STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Kocha amuonya Balotelli, amwambie akiharibu inakula kwake

http://assets2.sportsnet.ca/wp-content/uploads/2013/05/balotelli_mario640.jpgMARIO Balotelli yuko katika "nafasi yake ya mwisho" baada ya kujiunga na Liverpool kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 16, alisema kocha Brendan Rodgers.
Mshambuliaji huyo wa Italia mwenye umri wa miaka 24 aliishuhudia kutokea jukwaani Liverpool ililala 3-1 ugenini dhidi ya klabu yake ta zamani ya Manchester City juzi baada ya kujiunga akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu.
Balotelli alikuwa maarufu kwa matukio ya utata wakati akichezea Man City lakini Rodgers anakubali kuwa kumsajili nyota ni "kama kucheza kamari" lakini anasema anaweza kujirekebisha.
"Tunaweza kumfanya awe bora kama mchezaji na ajutambue kama mtu mzima," alisema.
"Ni kijana mzuri. Alikuwa mwerevu sana. Anatambua mahala alipo ni wapi, katika wakati wake huu, na anatambua kwamba pengine hii ni fursa yake ya mwisho.
"Muda utaongea. Hakika ni kama kamari. Sitasema kwamba hafiti, ila anatambua anapaswa kufiti katika utamaduni wetu."

No comments:

Post a Comment