STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 18, 2014

Burundi yafufua matumaini michuano ya CHAN 2014

http://www.yeswefoot.com/medias/burundi-team.jpg
Burundi
WAWAKILISHI wa CECAFA katika michuano ya CHAN 2014 inayoendelea Afrika Kusini, Burundi imefufua matumaini yake ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo baada ya muda mfupi uliopita kuicharaza Mauritania kwa mabao 3-2 na kuongoza kwenye msimamo wa kundi lao la D.
Ely Ould Voulany aliishtukiza Burundi kwa kuifungia Mauritania bao dakika ya pili ya mchezo huo kabla ya Abdoul Razak Fiston kusawazisha katika dakika ya 11 kutokana na kazi nzuri ya Suleiman Ndikumana, ambaye alifunga pia bao dakika ya 25 lakini lilikataliwa na mwamuzi na kuzifanya timu ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa ya kufungana bao 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa Burundi kupata bao la pili lililofungwa na Nduwarugira katika dakika ya 61 akitengeneza pande na Fiston kabla ya Mauritania kusawazisha dakika ya 70 kupitia Demma kabla ya Ndikumana kufunga bao la ushindi dakika za nyongeza za pambano hilo na kuifanya Burundi kuiengua Gabon kileleni licha ya kulingana nao pointi nne ila wanatofautiana mabao ya kufungwa na kufungwa.
Kipigo hicho cha Burundi limeifanya Mauritania kuwa timu ya tatu kuaga mashindano hayo ikiungana na timu za Msumbiji na Ethiopia zilizotangulia mapema katika makundi yao.
Kesho mechi za lala salama za raundi ya tatu ya makundi hayo zitaanza kwa Nigeria kuvaana na wenyeji wao Afrika Kusini katika pambano la kundi A na Msumbiji kuvaana na Mali, mechi zote zikichezwa wakati mmoja majira ya saa 2 usiku.

Abdi Kassim 'Babi' katika uzi wa UiTM ya Malaysia

Abdi Kassim 'Babi' (kulia-mbele) akiwa na wachezaji wenzake wa UiTM ya Malaysia, kiungo huyo mshambuliaji ametua katika timu hiyo mwishoni mwa mwaka jana kwa mkataba wa mwaka moja na tayari ameshaana kuonyesha makeke kwa kuifungia mabao kwenye mechi za kirafiki kujaindaa na Ligi kuu ya nchi hiyo.

Kado achekelea, akiapa kung'ara zaidi duru la pili

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiKEuWViBK1RvB2yszF1PxMhJ9oTDno9k9KRhyphenhyphennGjTRqcXKe0NrFPYNxFI7dlXI-3QjjBAfOVRNac5XEfoN6LD1rlraERS80n6_P6-mFCCORYMcAFnD-PqwN8vj-h31im-AGNf1Pg774b8/s640/shaaban+kado.jpg
Shaaban Kado 'Baba Munira'
KIPA wa kutaminiwa wa klabu ya Coastal Union, Shaaban Kado amesema anajisikia fahari kubwa kuweza kukaa langoni kwa muda wa dakika 1125 na kufungwa idadi ndogo ya mabao katika duru la kwanza la Ligi Kuu Tanzania Bara,. huku akijitabiria kung'ara zaidi katika duru lijalo litakaloanza wikiendi hii.
 
Aidha kipa huyo aliyepo nchini Oman na kikosi cha timu yake kikifanya mazoezi kujiandaa na duru hilo la pili, amekiri duru lililopita lilikuwa lenye ushindani na kutabiria duru lijalo litakuwa gumu zaidi kutokana na usajili wa dirisha dogo na klabu zinavyojiandaa kwa sasa.
 
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya mtandao kutoka Oman, Kado alisema anajisikia fahari kubwa kuona amesimama kwenye milingoti mitatu ya klabu yake kwa mechi zote 13 akitumia dakika 1125 na kuifanya Coastal kuwa timu iliyofungwa idadi ndogo ya mabao katika duru lote la kwanza.
 
Kado alisema alicheza dakika zote 90 katika mechi 12 kabla ya mechi yao na Mbeya City kudaka kwa dakika 45 na kutoka kumpisha Said Lubawa aliyekuja kufungwa bao la kusawazisha la penati la Mbeya.
 
