STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 11, 2014

SUAREZ, PELLEGRINI WASHINDA TUZO ZA MWEZI.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu nchini Uingereza huku meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini akitajwa kama kocha bora wa mwezi. Suarez ambaye anakipiga katika klabu ya Liverpool alianza mwezi vibaya baada ya timu hiyo kukubali vipigo kutoka kwa Hull City, Manchester City na Chelsea lakini alionyesha kiwango cha juu baadae kwa kufunga mabao 10 katika mechi nne pekee. 


Mabao hayo alifunga katika mechi dhidi ya Norwich City ambapo alifunga manne, West Ham United mabao mawili, Totehham Hotaspurs mabao mawili na mengine mawili katika mchezo dhidi ya Cardiff City. Mabao hayo yaliisaidia Liverpool kushika usukani wa ligi katika kipindi cha Christmas iangwa baadae waliteleza mpaka nafasi ya tano katika kipindi cha mwaka mpya. Naye Pellegrini mwezi Desemba ulikuwa mzuri kwake baada ya kushinda mechi zote sita kati ya saba walizocheza huku mmoja wakitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.

YANGA YAANZA KAMBI VEMA KWA KUICHAPA 3-0 ANKARA SEKERSPOR

Kikosi cha Young Africans kilichoanza leo dhidi ya Ankara Sekerspor
Young Africans imeanza vizuri katika kambi yake ya mafunzo nchini Uturuki baada ya kuifunga timu ya Ankara Sekerspor kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika pembeni kidogo ya eneo ililofikia katika mji wa Manavgat Antalya.

Kocha wa Young Africans aliwatumia wachezaji 18 jumla katika mchezo huo ambao wenyeji mara baada ya mchezo walimpongeza kwa timu yake kwa kucheza vizuri katika mchezo huo wa kirafiki.
Dakika ya 10 ya mchezo shuti lililopigwa na mganda Emmanuel Okwi lilishinda mlinda mlango wa Ankara Sekerspor ambapo aliutema mpira huo na kumkuta Didier Kavumbagu aliyeukwamisha mpira huo wavuni na kuhesabu bao la kwanza.

Timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamu na mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Ankara Sekerspor i0 - 1 Young Africans .
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na iliwachukua dakika moja Young Africans kujipatia bao la pili la mchezo kupitia kwa Emmanuel Okwi aliyeitumia vyema pasi ya mwisho ya kiungo Mrisho Ngasa aliywatoka walinzi wa Ankara Sekaspor na kumpasia mfungaji ambaye hakufanya makosa na kuukwamisha mpira wavuni.
Dakika ya 58 kocha Mkwasa alifanya mabadiliko, ambapo waliingia Hamis Kizza na Nizar Khalfani kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu na kiungo Hassan Dilunga.

Hamis Kizza aliipatia Young Africans bao tatu la mchezo na la ushindi dakika ya 61 ya mchezo baada mpira aliogongewa na Domayo kuwapita walinzi wa Ankara Sekerspor na kumkuta Kizza ambaye alipiga shuti liliomgonga mlinzi wa Ankara Sekerspor wakati akiokoa na kujaa wavuni.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Ankara Sekerspor 0 -3 Young Africans.
Mara baada ya mchezo kaimu kocha mkuu wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa alisema anashukuru vijana wake walicheza vizuri kwa kufuata malekezo na ndio maana wakaweza kupata ushindi huo,makosa yapo machache yaliyojitokeza na ataendelea kuyafanyia kazi.

