STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 5, 2013

Kenya yataja walishambulia Westgate

Washambuliaji ndani ya jumba la Westgate
Kenya imetoa majina ya wanaume wanne ambao inasema ndiyo walifanya shambulio la jengo la maduka la Westgate, mjini Nairobi majuma mawili yaliyopita ambapo watu zaidi ya 60 waliuwawa.
Wanaume hao walionekana kwenye picha za kamera za usalama zilizopatikana Westgate baada ya jumba hilo kuvamiwa kwa siku nne.
Msemaji wa jeshi aliwataja wanaume hao kuwa Abu Baara al-Sudani, Omar Nabhan, Khattab al-Kene na Umayr.
Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Taarifa mjini Nairobi zinaonesha kuwa wawili kati yao wana uhusiano na al-Qaeda na mmoja ana uhusiano na kundi la al-Shabaab ambalo lilisema lilishiriki katika shambulio la Westgate.

BBC

Simba yabanwa na Ruvu, Tambwe atupia kama kawa

Betram Mwombeki akijaribu kumtoka beki wa Ruvu Shooting (Picha:Francis Dande)
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba jioni hii imeshindwa kuendeleza ubabe wake baada ya kubanwa mbavu na Ruvu Shooting na kutoka sare ya bao 1-1, huku Amisi Tambwe akiendelea kufunga.
Simba ililazimika kusubiri hadi kipindi cha pili kuchomoa bao kupitia mkwaju wa penati iliyofungwa na Mrundi Amisi Tambwe likiwa bao lake la nane.
Ruvu Shooting walitangulia kupata bao lao dakika ya nane tu tangu kuanza kwa pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao la maafande hao waliokuwa wenyeji wa pambano hilo liliwekwa kimiani na Said Dilunga na kudumu hadi kipindi cha kwanza kilipomalizika.
Hata hivyo kipindi cha pili kilipoanza iliwachukua dakika sita tu Simba kulirejesha bao hilo baada ya Betram Mwombeki kuangushwa langoni mwa Ruvu na mwamuzi kuamuru ipigwe penati iliyolalamikiwa na wachezaji wa maafande hao.
Hata hivyo kwa kuwa uamuzi wa refa ni wa mwisho wachezaji wa Ruvu kwa shingo upande walikubali mkwaju huo upigwe na Tambwe kusawazisha.

Golden Bush Fc yapanda daraja

Golden Bush iliyopanda Daraja hadi la Tatu Kinondoni
TIMU ya soka ya Golden Bush Fc iliyokuwa ikishiriki Ligi Daraja la Nne Wilayani Kinondoni, imefanikuwa kupanda daraja hadi la Tatu.
Golden Bush klabu mpya katika na iliyokuwa ikishiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza imefuzu daraja la tatu kutokana na kufanya vyema katika mechi zake za mzunguko wa pili. 
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa klabu hiyo ni kwamba Chama cha Soka wilayani humo (KIFA) imeitangaza klabu hiyo kupanda daraja.
MICHARAZO inawapa pongezi vijana hao kwa mafanikio hayo na ikiwakumbusha hawapaswi kuvimba kichwa badala yake ijipange kukabiliana na michuano iliyopo mbele yao;
Taarifa hiyo ya uongozi wa Golden Bush unasomeka hapo chini kama ifuatavyo, l 

Wadau,
 
Nimekuwa kimya kwa muda mrefu hii inatokana na majukumu kuingiliana kidogo na kukosa muda wa kuwalisha taarifa mpyampya. Leo napenda niwataarifu kwamba ile timu yetu ya vijana imetangazwa rasmi na KIFA kwamba imepanda daraja la tatu. Hii imetokana na kumaliza mzunguko wa mwisho bila kutoteza mechi hata moja. mimi binafsi nilibahatika kuangalia mechi kama tatu hivi vijana wakifanya mamabo mazito, hakika mpira ni maandalizi na siyo kununua refa. Tumecheza games zote bila kumpa hata shilingi 500 refa nab ado tumefanilkiwa kumaliza ligi katika mzunguko wa pili ambao ni mgumu kabisa bila kufungwa.
 
Binafsi nawapongeza sana vijana kwa kazi kubwa sana lakini pongezi za pekee wanastahili bench la ufundi  chini ya Madaraka Selemani, Katina Shijja na Waziri Mahadhi kwa matokeo mazuri na kupandisha timu daraja ambayo kwa sasa hivi imekuwa gumzo hapa Dar es Salaam. Aidha ningependa kuwopongeza kwana namna ya pekee kabisa wachezaji wa timu yetu ya Veterans kwa msaada mkubwa wa kiushauri kwa mudawao wa kujitolea kutoa mawazo ya kila aina ambayo kwa hakika ndiyo yametufanya tufika hapoa tulipo leo. Nakumbuka hatua ya kwanza kabisa tulifungwa game ya kwanza 1-0, baada ya kupata matokeo yale wazee waliwaita vijana na kuwapa ushauri wa kisaikolojia, kiufundi na kuwaandaa kitalaam kabisa kwa game iliyofuata, nakumbuka tulishinda mecho zote zilizofuata na kuna timu ilikimbia baada ya kuona hadi half time tumewapiga 7-0. Nawashukuru sana watu wazima wakiongozwa na Macocha kwa kazi nzuri nzuri nzuri sana. Ni furaha kubwa nay a pekee unapokuwa na timu inayoandaliwa kucheza mpira siyo kwenda kuloga na kuhonga marefa. Tumefanya kazi yetu na wote kwa pamoja tunastahili sifa na kujipongeza.
 
Golden bush oyeeeeeeeeee!

Kiemba, Niyonzima hapatoshi tuzo za Mwanaspoti Bora 2013


Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda(kushoto)akisaini mkataba wa udhamini wa Tuzo ya Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013,wanaoshuhudia ni Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa (katikati) na Ofisa Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo Ibrahim Kaude.

Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa(katikati)akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kutangaza mdhamini mkuu wa Tuzo za Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013,Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda na kulia ni Ofisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude.
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda,akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kusaini mkataba na kutangaza udhamini wa kampuni yake kwa Tuzo za Mwanaspoti bora wa soka wa Vodacom 2013.
 =======
KATIKA kuhakikisha zinathamini na kuleta ladha na ubora wa mchango wa wanasoka nchini wadau wa mchezo wa soka; Mdhamini mkuu wa  ligi ya Tanzania bara Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania na kampuni ya  Mwananchi Communications Limited (MCL)wameungana katika kuwezesha zoezi la utoaji wa Tuzo ya Mchezaji bora wa soka kwa mwaka 2013.

