STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Chelsea haitaki mchezo, yanasa kinda la zamani la Everton

Baadhi ya Wachezaji wa Chelsea
MNAHESABU lakini? Klabu ya Chelsea imeanza hesabu zake za kuimarisha kikosi chao, ikiwa ni siku chache tangu watunguliwe mabao 2-0 na Tottenham Hotspur kwa kumsainisha beki kinda wa zamani wa timu ya vijana ya  Everton, Kyle Jameson.
Kwa mujibu wa duru za kispoti zinasema Jameson, 18, amejiunga na Chelsea kama mchezaji huru kwa mkataba wa soka la kulipwa utakaoishia msimu wa 2017/18.
Beki huyo wa kati Chipukizi huyo aliwahi kushiriki Ligi ya Vijana akiwa na klabu ya Southport alianza kucheza soka katika klabu hiyo ya Merseyside kabla ya kwenda kwenye klabu za chini.
Taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa klabu ya Chjelsea umeandika; "Mipango yetu ya kuboresha kikosi chetu tumemsainisha Kyle Jameson. Beki huyo wa kati mwenye miaka 18 hakuwa amesajiliwa kokote na amesaini nasi mkataba wa soka la kulipwa utakaoisha mwishoni mwa msimu ujao."
Jameson ni mchezaji wa kwanza kusajiliwa Stamford Bridge wakati dirisha la usajili wa Januari likiwa limefunguliwa mapema wiki hii.

Rais wa Caf katika kashfa kama ya Blatter

Rais wa Caf, Issa Hayatou
WALIOSEMA kuwa, mwenzako akinyolewa nawe tia kichwa maji, hawakukosea kabisa.
Miezi kadhaa tangu aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter kuingia kwenye kashfa nzito ya Rushwa kiasi cha kumlazimu ajiuzulu nafasi yake kabla ya kufungiwa, mzimu wa tuhuma hizo sasa umehamia kwa mshirikisha wake mkubwa, Issa Hayatou Rais wa Shirikisho la Soka Afrika, CAF.
Mamlaka zinazosimamia Mashindano mbalimbali nchini Misri zimethibitisha kuwa Rais huyo wa CAF, atafikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka kutokana na tuhuma za rushwa zinazomkabili zikiwemo zile za utoaji haki za matangazo ya ligi mbalimbali.
Mamlaka hizo zimebainisha kuwa Hayatou alikiuka kipengele namba vifungu (A), (B), (C), (D), (E) za sheria za uhifadhi na ulinzi wa mashindano, baada ya kukiuka matakwa ya kazi yake na kuwapa haki za matangazo kampuni ya Lagardere Sports pekee pasipo kuweka wazi ili kampuni nyingine zenye uwezo pia zijitokeze.
Ripoti inasema kuwa Hayatou aliwapa Lagardere haki za matangazo kwa miaka 12 kuanzia mwaka 2017 mpaka mwaka 2028. CAF ilisaini kandarasi na Lagardere mwezi June 2015, ikiwa ni takribani mwaka mmoja kabla makubaliano ya haki hizo hayajakwisha. Ni sahihi pia kusema kuwa CAF iliwapa haki hizo Lagardere mwaka  2008 mpaka 2016, ikimaanisha kampuni hiyo imepewa mzigo huo kwa miaka 20.
Haki hizi hazikuwa kwa upande wa urushwaji matangazo kwa njia ya satellite peke yake bali hata kwa wenye matumizi ya tovuti, na sio kwa Misri na Afrika peke yake, bali dunia kwa ujumla.
Mamlaka hizo za mashindano ya Misri, zimeomba  CAF kuchukua hatua za haraka kutokana na kifungu cha sheria namba 20 kilichopo kwenye sheria za mashindano, ikiwemo kuvunja mkataba uliopo kati yake na Lagardere kutokana na matokeo iliyonayo kwa Misri.
Mamlaka hiyo pia imetoa ruksa kwa kampuni ya BeIn media pamoja na kampuni nyingine zilizoomba haki ya kurusha matangazo mubashara kuendelea kufanya hivyo hasa kwa ajili ya mashindano ya mataifa ya Afrika, 2017 AFCON itakayoanza January 14.
CAF iabadili pia namna haki za matangazo za mashindano mbalimbali zinavyouzwa nchini Misri katika mantiki ya kugawanya vifurushi vinavyohakikisha kutengeneza mazingira yatakayovutia mahsindano hayo kurushwa na vituo.
Mamlaka za mashindano zinaweka wazi kuwa CAF ina mlengo wa kuhakikisha inalinda na kusimamia sheria za mashindano na pia inatakiwa  kufuata hivyo kulingana na makubaliano yaliyopo kati ya serikali ya Misri na CAF.
Na kwa taarifa zinazoendelea kutoka ni kuwa CAF ina mpango wa kuhamisha makazi yake kutoka nchini Misri, lakini mamlaka ya mashindano imesema kuweza kufanya hivyo asilimia 75 ya wanachama ambao ni nchi 54 wanatakiwa kupiga kura kukubali kwenye mkutano mkuu kutokana na sheria za CAF kifungu namba 1.
FIFA ambalo Hayatou aliwahi kuongoza kwa muda kama Rais baada ya Blatter kutangaz kujiuzulu mapema mwaka uliopita, lilikumbwa na kashfa kubwa kiasi cha kufanya chaguzi mkuu mara mbili katika msimu mmoja.