"Kwa kweli najisikia fahari sana kuona nimeidakia Coastal kwenye duru la kwanza karibu mechi zote na kufungwa mabao sita, nadhani duru lijalo kwa mazoezi ninayoendelea kuyafanya huku nitang'ara zaidi na kuipaisha timu yangu kwenye ligi," alisema Kado.
 
Kado alisema ligi ya msimu huu kwa ujumla imeonekana ngumu kutokana na ushindani uliopo na kukiri huenda duru lijalo likawa gumu zaidi kwa sababu timu zimepata nafasi yakupumzika na kurekebisha makosa yao kwa kusajili kwenye dirisha dogo na pia kujiandaa vyema wengine wakienda nje ya nchi.
 
Ukiondoa Coastal waliomaliza duru la kwanza katika nafasi ya nane ikiwa na pointi 16 waliopo Oman, Yanga nao wamejichimbia Uturuki ikifanya mazoezi huku Kagera Sugar yenyewe ikijifua nchini Uganda.

Arsenal, Man City zaua zikifukuzana England

Edin Dezko
Dzeko akitupia bao la kuongoza

Santi Cazorla (centre) scores the opener for Arsenal against Fulham
Arsenal ilipoiadabisha Fulham kwa mabao 2-0

MABAO mawili ya Santiago Cazorla yaalitosha kuiwezesha Arsenal kuendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya England na kujichimbia kileleni, huku wapinzani wao wa karibu Manchester City wakiwapumulia nyuma yao baada ya jioni ya leo kutoa kipiogo kingine kizito kwa wapizani wao kwenye ligi hiyo.
Arsenal iliyokuwa nyumbani iliinyoa timu ya Fulham kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wake wa Emirates yote yakiwekwa kimiani na Cazorla katika kipindi cha pili na kuifanya timu hiyo ifikishe pointi 51 na kujikitga zaidi kileleni.
Timu inayokamata nafasi ya pili, Man City, iliendelea kugawa dozi kwa wapinzani wake ikipata ushindi wa mechi saba mfululizo baada ya kuinyonyoa Cardiff City kwa mabao 4-2 mabao yaliyofungwa na Edin Dzeko, Jesus Navaz, Yaya Toure na Sergio kun Aguero.
Ushindi huo umeifanya City kufikisha pointi 50, moja nyuma ya vinara Arsenal.
Katika mechi nyingine, Newcastle United ilipata ushindi wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya West Ham United, huku Sunderland ikiendelea kuimarika na kutoka mkiani kwa kulazimisha sare ya 2-2 na Southampton, huku Crystal Palace ikikwanyua Stoke City kwa bao 1-0, huku Norwich City ikipata ushindi kama huo mbele ya wageni wao Hull City.
Hivi sasa Liverpool ikiwa nyumbani inapepetana na Aston Villa na matokeo ni sare ya mabao 2-2 baada ya Liverpool kusawazisha hivi punde ikitoka mapumziko ilipokuwa nyuma kwa mabao 2-1.

