGA SEMINARY
  S0115 KAHORORO   S0116 KANTALAMBA   S0117 KASITA SEMINARY
  S0118 KATOKE SEMINARY   S0119 KIBAHA   S0120 KIGONSERA
  S0121 ST. JAMES SEMINARY   S0123 KWIRO   S0125 LYAMUNGO
  S0128 MALANGALI   S0129 MARA   S0130 MAUA SEMINARY
  S0132 MILAMBO   S0133 MINAKI   S0134 MOSHI
  S0135 MOSHI TECHNICAL   S0136 MUSOMA   S0138 MPWAPWA
  S0139 MTWARA TECHNICAL   S0140 MZUMBE   S0142 GALANOS
  S0143 NJOMBE   S0144 NSUMBA   S0145 NYAKATO
  S0146 NYEGEZI SEMINARY   S0147 PUGU   S0148 RUBYA SEMINARY
  S0149 RUNGWE   S0150 SAME   S0151 SENGEREMA
  S0152 SHINYANGA   S0153 SONGEA BOYS   S0154 ST.PETER’S SEMINARY
  S0155 TABORA BOYS   S0156 TANGA TECHNICAL   S0158 TOSAMAGANGA
  S0160 UMBWE   S0164 USA SEMINARY   S0165 URU SEMINARY
  S0167 KIDUGALA LUTHERAN SEMINARY   S0168 SANU SEMINARY   S0174 CONSOLATA SEMINARY
  S0175 SALESIAN SEMINARY   S0178 MANOW LUTHERAN JUNIOR SEMINARY   S0179 ST.MARY’S SEMINARY MBALIZI
  S0181 KISARAWE LUTHERAN JUNIOR SEMINARY   S0182 AL-FAROUQ SEMINARY   S0184 AGAPE LUTHERAN J SEMINARY
  S0188 KIRINJIKO ISLAMIC SEMINARY   S0189 FEZA BOYS’   S0190 ST.JOSEPH-KILOCHA SEMINARY
  S0198 AILANGA LUTHERAN JUNIOR SEMINARY   S0201 ASHIRA   S0202 BWIRU GIRLS
  S0203 IRINGA GIRLS   S0204 JANGWANI   S0205 KIBOSHO GIRLS
  S0206 KILAKALA   S0207 KIRAENI GIRLS   S0209 KOROGWE GIRLS
  S0210 BIGWA SISTERS SEMINARY   S0211 LOLEZA   S0212 MACHAME GIRLS
  S0213 MASASI GIRLS   S0214 MSALATO   S0215 MTWARA GIRLS
  S0216 NGANZA   S0217 PERAMIHO GIRLS   S0218 RUGAMBWA
  S0219 SONGEA GIRLS   S0220 TABORA GIRLS   S0221 WERUWERU
  S0222 ZANAKI   S0223 MASAMA GIRLS   S0224 KIFUNGILO GIRLS
  S0227 MASWA GIRLS   S0228 MPANDA GIRLS   S0229 KONDOA GIRLS
  S0230 KIBONDO   S0233 ST.MARY’S MAZINDE JUU   S0234 ST.LUISE MBINGA GIRLS
  S0240 ST.JOSEPH GIRLS SEMINARY   S0245 PALLOTI GIRLS   S0246 MAASAE GIRLS LUTHERAN SCH
  S0247 BONICONSILI MABAMBA GIRLS SEC.SCHOOL   S0248 MARIAN GIRLS   S0249 LORETO GIRLS
  S0252 AL-KHEIR ISLAMIC GIRLS SEMINARY   S0255 ST.CHRISTINA GIRL’S SCHOOL   S0256 HURUMA GIRLS
  S0263 VISITATION GIRLS’   S0264 BARBRO-JOHANSSON   S0266 REGINAMUNDI GIRLS’
  S0271 MANYUNYU   S0272 AL-IHSAN GIRLS   S0276 IFUNDA GIRLS
  S0281 CHIEF IHUNYO SEC SCHOOL   S0298 FEZA GIRLS’   S0299 MKUGWA
  S0302 ARUSHA   S0303 ARUSHA-MERU   S0304 BUKOBA
  S0305 BULUBA   S0306 DODOMA   S0308 ENABOISHU
  S0309 FIDEL CASTRO   S0310 FOREST HILL   S0312 HIGHLANDS
  S0313 IKIZU   S0314 KAZIMA   S0316 KIBASILA
  S0320 KIGOMA   S0322 KOLILA   S0323 LAKE
  S0324 LINDI   S0325 LUGALO   S0326 LUMUMBA
  S0328 MAWENZI   S0329 MAKUMIRA   S0330 MBEYA
  S0332 MOROGORO   S0333 MWANZA   S0334 MWENGE
  S0335 MZIZIMA   S0338 NDANDA   S0341 SANGU
  S0342 SHAABAN ROBERT   S0345 USAGARA   S0346 UYUI
  S0347 TAMBAZA   S0348 TUMAINI   S0351 BAGAMOYO
  S0352 TARIME   S0353 PARANE   S0355 LOMWE
  S0356 VUNJO   S0359 KIGURUNYEMBE   S0360 KISHOJU
  S0361 SINGE   S0364 KARATU   S0367 KILOSA