"Mechi ilikua ni nzuri ukizingatia ndo mchezo wetu wa kwanza wa kirafiki tukiwa na siku ya tatu tangu tufike hapa Uturuki, kwa mazoezi ya jana vijana wameosha mabadiliko na leo wameweza kucheza vizuri na kuweza kupata ushindi, kikubwa naamini kwa siku zilizobakia nitaendelea kufanya marekebisho na kukifanya kikosi kuendelea kuwa bora pindi kitaporejea nchini tayari kwa mzunguko wa pili wa Lig Kuu ya Vodacom" alisema Mkwasa 

Kikosi cha Young Africans kilichocheza leo ni:
1.Juma Kaseja/Ally Mustafa "Barthez" (dk65), 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua/David Luhende(dk 82), 4.Mbuyu Twite (C), 5.Kelvin Yondani, 6.Frank Domayo/Ibrahim Job(dkk 80), 7.Haruna Niyonzima/Saimon Msuva (dk72), 8.Hassan Dilunga/Nizar Khalfan (dk58), 9.Didier Kavumbagu/Hamis Kizza (dk58), 10.Mrisho Ngasa/Jerson Tegete (dk 68), 11. Emmanuel Okwi/Said Bahanuzi (dk 85)

Chelsea yaiengua Arsenal kileleni

 Eden Hazard scores for Chelsea
MABAO mawili moja kutoka kwa Ezen Hazard na jingine la Fernando Torres 'El Nino' yameiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini na kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa muda.
Chelsea ilipata ushindi huo dhidi ya Hull City kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Kingstons Communication na kuifanya kufikisha pointi 46, moja zaidi ya Arsenal ambao watashuka dimbani keshokutwa.
Hazard alifunga bao la kwanza dakika ya 56 akimalizia kazi nzuri ya Ashley Cole kabla ya Torres kuongeza la pili dakika ya 87 na kuwakatisha tamaa wenyeji.
Jioni hii kuna mechi nyingine zinazoendelea katika ligi hiyo na baadaye Manchester United itaikaribisha Swansea City waliowatoa nishai kwenye michuano ya Kombe la FA katika dimba hilo hilo.

Simba yavunja mwiko, Kiemba we acha tu

 
AMRI Kiemba amezidi kudhihirisha kuwa yupo kikazi zaidi kama alivyopwahi kunukuliwa na Blogu hii baada ya usiku wa jana kuhusika na mabao mawili yaliyotosha kuvunja mwiko wa URA wa kutofungwa na Simba kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi.
Kiemba, alitengeneza bao la kwanza lililofungwa na beki Joseph Owino kabla ya kuongeza jingine na kuipa Simba ushindi wa mabao 2-0 na kuivusha hadi Fainali ya michuano hiyo.
Mabao yote mawili yalifungwa kwenye kipi8ndi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kuisha timu zikiwa hazijafungana na URA wakicheza punguyfu baada ya nyota wao Oweni Kasule kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Ramadhani Singano 'Messi'.
Kwa ushindi huo asmbao umeifanya Simba kuweka rekodi kwa kuondoa uteja kwa URAnma kutinga Fainali bila kupoteza mchezo zozote wala kufungwa bao lolote katika lango lao, limeifanya Simba sasa kukutana na KCC ya Uganda iliwatemesha taji waliokuwa watetezi, Azam.
Azam walikumbana na lkipindi cha mabao 3-2 katika mechi ya kwanza iliyochezwa jioni kwenye dimba la Amaan licha ya kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1, mabaoi yake yakiwekwa kimiani na kinda, Joseph Kimwaga.
Fainali ya michuano hiyo itachezwa Jumatatu kwenye uwanja huo wa Amaan.

