STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 23, 2013

Issa Matumla anyukwa kwa KO


Bondia Adamu Ngange (kushoto) akichapana na Issa Matumla,  wakati wa pambano lao lililofanyika jana jumapili katika ukumbi wa Kilimahewa uliopo Chanika Kigogo Fresh. Katika pambano hilo, Ngange alishinda kwa KO katika raundi ya pili.  
Mwamuzi, Saidi Chaku (kulia) akimpa huduma ya kwanza bondia Issa Matumla, baada ya kugaragazwa kwa ngumi na bondia Adamu Ngange.
Bondia Antony Mathias (kulia) akimpiga ngumi mfululizo bondia Ismail Ninja, wakati wa mpambano wao.
Bondia Antony Mathias akiwa amebebwa juu baa ya kupata ushindi wa KO
Mdau wa mchezo wa masumbwi, Halima Kaubanika, akiwa ni mmoja kati ya wadau waliojitokeza kufuatilia mchezo huo jana.

Tamasha la Filamu Dar es Salaam kuzinduliwa rasmi kesho Dar

Dar Films Festival hiyooooo!
TAMASHA la siku tatu la filamu lifahamikalo kama 'Dar Filamu Festival (DFF)-2013' linatarajiwa kuzinduliwa kesho kwa semina ya mafunzo ya uigizaji, utayarishaji, uongozaji na uandishi wa miswada wa filamu inayofanyika Chuo Kikuu Idara ya Sanaa.
Mabalozi wa tamasha hilo, Vincent Kigosi 'Ray'  na Elizabeth Michael 'Lulu' ndiyo watakaonogesha tamasha hilo kwa siku hizo tatu kabla ya kufungwa Alhamisi ambapo  mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Dk Funella Mukangara.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo, mmoja wa waratibu wa tamasha hilo lililoandaliwa kwa ushirikiano wa mtandao wa filamucentral na kampuni ya Haak Neel Production. Myovela Mfwaisa, alisema tamasha hilo litafanyikia viwanja vya Chuo cha Posta.
Mfwaisa alisema mbali na semina hiyo ya mafunzo pia leo kwenye uzinduzi kutakuwa na uonyeshwaji wa filamu nne za kibongo na utaratibu huo utafanyika siku zote tatu.
"Tamasha letu la DFF litazinduliwa rasmi Jumanne kwa semina ya mafunzo juu ya uigizaji, uandishi wa miswada, utayarishaji na uongozaji wa filamu chini wa wakufunzi toka Chuo Kikuu na jioni kutakuwa na uonyeshwaji wa filamu nne tofauti," alisema.
Mfwaisa alisema mabalozi wa tamasha hilo ni Mtayarishaji na Muongozaji Bora wa 2011-2012, Vincent Kigosi 'Ray' na Elizabeth Michael 'Lulu' ma kwamba watatumia kuonyesha kazi za kitanzania za lugha ya Kiswahili tu kwa mwaka huu .
Alisema keshokutwa itakuwa zamu ya makampuni ya kuzalisha na kusambaza filamu nazo zitakuwa na wasaa wao wa kutangaza kazi zao kwa wadau kabla ya siku ya mwisho kutakuwa na mjadala wa mustakabali wa filamu nchini utakaohusisha taasisi kama TRA, Bodi ya Ukaguzi wa Filamu, wasambazaji wa filamu na taasisi nyingine.

Sunday, September 22, 2013

Paulinho alibeba Spurs ugenini, Man Utd ikilala 4-1

Sergio Aguero of Manchester City (16) celebrates as he scores their first goal during the Barclays Premier League match between Manchester City and Manchester United (Getty Images)
Kun Aguero akishangilia moja ya mabao yake ya leo yaliyoizamisha Manchester United
Wayne Rooney akiwa hoi

Paulinho
BAO la dakika za lala salama lililofungewa na Paulinho liliisaidia Tottenham Hotspur kupata ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Cardiff City, huku Manchester United chini ya kocha wake David Moyes ikilala kwa mahasimu wao Manchester City kwa mabao 4-1.
Paulinho alifunga bao la Spur dakika ya tatu za nyongeza kabla ya mchezo huo kumalizika na kuipa timu yake pointi tatu muhimu zilizoifanya waende sambamba kileleni mwa msimamo na Arsenal iliyoshinda mapema mabao 3-1 dhidi ya Stoke City, japo inazidiwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa licha ya zote kufikisha jumla ya pointi 12.
Mabingwa watetezi Manchester United walijikuta wakipata kipigo cha aibu ikiwa na kocha wake David Moyes baada ya kunyukwa mabao 4-1 na Manchester City.
Mabao mawili ya Sergio 'Kun' Aguero, Yaya Toure na samir Nasir yalitosha kuipandisha City hadi nafasi ya tatu ikifikisha pointi 10 sawa na za Chelsea lakini ikiwa na uwianoi mzuri wa mabao ya kufunga na kufunga ikizipumulia Tottenham na Arsenal zilizopo kileleni.
Bao pekee la kufutia machozi ya Manchester United lilifungwa na nyota wake aliye katika kiwango cha juu kwa sasa Wayne Rooney.

