STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Chegge atambia video ya Wauwe

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Said Chegge 'Chegge Chigunda' ametamba video yao mpya ya wimbo 'Wauwe' ni funika bovu na anaamini itasumbua katika vituo vya runinga ndani na nje ya nchi.
Chegge aliyeshirikiana na Mheshimiwa Temba kutoa wimbo na video hiyo aliiambia MICHARAZO kuwa, ukali wa video hiyo unathibitisha Watanzania wanavyoweza kutengeneza kazi kinyume na wanaokimbilia nje ya nchi.
"Hatujisifu, lakini video ya 'Wauwe'  imetulia na ni bonge la kazi ambayo inathibitisha kuwa wapo Watanzania wenye uwezo mkubwa wa kuzalisha video tofauti na tazamo wa baadhi ya wasanii kukimbilia nje," alisema.
Chegge alisema kazi kubwa iliyofanywa na Adam Juma wa Next Level itazidi kuliweka kundi lao la TMK Wanaume Family matawi ya juu.
Wimbo huo Chegge na Mhe Temba wameshirikiana na mkali wa Moto Band aliyeibuliwa na kituo cha Mkubwa na Wanae, Maromboso na video yake imewajumuisha nyota mbalimbali akiwamo Jokate na Julio wa Big Brother

No comments:

Post a Comment