STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 17, 2013

Sheikh Ponda akwama kupata dhamana Morogoro



  Sheikh Ponda Akishuka kwenye basi la Magereza tayari kuingia Mahakamani Kusikiliza kesi yake inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro.
Sheikh Ponda anashtikiwa katika Mahakama hiyo akikabiliwa na Mashtaka Matatu ambayo inadaiwa aliyatenda Mkoani Morogoro katika Mkutano hadhara mwezi uliopita.
Kiongozi huyo wa umma wa Kiislam Tanzania amenyimwa dhamana na hivyo kurejeshwa tena rumande mpaka kesi yake itakaposomwa tena Oktoba  Mosi.






 Sheikh Ponda akiwa Chini ya Ulinzi Mkali wakati akiingia Mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro.




 
Sheikh Issa Ponda akiingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro leo kusikiliza kesi yake






 Wafusi wa Sheikh Ponda wakiwa wakiwa mahakamani leo kusikiliza kesi ya Kiongozi wao iliyokuwa imetajwa mahama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro.


Ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa mahakamani leo wakati kesi hiyo ikiendelea mjini Morogoro.

Newz Alert: Shule ya Ilboru yafungwa, kisa...!

Waziri Majaliwa alipowahi kwenda kuutuliza mgogoro wa wanafunzi wa Ilboru mwaka jana
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa, serikali imeamua kuifunga kwa muda usiojulikana Shule Maalum ya vipaji ya Ilboru ya jijini Arusha, baada ya kuwepo kwa tishio la kuchomwa moto kutokana na mgogoro uliodumu kwa muda mrefu shuleni hapo.
Imedokezwa wanafunzi wapatao wanne wanahojiwa kutokana na tishio hilo huku wengine karibu 800 wamerudishwa makwao mpaka watakapotangaziwa vinginevyo.
Tangu mwaka jana shule hiyo imekuwa na mgogoro baina ya wanafunzi na uongozi wake kiasi Naibu waziri wa Tamisemi (Elimu), Kassim Majaliwa kulazimika kuingilia kati, lakini hali haijatengemaa hadi hivi karibuni tena kiliponuka tena.

Msiba tena! Prince Ahmed Mgeni hayupo nasi afariki Zenji

Prince Ahmed Mgeni

TASNIA ya sanaa imeendelea kupata misiba baada ya muimbaji nyota wa zamani wa Zanzibar Stars, Prince Ahmed Mgeni kufariki dunia visiwani Zanzibar na jioni hii alitarajiwa kuzikwa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka visiwani humo zinasema kuwa, marehemu Mgeni aliyetamba na kuziba nafasi ya Mzee Yusuf alipojiengua katika kundi hilo na kuunda Jahazi, alifariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja alipokuwa amelazwa.
Taarifa za awali zinasema marehemu alikuwa akisumbuliwa na kifua kikuu (TB) na kulazwa hospitalini hapo kwa muda mrefu.
Mpaka mauti yalipomkuta jana marehemu Mgeni alikuwa mwanamuziki wa kundi la Zanzibar Njema Taarab.
Kifo cha msanii huyo ni muendelezo wa misiba katika tasnia ya sanaa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana ambapo imeshuhudiwa waigizaji na waimbaji wakipoteza uhai kwa sababu mbalimbali ikiwamo ajali na maradhi. Mungu aiweze mahali pema peponi roho ya marehemu Ahmed Mgeni na MICHARAZO inawapa pole familia, ndugu, jamaa na rafiki wa msanii huyo pamoja na wadau wote wa sanaa Tanzania. 

Sunday Kayuni kuhudhuria kozi ya wakufunzi CAF

Sunday Kayuni
MKURUGENZI wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Sunday Kayuni atashiriki warsha ya wakufunzi wa makocha wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itakayofanyika kuanzia Oktoba 22-24 mwaka huu.

Warsha hiyo iliyoandaliwa na CAF kwa ajili ya wakufunzi wake itafanyika nchini Cameroon. Wakufunzi 18 wa CAF kwa upande wa makocha watahudhuria warsha hiyo.

Madhumuni ya warsha hiyo ni kuainisha majukumu yao, kubadilishana uzoefu. Pia kuwapa methodolojia mpya ya ufundishaji na muongozo kuhusu mfumo wa leseni za makocha ambao watautumia katika nchi wanazotoka.

Mbali ya Kayuni Tanzania, wakufunzi wengine ni Ahmed Babiker (Sudan), Amadou Shaibu (Nigeria), Boy Bizzah Mkhonta (Swaziland), Duodu Fred Osam (Ghana), Edussei Anthony (Ghana), Fathi Nossir (Misri), Faouzy Altaisha (Sudan) na Fran Hilton Smith (Afrika Kusini).