Friday, January 10, 2014

Hapatoshi Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi leo

Kikisi cha Simba kitakachovaana na URA

Watetezi Azam watakaovaana na KCC

LEO ni kimbembe katika Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi wakati Azam itavaana na KCC ya Ungada wakati Simba ikishuka dimbani usiku kuivaa URA.
URA imekuwa ikiionea Simba kila wanapokutana nao kwa muda mrefu sasa iwe kwenye mashindano au mechi za kirafiki na kufanya mechi hiyo kuwa yenye mvuto zaidi kuliko ya KCC na watetezi Azam.
Hata hivyo mechi zote zinaonekana kusisimua kutokana na ukweli inazikutanisha timu za Tanzania na Uganda ambazo timu zao za taifa zimekuwa zina upinzani katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Simba ilitinga nusu fainali baada ya kuibamiza mabao 2-0 timu ngumu ya Chuoni FC ya Unguja katika mchezo wa robo fainali uliopigwa kwenye Uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia jana na URA URA ikifuzu baada ya kuifunga KMKM bao 1-0 kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba juzi.
Azam ambayo haijapoteza mchezo wowote katika michuano hiyo mpaka sasa itataka kuitoa nishai KCC ili kuweza kutinga fainali na kusubiri kuona itaumana na nani Jumapili kutetea taji lake.
Simba wenyewe itawavaa URA ikimtegemea nyota wake Ramadhani Singano 'Messi' na wakati wengine walioipaisha timu hiyo kwenye michuano hiyo.
Messi alifunga mabao mawili katika mechi ya robo fainali na kuibuka mchezaji bora wa michuano hiyo, japo Mrundi Amissi Tambwe ameling'ang'ania moja ya mabao hayo akidai alifunga yeye.
Makocha wa timu zote nne zilizotinga nusu fainali wamenukuliwa visiwani humo wakitamba kuwa wapo tayari kwa vita ili kuona vikosi vyao vikitinga fainali na hatimaye kunyakua taji hilo.
Tangu michuano hiyo ilipoanzishwa, hakuna klabu kutoka nje ya Tanzania imefanikiwa kutwaa taji hilo na hivyo Simba na Azam kuwa na mtihani wa kuhakikisha zinakutana tena zenyewe kwa zenyewe kulinda rekodi.

Yaya Toure atwaa tena tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika


KIUNGO nyota wa klabu ya Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya Toure ametawazwa kwa mwaka wa tatu mfululizo kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika.
Yaya aliwashinda Mnigeria John Obi Mikel aliyeshika nafasi ya pili na Didier Drogba.
Toure, aliyeshinda tuzo hiyo mwaka 2011 na 2012, alipata kura 373 dhidi ya 265 na 236 za Mikel na Drogba waliomfuatia.
Sherehe za utoaji tuzo hiyo na nyingine zilihudhuriwa na Maofisa mbalimbali wakiwemo Rais wa CAF, Issa Hayatou, Gavana wa Lagos, Babatunde Fashola Raji Fashola, Waziri wa Vijana na Michezo Nigeria, Alhaji Bolaji Abdullah, Wajumbe wa Kamati Kuu ya CAF na wengineo.
Kwa tuzo ya mchezaji bora anayecheza Afrika, ilienda kwa kiungo wa Misri, Mohamed Aboutrika aliwashinda  Ahmed Fathy  wa Misiri na Sunday Mba wa Nigeria.
Hiyo ilikuwa mara ya nne, Aboutrika, aliyetangaza   kustaafu soka hivi karibuni kushinda tuzo hiyo akifanya hivyo mwaka 2006, 2008 na 2012.

TUZO ZA CAF ZILIZOTOLEWA JANA:

Mchezaji Bora wa mwaka; Yaya Toure, Ivory Coast na Manchester City
Mchezaji bora wa mwaka anayecheza Afrika; Mohamed Aboutrika, Misri na Al-Ahly
Mwanasoka anayechipukia; Kelechi Iheanacho (Nigeria)
Timu bora ya mwaka; Nigeria
Timu bora ya vijana ya mwaka; Nigeria U-17 klabu bora ya mwaka; Al-Ahly (Misri)
Kocha bora wa mwaka; Stephen Keshi (Nigeria)
Refa bora wa mwaka; Haimoudi Djamel (Algeria)
Tuzo ya mchezo wa kiungwana; Mashabiki wa Nigeria
Magwiji wa CAF; Bruno Metsu, Mehdi Faria
Tuzo ya Platinum; Goodluck Jonathan (Rais wa Nigeria)
11 bora wa kuunda kombaini ya Afrika;
Kipa: Vincent Enyeama (Nigeria)
Mabeki: Ahmed Fathy (Misri), Mehdi Benatia (Morocco), Kevin Constant (Guinea)
Viungo: Jonathan Pitroipa (Burkina Faso), John Obi Mikel (Nigeria), Yaya Toure (Ivory Coast), Mohamed Aboutreika (Misri)
Washambuliaji: Emmanuel Emenike (Nigeria), Asamoah Gyan (Ghana) na Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon).