Msuva aiaibisha Simba mapema Kombe la Mapinduzi 2017

Simon Msuva
Hekaheka wakati wa pambano la Simba na Yanga Oktoba 1, 2016 lililoisha kwa sare ya 1-1.
HATA kabla ya Watani wa Jadi, Simba na Yanga hazijajua kama zitakutana kwenye mechi za nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 kule visiwani Zanzibar, tayari Vijana wa Jangwani wameipiga bao Simba.
Tena aliyeiopiga bao ni kijana mmoja mfupi hivi, ambaye amekuwa akipata wakati mgumu mbele ya mashabiki wa Jangwani kila Yanga inapocheza jijini Dar es Salaam. Mashabiki wasio na ustaarabu wala kuheshimu mchango wa nyota wao, Simon Msuva wamekuwa wakimtusi na kumtolea kejeli winga huyo, lakini ukirejea kwa kile anachjokifanya uwanjani utajua Msuva ni nani!
Winga huyo anayeongoza orodha ya ufungaji bora katika Ligi Kuu Bara kwa sasa akiwa sambamba na Amissi Tambwe anayecheza naye pale Jangwani na Shiza Kichuya wa Wekundu wa Msimbazi ni balaa.
Katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, Msuva ameifanyia mbaya Simba hata kama ya kukutana nao baada ya kufunga mabao manne ambayo ni moja zaidi ya iliyonao wapinzani wao hao kutoka Mtaa wa Msimbazi.
Katika mechi mbili tu za Kombe la Mapinduzi, Msuva amefunga mabao hayo, huku kikosi kizima cha Simba kikiwa kimecheza mechi tatu mpaka sasa, lakini kikiwa na mabao matatu tu, yaliyofungwa na Mzamiru Yassin mawili na Juma 'Ndanda' Liuzio.
Kwa lugha nyepesi unaweza kusema kuwa Msuva ameibwaga Simba kwa mabao 4-3 hata kabla timu yake na Wekundu wa Msimbazi hazijashuka uwanjani wikiendi hii kusaka tiketi ya kukutana ama kukwepana pale Unguja.
Msuva alianza kwa kufunga mabao mawili walipoikamua Jamhuri ya Pemba kwa mabao 6-0, kabla ya kuongeza mengine walipoizamisha Zimamoto na kama sio kukosa umakini katika mechi hiyo ya pili jamaa angetupia hat trick kwani alipata nafasi ya kupiga penalti, lakini akashindwa kukwamisha kimiani.
Bila ya shaka mashabiki wa Simba kokote walipo kwa sasa watakuwa wanajiuliza itakuwa vipi kama chama lao litakutana na Yanga katika michuano hiyo kwa mziki mnene iliyonayo wapinzani wao hao.
Katika mechi yao ya pili, Yanga iliwakosa washambuliaji wake wote wa kati baada ya Donald Ngoma na Amissi Tambwe kutocheza kabisa, lakini katika mechi yao ya kesho dhidi ya Azam huenda majembe hayo yakawepo.
Simba kwa upande wao makali yake kwa sasa yanabebwa na viungo wake wajanja, Mzamiru, Mohammed Ibrahim na Pastory Athanas, huku wakipigwa tafu na Liuzio ambaye katika mechi ya tatu ya Simba dhidi URA Uganda alianza sambamba na Laudit Mavugo ambaye amekuwa na hali mbaya klabuni.
Je, Msuva ataendelea kuikimbiza Simba ama Simba itatafuta upenyo wa kuukacha mziki wa Jangwani na kusubiri kujua majaliwa yao kwenye fainali ya michuano hiyo Januari 13? Tusubiri tuone.