Coastal yalazimishwa sare na Seeb Oman










Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’, leo wametoka suluhu tasa dhidi ya Seeb SC inayoshiriki ligi kuu ya Oman.
Mechi ya leo ambayo ni ya kirafiki imeisha kwa matokeo ya 0-0 ambayo inakuwa mechi ya nne tangu kuwasili nchini hapa Januari 9, kwa ziara ya wiki mbili kujiandaa na ligi mzunguko wa pili Tanzania Bara.
Coastal Union, imeonyesha uhai katika kipindi cha pili ambapo kipindi cha kwanza walishindwa kuonyesha makeke yao baada ya wachezaji wa Seeb, kujazana katikati hali iliyowafanya Wagosi kushindwa kumiliki mpira.
Aidha, golikipa wa Wagosi, Shaaban Kado alipoiona kasoro hiyo akawa anatumia muda mwingi kupiga mipira katikati kila inapomjia kwa lengo la kuamsha mashambulizi ili viungo wake wachangamke.
Kipindi cha kwanza kiliisha timu zote kizitoka vichwa chini kutokana na kukosa nafasi za kuonyeshana uwezo waliofundishwa na walimu wao.
Kipindi cha pili Seeb Club, walifanya mabadiliko kwa kutoa wachezaji wawili wa ndani na mlinda mlango. Coastal Union waliendelea kucheza bila kufanya mabadiliko.
Katika dakika za awali kipindi cha pili Seeb walionyesha uhai na kulisumbua sana lango la Wagosi, lakini kufuli za Juma Nyoso na Othman Tamim ziliendelea kuwa imara kuulinda mlango wa Shaaban Kado.
Aidha ilipofika dakika ya 76, kocha Yusuf Chipo alifanya mabadiliko ya haraka haraka kwa kutoa wachezaji wane na kuingiza wane ndani ya dakika 15 zilizosalia.
Alianza kutoka Othman Tamim akaingia Abdi Banda, baadae akatoka Danny Lyanga akaingia Mohammed Miraji. Halafu zikiwa zimesalia dakika chache mchezo kuisha alitoka Atupele Green akaingia Suleiman Kassim Selembe, halafu akamalizia mabadiliko kwa kumuingiza Abdullah Othman ‘Ustadh’ akatoka Yayo Kato.
Listi ya leo ilikuwa: Shaaban Kado, Hamadi Juma, Othman Tamim, Juma Said ‘Nyoso’, Mbwana Kibacha, Jerry Santo, Ally Nassor ‘Ufudu’, Danny Lyanga, Atupele Green, Haruna Moshi ‘Boban’, na Yayo Kato.
Coastal Union tangu iwasili Oman imeshacheza mechi nne, imeshinda mechi mbili kati ya Oman Club na Al Mussannah kwa mabao 2-0 kila mechi. Halafu ikafungwa bao 1-0 na Fanja Club, leo imetoka suluhu ya bila kufungana na Seeb Club.
COASTAUNION

Simba yadonyolewa kimoja na Mtibwa Sugar kirafiki

KIKOSI cha vijana wa Msimbazi, Simba jioni ya leo imejikuta ikipokea kipigo cha pili chini ya Kocha Zdravko Logarusic baada ya kukwanyuliwa na Mtibwa Sugar kwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki lililochezwa uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao pekee lililoinyamazisha Simba iliyotoka kupokea kipigo cha b aoa 1-0 toka kwa KCC ya Uganda katika fainali ya Kombe la Mapinduzi liliwekwa kimiani na Masoud Ally ‘Chile’ katika dakika ya 64 akimaliza kazi ya Jamal Mnyate.
Kikosi hicho cha Mtibwa Sugar kesho itashuka tena dimbani kwa kuvaana na AShanti United katika pambano jingine la kujiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza wiki ijayo.

DR Congo wanyukwa kimoja CHAM 2014

http://mtn.ensight-cdn.com/content/RD-Congo-v-Libye-RD-Congo-T~1.jpg
DR Congo
 BAO pekee lililofungwa dakika ya pili na Erwin N'Guema Obame wa Gabon lilitosha kuizima DR Congo katika pambano la Kundi D la michuano ya Kombe la CHAN lililochezwa jioni hii.
N'Guema alifunga bao hilo akimaliza kazi nzuri iliyofanywa na Samson Mbingui na kuifanya timu yake kuibuka na ushindi huo na kuchupa hadi kileleni mwa kundi hilo kwa kufikisha pointi nne baada ya mchez wake wa awali dhidi ya Burundi kumalizika kwa sare pacha ya 0-0.
DR Congo yenyewe imesaliwa na pointi zake tatu ilizopata kwa kuilaza Mauritania ambayo baadaye itavaana na Burundi katika mchezo wa pili wa kundi hilo kuhitimisha mechi za raundi ya pili kwa makundi yote manne kabla ya mzunguko wa tatu kujua timu zitakazotinga robo fainali kufahamika rasmi.
Kwani mpaka sasa hakuna timu hiyo iliyojihakikisha kutinga hatua hiyo kutokana na timu 16 zinazoshiriki michuano hiyo kubanana vilivyo japo nchi mbili za Msumbiji na Ethiopia zenyewe zimeshaaga mashindano kwa kufungashiwa virago baada ya kupoteza mechi zao mbili za awali katika makundi yao.