  S0369 RUVU   S0370 IFAKARA   S0380 UCHAMA
  S0381 UTAANI   S0383 BEN BELLA   S0385 UJIJI
  S0386 GEITA   S0387 KARAGWE   S0388 MARANGU
  S0389 SHAURITANGA   S0391 HAILE SELASSIE   S0392 VIKOKOTONI
  S0397 RULENGE   S0400 SHAMIANI   S0402 MKWAJUNI
  S0404 TUNDURU   S0405 BIHARAMULO   S0409 MORINGE SOKOINE
  S0413 KIBITI   S0417 MWAKALELI   S0418 LUTENGANO
  S0419 CHOME   S0427 MAKAMBAKO   S0430 UWEMBA
  S0431 MTWANGO   S0432 JABAL-HIRA MUSLIM JUNIOR SEMINARY   S0434 NDEMBELA
  S0437 AL-MUNTAZIR ISLAMIC SEMINARY   S0438 MASJID QUBAH MUSLIM SEMINARY   S0439 BUPANDAGILA
  S0443 META   S0444 ITAMBA   S0445 MWEMBETOGWA
  S0448 SADANI   S0449 J.J.MUNGAI   S0454 ST.JOSEPH NGARENARO
  S0457 IGAWILO   S0461 JOHN PAUL II KAHAMA   S0465 JAMHURI
  S0467 NYUKI   S0471 MBOZI   S0473 KANYIGO
  S0483 SAME SEMINARY   S0485 MAJENGO   S0488 RUTABO
  S0489 SUJI   S0491 KILOMENI   S0493 AL-HARAMAIN ISLAMIC SEMINARY
  S0496 JITEGEMEE   S0501 UWELENI   S0506 UNGWASI
  S0515 ILULA   S0516 MOMBO   S0526 MRINGA
  S0527 ULAYASI   S0531 RUAHA   S0534 ST.ANTHONY’S
  S0538 VWAWA   S0539 MAGU   S0540 MAPOSENI
  S0544 MKUU   S0546 PAMBA   S0548 SHAMBALAI
  S0549 LUGOBA   S0554 NGUDU   S0558 MWANGA
  S0560 KASULU   S0578 TAQWA   S0580 IGOWOLE
  S0581 ILEJE   S0584 LWANDAI   S0586 KAISHO
  S0590 WILIMA   S0596 LIWALE DAY   S0607 LULUMBA
  S0609 MATAI   S0610 NKASI   S0611 KABANGA
  S0612 KAGANGO   S0614 NYERERE   S0617 LUSANGA
  S0620 TEGETA   S0622 KUNDUCHI GIRLS ISLAMIC HIGH SCHOOL   S0629 EDMUND-RICE-SINON
  S0631 UMOJA   S0632 BONDENI   S0635 MSUFINI
  S0640 MBALIZI   S0641 MEATU   S0643 DAREDA
  S0645 VITUKA   S0647 NGARENANYUKI   S0652 POMERINI
  S0653 MWAKAVUTA   S0661 ISENYE   S0663 SANGITI
  S0665 MWEMBENI   S0667 NYAISHOZI   S0668 DAKAWA HIGH SCHOOL
  S0671 UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL   S0673 NANGWA   S0681 IVUMWE
  S0685 NAMABENGO   S0686 CHATO   S0688 MSAKILA
  S0692 ROSMINI   S0697 KIGWE   S0698 ECKERNFORDE
  S0706 KALANGALALA   S0710 BINZA   S0712 BARIADI
  S0713 IGUNGA   S0715 ILONGERO   S0716 MALECELA
  S0725 NEWMAN   S0726 MBEKENYERA   S0729 MSOLWA
  S0731 MAKONGO   S0738 RIDHWAA SEMINARY   S0740 ALI HASSAN MWINYI ISL.
  S0741 ITENDE   S0748 KAWAWA   S0751 RUHUWIKO
  S0752 RUNZEWE   S0754 URAMBO DAY   S0757 KYELA
  S0769 MALAGARASI   S0770 SUMVE   S0778 SONGE
  S0782 MWIKA   S0784 AIRWING   S0787 MSANGENI
  S0796 MCHANGAMDOGO   S0800 LOYOLA   S0804 MVUMI
  S0811 KIFARU   S0812 MAHIWA   S0818 TARAKEA
  S0823 THAQAAFA   S0825 MUDIO ISLAMIC SEMINARY   S0831 NANGWANDA GIRLS
  S0832 KIPONDA   S0841 HUMURA   S0851 USANGI DAY
  S0853 KIZWITE   S0857 LONGIDO   S0867 PANDAHILL
  S0870 KILANGALANGA   S0883 DONBOSCO-DIDIA   S0884 MAMBWE
  S0890 IWALANJE   S0896 KIZUKA   S0901 KISIWANI
  S0904 KONGWA   S0906 VUDOI   S0913 USONGWE
  S0922 MWINYI   S0936 KALIUA   S0938 MBEZI BEACH