Kipigo chaiporomosha Yanga, mabao 76 yafungwa mpaka sasa

Mabingwa watetezi
WAKATI mabingwa watetezi Yanga wakijikuta wakiporomoka kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara hadi nafasi ya nane toka ile ya nne iliyokuwapo awali kabla ya pambano lao la leo dhidi ya Azam, jumla ya mabao 76 yameshatinga wavuni hadi sasa ligi ikiwa katika raundi ya tano.
Yanga imesaliwa na pointi zake sita na ikiwa nyuma ya wageni wa ligi hiyo Mbeya City yenye pointi saba, huku Azam na Coastal zikizipumulia maafande wa Ruvu ambazo zote zilichezea vichapo katika mechi zao leo.
Vinara Simba wanaendelea kusalia kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 11 na mabao yao 13 ya kufunga na kufungwa magoli manne, huku JKT Ruvu ikifuatia ikiwa na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa ikiizidi Azam licha ya kulingana nao pointi 9 sawa na Ruvu Shooting na Coastal Union.
Azam yenyewe imefunga mabao nane na kuruhusu mabao matano, wakati JKT Ruvu imefunga mabao sita na kufungwa mawili na kuwa, ikifuatiwa na ndugu zao Ruvu Shooting waliofunga mabao sita na kufungwa matatu kisha Coastal iliyofunga magoli matano na kuruhusu nyavu zake zitikiswe mara mbili.
Kagera Sugar iliyoanza ligi kwa kusuasua ushindi wake wa jana dhidi ya Ashanti umeiweka katika nafasi ya sita ikiwa na pointi nane na kufuatiwa na Mbeya City wenye pointi saba kisha Yanga yenye pointi zake sita.
Oljoro JKT iliyokuwa nafasi ya pili toka mkiani imechupa hadi nafasi ya 11 mwa msimamo baada ya ushindi wake wa leo dhidi ya JKT Ruvu ikifikisha pointi nne na kuirithisha nafasi hiyo Prisons-Mbeya huku Ashanti wakiendelea kuzibeba timu zote 13 za ligi hiyo ikiwa na poingti moja tu.
Mpaka sasa ligi ikijiandaa kuingia raundi ya sita siku ya Jumatano kwa pambano moja tu kati ya Rhino Rangers ya tabora itakayoialika Ashanti United mjini Tabora jumla ya mabao 76 yameshatinga wavuni, huku Tambwe Amissi wa Simnba akiongoza orodha ya wafungaji wenzake akiwa na mabao sita.
Tambwe anafuatiwa kwa mbali na washambuliaji nyota wa Yanga, Jerry Tegete na Didier Kavumbagu na Haruna Chanongo, mchezaji wenzake wa Simba wenye mabao matatu kila mmoja.
Angalia msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa na orodha ya wafungaji pamoja na ratiba ya mechi zijazo.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014      
                                    P  W  D  L   F   A  GD  PTS
1.  Simba                      5   3   2   0  13  4    9   11
2.  JKT Ruvu                5   3   0   2   6   2    4    9
3.  Azam                       5   2   3   0   8   5    3    9
4.  Ruvu Shooting          5   3   0   2   6   3    3    9
5.  Coastal Union          5   2   3   0   5   2    3    9
6.  Kagera Sugar           5   2   2   1   6   3    3   8
7.  Mbeya City              5   1   4   0   5   4   1    7
8.  Yanga                       5   1   3   1  10  7   3   6
9.  Mtibwa Sugar           5   1   3   1   3  4   -1   6
10.Rhino Rangers           5   0   4   1   5  7   -2   4
11.Oljoro                       5   1   1   3   3   6  -3   4
12.Mgambo                   5   1   1   3   2  10 -8   4
13.Prisons                      5   0   3   2   2   8  -6   3
14.Ashanti                      5   0   1   4   2  11 -6   1

Wafungaji:

6- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete , Didier kavumbagu (Yanga), Haruna Chanongo (Simba),
2- Jonas Mkude (Simba), Jerry Santo (Coastal Union),Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Paul Nonga (Mbeya City), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, Haruna Moshi (Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Hamis Kiiza (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, Kipre Tchetche, John Bocco, Joseph Kimwaga (Azam), Mwagani Yeya, Steven Mazanda, Richard Peter (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally, Shaaban Nditi (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Themi Felix, Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Godfrey Wambura, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa (Oljoro JKT)

Mechi zijazo
Sept 25, 2013
Rhino Rangers vs Ashanti Utd

Sept 28, 2013

Yanga vs Ruvu Shooting
Rhino Rangers v Kagera Sugar
Mbeya City vs Coastal Union
Mgambo JKT vs Oljoro JKT

Sept 29, 2013

Ashanti Utd vs Mtibwa Sugar
JKT Ruvu vs Simba
Prisons vs Azam

Matokeo ya mechi zilizopita ni kama ifuatavyo:

Ratiba ya Ligi Kuu 2013-2014
DURU LA KWANZA
Agosti 24, 2013
Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013
Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)

Sept 18, 2013
Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Sept 21, 2013
Mgambo JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Prisons vs Mtibwa Sugar (1-1)
Simba vs Mbeya City (2-2)
Kagera Sugar vs Ashanti United (3-0)

Sept 22, 2013
JKT Ruvu vs Oljoro JKT (0-1)
Azam  vs Yanga (3-2)
Coastal Union v Ruvu Shooting (1-0)

Tevez akizidi kung'ara Italia, Inter yaua 7-0

Carlos Tevez
Tevez (10) akishangilia bao lake na wachezaji wenzake wa Juventus
 MSHAMBULIAJI nyota wa Argentina, Carlos Tevez ameendelea kung'ara kwenye Seria A baada ya leo kuisaidia Juventus kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Hellas Verona, huku mabingwa wa zamani wa Ulaya, Inter Milan ikipata ushindi wa kishindo wa mabao 7-0 ugenini dhidi ya Sassuolo.
Tevez aliyetua kwa mabingwa hao watetezi wa Seria A akitokea Manchester City, aliifungia Juventus bao la kusawazisha dakika ya 40 baada ya  wageni wao kutangulia kwa bao lililofungwa na Cacciatore kabla ya Fernando Lliorente kufunga bao la pili na la ushindi sekundu chache kabla ya mapumziko.
Nayo Inter Milan ikiwa ugenini iliisulubu Sassuolo mabao 7-0, wafungaji wake wakiwa ni Palacio aliyefunga dakika ya 7, Taide dakika ya 23 na Pucino wa Sassuolo aliyejifunga dakika ya 33 na hadi mapumziko washindi walikuwa mbele kwa magoli 3-0.
Mabao mengine yalifungwa na Alvarez, Diego Milito aliyefunga mawili na Cambiasso.
Katika mechi nyingine za ligi hiuyo Fiorentina ilipata ushindi ugenini wa mabao 2-0 dhidi ya Atalanta, Bologna kukubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Torino, As Roma kuizima lazio mabao 2-0 na Catania na Parma kushindwa kutambiana na muda mchache ujao itashuhudiwa pambano la kukata na mundu klati ya Ac Milan itakayoialika Napoli uwanja wa San Siro.















Yanga bado gonjwa, yanyukwa na Azam, JKT Ruvu 'nguvu ya soda', Boban anga'ra mkwakwani

'Muuaji' wa Yanga, Joseph Kimwaga akibebwa na wachezaji wenzake baada ya kuisidia Azam kushinda mabaop 3-2 leo Taifa.

