STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 4, 2013

WABUNGE WACHAPANA NGUMI ZA KAVU KAVU BUNGENI


Uuuh aaaah!
PICHANI ni baadhi ya  wabunge wa Taiwan 'walivyokuwa wakiadabishana' jana baada ya kupishana lugha kufuatia mpango wa kupiga kura ya maoni iliyoazimia kuidhinisha umaliziwaji wa mradi wa nne wa Nyuklia katika kisiwa ambacho kinakaliwa na watu wapatao milioni 23. Wabunge wa Tanzania ambao wamekuwa wakichimbana mkwara bungeni...wakifikia huku sijui itakuwaje? 
Acha mshikaji mnaharibu! Ngoja nimfunze adabu
Kuja hapa weweee!

Bahanuzi, Javu waizamisha Mtibwa Sugar Taifa

 Beki wa Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe akichuana na mshambuliaji wa Yanga wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga imeshinda 3-1. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Beki wa Mtibwa Sugar, Ally Lundega akimiliki mpira huku akizongwa na mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
 Mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima akimtoka beki wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhan wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 


 Kikosi cha Mtgibwa Sugar.
Kikosi cha Yanga.
 Mashabiki wa Yanga waklifuatilia mtanange huo.

Young Africans leo imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wakata miwa kutoka Morogoro timu ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu uliofanyika katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Ikiwatumia wachezaji wake wapya iliyowasajili kwa ajili ya msimu huu kikosi cha mholanzi kiliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha wanapata ushindi na kuendeleza heshima kwa timu wanazokutana nazo.
Dakika ya sita ya mchezo mshambuliaji mpya Shaban Kondo almanusura aipatie Young Africans bao baada ya kupokea krosi safi ya Said Bahanuzi kutoka upande wa kulia lakini kutokua makini kwa mshambuliaji huyo kulimfanya mlinda mlango wa Mtibwa Sugar Hussein Sharrif kuokoa hatari hiyo.
Said Bahanuzi aliwainua washabiki, wapenzi na wanachama wa klabu ya Yanga dakika ya 24 ya mchezo baada ya kuukwamisha mpira wavuni kufuatia mlinzi wa mtibwa kuokoa kwa kichwa mpira wa Jerson Tegete ulikokuwa ukielekea wavuni.
Mara baada ya bao hilo Mtibwa Sugar waliongeza kasi ya mashambulizi kwa lango la Yanga ili waweze kupata bao la kusawazisha laikini harakatia zao zilishia mikononi mwa mlinda mlango Deogratius Munishi 'Dida' 
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 1 - 0 Mtibwa Sugar.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ambapo Yanga iliwaingiza golikipa Ally Mustapha 'Barthez, Rajab Zahir, David Luhende, Bakari Masoud, Hussein Javu, na Abdallah Mguhi 'Messi, mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mchezo.
Dakika ya 57 ya mchezo Shaban Kisiga aliipatia Mtibwa Sugar bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penati kufuatia mlinzi Rajab Zahir kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari na Kisiga kufunga penati hiyo na kupata bao la kusawazisha.
Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 80 ya mchezo kufuatia mlinzi wa kati wa Mtibwa Sugar Salvatory Ntebe kumkwatua Tegete na mwamuzi kuamuru penati ambayo aliipiga Tegete na kuukwamisha mpira wavuni.
Huku washabiki wa soka wakianza kutoka nje na wengine wakiwahi kufuturu Hussein Javu aliifungia Yanga bao la tatu na la ushindi dakika ya 87 ya mchezo kufuatia mpira aliorudhishiwa golikpa Said Mohamed kushindwa kuuondoa na Javu kuuwahi na kuhesabu bao la tatu kwa watoto jangwani.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 1 Mtibwa Sugar.
Mara baada ya mchezo kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amesema kikosi chake kinaendelea kuimarika na wachezaji wanaonekana kushika vizuri mafunzo yake, anaendelea na mazoezi kwa hizi wiki mbili kabla ya kucheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya timu ya Azam FC Agosti 17 2013.
Young Africans: 1.Deogratius Munishi 'Dida'/Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua/David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro'/Rajab Zahir, 5.Issa Ngao, 6.Athuman Idd 'Chuji/Bakari Masoud, 7.Said Bahanuzi/Abdallah Mguhi 'Messi', 8.Salum Telela, 9.Jerson Tegete, 10.Shaban Kondo/Hussein Javu, 11.Haruna Niyonzima.