  S0947 DR. OLSEN   S0949 IRKISONGO   S0960 BENJAMIN WILLIAM MKAPA HIGH SCHOOL
  S0989 KIBARA   S0995 SOS HERMANN GMEINER SCHOOL   S1008 ST.MAURUS CHEMCHEMI
  S1009 BABATI DAY   S1011 CHANG’OMBE   S1032 ITIGI
  S1033 AMANI ABEID KARUME   S1043 TUKUYU   S1051 MKOLANI
  S1061 MAKIBA   S1071 ST.MATTHEW’S   S1072 KAMENE
  S1077 OCEAN   S1093 ALDERSGATE   S1098 MAJI YA CHAI
  S1107 MWAMASHIMBA   S1119 ZANZIBAR COMMERCIAL   S1141 SWILLA
  S1144 ISIMILA   S1148 MADIBIRA   S1157 IWAWA
  S1174 COASTAL   S1183 SANYA JUU   S1186 MAKITA
  S1187 ST.MARY GORETI   S1198 TANZANIA ADVENTIST   S1199 MADABA
  S1201 LUFILYO   S1202 MTERA   S1220 MSAMALA
  S1246 MIDLANDS   S1261 MERRIWA   S1262 MATEMA BEACH
  S1268 KISIMIRI   S1270 NYARUBANDA   S1272 KISARIKA
  S1278 MBEZI   S1284 NORTHERN HIGHLANDS   S1285 FLORIAN
  S1291 PEMBA ISLAMIC COLLEGE   S1298 KIEMBESAMAKI   S1340 LWANGWA
  S1343 ANNE MARIE   S1344 MWALIMU J K NYERERE   S1349 NYAKAHURA
  S1375 NEW ERA   S1383 MZINGA   S1392 NATTA
  S1430 KIUMA   S1450 EFATHA SEMINARY   S1454 LONDONI
  S1475 PERFECT-VISION   S1495 GENESIS HIGH SCHOOL   S1522 SCOLASTICA
  S1523 AGAPE MBAGALA   S1549 ENGUTOTO   S1556 DUNGA
  S1578 CHANGARAWE   S1584 KIWANJA   S1596 NYERERE HIGH SCHOOL-MIGOLI
  S1599 BAOBAB   S1600 BISHOP DURNING HIGH SCHOOL   S1608 NTUNDURU
  S1609 RORYA   S1645 LUBALA   S1648 SUMBAWANGA
  S1665 NYASAKA ISLAMIC   S1688 BAHARI BEACH   S1689 PEACE
  S1757 BENDEL MEMORIAL   S1766 CHUKWANI   S1770 IMAGE
  S1822 ANNAGAMAZO   S1888 PATRICK MISSION   S1918 AL-FALAAH MUSLIM
  S1939 MAWENI   S2153 AQUINAS   S2178 GOLDEN RIDGE
  S2211 MWILAMVYA   S2213 USEVYA   S2295 MAIRIVA
  S2315 KANDOTO SAYANSI   S2326 MANGUANJUKI   S2341 MLIMA MBEYA HIGH SCHOOL
  S2354 EAGLES   S2383 OSWARD MANG’OMBE S S   S2426 CHAMAZI ISLAMIC SEMINARY
  S2427 ISONGOLE   S2433 GANAKO   S2499 TUSIIME
  S2549 ALPHA   S2673 RAIDA   S2804 MUSOMA UTALII S S
  S3000 MAZIZINI   S3241 YOSIAH GIRLS’ HIGH SCHOOL   S3503 MWENDAKULIMA
  S3536 LILIAN KIBO   S3601 ILASI SEC SCHOOL   S3646 DULUTI
  S3661 BEROYA   S3733 MAHENJE SEC SCHOOL   S3804 MUHEZA HIGH SCHOOL
  S3811 OVERLAND   S3881 AHMES   S3885 WENDA HIGH SCHOOL
  S3886 SIMBA WA YUDA   S3905 UWATA   S3914 ALFAGEMS
  S4002 MWANAKWEREKWE ‘C’   S4007 AGUSTIVO   S4016 ISALU EXCEL HIGH SCHOOL
  S4039 ST. THERESA OF THE CHILD JESUS   S4096 UMBUYA   S4104 LORD BADEN POWELL MEMORIAL
  S4163 KIJOTA HULL HIGH SCHOOL   S4193 HARRISON UWATA   S4236 DINOBB HIGH SCHOOL
  S4340 GIRANGO   S4351 GENDA   S4419 LUKOLE
  S4535 JIKOMBOE   S4567 SACRED HEART   S4586 ZACHARIA
  S4605 MAGUFULI   S4624 PREMIER GIRLS   S4646 PAMOJA
  S4661 KAJUMULO ALEXANDER GIRLS   S4692 ST.JOSEPH’S CATHEDRAL   S4746 CORNERSTONE LEADERSHIP
  S4797 FARAJA SIHA SEMINARY   S4803 NDYUDA   S4862 GOMBE HIGH SCHOOL
  S4922 WATU   S4929 TINDE GIRLS HIGH SCHOOL   S5114 SUZA
Kama hujaona vizuri waweza kutumia link hii kuyatazama www.necta.go.tz/matokeo2014/ACSEE.htm