MABINGWA watetezi Yanga bado wana hali mbaya msimu huu baada ya jioni ya leo kunyukwa mabao 3-2 na Azam katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, huku bao la ushindi la Wana Lambalamba' likitupiwa kimiani dakika za nyongeza na chipukizi, Joseph Kimwaga.
Yanga ambao walitoa visingizio vya ubovu wa uwanja wa Sokoine-Mbeya kutokana na sare mbili ilizopata toka kwa wenyeji wao Mbeya City na Prisons, walishtukizwa kwa bao la mapema ya sekunde ya 33 lililofungwa na John Bocco 'Adebayor' bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kusawazisha bao dakika nne tu ya kipindi hicho kupitia Didier Kavumbagu kabla ya mtokea benchi Hamis Kiiza 'Diego' kuiongezea Yanga bao la pili dakika ya 65.
Hata hivyo mtokea benchi wa azam na mfungaji bopra wa msimu uliopita, Kipre Tchetche kuifungia Azam bao la pili kwa mkwaju wa penati dakika mbili baadaye baada ya Niyonzima kuunawa mpira katika haraki za kuokoa.
Wakati mashabiki wakiamini pambano hilo litamalizika kwa sate hiyo ya mabao 2-2, dakika mbili za nyongeza ziliztosha kuisaidia Azam kupata bao la tatu lililofungwa na Jospeh Kimwaga aliyeingia uwanjani kutokea benchi na kuwanyamazisha mashabiki wa Yanga ambao hawakuamini kama timu yao imelala.
Kwa ushindi huo Azam imefikisha pointi 9 na kuchupa hadi nafasi ya tatu nyuma ya JKT Ruvu ambayo jioni ya leo imedhihirisha kuwa ilikuwa na 'nguvu ya soda' kutokana na kukubali kipigoi cha pili mfululizo leo na maafande wenzao wa Oljoro JKT ya Arusha.
Bao la washindi liliwekwa kimiani na Paul Malipesa dakika ya 79 katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi na kusitisha makali ya Ruvu waliokuwa kileleni kabla ya kuenguliwa na Simba.
Nao mabingwa wa zamani wa Tanzania, Coastal Union ya Tanga ilitakata nyumbani mjini Tanga baada ya kuilaza Ruvu Shooting kwa bao 1-0, bao lililotupiwa kimiani na kiungo mshambuliaji,  Haruna Moshi 'Boban'.
Hata hivyo Coastal iliwabidi wasubiri hadi kwenye dakika ya 82 kujipatia bao hilo lililowapa pointi tatu muhimu zilizowafanya wafikishe jumla ya pointi 9 na kushika nafasi ya tano ikiwa na pointi 9 sawa na timu za JKT Ruvu, Azam, Ruvu Shooting Stars zikitofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Arsenal moto nchini yaibanjua Stoke 3-1 yarudi kileleni

Arsenal v Stoke City - Premier League
Bacary Sagna akishangilia bao lake jioni hii
VIJANA wa Arsene Wenger, Arsenal ya England imeendelea kutakata kwenye Ligi Kuu ya England baada ya jioni hii kuicharaza Stoke City kwa mabao 3-1 na kurejea kileleni mwa ligi hiyo ikiiengua Chelsea.
Arsena ikichezwa kwenye dimba la nyumbani la Emirates ilipata mabao yake  kupitia kwa Aaron Ramsey dakika ya 5 kabla ya Per Mertesacker kuongeza bao la pili dakika ya 36 kwa kazi nzuri iliyofanywa na Mesut Ozil, ambaye aliiwezesha pia kupatrika bao la pili dakika ya 72 lililofungwa na Bacary Sagna.
Baop la kufutia machozi kwa wageni, Stoke lilitumbukizwa wavuni na Geoff Cameroon dakika 26.
Kwa ushindi huo Arsenal wamefikisha pointi 12 na kukalia usukani wa ligi hiyo ikiizidi Chelsea iliyoshinda jana mabao 2-0 dhidi ya Fulham ikisaliwa na pointi zake 10.
Katika mechi nyingine jioni ya leo, Swansea City ikiwa ugenini iliifumuaCrystal Palace kwa mabao 2-0. mechi nyingine ambazo zimetoka mapumziko sasa hivi mabingwa watetezi wapo hoi mpaka sasa wakiwa wamekandikwa mabao 4-0 na mahasimu wao Manchester City, huku Tottenham Hotspur wakiwa suluhu ya Cardiff City.

Unyama! Watu watatu wa familia moja wauwawa kinyama

WATU watatu wa familia moja jijini Mwanza, akiwemo kichanga cha miezi saba, wameuawa kwa kunyongwa, kukatwa mapanga kichwani na kuchinjwa mithili ya kuku.

Mauaji hayo yamefanyika kati ya saa 9 na 10 usiku wa kuamkia jana, katika Kijiji cha Ihyila, Kata ya Buhongwa, jijini humo.

Waliofikwa na mauti hayo ni baba wa familia, Jones Elias Luhinga (44), mama wa familia, Lusia Elias Luhinga (35), na mtoto Eliud Elias Luhinga (mwaka mmoja).

Inadaiwa mauaji hayo yametekelezwa na mtu mmoja fundi wa kujenga nyumba (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyekaribishwa siku tisa zilizopita na Jones.

Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya majirani na ndugu wa familia hiyo ya marehemu, mtu huyo alifanya unyama huo usiku wa manane, na kwamba alfajiri alioga kisha kuwafungia ndani watoto wengine waliokuwa wamelala na kutokomea kusikojulikana.

Mmoja wa ndugu wa marehemu Jones, aliyejitambulisha kwa jina la Benjamin Luhinga alinukuliwa akidai kuwa ndugu yake aliuawa kwa kuchinjwa kama kuku, kisha kukatwa panga katikati ya kichwa na upande mmoja wa juu ya sikio.

"Jones ni mjomba wangu, ameuawa kwa kuchinjwa hapa kwenye koromeo. Amekatwa na panga hapa kichwani na eneo hili la juu ya sikio. Lakini tumekuta mabegi yamefunguliwa, labda alikuwa akitafuta fedha.

"Binafsi nina shaka huenda mjomba wangu ameuawa kwa sababu za fitna au fedha aliyouza kiwanja huko Buswelu baada ya kulipwa na jiji na baadaye akaja kujenga huku Buhongwa," alisema.

Benjamin alisema fundi ujenzi anayetuhumiwa kutekeleza mauaji hayo aliitwa na Jones na tangu awasili nyumbani hapo alikuwa akilala kwenye chumba cha watoto.

Alibainisha kuwa familia hiyo ina watoto tisa na haijulikani kwanini mtuhumiwa hakuwadhuru wengine nane waliokuwamo kwenye chumba alichokuwa akilala.

Inadaiwa kuwa mtoto aliyeuawa alikuwa amelala na wenzake na muuaji aliamua kumpeleka kwa mama yake ili akanyonye na ndipo alipokwenda kumnyonga.

Musa Sayi, mkazi wa Buhongwa alisema walipata taarifa za mauaji hayo jana alfajiri na walipofika walihisi kuna mtu amemaliza kuoga lakini hawakumuona.

