STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 24, 2013

TFF yawazuia usajili wa wachezaji, kisa....!

Mombeki (kushoto) mmoja wa waliozuiliwa na TFF
Na Boniface Wambura
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imezuia usajili wa wachezaji 37 wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kutokana na usajili wao kuwa na kasoro.

Klabu husika zimetakiwa kurekebisha kasoro hizo kabla ya kuanza kuwatumia wachezaji hao kwenye mechi za VPL ambazo zinaanza leo (Agosti 24 mwaka huu) katika viwanja mbalimbali nchini.

JKT Ruvu Stars inatakiwa kuwafanyia uhamisho (transfer) wachezaji Salum Machaku Salum aliyekuwa Polisi Morogoro na Emmanuel Leonard Swita (Toto Africans). Mgambo Shooting inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji Mohamed Hussein Neto (Toto Africans), Kulwa Said Manzi (Polisi Morogoro) na Mohamed Ally Samata (African Lyon).

Pia Salum Aziz Gilla anaonekana bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Coastal Union huku kukiwa hakuna vielelezo vyovyote kutoka kwa mchezaji mwenyewe, Coastal Union au Mgambo Shooting kama ulivunjwa au umenunulia na klabu anayotaka kuchezea msimu huu.

Tanzania Prisons inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji James Mjinja Magafu kutoka Toto Africans na Six Ally Mwasekaga (Majimaji). Nayo Coastal Union inatakiwa kumfanyia uhamisho mchezaji Kenneth Abeid Masumbuko kutoka Polisi Morogoro.


Kagera Sugar inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji Suleiman Kibuta Rajab (Toto Africans), Godfrey Innocent Wambura (Abajalo), Eric Mulera Muliro (Toto Africans), Adam Juma Kingwande (African Lyon) na Peter Gideon Mutabuzi (Toto Africans).

Pia Kagera Sugar imepata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Kitagenda Hamis Bukenya, lakini bado hana kibali cha kufanyia kazi nchini (work permit).

Kwa upande wa Ruvu Shooting inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji Abdul Juma Seif (African Lyon), Lambele Jerome Reuben (Ashanti United), Juma Seif Dion (African Lyon) na Cosmas Ader Lewis (African Lyon).

Oljoro JKT inatakiwa kumfanyia uhamisho mchezaji Tizzo Charles Chomba kutoka Polisi Morogoro, lakini imekataliwa kumsajili mchezaji Damas Mussa Kugesha wa Mlale JKT kwa kigezo kuwa ni askari na amehamishiwa Arusha kwa ajili ya mafunzo ya kijeshi. Kama Oljoro JKT inamtaka mchezaji huyo ni lazima ifuate taratibu za usajili kwa kumfanyia uhamisho kutoka Mlale JKT.

 Nayo Mtibwa Sugar inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji Ally Shomari Sharrif (Polisi Morogoro), Salim Hassan Mbonde (Oljoro JKT U20) na Hassan Salum Mbande iliyemsajili kwenye kikosi chake cha U20 akitokea Oljoro JKT U20.

Ashanti United haiwezi kumtumia Said Maulid Kalikula aliyekuwa akicheza Angola kwa vile hajapata ITC. Nayo Rhino Rangers inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji Ally Ahmad Mwanyiro (Mwadui FC), Laban David Kambole (Toto Africans) na Musa Boaz Chibwabwa (Villa Squad).

Klabu ya Simba inatakiwa kumfanyia uhamisho Betram Arcadi Mwombeki kutoka Pamba SC wakati wachezaji Gilbert John Kaze na Amisi Tambwe bado hawajapata ITC kutoka Burundi na hawana vibali vya kufanya kazi nchini. Mchezaji Joseph Owino tayari ITC imepatikana lakini hana kibali cha kufanya kazi nchini. Pia kipa Abel right Dhaila hana kibali cha kufanya kazi nchini.

Vilevile Simba inatakiwa kuwafanyia uhamisho wachezaji wawili iliyowasajili katika kikosi chake cha U20. Wachezaji hao ni Twaha Shekue Ibrahim kutoka Coastal Union 20 na Adeyun Saleh Seif (Oljoro JKT U20).

Nayo Yanga inatakiwa kumfanyia uhamisho mchezaji Rajabu Zahir Mohamed kutoka Mtibwa Sugar U20 wakati Hussein Omari Javu bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Mtibwa Sugar huku kukiwa hakuna vielelezo vyovyote kutoka kwa mchezaji mwenyewe, Mtibwa Sugar au Yanga kama mkataba huo ulivunjwa au umenunulia na klabu anayotaka kuchezea msimu huu.

Wachezaji waliosajiliwa kutoka nje ambao ITC zimefika na pia wana vibali vya kufanya kazi nchini ni Crispine Odula Wadenya kutoka Bandari ya Kenya na Yayo Wasajja Fred Lutimba kutoka URA ya Uganda waliojiunga na timu ya Coastal Union. Pia Mtanzania Hamis Thabit Nyige aliyejiunga na Yanga kutoka Ureno naye tayari na ITC.
Kwa mujibu wa kanuni, wachezaji wote wa ridhaa (wa madaraja ya chini ikiwemo Daraja la Kwanza) wanatakiwa kufanyiwa uhamisho (transfer) kwa klabu husika kujaza fomu za uhamisho na kulipia ada Chama cha Mpira wa Miguu cha Wilaya, Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa na TFF.
Pia TFF inakumbusha kuwa wachezaji wanaotajwa kuwa wamesajiliwa kama wachezaji huru (free agent) ni lazima waoneshwe kama huko walipokuwa mikataba imekwisha au la.

