STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Mkubwa na Wanae kutambulisha chipukizi wapya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6Kc_Ur8Lec9lYrBOF-IQAUaRSFQDK8Cdxz_8hhYUt4XGOWTORG7E7OH7FEYP_r6op9UjS_24xidUE0xrJVx_XNzUQTPr_8iyprsuw_DKzExTICOG6MOUOobngot5tCcegYMZg5V4AfR0/s1600/ya+moto+band.jpg
Said Fella akiwa nna wasanii wa Moto Band ambayo ni chimbuko lililoibuliwa na kito cha Mkubwa na Wanae
KITUO cha kukuzia na kuendeleza vipaji vya wasanii cha Mkubwa na Wanae kinatarajiwa kuwatambulisha rasmi wasanii chipukizi pamoja na nyimbo zao mpya siku ya Jumapili jijini Dar es Salaam.
Onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Maisha Club na wasanii hao watasindikizwa na 'kaka' zao wa TMK Wanaume Family na Moto Band.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa wakurugenzi wa kituo hicho, Said Fella 'Mkubwa Fella' alisema wasanii watakaotambulishwa katika onyesho hilo la Agosti 31 ni Dogo Muu, Getu, Dulla Yeyo, Mugogo na chipukizi wengine ambao wamekamilisha nyimbo zao mpya hivi karibuni chini ya kituo hicho.
"Tunatarajia kuwatambulisha rasmi wasanii wetu wapya ambao wamekamilisha nyimbo mpya. Onyesho hilo litafanyika Agosti 31 Masaki," alisema Fella.

No comments:

Post a Comment