“Mazingira tuliyoyakuta pale tulihisi kuna mtu anaoga, lakini hatukuona. Tulihisi ndiye muuaji labda amefanya mitambiko ya kichawi,” alisema.

Jeshi la Polisi kupitia kwa Mkuu wa Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Mwanza, Joseph Konyo (RCO), alisema Jones aliuawa kwa kukatwa panga kichwani na upande mmoja wa juu ya sikio, na si kuchinjwa kama kuku.

"Huyu baba mwenye nyumba yeye ameuawa kwa kukatwa panga katikati ya kichwa na likaingia sana na huku upande wa karibu na sikio. Hajachinjwa kama baadhi ya watu wanavyodai," alisema.

Konyo alisema walifika eneo la tukio hilo na kushuhudia miili ya marehemu hao.

Akizungumzia tukio la jana, RCO Konyo alisema yawezekana chanzo cha mauaji hayo yanatokana na fitna, visa na uhasama wa muda mrefu baina ya mwenye nyumba na baadhi ya watu na kuna uwezekano muuaji hakuwa peke yake.

Kamanda Konyo alisema polisi itawasaka wauaji hao ili iwafikishe kwenye vyombo vya sheria.

Tukio kama hilo limewahi kutokea Februari 16, 2010 huko Musoma mkoani Mara, baada ya watu 17 wa familia tatu za koo moja kuuawa kinyama na wengine watatu kujeruhiwa vibaya pamoja na ng’ombe kadhaa kuchinjwa huko Buhare.

Mauaji hayo ya Musoma yalielezwa kwamba yalikuwa ya kulipiza kisasi, baada ya kutokea wizi wa mifugo kisha watu kadhaa kuuawa miaka ya nyuma kabla ya mwaka huo 2010.

Mnamibia kuwania taji la IBF-Afrika Novemba

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AO9WimIAAAgLUj6xBwAAAB43WXc&midoffset=2_0_0_1_1294958&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331

DAR ES SALAAM, TANZANIA – Namibian Abraham 'Energy' Ndaendapo 10(3)-2(1)-0 will fight against a boxer to be named layer for the vacant "IBF Continental Africa Jr. Lightweight Title in November this year. Ndauendapo an elite boxer of hard punching club has elicited excitements in various quarters hence his nominal
 
The tournament will be promoted by one of the gurus of Namibian boxing fraternity Kinda Nangolo Managing Director of Kinda Boxing Promotions based in downtown Namibia  capital city of Windhoek. Kinda Nangolo himself a great former international boxier is a prominent businessman in Windhoek, the capital city of Namibia dealing with fish export among many business activities he is currently involved at.

 
 
Abraham Ndauendapo doing what he love most after hard training "listening to the music"
 
His company Kinda Boxing Promotions has highly contributed to the advancement of professional boxing in Namibia. Kinda Nangolo is proud to manage some of the most decorated IBF Continental champions in Gottlieb Ndokosho "The Bite" who is the current IBF AMEPG Featherweight Champion and the youthfulness King Albinus Felesianu, the current IBF Jr. Lightweight Youth Champion of the world.
 
Abraham "Energy" Ndaundendapo comes a long way to the professional boxing ranks and files, to the position that allows him to aim at the most prestigious IBF continental title in Jr. Lightweight. He had an awesomely amateur boxing career and pundits rank his future very high.
 
Watch this space as we build case for Abraham Ndauendapo of the Republic of Namibia as he lock on for the IBF Continental Africa Jr. Lightweight Title respectively!
 
Congratulations Abraham Ndauendapo and Kinda Nangolo. Africa is proud of YOU!

Nothing else like IBF/AFRICA as it advances the African interests to the Global professional boxing fraternity" 

They call it AFRICA….! We call it HOME. 


The United States Boxing Association (USBA) and International Boxing Federation (IBF) continental body to Africa, Middle East & Persian Gulf

Azam, Yanga leo ni vita kali Taifa

Kipre Tchetche na Nadir Haroub 'Cannavaro leo itakuwaje Taifa?
WACHEZAJI wa wa Azam FC kwa pamoja wameahidi ushindi katika mchezo wa leo dhidi ya Yanga utakaochezwa kwenye uwanja wa taifa, Azam FC ikiwa nyumbani.
Hata hivyo Kocha Msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro amesema 'aah wapi...tunataka pointi tatu baada ya sare tatu mfululizo'.
Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa Azam, wachezaji wa klabu hiyo iliyoshinda mechi moja na kupata sare mbili katika mechi zake nne za awali kama ilivyo kwa wapinzani wao, wamepania kushinda leo ili kutuliza mashabiki wao.
Ahadi ya wachezaji hao ilitolewa mbele ya Makocha Kally Ongalla na Ibrahim Shikanda, Mwenyekiti Said Muhammad, Katibu Mkuu Nassor Idrissa na Mratibu wa timu hiyo Patrick Kahemele kwenye kikao cha pamoja kati ya wachezaji na viongozi kutathmini mwenendo wa timu hiyo baada ya mechi nne za mwanzo za ligi.
 
Wachezaji hao wakiongozwa na John Bocco, Jabir Aziz na Salum Abubakar, walisema matokeo ya sare nyingi walizopata katika mechi zilizopita hayatokani na matatizo ya huduma isipokuwa ni mitihani ya kawaida kwenye soka ambapo timu inaweza kucheza vizuri na bado ikashindwa kupata matokeo.
Wachezaji wameahidi kuongeza nguvu kwa kuanzia mechi ya leo ili kupata matokeo ya ushindi badala ya sare.

Wachezaji kwa pamoja walionesha masikitiko yao kwa matokeo yaliyopita na kuahidi kuongeza kujituma kwenye mazoezi na mechi ili kurudisha makali yaliyoifanya Azam kuwa timu ya kuogopwa.