Tuesday, July 15, 2014

'Shujaa' waa Ujerumani haamini kama wametwaa ndoo

KIkosi cha Ujerumani na kocha wao wakishangilia ubingwa
Mario Gotze akiwa na famnilia yake akishangilia ubingwa
 MUUAJI aliyeizamisha Argentina na kuipata timu yake ya Ujerumani ubingwa wa Kombe la Dunia Mario Gotze amesema ilikuwa ni ndoto iliyokua kweli baada ya kuisaidia Ujerumani kutwaa Kombe la Dunia kwa kufunga goli pekee la mechi ya fainali dhidi ya Argentina kwenye Uwanja wa Maracana juzi.
Kiungo huyo wa Bayern Munich alianzia benchi katika mechi hiyo hiyo, lakini aliingizwa mwishoni mwa kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Miroslav Klose.
Gotze hakumuangusha kocha Joachim Low na akafunga goli katika dakika ya 113 kufuatia krosi ya Andre Schurrle na kuwapa Ujerumani ubingwa wa nne wa Kombe la Dunia.
"Ni hisia za aina yake, sijui nizielezee vipi. Nilipiga shuti tu na sikujua nini kitatokea. Ni ngumu kuamini," alisema nyota huyo mwenye umri wa miaka 21.
"Kwetu sisi,ndoto imekua kweli. Najivunia timu na nina furaha ya kupindukia kwa kila kilichotokea Brazil.
"Kila mchezaji katika timu yetu anastahili kutajwa hapa na tunajivunia kutwaa kombe hili."
Gotze amecheza mechi sita za Kombe la Dunia 2014 na amefunga magoli mawili.

MAYWEATHER KURUDIANA NA MAIDANA SEPTEMBA.

