STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 10, 2013

KASEBA ALIVYOMSAMBARATISHA SIMWANZA WA MALAWI

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Ibrahimu Maokola kushoto akioneshana kazi na
JOSEPHER NJELEKELA(KAMANDA WA KAMANDA) wakati wa mpambano wao Maokola alishinda kwa KO ya raundi ya tatu
Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Juma Fundi akioneshana umwamba na Moro Best wakati wa mpambano huo

Bondia Juma Fundi akioneshana umwamba na Moro Best wakati wa mpambano huo
Juma fundi alishinda kwa KO raundi ya sita

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Rasco Simwanza kutoka Malawi kushoto akipambana na Japhet Kaseba wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Kimataifa wa PST kaseba alishinda raundi ya tano

Bondia Japhet Kaseba akiwa amevishwa mkanda wake wa kimataifa wa PST

Bondia Kaseba akishangilia ushindi zaidi tembelea www.superdboxingcoach.blogspot.com

Watanzania wang'ara katika mbio nchini Kenya

KATIKA kuhakikisha riadha nchini Tanzania inafuta uteja kwa wakimbiaji
wake kwa wafukuza upepo wa Kenya, Klabu ya Holili (HYAC) ya Mkoani
Kilimanjaro imedhihirisha hilo katika Taveta Athletics Championship
kwa kuwabwaga Wakenya katika mbio za meta 5000, 1500, 800 na 100.

Michuano hiyo ya Taveta imefanyika mwishoni mwa wiki katika Kaunti ya
Taita-Taveta katika Mkoa wa Pwani nchini Kenya katika wilaya ya Taveta
kwa kuwakutanisha wanariadha wa nchini Kenya huku Holili Youth
Athletics Club ikialikwa kutoka nchini Tanzania.

Katika Mbio za meta 5,000 alikuwa ni Baraka Williams aliyekimbia kwa
dakika 14:45:22 nafasi ya pili ikishikwa na Mtanzania mwingine
Abubakar  Joel aliyekimbia kwa muda wa 16:00:00  na nafasi ya tatu
ikashikwa na Mkenya Kivoko Makao ambaye alikimbia kwa muda wa
16:34:00.

Wambura Lameck, Mtanzania kutoka katika klabu ya Riadha kwa vijana
(HYAC) alionyesha uwezo katika mbio za meta 100 na 800 kwa wanaume;
katika mbio za meta 100 Wambura alikimbia kwa muda wa sekunde 12:67
akiwatupa Wakenya Walter Kamujalo (13:12), Emmanuel Paulo (13:70) na
Joseph Daudi (14:20).

Mbio za mita 800 Wambura Lameck alikimbikia kwa muda wa dakika 2:02:16
akimwacha Mkenya Ropya Nyingi ambaye alichukua muda wa dakika 2:04::14
na nafasi ya Tatu ikishikwa na Mtanzania kutoka HYAC Paulo Jackson
aliyekimbia kwa muda wa dakika 2:05:98, Wakenya wengine Joseph Daudi
(3:00:00) na Philip Matheka (3:04) walisshika nafasi mbili za mwisho.

Pia Watanzania waliwaonyesha kazi nyingine Wakenya katika mbio za meta
1500 pale Baraka Williams kutoka HYAC alipowakimbiza na kuongoza baada
ya kumaliza kwa muda wa dakika 3:48:77 akifuatiwa na Mkenya Vicent
Daniel kutoka Taveta aliyemaliza kwa kutumia muda wa dakika 4:16:85
nafasi ya tatu ikishikwa na Mtanzania mwingine kutoka HYAC Paulo
Jackson ambaye alikimbia kwa dakika 5:04:66 na Mkenya Tumuna Ludovick
akikimbia kwa muda wa dakika 5:09:07.

Kwa upande wa wanawake Watanzania Furaha Sambeke na Pendo Pamba
walifanya kweli katika meta 800 kwa kushika nafasi mbili za juu.

Furaha Sambeke anayenolewa na Klabu ya Holili Youth Athletics
alikimbia kwa muda wa dakika 2:30:00 na Pendo Pamba akimaliza kwa
dakika 3:10, nafasi ya tatu ilishikwa na Mkenya Emily Wamboi na ya nne
ikishikwa na Mkenya mwingine Cecily Kimale ambao wote walikimbia kwa
kuda wa dakika 3:22:00 na 4:12:00.

Taveta Athletics Championship imefanyika ikiwa na makusudi ya
kutengeneza Timu ya Riadha ya Taifa la Kenya ambako mchujo rasmi
utafanyika Mjini Mombasa kwa watanzania walioshinda katika mbio hizo
nao watakuwemo katika kinyang’anyiro hicho kwa ajili ya kupata uzoefu
zaidi kutokana na ukweli kwamba taifa la Kenya limekuwa bora katika
riadha barani Afrika.

Mwandishi: Johnsona Jabir, Moshi-Kilimanjaro

Saturday, June 8, 2013

Wajasiriamali wanawake wazidi kupiga hatua Tanzania


EBU angalia matangazo ya bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wa kike wa Tanzania...unadhani wakiwezesha zaidi si watafika mbali zaidi?!

LICHA YA HUJUMA, STARS YAAPA KUIFANYIZIA MOROCCO

Straika wa Taifa Stars, John Bocco (wa pili kulia) akimiliki mpira huku akichungwa na Athuumani Idd 'Chuji' nyuma yake wakati wa mazoezi yao kuelekea mechi yao ya leo usiku ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Morocco mjini Marrakech.

Beki wa Stars, Erasto Nyoni (kulia) akikokota ngoma huku akichungwa na Frank Domayo huku Kelvin Yondani ( wa tatu kulia) na Mrisho Ngasa (kushoto) wakishuhudia wakati wa mazoezi yao kuelekea mechi yao ya leo usiku ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Morocco mjini Marrakech.

Straika wa Stars, Mbwana Samata (kushoto)akimiliki mpira wakati wa mazoezi yao kuelekea mechi yao ya leo usiku ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Morocco mjini Marrakech.