Wahabeshi kuwahukumu Yanga kwa Wakomoro

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Somalia kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Komorozine Sports ya Comoro.
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya mchujo itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu wakati ile ya marudiano itachezwa kisiwani Comoro kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.


Mwamuzi wa kati atakuwa Hassan Mohamed Hagi wakati wasaidizi wake ni Hamza Hagi Abdi, Bashir Abdi Suleiman na Bashir Olab Arab. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Eugene Musoke kutoka Uganda.

Timu ambazo zimeingia moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa ni Coton Sport ya Cameroon, El Ahly (Misri), TP Mazembe (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), El Hilal (Sudan), Club Sportif Sfaxien (Tunisia) na Esperance (Tunisia)

Nayo mechi ya kwanza ya raundi ya mchujo kati ya Azam ya Tanzania na Ferroviario Da Beira ya Msumbiji itakayofanyika Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu itachezeshwa na waamuzi kutoka Sudan.

Waamuzi hao ni Mutaz Abdelbasit Khairalla atakayepuliza filimbi, Waleed Ahmed Ali, Aarif Hasab Elton na El Fatih Wadeed Khaleel. Kamishna wa mechi hiyo ni Hassan Mohamed Mohamed kutoka Somalia. Mechi ya marudiano itachezwa Msumbiji kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.

Timu zilizotinga moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo ni Asec Mimosas ya Ivory Coast, Ismailia (Misri), Wadi Degla (Misri), Djoliba (Mali), MAS (Morocco), Bayelsa United (Nigeria), El Ahly Shandy (Sudan), E.S.S. (Tunisia), C.A.B. (Tunisia) na Zesco United (Zambia).

Ethiopia yaaga CHAN, Burundi ikijaribu bahati leo

http://www.futaa.com//images/350x300/ethiopia_1.jpg 
WAKATI Ethiopia ikipoteza matumaini ya kutamba kwenye michuano ya CHAN inayoendelea nchini Afrika Kusini baada ya jana kukubali kipigo cha pili, wawakilishi wengine wa CECAFA, Burundi leo itatupa karata yake ya pili kwa kuvaana na Mauritania.
Ethiopia ililala kwa bao 1-0 jana kwa Jamhuri ya Kongo, wakati Libya na Ghana zikishindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 1-1 katika mechi zao za Kundi C zilizochezwa kwenye uwanja wa Free State.
Kwa kipigo hicho Ethiopia ni kama imefungasha virago na inasubiri tu pambano la kukamilisha ratiba kwani hata ikishinda haiwezi kuzivuka pointi ilizonazo timu za Ghana na Libya zenye pointi nne kileleni.
Wakati Ethiopia ikiaga, Burundi leo itashuka dimbani kuumana na Mauritania katika mechi ya kundi D huku  DR Congo ikivaana na Gabon mapema jioni hii.
Katika mechi yao ya kwanza Burundi ililazimishwa suluhu na Gabon, huku DR Congo ikishinda 1-0 dhidi ya Mauritania.
Mpaka sasa mchezaji Bernard Parker wa Bafana Bafana ndiye anayeongoza kwa kufunga mabao matatu akifuatiwa na wachezaji wawili wenye mabao mawili kila mmoja akiwamo Mganda, Yunus Sentamu.
Mataifa yote hayo mawili yalishinda katika michezo yao ya ufunguzi Jumatatu usiku mjini Bloemfontein.
Ushindi kwa yoyote baina yao itakuwa unawapa nafasi ya kusonga mbele katika robo fainali ya michuano hiyo na la muhimu zaidi kumaliza katika nafasi ya juu katika kundi C.
Mshindi wa kwanza wa kundi hili atakutana dhidi ya mshindi wa nafasi ya pili wa kundi D, kundi ambalo linaonekana kama mchekea katika michuano hiyo.