Twanga Pepeta kumtambulisha Ige Moyaba na wengine Mango Garden siku ya Idd Pili

Ige Moyaba aliyerejea tena Twanga atatambulishwa Idd Pili
BENDI ya African Stars “Twanga Pepeta” itatambulisha wanamuziki wapya pamoja na warembo watakaoshiriki Miss Ilala siku ya Iddi Pili Katika ukumbi wao wa Mango Garden, Kinondoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo Asha Baraka alisema jana kuwa onyesho hilo limeandaliwa na Bob Entertainment na kudhaminiwa na Konyagi, Freddito Entertainment, Saluti5 na Twitter Pub.
Alisema wanamuziki watakaotambulishwa siku hiyo maalum ni wanenguaji wapya, muimbaji Ige Moyaba ambaye alikuwa mwanamuziki wa bendi hiyo kabla kwenda Ufaransa kuendeleza kipaji chake.
 “Tumeamua kuleta wanenguaji wapya kabisa, wenye damu changa ili kuleta mapinduzi kwenye muziki wa dansi. Madansa wetu ni mabinti warembo, pia tuna  wanenguaji watanashati,” alisema Asha na kuongeza kuwa awameamua kubadilisha wanenguaji ili kuenda na wakati pamoja na soko la muziki.
Kwa upande wa Ige Moyaba aliyetamba kwenye albamu ya ‘Mtu Pesa’ katika mwaka wa 2004,  Asha alisema ameanda vitu vipya kuwapa mashabiki wa bendi hiyo inayotamba kwa staili ya Kisigino.
“Kwa kweli hi siyo onyesho la kukosa kwani itakuwa ni zawadi yetu ya Idd kwa mashabiki wetu,” mkurugenzi huyo alisema.
Mwezi uliyopita Twanga Pepeta walizindua albamu yao ya 10 lijulikanayo kana “Nyumbani ni Nyumbani”.
Albamu zingine ambazo zitapigiwa siku hiyo ni Jirani, Fainali Uzeeni, Chuki Binafsi, Ukubwa Jiwe, Mtu Pesa, Safari, Password, Mtaa Wa Kwanza, Mwana Dar es Salaam na Dunia Daraja.
Naye mratibu wa onyesho hilo Joseph Kapinga alisema kuwa warembo watakoshiriki kwenye shindano la kumtafuta Redds Miss Ilala pia watatambulishwa siku hiyo.
BENDI ya African Stars “Twanga Pepeta” itatambulisha wanamuziki wapya pamoja na warembo watakaoshiriki Miss Ilala siku ya Iddi Pili Katika ukumbi wao wa Mango Garden, Kinondoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo Asha Baraka alisema jana kuwa onyesho hilo limeandaliwa na Bob Entertainment na kudhaminiwa na Konyagi, Freddito Entertainment, Saluti5 na Twitter Pub.
Alisema wanamuziki watakaotambulishwa siku hiyo maalum ni wanenguaji wapya, muimbaji Ige Moyaba ambaye alikuwa mwanamuziki wa bendi hiyo kabla kwenda Ufaransa kuendeleza kipaji chake.
 “Tumeamua kuleta wanenguaji wapya kabisa, wenye damu changa ili kuleta mapinduzi kwenye muziki wa dansi. Madansa wetu ni mabinti warembo, pia tuna  wanenguaji watanashati,” alisema Asha na kuongeza kuwa awameamua kubadilisha wanenguaji ili kuenda na wakati pamoja na soko la muziki.
Kwa upande wa Ige Moyaba aliyetamba kwenye albamu ya ‘Mtu Pesa’ katika mwaka wa 2004,  Asha alisema ameanda vitu vipya kuwapa mashabiki wa bendi hiyo inayotamba kwa staili ya Kisigino.
“Kwa kweli hi siyo onyesho la kukosa kwani itakuwa ni zawadi yetu ya Idd kwa mashabiki wetu,” mkurugenzi huyo alisema.
Mwezi uliyopita Twanga Pepeta walizindua albamu yao ya 10 lijulikanayo kana “Nyumbani ni Nyumbani”.
Albamu zingine ambazo zitapigiwa siku hiyo ni Jirani, Fainali Uzeeni, Chuki Binafsi, Ukubwa Jiwe, Mtu Pesa, Safari, Password, Mtaa Wa Kwanza, Mwana Dar es Salaam na Dunia Daraja.
Naye mratibu wa onyesho hilo Joseph Kapinga alisema kuwa warembo watakoshiriki kwenye shindano la kumtafuta Redds Miss Ilala pia watatambulishwa siku hiyo.