Ulimwengu (kushoto), Aggrey Morris, Mwinyi Kazimoto wakiwania mpira  wakati wa mazoezi yao kuelekea mechi yao ya leo usiku ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Morocco mjini Marrakech.
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars usiku wa kuamkia leo ilifanyiwa kilichoonekana kuwa hujuma baada ya kufanyiwa vurugu na kuzimiwa taa ishindwe kufanya mazoezi kwenye uwanja wa utakaotumika kwa mechi ya leo, siku moja kabla ya mchezo wao dhidi ya wenyeji wao Morocco ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014.

Sheria za FIFA zinasema timu mgeni, itapewa fursa ya kufanya mazoezi katika uwanja utakaotumika kwa mechi dhidi ya wenyeji katika muda ambao mechi itachezwa, lakini jana msafara wa Stars ulipofika Uwanja wa Marakech ulizuiwa kuingia ndani na askari wa uwanjani hapo.

Juhudi za kocha wa Stars, Kim Poulsen kuwaelewesha askari wa uwanja huo sheria ili wairuhusu timu kuingia uwanjani hazikuzaa matunda na ikabidi viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) waingilie kati, nao pia wakachemsha.

Ikawadia zamu ya viongozi wa Kamati ya Ushindi ya Stars, inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premum Lager, ambao nao walichemsha, ndipo baadhi wa Watanzania waishio hapa na wachache waliosafiri kutoka Dar es Salaam walipoongeza nguvu.

Walikwenda kufungua geti kwa nguvu, wakawaweka kando askari waliokuwa wanawazuia na kuiingiza timu uwanjani kufanya mazoezi.

Hata hivyo, Stars ilipofika uwanjani ililazimika kusubiri tena, kwani wenyeji Simba wa Atlas walikuwa wakiendelea na mazoezi.

Baada ya nusu saa, Morocco walimaliza awamu yao na Stars wakaanza kupasha misuli moto. Hata hivyo, baada ya dakika 34, taa za uwanja huo zilizimwa na uwanjani kuwa giza totoro, lakini viongozi wa TFF wakaenda kuomba, zikawashwa na timu ikafanya mazoezi kwa dakika 10 zaidi.

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos Makalla aliyekuwapo wakati wa vurumai zote hizo, alisikitishwa mno na kitendo hicho akisema si cha kiungwana na si cha kiunamichezo.

Makamu wa Rais wa TFF, Athumani Nyamlani alisema Morocco walikuja kucheza Dar es Salaam walipokewa vizuri na wakahudumiwa vizuri hadi wanaondoka, ajabu leo wanaifanyia ‘unyama’ Tanzania.

Mkuu wa Msafara wa Stars hapa, Crescentius John Magori alisema watapeleka malalamiko FIFA, waandaji wa michuano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia na kwa kuwa ushahidi upo, anaamini Morocco watachukuliwa hatua.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alishauri Stars icheze chini ya angalizo kwa kuwasilisha barua FIFA mapema ili wakae wanajua kuhusu hali halisi Morocco.

Kwa ujumla kilichotokea leo kimewatia woga Watanzania wengi waliopo hapa kuelekea mchezo wa leo, ambao Stars inahitaji ushindi ili kujiimarisha katika mbio za kuelekea Brazil 2014.

Hata ulinzi wa msafara wa Stars kutoka hotelini hadi uwanjani hakuwa wa kutosha na ilishuhuidiwa mara kadhaa ukiingiliwa na magari mengine barabarani wakati timu ikienda uwanjani kwa mazoezi.

Wenyeji nchini Morocco wanasema inapowadia mechi, huwa wanaogopa kwa sababu mara nyingi hutokea vurugu ya damu kumwagika.

Kwa ujumla Stars inaingia katika mchezo wa leo katika hali ya wasiwasi na woga mkubwa.

Stars itashuka dimbani saa 3:00 usiku leo kwa saa za hapa sawa na saa 5:00 za Tanzania kucheza na Morocco.

Stars inashika nafasi ya pili katika Kundi C, ikiwa na pointi sita nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, ambayo kesho itakuwa ugenini ikimenyana na Gambia katika mchezo mwingine wa kundi hilo.

Stars ilitua hapa Jumatatu ikitokea Ethiopia ambako iliweka kambi ya wiki moja na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan, ulioisha kwa sare ya bila mabao.

Kabla ya kuja hapa, Stars iliweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Karume na siku chache kabla ya kuondoka ilialikwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, aliyewapa hamasa kwa hotuba nzuri.

Waziri Makamba avisuta vyama vya upinzani


Naibu Waziri, Januari Makamba
NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba amesema dhamira ya kuwepo kwa vyama vingi bado haijafikiwa tangu kuanzishwa kwake kutokana na kukosa vyama na viongozi  wenye dira kwa Taifa.
Aliyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanafunzi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi ambao wanamaliza vyuo mbalimbali mkoa wa Dar es Salaam.
Makamba ambaye pia ni Mlezi wa Vyuo Vikuu Tanzania alisema  vyama hivyo vimekuwa vikijikita katika kulalamika bila kuonyesha dira na mwelekeo tofauti jambo ambalo linapelekea katika kufanya fujo ambazo zinakwamisha jitihada za serikali.
Makamba alisema Serikali inafanya kazi kutokana na mipango yake ambayo imejiwekea yenyewe hivyo inaamini kuwa itafikia malengo yake bila kusukumwa na mtu.
“Kwa  kweli najuta kwanini tuliruhusu uwepo wa vyama vingi hapa nchini kwani lengo letu lilikuwa ni kudumisha demokrasia kitu ambacho kimekuwa kinyume kwani vyama na  viongozi hao wamekuwa wakihubiri kinyume na dhima ya lengo husika,” alisema
Naibu Waziri alisema CCM ni chama ambacho kinaheshimika kitaifa na kimataifa hivyo wao wanaamini kuwa heshima hiyo itaendelea kuwepo milele kwa milele.
Alisema vijana wa CCM wahakikishe kuwa wanakisaidia chama na  nchi kwa ujumla ili nchi isije kuchukuliwa na vyama vya upinzani kwani itakuwa ni sawa na kuipeleka nchi kuzimu.
Aidha Mlezi huyo aliwataka vijana  hao wanaomaliza kujiamini na kuthubutu kushiriki katika fursa mbalimbali zinazojitokeza ili waweze kupata urahisi wa kushiriki katika chama na serikali kwani ni wajibu wao kulitumikia Taifa.
Makamba alisema vijana wanapaswa kushiriki katika harakati za kisiasa kwani hayupo mtu amnbaye atapata jambo bila kulihitaji mwenyewe na kuondokana na dhana ya kutafutiwa kazi kama wengi wanaofikiri.
Aliwataka wingi wao uwe ni sehemu muhimu ya kutafakari muafaka wa Taifa la Tanzania ijao ikiwa ni kushiriki katika ngazi mbalimbali za uongozi na kuondokana na dhana kuwa mwenye uwezo wa fedha ndio sababu ya kushinda.
Mlezi huyo alisema dhana ya fedha katika kutafuta uongozi  ipo kwa baadhi ya watu kutokana na tabia ya mtu mmoja mmoja lakini sio jambo la kusimamia kama kigezo.
Naibu Waziri aliwataka vijana wa CCM kuondoa uoga katika maamuzi ambayo yanahusu maslahi ya Taifa na jamii kwa ujumla iwapo sifa za uongozi unazo.
Makamba aliwaambia vijana kutambua kuwa kiongozi wema wanatoka kwa mungu na kuachana na tabia ya kulalamika kwakigezo kuwa nchi inaongozwa na wazee jambo ambalo wanalitengeneza wenyewe.
 