Wengine ni Francis Oti-Akenteng (Ghana), Honour Janza (Zambia), Kasimawo Laloko (Nigeria), Mahmoud Saad (Misri), Paul Hamilton (Nigeria), Serame Letsoaka (Afrika Kusini), Shawky Abdel Shafy (Misri), Thondoo Govinder (Mauritius) na Ulric Mathiot (Seychelles),

Tembo Mtoto, nyota iliyozimika ghafla katika ngumi za kulipwa

Bondia Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' (kulia) akichuana na Fadhili Awadh 'Mnyama Chui' katika moja ya mapambano yake enzi za uhai wake.
 Na Magendela Hamisi
SEPTEMBA 12 tasnia ya mchezo wa masumbwi ilimpoteza bondia mahili wa uzito wa kilo kilo 66, Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' (23), akiwa mazoezini kujindaa na pambano lake la ubingwa wa Taifa dhidi ya Abdallah Mohammed 'Prince Nassib'.
Pambano hilo lilipangwa kufanyika Oktoba mwaka huu, jijini Dar es Salaam na kusimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), lilionekana kuvuta hisia za mashabiki wengi.
Bondia huyo mahili ambaye jina lake lilianza kujulikana baada ya kufanya vema katika mapambano yake mengi, tena kwa kushinda kwa KO, wengi walimtabiri mafanikio makubwa kupitia mchezo huo.
Katika vitongoji vya Jiji la Dar es Salaam, hasa kwenye chimbuko la mchezo masumbwi yakiwemo maeneo ya Keko, Manzese, Tandale, Mburahati, Mabibo, Mwananyamala na maeneo mengine hakuna asiyefahamu jina la Tembo Mtoto.
Kwani kabla ya kuanza kushiriki katika ndondi za kulipwa na kuwatwanga mabondia wengi alitokea katika ujenzi wa mchezo huo kwenye ngumi za ridhaa ambako ndiko wanapotokea mabondia bora Tanzania na ulimwengu kwa ujumla.
Prince Nasseb ambaye ndiye anashikilia mkanda wa taifa wa PST, na ndiye alitakiwa kuzitwangwa na Tembo Mtoto,  anasema kifo cha bondia huyo ni pigo kubwa kwake kwani aliamini ndio alikuwa mpinzani wake aliyebaki katika uzito huo wa kilo 66, kutokana na wengi kuwa dhaifu kwake.
"Sikuweza kuamini baada ya kusikia kifo cha mpinzani wangu,  hali ambayo ambayo hadi leo bado inanipa shida kuamini kama ni kweli Tembo Mtoto amefariki, lakini kikubwa ni kumuombea Mungu ampumzishe kwa amani katika makazi ya milele," alisema.
Mratibu wa pambano hilo ambaye ndiye alikuwa kocha wa Tembo Mtoto, Faraji Ndame anasema kifo cha bondia huyo ni pigo katika klabu yake ya Kwame iliyopo Mburahati kutokana na kuw,a kinara wa kusshinda mapambano mengi.
"Ni bondia ambaye alikuwa na namtegemea katika mapambano mengi na siku ambayo anafariki, kwa kweli sikuamini hadi nilipothibitishiwa na daktari wa Hospitali ya Mwananyamala, kwani kabla hajaanguka wakati alipokuwa akifanya mazoezi ya kupiga begi nilikuwa nikimtazama kwa karibu.
"Hadi anaanguka nilikuwa nikimwona, nilipomfuata kumpa huduma ya kwanza alikuwa akitokwa povu na kizuia meno akawa ameking'ata, mdomo ukawa mgumu kufunguka, tulimtoa kizuia meno na kumvua viatu, kisha tukampeleka Hospitali ya Mwananyala, lakini tukaambiwa  amefariki," anasema.
Rais wa PST, Emmanuel Mlundwa akizungumza na Jambo Leo, kuhusu kifo hicho, alisema wamepokea kwa mshtuko,  lakini kazi ya Mola haina makosa, kinachopaswa kila mmoja kumuombea.
Ninachokifahamu kwa Tembo Mtoto ni kwamba, alikuwa bondia bora mwenye umri mdogo ambaye ndio kwanza alikuwa akiyafuta mafanikio, kwani mapambano mengi aliyocheza alikuwa akishinda kwa KO.
"Katika pambano lake la mwisho ambalo alipigana na Kea Kea alishinda kwa KO, nilikuwa mwamuzi wa mchezo huo, kikubwa ambacho naweza kusema, alikuwa bondia mzuri na atakumbukwa kwa kufanya vema," alisema.
Kocha wa kimataifa wa mchezo huo, Rajabu Mhamila 'Super D', anasema kifo cha Tembo Mtoto ni pigo kubwa katika tasnia ya ngumi kutokana na bondia huyo kuonesha kila dalili za mafanikio katika mapambano yake mengi.
"Kifo cha Tembo Mtoto, hakika kimenishtua kwani ni bondia niliyekuwa nikimfahamu tangu akiwa katika ridhaa, alikuwa akifuata ushauri kwangu," alisema.
"Alikuwa akiupenda mchezo husika, aliuheshimu, aliuthamini kama sehemu ya kazi yake, huku akifanya  mazoezi ya kutosha na kuuthamini mchango wake," anasema Super D.
Dk. Kulwa Killaga ambaye mara nyingi huwapima mabondia kabla ya mapambano, anasema kifo cha Tembo Mtoto kimemshtua, hasa baada ya kukubaliana mambo mbalimbali.
"Nilipozungumza naye mara ya mwisho, aliniomba niwe meneja wake, nikamshauri awe mbali na vitu vilivyo kinyume na maadili ya mchezo wa ngumi kwa lengo la kuepuka athari zinazoweza kujitokeza," anasema.
Anasema kuwa, mara nyingi alikuwa akilalamika kuhusu waratibu kuwapiganisha mabondia bila kufuata utaratibu wa muda wa pambano hadi pambano, madhara yake ni vifo.
"Mfano bondia kapigana wiki moja au mbili, kabla hajafikisha miezi mitatu anapigana tena, hali hiyo ni mbaya sana," anasema.
Anasema kuwa, waratibu wanatakiwa kudhibitiwa katika hilo ili kulinda maisha ya mabondia ambao wengi wao hawana elimu ya kutosha katika hilo na ndicho kinachowagharimu wengi. Pia, anawataka waachane na utumiaji wa bangi.
"Bangi ni kitu kingine kibaya kinachosababisha vifo kwa mabondia, hivyo wadau wa mchezo huo wanatakiwa kuwashauri mabondia wanaotumia madawa ya kulevya," anasema.
Bondia Fadhili Awadhi wa klabu ya Jitegemee, aliyewahi kutwangana na Tembo Mtoto, mwanzoni mwa mwaka huu, alisema kifo cha mwanamasumbwi huyo kimemhuzunisha.
"Niliwahi kupanda ulingoni na marehemu Tembo Mtoto enzi za uhai wake, nikamshinda kwa KO katika raundi ya nne, kifo chake kinanipa majonzi na wakati mwingine nashindwa kuamini," alisema.
Rekodi ya bondia huyo alipigana mapambano saba ya ngumi za kulipwa, alishinda mara nne na kupigwa mara moja na  kutoka sare mara mbili.
Tembo Mtoto alijiunga na ngumi za kulipwa mwaka 2011, akianza safari yake ya masumbwi kutwangana na Seba Temba wa Morogoro, pambano lingine lilikuwa Agosti na kufanikiwa kumtwanga Shujaa Keakea kwa TKO.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amin