Hebu msikieni Gerard Pique na ulalamishi wake

Wachezaji wa Barcelona wakimlalamikia mwamuzi katika mechi yao ya jana dhidi ya Atheltico Club
Beki Gerard Pique akisikitika akiwa nyavuni wakati timu yake ikipokea kipigo cha mabao 2-1.
KUMBE wepesiiii. Barcelona wameuanza mwaka vibaya baada ya kujikuta wakitunguliwa mabao 2-1 na Athletico Club, huku beki wake Gerard Pique akitupa lawama kwa waamuzi wa pambano hilo.
Pique amedai kuwa waamuzi nchini Hispania wanawapendelea mahasimu wao wakuu, Real Madrid baada ya klabu hiyo kuchapwa katika mchezo wa Kombe la Mfalme uliochezwa usiku wa jana.
Barcelona walilalamikia penalti mbili, moja iliyomhusisha Neymar na nyingine Pique, ambazo zilikataliwa katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya timu 16 bora, ingawa baadae wenyeji Bilbao walipoteza wachezaji wawili kwa kadi nyekundu Raul Garcia na Ander Iturraspe.
Akihojiwa beki huyo wa kimataifa wa Hispania alisema penalti hizo zilikuwa za wazi kabisa, lakini anadhani wanajua kwanini wanafanyiwa hivyo.
Pique aliendelea kudai kuwa waamuzi wamekuwa wakiwakwamisha kwa kuonyesha upendeleo kwa Madrid akitolea mfano wa mechi yao ya jana dhidi ya Sevilla ambayo walishinda mabao 3-0.

Pep Guardiola mzuka mtupu Kombe la FA

Kocha Guardiola
 
UKISIKIA mzuka unapanda ndiko huku bwana! Menaja wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola amesema ana hamu kubwa ya kusimamia mchezo wake wa kwanza wa michuano ya Kombe la FA wakati kikosi chake kitakapovaana na West Ham United usiku wa leo Ijumaa.
Man City iliyopo nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kushushwa na Tottenham Hotspur iliyoinyoa Chelsea kwa mabao 2-0, itavaana na Wagonga Nyundo hao wa London katika mchezo wa mzunguko wa tatu.
City wanatarajiwa kukwaana na West Ham katika Uwanja wa London baadae leo usiku na wakati akihojiwa Kocha Guardiola alisema michuano hiyo ni muhimu kwa sababu timu za chini zinaweza kuzifunga timu kubwa ndio maana inakuwa na msisimko.
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ana hamu kubwa na mchezo huo, lakini utazikutanisha timu zote za Ligi Kuu hivyo utakuwa mgumu.
Michezo mingine ya michuano hiyo maarufu na mikongwe barani Ulaya itachezwa wikiendi hii na Jumatatu kama ratiba inayoonyesha chini;     

    07.01. 15:30    Manchester United    Reading       
    07.01. 18:00    Accrington    Luton       
    07.01. 18:00    Barrow    Rochdale       
    07.01. 18:00    Birmingham    Newcastle Utd       
    07.01. 18:00    Blackpool    Barnsley       
    07.01. 18:00    Bolton    Crystal Palace       
    07.01. 18:00    Brentford    Eastleigh       
    07.01. 18:00    Brighton    Milton Keynes Dons

    07.01. 18:00    Bristol City    Fleetwood Town       
    07.01. 18:00    Everton    Leicester       
    07.01. 18:00    Huddersfield    Port Vale       
    07.01. 18:00    Hull City    Swansea       
    07.01. 18:00    Ipswich    Lincoln City       
    07.01. 18:00    Millwall    Bournemouth       
    07.01. 18:00    Norwich    Southampton       
    07.01. 18:00    QPR    Blackburn       
    07.01. 18:00    Rotherham    Oxford Utd       
    07.01. 18:00    Stoke City    Wolves       
    07.01. 18:00    Sunderland    Burnley       
    07.01. 18:00    Sutton    AFC Wimbledon       
    07.01. 18:00    Watford    Burton       
    07.01. 18:00    West Brom    Derby       
    07.01. 18:00    Wigan    Nottingham       
    07.01. 18:00    Wycombe    Stourbridge       
    07.01. 20:30    Preston    Arsenal
    08.01. 14:30    Cardiff    Fulham       
    08.01. 16:30    Liverpool    Plymouth       
    08.01. 18:00    Chelsea    Peterborough       
    08.01. 18:00    Middlesbrough    Sheffield Wed