Mara baada ya kupokea tuzo yake Yaya amewashuku kaka zake,Obi Mikel na Drogba.

Thursday, January 9, 2014

Kiemba yupo kikazi zaidi Msimbazi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEps_zFlpFfrIRTHTU257hsjXqtA3uCzF1EGsUAwBerMzrMu3p71BRHrvT_PAW8jmgbx_rRosYweFvnR2QgN-fg9FuvtsrJH864KdBbmabBo26I2G3mMzDW-LOY6-JuP35XAxWAxMRf5Q/s640/AMRIKIEMBASIMBA.jpg
Amri Kiemba kishangilia moja ya mabao yake
 KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Amri Kiemba, amesema kwa sasa hana muda wa kupiga blabla kwenye vyombo vya habari na badala yake anaelekeza ngumu na kuwaonyesha mashabiki wa kandanda kipi anachokifanya uwanjani.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu toka Zanzibar, Kiemba alisema anaamini wote ambao walikuwa na maoni tofauti dhidi yake watakuwa wamepata salama kutokana na kile anachokifanya.
Kiemba alisema kutokana na hilo kwa sasa ameamua kufunga mdomo wake kuzungumza lolote badala yake kufanya kazi kwa manufaa ya klabu yake.
"Dah kwa sasa nimeamua kukaa kimya ili nifanye kazi, naamini hivi ndivyo inavyotakiwa ili kuwafanya watu wapime kazi yangu uwanjani na siyo kwenye vyombo vya habari," alisema Kiemba.
Mchezaji huyo ambaye magoli yake mawili aliyoyafunga kwenye mechi mbili tofauti yaliisaidia Simba kuvuka hatua ya robo fainali ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar.
Kiemba alifunga bao la kwanza wakati Simba ikiilaza AFC Leopards katika mechi ya kwanza ya kundi B kabla ya kuifunga pia KMKM ya Zanzibar.
Nyota huyo wa zamani wa Kagera Sugar, Yanga, Miembeni na Moro United, alikuwa katika hatihati msimu huu kuondoka Simba kabla ya kupewa mkataba wa miaka miwili baada ya kuzima uvumi alikuwa akielekea Yanga.
Klabu hiyo ya Simba jana ilifanikiwa kuinyuka Chuoni katika mechi yao ya Robo Fainali ya Mapinduzi kwa mabao 2-0 na sasa wanakutana na timu inayowasumbua kwa muda mrefu ya URA toka Uganda.
Simba kwa miaka zaidi ya miwili ikikutana na URA imekuwa ikitepeta, japo ukali wa kocha Zdrakov Logarusic na msaidizi wake, Suleiman Matola wanatoa matumaini ya kupata dawa ya kuizima URA kab la ya kujua itavaana na nani kati ya Azam na KCC ya Uganda.