Kitimtim cha Ligi kuendelea kesho, Yanga kuvuna nini Mbeya, Simba kupigishana kwata na Mgambo, Azam,Ashanti Dar


Simba
Yanga

Azam
Ashanti United
 
Mgambo JKT

Na Boniface Wambura 
KIVUMBI cha Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kitaingia raundi ya nne kesho (Septemba 18 mwaka huu) kwa mechi saba katika viwanja saba tofauti.

Vinara wa ligi hiyo, JKT Ruvu wanaonolewa na Kocha Mbwana Makata watakuwa ugenini Uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani kuumana na 'ndugu' zao Ruvu Shooting ya Charles Boniface Mkwasa. 

Mechi hiyo inatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwa washabiki mkoani Pwani kutokana na aina ya soka inayochezwa na timu hizo.

Baada ya sare dhidi ya Mbeya City wikiendi iliyopita, Yanga inaendelea kubaki Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ambapo itacheza na Tanzania Prisons katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Simon Mbelwa kutoka Pwani.

Nayo Simba itaumana na Mgambo Shooting Stars ya Tanga katika mechi itakayopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Mechi hiyo itakuwa chini ya Kamishna David Lugenge kutoka Iringa.

Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Oljoro JKT kutoka Arusha na wenyeji Kagera Sugar wakati Azam na Ashanti United zitakwaruzana kwenye uga wa Azam Complex ulioko Chamazi jijini Dar es Salaam.

Mwamuzi Jacob Adongo kutoka Mara ndiye atakayechezesha mechi kati ya Coastal Union na Rhino Rangers itakayofanyika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. 

Mtibwa Sugar inarejea uwanja wake wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro ambapo inaikaribisha Mbeya City ya Kocha Juma Mwambusi.

Wakati huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo inaendelea kesho (Septemba 18 mwaka huu) kwa mechi moja ambapo Lipuli ya Iringa ambayo wikiendi iliyopita ilicheza Mkamba mkoani Morogoro inapita mjini Morogoro kuikabili Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri.

Kamati yafafanua uwakilishi wa wajumbe Mkutano Mkuu TFF



Na Boniface Wambura
KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesema uwakilishi wa ujumbe kwenye Mkutano Mkuu unaanzia kwenye chama cha mpira wa miguu cha mkoa, kufuatiwa na chama shiriki na baadaye klabu ya Ligi Kuu.

Mwongozo huo juu ya uwakilishi wa wajumbe kwenye Mkutano Mkuu umetolewa kutokana na maombi ya Sekretarieti ya TFF kwa kamati hiyo iliyokutana jana (Septemba 16 mwaka huu) baada ya kubaini baadhi ya wajumbe wanashikilia nafasi mbili kwenye vyama tofauti.

Kwa mujibu wa Ibara ya 5 ya Katiba, kuna makundi ya aina tatu ya wanachama wanaounda TFF. Makundi hayo ni vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu.

Sekretarieti ya TFF imebaini kuwa kuna baadhi ya viongozi wa kuchaguliwa wa mikoa ambao pia ni viongozi wa vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu, hivyo wana nafasi zaidi ya moja ya kuingia kwenye Mkutano Mkuu.

Hivyo, kutokana na mwongozo huo ushiriki wa wajumbe kwenye Mkutano Mkuu wa TFF utaanzia chama cha mkoa, kufuatiwa na chama shiriki na baadaye klabu za Ligi Kuu.

Pia nafasi ambazo zinaweza kuwakilishwa kwenye Mkutano Mkuu kama mhusika hayupo ni za Mwenyekiti atakayewakilishwa na Makamu Mwenyekiti, na Katibu atakayewakilishwa na Katibu Msaidizi.  Nafasi za ujumbe wa Mkutano Mkuu na ile ya mwakilishi wa klabu hazina uwakilishi kama mhusika hayupo.

Monday, September 16, 2013

Kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanza kesho, Moyes kuanza vipi?