Wanahabari wa Habari Group watoa msaada kwa yatima


Diwani wa Viti Maalumu na Mwenyekiti Mtendaji wa Aisha Sururu Foundition, Bi. Aisha Sururu kulia akiwakabidhi sehemu ya msaada alioutoa kwa ajili ya kuchangia yatima kwa wanachama wa kikundi cha Habari Group, Rabia Bakari (kushoto) na Asha Bani kwa ajili ya kupeleka kwa yatima katika vituo mbalimbali  Misaada mingine ilitolewa na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia, January Makamba, Mmiliki wa Maduka ya Silva Botique, Madam Nora, Katibu wa Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa kiislam Sheikh  Khamisi Mataka, na Mkurugenzi wa Kampuni ya QUALITY Printers And Stationers Amani Soko

Diwani wa Viti Maalumu na Mwenyekiti Mtendaji wa Aisha Sururu Foundition, Bi Aisha Sururu (kushoto) akiwakabidhi sehemu ya msaada alioutoa kwa ajili ya kuchangia yatima kwa wanachama wa kikundi cha Habari Group Rabia Bakari na Asha Bani kwa ajili ya kupeleaka kwa yatima wa vituo mbalimbali.

Wanachama wa kikundi cha Habari Group, Rabia Bakari (kulia) na Asha Bani wakiangalia baadhi ya vyakula na vitu mbalimbali walivyokabidhiwa kwa ajili ya kwenda kugawa kwa  yatima.
Sehemu ya misaada hiyo

Wanachama wa Habari Group wakia katika picha ya pamoja na na mwenyekiti mtendaji wa Aisha Sururu Foundition Bi. Aisha Sururu
Moja ya kituo cha kilichopewa misaada na Habari Group Leo

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada  walioutoa kwa  Katibu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni Bw. Abubakari Simba jijini Dar es salaam leo.

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha habari Group wakiwa katika picha ya pamoja na  yatima wanaolelewa katika Kituo cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni baada ya kutoa misaada mbalimbali leo

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani kulia akikabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa  Katibu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Hidaya Orphans Center and Tahfidhil-qur-an cha Buguruni Bw. Abubakari Simba Dar es salaam leo.

Mwanachama wa Kikundi cha Habari Group, Asha Bani (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada  walioutoa kwa  Msimamizi Mkuu wa kituo cha kulelea yatima cha Al Furqan Islamic Center cha Chanika Bw. Hamisi Omari  Dar es salaam leo
Baadhi ya wanachama wa kikundi cha habari Group wakiwa katika picha ya pamoja na  yatima wanaolelewa katika kituo cha Al Furqan Islamic Center cha Chanika baada ya kutoa misaada mbalimbali leo.

Meshack Abel kwenda Ulaya akiizitabiria Ashanti, Coastal kufanya maajabu Ligi Kuu 2013-2014