Tuzo hiyo itashuhudia wachezaji walioingia hatua ya Tano bora, AMRI KIEMBA, HARUNA NIYONZIMA, SHOMARI KAPOMBE, THEMI FELIX, na KELVIN YONDANI wakichuana kuwania umwamba wa soka nchini Tanzania, Baada ya kupigiwa kura na mashabiki na Kamati maalum chini ya Mwenyekiti wake Zamoyoni Mogela kuchambua majina hayo kulingana na kura walizopata.

Akizungumza katika Mkutano wa kutambulisha tuzo hizo Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda, amesema daima Vodacom imekuwa msitari wa mbele katika kuunga mkono michezo nchini, hususani mchezo wa soka na kuhakikisha unakuwa moja ya ajira muhimu kwa watanzania.

"Vodacom tumeendelea kuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya soka la Tanzania, sasa soka limekuwa zaidi ya burudani kwa watanzania kutokana na chachu ambayo tumeiweka tangu tuanze kudhamini ligi kuu, ambayo sasa imekuwa na ushindani mkuba na thamani yake inazididi kupanda siku hadi siku" alisema Kamuhanda na kuongeza,

"Mafanikio haya yanayopatikana katika soka letu, yanatokana na nguvu na kujitoa kwa hali na mali, lakini watu wa kwanza ambao wanaleta mafanikio haya ni wachezaji ambao wamekuwa wanapambana kufa na kupona kutoa burudani kwa Watanzania, Ni lazima tuwaenzi wachezaji hawa, Tunapouzungumzia mchezo wa soka tunazungumzia maisha ya watu sasa, Mpira ni maisha ya watu kwani umetoa ajira kubwa kwa jamii ya Watanzania" alisema.

Kamuhanda aliongeza kuwa wameamua kudhamini tuzo hizo ili kuendelea kuwa sehemu ya mafanikio ya soka Tanzania na kuleta mapinduzi katika soka la Tanzania kwa kutambua michango wa wachezaji mbalimbali ambao mpira kwao ndo ajira kuu.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa amesema kuwa, waliamua kuanzisha tuzo hizo ili kuendelea kuunga mkono jitihada za wachezaji wa Tanzania na kuleta ushindani na kujenga moyo miongoni mwa wachezaji wa soka nchini.

"Tuzo hizi zinatambulika rasmi kwa jina la zitaitwa MWANASPOTI BORA WA SOKA WA VODACOM 2013. Ni za kipekee na za kwanza kabisa nchini kwa wigo wa wachezaji wanaohusishwa, ushirikishwaji wa uteuzi wa mshindi, na vigezo husika." ALISEMA Mukasa na kuongeza.

"Kwa mwaka huu, licha ya kumpata Mwanaspoti Bora wa soka wa mwaka wa jumla, tuzo hizi zitakuwa na "categories" zaidi ya 10 ikiwemo kocha bora, mwamuzi bora, mchezaji bora wa kike, mchezaji bora chipukizi, "1st eleven", goli bora, mchezaji bora wa kigeni, Mchezi bora wa kulipwa anayecheza nje, na Kipengele kingine kitajulikana siku ya kilele (surprise)." Alisema Mukasa.

Mukasa alihitimisha kwa kusema kuwa ili kuweka usawa miongoni mwa wapenzi wa soka wachezaji hao walioingia katika Tano bora wanaweza kupigiwa kura na Mashabiki kwa  kuandika ujumbe mfupi unaoanza na neno KURA kisha jina la mchezaji anayemchagua kati ya hao waliotajwa na kisha kutuma kwenda namba 15678. Mshindi wa Tuzo hiyo atatangazwa siku ya kilele cha sherehe hizo.
Mwisho 

Botswana yajitosa kusapoti IBF

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AO9WimIAACEaUk%2BaDQAAACq2uhA&midoffset=2_0_0_1_1792922&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331
GABORONE,
BOTSWANA's Botswana’s Minister for Environment and Tourism Hon. Tshekedi Khama (seeing photo with the IBF/Africa President Onesmo Ngowi) pledged his government’s support to the success of "IBF Sports Tourism Program" for African countries.


Hon. Tshekedi Khama assured the IBF/Africa President, Onesmo Ngowi of his government's support towards the development of "Sports Tourism" to Africa as one of sustainable by-products of tourism sector.

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AO9WimIAACEaUk%2BaDQAAACq2uhA&midoffset=2_0_0_1_1792922&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331
Ngowi and Khana

The IBF/Africa President paid a courtesy visit to the Minister for Environment and Tourism Hon. Tsekedi Khama in the minister’s office as part of his marketing drive for the “IBF International Jr. Featherweight Title” which Botswana’s pro-boxer Lesley Sekotswe will meet a boxer from Britain to be announced soon.


This epic event will be televised live by Super Sports 9 and streamlined by VoxAfrica by to over 100 million homes in Europe, Asia, Africa and the USA.


The event will present great opportunity to Botswana to showcase its tourism attractions to millions of inbound tourists. Such a befitting event will also attract direct investments which Botswana needs for its economic diversification from its mineral based economy.


Over the decades, tourism has experienced continued growth and deepening diversification to become one of the fastest growing economic sectors in the world. Today, the business volume of tourism equals or even surpasses that of oil exports, food products or automobiles.


Tourism has become one of the major players in international commerce, and represents at the same time one of the main income sources for many developing countries. This growth goes hand in hand with an increasing diversification and competition among destinations.


"Sports Tourism" globally provides a forum where stakeholders leans how to properly utilize it to effect profound positive change for destination positioning.


Through the much needed awareness and interactions provided over by the "Sports Tourism", stakeholders  are able to learn new trends in the industry, provide much needed information on their respective destinations and also the various tourism by-products in place which are effective promotional tools within the various destinations.


According to the UNWTO, tourism sector generates over US$ 4.5 trillion per annual and out of this figure "Sports Tourism" generated over US$ 100 billion.


BOTSWANA has made gigantic strides to pro-boxing as a result of the President of IBF/AFRICA Onesmo Ngowi's historic visit, in April 1-6 2013 this year. The visit excited a lot of boxing stakeholders in this country. Also, the visit has also helped to encourage the number of experienced amateur boxers to join professional boxing ranks hence the October 5, tournament.


Upon arrival in Botswana in October 02, the IBF/Africa President met several high ranking government officials as well as corporate leaders to encourage them to support the "IBF Sports Tourism" initiative to Africa of which Botswana is one of the six pilot countries. Other countries are Namibia, Tanzania, Ghana, UAE, South Africa and Tunisia respectively.

 
Botswana is endowed with great wealth in terms of mineral resources (diamond, gold and uranium) and exports of meat to Europe, Asia and USA. It has great amateur boxing foundation as most of her boxers perform well in various international meets hence the great potential fueling pro-boxing.
  