Azam FC itashuka uwanjani leo kukwaana na Yanga SC ambapo katika mechi nne zilizopita Azam FC imeambulia kipigo toka kwa Yanga. Lakini timu zote mbili zinashuka uwanjani zikiwa na matokeo ya kufanana na idadi sawa ya pointi tatu 
Azam FC leo itamkosa Agrey Morris Ambrose ambaye alipewa kadi nyekundu kwenye mechi iliyopita dhidi ya Ashanti United na nafasi yake itajazwa na David Mwantika.
Wakati Azam wakijipanga hivyo kocha Minziro wa Yanga amesema vijana wake wapo kamili kuhakikisha wanaitungua Azam ili kuwafukuzia watani zao Simba waliopo kileleni.
Yanga kama Azam wana pointi 6, tano nyuma na zile ilizonazo Simba wanaoongoza wa kiwa na pointi 11 baada ya jana kubanwa na Mbeya City.
"Hatukubali kuona tukiendelea kupoteza pointi, tumerejea kwenye uwanja wa Taifa, ambazo ni mzuri na kuwapa nafasi wachezaji kufanya wanavyofanya hivyo tunaamini ushindi ni lazima," alisema.
Alisema kikosi chao kitawakosa baadhi ya wachezaji akiwamo kiungo mkabaji, Salum Telela ambaye ni majeruhi, lakini akidai waliosalia wapo tayari kwa vita na kwamba Azam ikae chonjo.
Timu hizo zinakutana mwezi mmoja na ushei tangu zilipokutana kwene mechi ya Ngao ya Jamii na Azam kulala bao 1-0 lililofungwa na Telela. Pia hilo ni pambano la 11 la Ligi Kuu baina ya timu hizo tangu mwaka 2008 ambapo Yanga imeshinda mara 5 na kupoteza 3 na michezo miwili iliishia kwa sare.

Waliokufa katika shambulizi la kigaidi Kenya wafikia 39

Hekeheka kila mtu akisalimisha roho yake
Mwanajeshi akitafuta mbinu za kuwasaidia mateka mikononi mwa watekaji
Baadhi ya majeruhi wakisaidiwa
IDADI watu waliopoteza uhai katika shambulio la kigaidi linalohusishwa na kundi la Al Shaabab imefikia 39 mpaka sasa.
Wapiganaji hao walishambulia jengo hilo saa saba za mchana Jumamosi

Milio ya risasi imeweza kusikika katika jengo la Westgate mjini Nairobi Kenya, ambako wanamgambo wa Al shabaab wanawazuilia mateka ambao idadi yao haijajulikana hadi sasa.
Wanajeshi wawili walijeruhiwa katika ufyatulianaji huo na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu huku watu wawili wakinusuriwa asubuhi ya leo.
Hadi sasa jeshi limeweza kudhibiti hali nje na ndani ya jengo hilo, magari ya kijeshi yakiwa yameletwa katika eneo hilo huku polisi na wanajeshi wakijaraibu kuwanusuru baadhi ambao wangali wanazuiliwa ndani ya jengo hilo.
Watu 39 wameuawa baada ya wanamgambo hao kushambulia jengo hilo mwanzo katika eneo la kuegeshea magari na kisha kuingia ndani ya mikahawa na maduka katika jengo hilo lenye ghorofa nne na kuwpaiga watu risasi kuholela.
Kuna taarifa kuwa wanamgambo hao wako ndani ya duka moja kubwa katika jengo hilo.
Rais Kenyatta anasema kuwa baadhi ya waliofariki ni jamaa zake. Miongoni mwa waliofariki pia ni mwanadiplomasia wa Canada na raia wawili wa Ufaransa. Rais Kenyatta anasema kuwa wale waliohusika lazima wakabiliwe na mkono wa sheria.
Jamaa na marafiki waliofika kujua hali ya jamaa zao wamezuiwa kuingia ndani ya jengo hilo. Wengi wa waathiriwa walifariki kutokana na majeraha yao.
Taarifa nyingine zinasema kuwa mpaka sasa majeruhi wa tukio hilo wamefikia 162.

BBC

Ngumi Dar watapata uongozi mpya, BFT yauruka kimanga


Baadhi ya viongozi waliochaguliwa kuiongoza Chama cha Ngumi Mkoa wa Dar es salaam (DABA) wakiwa katika picha ya pamoja na mwenyekiti wa uchaguzi huo Zuwena Kipingu  (katikati) na Mwangalizi mkuu wa uchaguzi, Remmy Ngabo.


Mwenyekiti wa Mkutano wa Uchaguzi wa viongozi wa mchezo wa Masumbwi Mkoa wa Dar es salaam Zuwena Kibena katikati akizungumza baada ya kumalizika uchaguzi huo na kupatikana viongozi wake
Baadhi ya wajumbe kutoka klabu ya Ashanti ya Ilala wakifatilia uchaguzi huo kutoka kushoto ni Emmanuel Mgaya, Hamisi Manyota na Juma Mwalimu  wakifuatilia uchaguzi mkuu wa chama cha mchezo wa ngumi mkoa wa Dar es Salaam (DABA) uliofanyika jana kwenye Ukumbi wa DDC Mlimani, Mwenge jijini Dar es Salaam.
Bondia Karama Nyilawaila akifuatilia uchaguzi huo, ambao hata hivyo umepingwa na Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT).

Mweka hazina wa klabu ya Ashanti ya Ilala, Emmanuel Mgaya akitumbukiza kura yake
Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Timothi Kingu akijinadi wakati wa kuomba kula

Baadhi ya viongozi wakipiga kula za kuchagua viongozi watakaokiongoza chama cha mchezo wa ngumi Mkoa wa Dar es Salaam DABA
Wamboi Mangore akiomba nafasi ya Ukatibu Mkuu
Mmoja wa Wajumbe Jafar Ndame akiomba Kura za Ujumbe wa Kamati ya Uhusiano Habari na Masoko.
Juma Uwesu akiomba kuchaguliwa kwa wapiga kula  ujumbe wa maendeleo ya vijana
Arnord Ngumbi akiomba nafasi ya ujumbe wa vilabu,wilaya na taasisi za umma
Mazimbo Ali akijinadi mbele ya wajumbe wa mkutano kumpigia kura katika nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.

Happiness Watimanywa ndiye Redd's Miss Tanzania 2013


MISS Tanzania 2013, Happiness Watimanywa akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 usiku wa Septemba 21, Ndani ya Ukumbi wa Mlimani City na kuwashinda warembo wenzake 29.
Na Father Kidevu Blog
HATIMAYE kitendawili cha nani atanyakua taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 kimeteguliwa usiku huu na mrembo Happiness Watimanywa kutoka Mkoa wa Dodoma na Kanda ya Kati kufanikiwa kutawazwa Mshindi wa taji hilo na kuwashinda warembo wengine 29 waiokuwa wakiwania taji hilo.
Nyota ya Happiness ilionekana dhahiri kung’aa vyema katika fainali hizo mwaka huu tangu pale alipofanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania Photogenic 2013 na kuwa mrembo wa kwanza kuingia nusu fainali.
Wakati Happiness akinyakua Taji hilo pamoja na zawadi ya Gari na kitita cha shilingi Milioni 8 nafasi ya pili ilikwenda kwa mrembo Latifa Mohamed kutoka Kitongoji cha Kigamboni na Kanda ya Temeke na nafasi ya Tatu ikienda kwa Miss Tanzania Sports Woman, Clara Bayo.
Pamoja nao warembo wengine walio ingia hatua hiyo ya tano bora ni Lucy Tomeka na Elizabeth Prety.
Hii ndio tano bora ya Redd's Miss Tanzania 2013. Je nani hapa ataondoka na taji, gari na kitita cha Milio ni 8? Warembo hao kutoka kushoto ni Happiness Watimanywa (Miss Photogenic), Elizabeth Pretty, Clara Bayo (Miss Sports Women), Lucy Tomeka na Latifa Mohamed.

