STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 3, 2014

Huu ndiyo usajili wa klabu za Ligi Kuu ya England 2014-2015

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article4073719.ece/alternates/s615/United-targets.jpg
DIRISHA la usajili kwa wachezaji barani Ulaya ulifungwa rasmi juzi, hapa chini tumewawekea orodha ya usajili kwa klabu za Ligi Kuu ya England. Ebu chungulia ujue nani kaenda wapi na nani katua wapi msimu huu.


ARSENAL

IN

Alexis Sanchez (Barcelona, £30m), Calum Chambers (Southampton, £12m), Mathieu Debuchy (Newcastle, £10m), David Ospina (Nice, £3m), Danny Welbeck (Manchester United, £16m)

OUT

Thomas Vermaelen (Barcelona, £15m), Johan Djourou (Hamburg, undisclosed), Thomas Eisfeld (Fulham, undisclosed), Bacary Sagna (Manchester City, free), Lukasz Fabianski (Swansea, free), Nicklas Bendtner (Wolfsburg, free), Park Chu-young (released), Chuks Aneke (Zulte Waregem, free), Daniel Boateng (released), Wellington Silva (Almeria, loan), Carl Jenkinson (West Ham, loan), Benik Afobe (MK Dons, loan), Ignasi Miquel (Norwich, undisclosed), Ryo Miyaichi (Twente, loan)

Click here for the latest Arsenal transfer news

ASTON VILLA

IN

Carlos Sanchez (Elche, £4.7m), Aly Cissokho (Valencia, £2m),  Philippe Senderos (Fulham, free), Joe Cole (West Ham, free), Tom Leggett (Southampton, undisclosed), Isaac Nehemie (Southampton, undisclosed), Kieran Richardson (Fulham, undisclosed)

OUT

Marc Albrighton (Leicester City, free), Nathan Delfouneso (Blackpool, free), Jordan Bowery (Rotherham, undisclosed), Samir Carruthers (MK Dons, undisclosed), Nicklas Helenius (Aalborg, loan), Yacouba Sylla (Kayseri Erciyesspor, loan), Jed Steer (Doncaster Rovers, loan), Antonio Luna (Hellas Verona, loan), Aleksandar Tonev (Celtic, loan), Joe Bennett (Brighton, loan), Gary Gardner (Brighton, loan)

Click here for the latest Aston Villa transfer news

BURNLEY

IN

Lukas Jutkiewicz (Middlesbrough, £2.5m), Michael Kightly (Stoke, undisclosed), Stephen Ward (Wolves, undisclosed), Marvin Sordell (Bolton, free), Matt Gilks (Blackpool, free), Matt Taylor (West Ham, free), Steven Reid (West Brom, free), George Boyd (Hull, £3m), Michael Keane (Manchester United, loan), Nathaniel Chalobah (Chelsea, loan)

OUT

Chris Baird (West Brom, free), Junior Stanislas (Bournemouth, free), David Edgar (Birmingham, free), Keith Treacy (Barnsley, free), Brian Stock (released), Nick Liversedge (Guisborough Town, free), Luke O'Neill (Scunthorpe, loan)

CHELSEA

IN

Cesc Fabregas (Barcelona, £30m), Diego Costa (Atletico Mdrid, £32m), Filipe Luis (Atletico, £16m), Loic Remy (QPR, £8m), Mario Pasalic (Hadjuk Split, undisclosed), Didier Drogba (Galatasaray, free)

OUT

David Luiz (Paris Saint-Germain, £50m), Romelu Lukaku (Everton, £28m), Demba Ba (Besiktas, £8m), Ashley Cole (Roma, £1.5m), Patrick van Aanholt (Sunderland, undisclosed), Samuel Eto'o (Everton, free), Frank Lampard (New York City, free), Sam Hutchinson (Sheffield Wednesday, free), Henrique Hilario (retired), Wallace (Vitesse Arnhem, loan), Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, loan) Thorgan Hazard (Borussia Monchengladbach, loan), Mario Pasalic (Elche, loan), Ryan Bertrand (Southampton, loan), Gael Kakuta (Rayo Vallecano, loan), John Swift (Rotherham, loan), Oriol Romeu (Valencia, loan) Christian Atsu (Everton, loan), Victor Moses (Stoke, loan), Marko Marin (Fiorentina, loan), Josh McEachran (Vitesse Arnhem, loan), Patrick Bamford (Middlesbrough, loan), Fernando Torres (AC Milan, loan) Marco van Ginkel (AC Milan, loan), Nathaniel Chalobah (Burnley, loan), Jamal Blackman (Middlesbrough, loan)

Click here for the latest Chelsea transfer news

CRYSTAL PALACE

IN

Martin Kelly (Liverpool, £1.5m), Fraizer Campbell (Cardiff, £800,000), Chris Kettings (Blackpool, free), Brede Hangeland (Fulham, free), Wilfried Zaha (Manchester United, loan),
Zeki Fryers (Tottenham, £3m), James McArthur (Wigan, £7m), Kevin Doyle (Wolves, loan)

OUT

Jonathan Parr (Ipswich, free), Dean Moxey (Bolton, free), Aaron Wilbraham (Bristol City, free), Kagisho Dikgacoi (Cardiff, free), Danny Gabbidon (Cardiff, free), Neil Alexander (Hearts, free), Ibra Sekajja (released), Alex Wynter (Portsmouth, loan), Kwesi Appiah (Cambridge, loan), Jose Campana (Sampdoria, undisclosed), Jack Hunt (Nottingham Forest, loan), Stephen Dobbie (Fleetwood, loan), Glenn Murray (Reading, loan)
EVERTON

IN

Romelu Lukaku (Chelsea, £28m), Gareth Barry (Manchester City, free), Samuel Eto'o (Chelsea, free), Muhamed Besic (Ferencvaros, £4m), Brendan Galloway (MK Dons, undisclosed) Christian Atsu (Chelsea, loan)

OUT

Apostolos Vellios, (Lierse, free), Magaye Gueye (Millwall, free), Shane Duffy (Blackburn, undisclosed fee)