Under its pet project of "IBF Sports Tourism", the IBF/AFRICA has projected Botswana as the strong foundation for future boxing tournaments given its strong amateur boxing foundation, vibrant economy and good governance.


"These are the three pillars and ingredients of boxing development so we can see positive signs ahead” echoed the IBF/AFRICA President, Onesmo Ngowi who was a professional boxer on how he sees Botswana's direction in pro-boxing.


Ngowi illustrated that Botswana’s "economy and good governance" are key towards sustainable boxing development. "You need to build up a strong foundation for "Sports Tourism" and many developing countries fail to succeed due to their poor economies and governance. When you have GDP Per Capita Income in the region of  US$ 3000 then you can afford to pay $ 200 - $ 500 to see boxing events". he emphasized.


Also, the IBF/AFRICA's President alluded that lack of "TV and Corporate Sponsorship" may be another contributing factor for poor showing of Africa in the boxing industry. "Our TV Networks want promoters to pay them when showing their boxing tournaments instead of them TV paying for the boxing broadcasting" continued Ngowi.


The Botswana's October 5, 2013 tournament is coming at a time when the world’s diamond merchants De Beers are moving its international auction headquarter from London to Gaborone Botswana. The move herald Botswana’s robust economic development and the country’s keen interests to diversify its economy hence  development of tourism sector.

Given these rather positive trends, Sports Tourism as one of by-products of tourism is coming at the right moment.

Ajali tena! Basi la Machinga uso kwa uso na Lori, dereva afa papohapo

Baadhi ya mashuhuda wakilishangaa basi la Machinga lililopata ajali

AJALI za barabarani zimeendelea kupoteza uhai wa watumiaji wake baada ya basi la Machinga kupata ajali mbaya ya kugongana uso kwa uso na lori na kusababisha kifo cha dereva wake.
Taarifa zinasema kuwa dereva aliyepoteza maisha yake anafahamika kwa jina la Noor, na ajali hiyo ilitokea katika eneo la Kilimahewa mbele kidogo ya Kimanzichana.
Basi hilo lilikuwa likitokea Dar kuelekea Mtwara na ndipo likagongana uso kwa uso na lori la mizigo na kusababisha kifo hicho na abiria wengine kadhaa kujeruhiwa.
Taarifa zaidi juu ya ajali hiyo itawajia kadri tukibahatika kuzipata kupitia hapa hapa www.micharazomitupu.blogspot.com

Friday, October 4, 2013

Masheikh wauwawa Mombasa, kanisa lachomwa moto katika ulipizaji kisasi

Sheikh Abuu Rogo enzi za uhai wake, huyu aliuwawa mwaka jana

POLISI Kenya imetangaza kuwa, watu wanne akiwemo Sheikh Ibrahim Ismail Rogo wameuawa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana ndani ya gari dogo jana usiku huko mjini Mombasa.

Taarifa ya Polisi Kenya imeeleza,  Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mrithi wa Sheikh Aboud Rogo ambaye  naye aliuawa na familia yake kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mwezi Agosti 2012.

Mauaji ya Sheikh Ibrahim Rogo ambayo yameutikisa mji wa Mombasa, yametokea  baada ya kupita takriban wiki mbili tokea kundi la al Shabab lilipovamia  na kuua  watu wasiopungua 63 na kujeruhi mamia ya wengine kwenye jengo la maduka ya biashara la Westgate jijini Nairobi.

Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu kikosi  maalumu cha kupambana na ugaidi kuwa ndicho kilichotekeleza  mauaji hayo.

Sheikh Ibrahim Rogo ambaye alikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa mjini Mombasa alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi  ya kigaidi.

Polisi Kenya imesema kuwa, Gaddafi Mohammad, Issa Abdallah  na Omar Abu Rumeisa ni miongoni mwa waliouawa, naye Salim Aboud alinusurika kwenye shambulio hilo.

=========

Protestors on Friday engaged armed police in running battles in Mombasa following killing of a Muslim cleric, and three others.

The rioting youths in Majengo area set a church on fire.

Earlier in the morning, hundreds of armed police were deployed across islamist strongholds in Majengo and Kisauni  as authorities anticipated riots from slain Sheikh Ibrahim Rogo’s militant supporters.

Tension which has been building up since Thursday’s blood end of Sheikh Rogo and his three friends was expected to reach boiling point at the afternoon Friday prayers in areas like Majengo especially at Musa Mosque where the slain preacher delivered controversial ceremonies.

Reports show that Sheikh Ibrahim delivered a lecture at the mosque at about 8.00pm on Thursday before  embarking on his last journey to meet his end in a drive by shooting near the Butterfly Pavillion afew minutes before 10.00pm long the Mombasa-Malindi road.

Unconfirmed reports indicate  the four were buried in the early hours of Friday at the same cemetery where slain radical islamist Sheikh Aboud Rogo Mohamed was buried on August 27 last year.

It is not clear whether the two Rogos are related.

Reports indicate the four victims were buried in a single grave at the Tudor Muslim Cemetery and accorded the rites of martyrs.

Supporters have identified the other victims as Abu Rumaysa Omar and others identified only as Issa and Shebe Gaddafi.

Salim Aboud who was with them escaped unscathed but with brief facial injuries after playing dead among the slumped corpses inside a bullet ridden car.

Militant islamist Sheikh Abubakar Shariff alias Makaburi who was among the first people to reach the scene of crime declared Thursady’s events as “an assassination” claiming state agents slew the four muslims “in retaliation” for the terrorist carnage at the Westgate Mall in Nairobi last month.

Makaburi who is facing terrorist charges and was  an ally of slain islamist Sheikh Aboud Rogo Mohamed claimed Sheikh Ibrahim Rogo was the target of Thursday’s shooting because of his past links to the former Rogo who was killed on August 27 last year.

And Makaburi denounced the Kenya government and  muslims collaborating with it following the Westgate massacre and in light of Thursday’s events.

He further warned that muslims are now justified to disobey Kenyan laws “because we cannot sit back and be slaughtered or see our sheikhs killed everyday.”

As they descended on the scene where the four were killed militant supporters of the slain preacher swore to avenge the killing.

According to Kisauni OCPD Julius Wanjohi who covers Bamburi where the killings took place, the four were killed when a “vehicle with unknown occupants sped past the car which was carrying Sheikh Ibrahim and four others and slowed a few metres from the vehicle.”

The OCPD says the occupants of the unknown car opened fire on the right side of the approaching car carrying Sheikh Ibrahim.

Wanjohi further says Sheikh Ibrahim and three others were killed “on the spot and the vehicle sped away” apparently towards Bamburi.