Aidha aliwataka wasomi kutafuta maandiko ambayo aliandika Hayati Mwalimu Nyerere kwani yana msingi mkubwa katika kujitambua na kufanya maamuzi sahihi kuhusu nchi yao na uongozi kwa ujumla.
Naye Mwenyekiti  Vyuo Vikuu Wilaya ya Dar es Salaam Abubakari Asenga alisema katika mahafal;i hayo wanafunzi zaidi ya mmia nne kutoka vyuo 28 vya mkoa wa Dar es Salaam walishiriki katika sherehe hiyo.
Asenga alisema huo ni uataratibu ambao wamekuwa nao tangu kuoanzishwa kwa shirikisho hilo lengo likiwa ni kuwatambua na kuwapatia vyeti vya utambulisho wao ndani ya CCM.
Alitaja vyuo ambavyo vilishiriki ni pamoja na Mwalimu Nyerere, Ustawi, Ardhi, UDSM, IFM, CBE, DIT, TSJ na vingine vingi.
Kwa upande wa msoma risala kwa niaba ya wahitimu Innocent Nsena  alisema wanakiomba Chama Cha Mapinduzi CCM kuwatumia wahitimu wanaomaliza vyuo kwani wana ujuzi na uwezo wa kukabiliana na  changamoto za jamii pamoja na vyama vya upinzani hapa nchini.
Aidha alisema wanavyuo wanapendekeza maoni yao kuhusu rasimu ya katiba ambapo wanaomba nchi ya Tanzania kutokubali kuwa na serikali ya shirikisho kwani uwezo wa nchi bado ni mdogo kuendesha nchi ambayo bado ni change kuichumi.
Pia wanapendekeza upatikanaji mpya wa kupata mgombea urais ili kuondoa mpasuko ambao unatokea mara kwa mara baada ya uchaguzi kufanyika.
Alisema katika mazingira yoyote yale Rais bora lazima atokee CCM ila kutokana na mazingira mbalimbali ambayo yamekuwa yakitokea baada ya uchaguzi ni vyema wakatumia mfumo wa kujaza dodoso ili wana CCM wapendekeze Rais wanayemuhitaji kwa manufaa ya Taifa.

Huyu ndiye Miss Sinza 2013 arithi taji la Miss Tanzania 2012



Redd's Miss Sinza 2013, Prisca Element (katikati) akiwa na Mshindi wa pili Happynes Maira (kulia) na Mshindi wa tatu, Sarahy Paul, wakiwa na furaha mara baada ya kutangazwa washindi katika shindano lao lililokuwa likishikiliwa na Redd's Miss Sinza na Miss Tanzania 2012-2013, Brigitte Alfred

MREMBO Prisca Element jana usiku alifanikiwa kumvua taji la kwanza Redd’s Miss Tanzania, Brigitte Alfred baada ya kufanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Sinza katika mchuano mkali uliofanyika ukumbi wa Meeda, uliopo Sinza Mori, Dar es Salaam.
Brigitte mbali na kushikilia taji la Redd’s Miss Tanzania ndiye pia aliyekuwa mrembo wa Redd’s Miss Tanzania, hivyo kuvuliwa taji hilo la kwanza ni kudhihirisha kinyang’anyiro cha kumsaka mrithi wake kimeshika kasi.
Katika shindano hilo lililokuwa kali na la kuvutia, huku burudani ikinogeshwa na kundi la African Stars ‘Twanga Pepeta’, nafasi ya pili ilichukuliwa na Happynes Maira na ile ya tatu akaitwaa Sarah Paul.
Warembo wengine wawili waliofanikiwa kuingia katika tano bora walikuwa ni Nicole Michael na Nasra Hassan, ambao walitoa upinzani mkali katika shindano hilo lililokuwa likifuatiliwa kwa karibu na watu wengi.
Akizungumza mara baada ya kufanikiwa kutwaa taji hilo, Prisca alisema ana uhakika mkubwa wa kufuata nyayo za Brigitte na kudai atahakikisha anaipigania Sinza kwa nguvu zake zote ili iweze kufanya vyema katika Redd’s Miss Tanzania.
Brigitte alipoulizwa kuhusu shindano hilo na kuvuliwa kwake taji, alisema anaamini kwa dhati mrembo aliyechaguliwa atahakikisha kitongoji cha Sinza kinaendelea kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.
“Kikubwa zaidi ni kujiamini na kufuata maelekezo unayopewa, lakini mrembo wetu naamini ana sifa zote zinazostahili na ni matumaini yangu atasonga mbele zaidi katika hatua inayofuata,” alisema.
Redd’s Miss Tanzania kwa sasa inadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

Mfanyabiashara mbaroni kwa kulawiti wanafunzi


MFANYABIASHARA maarufu mjini Morogoro, Mohamed Mauji, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaingilia kinyume na maumbile wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Mwere B.

Tukio hilo linadaiwa kutokea wiki iliyopita kwenye eneo la mazingira ya ofisi ya mfanyabiashara huyo anayeuza vinywaji laini kwa jumla.

Akizungumzia tukio hilo kwa niaba ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Mkuu wa polisi wilaya ya Morogoro, Sadick Tindwa, alisema kuwa inadaiwa kutokea Mei 31 na kuripotiwa katika kituo hicho Juni 3 na wazazi wa watoto hao.