Eti babu we ulikuwa unafanyaje mpaka ukatisha? Kama Moyes akimuuliza Sir Alex Ferguson

KIVUMBI cha Ligi ya Mabingwa wa Ulaya hatua ya makundi kinatarajiwa kuanza kesho, ambapo 'Mashetani Wekundu', Manchester United itaanza nyumbani dhidi ya Bayer Liverkusen ambapo mashabiki watataka kuona kocha David Moyes atavuna nini katika mechi yake ya kwanza katika michauno hiyo akiwa na Man Utd
Moyes aliyemrithi kocha mwenye mafanikio wa klabu hiyo aliyestaafu Mei mwaka huu, Sir Alex Ferguson atakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford, akiwa na kumbukumbu ya kukwama na Everton aliyokuwa akiinoakutinga hatua ya makundi msimu wa 2005-2006 baada ya kutolewa hatua ya mwisho wa mchujo kwa kung'olewa na Villarreal ya Hispania kwa jumla ya mabao 4-2.
Je, mbinu alizorithi toka kwa SAF zitamsaidia kuweza kufanya kweli kwenye kundi lake la A ambalo linaoonekana kuwa jepesi kulinganisha na mengine? Bila shaka ni suala la kusubiri kuona baada ya mechi hiyo ya kesho na nyingine za kundi lake lenye timu nyingine za Real Sociedad ya Hispania ambayo kesho pia itakuwa nyumbani kuialika Shakhtar Donetsk ya Ukraine.
Katika kivumbi hicho kesho pia itashuhudiwa mechi za makundi mengine matatu ya BC na Dna ratiba yake inaonyesha kuwa Galatasaray ya Uturuki itaumana na Real Madrid ambayo juzi ilimuongezea mkataba mpya nyota wake Cristiano Ronaldo na kumfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani, huku ikiwa na mchezaji ghali zaidi duniani kwa usajili Gareth Bale.
Pambano jingine la kundi B kwa kesho ni København  itakayoumana na Juventus, wakati mechi za kundi C itazikutanisha timu za Benfica ya Ureno dhidi ya Anderlecht ya Ubelgiji, huku Olympiakos Piraeus ya Ugiriki ikitarajiwa kuvaana na PSG ya Ufaransa.
Mabingwa watetezi, Bayern Munich ya Ujerumani yenyewe itaanza kibarua cha kutetea taji hilo iliyotwaa Mei mwaka huu kwa kuilaza Borussia Dotmund, nyumbani kuvaana na CSKA Moskva na Viktoria Plzeň itaialika Manchester City.
Keshokutwa Jumatano, kutakuwa na mechi nyingine za makundi manne yaliyosalia ambapo ratiba kamili ni kama ifuatavyo:
Schalke 04 vs Steaua BucharestChelsea   vs Basel
Olympique Marseille vs Arsenal
Napoli   vs Borussia Dortmund 
Austria Wien vs Porto
Atlético Madrid  vs Zenit
AC Milan vs Celtic
Barcelona  vs Ajax

Jeshi la Polisi Mbeya laonya mashabiki wa soka wenye vurugu


  RPC Mbeya, Diwani Athuman
 
JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limewaonya mashabiki wa soka mkoani humo ambao Jumamosi walifanya vurugu kubwa na kusababisha kuutia doa mkoa huo katika medani ya soka.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo mkoani humo limewaonya mashabiki hao kuwa kama watgaendelea kufanya 'upuuzi' wao kama walivyofanya katika pambano kati ya Mbeya City na Yanga basi watakiona cha moto.
 Jeshi hilo limelaani vurugu hizo ikidai linauchafua mkoa wao na pia ni tishio kwa Mbeya kuweza kufungiwa na hivyo kuwanyima mashabiki wa kweli wa soka kushuhudia mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Taarifa rasmi ya jeshi hilo la Polisi iliyotiwa saini na ASP P Mhako kwa niaba ya RPC Diwani Athuman isome mwenyewe hapo chini;
--
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAWATAKA MASHABIKI NA WAPENZI WA MPIRA WA MIGUU WAACHE VITENDO VYA KUFANYA VURUGU KATIKA MICHEZO ITAKAYOKUWA IKIFANYIKA KATIKA UWANJA WA KUMBUKUMBU YA SOKOINE NA MKOA KWA UJUMLA, KWANI VURUGU HIZO ZITASABABISHA MICHEZO HIYO KUHAMISHIWA SEHEMU NYINGINE NA WAPENZI KUKOSA BURUDANI  PIA WANANCHI KUKOSA KIPATO, HIVYO KUUTANGAZA MKOA WETU VIBAYA. 
 
VURUGU ZILIZOTOKEA JUMAMOSI TAREHE 14/09/2013 KWA MASHABIKI KULISHAMBULIA GARI LA VIONGOZI WA TIMU YA YANGA LILILOKUWA LIMEPAKI NJE YA UWANJA PIA KULISHAMBULIA KWA MAWE GARI LILILOKUWA LIMEBEBA WACHEZAJI WA TIMU YA YANGA NA KUHARIBU KIOO CHA MLANGO WA DEREVA NA KUFANYA MAANDAMANO AMBAYO YAMESABABISHA USUMBUFU KWA WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA SI CHA KIUNGWANA NA KISIJIRUDIE TENA KATIKA MICHEZO MINGINE.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA HAKURIDHISHWA NA VITENDO HIVYO NA KUWATAKA MASHABIKI NA WAPENZI WA MPIRA WA MIGUU KUWABAINI NA KUWATAMBUA  WALE WOTE WATAKAOFANYA VURUGU NA KULIJULISHA JESHI LA POLISI.