Tom Olaba akimwagia sifa kikosi cha Ruvu Shooting

http://images.supersport.com/AFC-Tom-Olaba-300.jpg
Tom Olaba

KOCHA Mpya wa klabu ya Ruvu Shooting, Mkenya Tom Olaba amekimwagia sifa kikosi cha timu yake akidai kina wachezaji wenye vipaji na uwezo mkubwa wa soka na kudai wanampa imani ya kufanya nao vema katika Ligi Kuu.
Aidha kocha huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, alisema amebaini udhaifu wa aina tatu katika kikosi hicho na kueleza ameanza kurekebisha ili kuwahi pambano lao la kwanza la duru la pili la Ligi Kuu dhidi ya Prisons.
Akizungumza na MICHARAZO, Olaba aliyetua Ruvu Shooting kuziba nafasi ya kocha Charles Boniface aliyehamia Yanga, alisema kwa siku chache tangu aanze kukinoa kikosi chake amebaini kimejaliwa 'vijana wa kazi'.
Olaba alisema asilimia kubwa ya wachezaji wa timu hiyo wana vipaji na uwezo mkubwa wa soka kitu kinachomtia moyo kwamba watafanya kazi kwa ufanisi na kuipaisha Ruvu kwenye duru la pili la ligi kuu.
"Kwa kweli ndiyo kwanza nina siku kama tata au nne tangu nianze kuinoa timu yangu, nimebaini vipaji na vijana wenye uwezo wa soka kitu kinachonitia moyo na kuamini tutafanya kazi vyema," alisema.
Olaba alisema pamoja na vipaji na uwezo wa kisoka, amebaini mapungufu matatu katika kikosi hicho na tayari ameanza kuyafanyia kazi kuyarekebisha.
"Wachezaji hawana uwezo wa kukaa na mipira, kutoa pasi na kunyang'anya mipira, kitu ambacho nimeanza kufanyia kazi mapema ili hata tukienda Mbeya kuvaana na Prisons tuwe tumekamilika, ila nimevutiwa na aina ya wachezaji walipo Ruvu kwani wanajua soka na wana vipaji," alisema.
Ruvu Shooting iliyomaliza duru la kwanza ikiwa kwenye nafasi ya saba kwa kujikusanyia pointi 17 kutokana na mechi 13, imemnyakua Olaba kwa mkataba wa muda mfupi wa miezi sita kwa ajili ya mechi za duru la pili.

TASWA kuchaguana Februari 16

KATIBU wa TASWA, Amir Mhando 'Mgosi'
UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), utafanyika Februari 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam. 
Uamuzi huo ulifikiwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya TASWA kilichofanyika Dar es Salaam jana kujadili masuala mbalimbali ya chama na waandishi wa habari za michezo kwa ujumla. 
Kikao kilikubaliana kuwa uchaguzi ufanyike kwa katiba ya zamani, kwani mchakato wa katiba mpya unaweza kuchukua muda mrefu, hivyo kusababisha viongozi waliopo madarakani kuendelea kukalia viti kinyume cha katiba, jambo ambalo si sahihi. 
Kutokana na hali hiyo viongozi wapya watakaochaguliwa moja ya kazi yao kubwa itakuwa kuifanyia marekebisho makubwa katiba ya chama chetu ili iende na wakati. 
Fomu za kuwania uongozi zitaanza kutolewa Februari 10 hadi Februari 14 mwaka huu saa kumi alasiri, masuala mengine yahusiyo uchaguzi huo, ikiwemo mahali utakapofanyika yatatangazwa baada ya kikao cha sekretarieti ya TASWA na Kamati ya Uchaguzi kitakachofanyika Februari 3.

Jennifer Mgendi aachia video mpya iitwayo 'Hongera Yesu'