Yanga, Coastal, Ruvu zaua, Simba, Azam zang'ang'aniwa

Yanga iliyoanza kwa kishindo Dar

Ashanti United waliotunguliwa mabao 5-1

JKT Ruvu walioshinda ugenini jijini Tanga

Simba waliong'ang'aniwa na Rhino Rangers

Kagera Sugar waliotoshana nguvu na Mbeya City

JKT Oljoro walilala mabao 2-0 mbele ya Coastal Union
PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara limefunguliwa jioni ya leo kwa kushuhudiwa mabingwa watetezi, Yanga kuikaribisha kwa kipigo cha aibu Ashanti Utd, huku watani zao Simba waking'ang'aniwa ugenini na 'wageni' wa ligi hiyo Rhino Rangers mjini Tabora.
Yanga ikiwa kwenye uwanja wa Taifa iliishindilia Ashanti kwa mabao 5-1, wakati Simba iliyokuwa ikiongoza kwa mabao 2-1 ilijikuta wakizembea na kulazimishwa sare ya 2-2 na Rhino.
Mabao ya Yanga katika mechi hiyo yalifungwa na Jerry Tegete aliyefunga mawili, Simon Msuva, Haruna Niyonzima na Nizar Khalfan.
Mjini Tabora kwenye uwanja wa Ali Hassani Mwinyi, Simba ilipata mabao yake kupitia Jonas Mkude, wakati Rhino walipanda daraja walipata mabao yao kupitia Imani Noel na Soud Kipanga.
Katika mechi nyingine Coastal Union ikiwa jijini Arusha ilionyesha ilivyopania msimu huu kwa kuilaza JKT Oljoro kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Abdul Banda kwa shuti la mita 40  na Mkenya Crispian Odulla.
Coastal walioshinda mabao 2-0
Nao Azam wakiwa ugenini Manungu kuumana na Mtibwa Sugar ililazimisha sare ya 1-1 wakisawazisha bao kwa mkwaju wa penati ya Aggrey Morris baada ya kutanguliwa kufungwa na Juma Liziwa.
Maafande wa JKT Ruvu wakiwa ugenini mjini Tanga waliishindilia Mgambo JKT kwa  mabao 2-0, huku Ruvu Shooting wakipata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Prisons Mbeya.
Nao wageni wengine wa ligi hiyo, Mbeya wakiwa nyumbani uwnaja wa Sokoine walilazimisa sare ya bila kufungana dhidi ya Kagera Sugar inayonolewa na Jackson Mayanja.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena siku ya jumatano kwa michezo kadhaa mabapo Simba itasafiri kuifuata Oljoro jijini Arusha, huku Ruvu ikielekea Mbeya kuwakabilia wenyeji wao Mbeya City.

Friday, August 23, 2013

Polisi Dar wanamnasa msanii Bongo Movie kisa picha za utupu alizopiga na mademu na kusambaza mitandaoni


 
 JESHI la polisi kanda ya Dar es Salaam linadaiwa kumtia mbaroni msanii anaetuhumiwa kupiga picha chafu na wanawake mchanganyiko wakiwema mamiss maarufu na baadae kusambaza kwenye mitandao yote ya kijamii pamoja na kuripotiwa kwenye magazeti mbalimbali
 
Mwandishi wetu amefanikwa  kuzinasa  picha  za  Manaiki  akiwa chini ya ulinzi wa  polisi huku akiwa amevishwa pingu na kurukishwa kichurachura.
 
Manaiki mbaroni-Udaku

Mbongo mwingine anaswa na dawa za kulevya Dubai, watatu wauwawa Afrika Kusini

WAKATI kukiwa na taarifa kwamba watanzania watatu wanaodaiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya kuuwawa kwa kufyatuliwa risasi nchini Afrika Kusini, Tanzani imeendelea kuaibika baada ya Mbongo mwingine kutiwa mbaroni akiingiza 'unga' Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE)

Mtanzania huyo aliyenaswa umangani, inaelezwa lidakwa tarehe 19/8/2013 baada ya Polisi mjini Sharjah na wale wa Dubai kuwakamata watu watano mmoja akiwa ni raia wa Tanzania.
Watuhumiwa hao walinaswa na kilo kilo 19 za heroin na kilo 4 za bangi na kwa mujibu wa sheria za nchi hiyo wanaonaswa na 'unga' adhabu yake ni kifungo cha maisha
Isome mwenyewe habari juu ya aibu hiyo nyingine kwa Tanzania ambayo imekuja huku kukielezwa Watanzania watatu wanaohusika na 'unga' wameuwawa Afrika Kusini kwa kufyatuliwa risasi.

The anti-narcotics department of police and other police teams have tracked down and arrested a five-strong gang accused of smuggling a large amount of drugs into the country.The group members, including three Emirati men, one man from the Comoros Islands and another from Tanzania, were arrested and charged with smuggling and possession of 19kg of heroin and four kilograms of marijuana.
The group is accused of smuggling drugs in order to sell them.
The arrest was made after the anti-narcotics department was able to gather information through confidential sources about a group of people who were in possession of a large amount of drugs.

Sharjah Police, in collaboration with Dubai Police and the anti-narcotics departments of the Ministry of Interior and Ajman Police, were able to track down two of the offenders who were in possession of two kilograms of marijuana along with 150 grams of heroin.