AIDHA JESHI LA POLISI HALITAVUMILIA VITENDO HIVYO NA KWA YEYOTE ATAKAYE/WATAKAO BAINIKA HATUA KALI ZA KISHERIA ZITACHUKULIWA ZIDI YAKE/YAO.

Signed by:
[P.A MHAKO – ASP]
Kny: KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Vijana wa Airtel Rising Stars wakabidhiwa bendera

 Katibu Mkuu wa Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania,Angetile Osia (kushoto) akimkabizi bendera ya Taifa,kapteni wa timu ya vijana ya wasichana wa Artel Rising Stars,Stumai Abdallah timu hiyo inaondoka leo kuelekea Nigeria kushiriki mashindano ya Afrika ya Airtel Rising Stars.
 Katibu Mkuu wa Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania,Angetile Osia (kushoto) akimkabizi bendera ya Taifa,kapteni wa timu ya vijana ya wanaume wa Artel Rising Stars,Athanas Shindeka timu hiyo inaondoka leo kuelekea Nigeria kushiriki mashindano ya Afrika ya Airtel Rising Stars.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania,Angetile Osia (kushoto) akikabizi bendera ya Taifa,kwa timu za vijana za wasichana na wanaume wa Artel Rising Stars ,timu hiyo inaondoka leo kuelekea Nigeria kushiriki mashindano ya Afrika ya Airtel Rising Stars.

Wamalawi wamiminika uhamiaji kujiandikisha zoezi la utambuzi wa wahamiaji haramu

Raia wa Malawi wakijiandikisha katika Idara ya Uhamiaji, Mkoa wa Dar es Salaam leo kuhusu zoezi linaloendelea la kuwatambua wahamiaji haramu jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).


Baadhi ya raia wa Malawi wakiwa katika foleni ya kujiandisha leo kwenye ofisi za uhamiaji jijini Dar es salaam 
Zoezi la utambuaji ya wahamiaji  haramu likiendelea wahamiaji wakiwa katika ofisi ya uhamiaji leo jijini Dar es salaam

Ivory Coast vs Senegal, Ghana dhidi ya Misri Top 10 WC Afrika


SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF limetangaza ratiba ya mchujo wa mwisho kwa timu za nchi za Afrika kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za mwakani ambapo vinara wa kandanda Afrika na wababe wa Tanzania, Ivory Coast imepangwa kuanzia nyumbani dhidi ya majirani zao Senegal.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ya CAF ni kwamba mechi za kwanza zitachezwa Oktoba 10 na zile za mwisho zitakazoa wawakilishi watano wa Afrika watakaoenda Brazil zitachezwa Novemba 14 mwaka huu.
Wakati Ivory Coast walionyakua nafasi ya kwanza katika kundi C lililokuwa na timu za Morocco, Tanzania na Gambia ikipangwa na Senegal iliyoiengua Uganda wiki iliyopita, wawakilishi wa ukanda wa CECAFA, Ethiopia yenyewe imepangwa na Nigeria na itaanza kibarua chake nyumbani mjini Addis Ababa.
Mechi nyingine itakzikutanisha Tunisia dhidi ya Cameroon, huku Burkina Faso kuumana na Algeria na Ghana watavaana na Misri.

Hawa ndiyo warembo walioingia Top 5 ya Redd's Miss Tanzania 2013

Warembo watano waliofanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali ya Redd’s Miss Tanzania 2013 wakiwa katika picha ya pamoja jana. Kutoka kushoto  ni Miss Tanzania Photogenic 2013, Happiness Watimanywa, Miss Tanzania Talent 2013, Prisca Clement, Miss Tanzania Personality, Severina Lwinga, Miss Tanzania Top Model 2013, Narietha Boniface na Miss Tanzania Sports Woman, Clara Bayo. (Na Mpigapicha Wetu). 

Hafsa Kizinja amuenzi Mzee Gurumo kiaina

 Malkia wa Zouk nchini Hafsa Kazinja akiwa na Omari Mkali (kushoto) na Abdul Salvador baada ya kukamilisha kurekodi wimbo wa 'NIMUOKEOE NANI' katika Studio za OM Productions jijini Dar es salaam wikiendi hii.
Omary Mkali akiwa katika pozi la picha na Hafsa.
Hafsa Kazinje akiwa Studio.

DAR ES SALAAM, Tanzania
Baada ya ukimya wa muda mrefu,   Malkia wa Zouk Tanzania,  Hafsa Kazinja,  anaibuka upya katika fani akiwa na ingizo lake la kwanza kati  ya kumi aliyoandaa kwa kuimba wimbo maarufu wa NUTA Jazz Band uitwao “NIMUOKOE NANI”  anauouleta hewani katika mahadhi ya Zouk.

Hafsa Kazinja anasema ameamua kurudi ulingoni kwa kutoa wimbo huo ili kumuenzi Mzee Muhidin Maalim Gurumo ambaye amestaafu rasmi fani ya muziki baada ya kufanya kazi hiyo akiwa na bendi mbalimbali tokea mwaka wa 1960.

“Nimeamua kuimba wimbo huu wa “NIMUOKOE NANI” ili  kumuenzi gwiji huyu wa muziki kwani wakati yeye anastaafu na mimi ndiyo naibuka upya baada ya kukaa kimya kwa muda”, anasema Hafsa ambaye alitoka kwa wimbo wake wa “PRESHA” aliomshirikisha Banana Zorro.