Click here for the latest Everton transfer news

HULL

IN

Robert Snodgrass (Norwich, £8m), Jake Livermore (Tottenham, £6m), Michael Dawson (Tottenham, £6m), Mohamed Diame (West Ham, £3.5m), Harry Maguire (Sheffield United, £2.5m), Andrew Robertson (Dundee United, £2.85m), Brian Lenihan (Cork City, undisclosed), Tom Ince (Blackpool, free), Gaston Ramirez (Southampton, loan), Hatem ben Arfa (Newcastle, loan), Abel Hernandez (Palermo, £10m), Mohamed Diame (West Ham, £3.5m)

OUT

Shane Long (Southampton, £12m)Matty Fryatt (Nottingham Forest, free), Cameron Stewart (Ipswich, free), Nick Proschwitz (Brentford, free), Robert Koren (Melbourne City, free), Abdoulaye Faye (released), Conor Henderson (Crawley, free), Dougie Wilson (released), Conor Townsend (Dundee United, loan), Joe Dudgeon (Barnsley, loan), George Boyd (Burnley, £3m)
LEICESTER CITY

IN

Leonardo Ulloa (Brighton, £7m), Danny Simpson (QPR, undisclosed), Esteban Cambiasso (Inter Milan, free), Matthew Upson (Brighton, free), Marc Albrighton (Aston Villa, free), Ben Hamer (Charlton, free), Jack Barmby (Manchester United, free), Louis Rowley (Manchester United, free), Tom Lawrence (Manchester United, £1m), Nick Powell (Manchester United, loan), Kris Scott (Swansea, free)

OUT

Lloyd Dyer (Watford, free), Neil Danns (Bolton, free), Sean St Ledger (released), Zak Whitbread (Derby, free), Paul Gallagher (Preston, loan), Marko Futacs (Mersin Idmanyurdu, free), George Taft (Burton Albion, free), Conrad Logan (Rochdale, loan), Ryan Watson (Northampton, loan)

LIVERPOOL

IN

Adam Lallana (Southampton, £23m), Lazar Markovic (Benfica, £20m), Mario Balotelli (AC Milan, £16m), Alberto Moreno (Sevilla, £12m), Emre Can (Bayer Leverkusen, £9.8m), Rickie Lambert (Southampton, £4m) Dejan Lovren (Southampton, £20m), Divock Origi (Lille, £10m), Kevin Stewart (Tottenham, free), Javier Manquillo (Atletico Madrid, loan)

OUT

Luis Suarez (Barcelona, £75m), Pepe Reina (Bayern Munich £2m), Martin Kelly (Crystal Palace, £1.5m), Conor Coady (Huddersfield, £500,000), Daniel Agger (Brondby, undisclosed), Jack Robinson (QPR, undisclosed), Luis Alberto (Malaga, loan), Iago Aspas (Sevilla, loan), Andre Wisdom (West Brom, loan), Divock Origi (Lille, loan), Brad Smith (Swindon, loan), Joao Carlos Teixeira (Brighton, loan), Tiago Llori (Bordeaux, loan), Jordan Ibe (Derby, loan), Sebastian Coates (Sunderland, loan), Oussama Assaidi (Stoke, loan)

Click here for the latest Liverpool transfer news

MANCHESTER CITY

IN

Eliaquim Mangala (Porto, £32million)Fernando (Porto, £12m), Willy Caballero (Malaga, £6m), Bruno Zuculini (Racing Club, £3m), Bacary Sagna (Arsenal, free), Frank Lampard (New York City, loan)

OUT

Javi Garcia (Zenit, £13m), Costel Pantilimon (Sunderland, free), Joleon Lescott (West Brom, free) Gareth Barry (Everton, free), Alex Nimely (released), Rony Lopes (Lille, loan), Emyr Huws (Wigan, undisclosed), Reece Wabara (Doncaster Rovers, free), Jack Rodwell (Sunderland, £7m), Jason Denayer (Celtic, loan), Micah Richards (Fiorentina, loan), Alvaro Negredo (Manchester City, loan)

Click here for the latest Manchester City transfer news

MANCHESTER UNITED

IN

Angel di Maria (Real Madrid £59.7m), Luke Shaw (Southampton, £31.5m), Ander Herrera (Athletic Bilbao, £29m), Marcos Rojo (Sporting Lisbon, £16m), Daley Blind (Ajax, £14m), Vanja Milinkovic (FK Vojvodina, undisclosed), Radamel Falcao (Monaco, loan)

OUT

Shinji Kagawa (Borussia Dortmund £6.3m), Alexander Buttner (Dinamo Moscow, £5.6m)Patrice Evra (Juventus, £2.5m) Bebe (Benfica, £2.4m), Rio Ferdinand (QPR, free), Nemanja Vidic (Inter Milan, free), Federico Macheda (Cardiff City, free), Jack Barmby (Leicester, free), Louis Rowley (Leicester, free) Ryan Giggs (retired), Angelo Henriquez (Dinamo Zagreb, loan), Nani (Sporting Lisbon, loan), Wilfried Zaha (Crystal Palace, loan) Javier Hernandez (Real Madrid, loan), Tom Lawrence (Leicester, £1m), Danny Welbeck (Arsenal, £16m), Nick Powell (Leicester, loan), Michael Keane (Burnley, loan)

Click here for the latest Manchester United transfer news

NEWCASTLE

IN

Remy Cabella (Montpellier, £12m), Emmanuel Riviere (Monaco, £6m), Siem de Jong (Ajax, £6m), Daryl Janmaat (Feyenoord, £5m), Jamaal Lascelles and Karl Darlow (Nottingham Forest, £7million - joint fee), Ayoze Perez (Tenerife, £1.5m), Jack Colback (Sunderland, free), Facundo Ferreyra (Shakhtar Donetsk, loan)