Yanga kuwavaa KS Flamurtari Vlore

MABINGWA wa soka nchini Young Africans leo itashuka dimbani kucheza na timu ya KS Flamurtari Vlore inayoshika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Albania, ikiwa ni sehemu ya mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu kwa timu zote ambao utakaofanyika katika eneo la Side Manavagat.
Huu utakua ni mchezo wa tatu wa Young Africans wa kujipima nguvu dhidi ya timu hiyo ya Ligi Kuu nchini Albani baada ya kuwa imeshacheza michezo miwili na kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Ankara Sekerspor na 2-0 dhidi ya timu ya Altay SK.
Taarifa kupitia mtandao wa klabu hiyo imesema kuwa Kocha mkuu wa klabu hiyo Hans Van Der Plyum ameendelea na mazoezi leo asubuhi na jioni ataendelea na mazoezi pia kuwaandaa vijana wake kuwa tayari kwa mchezo huo, lakini pia kuwaweka tayari kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.
  
Baada ya mchezo dhidi ya timu KS Flamurtari Vlore kesho, Young Africans itakamilisha ziara yake ya kambi ya mafunzo nchini Uturuki kwa kucheza na timu ya Simurq PIK inayoshikri Ligi Kuu nchini Azerbaijan katikati ya wiki ijayo kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini Tanzania. 
Hali ya hewa jijini Manavgat ni nzuri na sio ya baridi kali kiasi kwamba haiwalazimu wachezaji kuwaa vifaa vya michezo vya baridi kwani hali inawaruhusu kuweza kufanya mazoezi na kucheza bila kuwa na mataitzo yoyote.
Mpaka sasa hakuna katika kambi ya klabu ya Young Africans nchini Uturuki hakuna mchezaji yoyote majeruhi isipokuwa kiungo Hassan Dilunga ambaye anasumbuliwa na malaria na tayari anaendelea vizuri baada ya kupatiwa tiba na daktari wa timu Dr. Suphian Juma.

Waamuzi 8 waula michuano ya CAF

WAAMUZI nane wa Tanzania wameteuliwa kuchezesha mechi mbili za marudiano za raundi ya awali za Ligi ya Mabingwa Afrika (CL) na Kombe la Shirikisho (CC) zitakazochezwa wikiendi ya Februari 14 na 16 mwaka huu.

Waamuzi hao walioteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ni Israel Mujuni atakayechezesha mechi ya CL kati ya Rayon Sport ya Rwanda na AC Leopards de Dolisie ya Congo itakayofanyika jijini Kigali.

Mujuni atasaidiwa na Josephat Bulali, Samwel Mpenzu na Ramadhan Ibada, wakati Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Jean Marie Hicuburundi wa Burundi.

Naye Waziri Sheha ataongoza jopo lingine kwenye mechi ya CC kati ya FC MK ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na El Ahly Atbara ya Sudan. Mechi hiyo itachezwa jijini Kinshasa.

Sheha atasaidiwa na Ferdinand Chacha, John Kanyenye na Israel Mujuni. Kamishna wa mechi hiyo ni Chayu Kabalamula kutoka Zambia.

Semina ya kupandisha daraja waamuzi J'4

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-_FZ5LRs-CTRVIXHK_m_6vV8Q1IZ_9ZBWFI-Ko3Z4SpHpeEOfVggBRF2mOT_cdJe_t_V-6Uu1gHzOT37cJMOyTDsa5h6LUHf22Ei-51zTgbJxEySpdogLZaNub5ZiVSb_s4_2fgkMyUU/s640/DSC04815.JPG
Semina kwa ajili ya kupandisha madaraja waamuzi itafanyika Januari 21 na 22 mwaka huu katika vituo vitatu vya Dodoma, Mwanza na Songea.

Waamuzi watakaoshiriki katika semina hizo ambazo pia zitahusisha mitihani ya utimamu wa mwili (physical fitness test) watajigharamia wenyewe na wanatakiwa kufika vituoni siku moja kabla. Waamuzi hao ni wa daraja la pili na tatu.

Kituo cha Dodoma kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, Pwani, Singida na Tanga. Wakufunzi katika kituo hicho ni Paschal Chiganga, Said Nassoro na Soud Abdi.

Wakufunzi wa kituo cha Mwanza kwa ajili ya waamuzi wa mikoa ya Geita, Kagera, Katavi, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Tabora ni Alfred Kishongole, Kanali Issarow Chacha, Saloum Chama na Zahra Mohamed.