Alisema kuwa wazazi hao walieleza kuwa waliwabaini watoto wao baada ya kupewa taarifa na walimu wa shule hiyo kuwa watoto hao wamekuwa wakija shuleni na fedha nyingi za matumizi pamoja na vitu mbalimbali.

Mkuu huyo wa Polisi wilaya ya Morogoro alisema kuwa baada ya wazazi hao kupewa taarifa hizo, waliwauliza watoto hao na kueleza kuwa wamekuwa wakipewa na mtu waliyemtaja kwa jina la mzungu na kuwafanyia vitendo hivyo.

Alisema kuwa wazazi hao walipowapekua watoto wao waliwakuta wana michubuko katika sehemu za kutolea haja kubwa na kuamua kulifikisha suala hilo kwa afisa mtendaji wa kata Kingo jirani na mfanyabiashara huyo.

Mkuu huyo wa Polisi Wilaya ya Morogoro alisema kuwa afisa huyo mtendaji wa kata ya Kingo aliamuru suala hilo lifikishwe kwenye kituo cha polisi kwa ajili ya kufanyiwa upelelezi.

Alisema kuwa baada ya kulifikisha , jeshi la polisi lilimkamata mtuhumiwa huyo kwa ajili ya uchunguzi ikiwa pamoja na watoto hao kupelekwa hospitali ya rufaa ya Morogoro kuchunguzwa afya zao.

Hata hivyo, alipoulizwa na gazeti hili kuhusiana na tuhuma hizo, mfanyabiashara huyo alikiri kuwafahamu wanafunzi hao ambao wamekuwa wakipita nje ya ofisi yake na kuomba pesa ya soda na yeye aliwahi kuwapatia kiasi cha sh 500 lakini hajawahi kuwafanyia kitendo hicho.

Moyes, Wenger katika vita ya kumwania Fabregas

2013 cesc fabregas barcelona
KLABU ya Manchester United imeingia vitani dhidi ya mahasimu wao Arsenal baada ya kocha wake David Moyes kuweka bayana kwamba ipo tayari kumnyakua kiungo wa Barcelona Cesc Fabregas anayewindwa pia kurejeshwa Emirates na klabu yake ya zamani.
Moyes, amenukulia akisema angependa kumsajili kiungo wa zamani wa Gunners ambaye hata hivuo majuzi aliweka bayana nia yake ya kuendelea kusalia kwa mabingwa wa Hispania, Barcelona.
Kiungo alikaririwa akisema angependa kusalia Nou Camp Nou ili kupigania namba yake licha ya kusajiliwa Mbrazili mwenye thamani ya Paundi Mil 50, Neymer.
Hata hivyo Moyes amesema atafanya kila njia kumnyakua mshindi huyo wa Kombe la Dunia aliyenyakua na timu yake ya taifa katika fainali zilizopita za 2010 ili kujenga kikosi chake.
Mipango ya Fabregas kurejeshwa Ligi Kuu ya England ilianza kitambo hata kabla Moyes kuchukua nafasi ya Ferguson mwzi uliopita.
Mabingwa hao wanamhitaji kiungo huyo baada ya Paul Scholes kustaafu na Michal Carrick kuondoka huku Tom Cleverley akibebeshwa majukumu yote.
Licha ya viungo toka Brazil, Anderson na Mjapan Shinji Kagawa kufanya vyema Old Trafford, lakini wanaelezwa sio wa daraja la Fabregas na ndiyo maana Moyes anamtolea macho akichuana na Wenger aliyetangaza kutaka kumrejesha nyota wake huyo wa zamani aliyemuuza mwaka uliopita.

Moyes amnyakua kinda toka Uruguay

http://e2.365dm.com/13/06/660x350/Guillermo-Varela_2955853.jpg?20130607111408
Guillermo Varela
KOCHA mpya wa Manchester United, David Moyes ameanza kazi kwa kumsainisha beki la kulia kinda  kutoka Uruguay, Guillermo Varela.
Valera mwenye umri wa miaka 19 aliyekuwa katika majaribio kwa mahasimu wa United, Manchester City msimu uliopita anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Moyes tangu amrithi Sir Alex Ferguson.
Mabingwa hao wa England watalazimika kuilipa klabu inayoshikilia taji la Ligi Kuu ya Uruguay, Penarol kiasi cha Paundi Milioni 1 kwa ajili ya saini ya mchezaji huyo, japo uhamisho wake unaweza kufikia mpaka Paundi Mil 2.5.
Varela alinukuliwa na gazeti la The Sun akithibitisha suala la kuhamia kwake United akisema alikuwa afanyiwe vipimo hivyo jana kabla ya leo Jumamosi kujiunga na kikosi cha timu yake ya taifa ya vijana U20.
Pia mchezaji huyo alisema atajifunza Kiingereza ili aweze kumudu kuwasiliana na wenzake.
United imemnyakua mchezaji huyo kijana baada ya misimu michache kuwanyakua makinda wengine waliopo katika kikosi chake kutoka nchi za Amerika ya Kusini na Kati baada ya kuwavuta Javier Hernandes 'Chicharito', Angelo Henriquez na Wabrazil mapacha, Rafael na Fabio .
Duru za kimichezo zinasema tayari mchezaji huyo alishafanyiwa vipimo hivyo vya afya jana na hivyo kuwa rasmi mchezaji wa Old Trafford.

Friday, June 7, 2013

Mbunge wa CCM ahukumiwa kifungo cha miezi 10 jela

MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM) amehukumiwa kifungo cha miezi 10 baada ya kupatikana na hatia ya kutishia kuua, Mbunge huyo (51) alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 10 akidaiwa kutishia kumuua Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ruiwa, Mbarali, Jordan Masweve.

Kabla ya kusoma hukumu hiyo leo Mbunge aliomba Mahakama impunguzie adhabu, kwani ana watoto watano kati yao wawili wanasoma Chuo Kikuu na wananchi wanamtegemea kuwasilisha matatizo yao bungeni.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, Michael Mteite, alisema ameridhika na ushahidi wa upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Epimack Mabrouk na Griffin Mwakapeje, pia mawakili wa upande wa mashitaka walimwomba Hakimu Mteite kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa, ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

"Kutokana na maelezo hayo na ushahidi ulioletwa mahakamani, ninakuhukumu kifungo cha miezi 10" alisema Hakimu Mteite.

