STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Sanchez aibeba Arsenal, Napoli hoi Ulaya

Alexis Sanchez
Cazorla akishangilia nao la sanchez. Yeye alikosa penati usiku huu
Alexis Sanchez
Sanchez akishangilia bao lake
Jack Wilshere
Welshere akisikitika baada ya kukosa bao
Nenda nje bwana we si uonyeki mara moja'

Alexis Sanchez
Sanchez akifunga bao la Arsenal
Mathieu Debuchy
Mathieu Debuchy akisikitika baada ya kulimwa kadi ya pili ya njano iliyoambana na nyekudnu na kutolewa uwanjani usiku huu.
Alexis Sanchez pays off his transfer fee in one swoop.
Oyooooooooooooo!
STRIKA mpya wa Arsenal kutoka Chile, Alexis Sanchez  usiku huu ameibuka shujaa baada ya kuivusha timu yake hiyo kwenye hatua ya makundi kwa mwaka wa 17 mfululizo baada ya kufunga bao pekee dhidi ya Besiktas ya Uturuki.
Katika mchezo huo Arsenal ilijikuta wakicheza pungufu baada ya Methieu Debuchy kulimwa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi mbili za njano, moja kila kipindi katika pambano hilo lililochezwa uwanja wa Emirates, mjini London.
Sanchez aliyesajiliw ana Arsenal hivi karibuni akitokea Barcelona alifunga bao hilo pekee katika dakika ya 45 za kipindi cha kwanza akimalizia kazi nzuri ya Jack Wilshere na kuifanya Ze Gunnerz kufuzu kwa ushindi wa jumla wa bao 1-0.
Katika mechi ya kwanza baina ya timu hiyo wiki iliyopita zilishindwa kutambiana kwa kutofungana mjini Instabul.
Katika mechi nyingine za Ligi hiyo ya mabingwa Ulaya,  Malmo ya Sweden iliitambia Salzburg ya Uswisi kwa kuichapa mabao 3-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-2 kwani katika mechi ya kwanza Malmo walifungwa mabao 2-1 ugenini.
Bayer Leverkusen wakiwa nyumbani nchini Ujerumani walipata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya  Copenhagen na kufuzu kwa mabao 7-2 kwani mechi ya awali walishinda ugenini mabao 3-2, huku Athletico Bilbao ikiizima napoli kwa mabao 3-1 baada ya wiki iliyopita kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1.

No comments:

Post a Comment