STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Hatimaye Di Maria rasmi Man Utd




HATIMAYE Muargentina, Angel Di Maria ametua na kusaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Manchester United.
Mkataba huo ndiyo rekodi mpya ya usajili baada ya Man United kukubali kutoa pauni milioni 59.7 ambazo ni pauni milioni 60 ili kumpata.
Atakuwa akilamba mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki, anachukua nafasi ya pili kwa mshahara mkubwa baada ya nahodha wake, Wayne Rooney.
Mchezaji huyo hata hivyo aliingia Old Trafford na mguu mbaya baada ya klabu yake hiyo kulambwa mabao 4-0 na timu ya Daraja la Kwanza katika mechi ya Kombe la Ligi na anategemea kuwemo katika kikosi cha Mashetani hao Wekundu katika mechi ya Ligi Kuu siku ya Jumamosi dhidiya Banley.

No comments:

Post a Comment