Kituo cha Songea ni kwa ajili ya waamuzi kutoka Iringa, Lindi, Mbeya, Mtwara, Njombe, Rukwa na Ruvuma. Wakufunzi katika kituo hicho ni Charles Ndagala, Joseph Mapunda, Riziki Majala na Victor Mwandike.

Waamuzi wote wanatakiwa kwenda katika kituo walichapangiwa. Vilevile wanatakiwa kuwa na barua kutoka kwa makatibu wa Vyama vya Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) wa mikoa yao ikiwatambulisha pamoja na kuonesha madaraja yao.

Friday, January 17, 2014

Huyu ndiye Amri Kiemba; Kiungo asiyechuja Msimbazi

Amri Kiemba akipowatungua Yanga na kutega sikio kusikiliza kelele za mashabiki wa Msimbazi
WAPO wanaoamini kadri umri wa makipa unavyozidi kusonga mbele ndivyo wanavyozidi kuwa mahiri langoni, tofauti na wachezaji wa nafasi nyingine hasa ya kiungo, beki au ushambuliaji.
Hata hivyo, kwa kiungo mshambuliaji Amri Kiemba, ni tofauti, kwani ujuzi wake wa kucheza na mpira na kufumania nyavu unazidi kuongezeka kadri siku zinavyozidi kusonga mbele na kushangaza mashabiki wa soka.
Msimu mmoja uliopita, kiungo huyo alikuwa akionekana siyo lolote ndani ya Simba kiasi cha kufungashiwa virago na kutakiwa kwenda kwa mkopo katika timu ya Polisi Dodoma iliyokuwa ikichechemea katika ligi msimu wa 2011/12.
Hata hivyo, mchezaji huyo akijiamini bado analiweza soka aliamua kuchomoa kwenda Polisi na kukubali kukaa nyumbani kabla ya kurejeshwa tena Msimbazi msimu uliopita na kuonyesha kiwango kikubwa kiasi cha kuwa 'lulu' ndani ya timu ya Taifa, Taifa Stars.
Katika msimu huo uliopita, Kiemba pia alikuwa gumzo kubwa ndani ya Simba, iliyokuwa imemuona amekwisha kwa kuifungia mabao muhimu na kuziba vilivyo pengo lililokuwa limeachwa na nyota wa Kimataifa wa Rwanda mwenye asili ya DR Congo, Patrick Mafisango aliyefariki kwa ajali ya gari.
Kasi yake uwanjani, akili ya kuwatoka mabeki na kufumua mashuti makali yaliyolenga lango la mpinzani na kuipa ushidi Simba na Taifa Stars, ilimfanya Kiemba anyakue tuzo ya Mwanasoka Bora kwa msimu wa 2012/13.
Tuzo hiyo iliyoandaliwa na Chama cha Wanasoka Tanzania (SPUTANZA) ilikuwa kama faraja kwa mchezaji huyo mpole na mcha Mungu kwa jinsi ilivyomfuta machozi kutoka kwenye misukosuko klabuni kwake.
Msimu huu pia mchezaji huyo ameendelea kuonyesha ni moto wa kuotea mbali akiisaidia timu yake kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara duru la kwanza na hata sasa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyotarajiwa kumalizika jana.
Mabao yake mawili, moja dhidi ya AFC Leopards na jingine dhidi ya KMKM yaliisaidia kuivusha Simba hatua ya Robo Fainali kutoka Kundi B kabla ya kufunga jingine na kutengeneza jingine lililoipeleka Wekundu wa Msimbazi kucheza fainali na kulala bao 1-0 kwa KCCA.
Amri Kiemba (kulia) akiitumikia timu ya taifa, Taifa Stars
MKALI
Kiemba aliyewahi kung'ara na Klabu za Kagera Sugar, Moro United, Yanga na Miembeni, licha ya kwamba hana makeke, lakini ni mkali na anayejua majukumu yake uwanjani.
Ingawa amekuwa mkimya na asiyependa kuzungumza na vyombo vya habari, Kiemba anasema siri ya mafanikio yake ni kujituma, kusikiliza makocha na kushirikiana na wenzake mbali na kumtegemea Mungu kwa kila kitu.