Hafsa ameandaa wimbo huo wa “NIMUOKOE NANI” katika studio za OM Productions ya jijini Dar es salaam chini ya wanamuziki nguli, Abdul Salvador na Omari Mkali.
“Nafurahi kwamba wimbo wa NIMUOKOE NANI nimeuimba baada ya kupata Baraka zote toka kwa mtunzi na mwimbaji wake Mzee Gurumo mwenyewe.

“Haikuwa rahisi kama inavyoweza kudhaniwa kwani baada ya kwenda kumuona nyumbani kwake alinifanyisha mtihani wa kuuimba wote kabla ya kuridhika maana alisema asingefurahi kuona wimbo wake unaimbwa hovyo hovyo na kuharibiwa radha yake”, anasema Hafsa, ambaye hivi sana anamalizia ngoma zake zingine tisa alizotunga mwenyewe, kabla ya kuvamia anga kwa mara ingine.

Hafsa anasema katika ukimya wake amekuwa akifanya utafiti na kujifunza kwa undani zaidi fani ya muziki, akipata mawaidha maridhawa toka kwa wanamuziki nguli ndani nan je ya nchi wakiwemo Muhidin Maalim Gurumo, Omar Mkali, Abdul Salvador na Lokassa ya Mbongo wa Congo aliyekutana na kufanya naye kazi alipokuwa ziarani Marekani hivi karibuni.

Msanii huyu wa kizazi kipya anasema ataitambulisha rasmi ngoma ya “NIMUOKOE NANI” katika tamasha la kumuenzi Mzee Gurumo lililopangwa kufanyika OKtoba 1, 2013 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

“Natumaini wapenzi wa muziki watafurika kwa wingi kwenye tamasha hilo name naahidi kuitendea haki ngoma ya “NIMUOKOE NANI” hivyo wasikose kuja kujionea wenyewe jinsi sie wa kizazi kipya tunavyoweza kufanya kazi na wakubwa wetu wa kazi, anaongezea Hafsa ambaye pia anaandaa video yake pamoja na ya ngoma zake zingine mpya.

Mkongwe Abdul Salvador, ambaye alikuwa mmoja wa waanzilishi wa  bendi ya TANCUT ALMASI YA Iringa iliyotamba na mtindo wake wa “FIMBO LUGODA”, anamtaja Hafsa kazinja mmoja wa wanamuziki wa kike waliojaaliwa sauti nzuri na kipaji cha hali ya juu hapa nchini.

“Kwa kuweza kuimba wimbo wa Mzee Gurumo na kupatia kisawasawa inadhihirisha kwamba Hafsa ni mwanamuziki aliyekomaa maana si mchezo kuimba nyimbo ya wakongwe kwa ufasaha kama alivyofanya Hafsa.
“Na hii inadhihirisha kwamba uwezekano wa kizazi kipya na cha zamani kufanya kazi pamoja ni mkubwa sana na sioni kwa nini isiwe hivyo”, anasema Salvador.

Omari Mkali, aliyetamba na bendi ya CHUCHU SOUNDS, chini ya marehemu Yusuf Chuchu, naye anamwelezea Hafsa Kazinja kama moja ya majembe ya muziki hapa nchini kwa upande wa kinamama, na kwamba anaweza kufika mbali endapo kama moto aliokuja nao upya atauendeleza.

IMETOLEWA NA
OM PRODUCTIONS NA HISIA SOUNDS

Sunday, September 15, 2013

Ronaldo asaini mkataba mpya Madrid kulipwa donge nono kuliko Messi

 
KLABU ya Real Madrid imethibitisha kumalizana na nyota wao kutoka Ureno, Cristiano Ronaldo kwa kumsainisha mkataba mpya wa miaka mitano wa kuitumikia klabu hiyo.
Rais wa Madrid, Florentino Perez amethibitisha kuwa, Ronaldo ameongeza mkataba huo ambapo sasa atakuwa akilipwa mshahara wa euro mil. 17 kila mwaka.
Mshahara huo utamfanya Mreno huyo aliyewahi kutamba na Manchester United amzidi nyota wa dunia Lionel Messi wa Barca kwa euro mil. 1 na kiwango anacholipwa na klabu yake.
Kusaini kwa nyota huyo kumezima uvumi kwamba Ronaldo alikuwa njiani kutaka kuihama klabu hiyo ili kurejea England kukipiga Manchester iliyokuwa ikitajwa kutaka kumrejesha.

Unakikumbuka kikosi hiki? Kama ndiyo tueleze ni timu gani na kama vipi tupia majina ya wanaounda timu hii


Balotelli aiokoa Milan na kipigo cha ugenini

Mario Balotelli akishangilia bao

STRAIKA Mario Balotelli jana aliiokoa timu yake ya AC Milan isiaibike ugenini baada ya kufunga bao dakika za nyongeza na kuipa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Torino katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Italia Seria A.
Balotelli aliyetoka kuipeleka nchi yake kwenye michuano ya Fainali za Kombe la Dunia za mwakani, alifunga bao hilo kwa mkwaju wa penati dakika ya 90+6 na kuiepushia aibu Milan walioonekana kulala 2-1.
Kabla ya hapo Milan ilijipatia bao la kufutia machozi kupitia kwa Sulley Muntari baada ya wenyeji kutangulia kupata mabao mawili yaliyofungwa na D'Ambrosio na Cerci.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo mabingwa watetezi, Juventus wakiwa ugenini mjini Milan dhidi yasa Inter Milan waliambulia sare ya bao 1-1, huku Napoli ikipata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Atalanta, huku Fiorentina nayo ikilazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Cagliari.