Mbunge akihojiwa katika chumba cha mahakama alisema unajuwa siku hizi haki inatendeka pale tu iwapo mwanaCCM ametiwa hatiani, lakini kama ni mpinzani ametiwa hatiani utasikia ooh kaonewa au hii ni hukumu kutoka ikulu, hata hivyo alisema atakata rufaa katika hukumu hiyo.
Chanzo  http://networkedblogs.com

Mwili wa mume wa Khadija Kopa azikwa kwao Bagamoyo jioni hii

MWILI ya mume wa Malkia wa Mipasho nchini,Khadija Kopa, Jaffar Ally umezikwa jioni hii wilayani Bagamoyo baada ya kufariki jana jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa watu waliousindikiza mwili wa marehemu Jaffar ambaye anayetajwa kuwa alikuwa pia ni Diwani wa CCM Kata ya Magomeni mazishi hayo yamefanyika muda mfupi uliopita.
Pichani juu ni baadhi ya wakazi wa mtaa wa Magomeni wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani na waombolezaji wengine wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mume huyo wa muimbaji huyo wa kundi laTOT Taarab kuelekea kwenye makaburi kwa ajili ya kuhifadhiwa.
Picha: Said Swala Iddy.

TFF yawashukuru wadhamini Stars kujitosheleza

Viongozi wa TFF, Rais Leodger Tenga na Katibu Mkuu, Angetile Osiah
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa kuiwezesha timu ya taifa, Taifa Stars kuondokana na matatizo na kuwaomba Watanzania kuiombea timu ili ifanye vizuri katika mechi yake ya kesho (Juni 8 mwaka huu) dhidi ya Morocco mjini Marrakech.

Stars, ambayo inashika nafasi ya pili kwenye kundi lake la mashindano ya awali ya Kombe la Dunia ikiwa nyuma ya Ivory Coast kwa tofauti ya pointi moja, inacheza na Morocco katika mechi ya nne itakayofanyika Marrakech baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika mechi ya kwanza iliyofanyika Dar es Salaam mwezi Machi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema kuwa tangu kuanza kwa udhamini, TFF haijawahi kupata udhamini mkubwa kama wa Kilimanjaro Premium Lager ambayo imeingia mkataba wa miaka mitano wa kuidhamini Stars wenye thamani ya dola milioni 10 za Marekani.

“Katika kipindi chote hiki hatujawahi kupata udhamini ambao umekidhi mahitaji yote ya timu kama huu wa TBL,” alisema Tenga kwenye mkutano na waandishi uliofanyika kwenye ofisi za TFF.

“Lakini katika mwaka mmoja uliopita (tangu TBL ianze kudhamini) hatujawahi kushindwa kuisafirisha timu; kushindwa kulipa posho za wachezaji; kutanguliza watu wetu kwenda nje kuiandalia timu sehemu nzuri; kuzilipia tiketi za ndege timu tunazocheza nazo mechi za kirafiki na hata kuzilipia ada ya kucheza mechi (appearance fee).

“Posho za wachezaji zimepanda kwa karibu mara mbili na ndio maana leo wachezaji wanaijali timu yao. Yote haya ni kutokana na udhamini huu. Watu wanasema usione vinaelea….”

Tenga alisema kuwa udhamini huo ndio sasa umeanza kuzaa matunda na timu inafanya vizuri ikiwa ni pamoja na kuwa na maandalizi ya muda mrefu.

“Sasa tunawaomba Watanzania waiombee timu na tunawashukuru wale waliokwenda Morocco kuishangilia kwa kuwa vijana wetu wanapata nguvu pale wanapoona kuna watu wako nyuma yao,” alisema Tenga.

Rais huyo wa TFF pia alisifu kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuiita timu Ikulu na kuongea na kula na wachezaji, akisema kitendo hicho kitasaidia kuongeza hamasa kwenye timu.

Naye Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema kampuni yake itaendelea kuwa bega kwa bega na TFF na kwamba uhusiano baina ya pande hizo mbili umeimarika na utaendelea kuimarika.

Katika mkutano huo, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lilikabidhi fulana maalum kwa ajili ya mashabiki ambao wamekwenda Morocco kuishangilia timu.

Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu alisema tayari fulana 250 zimegawiwa kwa mashabiki walioko Morocco na nyingine zilitarajiwa kusafirishwa jana.

Tenga aitega serikali ushiriki timu za Tz Kagame Cup Darfur

Rais wa TFF, Leodger Tenga
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema kuwa ushiriki wa klabu za Tanzania kwenye mashindano ya Kombe la Kagame yaliyopangwa kufanyika kwenye miji ya Darfur Kaskazini na Gordofan Kusini nchini Sudan unategemea tamko la Serikali ambayo kwa sasa inafanya tathmini ya hali ya usalama.

Tenga, ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF, alisema tayari TFF na Serikali zimeshafanya mazungumzo, na Serikali imepewa taarifa zote muhimu kuhusu mashindano kwa ujumla, malazi ya klabu za Tanzania, uhakika wa usalama, usafiri wa ndani na mambo mengine muhimu hivyo kwa sasa Serikali inatathmini taarifa hizo kabla ya kutoa tamko.

“Masuala ya usalama yako nje ya uwezo wa CECAFA. Kwa hiyo, kama Serikali itabaini kuwa hali usalama ya huko si nzuri, hatutaziruhusu na kama ikiona hali ni nzuri, itaruhusu,” alisema Tenga.

“Jukumu la CECAFA (Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu vya Nchi za Afrika Mashariki na Kati) ni kuandaa mashindano na kupata uhakika wa usalama kutoka nchi mwenyeji.

“Kama tukipata uhakika huo wa usalama, mashindano yanafanyika. Lakini nchi moja moja zinayo haki ya kuhoji usalama kwa kuwa ni wajibu wa Serikali hizo kujali maisha ya wananchi wake.”

Tenga alisema kuwa mashindano hayo yalikuwa yafanyike Ethiopia, lakini katika dakika za mwisho nchi hiyo iliomba isiandae mashindano hayo hadi mwakani na ndipo Sudan ilipojitokeza kuokoa mashindano hayo.