Meshack Abel (kulia) akiwa na wachezaji wenzake wa Kitanzania wanaoichezea Bandari-Kenya, Mohammed Banka, Thomas Mourice na David Naftar
BEKI wa kimataifa zamani wa Simba anayecheza soka la kulipwa nchini Kenya katika timu ya Bandari, Meshack Abel, anajiandaa kuitema timu hiyo na kwenda Ulaya kusaka timu ya kuichezea.
Aidha Abel amezitabiria timu za Ashanti United na Coastal Union ya Tanga kufanya vyema kwenye msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza rasmi Agosti 24, akiamini itazipiku vigogo Simba na Yanga zinazopokezana taji kila msimu.
Akizungumza na MICHARAZO toka Kenya, beki huyo wa kati alisema anatarajiwa kuachana na timu hiyo na kutimka Ulaya mara baada ya mkataba wa kuitumikia klabu hiyo ya Ligi Kuu nchini humo utakapomalizika Desemba mwaka huu.
Abel, aliyewahi kuzichezea pia timu za Ashanti United na African Lyon, alisema tayari mipango ya safari ya kwenda Ulaya inafanywa na meneja wake.
Beki huyo aliyejaliwa mwili mkubwa, alisema ingawa bado hajadokezwa anatafutiwa timu katika nchi gani barani huko, lakini mipango ya awali ilikuwa kati ya nchi za Sweden, Norway au Uswisi.
"Mkataba wangu unakaribia kuisha na tayari sina mpango wa kuongeza kwa vile najiandaa kwenda kusaka timu ya kucheza soka la kulipwa barani Ulaya, wakati wowote natimkia huko," alisema.
Alipoulizwa kama alikuwa na mipango ya kurejea nchini kucheza soka baada ya kutamba na timu kadhaa ikiwamo Simba, Abel alisema kwa sasa hafikirii kabisa jambo hilo zaidi ya kusonga mbele kwa madai soka la Bongo limejaa mizengwe tofauti na hali aliyokutana nayo nchini Kenya ambapo klabu zinawathamini na kuwajali wachezaji huku mashabiki wakiwaunga mkono.
"Sifikirii kurudi nyumbani kwa sasa, mawazo yangu ni kusonga mbele zaidi ndiyo maana najiandaa kuondoka Kenya," alisema.
Kuhusu Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013-2014 inayoanza Agosti 24, Abel alisema kwa namna anavyozifuatilia timu shiriki anaweka turufu yake kwa klabu za Coastal Union na Ashanti United kuzifunika Simba na Yanga katika mbio za kuwania ubingwa.
"Simba na Yanga zilikuwa zamani, kama siyo mizengwe Azam ilishazifunika na msimu huu naamini Coastal Union na Ashanti United itaongeza ushindani kwa klabu hizo na kufanya vyema katika ligi ijayo," alisema.
Alisema hata hivyo klabu hizo hazipaswi kujiamini kupita kiasi na badala yake wachezaji wake wajitume na kuhakikisha kila mechi wanapata ushindi na kusaidia kutimiza utabiri wake kwa klabu hizo msimu huu.

Zahoro Pazi hahofii chochote Simba

Zahoro Pazi
 MSHAMBULIAJI mpya wa Simba, Zahoro Pazi amesema hahofii ushindani wa namba katika kikosi cha timu hiyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Pazi, mtoto wa kipa wa zamani wa 'Wekundu wa Msimbazi', Idd Pazi 'Father' alisema licha ya kutambua ametua Msimbazi wakati kikosi hicho kikiimarishwa kwa kusajiliwa wachezaji wapya wakiwemo wa ndani na wale wa kigeni bado anajiamini kupata nafasi kwa kipaji na uwezo mkubwa alionao katika soka.
Pazi, alisema kitu cha muhimu kwake atakachozingatia ni kujituma mazoezi, kucheza kwa bidii akipata nafasi kama ilivyotokea katika mechi za kirafiki ambazo Simba imeshacheza hivi sasa zikiwemo mbili zilizopita dhidi ya URA na Coastal Union ambapo timu hiyo ilipoteza mechi zote.
"Ni kweli kuna ushindani mkubwa katika kikosi cha Simba, tumekutana wachezaji wapya wenye uwezo mkubwa, lakini sihofii chochote kwa vile najiamini na nitajitahidi kumridhisha kocha Abdallah Kibadeni kisha kuliacha jukumu mikononi mwake kuamua nani wa kumpanga katika mechi za Ligi zinazotarajiwa kuanza karibuni," alisema.
Pazi alisema katika mechi zote za kujipima nguvu anashukuru alipewa nafasi ya kucheza na kuonyesha uwezo wake, ingawa bado hajafunga bao lolote, akiamini anaendelea kuzoea mazingira ya klabu hiyo iliyowahi kuchezwa na baba yake.
Mshambuliaji huyo alisema kwa namna kikosi chao kilivyo chini ya kocha anayemzimia aliyewahi kumnoa alipokuwa Mtibwa Sugar, anaamini Simba itatamba katika msimu ujao, ingawa alikiri huenda ikakamiwa na kupata wakati mgumu kutimiza ndoto za kurejesha ubingwa baada ya msimu uliopita kuupoteza kwa watani zao Yanga.
Simba inatarajiwa kufungua dimba la pazia la ligi kuu msimu huu kwa kuumana ugenini na timu 'ngeni' ya JWTZ, Rhino Rangers ya Tabora iliyopanda toka daraja la kwanza sambamba na timu za Ashanti United na Mbeya City.