The other three suspects were tracked down and arrested soon after, along with a larger quantity of drugs that were found buried in the desert in Sharjah and Ajman.

Major General Humaid Mohammad Al Hudaidi, commander in chief of Sharjah Police, said that collaboration of all the police teams in the UAE led to tracking down of the suspected drug smugglers and distributors.

He said that through the use of strategic tools and sources, police were able to disclose the group’s plan to distribute and sell the drugs to young people in the country.
source -jamii forums

Hawa ndiyo waombaji Uchaguzi Mikuu TFF, Wambura 'aingia' mitini

Athuman Nyamlani aliyejitosa kwenye Urais
Jamal Malinzi naye yumo
 Na Boniface Wsambura
KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imebandika rasmi kwenye ubao wa matangazo majina ya waombaji uongozi kwenye uchaguzi wa TFF na Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board) ili kutoa fursa kwa pingamizi.

Kipindi cha pingamizi kinaanza kesho (Agosti 24 mwaka huu) hadi sas 10 kamili jioni ya Agosti 26 mwaka huu ambapo waweka pingamizi wanaruhusiwa kupitia taarifa za wale wanaokusudia kuwawekea pingamizi kabla ya kuwasilisha pingamizi husika.

Kwa mujibu wa tangazo la uchaguzi, Agosti 27 hadi 29 mwaka huu ni wawekaji pingamizi na wawekewa pingamizi kufika mbele ya Kamati ya Uchaguzi kwa ajili ya kusikiliza pingamizi.

Waombaji kuwania uongozi katika TFF ambao majina yao yamebandikwa ni Athuman Jumanne Nyamlani, Jamal Emil Malinzi, Omari Mussa Nkwarulo na Richard J. Rukambura (urais). Nafasi ya Makamu wa Rais ni Imani Omari Madega, Ramadhan Omari Nassib na Walace John Karia.

Walioomba nafasi za ujumbe kuwakilisha kanda ni Kanda Namba Moja (Kagera na Geita) ni Abdallah Hussein Mussa na Kaliro Samson. Kanda Namba Mbili (Mara na Mwanza) ni Jumbe Odessa Magati, Mugisha Mujwahuzi Galibona, Samwel Nyalla na Vedastus Kalwizira Lufano.

Kanda Namba Tatu (Shinyanga na Simiyu) ni Epaphra Amana Swai, Mbasha Matutu Mong’ateko na Stanslaus Haroon Nyongo. Kanda Namba Nne (Arusha na Manyara) ni Ally Mtumwa, Elley Simon Mbise na Omari Walii Ali.

Kanda Namba Tano (Kigoma na Tabora) ni Ahmed Idd Mgoyi na Yusuf Hamisi Kitumbo. Kanda Namba Sita (Katavi na Rukwa) ni Ayoub Nyaulingo, Blassy Mghube Kiondo, Nazarius A.M. Kilungeja. Kanda Namba Saba (Iringa na Mbeya) ni Ayoub Shaibu Nyenzi, Cyprian Charles Kuyava, David Samson Lugenge, Elias Lusekelo Mwanjala, Eliud Peter Mvella na John Mwachendang’ombe Kiteve.

Waombaji wa Kanda Namba Nane (Njombe na Ruvuma) ni James Patrick Mhagama, Kamwanga Rajabu Tambwe na Stanley William Lugenge. Kanda Namba Tisa (Lindi na Mtwara) ni Athuman Kingome Kambi, Francis Kumba Ndulane na Zafarani Mzee Damoder.

Kanda Namba Kumi (Dodoma na Singida) ni Charles Komba, Hussein Zuberi Mwamba na Stewart Ernest Masima. Kanda Namba 11 (Morogoro na Pwani) ni Farid Salum Mbarak, Geoffrey Irick Nyange, Juma Abbas Pinto, Riziki Juma Majala na Twahil Twaha Njoki.

Wanaowania kuteuliwa kugombea kupitia Kanda Namba 12 (Kilimanjaro na Tanga) ni Davis Elisa Mosha na Khalid Abdallah Mohamed wakati Kanda Namba 13 (Dar es Salaam) ni Alex Chrispine Kamuzelya, Muhsin Balhabou, Omar Isack Abdulkadir, Shaffih Dauda Kajuna na Wilfred Mzigama Kidao.

Kwa upande wa TPL Board waliotangazwa kuomba kuwania uongozi wa juu ni Hamad Yahya Juma (Mwenyekiti) na Said Muhammad Said Abeid (Makamu Mwenyekiti).

Wajumbe wa Kamati ya Uendeshaji ni Kazimoto Miraji Muzo, Michael Njunwensi Kaijage, Omari Khatibu Mwindadi, Salum Seif Rupia na Silas Masui Magunguma.

Mmoja wa wagombea machachari aliyewahi kuongoza Shirikisho hilo enzi za FAT, Michael Wambura hajajitokeza safari hii kuwania nafasi yoyote bila kufahamika kitu gani kilichomkuta.