Saturday, September 21, 2013

Chelsea, Mourinho wapumua, Liverpool ikifa nyumbani EPL

Oscar
Oscar akishangilia bao lake jioni hii
Beki Lavren akiitungua Liverpool kwa kichwa

VIJOGOO vya England, Liverpool leo wamejikuta wakiiangukia pua wakiwa uwanja wao wa nyumbani wa Anfield baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Southampton, na kuipisha Chelsea iliyozinduka leo kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mahasimu wao wa Fulham kukaa kileleni mwa msimamo.
Liverpool iliyokuwa haijaonja chungu ya kipigo katika mechi nne zilizopita za Ligi Kuu ya England ilitunguliwa bao hilo lililofungwa na Dejan Lavren katika dakika ya 53 na kuzima ubabe wake wa kuwafunga wenzake.
Nayo Newcastle United ikiwa nayo nyumbani ilicharazwa mabao 3-2 na Hull City, licha ya kuongoza hadi mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1.
Chelsea muda mchache uliopita imetoka kupata ushindi kwa kuilaza Fulham kwa mabao 2-0, mabao yaliyofungwa na Oscar katika dakika ya 52 na Obi Mikel aliyefunga la pili dakika sita kabla ya pambano hilo lililochezwa Stanford Bridge kumalizika na kumpa afueni kocha Jose Mourinho.
Mechi nyingine za ligi hiyo ya England, Everton ikiwa ugenini imeisulubu West Ham kwa mabao 3-2 nayo Sundeland ikiwa ugenini imetandikwa mabao 3-0 na West Brom na Aston Villa ikiizima Norwich City ikiwa kwake kwa bao 1-0.
Kipute cha ligi hiyo kinatarajiwa kuendelea kesho kwa michezo nne, Arsenal itakuwa ikiufukuzia uongozi wa ligi hiyo baada ya kuenguliwa wiki iliyopita na Liverpool itaikaribisha Stoke City, Manchester City itakuwa nyumbani kuialika Manchester United, Tottenham Hotspur watasafiri hadi nyumbani kwa Cardiff City na Crystal Palace wataikaribisha Swansea City.

Mbeya City yapunguza kasi Msimbazi, Tambwe aendelee kufumania nyavu, Ashanti yaendelea kuwa mdebwedo


Mbeya City wakiomba dua
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi003q9axgmcyEwn769yPSk0p-qvp7iBWnxb70zu3q8AEvcVy2CrW_ALBPLt_ui4VS13-PzWbTpfaDxDBACnTatNnxlIyckN4u5SXDOATdaTiRtWevZ5goB1IekVocBA9ddoiZP-GkDw90/s400/kikosi1.JPG
Kikosi cha Simba

LILE 'fupa' lililowashinda Yanga kulitafuta, Mbeya City imedhihirisha wapo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kikazi baada ya jioni ya leo kuibana mbavu Simba na kwenda nao sare ya mabao 2-2 kwenye uwanja wa Taifa, huku mshambuliaji nyota toka Burundi, Tambwe Amissi akiendeleza libeneke lake kwa kufumania nyavu.
Simba ambayo hata hivyo inaendelea kukalia uongozi wa msimamo wa ligi hiyo ilishindwa kulinda mabao yake mawili yaliyofungwa na Tambwe katika kipindi cha kwanza na kuwapa mwanya 'wageni' Mbeya City kuyarejesha na kupata ponti yake ya pili ugenini.
Tambwe alifunga bao la kwanza dakika ya 22 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 33 na kumfganya afikishe jumla ya mabao sita na kuwaacha mbali wafungaji wenzake wanaomfukuzia kwenye orodha ya wafumania nyavu.
Hata hivyo Mbeya inayonolewa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi ilijipatia bao la kwanza dakika nne baada ya kufungwa bao la pili na Simba kupitia Paul Nonga na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 2-1.
Kipindi cha pili kilishuhudiwa kosa za hapa na pale kwa timu zote na hasa Mbeya kuonyesha kucharuka na katika dakika ya 69, Richard Peter aliisawazishia timu yake bao la pili na kuifanya Simba ipoteze umakini wake na kama siyo papara za washambuliaji wa Mbeya huenda wangeweza kuibuka na ushindi leo Taifa.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Mgambo JKT ikiwa uwanja wa Mkwakwani ililazimishwa sare ya bao 1-1 na maafande wenzao wa Rhino Rangers ya Tabora. Bao la wenyeji lilifungwa na Mwalimu Musuku dakika ya 60 kabla ya Rhino kuchomoa dakika za jioni kupitia Hamis Msafiri.
Nayo timu ya Prisons Mbeya imeendelea kujikongoja baada ya kuambulia sare ya pili mfululizo dhidi ya Mtibwa Sugar, mechi iliyochezwa uwanja wa Sokoine Mbeya, wageni wakianza kupata bao kupitia nahodha Shaaban Nditti aliyefunga kwa kichwa dakika ya 26 akiiunganisha mpira wa adhabu ndogo iliyopigwa na Said Mkopi kabla ya wenyeji kuchomoa bao dakika ya 58 kupityia kwa Peter Michael.
Kagera Sugar ikiwa uwanja wake wa Kaitaba, Bukoba iliishindilia bila huruma 'vibonde' wa ligi hiyo Ashanti United ya Dar kwa mabao 3-0. Mabao ya washindi yalitupiwa kimiani na Daud Jumanne, Seleman Kibuta na Clement Douglas.
 Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea kesho kwa mechi tatu zitakzaochezwa viwanja vitatu tofauti jijini Dar mabingwa watetezi watapimana ubavu na Azam watakaokuwa wenyeji, huku mjini Tanga Coastal Union itapepetana na Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani na JKT Ruvu itawalika Oljoro JKT.