Golden Bush wagawa msaada kwa yatima, Kaseja kivutio

Juma kaseja akiwa kando yawatoto yatima

'Tanzania One' Juma Kaseja akiwa amekaa na  yatima wanaolelewa katika kituo cha New Life Orphans Home wakati timu ya Golden Bush ilipopeleka msaada katika kituo hicho. Kipa huyo alikuwa kivutio kwa watoto hao.
Wachezaji wa Golden Bush wakiwa pamoja na yatima hao

Mmoja wa wachezaji wa Golden Bush akiwa amebeba mmoja wa yatima hao

Watoto wakifurahia kujumuika na wachezaji wa Golden Bush

Naondoka na wewe! Yatima akiwa mikononi mwa mmoja wa wachezaji wa Golden Bush

Salum Swedi akizungumza jambo, kushoto  KR Mulla na kulia kwake ni Herri Morris
Yatima wa kituo cha New Life Orphans Home wakiimba wakati wachezaji wa Golden Bush walipowatemebelea leo

Katibu wa kituo cha Kulelea Yatima cha New Life Orphans Home, Hamad Kombo (kushoto) akisoma risala fupi mbele ya uongozi wa Golden Bush

Yahya Issa kati akiwa amempakata mtoto kando ya Mkuu wa Nidhamu wa kituo cha kulelea Yatima Mbwana Said huku Herry Morris akiwa kando yake kushoto
Rashid Ziada 'KR Mullah' naye alikuwa mmoja wa wana Golden Bush waliotembelea kituo cha yatima na kuwaonyesha namna ya kucheza Mapanga Shaa'
TIMU ya soka ya Golden Bush Fc kimewatembelea yatima wanaolelewa katika kituo cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo, jijini Dar es Salaam na kuwafariji kwa kuwapa msaada wa vitu mbalimbali ikiwamo chakula kwa ajili ya sikukuu ya Eid.
Msaada huo Golden Bush ulitolewa leo asubuhi na wachezaji hao wakiongozwa na mlezi wao, Onesmo Waziri 'Ticotico', viongozi na nyota kama Juma Kaseja, Salum Swedi 'Kussi' , Yahya Issa, Amani Simba, Waziri Madhi na wengine una thamani ya Sh. 3.5.
Baadhi ya msaada huo ni sabuni, juisi, mchele, sukari, mafuta ambavyo vilikabidhiwa na timu hiyo kwa uongozi wa kituo hicho ukiongozwa na Katibu Mkuu wake, Hamad Kondo na Mkuu wa Nidhamu, Mbwana Said.
Yatima hao wakiwa na bashasha na hasa baada ya kuwaona wachezaji hao mastaa waliwaimbia Golden Bush na kuchezewa miondoko ya Mapanga Shaa na msanii Rashid Ziada 'KR Mullah' ambaye naye ni mchezaji wa timu hiyo kabla ya Katibu wa kituo kusoma risala fupi.
Hamad akieleza kwa ufupi kwamba historia ya kituo hicho kilichoanzishwa mwaka 2001......kikiwa na watoto 17 tu tofauti na sasa wanafikia 103 wasichana wakiwa 38 na waliosalia wakiwa ni wavulana.
Katibu huyo alieleza kuwa kituo chao kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo ada za kuwalipia wanafunzi wanaosemeshwa na kituo hicho ambapo baadhi wapo Shule ya Msingi na wengine wa Sekondari.
Pia Hamad aliweka bayana kuwa kituo chao kimefanikiwa kupata eneo huko Boko-Dawasa na wamejenga jengo la ghorofa moja ambalo walisaidiwa kiwanja na mlezi wao na mpaka sasa jengo hilo limesimama isipokuwa bado halijamalizika kutengenezwa sakafu.
Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' akizungumza kabla ya kuupisha uongozi wa juu wa timu hiyo, alisema wanafahamu walichokitoa ni kidogo, lakini waliuomba uongozi upokee kwa mikono  miwili na kuahidi kutoa msaada wa kifedha kupitia akaunti ya kituo hicho.
"Nimesikia kilio chenu, ninachoomba nipeni namba yenu ya akaunti nami nilichojaliwa nitakituma huko, ila kwa sasa tunaomba mpokee japo hiki kidogo kwa ajili ya kuwafariji watoto katika kuelekea sikukuu ya Eid," alisema Ticotico.
Nao Mwenyekiti wa timu hiyo, Salum Swedi na Katibu wake, Herry Morris waliwataka watoto hao kuwa watiifu na kuishi kwa wema na Mungu akiwajalia waje kuwa nyota kama walivyokuwa wao katika soka, huku wakijinadi wapo wanaodaka kama Kaseja ambaye walimshangilia zaidi na kuonyesha kumjua na kutaka kupiga naye picha kila mara.
Naye Kaseja alipata nafasi ya kuzungumza na watoto hao na kuwataka kujibidiidha katika masomo, kumcha Mungu na kuwa watiifu kwa kila mtu na kwa wale wenye vipaji waviendeleze ili vije kuwasaidia ukubwani kama ilivyokuwa kwake na wenzake waliowatembelea.