    08.01. 19:00    Tottenham    Aston Villa       
    09.01. 22:45    Cambridge Utd    Leeds

Mashetani Wekundu kumbe hawatanii kwa Griezmann

WAMEPANIA aisee! Klabu ya Manchester United inadaiwa imeanza kufanya mazungumzo ya kumuwania straika wa kimataifa wa Ufaransa, Antoine Griezmann, huku ikielezwa kuwa inatarajiwa kumpa ya mshahara wa pauni 220,000 kwa wiki ili kumshawishi kutua Old Trafford.
Duru za michezo zinadai kuwa, Mashetani Wekundu tayari wameanza mazungumzo na wawakilishi wa nyota huyo wa Atletico Madrid na imeahidi mshahara wake utafikia ule anaolipwa kiungo Paul Pogba aliyepo ndani ya klabu hiyo ya EPL.
Griezmann ameshawahi akikaririwa akieleza jinsi anavyoihusudu United na Mourinho katika mahojiano yake huko nyuma. Kama wakifikia makubaliano hayo United inadaiwa italazimika kutoa kitita cha pauni milioni 86 ili kutengua kitenzi katika mkataba wa mshambuliaji huyo ambaye amekuwa akizitoa udenda klabu nyingi barani Ulaya kwa soka lake murua.

Kocha Mourinho kiroho safi ongezeko la timu WC

AMEKUBALI. Kocha wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho 'Special One', amekuwa kocha wa kwanza kuunga  mkono mapendekezo ya kuongeza timu kufikia 48 katika Kombe la Dunia akiamini kuwa wachezaji watalindwa vyema.
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino ana matumaini mpango wake kuwa na makundi 16 yenye timu tatu kuanzia michuano ya mwaka 2026 utapitishwa wakati wa kikao cha kamati ya utendaji ya shirikisho hilo wiki ijayo.
Muungano wa Klabu Ulaya ambao United pia ni mjumbe wake, tayari wameshaonyesha kutounga mkono pendekezo hilo, lakini Kocha Mourinho yeye anaunga mkono.
Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Mourinho alisema anaunga mkono kwa vile ana uhakika FIFA itazingatia maslahi ya wachezaji kwa kutowachezesha mechi nyingi zaidi kuliko sasa.

Msuva mkimchekea tu, kabeba mwanangu!

Msuva Kulia akiwajibika katika mechi za Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam. Timu hizo kesho zitavaana kwenye Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar.
UMEIANGALIA orodha ya Wafungaji Bora wa sasa wa michuano ya Kombe la Mapinduzi? Jina la Simon Msuva bila shaka ndilo linaloongoza kwa sasa akiwa ametupia kambani mabao manne.
Sasa kama hujui, idadi hiyo ya mabao aliyonayo sasa ndiyo iliyompa tuzo Mwaka 2015 alipochaguliwa kuwa Mfungaji Bora akiwafunika wakali wengine.
Msuva kwa sasa anaongoza orodha hiyo na kama kesho Jumamosi atatupia tena kambani kuna uwezekano mkubwa wa kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao mengi kwenye michuano hiyo iliyoasisiwa 2007.
Michuano ya Mapinduzi kwa mwaka jana wa 2016, Peter Lwasa wa URA ndiye aliyekuwa Mfungaji Bora akitupia kimiani mabao matatu.
Msuva amekiri kwamba kiu yake katika michuano ya mwaka huu ni kuona anaibuka Mfungaji Bora na hata kunyakua Mchezaji Bora na kuisaidia pia Yanga kubeba taji lao la pili la michuano hiyo inayoendelea visiwani Zanzibar.
Mpaka sasa Msuva amafukuziwa kwa karibu na wachezaji wawili, Abdul-Samad Kassim wa Jang'ombe Boys aliyepiga hat trick ya kwanza katika michuano hiyo na Bokota Labama wa URA-Uganga wenye mabao matatu kila mmoja.
Kwenye michuano ya mwaka huu Mfungaji Bora na Mchezaji Bora atazawadiwa kila mmoja kitita cha Sh. 1 milioni moja kama atakachopewa Kipa Bora, Mchezaji Bora Chipukizi, Mwamuzi Bora na Kocha Bora, fedha ambazo zimetolewa na mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Khamis Chuma.