Gareth Bale aanza na bao Real Madrid ikipata sare ugenini la liga

bale bale bale bale
NYOTA mpya wa Real Madrid na mchezaji ghali kuliko wote duniani, winga Gareth Bale usiku wa kuamkia leo alianza makeke yake katika klabu yake kwa kuifungia moja ya mabao yaliyoisaidia vinara hao wa Hispania wasiumbuke ugenini walipotoka sare ya 2-2 na Villareal.
Hiyo ilikuwa mechi ya kwanza kwa mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur na alionyesha uwezo mkubwa, akifunga bao hilo la kusawazisha baada ya wenyeji kuwatangulia Madrid kwa bao la Cani na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe nguvu sawa ya bao 1-1.
Kipindi cha pili Cristiano Ronaldo aliiongezea Madrid bao ambalo hata hivuo lilikuja kurejeshwa na wenyeji kupitia kwa Giovani Dos Santos.
Katika mechi iliyochezwa mapema leo, Espanol ikiwa ugenini imeizabua Granada kwa bao 1-0 lilitupiwa kambani na Lanzarote.
Matokeo ya mechi nyingine zilizochezwa jana katika ligi hiyo maarufu kama La Liga, mabingwa watetezi Barcelona ikiwa nyumbani ilishinda mabao 3-2 dhidi ya Sevilla, shukrani ya mabao ya Dani Alves , Lionel Messi na Alexis Sanchez.
Wageni mabao yao yalitupiwa kimiani na Coke na Ivan Rakitic. Nao Atletico Madrid walipata ushindi wao wa nne mfululizo kwa kuwalaza Almeria mabao 4-2 na kuwaweka kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakati Levante walilazimishwa suluhu na Real Sociaded.

Warembo wa Miss Tanzania waitembelea DTL

Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' David Mgwassa akizungumza na waandishi wa habari baada ya warembo wanaowania taji la Miss Tanzania kufanya zihara katika Kampuni hiyo mwishoni juzi ambayo imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Zanzi  .Picha na mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakichukua chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' juzi   ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi  Konyagi  ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmaria kushoto na meneja masoko wa ksampuni hiyo Joseph Chibhee wakigonganisha grass na Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi Konyagi ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmariakatikati akiwa katika pozi na baadi ya washiriki wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi konyagi  ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
 Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi konyagi ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu

Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakipata chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'    ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
NA MWANDISHI WETU

WAREMBO wanaowania taji la Miss Tanzania wametakiwa kupenda na kuthamini bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mkuu wa Kiwanda cha Tanzania Distilleries (KONYAGI) Bw. David Mgwassa wakati akiongea na Warembo 30 wanaowani taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwanda hicho jijini Dar es salaam.

"Nyinyi ni mabalozi wazuri wa kutangaza bidhaa za humu ndani  hivyo nawaomba sana mzipende na kuthamini sana bidhaa zote zinazozalishwa na viwanda vya ndani" alisema Bw. Mgwassa.

Amesema kuwa TDL kupitia kinywaji cha Zanzi imeamua kudhamini shindano la Miss Tanzania kwa kiasi cha Milioni 40 ikiwa na lengo la kutangaza kinywaji hicho na pia kuboresha shindano hilo.

Kwa mujibu wa Bw. Mgwassa shindano la Miss Tanzania ni kielelezo muhimu kwa taifa hili na kuwataka warembo hao kutangaza milima kilimanjaro na pia kuitangaza Zanzi kuwa ni bidhaa bora kwa Watanzania kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.

"Nyinyi warembo naombeni sana  Zanzi iwe kwenye mawazo yenu kila siku na muitangaze Zanzi baada ya mlima kilimanjaro kwa kufanya hivyo basi uchumi wa nchiu pia utakua mzuri zaidi." alisema

Kwa upande wake meneja masoko wa TDL, Bw. Vimal Vaghmaria aliwataka warembo hao kuwa na nidhamu kubwa wanapokuwa kambini kwa lengo la kupata mrembo mwenye viwango vya juu na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.

"Sisi kama TDL kupitia kinywaji cha Zanzi tumemua kudhamini shindano hili la Miss Tanzania tukiamini kuwa nyinyi ni mabalozi wazuri wa kuitangaza kinywaji hichi na kuiletea sifa Tanzania" alisema Bw. Vaghmaria.

Katika ziara hiyo warembo walipata nafasi ya kujione shughuli mbalimbali za kiwanda hicho kuanzia mwanzo wa vinywaji vinapozalishwa hadi kwenye sehemu ya mwisho ya upakiaji.