OUT

Mathieu Debuchy (Arsenal, £10m), James Tavernier (Wigan, undisclosed), Dan Gosling (Bournemouth, free), Shola Ameobi (Gaziantep, free), Romain Amalfitano (Dijon, free), Conor Newton (Rotherham, free), Michael Richardson (released), Sylvain Marveaux (Guingamp, loan), Jamaal Lascelles (Nottingham Forest, loan), Karl Darlow (Nottingham Forest loan), Adam Campbell (Fleetwood, loan), Mapou Yanga-Mbiwa (Roma, loan),Hatem ben Arfa (Hull, loan)

Click here for the latest Newcastle transfer news

QUEENS PARK RANGERS

IN

Steven Caukler (Cardiff, £8m), Leroy Fer (Norwich, £7m), Jordon Mutch (Cardiff, £6m), Alex McCarthy (Reading, £6m), Jack Robinson (Liverpool, undisclosed), Rio Ferdinand (Manchester United, free), Mauricio Isla (Juventus, loan), Eduardo Vargas (Napoli, loan), Sandro (Tottenham, £10m), Niko Kranjcar (Dynamo Kiev, loan)

OUT

Loic Remy (Chelsea, £8m), Yossi Benayoun (Maccabi Haifa, undisclosed), Esteban Granero (Real Sociedad, undisclosed), Danny Simpson (Leicester, undisclosed), Julio Cesar (Benfica, free), Tom Hitchcock (Mk Dons, free), Aaron Hughes (Brighton, free), Gary O'Neil (Norwich, free), Stephabne Mbia (Sevilla, free), Andrew Johnson (released), Luke Young (released), Hogan Ephraim (released), Angelo Balanta (released), Park Ji-sung (retired), Jack Robinson (Huddersfield, loan), Samba Diakite (Al-Ittihad, loan)

Click here for the latest Queens Park Rangers transfer news

SOUTHAMPTON 

IN

Shane Long (Hull, £12m), Sadio Mane (Red Bull Salzburg (£11.8m), Dusan Tadic (Twente, £10.3m), Fraser Forster (Celtic, £10m), Graziano Pelle (Feyenoord, £8m), Florin Gardos (Steaua Bucharest, undisclosed), Ryan Bertrand (Chelsea, loan), Toby Alderweireld (Atletico Madrid, loan)

OUT

Luke Shaw (Manchester United, £31.5m), Adam Lallana (Liverpool, £23m),  Dejan Lovren (Liverpool, £20m), Calum Chambers (Arsenal, £12m), Rickie Lambert (Liverpool, £4m), Billy Sharp (Leeds, undisclosed), Tom Leggett (Aston Villa, undisclosed), Isaac Nehemie (Aston Villa, undisclosed), Guly do Prado (released), Lee Barnard (Southend, free), Jonathan Forte (Oldham, free), Danny Fox (Nottingham Forest, free), Andy Robinson (Bolton, free), Dani Osvaldo (Inter Milan, loan), Jos Hooiveld (Norwich, loan), Gaston Ramirez Hull (loan), Jack Stephens (Swindon, loan)

Click here for the latest Southampton transfer news


STOKE

IN

Mame Biram Diouf (Hannover, free), Dionatan Teixeira (Banska Bystrica, undisclosed), Phil Bardsley (Sunderland, free), Steve Sidwell (Fulham, free), Bojan Krkic (Barcelona, undisclosed), Victor Moses (Chelsea, loan), Oussama Assaidi (Liverpool, loan)

OUT

Michael Kightly (Burnley, undisclosed), Cameron Jerome (Norwich, undisclosed), Matthew Etherington (released), Juan Agudelo (released), Jamie Ness (Crewe, loan), Ryan Shotton (Derby, loan)

Click here for the latest Stoke transfer news

SUNDERLAND

IN

Jack Rodwell (Man City, £7m), Patrick van Aanholt (Chelsea, undisclosed), Billy Jones (West Brom, free), Jordi Gomez (Wigan, free), Costel Pantilimon (Manchester City, free), Santiago Vergini (Estudiantes, loan), Will Buckley (Brighton, £2.5m), Sebastian Coates (Liverpool, loan), Ricky Alvarez (Inter Milan, loan)

OUT

Ignacio Scocco (Newell's, £800,000), David Moberg Karlsson (Nordsjaelland, undisclosed), Jack Colback (Newcastle, free), Craig Gardner (West Brom, free), Phil Bardsley (Stoke, free), Billy Knott (Bradford, free) Keiren Westwood (Sheffield Wednesday, free), Carlos Cuellar (Norwich, free), Andrea Dossena (released), Louis Laing, Nottingham Forest, free), Oscar Ustari (Newell's, free), David Vaughan (Nottingham Forest, free), John Egan (Gillingham, free), Alfred N'Diaye (Real Betis, free), El Hadji Ba (Bastia, loan), Modibo Diakite (free), Valentin Roberge (Stade de Reims, loan)

Click here for the latest Sunderland transfer news

SWANSEA

IN

Federico Fernandez (Napoli, £8m), Jefferson Montero (Monarcas Morelia, £4m), Marvin Emnes (Middlesbrough, £1.5m), Stephen Kingsley (Falkirk, undisclosed), Gylfi Sigurdsson (Tottenham, swap), Adnan Maric, GAIS, undisclosed), Daniel James (Hull, undisclosed), Bafetimbi Gomis (Lyon, free), Lukasz Fabianski (Arsenal, free), Giancarlo Gallifuoco (Tottenham, free), James Demetriou (Nottingham Forest, free), Tom Carroll(Tottenham, loan), Modo Barrow (Ostersunds, undisclosed fee)

OUT

Ben Davies (Tottenham, £10m), Michel Vorm (Tottenham, £5m) Alejandro Pozuelo (Rayo Vallecano, undisclosed), Leroy Lita (Barnsley, free), Chico Flores (Lekhwiya, free), Pablo Hernandez (Al Arabi, free), Darnel Situ (AGF, free), David N'Gog (Stade de Reims, free), Jose Canas (Espanyol, free), Jernade Meade (released), Michu (Napoli, loan), Daniel Alfei (Northampton, loan), Alex Bray (Plymouth Argyle, loan), Kris Scott (Leicester, free)