Orodha ya Wafungaji;

4 Simon Msuva                     (Yanga)
3 Bokota Labama                    (URA)
   Abdul Kassim 'Hasgut' (Jang'ombe)
2 Khamis Makame         (Jang'ombe)
   Donald Ngoma                  (Yanga)
   Mzamiru Yassin                 (Simba)
1 Seif Hassan 'Banda'             (Taifa)
   Juma Liuzio                      (Simba)
   Laudit Lufunga  o.g           (Simba)
   Thabani Kamusoko            (Yanga)
   Bakar Mahadhi                  (Yanga)
   Shaaban Idd                      (Azam)

   Salum Songoro                    (KVZ)

Hiki ndicho kikosi bora cha Afrika 2016

Pierre-Emerick Aubemeyang wa Gabon

Sadio Mane wa Senegal
MASTRAIKA waliokuwa wakichuana kwenye Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mwaka 2016, Pierre-Emerick Aubameyang, Riyad Mahrez na sadio Mane ndio wanaouunda safu ya ushambuliaji ya Kikosi cha Timu Bora ya Afrika ya Mwaka 2016.
Kikosi hicho kilitangazwa jana kwenye sherehe za utoaji tuzo za Caf ambapo kipa Mganda, Dennis Onyango ndiye pekee toka Ukanda wa Afrika Mashariki aliyeingia kikosini.
Kwa mujibu wa Caf kikosi hicho kipo hivi;
Kipa: Dennis ONYANGO (Uganda & Mamelodi Sundowns)
Mabeki: Serge AURIER (Cote d’Ivoire & Paris Saint-Germain), Aymen ABDENNOUR (Tunisia & Valencia), Eric BAILLY (Cote d’Ivoire & Manchester United), Joyce LOMALISA (DR Congo & AS Vita)
Viungo: Khama BILLIAT (Zimbabwe & Mamelodi Sundowns), Rainford KALABA (Zambia & TP Mazembe), Keegan DOLLY (South Africa & Mamelodi Sundowns),
Mastraika: Pierre-Emerick AUBAMEYANG (Gabon & Borussia Dortmund), Sadio MANE (Senegal & Liverpool), Riyad MAHREZ (Algeria &Leicester City).


Wachezaji wa Akiba: Aymen MATHLOUTHI (Tunisia & Etoile du Sahel), Kalidou KOULIBALY (Senegal & Napoli), Salif COULIBALY (Mali & TP Mazembe), Islam SLIMANI (Algeria & Leicester City), Mohamed Salah (Egypt & Roma), Kelechi IHEANACHO (Nigeria & Manchester City), Alex IWOBI (Nigeria and Arsenal).

