STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Crystal Palace yamrejesha Neil Warnock klabuni


http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2010/01/04/article-1240631-07C239A3000005DC-843_306x423.jpg
Kocha Warnock aliyerejea tena Crystal Palace
KLABU ya Crystal Palace imemrejesha kikosini aliyekuwa meneja wake, Neil Warnock.
Kocha huyo alitimka katika klabu hiyo 2010 kwenda kuiongoza QPR na kuipandisha Ligi Kuu kabla ya kutimuliwa mwaka 2012 amesaini mkataba wa miaka miwili kuinoa timu hiyo ambayo ilikuwa ikifundishwa na Keith Millen.
"Neil amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili na anatarajiwa kuongoza timu katika pambano la Jumamosi dhidi ya Newcastle United," Mtandao wa klabu hiyo (www.cpfc.co.uk) uliandika leo Jumatano.

No comments:

Post a Comment