Click here for all the latest Swansea transfer news

TOTTENHAM

IN

Federico Fazio (Sevilla, £8m), Ben Davies (Swansea, swap), Michel Vorm (Swansea, £5m), Benjamin Stambouli (Montpellier, £4.7m), Eric Dier (Sporting Lisbon, £4m) DeAndre Yedlin (Seattle Sounders, undisclosed)*

*will join in summer 2015

OUT

Jake Livermore (Hull, £6m), Michael Dawson (Hull, £6m), Gylfi Sigurdsson (Swansea, swap), Iago Falque (Genoa, £4m) Heurelho Gomes (Watford, free), Giancarlo Gallifuoco (Swansea, free) Cameron Lancaster (Stevenage, free), Kevin Stewart (Liverpool, free), Alex Pritchard (Brentford, loan), Shaquile Coulthirst (Southend, loan), Tom Carroll (Swansea, loan), Ryan Fredericks (Middlesbrough, loan), Zeki Fryers (Crystal Palace, £3m), Jonathan Obika (Swindon Town, undisclosed), Tomislav Gomelt (Bari, undisclosed), Souleymane Coulibaly (Bari, undisclosed), Lewis Holtby (Hamburg, loan), Sandro (QPR, £10m)

Click here for the latest Tottenham transfer news

WEST BROMWICH ALBION

IN

Brown Ideye (Dynamo Kiev, £10m), Sebastien Pocognoli (Hannover 96, undisclosed), Sebastian Blanco (Metalist, undisclosed), Jason Davidson (Heracles, undisclosed), Cristian Gamboa (Rosenborg, undisclosed), Georgios Samaras (Celtic, free), Craig Gardner (Sunderland, free), Joleon Lescott (Manchester City free), Chris Baird (Burnley, free), Andre Wisdom (Liverpool, loan), Silvestre Varela (Porto, loan)

OUT

Liam Ridgewell (Portland Timbers, free), Billy Jones (Sunderland, free), Steven Reid (Burnley, free), Cameron Gayle (Shrewsbury, free), Diego Lugano (released), Zoltan Gera, Ferencvaros), Nicolas Anelka (released), George Thorne (Derby County, undisclosed)

Click here for the latest West Bromwich transfer news

WEST HAM

IN

Enner Valencia (Pachuca, £12m), Cheikhou Kouyate (Anderlecht, £7m), Mauro Zarate (Velez Sarsfield, undisclosed), Diafra Sakho (Metz, undisclosed), Aaron Cresswell (Ipswich, undisclosed), Diego Poyet (Charlton, undisclosed), Carl Jenkinson (Arsenal, loan), Alex Song (Barcelona, loan), Morgan Amalfitano (Marseille, £1m)

OUT

Mohamed Diame (Hull, £3.5m), Joe Cole (Aston Villa, free), Matt Taylor (Burnley, free), Stephen Henderson (Charlton, free), Jack Collison (released), George McCartney (released), Callum Driver (Whitehawk, free), Jordan Spence (MK Dons), George Moncur (Colchester, free), Alou Diarra (released), Modibo Maiga (Metz, loan), Mohamed Diame (Hull, £3.5m)

Click here for the latest West Ham transfer news


Simba kuivaa Gor Mahia, APR Rwanda Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgS8yGNNyLUxojSyJgWfzxjwspJTmCCQTtAXWGZi_oPH8C6Muu3uhYBA_5qD7blI4qL-uZZ51CCeNXk31YX8vvqn6StZcrA9evQMyIgs7VOmqssvhti3RuJpWiYm9Zr_hEhQ2ziA0PGPoLr/s1600/simba+sc.JPGTIMU kongwe ya soka nchini, Simba mwishoni mwa wiki hii itacheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Gor Mahia ya Kenya. 
Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo awali ilielezwa kuwa Simba ingecheza na Mtibwa Sugar kabla ya kuwepo kwa mabadiliko hayo. Taarifa toka ndani ya Simba zimesema maandalizi ya mechi hiyo yanaendelea vizuri, timu ikiwa kambini Zanzibar, chini ya Kocha wake mzoefu, Patrick Phiri kutoka Zambia. Kwa mujibu wa habari hizo, Simba huenda ikacheza mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa wiki ijayo kwa kumenyana na APR ya Rwanda. Mechi dhidi ya Gor Mahia itapigwa Jumamosi wakati mechi dhidi ya APR itapigwa Jumatano ijayo kwenye uwanja huo na ni maelekezo ya kocha Phiri.