Alisema wakati wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA) uliofanyika Mauritius, CECAFA iliitisha mkutano mkuu wa dharura na kupewa taarifa ya maandalizi ya mashindano hayo kutoka uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Sudan na wanachama wakaridhia baada ya kuhakikishiwa usalama.

“Hivyo nchi wanachama wa CECAFA zimeridhia kushiriki baada ya kuhakikishiwa usalama, lakini kwa kuwa Waziri wetu ameonyesha wasiwasi kuhusu usalama wa Darfur, hatuna la kufanya zaidi ya kumsikiliza. Ni kauli ya kiongozi anayeonekana kuwajibika na ni lazima tusubiri tamko la Serikali,” alisema Tenga.

“Lakini napenda kuishukuru Serikali ya Sudan kwa uamuzi huo kwa sababu kuandaa mashindano hayo si kitu kidogo. Tayari Katibu Mkuu wa CECAFA (Nicholas Musonye) ameshakwenda kwenye maeneo hayo na kukaa wiki nzima akikagua viwanja na hoteli zitakazotumika na kuridhika nazo,” alisema.

Alisema watu wasipotoshe tamko la Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alilolitoa Bungeni kuhusu ushiriki wa timu zetu Darfur.

“Mhe. Membe alisema Serikali itafanya uchunguzi ijihakikishie kuwa hali ya usalama ni nzuri… alisema Serikali haitakubali kuruhusu raia wake kwenda Darfur wakati hali ya usalama si nzuri,” alisema Tenga.

“Kwa maana hiyo, na baada ya TFF kuipa Serikali taarifa zote muhimu kuhusu hali itakavyokuwa wakati wa mashindano, sasa tunasubiri tamko la Serikali. Na hii ni kawaida kabisa kwa kuwa hata hapa tunapoaandaa mashindano, ni lazima kwanza tupata uhakika wa usalama kutoka serikalini ndipo tuziite timu.”

Alifafanua kuwa si jukumu la CECAFA kuamua mashindano yafanyike mji gani na kwamba chama cha nchi mwenyeji ndicho kinachoamua mashindano yafanyike mji gani.

“Sasa kwa suala la Sudan, magavana wa majimbo hayo mawili ya Darfur Kaskazini na Gordofan Kusini waliomba kwa chama chao mashindano hayo yafanyike kwenye miji hiyo na Serikali ya Sudan ikaihakikishia CECAFA usalama,” alisema.

“Sasa ikitokea Serikali yetu ikasema hali si nzuri, hatutaziruhusu timu zetu ziende kwa sababu masuala ya usalama yako nje ya CECAFA.”

Kaseba atamba kumnyuka Mmalawi kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFKxyn1zY5N0LdqD-e-U0vmTvTHRxMFaw14h7F1xRM5apKF6x1EdSsAEfYW5qjbiA4G1nJXaEGwTOENecckOdcCgwcNJN2_uZE5wh4UL_reh1bBEAcHHCNlBFXVJhst64EnmZwbvAOksE/s640/Japhet+Kaseba.jpg
Japhet Kaseba
 
 
Baadhi ya Mabondia watakaomsindikiza Kaseba atakapovaana na Mmalawi kesho
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchinim, Japhet Kaseba kesho anatarajiwa kupanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake kutoka Malawi, Rasco Chimwanza akiahidi kupata ushindi katika pambano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa, Dar es Salaam.
Mabondia hao wawili walipimwa uzito na afya zao leo zoezi lililosimamiwa na Anthony Ruta, Ibrahim Kamwe, Pendo Njau na Dk John Lugambila na kugundulika kuwa wote wapo fiti tayari kuonyeshana kazi kesho.
Katika upimaji huo, Kaseba amejinadi atamsambaratisha mpinzani wake katika raundi za mapema za mchezo huo.
Kaseba na Mmalwi huyo watasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi ambapo Juma Fundi atapigana na Hassani Kiwale maarufu kama Moro Best,Joseph Onyanyo wa Kenya ataonyeshana kazi na Seba Temba wa Morogoro, huku Issa Omar 'Peche Boy'atavaana na Juma Seleman na michjezo mingine kadhaa.

Kim Poulsen aahidi ushindi ugenini kesho dhidi ya Morocco

Kocha Kim Poulsen

Kikosi cha Stars

Na Boniface Wambura, Morocco
TIMU ya taifa, Taifa Stars inatupa karata yake ya pili ugenini kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia kwa kesho (Juni 8 mwaka huu) kuikabili Morocco (Lions of the Atlas) kwenye Uwanja wa Grand Stade hapa Marrakech, Morocco.

Ilipoteza ya kwanza ugenini dhidi ya Ivory Coast mwaka jana, na kushinda mbili mfululizo nyumbani dhidi ya Gambia na Morocco. Mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za Morocco ni ya pili kwa Stars katika uwanja huo ambapo mwaka juzi ilifungwa mabao 3-1.

Washabiki wa Morocco wanaonekana kuikatia tama timu yao yenye pointi mbili tu nyuma ya Ivory Coast inayoongoza kundi hilo la C ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Tanzania yenye sita. Huo ni mtazamo wa washabiki, lakini kwa upande wa timu inaonekana imepania kujichomoa katika nafasi za chini.

Kwa upande wa Kocha wa Stars, Kim Poulsen amesema timu yake imepania mechi hiyo, lengo likiwa ni kuona inapata matokeo mazuri baada ya dakika 90 za mechi hiyo itakayokuwa chini ya refa Daniel Frazier Bennett wa Afrika Kusini.

Amesema timu yake itacheza kwa umakini na uangalifu kwa vile wanajua wapinzani wao wakicheza mbele ya washabiki wao watakuwa katika shinikizo za kushinda, jambo ambalo wamejiandaa kukabiliana nalo.

Kwa upande wa maandalizi, Kim amesema Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wadhamini wa timu hiyo Kilimanjaro Premium Lager wameiandaa vizuri kwani iko kambini kwa wiki tatu sasa na kupata mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan iliyochezwa wiki iliyopita nchini Ethiopia.

Stars iliifunga Morocco mabao 3-1 zilipokutana Machi 24 mwaka huu jijini Dar es Salaa. Lakini zilipokutana hapa Marrakech mara ya mwisho mwaka 2011, Morocco iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Kim amesisitiza kuwa kikosi chake kimepania kufanya vizuri katika michuano hii ya mchujo ya Kombe la Dunia, ha hiyo inathibitishwa na matokeo ya timu kadri inavyoendelea kucheza mechi za mashindano.