BINGWA wa masumbwi wa uzito wa welter ambaye hajapigwa mpaka sasa, Floyd Mayweather anatarajiwa kucheza pambano la marudiano na Marcos Maidana wa Argentina. 
Mayweather mwenye umri wa miaka 37 raia wa Marekani anatarajiwa kutetea mikanda yake ya ubingwa inayotambuliwa na Baraza la Ngumi Duniani-WBC na Chama cha Ngumi Duniani-WBA dhidi ya maidana aliyemdunda katika pambano lililofanyika Mei 3 mwaka huu. 
Wawili hao wanatarajiwa kupambana tena jijini Las Vegas, Septemba mwaka huu. 
Akihojiwa Mayweather ametamba kuwa ana uhakika wa kushinda pambano hilo pamoja na kukiri kuwa utakuwa mpambano na mgumu. 
Katika pambano lililofanyika Mei, jaji wa kwanza alitoa alama 114-114, wakati majaji wawili waliobakia walitoa alama 116-112 na 117-111 ambapo alama zote za juu zilikwenda kwa Mayweather. 
Mayweather anakaribia kufikisha rekodi ya kucheza mapambano 49 bila kupigwa iliyowekwa na bingwa wa zamani wa uzito wa juu Rocky Marciano, ambapo mpaka sasa ameshashinda mapambano 46 bila kupigwa.

Mnigeria, Wema, Sir Nature kupamba Usiku wa Matumaini

Wema Sepetu
TAMASHA la Usiku wa Matumaini la mwaka 2014 linatarajiwa kufanyika  Agosti 8 na litapambwa na wasanii mbalimbali nyota nchini pamoja na mwanadada mkali toka Nigeria Yemi Alade anayetamba na wimbo wa 'Johnny'
Kawaida ya tamasha hilo hufanyika Julai 7, lakini kutokana na mwaka huu tarehe hiyo kuangukia kwenye mfungo wa mwezi wa Ramadhani, waandaaji wake wameamua kupeleka hadi Nanenane kwa heshima ya waumini wa Kiislam.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo, Abdallah Mrisho alisema kuwa 'Usiku wa Matumaini' safari hii umeboreshwa kwa upande wa burudani ambapo Mnigeria Yami Alade anatarajia kutua kutumbuiza.
Mrisho alisema kwa upande wa wasanii wa nyumbani 'ujazo'umeongezwa kwa kuwakusanya wakali watupu kuanzia waigizaji, wasanii wa muziki wa kizazi kipya hadi wanamiochezo.
Wasanii wanaoatarajiwa kupanda jukwaani siku hiyo ni pamoja na Ali Kiba, Roma Mkatoliki, Madee, Juma Nature na wengineo kibao akiwamo Wema Sepetu atakayeimba na kucheza nyimbo za 'baby' wake, Diamond Platnumz.
"Upande wa masumbwi kutakuwa na pambano kati ya Mada Maugo na Thiomas Mashali, huku Khaleed Chokoraa aliyehamia kwenye ngumi atazipiga siku hiyo na Saim Memba, " alisema Mrisho kutoka kampuni ya Global Publishers ambao ndiyo waandaaji wa tamasha hilo la kila mwaka.
Aliongeza kuwa, Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge, Mwingulu Nchemba atapanda ulingoni kuzipiga na Dk Hamis Kigwangala, huku wana Bongo Movie JB atazipiga na Cloud 112 na Irene Uwoya atappetana na Jackyline Wiolper.
"Pia kutakuwa na pambano la soka la Bongo Movie dhidi ya wapinzani wao Bongofleva na mechi ya wabunge wa Simba na Yanga ambao safari hii watakuwa na nyota wapya, Yanga wana Ridhiwani Kikwete na Simba wanaye Godfrey Mgimwa," alisema Mrisho.
Mwaka jana pambano la wabunge lilianzishwa na Rais Jakaya Kikwete kabla ya kupokewa na mwamuzi wa zamani wa kimataifa nchini, Othman Kazi 'Collina'.


KAJALA ampa UJUMBE mzito MWANAE akisherehekea miaka 12 ya kuzaliwa kwake

Paula
Kajala na mwanae Kajala
SIKU kama ya leo miaka 12 iliyopitaq  mwanadada Kajala Masanja alifanikiwa kujifungua mtoto wake aliyezaa na P Funk Majani aitwaye Paula.
Katika kuikumbuka siku hiyo muhimu kwa mwanae, Kajala kupitia ukursa wake wa INSTAGRAM ameandika ujumbe maalu kwa mtoto wake kueleza magumu yao yote waliopitia tangu siku ya kwanza Paula alipokuja duniani kwa kuzaliwa mpaka sasa...Kiukweli Kajala amefunguka mengi sana.....