Ofisi ya Mkemia Mkuu yafichua siri nzito

https://2.bp.blogspot.com/-syyeXsLD9iE/VAWl9uREXOI/AAAAAAAAXks/rKiF1w4_3L4/s1600/Gloria%2BOmary.jpg
Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Makosa ya Jinai na Vinasaba Gloria Omar (kushoto) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. 
SULEIMAN MSUYAOFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imesema upungufu wa rasilimali watu, gharama kubwa za undeshaji, mchakato mrefu wa manunuzi ni baadhi ya changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili ofisi hiyo.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Makosa ya Jinai na Vinasaba Gloria Omar wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
Alisema changamoto nyingine ni uhitaji wa mitambo mipya inayoweza kubaini dawa za kulevya zenye mchanganyiko na kemikali bashirifu pamoja na matengenezo ya jingo la maabara ya uchunguzi wa makosa ya jinai.
Omar alisema iwapo changamoto hizo zitatatuliwa kwa wakati ofisi yao itaongeza tija katika ufanikishaji wa kazi zake kila siku kama ilivyo kuwa hapo awali.
Mkurugenzi huyo alisema baadhi ya mashine zina muda mrefu na pia zinauzwa bei kubwa ufinyu wa bajeti unakwamisha kununua zingine hali ambayo inasababisha kutoendana  na wakati kulingana na mabadiliko ya sampuli ambazo zinapatikana.
“ Ofisi yetu imepata mafanikio baadhi lakini changamoto ni kubwa kama nilivyozitaja hapo awali jambo ambalo kwa njia moja zinakwamisha malengo yetu” ,alisema.
Alitaja baadhi ya mafanikio ambayo yalipatikana  kwa kipindi cha mwaka 2013  ni Ofisi hiyo kuchunguza majalada 208, utoaji ushahidi mahakamani umeimarishwa na takwimu zimehuhishwa kwa kutumia mfumo wa komputa.
Mafanikio mengine ni kushirika maonyesho ya kimataifa yanayohusu uzuiwaji usafirishaji wa dawa za kulevya na kushiriki katika shughuli za kikosi kazi cha kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Mkurugenzi huyo wa Idara ya Sayansi ya Makosa ya Jinai na Vinasaba alisema bajeti ya shilingi bilioni 1.4 imetengwa kwa ajili ya mitambo ya LCMS MS na GCMS MS kwa kipindi cha mwaka 2014/2015.
Aidha Omar alisema Ofisi ya Mkemia inapendekeza kuongezewa rasilimali watu pamoja na matumizi ya teknohama kwa kufanya mfumo mzima wa ununuzi, kutenga bajeti ya kotosha katika ofisi hiyo.
Mapendekezo mengine ni Serikali kuhakikisha kuwa inawapatia mashine za kisasa ambazo zitakuwa zikitoa majibu kulingana na wakati pamoja na mahitaji ya watu.
Kuhusiana na matokeo ya watu wanaopima vinasaba (DNA) kuonyesha asilimia 50 ya watu waliopima kuwa wanasingiziwa watoto alisema matokeo hayo ni sahihi jambo ambalo linapaswa kuangaliwa kwa makini nini sababu yake.
Alisema kwa mtu yeyote ambaye anahitaji kufanya vipimo anahitajika kufuata taratibu zote za kisheria pamoja na kulipa kiasi cha shilingi laki moja kwa kila sampuli moja.
Mwisho.

Azam, Yanga sasa kukipiga Sept 14 Ngao ya Hisani


Azam
Yanga
PAMBANO la kuwania Ngao ya Hisani kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania 2014-2015 uliokuwa ufanyike Septemba 13 kati ya mabingwa Azam na Yanga walioshika nafasi ya pili msimu uliopita utacheza siku ya Jumapili ya Septemba 14 imefahamika.
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, mchezo utapigwa kwenye uwanja wa Taifa siku moja mbele tofauti na tarehe ya awali.
Mchezo huo utaambatana na shughuli za kijamii kama uchangiaji damu na maonyesho ya shughuli za wadau na maendeleo ya jamii Shirikisho la soka Tanzania (TFF) hutoa sehemu ya mapato ya mchezo huu kwa shirika/shughuli ya kijamii iliyochaguliwa kwa mwaka husika.
Yanga na Azam kwa sasa zipo kwenye maandalizi ya pambano hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa kutokana na ushindani ulioibuka baina ya timu hizo kwa siku za karibuni.

Yanga kujipima kwa Wakenya leo

Yanga
http://static.goal.com/258600/258645_heroa.jpg
Thika United
BAADA ya kupata ushindi katika mechi tatu mfululizo za kujipima nguvu dhidi ya timu za visiwani Zanzibar, Yanga ya kocha Marcio Maximo itakuwa kibaruani leo itakapowakabili Thika Utd ya Kenya.
Thika United inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya, imeshatua jijini Dar tayari kwa mechi hiyo itakayokuwa ya kwanza ya kwanza ya kirafiki ya kimataifa kwa Maximo.

Pia ni mechi ya kwanza kwa Yanga na Maximo kucheza kwenye dimba la Taifa, litakalotumika kwa mchezo huo ambao mashabiki wangependa kuona vipaji vyao vipya vilivyosajiliwa na kukimbizwa Pemba kwenye kambi.
Baadhi ya wachezaji wa Yanga wanaotarajiwa kuwa kivutio leo ni Geilson Santana 'Jaja' na ,Andrey Coutinho toka Brazil, Edward Charles na Said Juma waliosajiliwa hivi karibuni pamoja na vifaa vingine vya zamani.
Viingilio vya mchezo huo ni: VIP A Tshs 30,000/=
VIP B & C Tshs 20,000/= Orange Tshs 10,000/=
Bluu & Kijani Tshs 5,000/= 

Jumba la Big Brother Laungua moto uzinduzi waahirishwa

M-Net na kampuni ya production ya Endemol wamethibitisha kuungua kwa moto jumba la mashindano ya Big Brother Huko South na kutoa taarifa kuwa mashindano haya yamehairishwa mpaka itakapotolewa taarifa zaidi.
Hakuna mtu aliyumia wala kupoteza maisha na mpaka sasa haijajulikana chanzo cha moto ni nini. M-Net na Endemol wameshaanza kutafuta jumba la kufanyia show ya mwaka huu na kutafuta vifaa vipya baada ya camera na editing instruments kuungua moto.
bba 1 bba 4 bbabba 7

Lady Jaydee Balozi wa Uzazi wa Mpango wa Maria Stopes

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marie Stopes Tanzania (MST), Uller Muller (kulia) akikabidhi kisanduku chenye vifaa vinavyohusika na masuala ya uzazi wa mpango kwa Balozi mpya wa Marie Stopes ambaye pia ni msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura 'Lady jaydee' katika hafla ya utiaji saini makubaliano hayo katika ofisi za MST, jijiji Dar es Salaam jana