According to the OCPD Sheikh Ibrahim̢۪s car was heading towards Mtwapa where he is believed to live.
Source: Standard

Kaburi ya anayedaiwa kufufua lafukuliwa kuchunguza viungo vilivyokuwepo ndani yake

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kaburi ambalo alizikwa mtoto Shabani Maulidi (15), ambaye anadaiwa kufariki dunia miaka mitatu iliyopita na kuonekana akiwa hai hivi karibuni, jana lilifukuliwa na viungo vya mwili wake kukutwa ndani.
Kazi hiyo iliyofanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi pamoja na Mtafiti wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, Lucas Ndungulu, ilizua taharuki kwa umati wa watu waliokuwa eneo hilo, baada ya nyumba ya jirani lilipo kaburi hilo, Masanja Marwa, kubomoka ghafla wakati ufukuaji huo ukiendelea, huku mwanamke mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja naye akianguka na kuzirai.
Kwa sasa mtoto huyo ambaye alionekana hai, amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa uangalizi wa kitaalamu.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, Ndungulu alisema kuwa wameamua kufukua kaburi hilo ili kupata sehemu ya viungo vya mwili kwa ajili ya vipimo.
“Lengo la kufukua kaburi hili ni kutaka tupate kiungo chochote cha mwili wa marehemu ili tufanye utafiti wa kitaalamu ili tujue kama ni kweli huyu anayedaiwa kuwa ni mtoto wao ndiye,” alisema.
Alisema kuwa ufukuaji huo umemalizika na kwamba wamepata baadhi ya viungo vya mwili wa marehemu na kuchukua baadhi ya mifupa ya mapaja yote mawili ambayo itapelekwa katika hospitali ya rufaa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kwa mujibu wa Ndugulu, majibu ya vipimo hivyo yatatolewa baada ya wiki mbili kama hakutakuwa na tatizo lolote la kukatika kwa umeme.
Naye Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Adamu Sijaona, alisema kuwa pamoja na kuchukua viungo hivyo, pia watachukua damu ya wazazi na mtoto mwenyewe.
“Tumechukua pia damu ya mama na baba wa Maulidi mwenyewe ili tukapime vinasaba (DNA) na kama alivyosema mtafiti, majibu yatatoka baada ya wiki mbili,” alisema.
Akizungumza baada ya kazi ya ufukuaji kumalizika, baba mzazi wa mtoto huyo, Maulidi Shabani, alisema kuwa endapo majibu yatakuja tofauti au vile wanavyokusudia, wapo tayari kuyapokea na kwamba ikigundulika huyo aliyeonekana ni Maulidi, pia watampokea na kuendelea kumtunza.
“Lakini nina imani kuwa huyu aliyeonekana ni mwanangu Maulidi kabisa, kwa sababu anazo alama zote,” alisema mzazi huyo.
Mtoto Maulidi aliyefariki dunia miaka mitatu iliyopita na kufanyiwa matanga, alionekana akiwa hai baada ya kukutana na mama yake ana kwa ana mapema wiki hii asubuhi wakati akienda kwenye shughuli zake za biashara.
Ilidaiwa na wazazi wake kuwa Maulidi alitoweka ghafla na kushindwa kurudi nyumbani kwao Januari mosi 2011, wakati alipokuwa amewapeleka mbuzi malishoni na mwili wake kuonekana baada ya siku tatu akiwa amefia kwenye kisima cha maji.
Kwa mujibu wa baba yake, Maulidi hakurudi nyumbani siku hiyo, ambapo waliendelea kumtafuta bila mafanikio na ndipo baada ya siku tatu walimkuta akiwa amefia ndani ya kisima cha maji kilicho maeneo ya Kijiji cha Nyankumbu, Kitongoji cha Mwembeni.
Tukio hili ni la tatu kutokea mkoani hapa ambapo wilayani Kasamwa, mwanamke aliyefariki dunia miaka mitano iliyopita alionekana hai na kutambuliwa na ndugu yake. Tukio la pili lilitokea Wilaya ya Chato, wakati kijana aliyefariki dunia miaka miwili iliyopita alionekana akiwa hai.
Tanzania Daima

Kuziona Simba na Ruvu Buku 5 tu, Mohammed Theofil kuzihukumu Taifa

Ruvu Shooting wakataokuwa wenyeji wa Simba
Vinara wa Ligi Kuu, Simba watakaovaana na Ruvu Shooting kesho jijini Dar
Na Boniface Wambura
KITIMTIM cha michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kinatarajiwa kuingia raundi ya saba kesho (Oktoba 5 mwaka huu)  kwa mechi nne ambapo Ruvu Shooting itakuwa mwenyeji wa vinara Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Viingilio katika mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Mohamed Theofil kutoka Morogoro kuanzia saa 10 kamili jioni vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani kuanzia saa 4 asubuhi.

Mechi nyingine za kesho ni JKT Ruvu itakayoumana na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam huku Coastal Union ikiwa mwenyeji wa Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha ndiyo utakaotoa fursa kwa timu za Oljoro JKT na Mbeya City kuoneshana ujuzi katika kusaka pointi tatu.

Ligi hiyo itaendelea Jumapili (Oktoba 6 mwaka huu) kwa mechi kati ya Yanga na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Mgambo Shooting itaialika Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Maamuzi ya Kamati y Maadili TFF kufanyiwa mapitio upya, kisa...!

MCHAKATO wa Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unaelekeo ukingoni ambapo Maamuzi ya Kamati ya Maadili yanatarajiwa kupitiwa kabla ya kuelekea kwenye uchaguzi huo utakaofanyika Okt 26/27 jijini Dar es Salaam.

Hivi sasa, wagombea wanasubiri vyombo vya juu vya uamuzi kwa ajili ya kutoa uamuzi wa mwisho kabla ya kuanza kampeni na hatimaye uchaguzi.

Hata hivyo, baada ya Kamati ya Maadili kufanya uamuzi dhidi ya kesi nane zilizowasilishwa mbele yake, Sekretarieti imeona kuwepo kwa ukakasi katika utekelezaji wa uamuzi huo kutokana na ukweli kuwa kuna baadhi ya mambo yanaonekana kuwa na ugumu katika kuyatekeleza.

Sekretarieti si chombo chenya mamlaka ya kutafsiri uamuzi wa vyombo huru vya Shirikisho, kazi yake kubwa ni kupokea uamuzi na kuutekeleza, hivyo kwa kuwa kuna ukakasi huo imeamua kuwasilisha uamuzi huo kwenye Kamati ya Rufani ya Maadili kwa ajili ya kuufanyia mapitio (revision) na pia kutoa mwongozo kabla ya kurejesha uamuzi huo kwenye Kamati ya Uchaguzi kwa ajili ya kuendelea na mchakato.