MUIMBAJI nyota wa muziki wa nyimbo za Injili, Jennifer Mgendi ameibuka na albamu mpya ya video iitwayo 'Hongera Yesu' yenye nyimbo saba.
Akizungumza MICHARAZO, Mgendi alisema kuwa albamu hiyo tayari imeshatua madukani na aliwataka wapenzi wa muziki huo kutonunua CD 'feki' kwani kufanya hivyo kunawavunja moyo wasanii.
Video hiyo mpya mbali na kibao cha 'Hongera Yesu' kilichobeba jina la albamu, pia ina nyimbo kama 'Nikufanyie Nini?', 'Kikulacho', 'Mimi ni Wako', 'Baraka Zangu', 'Fumbua Macho' na 'Msimamo'.
Katika nyimbo za albamu hiyo Mgendi amewashirikisha nyota wengine wa muziki wa Injili kama Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Christina Matai na Martha Ramadhani.
Mbali na kutoa video, Mgendi pia ametoa albamu ya audio ya vibao hivyo, ambayo nayo tayari iko madukani.
Muimbaji huyo amewahi kutamba na albamu kadhaa zilizomtangaza vyema kwenye ulimwengu wa muziki wa miondoko hiyo ikiwamo ile ya 'Mchimba Mashimo' iliyokuwa na nyimbo kama 'Moyo Tulia', 'Nalia', 'Baba ni Wakuaminiwa', 'Niongoze Safarini' na 'Rudi Nyumbani'.
Aidha, Mgendi alisema kuwa mwaka huu anatarajia pia kuzindua filamu yake mpya ambayo hata hivyo hakupenda kuitaja jina kwa sasa kwavile bado ni mapema.

Steve Nyerere aomba kukutana na serikali, wasambazaji


MWENYEKITI mpya wa Bongo Movie Unity, Steven Mengele 'Steve Nyerere' ameiangukia serikali akiomba kukutana nao pamoja na wasambazaji wa kazi za wasanii ili kujadili mambo mbalimbali yanayowakabili.
Steve Nyerere alisema kwa muda mrefu wasanii wamekuwa wakinyonywa jasho lao na yeye kama kiongozi mwenye dhamana wa kuwasaidia wasanii wenzake ameona ni vyema kukutana na serikali na wasambazaji kuweka mambo sawa.
Alisema wasanii wamekuwa wakinyonywa katika jasho lao, na kumekuwa na juhudi kubwa za kuwasaidian wasanii, lakini bila mafanikio hivyo anaamini mkutano wake na serikali na wasambazaji utaleta jibu zuri.
"Baada ya kuchaguliwa na wasanii wenzangu, nimepanga kuanza kuomba kukutana na serikali na wasambazaji ili kuweza kumaliza kilio cha muda mrefu cha unyonyaji wanaofanyiwa wasanii," alisema.
Steve aliyechaguliwa mwishoni mwa wiki katika uchaguzi mkuu wa umoja huo, alisema ni Tanzania pekee ambayo msanii na mtayarishaji ndani ya mwaka anaweza kutengenezea filamu kuanzia 6 mpaka zaidi ya 10.
"Duniani kote mtayarishaji anaweza kutengeneza filamu kati ya moja mpaka mbili, lakini hapa msanii mmoja anazalisha filamu zaidi ya 10 kwa mwezi na kuuza kazi hiyo kati ya Sh. milioni 10-20, huu ni wizi," alisema.
Alisema ni vyema msanii akaweza kutengeneza filamu angalau moja kwa mwaka na kuiuza pengine hata kwa Sh. milioni 200 kuliko mtindo wa sasa ambao unawanufaisha wasambazaji wanaouziwa 'master' na kuzalisha filamu maradufu tofauti na fedha walizonunulia kazi hizo.
Alisema Tanzania ina watu zaidi ya milioni 40, lakini alisema kwa mauzo ya hata nakala 10,000 tu kwa bei ya Sh.5,000 kwa nakala, muuzaji anapata Sh. milioni 50 hivyo si sawa kuwapa wasanii waliotoka jasho Sh. milioni 10 wakagawane.
Mwenyekiti huyo aliyechukua nafasi ya Vincent Kigosi 'Ray' aliyekuwa akiiongoza Bongo Movie kabla ya uchaguzi huo, alisema anaamini serikali ikiweka mikakati mizuri kuwabana wasambazaji wasanii watanufaika na kulipa kodi itakayosaidia kuleta maendeleo ya nchi kuliko ilivyo sasa.