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Judith Wambura 'Lady Jaydee', ameteuliwa kuwa Balozi mpya wa Marie Stopes,katika kampeni za uzazi wa mpango.
Akitangazwa rasmi kuwa balozi mpya msanii Jay Dee aliibua shangwe na nderemo zilizotoka kwa baadhi ya wazazi na watu waliohudhuria hafla hiyo iliyofanyika kwenye Ofisi za MST zilizopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Jay Dee sasa anaungana na Marie Stopes kwenye kampeni ya “Chagua Maisha” ambayo inalenga kuboresha upatikanaji wa huduma za uzazi wa mpango katika jamii.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutangazwa rasmi, Jaydee alisema kuwa amefurahi sana kupata nafasi hiyo ambayo anaamini ataitendea haki kulingana na nafasi yake kwa jamii.
“Nina furaha kubwa kuchukuka nafasi hii ya kipekee kama Balozi wa Marie Stopes kwa sababu wanafanya mengi kuwawezesha kina mama kusimama na kujitegemea, na pia naamini nitafanya kazi nzuri kwa ushirikiano na Marie stopes ili kuiwezesha Jamii kufikia na kuelewa vyema lengo la Uzazi wa mpango''. alisema Jay dee
Lengo kuu la Kampeni hii ya Chagua Maisha nikuhakikisha kila Mtanzania ana haki ya kuchagua mfumo wa uzazi wa mpango ili kulinda afya zao na kutimiza malengo yao ya kimaisha, hususan mabinti wadogo”.
Akitafakari sababu zilizompeleka kuungana na kampeni hii, Lady Jaydee alieleza: “siku zote nilikuwa naamini kuwa wanawake wana uwezo wa kubadilisha Tanzania kimaendeleo. Hivyo niliumizwa moyo sana nilipoambiwa hivi leo kuwa Wanawake wengi hupoteza maisha, na wasichana wengi wanalazimishwa kuacha masomo kutoka na ujauzito. Mimi nimeamua kusaidiana na Marie Stopes kuelimisha jamii nzima wanaweza kubalili fikra na hatima zao, kwa kutumia uzazi wa mpango”.
Takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza kwenye idadi ya vijana, 54% wakiwa chini ya umri wa miaka 20. Vijana hawa wana uwezo wa kubadili na kukuza hali ya kiuchumi ya Tanzania ndani ya miaka 10 ijayo iwapo watapata msaada.
Akiwa amesimama Pamoja na Lady Jaydee, Bi Muller alikuwa na haya ya kusema: “Leo hii nchini Tanzania, mmjoa kati ya kila Wanawake wane chini ya umri wa miaka 19 wamekwisha kuwa wazazi na asilimia 20% ya Wanawake chini ya umri wa miaka 20 wamo katika ndoa za kulazimishwa.
Zaidi ya hayo, kama binti akipata ujauzito hata kwa kubakwa, anafukuzwa shule na huo ndio unakuwa mwisho wa elimu yake. Haya siyo mazingira mazuri ambayo vijana wetu wanahitaji iwapo wana matumaini ya kukuza uchumi wa taifa letu na kuliweka kuwa katika kipato cha kati (middle income). Wanawake wana uwezo mkubwa wa kuchangia kukua kwa taifa letu, hivyo ni jukumu letu kuwapa fursa hizo”.
“Nina imani kubwa kuwa tutafanikiwa”, aliongeza Lady Jaydee, “tunataka kila mmoja atambue kuwa ana haki ya kuchagua muda na wakati wa kupata watoto, na pia idadi ya watoto wanaowataka. Marie Stopes na taasisi nyingine zinaweza kukusaidia kumaliza masomo yako na kuhakikisha kuwa una maliza elimu na kuwa na mwanzo mzuri wa maisha, kabla hujaamua kuwa mzazi. Name nitaanza kueneza ujumbe huu Jumamosi hii kwenya Nyama Choma Festival, Dar es Salaam!”
Tukio hili la Lady Jaydee kutembelea Hospitali ya Marie Stopes jijini Dar es Salaam litaonyeshwa jumapili tarehe 07 Septemba kwenye East Africa TV. Kituo hiki kilichopo Mwenge ni miongoni mwa hospitali 11 za Marie Stopes nchini Tanzania. Zote hizi zinatoa huduma za uzazi wa mpango kwa Wanawake bure kabisa bila malipo yoyote.

Vyombo vya Dola lawamani Haki za Binadamu

SULEIMAN MSUYA
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHGG) imesema asilimia kubwa ya ukiukwaji wa haki za binadamu hapa nchini unaanzia pale mtu anapokamatwa na vyombo vya dola kwenye mahojiano pamoja na mahabusu.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Kisheria (CHGG) Nabor Assey wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Assey alisema utafiti unaonyesha kuwa wengi wao wanakamatwa pasipo utaratibu, kudhalilishwa, kuteswa, kubambikiwa kesi, kuwekwa muda mrefu bila kufikishwa mahakamani na kuwepo mazingira magumu ya dhamana jambo linalokiuka haki za binadamu zilizoainishwa katika ibara ya12 mpaka 24 ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na sheria zingine za nchi na mikataba ya kimataifa iliyoridhiwa.
Mkurugenzi huyo utafiti huo unaonyesha kuwa asilimia 50 ya watu wanaoshikiliwa maeneo mbalimbali nchini ni mahabusu ambao ama wanasubiri kufikishwa mahakani au kesi zao zinaendelea katika mahakama mbalimbali bado hawajahukumiwa.
“Napenda kuweka wazi kuwa hii ni Idara huru ya Serikali tunachokisema hapa ni katika juhudi za kusaidia serikali kutatua changamoto ambazo zinaikabili jamii yake hasa katika masuala ya haki za binadamu” alisema.
Assey alisema ni wazi kuwa vyombo vya dola hasa jeshi la polisi limekuwa likishutumiwa kwa ukiukwaji wa haki za binadamu hali ambayo inahitaji elimu zaidi ambayo inaweza kusaidia kutatua tatizo hilo.
Alisema ni vema dhana halisi ya jina la polisi (Pilice Force) kubadishwa na kuwa (Police Service) ili kuwapatia uelewa kuwa wanapaswa kutoa huduma na sio kutumia nguvu zaidi kama njia ya kukabiliana na tatizo.
Mkurugenzi huyo alisema pia kuna mapungufu katika mfumo wa sheria za jina za Tanzania akitolea mfano ibara ya 13(6) (e) ya Katiba ya Tanzania ya 1977  inakataza utesaji kwa watuhumiwa na kuelekeza mamlaka za nchi kutunga sheria kwa minajili hiyo.
Alisema bado kuna  upungufu katika sheria kwani kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi  sura ya 6 ya sheria za Tanzania kinakata ushahidi uliopatikana kwa shinikizo la aina yoyote kutumika kama ushahidi halali mbele ya mahakama.
Assey alisema pamoja na sheria hizo kuonyesha ukatazo bado hazijaonyesha ni hatua gani atachukuliwa mtumishi yeyote ambaye atabainika kufanya vitengo vinavyokiuka haki za binadamu.
Alisema Tume yao ipo katika mchakato wa kuhakikisha kuwa vyombo vya usalama vinapatiwa elimu yakutosha juu ya nini majukumu yao pale ambapo wanamshikilia mtu ambaye amefanya kosa.
Mkurugenzi huyo alisema jitihada hizo zinatakuwa zikishirikisha wananchi hasa kwa kudai haki zao ambazo hazipo kisheria ambao wanaonekana kuwa waathirika wakubwa kutokana na vyombo vya dola hasa Jeshi la Polisi.