Sekretarieti imefanya hivyo kwa lengo la kusaidia wagombea ambao wengi wanaonekana kuwa njia panda baada ya kupokea uamuzi wa Kamati ya Maadili na kuiuliza Sekretarieti kuwa inakuwaje Kamati ya Maadili iwaone hawana hatia, lakini hapo hapo ikubaliane na uamuzi wa kuwaengua, jambo ambalo kwa kweli limetufanya tukose majibu sahihi na hivyo kuamua kuomba revision na mwongozo.

Pia mwongozo utakaotolewa na Kamati ya Rufani ya Maadili utasaidia kuweka mwelekeo mzuri wa masuala ya Maadili katika siku zijazo.

Miongoni mwa mambo yanayoonekana kuwa na ukakasi ni kuwaona watu wote ambao kesi zao ziliwasilishwa kwenye Kamati ya Maadili hawana hatia, lakini hapo hapo kukubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi wa kuwaengua baadhi yao kwa sababu za kinidhamu ikisema haiwezi kuwahukumu mara mbili kwa kuwa wameshaadhibiwa kwa kuenguliwa kwenye uchaguzi.

Ili haki itendeke na ionekane inatendeka, Sekretarieti imeona ni vizuri masuala hayo yakafanyiwa revision (mapitio) na kutolewa mwongozo ili kuondoa ukakasi uliojitokeza miongoni mwa wagombea, Shirikisho na wadau na hivyo kujenga hisia kuwa kuna mbinu zimefanyika dhidi ya baadhi ya wagombea.

Uamuzi huu haumaaniishi kuwa Sekretarieti inapingana na uamuzi wa Kamati ya Maadili, bali ni utaratibu wa Sekretarieti kuomba ufafanuzi au mwongozo kutoka vyombo husika pindi inapotokea ukakasi katika utekelezaji wa uamuzi wa vyombo vya uamuzi vya Shirikisho.

Sekretarieti imeshamwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani za Maadili ili aitishe kikao kwa manajiri ya kufanya mapitio na kutoa mwongozo ambao utasaidia Shirikisho kuendelea na uchaguzi bila ya ukakasi.

TFF yaipigia goti serikali, taasisi kuisaidia U20 WanawakeSerikali, T

Lina Kessy
Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeiomba Serikali, taasisi na kampuni mbalimbali kuisaidia timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 inayojiwinda kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Msumbiji.

Timu hiyo hivi sasa iko kambini Mlandizi mkoani Pwani chini ya Kocha Rogasian Kaijage kujiandaa kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza itakayochezwa Oktoba 26 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Miguu ya Wanawake ya TFF, Lina Kessy amesema hiki ndio kipindi muafaka cha kuisaidia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Ameitaka jamii kujitokeza kuisaidia timu hiyo ambayo haina mdhamini wala mfadhili, kwani timu za Taifa ni za Watanzania badala ya kusubiri ifanye vibaya na kusema ni kichwa cha mwendawazimu.

Kessy ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), ameishukuru kambi ya JKT Ruvu kwa kutoa fursa ya kambi kwani timu hiyo hailipii malazi badala yake inalipia huduma nyingine inazopata hapo.

Vilevile amewashukuru wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakijitolea kutokana na ukweli kuwa tangu kuanza mashindano ya mpira wa miguu wa wanawake kumekuwepo uungwaji mkono mkubwa.

“Shukrani za kipekee kwa wazazi kukubali watoto wao wachezee timu ya Taifa, kwani wengi bado wanasoma na wapo chini ya uangalizi wa wazazi. Pia tunawaomba wazazi wajitokeze mazoezini ili kuwajenga kisaikolojia wachezaji wetu,” amesema.

Fainali za Dunia za U 20 kwa wanawake zitafanyika mwakani nchini Canada. Iwapo Tanzania itaitoa Msumbiji katika raundi hiyo, raundi inayofuata itacheza na mshindi kati ya Botswana na Zimbabwe.

TFF, Polisi wapiga mkwara 'wakora' viwanjani

http://reluctantgourmet.com/media/k2/items/cache/2e2c1711fe12b24ae23d95c35bfd21c2_XL.jpg
Kisu, moja silaha hatari inayowezwa kutumiwa vibaya na mashabiki uwanjani kuleta maafa
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia Jeshi la Polisi kuanzia sasa halitashikilia silaha za washabiki, na badala yake litawazuia kabisa kuingia viwanjani wakati wa mechi.

Jeshi la Polisi limekuwa likihifadhi silaha za washabiki wanaokwenda viwanjani, na baadaye kuwarejeshea baada ya mechi kumalizika kwa vile Kanuni za Usalama Viwanjani za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) zinakataza silaha viwanjani.

Wikiendi iliyopita katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jeshi la Polisi lilikamata bastola 17 katika upekuzi wa washabiki waliokwenda kushuhudia mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting na ile kati ya JKT Ruvu na Simba. Wote waliokutwa na silaha hizo walikuwa na leseni za kuzimiliki.

Hivyo, kwa washabiki wanaomiliki silaha hatawaruhusiwa kabisa kuingia viwanjani, na badala yake tunawashauri kuzihifadhi huko wanakotoka kabla ya kufika viwanjani.

Pia tunatoa mwito kwa shabiki ambaye atamuona mwenzake akiwa na silaha uwanja kutoa taarifa kwa mamlaka husika likiwemo Jeshi la Polisi ili aweze kuchukuliwa hatua.

Viwanja 10 kutimka vumbi FDL wikiendi hii

Polisi  Moro, moja ya timu inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza
Na Boniface Wambura
KIVUMBI cha Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuwania tiketi za kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao (2014/2015) inaendelea wikiendi hii (Jumamosi na Jumapili) kwa kuzikutanisha timu 20 zitakazopambana katika viwanja kumi tofauti.

Jumamosi kutakuwa na mechi kati ya Green Warriors na Friends Rangers (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi), Kimondo na Burkina Faso (Uwanja wa CCM Vwawa, Mbozi), Mlale JKT na Mkamba Rangers (Uwanja wa Majimaji, Songea) na Kurugenzi dhidi ya Polisi Morogoro (Uwanja wa Wambi, Mafinga).

Polisi Dodoma na Stand United (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), Toto Africans na JKT Kanembwa (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Mwadui na Polisi Mara (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) na Polisi Tabora na Pamba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora).

Keshokutwa (Jumapili) kutakuwa na mechi kati ya African Lyon na Transit Camp (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi) na Villa Squad dhidi ya Polisi Dar es Salaam (Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam).