Simba, Mbeya City nini bwana, ngoma kesho Yanga vs Azam

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPnNutozTJ6LUNDdmv05v7BvLNYLIQ6dp4CQ2ET3L3oazDgFevrgY8oyJQYiRwp0q85aEDxXie6rSVYqBOkl6hngu5QSM5xh24P58eJEep1bVkTQhE8P0a20N1ChhRt5YTQlf4pHuVo4dH/s1600/MWAIKIMBA.jpg
Wachezaji Azam wakishangilia mabao yao

WAKATI Mbeya City ikiwa na kibarua kigumu mbele ya vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, macho na masikio ya mashabiki yapo kwenye pambano la kesho kati ya mabingwa watetezi Yanga na makamu bingwa, Azam zitakazopepetana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Yanga wakishangilia moja ya mabao yao
Simba na Mbeya zinaumana leo pia kwenye uwanja huo katika mfululizo wa ligi hiyo utakaoshuhudiwa pia mechi nyingine tatu katika miji tofauti.
Hata hivyo mashabiki wa soka watakuwa na hamu kubwa ya kushuhudia pambano la Yanga na Azama ambazo zote zimeshindwa kuonyesha makeke katika mechi zake mbili zilizopita.
baada ya kubanwa mbavu jijini Mbeya ikilazimishwa sare mbili mfululizo dhidi ya wenyeji wao Mbeya City na Prisons, Yanga kesho inarejea katika dimba lake la nyumbani kujaribu bahati yake tena kwa Azam.Azam nao kama ilivyo kwa Yanga imetoka kuambulia sare mbili dhidi ya Kagera Sugar na Ashanti na kujikusanyia pointi sita sawa na ilizonazo Yanga, Mbeya City na Coastal Union.
Pambano hilo la Yanga na Azam ni kati ya mechi tatu zitakazochezwa kesho katika ligi hiyo iliyoingia raundi ya tano, michezo mingine ikiwa ni maafande wa JKT Ruvu na Oljoro JKT zitakazopepetana kwenye dimba la Chamazi, Mbagala Dar es Salaam na ile ya 'Wagosi wa Kaya' Coastal Union itakyokuwa nyumbani uwanja wa Mkwakwani, Tanga kuumana na Ruvu Shooting.
Hata hivyo pamoja na mechi hizo nyingine kuwa na mvuto wake, pambano la Yanga na Azam ndilo linaloangaliwa kwa ukaribu na mashabiki wa soka nchini kutokana na upinzani uliopo baina ya timu hizo kila zinapokutana.
Timu hizo zenye pointi sita kila mmoja zikitofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa zitakutana katika pambano lao la 11 la Ligi Kuu tangu 'Wana Lambalamba' wapande daraja mnamo mwaka 2008.
Klabu hizo zimeshakutana katika michuano kadhaa ikiwamo ya Kombe la Mapinduzi, Kombe la Kagame na Ngao ya Hisani ambayo mara ya mwisho walivaana Agosti 17 na Yanga kuitambia Azam kwa bao 1-0, lakini katika mechi za ligi kuu huwa na matokeo mengi ya kushangaza.
Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo tangu mwaka 2008 Yanga na Azam zimekutana mara 10 katika Ligi Kuu na Yanga kushinda mechi tano na Azam ikishinda mechi tatu huku michezo yao miwili ikiishia kwa sare.
Hivyo katika pambano hilo klabu hizo zitakuwa zikifukuzia nafasi ya kuvuna pointi tatu na wakati huo huo kulinda au kuboresha rekodi yao dhidi ya mwenzake, huku wadau wa soka wakitaka kuona kama wafungaji bora wa msimu uliopita nani anatayemfunika mwenzake.
Kipre Tchetche wa Azam ndiye aliyeongoza orodha ya wafungaji bora kwa kufunga mabao 17 na amezinduka majuzi baada ya kufunga bao lake la kwanza, huku aliyeyemfuata msimu uliopita, Didier Kavumbagu tayari akiwa na mabao mawili kibindoni mpaka sasa.
Kadhalika ni mechi itakayokuwa ikishindanisha makocha wawili wa kigeni wenye rekodi nzuri kwa msimu uliopita, Ernie Brandts wa Yanga aliyeiongoza Yanga kwa mechi zaidi ya 24 bila kufungwa tangu walipolala bao 1-0 toka kwa Kagera Sugar msimu uliopita.
Kocha wa Azam, Muingereza, Stewart John Hall, yeye naye atataka kulipa kisasi kwa mpinzani wake ambaye amemtambia kwa msimu uliopita katika mechi zote za ligi na majuzi kwenye ngao ya Hisani.
Je ni Yanga au Azam itakayocheka au Kipre Tchetche atakayemtambia Didier Kavumbagu ama ni kocha Brandts kuendelea kumfunika Stewart? Tusubuiri tuone.
Rekodi za Yanga na Azam katika Ligi tangu 2008:
Oktoba 15, 2008
Yanga 3-1 Azam
Aprili 8, 2009
Azam 3-2 Yanga
Oktoba 17, 2009
Azam 1-1 Yanga
Machi 7, 2010
Yanga 2-1 Azam
Oktoba 24, 2010
Yanga 0-0 Azam
Machi 30, 2011
Yanga 2-1 Azam
Septemba 18, 2011
Azam 1-0 Yanga
Machi 10, 2012
Azam 3-1 Yanga
Novemba 4, 2012
Yanga 2-0 Azam
Februari 23, 2013
Yanga 1-0 Azam
Sept 22, 2013?

Masogange, Melisa waachiwa huru hatimaye

http://api.ning.com/files/It3-odgnrfRW80PWalq53lRwVSPptJtp*DOsLRl-yTPt24Tlnfb-fOv0Dzh6ppWTIjHud9Q--mi-9R3wu5ArUT7KY4Lt9FlD/MASOGANGE.jpg?width=450
Masogange
WATANZANIA wawili Agness Gerard ‘Masogange’ na Melissa Edward wameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg baada ya kutakiwa kulipa faini ya Sh 4.8 milioni (Randi 30,000) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumiwa kutengeneza dawa za kulevya.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini (hawk) Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo mahakama ilibaini kuwa Melissa hana hatia kwa kuwa ilionekana amemsindikiza Masogange, aliyemuomba amsaidie kubeba mzigo huo.
Mosagange alilipa faini ya Shilingi 2.5 milioni (R15, 000), huku akiahidi kumaliza nusu yake ambayo juhudi zilikuwa zinafanyika amalize kulipa jana Ijumaa.
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu kusaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini haikuwa mizigo yake. Mizigo yote iliandikwa jina la Agness Masogange na si Melissa,” alisema Kapteni Ramaloko.
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa amesafiri na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na Masogange alimuomba amsaidie mizigo hiyo kwani ilikuwa mikubwa.
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba kemikali zozote ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria hivyo mahakama iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela miezi 30 (miaka miwili na miezi sita) au alipe faini ya R30, 000(Sh 4.8 milioni).
Hata hivyo alilipa faini na nusu ya fedha hizo ilishalipwa na nyingine ilikuwa inakaribia kulipwa.
Ingawa Kamishana Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa juzi Alhamisi alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni dawa za kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS) Marika Muller, alieleza kuwa timu ya SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5, mwaka huu ni methamphetamine.