Golden Bush Veterani, Mwanza United kuvaana Jumapili


Kikosi cha Golden Bush
WAKALI wa soka la jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani Jumapili inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na Mwanza United inayoundwa na wakali wa zamani kama George Masatu.
Kwa mujibu wa msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico', pambano hilo litachezwa asubuhi kwenye uwanja wa Kines, maarufu kama St James Park.
Ticotico alisema kikosi chao kipo imara kwa ajili ya pambano hilo ambalo Mwana Utd inatarajiwa kusheheni wakali kama Masatu, Benjamin Magadula, Aaron Nyanda, George Nyanda Emmanuel Switta na wengineo.
"Baada ya kutoa vipigo kwa wapinzani wetu wengine wakifikia hatua ya kugoma kucheza nasi, Jumapili tutavaana na Mwanza United hivyo mashabiki waje waone soka la kutakata," alisema.
Ticotico alisema mashabiki wake washuhudie beki kisiki, Masatu akatavyokuwa na kazi ya kuwazuia washambuliaji hatari wa Golden Bush ambayo inaundwa na nyota wa zamani wa Simba, Yanga na Taifa Stars pamojana wakongwe wanaoendelea kucheza sasa.

Tiketi za Elektroniki kutumika mzunguko wa nne

Rais wa TFF leodger Tenga
Na Boniface Wambura
TIKETI za elektroniki zitaanza kutumika katika mzunguko wa nne wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) utakaoanza Septemba 18 mwaka huu. Tayari benki ya CRDB ambayo ndiyo ilishinda tenda hiyo imeshakamilisha ufungaji wa vifaa kwa ajili ya matumizi ya tiketi hizo katika viwanja vyote.

Hivi sasa Serikali ambayo ndiyo inamiliki Uwanja wa Taifa, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pamoja na CRDB zinashughulikia mfumo wa tiketi hizo kwenye uwanja huo ambao ndiyo ulikuwa haujakamilika kwa matumizi katika upande huo.

Mfumo (system) iliyoko kwenye uwanja huo inapishana na ule utakaotumiwa na CRDB, hivyo pande husika zinashughulikia suala hilo ili mifumo hiyo iweze kuingilia.

Pia mashine za kuchapia (printer) kwa ajili ya tiketi ambazo CRDB wameziagiza kutoka nje ya nchi zinatarajiwa kuwasili mwishoni mwa mwezi huu.

Hivi sasa CRDB inashughulikia ufungaji wa vifaa vya matumizi ya tiketi za elektroniki iwemo turnstiles kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ambao mwanzoni hakuwemo kwenye mpango huo kutokana na Mkoa wa Tabora kutokuwa na timu ya Ligi Kuu.

Kivumbi cha Ligi Kuu kuanza kesho, Yanga, vijana wa Ashanti hapatoshi Dar

Mabingwa watetezi Yanga watakaoanza kibarua dhidi ya Ashanti United iliyorejea ligi Kuu tena
Na Boniface Wambura
PAZIA la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2013/2014 litafunguliwa kesho (Agosti 24 mwaka huu) katika viwanja saba tofauti ambapo mabingwa watetezi Yanga wakianza kutetea ubingwa wao kwa kuikaribisha Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Azam ya Dar es Salaam na wenyeji Mtibwa Sugar. Oljoro JKT itaikaribisha Coastal Union kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha.

Mgambo Shooting itaoneshana kazi na JKT Ruvu ambayo hivi sasa iko chini ya Kocha Mbwana Makata. Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Rhino Rangers itakwaruzana na Simba katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Mbeya City iliyopanda VPL msimu huu itapimana ubavu na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya huku Ruvu Shooting ikiialika Mabatini, Mlandizi timu ya Tanzania Prisons kutoka Mbeya.

Mzunguko wa pili wa ligi hiyo utachezwa Agosti 28 mwaka huu. Baada ya hapo ligi itasimama kupitisha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Gambia na Tanzania (Taifa Stars) itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu jijini Banjul. VPL itaingia mzunguko wa tatu Septemba 14 mwaka huu.

Kumekucha BSS, Fainali zake kufanyika Nov.17

Madam Ritha akiwa na mshindi wa mwaka jana Walter Chilambo

FAINALI za mashindano ya kusaka vipaji vya kuimba ya Epiq Bongo Star Search (EBSS) mwaka huu zitafanyika Novemba 17 jijini Dar es Salaam, waandaaji walisema jana.
Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions, Ritha Poulsen, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa wamejipanga kuboresha mashindano hayo na wadau watarajie kushuhudia fainali zilizoandaliwa katika kiwango cha kimataifa.
Alisema kuwa awali walipata washiriki 50 lakini sasa baada ya kuwachuja wamebaki 20 ambao wataingia kambini na kupewa mafunzo mbalimbali ya muziki kabla ya kuwachuja na kubaki wanane watakaoingia fainali.
“Lengo la kuanza kambini mapema ni kuwapa fursa washiriki kujifunza zaidi vitu muhimu katika muziki na hii itawasaidia kuboresha vipaji vyao," alisema mratibu huyo.
Alisema kuwa washiriki hao waliopatikana wametoka katika mikoa sita ya Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar.
Naye mshindi wa shindano hilo kwa mwaka jana, Walter Chilambo, aliwataka vijana kuondoa aibu ili wajiandae kutimiza ndoto zao za maisha.
“Vijana wengi wamejitokeza msimu huu ila wameonekana kuwa na aibu baada ya kuwaona majaji, hali hii si nzuri na huwezi kufikia malengo," alisema mshindi huyo.
Naye Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan, alisema wamejipanga kuhakikisha shindano hilo linakuwa la aina yake mwaka huu kupitia udhamini wa kampuni yake.
Alisema pia bado washiriki wanaendelea kusailiwa kupitia namba ya simu  0901551000 au kutuma ujumbe mfupi kwenda 15530 kama ilivyokuwa kwa mshiriki Meninah Abdulkarim aliyepatikana kwa njia huyo wakati wa mchakato wa mwaka jana.