Simba yabanwa, Yanga ikiisubiri nusu fainali Mapinduzi Cup


Benchi la Simba likifuatilia moja ya mechi zao za Mapinduzi Cup 2017
Yanga kabla ya mechi yao ya Jamhuri Pemba
NA RAHMA WHITE, Z'BAR
SIMBA, jana usiku ilishikwa shati na Watoza Ushuru wa Uganda, URA, lakini kesho Jumamosi kutakuwa na kazi kubwa itakayozikutanisha timu za Yanga na Azam ili kuamua hatma ya Kundi B katika Kombe la Mapinduzi 2017.
Michuano hiyo inayoendelea usiku wa leo kwa pambano moja tu la Kundi A kati ya Taifa Jang'ombe 'Wakombozi wa Ng'ambo dhidi ya KVZ, inachezwa kwenye Uwanja wa Amaana, Zanzibar na jana Simba ilitoka suluhu na URA.
Kwa matokeo hayo Simba imeendelea kuongoza kundi A ikiwa na pointi saba baada ya kushushwa kwa muda katika nafasi hiyo na Jang'ombe Boys ambayo jioni ya jana ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KVZ.
Katika pambano hilo la mapema, Abdul Samad Kassim Hasgut alikuwa mchezaji wa kwanza kwa msimu huu kufunga hat trick wakati wakiizamisha KVZ ambayo ilitangulia kupata bao dakika ya tano tu kupitia Salum Songoro.
Hata hivyo kazi ipo kesho asikuambie mtu, Yanga na Azam zitavaana kuamua nani aongoze kundi ili kuelekea mechi za njusu fainali zitakazopigwa wiki ijayo.
Yanga inaongoza msimamo wa kundi hilo ikiwa na pointi sita huku Azam ikiwa nyuma yao na pointi zao nne na Jamhuri ni ya tatu ikiwa na pointi moja ambapo mapema jioni ya kesho itavaana na Zimamoto ambayo imeshaaga mashindano hayo mapema kwa kupigwa mechi zao mbili za awali.
Pambano la Yanga na Azam linavuta hisia kubwa kutokana na ushindani uliopo baina ya timu hiyo, japo safari hii Azam inaonekana wanyonge kwa kufanya vibaya katika Ligi Kuu Bara na juzi kati ilibanwa mbavu na Jamhuri na kutoka nao suluhu. Jamhuri ilitunguliwa na Yanga mabao 6-0 katika mechi yao ya kwanza na wengi walidhani Azam ingefuata nyayo hizo, lakini ikajikuta ikiomba pambano limalizike kwa namna Jamhuri walivyowakimbiza uwanjani.
Matokeo yoyote kwa Yanga mbali na kipigo yataifa uongozi wa kundi hilo na kusikiliza mechi za keshokutwa Jumapili za Kundi A ili kujua itavaana na nani kwenye hatua ya nusu fainali.
Jumapili vinara wa Kundi A, Simba itavaana na Jang'ombe Boys iliyopo nafasi ya pili majira ya usiku na mapema jioni ya siku hiyo URA iliyopo nafasi ya tatu itamaliza kazi dhidi ya Taifa Jang'ombe.
Matokeo yoyote ya kundi hilo yanaweza kuzifusha timu za Simba, Jang'ombe Boys, URA  na hata Taifa jang;ombe kucheza nusu fainali na moja yao itakuwa na nafasi ya kuvaana na Yanga ambayo katika mechi mbili za awali imeshinda kwa mabao nane huku wavu wao ukiwa haujaguswa tofauti na wapinzani wa kundi hilo la A.
Mechi za wikiendi hii za kukamilishia hatua ya makundi za michuano hiyo ndizo zitakazoamua timu zipi tatu za mwisho za kuungana na Yanga iliyotangulia mapema kucheza nusu fainali.

Mambo yalivyo Kombe la Mapinduzi 2017

Des 30, 2016
Taifa Jang'ombe 1-0 Jang'ombe Boys (Seif Hassan 'Banda')

Jan 01, 2017
URA 2-0 KVZ  (Bokota Labama  57', 90')
Taifa Jang'ombe 1-2 Simba (Mzamiru 27', Liuzio 41'; Lufunga 76 Og)

Jan 02, 2017
Azam 1-0 Zimamoto (Shaaban Idd 79')
Yanga 6-0 Jamhuri (Msuva 19', 40', Ngoma 23', 37', Kamusoko 59', Mahadh 85')

Jan 03, 2017
URA 1-2 Jang'ombe Boys (Bokota Labama 31'; Khamis Makame '19', 51')
KVZ 0-1 Simba (Mzamiru 44')

Jan 04, 2017
Yanga 2-0 Zimamoto (Msuva 11', 21')
Azam 0-0 Jamhuri

Jan 05, 2017
KVZ 1-3 Jang'ombe Boys (Salum Songoro 5'; Abdul Kassim 20', 35', 45)
Simba 0-0 URA

Ratiba ilivyo sasa


Leo Ijumaa

Taifa Jang'ombe v KVZ Saa 2:30 usiku

Kesho Jumamosi

Jamhuri v Zimamoto Saa 10:00 jioni
Azam v Yanga Saa 2:30 usiku

Jumapili Jan 08, 2017

Simba v Jang'ombe Boys Saa 10:00 jioni
Taifa Jang'ombe v  URA Saa 2:30 usiku

Jan 10, 2017
Nusu Fainali

Mshindi A v Wa Pili B Saa 10:00 jioni
Mshindi B v Wa Pili A Saa 2:30 usiku

Jan 13, 2017

Mshindi NF1 v Mshindi NF2 Saa 2:30

Msimamo
Kundi A:
                         P  W  D  L  F  A  Pts
1. Simba           3   2   1   0  3  1   7
2. Jang'ombe     3   2   0  1   5  3   6
3.  URA             3   1   1  1   3  2   4
4. Taifa              2   1   0  1   2  3   3
5. KVZ               3   0   0  3   1  6   0