“Moja ya mipango yetu katika mechi hizi za Kombe la Dunia ni kushinda nyumbani, hilo hadi sasa tumelifanya kwa asilimia 100. Lakini ili tukae vizuri zaidi tumekuja hapa Morocco kwa lengo la kupata matokeo mazuri, ingawa tunajua mechi itakuwa ngumi,” amesema kocha huyo raia wa Denmark.

Kwa hapa Marrakech mechi hiyo imekuwa haizungumzwi mara kwa mara, na kubwa ni kuwa Wamorocco wengi wanaamini kuwa timu yao ambayo hadi sasa ina pointi mbili haina nafasi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata ya michuano hiyo.


Arsenal yaridhia Wenger kumsajili Rooney


http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2012/12/21/article-2251594-165E1B03000005DC-807_634x569.jpg
Wayne Rooney

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2009/8/1/1249153548354/Arsene-Wenger-001.jpg
Kocha Arsene Wenger

KLABU ya Arsenal ya England imempa ruksa Meneja wake Arsene Wenger kumnunua mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney  endapo atahisi kuwa mchezaji huyo anahitajika kwenye klabu hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa Arsenal, Ivan Gazidis amenukuliwa na gazeti la The Sun akisema kuwa klabu yake ina uwezo wa kumnunua, Wayne Rooney kwa paundi milioni 25 na kumlipa mshahara wa paundi 200,000 kwa wiki sawa na anaolipwa kwenye klabu ya Manchester United kwa sasa .
Gazidis aliongeza kuwa, iwapo kocha wao (Wenger) atapeleka maombi ya kutaka kumnunua mchezaji huyo  bodi ya wakurugenzi haitakuwa na sababu ya kuyakataa kwa vile wanao uwezo wa kumnunua na kumlipa  mshahara huo mnono.
Rooney amekuwa kwenye wakati mgumu ndani ya klabu ya Manchester siku za karibuni juu ya hatma yakee Old Trafford baada ya kupeleka maombi ya kutaka kuuzwa mwishoni mwa msimu ulioisha hivi karibuni, huku klabu yake ikinyakua taji kwa kuwapokonya mahasimu wao Manchester City.
Hata hivyo duru za kimichezo zinasema kuwa, Rooney anajiandaa kubadilisha uamuzi wake wa kutaka kuondoka Old Trafford kwa kusalia baada ya kocha Sir Alex Ferguson kustaafu akitajwa hakuwa na uhusiano mzuri naye kwa siku za karibuni.
Tangu ilipotangazwa nia yake ya kuondoka United, klabu kadhaa zimekuwa zikipigana vikumbo kumnyemelea mshambuliaji huyo tegemeo wa timu ya taifa ya England zikijiandaa kumnunua zikiwemo Arsenal na PSG , lakini wakisubiri kupata maafikiano na klabu yake ya sasa ya United.

Miss Kigamboni, Sinza, Mbeya kupatikana leo


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi9yOYtTf6fzueqNlsH73yKCUSBSeVTNa7vumcj64AoXUic6tYCJnyfg5B8WormJKggH2bCA5_4zblvWCiaMWq_oCQT0Ks2fHyyi4M8WA7PtIoC3659MnuhVZp8ONatHK0g4f2gnIm8QcM/s1600/fm8.jpg
Bendi ya FM Academia itakayopamba shindano la Redd's Miss Kigamboni

MREMBO atakayefanikiwa kutwaa taji la kitongoji cha Kigamboni mwaka huu "Redd's Miss Kigamboni 2013" katika shindano litakalofanyika leo usiku kwenye ukumbi wa Navy Beach, Kigamboni atajinyakuliwa zawadi ya Sh.500,000, imeelezwa.
Maandalizi ya shindano hilo yamekamilika na warembo 12 kutoka sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam watapanda jukwaani kuwania taji hilo.
Akizungumza jana, mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng'itu, alisema kuwa mrembo atakayeshika nafasi ya pili katika shindano hilo atapata zawadi ya Sh.300,000, mshindi wa tatu Sh.250,000 huku wawili watakaotangazwa kushika nafasi ya nne na ya tano kila mmoja ataondoka na Sh.200,000.
Somoe alisema kuwa warembo wengine saba waliobaki kila mmoja atapata kifuta jasho cha Sh.100,000.
Alisema bendi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma itatumbuiza katika shindano hilo ambalo kiingilio cha viti maalum ni Sh.10,000 na viti vya kawaida ni Sh. 5,000.
Warembo watano watakaoshika nafasi za juu kwenye shindano hilo watapata nafasi ya kushiriki kinyang'anyiro cha Redd's Miss Temeke baadaye mwaka huu.
Taji la Redd’s Miss Kigamboni linashikiliwa na Edda Sylivester ambaye pia ndiye mshindi wa kanda ya Temeke na alishika nafasi ya tatu katika shindano la Redd’s Miss Tanzania mwaka jana.
Aidha, shindano la Redds Miss Sinza pia litafanyika leo ambapo warembo 12 wanaowania taji la hilo watakapopanda jukwaani kwenye ukumbi wa Meeda Club kushindania taji hilo.
Mashindano hayo ambayo yamepangwa kuanza saa 1.00 usiku, yatashuhudia Redds Miss Tanzania, Brigitte Alfred akivua taji lake la kwanza katika usiku huo ambao utakuwa na burudani za kila aina. Mbali ya kuwa Miss Sinza, Brigitte  pia anashikilia taji la Redds Miss Tanzania.
Mratibu wa mashindano hayo, Majuto Omary alisema jana kuwa maandalizi yameshakamilika na bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' itatumbuiza siku kwa mara ya kwanza na kutoa zawadi kwa wakazi wa Sinza na vitongoji vyake.
Wakati huo huo, Furaha Eliab anaripoti kutoka Mbeya kuwa warembo 12 kutoka katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Mbeya watachuana kuwania taji la Redd’s Miss Mbeya yatakayofayika kesho.
Akizungumza na waandishi wa habari, muandaaji wa mashindano hayo, Gabriel Mbwile, alisema kuwa mashindano hayo yatafanyika kesho kwenye viwanja vya City Pub vya jijini Mbeya na yatapambwa na msanii wa kizazi kipya, Bob Junior, maarufu kama Rais wa Masharobaro.
Alisema mshindi wa kwanza atajinyakulia zawadi ya Sh. milioni 1, mshindi wa pili Sh.750,000 na wa tatu Sh.500,000.