Mtikisiko katia Dansi! Mzee Gurumo ang'atuka kwenye muziki

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi wa bendi ya Msondo Ngoma, Mzee Muhidin Gurumo, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wake wa kustaafu rasmi kazi ya muziki aliyoifanya kwa muda wa miaka 53 sasa. Gurumo alitoa kauli hiyo leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Picha na Magreth Kinabo.
************************************
Na Jennifer Chamila, Maelezo.
MWANAMUZIKI mkongwe wa bendi ya Msondo Ngoma Mzee Muhidin Gurumo amestaafu rasimi kazi ya muzika alioifanya kwa muda wa miaka 53.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Mzee  Gurumo mwenye umri wa miaka 73 amesema ameamua kustaafu kazi hiyo kwa hiari yake mwenyewe kutokana na umri wake kuwa mkubwa.
“Muziki kwangu umekuwa kama asili yangu na kazi yangu lakini nimeamua kustaafu kutokana na umri wangu na nitabaki kuwa mshauri tu kwa mwanamuziki yeyote atakayetaka ushauri wangu,”alisema  Mzee Gurumo.
Pamoja na kufanya kazi ya muziki Gurumo alisema kuwa hakupata mafanikio makubwa zaidi ya kujenga nyumba anayoishi na familia yake.
 “Mimi  nimeimba kwa muda mrefu sana lakini hata baiskeli sina,”alisema Mzee Ngurumo. Hata hivyo alisema  nashukuru kuwa ana nyumba ya kuishi na familia.
Vilevile Mzee Gurumo amewaasa vijana kuwa wabunifu na kuupenda mziki wa zamani kwani ndio chimbuko la bongofleva na kuwashauri wanamuziki wa sasa kuwa wavumilivu kukaa muda mrefu kwenye bendi moja ili hata wanapoondoka mchango wao uthaminiwe.
 Mzee   Gurumo  ambaye ana mke na watoto wanne alisema kuwa katika maisha yake ya muziki alifanikiwa kutunga nyimbo 60,000 na anavutiwa zaidi na mwanamziki Hussein Jumbe na Hassani Lehan Bichuka na kwa wanamuziki wa kizazi kipya anavutiwa na Nassibu Abdul ’Diamond’. 
Mwanamuziki huyo mkongwe alianza kufahamika katika tasnia ya muziki wa dansi kwenye miaka ya 1960 ambapo mwaka 1964 alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa bendi ya Nuta Jazz na Mlimani Park.
Alidumu na Mlimani Park mpaka mwaka 1985 na kuhamia Safari Sound aliyofanya nayo kazi mpaka mwaka 1990 na kujiunga na Msondo Ngoma mpaka sasa alipoamua kutangaza rasmi kustaafu kazi hiyo ya Kimuziki.

Twanga Pepeta, ROMA kupamba tamasha la Gym kesho K'Nyama


KATIKA kuhakikisha Watanzania wanakuwa na afya bora, kinywaji kisicho na kilevi cha Vita Malt, kimeandaa bonanza maalumu litakalowashirikisha wafanya mazoezi na litakalofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Vinywaji visivyo na Vileo katika Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Consolata Adam alisema, wameamua kuandaa bonanza hilo ili kuwakutanisha pamoja wafanya mazoezi wote, ambao mara nyingi wanafanyia katika vituo maalumu (gym).

Consolata alisema, bonanza hilo la aina yake kwa Dar es Salaam litafanyika katika Viwanja vya Posta vilivyopo Kijitonyama kuanzia saa 12 asubuhi hapo kesho (Jumamosi).

“Tumeamua kuandaa bonanza linalowakutanisha wanamichezo mbalimbali hasa wafanya mazoezi ili kuweza kukutana na kufanya mazoezi kwa pamoja.

“Siku hiyo katika Viwanja vya Posta kutakuwa na gym kumi na mbili zilizo maarufu ambazo zitashiriki na kutakuwa na wakufunzi kumi ambao wataongozwa na mkufunzi wa kimataifa SAAS,” alisema, huku akidai mtu anatakiwa kwenda tu kwani mazoezi hayo yatakuwa bure.

Alisema, lengo kuu kuu la bonanza  ni kuhamasisha jamii nzima kutambua umuhimu wa kufanya mazoezi ili kujenga afya bora za miili yao na pia kujenga umoja imara wa gym zilizopo nchini.

Consolata alisema, katika kuhakikisha bonanza hilo linakuwa bora na la kufana jumla ya gym kumi na mbili zitashiriki ambazo ni Better Life, Genessis ya Kijitonyama, Segerea Gym, Rio Gym,Genessis ya Kimara, Azula ya Mikocheni na Serena Gym.

Alisema pia baa zilizoshinda katika kuchoma nyama katika mashindano yaliyofanyika hivi karibuni za Fyatanga ya Tegeta na Kisuma Bar ya Temeke, zitaonyeshana umwamba kwa kuchoma nyama bomba kwa kipindi chote hicho.

“Tumeweka burudani za kila aina kwani kutakuwa na michezo mbalimbali ya kufurahisha kama soka, netiboli, kuvuta kamba, kukimbiza kuku, Sehemu za watoto kuchezea pia na zawadi nyingi toka Vita Malt zitakuwepo.”