Kundi B
                       P  W  D  L  F  A  Pts
1. Yanga           2   2   0  0  8  0  6
2. Azam            2   1  1   0  1  0  4
3. Jamhuri        2   0   1   1  0  6  1
4. Zimamoto     2   0   0   2  0  3  0

Wafungaji:
4 Simon Msuva         (Yanga)
3 Bokota Labama     (URA)
   Abdul Kassim 'Hasgut' (Jang'ombe)
2 Khamis Makame    (Jang'ombe)
   Donald Ngoma      (Yanga)
   Mzamiru Yassin     (Simba)
1 Seif Hassan 'Banda' (Taifa)
   Juma Liuzio            (Simba)
   Laudit Lufunga  o.g (Simba)
   Thabani Kamusoko(Yanga)
   Bakar Mahadhi        (Yanga)
   Shaaban Idd            (Azam)

Orodha ya Mabingwa wa Mapinduzi
Mwaka     Bingwa            Mshindi wa Pili
2007         Yanga SC          Mtibwa Sugar
2008         Simba SC          Mtibwa Sugar
2009         Miembeni          KMKM
2010         Mtibwa Sugar    Ocean View
2011         Simba SC          Yanga SC
2012         Azam FC           Simba SC
2013         Azam FC           Tusker FC
2014         KCCA                Simba SC
2015         Simba SC          Mtibwa Sugar
2016         URA                  Mtibwa Sugar
2017          ??                          ??

Mahrez ndiye Baba lao Afrika, Onyango amrithi Samatta


Mahrez akiwa na tuzo yake ya Mchezaji Bora wa Afrika 2016
Akiwa kazini Leicester
Kipa Dennis Onyango wa Uganda aliyemrithi Samatta
RIYAD Mahrez amembwaga straika wa kimataifa wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang katika kinyang'anyiro cha Tuzo za Mchezaji Bora wa Afrika 2016 baada ya Mualgeria huyo kunyakua tuzo hiyo kwa mara ya kwanza.
Tuzo hizo za Wanasoka waliofanya vema kwa mwaka 2016 zilifanyika usiku wa kuamkia leo mjini Abuja, Nigeria na kusindikizwa na burudani toka kwa wasanii mbalimbali akiwamo Diamond Platinumz na Rayvan.
Mahrez anayekipiga Leicester City ametwaa tuzo hiyo kwa kupigiwa kura 361 akimzidi Aubameyang aliyekuwa akitetea tuzo hiyo aliyevuna pointi 313 na Sadio Mane wa Senegal akiambulia nafasi ya tatu na pointi 186.
Hiyo ni tuzo ya pili Afrika kwa Mahrez kwani hivi karibuni alitwaa tuzo ya Mwanasoka wa Afrika wa BBC 2016.
Mahrez na tuzo yake ya BBC

Kwa upande wa Mchezaji Bora wa Afrika Wanaocheza barani humu, nafasi hiyo ilitwaliwa na kipa Dennis Onyango aliyewafunika washindani wake, Khama Brilliat anayecheza naye Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Rainford Kalaba wa TP Mazembe.
Mganda huyo ametwaa tuzo hiyo akimpokea Mtanzania anayekipiga Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta aliyeitwaa mwaka jana nchini humo akiwa na klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.
Uganda iliendelea kutisha baada ya timu yao ya taifa, The Cranes kushinda tuzo ya Timu Bora ya Taifa, huku Mamelodi Sunsdowns ikiwa Klabu Bora ya Mwaka ya Afrika na Kocha wa klabu hiyo Pitso Mosimane akitwaa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka.
Tuzo nyingine zimeenda kwa Kelechi Iheanacho kama Mchezaji Mwenye Kipaji na Alex Iwobi anayeichezea Arsenal akitwaa tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Afrika, wote hao wanatokea Nigeria, huku Mwanasoka Bora wa Kike nafasi ikienda kwa Asisat Ashoala kutoka Nigeria.
Tuzo ya Gwiji wa Afrika ilienda kwa wakali wawili wa zamani wa Laurent Pokou wa Ivory Coast na Emilienne Mbango wa Cameroon, huku timu ya wanawake ya Nigeria ikishinda kuwa Timu Bora ya Soka la Wanawake.
Mwamuzi Bakary Gassama wa Gambia alipiga 'hat trick' ya kuwa Mwamuzi Bora wa Afrika kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kufanya hivyo pia mwaka 2014 na 2015 kabla ya jana usiku mjini Abuja, Nigeria kutwaa tuzo hiyo tena naye  Rais wa Shirikisho la Soka la Guinea Bissau, Manuel Lopes Nascimento alitwaa tuzo ya Kiongozi Bora wa Soka wa barani Afrika.