Uhuru Seleman awataka 'Wagosi wa Kaya' kuwaiga wenzao wa Mbeya

Uhuru Seleman akiwa na taji la ubingwa la Ligi Kuu alipokuwa Simba
KIUNGO wa Coastal Union, Uhuru Seleman amesema amekunwa na mashabiki wa soka wa mkoa wa Mbeya kwa namna wanavyoisapoti timu yao ya Mbeya City kiasi cha kuzisahau Simba na Yanga na kuwataka mashabiki wa Coastal Union na Tanga kwa ujumla kuiga mfano huo.
Uhuru ambaye ni mwenyeji wa Mbeya, alisema wiki iliyopita Coastal ilipoenda kuumana na Mbeya City alishangazwa na namna wakazi wa mkoa huo walivyoungana pamoja na kuishangilia timu yao mwanzo mwisho kitu alichodai hajawahi kukiona Tanga na kuwataka 'Wagosi wa Kaya' kuzinduka.
Kiungo aliyewahi kuzichezea Mtibwa Sugar, Simba na Azam, alisema kwa namna mashabiki wa mkoa Mbeya wanavyoungana na kuzisahau kabisa Simba na Yanga inawatia moyo na kuwapa nguvu wachezaji wa timu hiyo kujituma uwanjani.
"Huwezi amini ukiwa Mbeya husikii habari za Simba na Yanga wao na Mbeya City na Prisons, kitu ambacho nilikuwa napenda kuwaomba mashabiki wa soka wa mkoa wa Tanga kuiga jambo hilo na kuwa na uzalendo kwa timu zao na hasa Coastal Union iliyopo Ligi Kuu," alisema.
Alisema sapoti wanayopewa wachezaji wa Mbeya City inawatia moyo na kupata nguvu ya kuipigania timu yao kuweza kuwa na matokeo mazuri licha ya ugeni wake katika ligi hiyo inayozidi kushika kasi.
"Uzalendo wa namna hiyo wa kuziunga mkono timu za nyumbani husaidia kuwatia nguvu wachezaji badala ya utamaduni wa mashabiki kugawanyika kwa unazi wa Simba na Yanga na kuzisahau timu zao ambazo zinawapelekea mechi kubwa na kuziona timu wanazoziota," alisema Uhuru.
Kiungo huyo na wachezaji wenzake watakuwa uwanja wa Mkwakwani Tanga kesho kwa ajili ya kuwakabili Azam katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, timu hizo zote zinatokea Mbeya walipoumana na wenyeji wao Mbeya City na Prisons na kuambulia sare ya bao 1-1 kila moja.

Julio aitisha Ruvu Shooting, wawili kulikosa pambano kesho Taifa

Julio akitetea na Mombeki na Henry Jospeh akiwa kando yake
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wanatarajiwa kushuka kesho dimbani kuvaana na Ruvu Shooting bila ya wachezaji wake, Miraj Adam na Abdallah Seseme ambao ni majeruhi huku wakiwa hana hakika ya kumtumia Issa Rashid 'Baba Ubaya' ambaye hali yake bado haijatengemaa vyema.
Hata hivyo kitu cha kufurahisha ni kwamba nahodha wake msaidizi, Nassoro Masoud 'Chollo' na mkongwe Henry Joseph wenyewe wapo fiti tayari kuwakabili maafande hao wanaonolewa na kocha Charles Boniface Mkwasa.
Akizungumza na MICHARAZO  kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema Simba ipo kamili kuivaa Ruvu licvha ya kuwakosa Abdallah Seseme na Miraji Adam ambao wote wamefungwa plasta gumu (POP) miguuni.
Julio alisema ukiondoa wachezaji hao wengine wanaendelea vyema japo hali ya Baba Ubaya aliyeanza mazoezi na wenzake bado haijatengemaa vizuri na hivyo kutokuwa na hakika ya kumtumia katika mechi hiyo itakayochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kudai itakuwa ngumu na yenye ushindani mkubwa.
"Kikosi kipo tayari kwa vita dhidi ya Ruvu Shooting, japo tunasikitika kusema kuwa hatutakuwa na Seseme na Miraj ambao wote wamefungwa POP huku Baba Ubaya akitupa mashaka, japo Henry Joseph na Chollo wamerejea dimbani kuungana na wenzao ambao wana ari ya ushindi," alisema.
Kuhusu mfungaji wao bora, Amisi Tambwe ambaye majuzi alishindwa kuendelea na mazoezi na wenzake kutokana na kusumbuliwa na tumbo, Julio alisema anaendelea vyema na Jumamosi ataendelea kuongoza 'mauaji' kwa Ruvu.
"Aaah alichafukwa na tumbo tu na wala halikuwa tatizo kubwa na panapo majaliwa ataendelea kuongoza mauaji dhidi ya wapinzani wetu katika Ligi Kuu," alisema Julio beki wa zamani wa Plisner, Simba na Taifa Stars.
Mbali na mechi ya Simba na Ruvu, kesho kutakuwa na mechi nyingine nne zitakazozikutanisha timu za JKT Ruvu dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa Chamanzi, Coastal Union kuialika Azam jijini Tanga na Oljoro JKT kuikaribisha Mbeya City kabla ya Jumapili Yanga kupepetana na Mtibwa Sugar na Mgambo JKT kuumana na Prisons kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga

Gari laacha njia na kuua wawili Mbeya, wengine wanaswa na bangi gramu 900

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbSKddVeeyHTyKf5ybVJhtXhjjGjgBrBwlffjXY7411udEf3xhx7lKaamyX8nf6GDoTTpcl46_dmR43D3Qz68E3q_lkYa3MX0qj0z7BBK8jJTKBwPpBBG6g038Al0GJJShhP09FkJnDXU/s640/Kamanda+wa+Polisi+Mbeya+.JPG

WATEMBEA kwa miguu wawili wamepotea maisha yao baada ya kugongwa na gari lililoacha njia mjini Mbeya huku watu wengine wawili wakinaswa na dawa za kulevya aina ya Bangi yenye uzito wa gramu 900.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la Polisi mjini humo inayosemeka hapo chini ni kwamba watu hao walipatwa na ajali hiyo jana saa 1 usiku. Isome mwenyewe taarifa hiyo.