Naye Meneja Mawasiliano na Mahusiano wa TBL, Edith Mushi alisema mbali na hayo kutakuwa na burudani mbalimbali toka kwa bendi African Stars ‘Twanga Pepeta’ na msanii mkali wa Hip hop, Roma Mkatoliki sambamba na burudani nyingine nyingi kwa kipindi chote cha tamasha.

“Hii ni siku ya familia napenda kuwajulisha watanzania wote na wapenda michezo kote nchini kuwa waje mapema na familia zao siku ya Jumamosi, hakutakuwa na kiingilio chochote na vinywaji vyote toka TBL vitakuwepo.

“Lakini pia watu wa kawaida na wa rika zote siku hiyo hakutakuwa na kikwazo chochote cha kufanya mazoezi, kwani ni bure kabisa, hivyo nawashauri tufike kwa pamoja ili tuweze kupata pia ushauri mbalimbali juu ya kupunguza uzito na aina ya mazoezi yanayotakiwa,” alisema.

Vita Malt ni kinyaji kinachozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

Wednesday, August 21, 2013

Kimenuka! 3 Pillars ya Nigeria yatelekezwa, kisa deni ya Sh Mil. 17 la hoteli waliyohifadhiwa..yadaiwa walikuja kwa 'dili' nyingine kabisa....!

  •  
  • MFADHILI ALIYEWALETA AWATELEKEZA
  • YADAIWA WALIKUJA KUFANYA BIASHARA HARAMU
  • BAADA YA MIANYA KUZIBWA - MFANYABIASHARA ALIYEWALETA AWATEMA
Imefahamika kwamba klabu ya 3 Pillars ya Nigeria ipo katika hali ngumu sana kimaisha jijini Dar es Salaam baada ya mtu mmoja aliyeleta timu hiyo nchini ambaye ana makazi Tanzania na huko Falme za Kiarabu kutokomea na kuitelekeza timu hiyo. 

 Kwa mujibu wa chanzo cha habari  hii - mtu ambaye amekuwa akihusishwa na kuileta timu hiyo nchini kwa ajili ya mechi za kujipima nguvu - ni kwamba 3 Pillars waliletwa nchini na mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya kiarabu kwa madhumuni ya kufanya biashara haramu na ndio maana timu hiyo ilikuwa haichukui hata shilingi katika mechi mbili za kirafiki ilizocheza hapa nchini na Klabu ya Yanga pamoja na Coastal Union kwa kuwa walikuwa wanapewa kila kitu na mfanyabiashara aliyewaleta nchini.

Lakini kutokana na hali ya ulinzi kuimarika nchini kutokana na mfululizo wa watanzania kukamatwa na wakiwa wamebeba baishara haramu - kazi ambayo 3 Pillars walitumwa kuja kuifanya Tanzania na mfadhili wao ikawa imeingia mdudu, hivyo mfanyabaishara huyo ameitelekeza timu hiyo ya Nigeria katika hoteli ya Itumbi iliyopo Magomeni Mwembechai ambapo mpaka kufikia siku wanarudi kucheza mechi dhidi ya Yanga tayari walikuwa na deni la millioni 12. Mpaka hivi sasa timu hiyo inadaiwa zaidi ya millioni 17 wakiwa hawajui namna ya kulipa deni hilo.

Mtandao huu uliwasiliana na meneja ya hoteli ya Itumbi na alithibitisha ni kweli klabu hiyo ya 3 Pillars inadaiwa deni hilo: "Ni kweli kabisa hawa jamaa tunawadai kiasi cha millioni 17, mpaka kufikia jana walikuwa hawajatupa muelekeo wa namna watakavyolipa deni hili. Mmiliki wa Hoteli jana alikuwa na kikao na viongozi wao wametoa ahadi kwamba wanaongea na ubalozi wao ili kuweza kupata msaada wa kulipa deni hilo waweze kuondoka nchini na kurudi kwao. Kwa sasa imebidi tusiwape huduma ya chakula ili kutokuongeza deni, hivyo haifahamiki wanakula au vipi," alisema meneja wa hoteli hiyo.

Wakati huo huo imefahamika kwamba ulifanyika mchezo mchafu katika kuzuia 3 Pillars isicheze michezo ya kujipima nguvu Tanzania na baadhi ya viongozi wa TFF kwa maslahi yao binafsi - yanayohusiana na uchaguzi mkuu wa TFF

...........................itaendelea 
 
SHAFII DAUDA 

Sifa zamtokea puani Diamond...Dk Mwakyembe ataka achunguzse ukaribu wake na 'wauza unga'

Diamond
BAADA ya msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya nchini Diamond Platnum kutajwa kujihusisha na mtandao wa dawa za kulevya waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe atoa agizo msanii huyo aanze kuchunguzwa.
Msanii huyo leo ameripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kujihusisha na dawa za kulevya.
Uchunguzi huo utahusisha kuangalia vyanzo vyake vya mapato kama vinaendana na matumiz yake, wakati inasemekana  akaunti za diamond ambazo zinaonekana kubwa mno kulinganisha na kipato cha kawaida cha wasanii.
Hali hiyo imetokana na vugu vugu la kujaribu kuisafisha tanzania kutokana na kushamiri kwa madawa ya kulevya limefikia hatua nzuri na ya kipekee. Dk Mwakyembe amejitosa haswa kupambana na wauza unga, moja kati ya majina yanayosemekana ya wauza unga yanayodaiwa yapo ktk kitengo internal intelligency lipo jina la msanii Diamond.
Inasemekana Diamond ana urafiki wa karibu na mabosi wa Masogange, ambao wengine wapo nchini Afrika Kusini, kamera za cctv za uwanja wa wa ndege wa kitaifa JNIA zimekuwa zikionesha ukaribu wa Diamond na wale watu waliotajwa na Waziri Mwakyembe kuwa walimsaidia Masogange kupitisha mzigo.
Pia safari za kimuziki sehemu mbalimbali duniani ambazo nyingi hupangwa/kutafutwa na vigogo wa madawa ya kulevya waliopo tanzania na wale waliopo Afrika Kusini .
Wakati pia sasa serikali inajaribu kuchunguza akaunti za diamond ambazo zinaonekana kubwa mno kulinganisha na kipato cha kawaida cha wasanii. 
Uchunguzi bado unaendelea, lakini Diamond amekanusha kuhusika na sembe.
 