Orodha ya Washindi wa Tuzo za CAF 2016

Mchezaji Bora wa Afrika wa Mwaka
Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City)

Mchezaji Bora wa Mwaka Anayecheza Afrika
Dennis Onyango (Uganda & Mamelodi Sundowns)

Mchezaji Bora wa Kike wa Mwaka
Asisat Oshoala (Nigeria & Arsenal)

Chipukizi Mwenye Kipaji cha Aina Yake
Kelechi Iheanacho (Nigeria & Manchester City)

Chipukizi Bora wa Mwaka
Alex Iwobi (Nigeria & Arsenal)

Kocha Bora wa Mwaka
Pitso Mosimane (Mamelodi Sundowns)

Klabu Bora ya Mwaka
Mamelodi Sundowns

Timu Bora ya Taifa ya Mwaka
Uganda The Cranes

Timu Bora ya Taifa ya Wanawake
Nigeria

Mwamuzi Bora wa Mwaka:
Bakary Papa Gassama

Friday, September 9, 2016

Wilshere mbona mtamu, subirini tu muone-Wenger

http://www.telegraph.co.uk/content/dam/football/2016/04/07/jack-wilshere8-large_trans++qVzuuqpFlyLIwiB6NTmJwfSVWeZ_vEN7c6bHu2jJnT8.jpgMBONA freshi tu! Kocha wa klabu ya NEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa Jack Wilshere anaweza kuitumikia klabu hiyo kwa kipindi kirefu mbele ya safari huku akisisitiza kuwa kiungo huyo hana chochote cha kumuonyesha zaidi ya kuwa fiti. Wilshere ameenda kwa mkopo wa msimu mzima katika klabu ya AFC Bournemouth dakika za mwisho kabla ya dirisha la usajili majira ya kiangazi halijafungwa ikiwa kama sehemu ya mikakati ya kujijenga upya kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara katika misimu miwili iliyopita.
Akizungumza kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton, Wenger alipuuza habari kuwa amekuwa haelewani na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye amekuwa akimtaja kuwa na uwezo mkubwa.
Kocha Wenger alisema alizungumza na Wilshere naye alimwambia hadhani kama ataweza kupata muda wa kutosha kucheza akibakia hapo kwa vile anataka  kucheza zaidi msimu huu baada ya kupona majeruhi yake.
Wengeraliendelea kudai kuwa alimruhusu kuondoka kwasababu alikuwa hawezi kumuahidi muda wa kutosha wa kucheza kama alivyotaka mwenyewe.

Ronaldo kamili gado kuanza mambo La Liga

http://www.ronaldo7.net/news/2014/04/824-cristiano-ronaldo-fitness-drills.jpgUSIYEMPENDA Kaja. Ndivyo ambavyo Osasuna watakuwa wanawaza sana, baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo yupo fiti na kesho huenda akashuka uwanjani kuvaana nao.
Straika huyo amebainisha kuwa atarejea uwanjani Jumamosi hii katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akijiuguza goti lake katika majeruhi aliyopata katika mchezo wa fainali ya michuano ya Ulaya hali iliyomfanya kukosa mechi ys Super Cup ya Ulaya na zingine walizocheza Madrid katika La Liga msimu huu. Akihojiwa kuhusiana na hali yake inavyoendelea, nahodha huyo wa Ureno amesema yuko tayari kurejea uwanjani na anatarajia kucheza katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Madrid wameshinda mechi zao zote mbili za la Liga walizocheza msimu huu, kwa kuzifunga Real Sociedad na Celta Vigo.