Kiemba anayependa kula wali kwa marahage na vinywaji visivyo na kileo, anasema japo amekuwa hapendi kufichua mambo yake hadharani, lakini anashukuru soka kumsaidia kwa mengi na kumuomba Mungu amzidishie umri na kipaji chake aendelee kusakata kandanda.
Nyota huyo, aliyewahi kuzichezea kwa nyakati tofauti timu za taifa kuanzia za vijana U-17 na U-20 kabla ya kuitwa timu ya wakubwa anayoichezea mpaka sasa, anaseme hakuna mechi ngumu aliyowahi kuicheza au kukutana nayo kama ile ya Yanga dhidi ya Esperance ya Tunisia waliposhiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
Anasema anaikumbukwa kwa jinsi wapinzani wao walivyowafunika na ugenini kuwazabua mabao 3-0 kabla ya kutoshana nao nguvu ya kufungana bao 1-1 nyumbani na kung'olewa mashindanoni mwaka 2007.
Kiemba aliyekuwa akicheza soka kama beki wa kati, anasema licha ya kufunga mabao mengi, bao tamu kwake ni lile alililoifungia Kagera Sugar 2004 dhidi ya Polisi iliyosaidia timu yao kupanda Ligi Kuu.
"Nalikumbuka bao lile kwa jinsi nilivyolifunga kiufundi, mbali na kuisaidia kuipandisha Kagera Ligi Kuu msimu wa 2005/2006 tulipowafunga Polisi mabao 3-0," anasema.
Mkali huyo anayependa kutumia muda wake mwingi kusikiliza taarifa mbalimbali za habari kupitia redio na kufanya ibada, anasema soka la Tanzania bado linahitaji mabadiliko makubwa kuweza kufikia kwenye kilele cha mafanikio kwa kuwapo kwa mipango ya kuendeleza vipaji vya vijana.
Kiemba akiwajibika uwanjani kwenye mechi za Ligi Kuu
Kiemba akionyesha manjonjo yake
CHIMBUKO
Kiemba anaitaja Klabu ya Kagera Sugar kama ya mafanikio kwake, huku akiwataja walimu Malume na Kabuta waliomnoa kwenye michezo ya Umishumta na Idd Kipingu aliyempokea Shule ya Sekondari Makongo, kuwa ni watu asiowasahau kwa kukuza kipaji chake.
"Siwezi kuwasahau watu hawa kwa walivyosaidia kukuza na kuendelea soka langu," anasema.
Nyota huyo aliyewaasa wachezaji wenzake kuzingatia miiko na maadili ya uchezaji ili wacheze kwa muda mrefu, alizaliwa mwaka 1983 mjini Kigoma akiwa ni mtoto wa pili kati ya watano wa familia yao iliyokuwa na watoto wa kiume watatu na wa kike wawili.
Alisoma Shule ya Msingi Burka, Arusha alipoanza kuonyesha kipaji chake cha soka akiteuliwa katika timu ya shule na timu za Mkoa wa Arusha kwenye michuano ya Umishumta akishiriki fainali tatu za taifa kuanzia 1997-1999.
Chandimu alicheza katika timu ya Small Tiger na timu yake ya kwanza ya ligi ni Home Boys ya Arusha kabla ya kujiunga Shule ya Makongo alipoteuliwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana ya U-17, wakati akiwa anaichezea pia Karume Rangers.
Aliondoka Karume iliyokuwa na maskani yake Mbeya ikifahamika pia kama 44 KJ na kwenda kwa muda Pallsons ya Arusha, kisha kukimbilia Kagera Sugar aliyosaidia kuipandisha Ligi Kuu mwaka 2005 na kuonwa na Yanga iliyomnyakua msimu wa 2006/2007.
Aliachana na Yanga na kwenda Zanzibar kuichezea Miembeni kwa muda na kurejea Bara kujiunga na Moro United hadi msimu wa 2009/2010 aliponyakuliwa na Simba aliko hadi sasa.
Mafanikio yake kama mchezaji, Kiemba anasema ni kutwaa mataji kadhaa yakiwamo ya Ligi Kuu, Mapinduzi na Tusker akiwa na timu za Simba na Yanga.