Fainali za Usomaji wa Qur'an Julai 25

FAINALI za kumtafuta bingwa wa kuhifadhi Q'uran kwa njia ya kughani (Tajuweed) mwaka huu zitafanyika kwenye Msikiti wa Manyema jijini Dar es Salaam, Ijumaa ya mwisho ya mfungo mtukufu wa Ramadhani Julai 25 mwezi huu.
Aidha, siku hiyo itakuwa ni sawa na funga ya 27 ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani, hivyo waumini wa dini ya Kiislamu watakuwa ndani ya maombi maalum maarufu kama “Lailatul Qadir” ambayo huyatumia kuomba msamaha na kufutiwa madhambi maradufu na Mwenyezi Mungu.
Hayo yalisemwa na Katibu wa Taasisi ya Kuhifadhi na Usomaji wa Kuran ya Sheikh Yahya Hussein (Sheikh Yahya Hussein Tahfidh Q’uran and Tajweed Foundation), Maalim Hassan Yahya katika taarifa aliyotuma kwenye vyombo vya habari mwishoni mwa wiki.
 Maalim alisema  fainali hizo zitawakutanisha washindi wote wa michuano ya kusoma Koran watakaokuwa wameshinda kwenye michuano ya taasisi mbalimbali inayoendelea hivi sasa Afrika Mashariki na Kati.
“Tutakuwa na washindanaji walioshinda kutoka nchi zote za Afrika Mashariki na Kati ambazo ni Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Congo DRC, Sudan Kusini na Tanzania,”alisema Maalim
Aidha alisema kuwa kutakuwa na majaji kutoka nchi hizo na wengine kutoka Saudi Arabia na Iran.
Alisema kuwa ni  washindi watatu wa mwanzo watapata nafasi ya kwenda Hijjah kwa gharama za taasisi yake pia watazawadiwa vyeti na fedha taslimu.

Brazili yamtimua 'Big Phil' ni baada ya aibu aliyowapa nyumbani


Scolari katika picha tofauti kabla ya kutimuliwa kocha wa Brazil
BRAZIL imemtimua kocha Luiz Felipe Scolari saa chache tu baada ya kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia ambalo walikumbana na vipigo vyao viwili vibaya zaidi katika historia yao ya michuano hiyo, moja ya magazeti yanayoongoza Brazil liliripoti jana.
Kikosi cha kocha Scolari cha Brazil kilikuwa kikipewa nafasi ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo lakini kilikumbana na kipigo cha aibu cha magoli 7-1 katika nusu fainali dhidi ya waliokuja kuwa mabingwa Ujerumani. Katika kukamilisha mwisho wao mbaya, walikumbana na kipigo kingine cha 3-0 dhidi ya Uholanzi katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu.
Scolari, ambaye aliiongoza Brazil kutwaa taji lao la tano na la mwisho la Kombe la Dunia 2002, alisema baada ya mechi hiyo kwamba atawasilisha ripoti kwa mabosi wake katika Shirikisho la Soka la Brazil (CBF) na ni wakati huo tu hatima yake itaamuliwa.
Lakini gazeti la O Globo liliripoti jana kwamba Scolari alitimuliwa Jumapili usiku. Gazeti hilo lilisema taarifa rasmi ingetoka baadaye jana.
Hapakuwa na uthibitisho kutoka CBF, wala mshauri wa habari wa Scolari.
Scolari aliichukua timu hiyo Novemba 2012 na amepoteza mechi tano tu kati ya 29 alizokuwa madarakani. Aliiongoza Brazil kutwaa Kombe la Mabingwa wa Mabara mwaka jana kwa ushindi wa kukumbukwa wa 3-0 dhidi ya mabingwa wa dunia wa wakati huo Hispania katika mechi ya fainali.
Alikuwa ni mtu anayependwa sana Brazil kwa ucheshi wake na pia kwa wachezaji ambao humchukulia kama baba yao.
Alikuwa na sapoti ya taifa kuelekea kwenye Kombe la Dunia na kulikuwa na upinzani mdogo kwa kikosi alichoteua, jambo ambalo ni nadra sana nchini Brazil, kunakofahamika kama "taifa la makocha milioni 200."
Kama kuondoka kwake kutathibitishwa, makocha wanaopewa nafasi ya mapema kama warithi wake watakuwa ni Tite, kocha ambaye aliiongoza Corinthians kutwaa Kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Amerika Kusini (Copa Libertadores) na Kombe la Dunia la Klabu 2012, na Muricy Ramalho, ambaye ni kocha wa sasa wa klabu ya Sao Paulo.