Chanzo:Pro24 

Hatimaye Abdi Kassim 'Babi' atua KMKM

Abdi Kassim 'Babi'
KIUNGO mshambuliaji nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, aliyekuwa akiichezea Azam katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita, Abdi Kassim 'Babi' au Ballack wa Ugunja' amemwaga wino wa kuichezea mabingwa wa Zanzibar KMKM.
Babi ambaye alikanusha taarifa za kutemwa na Azam na badala yake kueleza kwamba baada ya mkataba wake kumalizika aliamua kuachana na timu hiyo, ametgoa taarifa kupitia akaunti yake ya FB kwamba kwa sasa yeye ni mali ya KMKM baada ya kumwaga wino na kufurahi kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.
Mkali huyo aliyewahi kucheza soka la kulipwa Vietnam alisema kutua kwake KMKM kumempa faraja kutokana na kufanya kazi chini ya kocha mzoefu nchini, Ali Bushiri.
Ujumbe wake kwa mafans wake uliotumwa na mkali huyo mwenye mashuti makali unasomeka kama hivi hapo chini:
"Hi nyote ..Nashukuru Mungu mzima wa afya ..nimesaini mkataba na kmkm mabingwa wa soka zanzibar na timu inayo shiriki mashindano ya kimataifa na mashindano mbali mbal ..ikiongozwa na coach mzoefu na mwenye ujuzi wa hali ya juu..ali bushir .so natowa shukrani dha dhati kwa uwongozi wa kmkm kwa kumaliza soezi la usajil kati yangu.na wao na napenda kuwashukuru wote wapenzi wa kmkm ..kwa kuniunga mkono bamoja na uwongozi wa juu na nafurahi zaid kwa vile nipo nyumbani ..na famly yangu na biashara zangu za hapa na pale..asanten sana..watanzania wote .."
 

Arsenal Wenger asalimu amri, atangaza kuingia sokoni kusaka nyota

http://images.football365.com/12/11/800x600/Manchester-United-v-Arsenal-Arsene-Wenger-pa2_2855230.jpg 
LONDON, England
BAADA ya kuona mambo yanamwendea vibaya na hana njia nyingine ya kunusuru ajira yake Arsena, Kocha Arsene Wenger ametangaza kurejea sokoni kusaka wachezaji akitumia akiba aliyonayo ya Pauni Milioni 65.

Wenger ambaye kipigo cha mabao 3-1 toka kwa Aston Villa kimemweka pabaya mbele ya mashabiki wa klabu hiyo ya Emirates alitangaza uamuzi huo usiku wa kuamkia juzi.
 
Kocha huyo alisema kuwa bado anatafuta ufumbuzi mwingine na kwamba atazitumia fedha hizo kwa ajili ya kusaka nyota wengine kwenye michuano hiyo ya Ligi Kuu ya England.
 
Kwa sasa Gunners imeshatangaza dau la pauni milioni 12 ikimsaka kiungo wa timu ya Taifa ya Ufaransa, Yohan Cabaye dau ambalo limekataliwa na  Newcastle ambayo inataka dau hilo liongezeke zaidi.

Hata hivyo kwa mujibu wa  Starsport klabu hiyo iliyokumbwa na mgogoro inawawinda nyota wengine watatu ambao huenda wakaigharimu pauni hizo milioni 65.

Wanaotajwa kuwa mawindo ya timu hiyo ni nyota wawili wa timu ya  Swansea, Michu na  Ashley Williams pamoja na nyota wa Manchester City, Micah Richards, ambaye mwenyewe binafsi anataka kujiunga na  Gunners.

Awali kabla ya kutangaza nyota hao, Arsenal  iliwahi kujaribu kurusha karata yake kuwashawishi nyota wengine kama  Luis Suarez, Wayne Rooney na  Gonzalo Higuain,lakini ikashindwa na badala yake kocha  Wenger akajikuta akikaliwa kooni na mashabiki kwa kushindwa kutumia fedha msimu huu.

Mfaransa huyo tayari ameshaomba radhi kwa mashabiki kufuatia kipigo cha  Aston Villa aliwatumia ujumbe wa barua pepe uliosomeka: 

"Tunataka mashabiki wetu wawe na furaha. Unaposhindwa kufikia mafanikio hayo ni lazima ujihisi mnyonge na mwenye kuchanganyikiwa. Watu wanadhani hatutaki kutumia fedha ila tunataka kuzitumia."