MNAMO TAREHE 03.10.2013 MAJIRA YA SAA 19:46HRS HUKO KATIKA ENEO LA SIMIKE JKT – ITENDE BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA JIJI NA MKOA WA MBEYA.  GARI T.170 AUM AINA YA  TOYOTA CRESTA LIKIENDESHWA NA DEREVA MAHUNDI S/O KAPITI, MIAKA 27, KYUSA, MKAZI WA ITIJI LILIACHA NJIA NA KUWAGONGA WATEMBEA KWA MIGUU WAWILI  KISHA KUPINDUKA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WAWILI AMBAO NI 1. DEREVA MWENYEWE 2. NEEMA D/O MWINUKA, MIAKA 32, MNDALI, MWALIMU AMBAYE ALIKUWA MTEMBEA KWA MIGUU MKAZI WA NZOVWE PIA KUSABABISHA MAJERUHI KWA WATU WAWILI AMBAO NI 1.TWINZA S/O MWAKIYOMA, MIAKA 36, KYUSA, MKAZI WA MAJENGO AMBAYE AMELAZWA HOSPITALI YA  RUFAA MBEYA NA 2. STIVIN S/O MWAKALINGA, MIAKA 36, KYUSA, MKAZI WA NZOVWE AMBAYE ALIPATIWA MATIBABU NA KURUHUSIWA.  MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. CHANZO NI MWENDO KASI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANAENDELEA KUTOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOENDESHA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA. 


WILAYA YA  MOMBA – KUPATIKANA NA BHANGI.

MNAMO TAREHE 03.10.2013 MAJIRA YA  SAA 11:00HRS  HUKO KATIKA MTAA WA MAPOROMOKO TUNDUMA  WILAYA YA  MOMBA  MKOA WA MBEYA.  ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIWAKAMATA 1. IZDORI S/O PELLA, MIAKA 24, MKINGA, MFANYABIASHARA, MKAZI WA MAPOROMOKO NA 2. AMOS S/O ALISON MELLA, MIAKA 28, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA MTAA WA MIGOMBANI WAKIWA NA BHANGI YENYE UZITO WA GRAM 900. MBINU NI KUFICHA BHANGI HIYO KATIKA KIBANDA CHA BIASHARA CHA IZDORI S/O PELLA. WATUHUMIWA NI WAVUTAJI NA WAUZAJI WA BHANGI. TARATIBU ZINAFANYWA ILI WAFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA  WITO KWA  JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA   KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA  MTUMIAJI. AIDHA ANATOA RAI KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA BIASHARA HARAMU ZA MADAWA YA KULEVYA AZITOE KWENYE MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE.
Signed by:
                           [DIWANI ATHUMANI - ACP]
  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Kwa Mombeki Soka kwanza blabla baadaye


MSHAMBULIAJI mrefu wa Simba, Betram Mombeki amesema yeye kazi yake kubwa katika klabu hiyo ni kucheza mpira na siyo kuzungumza na vyombo vya habari.
Alisema iwapo kutakuwa na watu wanaotaka kumpamba au kumponda basi wapime uwezo wake uwanjani wakati anaitumikia Simba.
Akizungumza na gazeti hili katika mazoezi ya Simba, Mombeki aliyesajiliwa akitokea Pamba ya Mwanza, alisema huwa hapendi kuzungumza na vyombo vya habari kwa sababu siyo kazi yake.
"Unajua kazi yangu ni kucheza soka, ndiyo kazi yangu pekee ninayoijua yaani kujipanga vyema kuisaidia timu yangu iwe ni kwa kufunga au kutoa pasi ya mwisho, lakini siyo kuzungumza na wanahabari kila mara," alisema.
Mombeki alisema kama kuna mtu anataka kujua sifa na ubaya wake wampime kwa majukumu yake uwanjani badala ya kuzungumza au kutaka kujisifia yeye mwenyewe.
Mkali huyo ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Simba tangu atue katika klabu hiyo akionyesha makali yake kwenye mechi za kirafiki na hata kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kutoa pasi za mwisho kwa Amisi Tambwe.
Mombeki, alisema kama mchezaji anajua majukumu yake ni kucheza kwa bidii ili mwishowe Simba imalize vyema ligi hiyo.
Mchezaji huyo mpaka sasa ametupia bao moja tu kimiani, huku mchezaji ambaye amekuwa akimpa pasi za mwishjo, Tambwe akiwa na mabao saba akiwa ndiye kinara wa mabao mpaka sasa.

Thursday, October 3, 2013

Athuman Machuppa ampongeza na kumuonya Amisi Tambwe

Athuman Idd Machuppa akishangilia moja yha mabao yake alipokuwa akiichezae Vasalund ya Sweden

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Athuman Machuppa amempongeza mfungaji mpya wa klabu hiyo Amisi Tambwe huku akimuonya ajipange zaidi ili asiye 'akafulia'.
Machuppa aliliambia MICHARAZO akiwa nchini Sweden kwamba japo hajamuona Tambwe akiwajibika uwanjani, lakini kwa sifa anazozisikia kuhusu mshambuliaji huyo Mrundi bila ya shaka ni 'bonge la Strika'.
Alisema kuanza kufumania nyavu mfululizo ni mwanzo mzuri kwa nyota huyo na kudai huenda anaisaidia Simba kurejesha heshima yake iwapo kama ataendelea kufunga.
Hata hivyo alisema kwa anavyoitambua Ligi ya Tanzania ni vyema mkali huyo akajipanga ili asije akaishia njiani kakma ilivyomtokea Mrundi mwenzake anayeichezea Yanga, Didier Kavumbagu.
"Kwa jinsi ninavyosikia simulizi zake ni wazi ni mmaliziaji mzuri na ataisaidia sana Simba na kwa kuanza kwake vyema na kuizoea mapema ligi ya Tanzania nampongeza na kumtaka aendeleze moto huo huo," alisema.
Machuppa aliongeza hata hivyo Tambwe hapaswi kulewa sifa  anazopewa na badala yake aongeze kasi ili aendelea kutamba na kuwapa raha wana Msimbazi sambamba na kutimiza ndoto zake za kuwa Mfungaji Bora.
"Unajua soka la Bongo halitabiriki, hata Kavumbagu alianza kwa kasi hiyo hiyo lakini mwisho wake umekuwaje, hivyo namsihi Tambwe asilewe sifa badala yake alinde kiwango chake kwa vile ligi ni ngumu," alisema.
Machuppa aliyemaliza mkataba wake wa kuichezea Vasby Utd inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ya Sweden akitokea Vasalund pia ya nchini humo, alisema hata mashabiki wa Simba wanapaswa kumsaidia Tambwe.
Juu ya kitendo cha Tambwe kufunga mabao manne katika mechi moja, Machuppa alisifu ni jambo zuri linalovutia, ila hapaswi kupambwa kama ni kitu cha ajabu sana, wakati wapo wabongo waliowahi kufanya hivyo na pia kuna vijana wenye makali zaidi yake ila hawaaminiwi na makocha wao.
Kadhalika Machuppa alidokeza kusudio lake la kutaka kubadilisha uraia ili awe raia wa Sweden, akidai kwa sasa anasikilizia maombi yake aliyoomba Idara ya Uhamiaji wa nchi hiyo akitaka kufuata nyayo za Shekhan Rashid nyota mwingine wa Tanzania aliyewahi kutamba Simba na Taifa Stars.