Tuesday, September 2, 2014

Hatem Ben Arfa atimkia Hull City kwea mkopo

Kiungo Ben Hatem wakati akiitumikia Newcastle United

MCHEZAJI Hatem Ben Arfa wa Newcastle United amejiunga na klabu ya Hull City kwa mkopo kwa kipindi kilicho baki cha msimu akimaliza safari yake ndani ya klabu yake ya Newcastle.
Ben Arfa amekuwa katika wakati mgumu katika kikosi cha Newcastle, licha ya mchango wake mkubwa tangu alipojiunga nao.

Blind atua Mashetani Wekundu mtazame katika uzi mpya

Daley Blind aliyekamilisha uhamisho United
KLABU ya Ajax imethibitisha kuwa Daley Blind amejiunga na  Manchester United.
Vilabu hivyo vimefikia makubaliano kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi uwanjani wiki iliyopita ambapo United na Ajax walikubaliana ada ya uhamisho wake kufikia pauni milion £14.2 hii ikiwa ni baada ya mawindo ya muda mrefu ya mashitani wekundu.
Sasa imethibtishwa kua Blind atakuwa akiichezea United msimu huu baada ya kufanikiwa vipimo vya afya na kukubali maslahi ndani ya mshahara wake na kigogo hicho cha Premier League.
Blind ni mtoto wa nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi Danny, ambaye alikuwa ni msaidizi wa bosi wa United Louis van Gaal katika kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi katika michuano ya kombe la dunia na alianza kucheza soka kama mlinzi wa kushoto kabla ya kugeukia katika nafasi ya ulinzi wa kati katika klabu ya Ajax.

Miyeyusho kuyeyushana na Emilio Mkwakwani Nov 5

Miyeyusho na Emilio katika pozi
Wakitunishiana misuli
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa anayeshikilia mataji ya WBF na UBO, Francis Miyeyusho anatarajiwa kupanda ulingoni jijini Tanga kuzipiga na Mtanzania anayepigana nchini Kenyam Emilio Norfat.
Mabondia hao watapambana katika pigano la uzito wa Feather (kilo 57) siku ya Novemba 5 kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mratibu wa pambano hilo Anthony Rutta alisema maandalizi yameanza kwa kumalizana na mabondia hao wenye sifa zinazolingana kwa sasa katika medani ya ngumi ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
"Mabondia Francis Miyeyusho na Emilio Norfat wanatarajiwa kupanda ulingoni kupigana kwa mara ya kwanza Novemba 5 na watasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi siku hiyo," alisema Rutta.
Rutta alisema itakuwa mara ya kwanza kwa Miyeyusho kupanda ulingoni mkoani Tanga sawa na ilivyo kwa Emilio anayeshikilia nafasi ya pili nchini katika uzito huo wa Feather kati ya mabodia 60.
Emilio anashikilia kwa sasa taji la Afrika Mashariki na Kati la WPBC na rekodi zinaonyesha amecheza michezo 27 akishinda 23 na kupoteza minne, wakati Miyeyusho amecheza 51 ameshinda 38 na kupoteza 11 na kudroo miwili..
Pambano la mabondia hao litasimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) ambalo Rutta ndiye Katibu Mkuu wake.

Falcao katika uzi mpya baada ya kutambulishwa Old Trafford

Falcao akiwa katika uzi mpya wa Mashetani Wekundu
Akiteta na Kocha msaidizi, Ryan Giggs

KLABU ya Manchester United imemtambulisha mshambuliaji wake mpya kutoka Monaco, Ramadel Falcao, huku baadhi ya mashabiki wakipigwa na butwaa na kitendo cha kuongezwa mshambuliaji kikosini badala ya mabeki safu inayoonekana kupwaya baada ya kuondoka kwa visiki Rio Ferdinand, Nemanja Vidic na patrci Evra.

Ndege yaanguka Serengeti na kuua abiria wote


Ndege iliyopotea mapema jana ikitokea Mwanza kuelekea Magadi nchini Kenya, imepatikana huko eneo la Serengeti Mara, na abiria wote watatu waliokuwa kwenye ndege hiyo imetaarifiwa wamekufa.

