STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Balotelli aandaliwa kuiua Spurs Jumapili

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiaVQQWvCjgmGQoV60H_iQem7DH3sMHClKoS-HrMHiFyPnB5CMmYLIOJJXsYdpV2cLgqx3InxajvilHnHSm7LuExKxBqGyR5yVYYrNIRz2jg_5LTLapESn3zHuiCXdGWTTlVQ7dpsCwwva0/s1600/1409137512960_wps_12_Mario_Balotelli_joins_the.jpg
Balotelli akiwa na wachezaji wenzake wakifanya mazoezi
KOCHA Brendan Rodgers wa Liverpool ameweka bayana kwamba anatarajia kumtumia Mario Balotelli, mshambuliaji wake mpya waliyemsajili akitokea AC Milan kwa mechi yao ya Jumapili dhidi ya Tottenham Hotspur.
Nyota huyo wa Italia alijiunga na vijogoo hao wa Merseyside na kuishuhudia Liverpool ikikanyagwa mabao 3-1 na Manchester City walipoifuata Etihad, uwanja aliokuwa akiiutumia strika huyo miezi sita iliyopita.
Rodgers, aliuambia mtandao kwamba anamuandaa nyota huyo mwenye vituko ambaye tayari ameanza kuyazoea mazingira ya Anfield kwa kufanya mazoezi na wenzake ili kuwakabili vinara hao wa ligi, Spurs kwenye uwanja wa ugenini wa White Hartlane.
"Nadhani wikiendi hii atakuwa tayari kuanza kuitumia timu," kocha Rodgers alisema.
Vijogoo hao walioanza ligi kwa kishindo kwa kuifunga Southampton kwa mabao 2-1 na kushtukizwa na mabingwa watetezi kwa kulazwa mabao 3-1 huku Balotelli akishuhudia jukwaani.

No comments:

Post a Comment