STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Diamond azidi kutusua kimataifa, Mdogomdogo wambeba

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasib Abdul 'Diamond' amezidi kuangukiwa na neema ibaada ya kuteuliwa kuwania tuzo za muziki za kimataifa za IRAWMA kupitia wimbo wake mpya wa Mdogo Mdogo.
Nyimbo nyingine zilizopo katika kinyang'anyiro hicho katika category ya 'Best African Song/Entertainer' ni pamoja na Aye wa Davido toka Nigeria, Bundeke wa Awilo Longomba toka Congo, Tam Tam wa Willy Paul Msafi toka Kenya, Sitya Loss wa Eddy Kenzo toka Uganda na Mama Africa wa Brakets toka Nigeria
Hii ni mara ya nne kwa Diamond kupenya kwenye tuzo za kimataifa baada ya mwaka huu kuteuliwa kuwania tuzo za MTV za Afrika Kusini, BET za Marekani na AFRIMMA ambapo ndipo pekee alipoibuka kidedea.
Kuteuliwa kuwania tuzo hizo za sasa zinazidi kumpa nafasi msanii huyo kuzidi kutamba anga la kimataifa.

No comments:

Post a Comment