Saturday, August 3, 2013

Hamis Kiiza mshambuliaji wa 7 Jangwani

MSAHAMBULIAJI WA YANGA HAMIS KIIZA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI KUENDELEA KUKIPIGA YANGA

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamis Kiiza hatimaye amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya Jangwani na kufanya idadi ya washambuliaji katika kikosi hicho cha Jangwani kufikia saba mpaka sasa. 
Kiiza alisaini mkataba huo katika hoteli ya Protea, Dar es Salaam na kufanya idadi ya wachezaji wa kimataifa kufikia wanne akiwamo Haruna Niyonzima wa Rwanda, Mbuyu Twitte wa DR Congo na Didier Kavumbagu kutoka Burundi.

Kusainishwa kwa Mganda huo kumemaliza sintofahamu ya muda mrefu juu ya mustakabali wa mchezaji huyo aliyeibeba Yanga tangu alipotua klabuni hapo na kufanya safu ya mbele ya jangwani iwe na wafumania nyavu saba.
 
Wakali wengine ni Jerryson Tegete, Kavumbagu, Hussein Javu, Said Bahanuzi Shaban Kondo (aliyesajiliwa toka Msumbiji) na Realintus Lusajo (kutoka Machava- Moshi).

Barcelona waitafuna Santos ya Neymar 8-0

Headlines News :



Masupastaa: Lionel Messi na Neymar wakifurahi kabla ya mechi
ndiyo mwanzo wa mataji?

BARCELONA imeiangushia kipigo kizito cha 8-0 Santos ya Brazil kwenye uwanja wa Nou Camp na kutwaa taji la Joan Gamper katika mwendelezo wa mechi za maandalizi ya msimu mpya.

Neymar aliyesajiliwa kwa pauni 48 alianzia benchi dhidi ya timu yake ya zamani sambamba na mchezaji anayewaniwa na Manchester United Cesc Fabregas ingawa kiungo huyo wa zamani wa Arsenal alifunga mabao mawili katika kipindi cha pili.

Alexis Sanchez, Pedro na Lionel Messi kila mmoja alifunga bao moja katika kipindi cha kwanza, wakati bao la kujifunga mwenyewe la Leo na magoli mengine kutoka kwa Adriano, Jean Marie na mawili ya Fabregas yalihitimisha karamu hiyo ya magoli.

Supastaa wa samba Neymar ambaye alicheza mchezo wake wa kwanza kwenye jezi ya Barcelona katika mchezo wa sare ya 2-2 huko Poland, alionekana akitaniana na mchezaji bora wa dunia Messi kabla ya kucheza mechi yake ya kwanza mbele ya mashabiki wa Barcelona kwenye uwanja wa Nou Camp.

Messi alikuwa wa kwanza kufunga katika dakika ya 8 na muda mfupi baadae krosi ya nguvu ya Dani Alves ikamlazimisha beki Leo kujifunga.

Uchawi wa Messi ukahamia kwenye kusaidia kufunga mabao baada kumtengenezea winga wa Chile, Sanchez aliyekwamisha wavuni bao la tatu kabla ya Pedro kumalizia pasi ya Jordi Alba na kuhesabu goli la nne.

Kuingia kwa Neymar kulipokewa kwa shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki waliojazana Nou Camp ingawa mtu mmoja aliyevalia nguo zenye nembo ya timu pinzani ya Santos, Internacional alivamia uwanja huku akimfuata Neymar kabla hajazuiliwa na kuondolewa uwanjani.