Thursday, June 6, 2013


WAPINZANI WA MIYEYUSHO, MASHALI WAFAHAMIKA KUPIGANA NAO TAMASHA LA USIKU WA MATUMAINI UWANJA WA TAIFA

Bondia Thomas Mashali (kulia) akitia saini ya dole gumba kwenye mkataba wa kupambana kwa ajili ya kuchangia elimu siku ya Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7, mwaka huu katika uwanja mpya wa Taifa jijini Dar. Mashali atacheza na Bondia Patrick Amote kutoka Kenya. Tamasha hilo litawashilikisha wasanii mbalimbali pamoja na wabunge. Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akisaini mkataba kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya katika Tamasha la Usiku wa Matumaini. Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Thomas Mashali akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Patrick Amote katika Tamasha la Usiku wa Matumaini.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya.

Ajali nyingine mbaya jijini Mbeya, 17 wanusurika kufa kiajabu





Daladala ambayo ilikuwa inatoka Mbalizi kwenda Songwe  yenye namba za usajili T 635 ALS ikiwa imeharibika vibaya Baada ya Ajali kutokea Eneo la Ifisi Mbalizi Mbeya
Hapa ndipo eneo ambalo Daladala iliingia wakati ilijaribu kulipita Gari lengine akiwa mwendo kasi na kuukutana na Tela la Mafuta
Daladala upande wa nyuma
 Lori aina ya Scania yenye namba ZA usajili T378 AGD likiwa limepaki Baada ya ajali hiyo kutokea

Mabaki ya daladala
Wananchi mbalimbali wakiwa wanashuhudia ajali hiyo iliyo tokea Ifisi Mbalizi Mbeya
Hivi ndivyo Daladala inavyo onekana upande wa Mbele baada ya Ajali kutokea


 Dereva wa daladala ambaye ndiye aliye sababisha ajali hiyo Nikutusya Mwanja akiwa anapelekwa chumba cha matibabu ya Haraka.

 
 Baadhi ya Majeruhi waliokuwemo katika ajali hiyo
Wakazi mbalimbali wakiwa katika Hospitali ya Ifisi Mbalizi Mbeya kutazama ndugu zao waliopata ajali.
Askari wa usalama barabarani wakiandikishana Dhamana na ndugu wa Dereva wa Daladala ili apate dhamana ya kutibiwa
*****************


WATU  17 wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuharibika vibaya kufuatia ajali iliyohusisha Gari la abiria aina ya Toyota Hiace na Scania.
Ajali hiyo imetokea  leo majira ya Saa Saba Mchana katika eneo la Ifisi nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Ifisi(ICC) Mbeya Vijijini.
Mashuhuda  wa ajali hiyo wamesema gari la abiria Toyota Hiace lenye namba za usajili T 635 ALS likiendeshwa na Nikutusya Mwanja likitokea Mbalizi kuelekea Songwe iliingia kwenye Trela la Scania lililokuwa likitokea Tunduma kuelekea Dar Es Salaam.
Wamesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa gari ndogo ambapo Dereva alikuwa akijaribu kulipita gari lingine lakini mbele akakutana na Lori ambalo alipojaribu kulikwepa akaingia kwenye Trela lake na kupinduka vibaya.
Trela hilo lenye namba za usajili T 675 ACT likiwa linavutwa na Kichwa chenye namba za usajili T 378 AGD halikuweza kuumia sana kutokana na kwenda kwa mwendo mdogo ambapo majeruhi wote wamekimbizwa katika Hospitale teule ya Ifisi kwa matibabu zaidi.
Muuguzi Msaidizi wa Hospitali Teule ya Ifisi Elimath Sanga amethibitisha kupokelewa kwa majeruhi 17 na kwamba kati ya majeruhi hao 3 hali zao siyo nzuri sana ingawa majina yao hayakuweza kupatikana.
Ameongeza kuwa majeruhi wengi wameumia sehemu za kichwani na miguuni na kwamba baada ya kumaliza kupatiwa huduma ya kwanza wataangalia ni wangapi wanaweza kuruhusiwa na wengine kulazwa.
Hata hivyo habari kutoka eneo la tukio zimesema kuwa Kondakta wa gari dogo aliyefahamika kwa jina moja la Ayubu alitoweka mara baada ya kutokea kwa ajali ingawa haifahamiki kama ni kurukwa kwa akili au ni kukimbia kesi.

Uholanzi yaingia Tano Bora, Tanzania yapaa FIFA

WAKATI Tanzania ikizidi kupaa katika viwango vya ubora wa soka duniani kutoka nafasi ya 116 hadi 109 ikiwa na maana imepanda nafasi saba, nchi ya Uholanzi imefanikiwa kuingia kwenye Tano ya orodha mpya iliyotangazwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka, FIFA, huku nchi ya England ikiporomoka kwa nafasi mbili.
Katika orodha mpya nafasi nne za juu imeendelea kubaki vile vile kama ilivyokuwa mwezi uliopita ambapo Hispania ianongoza , ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Croatia.
Ureno ya Cristiano Ronaldo imeshuka kwa nafasi mopja hadi nafasi ya sita, ikifuatiwa na Colombia, Italia, England na Ecuador.
Kwa ukanda wa Afrika Ivory Coast wameendelea kuongoza orodha ikiwa nafasi ya 13 duniani ikifuatiwa na Ghana iliyopo nafasi ya 21 duniani na Mali (23).
Ukanda wa Afrika Mashariki na kati, Uganda inaongoza ikishika nafasi ya 24 Afrika na 93 duniani ikifuatiwa na Ethiopia, kisha Tanzania iliyopanda kwa nafasi saba hadi nafasi ya 109 duniani na 32 Afrika.
Inayofuata baada ya Tanzania ni Kenya iliyolala jana 1-0 kwa Nigeria, kisha Burundi, Rwanda, Sudan, Eritrea, Sudan Kusini, Somalia na Djhibout inayoshika mkia.