Maskini Niyonzima! Umeme wamtia hasara kwa kuunguliwa na vitu nyumbani kwake Magomeni Kondoa

Baadhi ya vitu vilivyoungua ndani ya nyumba ya Haruna Niyonzima wa klabu ya Yanga.
Hii ndiyo nyumba ya kiungo mahiri wa Yanga, Haruna Niyonzima iliyoshika moto baada ya hitilafu ya umeme.
Nyumba anayoishi Haruna Niyonzima ambayo ilipatwa hitilafu ya umeme na kuuguza baadhi ya vitu kabla moto huo kuzimwa usilete madhara zaidi. Tukio hilo limetokea leo asubuhi jijini Dar.
Baadhi ya samani za nyota huyo wa Kinyarwanda vilivyoungua kutokana na moto huo uliozuka asubuhi na kuwahiwa.

Haruna Niyonzima akiwa nje ya nyumba yake hiyo.
Kiungo Haruna Niyonzima akiwa nje ya nyumba yake iliyonusurika kuteketea kwa moto uliozuka ghafla majira ya asubuhi ya leo.
NYOTA wa klabu ya Yanga, Haruna Niyonzima asubuhoi ya leo ameunguliwa nyumba yake iliyopo Magomeni Kondoa kwa kile kilichoelezwa hitilafu ya umeme ambapo baadhi ya mali zake ziliungua kabla ya kuokolewa.
Inaelezwa kuwa moto huo ulizuka wakati wakiwa wamelala na kwa bahati mfanyakazi wake wa ndani alikuwa ameshamka na kuona tukio kabla ya kutoa taarifa na kufanyika juhudi za kuuzima moto huo ulioungua masofa na samani nyingine za mwanandinga huyo.
Hata hivyo ni heri hakukuwa na madhara yoyote kwa wakazi wa nyuma hiyo zaidi ya mali zilizoungua ambazo hata hivyo bado hazijafahamika thamani yake.

Mamlaka ya viwanja vya ndege (TAA) yajitosa bonanza la nyota wa Simba na Yanga Kisarawe


MAMLAKA ya viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imejitosa kudhamini Bonanza la Soka litakalowahusisha nyota wa zamani wa klabu za Simba na Yanga litakalofanyika kesho (jumamosi) wilayani Kisarawe Pwani.
Bonanza hilo lililoandaliwa na klabu ya Kisarawe Veterani, linatarajiwa kufanyika Oktoba 5 kwenbye uwanja wa Bomani likishirikisha klabu 10 toka mkoa wa Dar na Pwani.
Mratibu wa bonanza hilo kutoka kampuni ya Mdau Entertainment, Mohammed Masenga alisema mamlaka hiyo imekubali kuwadhamini ili kufanikisha michezo hiyo ambayo itawakutanisha wachezaji waliowahi kutamba katika soka nchini.
Masenga, alisema kujitokeza kwa mamlaka hiyo ni faraja kwao kwa vile ni nadra kuziona taasisi za serikali zikijitokeza kusaidia michezo kama hiyo ya maveterani.
Aliongeza kuwa wanaishukuru mamlaka hiyo na kutaka taasisi nyingine za kiserikali kuiga mfano huo.
Kuhusu bonanza hilo, Masenga alisema maandaliai yake yanaendelea vyema na kwamba kivumbi kitatimka jumamosi kwa kuwashuhudia nyota hao wa zamani wa Simba na Yanga wanazozichezea timu shiriki za veterani.
Masenga alisema timu shiriki zitakazochuana katika bonanza hilo ni pamoja na Majohe Veterani, Pugu Veterani, Kigogo Veterani, Ukonga, Segerea ya akina Spear Mbwebwe na Willy Martin 'Gari Kubwa', Mbagala ya akina Yusuph Macho 'Musso', Kinyerezi Veterani, Bandari ya akina Kennedy Mwaisabula na Yobo.
Nyingine ni Vituka, New Ukonga na wenyeji Kisarawe Veterani na mshindi wa kwanza atanyakua seti nzima ya jezi, huku wa pili ataambulia 'bips' na wa tatu kubeba mpira mmoja.

Beki Simba achekelea ushindani wa namba Msimbazi

Adeyum Saleh Ahmed
BEKI mpya wa klabu ya Simba Adeyum Saleh amekiri kuna ushindani mkubwa wa namba katika kikosi cha vinara hao wa Ligi Kuu ya Vodacom, lakini akidai anafurahia hali hiyo akiamini itasaidia kuinua kiwango chake na cha timu nzima.
Aidha beki huyo aliyesajiliwa Simba akitokea Miembeni ya Zanzibar, anasema Ligi Kuu ya Tanzania Bara ni ngumu na yenye ushindani huku wachezaji wake wakicheza kwa malengo kuliko ilivyo Ligi Kuu ya visiwani Zanzibar alitokea.
Akizungumza na MICHARAZO kwenye mahojiano maalum, Adeyum aliyewahi kuzichezea Malindi, Mafunzo na Oljoro JKT, alisema ndani ya Simba hakuna mchezaji wenye uhakika wa namba mpaka sasa kutokana na ushindani uliopo kitu kinachowafanya wachezaji wote kujifua vilivyo ili kuwavutia makocha.
"Hivi ndivyo inavyotakiwa kwa timu yoyote, kadri ushindani unapokuwa mkubwa ndivyo wachezaji wanaimarisha viwango vyao, naamini hata mimi kiwango changu kitapanda zaidi na kutimiza ndoto nilizojiwekea," alisema.
Beki huyo wa kushoto alisema moja ya ndoto zake ni kucheza soka la kulipwa nje ya nchi pamoja na kutamani aje kuitwa kuichezea timu ya taifa (Taifa Stars) kwani hajaridhika na kuichezea Zanzibar Heroes tu.
Pia mkali huyo aliyewavutia makocha na mashabiki mara alipojitokeza kwenye majaribio ya timu hiyo alisema Ligi ya Tanzania Bara ni tofauti kiushindani na ile ya visiwani Zanzibar.
Alisema Ligi ya Bara ni ngumu na wachezaji wanacheza kwa malengo kitu ambacho anatamani nyota wa visiwani wangepata fursa ya kuja kuicheza ligi hiyo ili kukuza viwango vyao na kuisaidia timu ya taifa ya visiwa hivyo.
Adeyum anayeisaidia timu ya taifa ya Zanzibar, kunyakua nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Chalenji ya mwaka jana, alisema ugumu wa ligi hiyo unafanya awe mgumu kutabiri itakavyokuwa mbeleni japo anatamani kuibebesha Simba taji la ligi la Vodacom.