CREDIT: SAIDI MDOE, SALUTI 5
                      Vurugu: Neymar akiokolewa dhidi ya shabili mwenye hasira

 Maelekezo: Kocha mpya Tata Martino (kulia) akimpa maelekezo Neyma
Magoli yake ya mwisho? Fabregas alitokea benchi na kufunga mabao mawili
 
Credit:Salute5

NMB yatoa msaada wa mashuka Hospitali ChakeChake Pemba


 Meneja wa Tawi la Benki ya NMB Chake Chake, Pemba, Hamidu Mughamba, (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa, Mhe. Hanuna Ibrahim, sehemu ya mashuka yaliyotolewa na Benki hiyo kama msaaada kwa hospitali za Wilaya ya Chake Chake.
 
NMB imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia mahitaji mbalimbali yanayoizunguka jamii.Kwa kutambua hilo hivi karibuni  maofisa wa NMB tawi la Chake chake walitoa mashuka ya hospitali yenye thamani ya shilingi million tano kwenye hospitali mbali mbali ikiwamo hospitali ya wilaya ya Wete, Chakechake, Mkoani na Micheweni. Mashuka haya  yatasaidia kupunguza hitaji kubwa la mashuka lililokua likizikumba hospitali hizi.

 Maofisa wa Benki ya NMB pamoja na Mganga Mkuu wa Hosipitali ya Chake Chake, Pemba, wakiyatizama baadhi ya mashuka  yaliyokabidhiwa na Benki ya NMB.
Maofisa wa Benki ya NMB pamoja na Mganga Mkuu wa Hosipitali ya Chake Chake, Pemba, wakiyatizama baadhi ya mashuka  yaliyokabidhiwa na Benki ya NMB.

CHADEMA YALAANI POLISI KUMDHALILISHA MWANDISHI CHANNEL 10

  https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEik9fmVEvTrvMxg4Kro3HAJDvaFvMsjDK6g3-Y9yKXaH8nGcFmuichIzChQ0dwIaLC6e5QLxYYfA4OT2b8OCVz-tlb0WfPCGooGPnPM4n7MJupnlQ-1DtdyE2JxlbPCmgw4FolZQBJrKCc/s1600/528890_103622173103898_656595116_n.jpg

CHADEMA, kupitia Kurugenzi ya Habari na Uenezi, inatoa kauli ya awali, kulaani kitendo cha kupigwa, kuchaniwa nguo, kujeruhiwa, kunyang'anywa vifaa na kufungwa pingu kwa mwanahabari wa Channel ten, Eliah Ruzika, kilichofanywa na askari wa Jeshi la Polisi eneo la Tazara, Dar es Salaam, wakati mwandishi huyo akitimiza majukumu yake kwenye mkutano wa wafanyakazi wa Tazara.

Huu ni mwendelezo wa unyanyasaji wa raia wasiokuwa na hatia, huku wengine wakiwa katika majukumu ya kazi zao, unaofanywa na Jeshi la Polisi.

Ni mwendelezo wa askari wa jeshi hilo kunyanyasa na kuingilia wanahabari katika utekelezaji wa majukumu yao, vitendo ambavyo vimekuwa vikifanyika kwa muda mrefu sasa, hata kusababisha mauaji, bila wahusika kuchukua au kuchukuliwa hatua za kisheria, kuzuia na kukomesha kabisa udhalimu huu.

Bila shaka pia ni utekelezaji wa kauli mbovu kabisa na inayokiuka vigezo vyote vya uongozi bora, siasa safi, misingi ya demokrasia na haki za binadamu, iliyotolewa bungeni hivi karibuni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. 

Kauli iliyoruhusu kuvunjwa kwa haki na hivyo kusababisha uvunjifu wa amani kama inavyotokea sasa. 

Kuminya au kujaribu kuminya utendaji kazi wa vyombo vya habari na wanahabari, ni hatua ya juu sana kuelekea kuminya haki na uhuru wa kufikiri na kutoa maoni, kwa mtu mmoja mmoja, kundi au makundi ya watu katika jamii. 

Kuminya uhuru na haki ya habari na kutoa maoni, huku ukitegemea polisi kutawala (kwa kuigeuza nchi police state) ni moja ya dalili za mwisho mwisho ya watawala waliochoka, wanaotakiwa kupisha madarakani.