AIBU! Wanawake wawili wanaswa na bangi Arusha

GEDSC DIGITAL CAMERA
Mkuu wa kitengo cha kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya Mkoa wa Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Aben Mgode akiwaonyesha waandishi wa habari misokoto 5000 pamoja na baadhi ya magunia 16 ya madawa ya kulevya aina ya bangi yaliyokamatwa kutokana na misako mbalimbali iliyofanyika mkoani hapa. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la
Polisi Arusha)
****
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
WATU saba wakiwemo wanawake wawili wamekamatwa na misokoto 5000 ya madawa ya kulevya aina ya bangi pamoja na mirungi kilo 47. Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Mti mmoja lililopo wilaya ya Monduli.
Mafanikio hayo yalitokana na msako shtukizi uliofanywa na jeshi la polisi Mkoani hapa kuanzia saa 12:00 asubuhi mpaka saa 10:00 jioni baada ya kufanya upekuzi katika magari mbalimbali na kupata madawa hayo ambayo yalikuwa yanasafirishwa na watuhumiwa hao kupitia magari ya abiria yaliyokuwa yakielekea Manyara, Singida, Dodoma na Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas watuhumiwa hao walikuwa wanayahifadhi madawa hayo kwenye mifuko ya “plastic” ili yasitoe harufu na kisha kuweka kwenye mabegi.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Godwina Munisi (31) Mkazi wa Sombetini , Mwajuma Kingu (48) Mkazi wa Mbauda,  Fidelis Joseph (48) Mkazi wa Ngarenaro, Selemani Ally (34) Mkazi wa Olmatejoo, Omari Ally (25) Mkazi wa Babati Mkoani Manyara Kasimu Ayubu (39) Mkazi wa Tarakea Rombo Mkoani Kilimanjaro na Yasini Talian (40) Mkazi wa Ngarenaro.
Kamanda Sabas alisema kwamba watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Wakati huo huo katika msako unaoendelea wilayani Longido, jumla ya magunia 16 ya madawa ya kulevya aina ya bangi yamepatikana katika eneo la kijiji cha Leboo baada ya askari Polisi kufanya msako na kufanikiwa kupata magunia hayo 16 yaliyokuwa yanasafirishwa .
Kamanda Sabas alisema kwamba, askari hao walikuwa wanafanya msako usiku na mara baada ya watuhumiwa hao kugundua kuwa wanafuatiliwa walitelekeza magunia hayo 16 na kukimbia. Inasemekana kwamba watuhumiwa hao walikuwa wanatumia wanyama aina ya Punda kusafirishia madawa hayo ambapo magunia yalikuwa yamefungwa mawili mawili.
Hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoani hapa bado linaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao ili wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Hawa ni baadhi ya wasanii wanaodaiwa kuwa membaz wa Freemasons

Rihanna amekuwa akitajwa kama kinara kwa wasanii wa kike
Jay Z na Kanye West wakisalimiana kwa ishara inayodaiwa ya Freemason

 
CHINI ni baadhi ya wasanii wanaotajwa kujihusisha au waliokuwa waabudu mashetani (Freemason)
 
Tupac Shakur (2Pac) – (Murdered For Trying To Expose Satan)
Ke$ha
Katy Perry
Justin Bieber
Chief Keef
Snoop Dogg
Skrillex (Sonny Moore)
Amy Winehouse – (Blood Sacrifice)
Britney Spears
Jay-Z – (Illuminati Recruit)
Kanye West
Rhianna
Beyonce
Whitney Houston – (Murdered For Trying To Expose Satan)
Miley Cyrus
Billy Ray Cyrus
Nicki Minaj
Carly Rae Jepsen
Lady Gaga
Katy Perry
Michael Jackson – (Murdered For Trying To Expose Stan)
Bob Dylan
Dr. Dre
Eminem
Cypress Hill
David Bowie
Madonna
Lil Wayne
Nas
Notorious B.I.G. – (Murdered For Trying To Expose Satan)
T-Pain
Aayliah
Chris Brown
Rick Ross
P-Diddy
Justin Timberlake – (Illuminati Recruit)
Drake
Wiz Khalifa
Frank Sinatra
Elvis Presley
Bob Marley
Rebecca Black
Pitbull
David Guetta
Adelle
Alicia Keys
Jennifer Lopez
50 Cent
DMX (Ex Member)
Taylor Swift
Demi Lovato