WWF yatoa mafunzo kwa watumishi wa Manispaa ya Kinondoni

http://www.tic.co.tz/media/kinondoni.jpgSHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la WWF, limeendesha mafunzo kwa watumishi wa idara mbalimbali za Manispaa ya Kinondoni , kuhusiana na ueneaji wa hewa ukaa na matumizi sahihi ya nishati jadidifu nchini.
Mafunzo hayo yametolewa na Mratibu kutoka WWF.  Teresia Olemako aliyesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha  watumishi wa umma wanakuwa na ufahamu juu ya kukabiliana na madhara ya hewa ukaa na umuhimu wa kutumia nishati jadilifu.
Alisema mafunzo hayo yanahusu watumishi kutoka mikoa mitatu ambayo ni Dar es Salaam, Kilimanjaro na Arusha ambao majiji na miji yao imeingia katika shindano la kimataifa la kukabiliana na utunzaji wa mazingira ambalo litafanyika mwakani kwa kushirikisha nchi 18 duniani, Tanzania ikiwa ni mara ya kwanza.
Olemako alisema juhudi za WWF kwa kushirkiana na ICLEI ni kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya matumizi sahihi ya nishati jadilifu kwa lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira ambao unachangia kuwepo kwa mabadiliko ya tabia nchi kote duniani.
“WWF tumejipanga kushirikiana na watumishi wa mikoa hiyo niliyoitaja hapo juu kuhakikisha suala la kupunguza hewa ukaa na kuhimiza matumizi ya nishati jadilifu ni moja ya majukumu yao ambao watatumia mafunzo hayo kuwapatia wananchi elimu zaidi”, alisema.
Mratibu huyo wa Programu ya Nishati Jadilifu alisema mradi huo utakuwa ukitambaulika kwa kauli mbiu ya (Chakula, Nishati, Taka Ngumu na Maji) kutumika kama njia mbadala ya kukabiliana na uharibifu mazingira katika maeneo husika.
Alisema nishati jadilifu ikitumika ipasavyo itakuza uchumi wanchi pamoja na wananchi kwa ujumla kutokana na ukweli haina madhara na ipo kwa wakati wote hivyo ni vema kila mmoja kuwa balozi mzuri katika kuelimisha jamii.
Akizungumzia juu ya shindano hilo alisema ni vema kwa mikoa husika kufanya kila liwezekano ili kuweza kuleta ushindani wa kweli jambo ambalo linaweza kupelekea Tanzania kuibuka na ushindi ambao utakuwa kichochoe cha utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati jadilifu kuongezeka zaidi.
Aidha alisema kutokana na tathmin iliyofanywa na WWF inakadiriwa hadi mwaka 2025 jiji la Dar es salaam litakuwa na wakazi zaidi ya mil. 6.2 huku mahitaji ya kibinadamu yakiongezeka mara mbili zaidi ya sasa jambo ambalo linahitaji kufanyika maandalizi mapema kabla hali haijawa mbaya.
Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Injinia Mussa Natty, alisema kila idadi ya watu inapoongezeka, miundombinu na mahitaji ya kibinadamu pia huongezeka hivyo kuifanya jamii kuboresha mahitaji muhimu.
Natty alisema kutokana na hali hiyo WWF inapaswa kuongeza juhudi zaidi za kutoa elimu na kusaidia utekelezaji wa miradi ambayo inaweza kuwa na tija kwa Taifa na wananchi wake kwa vizazi vijavyo kwani kutokufanya hivyo kunaweza kuwa sababu ya kuleta mitafaruku mijini.
Mkurugenzi huyo alisema miradi kama hiyo ikiwa endelevu ni wazi kuwa kila mwanajamii atakuwa balozi mzuri wa kuhitaji mbadilo chanya ambao hayatamuathiri yeye na kizazi chache.
“Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza WWF Tanzania kwa kushirikina na WWW Sweden kwa kuja na mradi huu na manispaa yangu ikawa moja wapo naamini tutaufanyia kazi vizuri kwani sisi Kinondoni na Dar es Salaam kwa ujumla tumeathirika sana na mabadiliko ya Tania nchi”, alisema.
“Pia kila mmoja wetu ambaye ni mkazi wa jiji la Dar es salaam, anahitaji kuwajibika katika sehemu yake ili kuhakikisha mahitaji muhimu ya kibinadamu yanapatikana jirani na jamii ili kuiondoa jamii katika hali ya umasikini unaosababisha ukataji na uharibifu wa misitu”, alisema.
Naye Mwanasheria wa Jiji, Philip Mwakyusa aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Jiji, Wilson Kabwe alisema jiji limeupokea mradi kwa mikono yote na watatoa ushirikiano kwa WWF ili iweze kutekeleza mradi huo kwa mafanikio makubwa na ya yenye tija kwa jiji.

Arsenal yamnyakua Welbeck wa Man Utd

http://articles.squarefootball.net/.a/6a00e5521030508834019104738508970c-pi 
KOCHA Arsene Wenger amefanya jambo la maana katika kutatua tatizo la safu yake ya ushambuliaji baada ya kukubali kumsaini kwa Pauni Milioni 16 mshambuliaji wa England, Danny Welbeck.
Kocha huyo wa Arsenal, alikuwa Italia kuthibitisha ahadi ya kucheza mechi hisani, ameonyesha hisani inaanzia nyumbani baada ya kuwapiga bao Spurs kwa kumsaini mshambuliaji huyo wa Manchester United.
Welbeck, anayeondoka Old Trafford baada ya kushindwa kumvutia kocha Louis van Gaal tangu Mholanzi huyo awasili msimu huu, awali alitolewa kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kwa Pauni Milioni 3.
Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 akalazimishwa kuuzwa moja kwa moja aka pate mwanzo mzuri mpya na kuisaidia Arsenal kuilazimisha United kupunguza bei kutoka Pauni Milioni 18 walizotaka awali kabla ya mchezaji huyo kusaini Mkataba wa miaka mitano.

Ajali yaua baba, mtoto akiwa hoi kwa majeraha

MTU mmoja aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili  T. 495 ALM aina ya Nissan Pick Up amefariki dunia katika ajali mbaya, huku mtoto wake akijeruhiwa vibaya maeneo ya Nane Nane  jijini Mbeya usiku wa kuamkia jana majira ya saa saba za usiku.
Dereva huyo aliyefariki dunia amefahamika kwa jina la Boniface Mwasoba alifariki dunia baada ya gari hilo kuacha njia na kupinduka katika maeneo hayo ya Nane Nane achali iliyopelekea pia kujeruhiwa kwa mtoto wake anayefahamika kwa jina la Willy Boniface Mwasoba mwenye miaka 7 na mwanafunzi wa shule ya msingi Mkapa na amelazwa katika hospitali ya Rufaa jijini Mbeya.
Mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika japokuwa polisi bado wanaendelea na uchunguzi ili kubaini, lakini kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto kwa kuzingata sheria na alama za usalama wa barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.