Kurugenzi ya Habari CHADEMA

Kazimoto asaini mwaka Al Markhiya

Mwinyi Kazimoto
ALIYEKUWA kiungo wa Simba Mwinyi Kazimoto jana amesaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu kwa ajili kuitumikia klabu ya Al Markhiya SC ya Doha, Qatar.
Habari za uhakika kutoka Qatar zinaeleza kwamba, Kazimoto amesaini mkataba baada ya kufaulu majaribio yake, sambamba na kukubaliana na uongozi ofa aliyopewa.
Imeelezwa kwamba, hatua ya Kazimoto kusaini mkataba huo imekuja baada ya uongozi wa timu hiyo kuongeza dau la kumnunua baada ya awali kugomea kwa madai kuwa halilingani na thamani waliyomnunulia.
Chanzo hicho kimeeleza kwamba, Al Markhiya iliwaangukia Simba kwa dau waliloafikiana kutokana na ukweli kwamba kwa sasa ipo katika hali mbaya ya kifedha na hasa ikizingatiwa kuwa wanahitaji kusajili wachezaji watakaoipandisdha tena daraja.
“Unajua timu imeshuka daraja hivi karibuni sasa wanajiimarisha kwa kusajili wachezaji wazuri na fedha waliyonayo haitoshelezi hivyo wameiomba Simba ipokee hicho walichonacho,”kilieleza chanzo hicho.
Juzi uongozi wa Simba kupitia kwa msemaji wake Ezekiel Kamwaga ulisema umeitupilia mbali ofa iliyotumwa na klabu hiyo kwa madai kuwa ni ya kipuuzi, huku ikidai pia Kazimoto ana maswali kwanza ya kujibu kwa Watanzania na mashabiki wa Simba kwa ujumla.
Simba pia ilidai inakusudia kuketi na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya kumjadili nyota huyo kwa kitendo chake cha kutoroka nchini.

Kazimoto ambaye alisajiliwa na Simba mwaka juzi kutokea JKT Ruvu, alitoroka nchini akiwa na timu timu ya Taifa iliyokuwa ikijiandaa na mechi yake ya kufuzu fainali za Afrika zinazoshirikisha nyota wanaocheza ligi za ndani (CHAN) dhidi ya Uganda ‘The Cranes’.
 
Sports Lady

Mtanzania mwingine anaswa na 'Unga'' Zimbabwe


WIMBI la kukamatwa kwa watanzania nje ya nchi wakiwa na dawa za kulevya likiendelea kuzua mjadala nchini, Mwanamke mwingine wa Kitanzania anadaiwa kunaswa Zimbabwe akiwa na 'unga' unaokadiriwa kuwa na thamani yaDola za 45,000 akitokea India.
Mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Jacklyne Mollel (34) anayeishi Afrika Kusini, inadaiwa alinaswa kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Harare Julai 27 akiwa na dawa hizo zenye uzito wa kilo 15 alipowasili na ndege ya Emirates akitokea India.
Taarifa zaidi zinasema mtanzania huyo ameshafikishwa mahakamani akikabiliwa na kesi hiyo ya kuingiza dawa hizo aina ya Ephedrine zikiwa na uzito wa Kilo 15 na kusomewa shtaka lake mbele ya Hakimu Mkazi Donald Ndirowei juzi jijini humo.

ISOME TAARIFA NZIMA ILIYORIPOTIWA NCHINI HUMO JUU YA MKASA HUO

A 34–year–old Tanzanian woman was last week arrested at the Harare International Airport after she was found in possession of an illicit drug with a street value of $45 000 upon arrival from India.
SENIOR REPORTER
Mollel Jackline Richard, who stays in South Africa, was not asked to plead when she appeared before Harare magistrate Donald Ndirowei yesterday.
She was remanded in custody to July 27.
Richard was allegedly found in possession of 15kg of ephedrine which stimulates the heart and nervous system. It is often found in herbal and diet pills.
The State alleged that Richard arrived at Harare International Airport aboard an Emirates flight from India.
The alleged drug pusher produced her passport at the immigration desk at the airport where an alert officer tipped CID Drugs detectives that Richard had a visa for India which is a known source for illicit drugs.
The court heard that Richard was taken for interviewing and during a search conducted on her by detectives they recovered 30 khaki envelopes containing a whitish substance which was wrapped with fabric sheets inside a maroon bag.
Tests were conducted on the substance and revealed that it was ephedrine. The drug was then taken for recording and weighing.