Waliochinja na kumnyofoa mtu viungo wanaswa Simiyu

Kamanda Msangi
Na Samwel Mwanga, Simiyu
JESHI la Polisi mkoani Simiyu limefanikiwa kuwatia mbaroni watu wawili wanaotuhumiwa kwa mauaji ya kikatili ya kumchinja mtu mmoja, kunyofoa na kumkata sehemu za siri na nyayo za mguu wake wa kushoto na kutoweka navyo.
Watu hao wanasadikiwa pia kushiriki katika mauaji ya kijana Mabula Hamisi (37) ambaye hapo awali hakufahamika jina, makazi wala umri wake Agosti 23, 2012 majira ya saa 2 usiku katika Kijiji cha Ikinabushu, Kata ya Gilya, Tarafa ya Dutwa, Wilaya ya Bariadi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Kamishina Msaidizi, Salumu Msangi aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Bamba Ndubiga (27), mkazi wa Kijiji cha Ngalamila, Wilaya ya Bariadi, na Marando Shaban (26) mfanyabiashara wa Kijiji cha Isuyu, Tarafa ya Dutwa pia wilayani humo.
Watuhumiwa wote hao walikamatwa juzi baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa ndio walikuwa na Mabula siku ya mwisho wakiwa wamepakizana katika pikipiki moja.


58 WAJITOSA UCHAGUZI TFF, BODI YA LIGI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4gRKoRzq365Nfvufupjmf66bFRq2WMCeqE3ufWX2EpKPbkI8uqn-u2DI0HfR82OR1wqctpyq68-QoUi3U-Wk7Z4Jp8gi7t3HJQohnWQ-A0Z_V6U2ENYrFSPHi1tMDtLGa3bnt3O_kcYs/s640/75502_562847213733654_1058456517_n.jpg
Jamal Malinzi kajitosa tena
Na Boniface Wambura
JUMLA ya wanamichezo 58 wamerusha fomu kuomba kuteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na ule wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board) utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Kwa upande wa TFF waliorejesha fomu kwa upande wa urais ni Athuman Jumanne Nyamlani, Jamal Emil Malinzi, Omari Mussa Nkwarulo na Richard Rukambura. Nafasi ya Makamu wa Rais wamejitokeza Imani Omari Madega, Nasib Ramadhan na Walace Karia.

Walioomba nafasi za ujumbe kuwakilisha kanda mbalimbali ni Abdallah Hussein Mussa, Kaliro Samson, Jumbe Odessa Magati, Mugisha Mujwahuzi Galibona, Vedastus Kalwizira Lufano, Samwel Nyalla, Epaphra Amana Swai, Mbasha Matutu Mong’ateko, Stanslaus Haroon Nyongo, Ally Mtumwa, Elley Simon Mbise na Omari Walii.

Ahmed Msafiri Mgoyi, Yusuf Hamisi Kitumbo, Ayoub Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius Kilungeja, Ayoub Shaib Nyenzi, Cyprian Charles Kuyava, David Lugenge, Elias Mwanjala, Eliud Peter Mvela, John Mwachendang’ombe Kiteve, James Patrick Mhagama, Kamwanga Rajabu Tambwe na Stanley William Lugenge.

Athuman Kambi, Francis Kumba Ndulane, Zafarani Damoder, Charles Komba, Hussein Mwamba, Stewart Ernest Masima, Farid Salum Nahdi, Geoffrey Nyange, Riziki Majala, Twahil Twaha Njoki, Davis Elisa Mosha na Khalid Abdallah Mohamed.

Wengine ni Alex Chrispine Kamuzelya, Juma Abbas Pinto, Muhsin Balhabou, Omar Isack Abdulkadir, Shaffih Dauda Kajuna na Wilfred Mzigama Kidao.

Kwa upande wa uchaguzi wa TFF mwombaji ambaye hakurudisha fomu ni Venance Mwamoto pekee.

Kwa upande wa TPL Board waliojitokeza kuwania uongozi wa juu ni wawili tu; Hamad Yahya Juma (Mwenyekiti) na Said Muhamad Said (Makamu Mwenyekiti).

Walioomba nafasi za ujumbe wa TPL Board ni Kazimoto Miraji Muzo, Michael Njunwensi Kaijage, Omari Khatibu Mwindadi, Salum Seif Rupia na Silas Masui Magunguma.
                         

Ramadhani Shauri, Cosmas Cheka kuwania mkanda wa UBO

Bondia Ramadhani Shauri kushoto akisaini mkataba wa kucheza ubingwa wa UBO utakaofanyika tarehe 27 mwezi wa 10 jijini Dar es salaam na mpinzani wake kushoto Cosmas Cheka wa Morogoro wengini ni Promota Kaike Silaju na Makamu Mwenyekiti wa PST Aga Peter nyuma
Bondia Cosmas Cheka wa Morogoro  akisaini mkataba wa kucheza ubingwa wa UBO utakaofanyika tarehe 27 mwezi wa 10 jijini Dar es salaam na mpinzani wake  Ramadhani Shauri kushoto wengini ni Promota Kaike Silaju na Makamu Mwenyekiti wa PST Aga Peter nyuma pamoja na kocha wa Cheka Power Iranda  
Promota wa Mpambano wa Ubingwa wa UBO Kaike Siraju katikati akiwanyoosha mikono juu mabondia Ramadhani Shauri kushoto na Cosmasi Cheka watakaopigana tarehe 27 jijini Dar es salaam
Bondia Ramadhani Shauri akizungumza na waandishi wa habari kushoto ni kocha wake Christopher Mzazi na Promota Kaike Siraju
Bondia Ramadhani Shauri akizungumza na waandishi wa habari
Bondia Cosmas Cheka akiongea na waandishi wa habari