JKT Ruvu hawakamatiki, Kavumbangu, Maguri, Kipanga wawanasa akina Tegete, Mkude katika magoli

Didier Kavumbagu
USHINDI wa tatu mfululizo uliopata JKT Ruvu katika Ligi Kuu Tanzania Bara imeifanya timu hiyo izidi kuchanja mbuga ikiongoza msimamo wa ligi hiyo na kuwa timu pekee ambayo haijapoteza mchezo wala kufungwa bao lolote mpaka sasa.
Ruvu inayonolewa na kipa wa zamani wa Tukuyu Stars na Yanga, Mbwana Makatta, iliitafuta Ashanti United jana kwa bao la Amos Mgisa na kuifanya ifikishe pointi 9 na magoli sita ya kufungwa huku yenyewe ikiwa na ukuta wa chuma kwa kutoruhusu kufungwa bao lolote.
Kikosi cha JKT Ruvu
Simba ambayo ilianza mechi zake kwa kulazimishwa sare ya wageni Rhino Rangers imechupa hadi nafasi ya pili kutokana na ushindi wa mechi yao ya jana dhidi ya Mtibwa Sugar, huku Ruvu Shooting ikiwa kwenye nafasi ya tatu kutokana na jana kuing'ata  Mgambo JKT.
Bao pekee lililofungwa na Elius Maguri lilitosha kuifanya maafande hao kufikisha pointi sita, huku mfungaji huyo akiingia kwenye orodha ya wafungaji watano wanaoongoza kwa sasa katika ligi hiyo kila mmoja akiwa na mabao mawili.
Maguri aliyesajiliwa na Ruvu Shooting toka Prisons ameungana na akina Jerry Tegete na Didier Kavumbagu wa Yanga, Jonas Mkude wa Simba, Saad Kipanga aliyeanza kuonyesha makeke licha ya ugeni wake katika ligi hiyo naye akiwa na mabao mawili baada ya jana kuisaidia timu yake ya Rhino kupata sare dhidi ya Olojoro JKT jijini Arusha.
Mchezaji mwingine aliye katika orodha hiyo ya wafungaji bora kwa sasa wakati ligi ikiwa ndiyo kwanza ipo raundi ya tatu ni Bakar Kombo wa JKT Ruvu.
Wakati Prisons ikiwa ndiyo timu pekee ambayo haijafanikiwa kufunga bao lolote mpaka sasa angalau wenyewe wameambulia pointi jana jijini Tanga mbele ya Coastal, kuliko Ashanti United ambayo licha ya kuwa na goli moja, lakini haijaonja furaha ya kumiliki pointi baada ya kupoteza mechi zake zote tatu.
Ilianza kwa kufungwa na Yanga mabao 5-1 kabla ya kunyolewa bao 1-0 katika mechi zilizofuata dhidi ya Mgambo na jana JKT Ruvu na kuwa ndiyo inayoburuza mkia ikizibeba timu zote za ligi hiyo yenye klabu 14.
Ashanti ni kati ya timu tatu zilizopanda daraja msimu huu sambamba na Rhino Rangers iliyokusanya pointi mbili mpaka sasa katika mechi zake tatu na Mbeya City iliyokaribia kuiadhiri mabingwa watetezi Yanga jana kwenye mechi yao ilioisha kwa sare ya 1-1 yenyewe ikiwa na pointi tano sambamba na klabu nyingine wakiwamo Yanga, Coastal Union na Azam.
Msimamo kamili wa ligi hiyo baada ya mechi ya jana ni kama ifuatavyo na wafungaji na ratiba ya mechi zijazo utachungulia hapo chini:

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                         
                                     P  W  D  L    F  A  GD PTS
1.  JKT Ruvu                 3    3   0   0   6   0    6    9
2.  Simba                       3    2   1   0   5   2    3    7
3.  Ruvu Shooting           3    2   0   1   5   2    3    6
4.  Yanga                        3    1   2   0   7   3   4    5
5.  Azam                        3    1    2   0   4   2   2    5
6.  Coastal Union            3   1    2    0   3   1  2    5
7.  Mbeya City                3   1    2    0   3   2   1   5
8.  Mtibwa Sugar             3   1    1   1    2   3  -1  4
9.  Mgambo                    3    1    0   2    1   3  -2   3
10. Rhino Rangers           3    0    2   1    3   5  -2   2
11. Kagera Sugar            3    0    2    1   1   2  -1   2
12. Oljoro                       3    0    1    2   1   4  -3   1
13. Prisons                      3    0    1    2   0   6  -6   1
14. Ashanti                      3    0    0    3   1   7  -6   0

Wafungaji:

2- Jerry Tegete, Didier Kavumbangu (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, Jerry Santo (Coastal Union), Haruna Chanongo, Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris (Azam), Mwagani Yeya, Steven Mazanda, Paul Nonga (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga (Mgambo JKT), Themi Felix (Kagera Sugar), Amir Omary (Oljoro JKT)

Mechi zinazofuata siku ya Jumatano 
Sept 18, 2013Prisons vs Yanga
Simba vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs JKT Oljoro
Azam  vs Ashanti United
Coastal Union  vs Rhino Rangers
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu

Mjini Magharib mabingwa wa Copa Coca Cola


MJINI Magharibi imetwaa ubingwa wa michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya jana (Septemba 14 mwaka huu) kuifunga Ilala bao 1-0.

Mechi hiyo ya fainali ilichezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam. Ilala iliwavua ubingwa Morogoro baada ya kuwafunga kwenye mechi ya nusu fainali kwa kuivua ubingwa Morogoro katika mechi iliyoamriwa kwa mikwaju ya penalti.

Kwa upande wa wasichana, Mwanza ndiyo imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 kwa njia ya penalti dhidi ya Ilala. Hadi muda wa kawaida wa mchezo huo uliochezwa jana (Septemba 14 mwaka huu) jioni Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam timu hizo zilikuwa suluhu.