MWANASPOTI

Amani Simba aanza tambo Ashanti United

Amani Simba
KIPA mpya wa Ashanti United, Amani Simba ametamba kwamba bado muda mfupi tu kabla ya mashabiki wa soka kuikubali timu yao ambayo imeanza vibaya Ligi Kuu Tanzania Bara kiasi cha kuruza mkia katika msimamo wa ligi hiyo.
Aidha kipa huyo alisema ni mapema mno kuanza kuitabiria ligi ya msimu huu kwa sababu anaamini lolote linaweza kubadilika kwa sasa kutpkana na ukweli ligi ndivyo kwanza ipo raundi ya nne kwa sasa.
Simba aliyeidhinishwa hivi karibuni na TFF kuidakia timu hiyo baada ya kuitema timu aliyoipandisha daraja ya Mbeya City, alisema Ashanti inasumbuliwa na ugeni wa ligi, ila kadri siku zinavyosonga mbele wachezaji wataizoea na kutisha.
Kipa huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Moro United, Simba na Taifa Stars alisema ni mapema mno kuanza kuihukumu Ashanti na matokeo iliyopata kwa sasa kwa sababu ligi bado mbichi na wachezaji wao wanaendelea kuizoea ligi hiyo.
"Ni mapema mno kuijadili Ashanti, naamini muda mfupi ujao wanayoibeza wataikubali baada ya kuanza kupata matokeo mazuri, unajua ugeni wa ligi ndiyo tatizo lakini kadri siku zinavyoenda mbele wachezaji wanaondoa woga," alisema.
Simba, aliyewahi pia kuzidakia Lipuli Iringa, Prisons Mbeya na JKT Ruvu, alisema akishirikiana na wenzake watahakikisha Ashanti inafanya vyema katika mechi zilizopo mbele yake.
Ashanti United inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa pointi moja ni kati ya timu tatu zilizopanda Ligi Kuu msimu huu, nyingine zikiwa ni Mbeya City na Rhino Rangers ya Tabora.

Gaucho bado aliota soka la kulipwa

http://api.ning.com/files/Z311HW*8BLsTaHW*p4y9dVjDgbR8cx2tskdyBtk0ZluRwicT9*Nf2fkCQ3unhX6sg*ce5TuwMHaY4TPmDCzkUwHTqR41EqDZ/GLOBALHUMUD.jpg?width=351
Gaucho
KIUNGO nyota wa klabu ya Simba, Abduhalim Humud 'Gaucho' amesema bado hajakata tamaa na mipango ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi hata baada ya mipango ya kwenda nchini Afrika Kusini kukwama.
Akizungumza na MICHARAZO, Gaucho, aliyerejea tena Simba akitokea Azam aliyoichezea msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema japo ametuliza akili zake kuitumia kikamilifu Simba, bado analiwaza soka la kulipwa.
Gaucho, alisema bado ana kiu kubwa ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi na imani yake siku yoyote ataenda nje ksa kuamini ana kipaji na uwezo wa kucheza soka kokote akipata fursa hiyo.
"Sijakata tamaa na soka la kulipwa, bado naamini ipo siku nitaenda nje kwa uwezo wa Muingu kwani yeye ni Muweza na Mpangaji wa kila jambo," alisema Gaucho nyota wa zamani wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars.
Hata hivyo Gaucho aliwataka viongozi swa soka nchini kuepukana hali ya kibabaishaji na tabia za kuwawekea kauzibe wachezaji wanapopata nafasi ya kwenda nje ya nchi kusakata kandanda akidai ni faifa kwa taifa.
Mapema mwaka huu Gaucho alifaulu majaribio yake ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Jomo Cosmos ya Afrika Kusini, lakini wakati akiwa katika maandalizi ya kuondoka alitangaza ghafla kutua klabu ya Simba.
Hata hivyo alinukuliwa katika mahojiano na kituo kimoja cha redio kwamba klabu yake ya zamani ya Azam ndiyo iliyomwekea vikwazo kabla ya uongozi wa Azam kukanusha taarifa hizo na kutangaza kuachana naye.

Ile Ile atoa Wazazi akijipanga upya

Msani Ile Ile katika pozi
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya, Maishani Ndee 'Ile Ile' ameachia kibao kipya kiitwacho 'Wazazi' ukiwa ni wimbo wake wa tatu tangu atumbukie kwenye fani hiyo miaka minne iliyopita.
Wimbo huo na video yake umeanza kuwa gumzo kwenye vituo vya redio na runinga kutokana na maudhui wake na Ile Ile alisema amefarijika na anajipanga kuandaa kazi nyinginje mbili kwa mpigo.
Ile Ile aliyewahi kukimbiza na nyimbo za 'Ileile' alioutoa mwaka 2010 na 'Bora Twende' wa mwaka jana alisema nyimbo ambazo zitafuata baada ya 'Wazazi' ni 'Amani na Upendo' na 'Sheila'.
"Hizi zimeshakamilika kila kitu na wakati wowote naziingiza studio kuzirekodi ili kuendelea kuwapa burudani mashabiki wangu na muziki kwa ujumla," alisema Ileile anayejishughulisha na biashara za nguo na hasa lebo yake ya Ile Ile Wears.
Msanii huyo mwenyeji wa Kondoa, alisema angetamani kutoa albamu yake ya kwanza, lakini soko la muziki kwa sasa nchini linamtisha na hivyo anaona bora aendelee kurtoa 'singo' moja moja na video zake ili kujitengenezea mazingira mazuri ya kupata shoo zitakazomuingiza pato la kutosha.

Steve Nyerere 'ala shavu' kifo cha Baba wa Taifa


MSANII wa filamu nchini, Steve Mangendela 'Steve Nyerere' amepata shavu la kutangaza kwa kutoa hotuba mbalimbali za baba wa taifa zitakazokuwa zikirushwa hewani na  Luninga ya TBC mpaka siku ya kilele cha kifo cha hayati Baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Hotuba hizo ambazo zilikuwa zikitolewa na baba wa Taifa sasa Steve Nyerere atakuwa akizitoa kwa kuiga sauti hile hile
Msanii huyo aliyejizolea umaarufu kwa kuiga sauti za viongozi mbalimbali nchini na Duniani kwa ujumla amekuwa akipendwa na wengi kutokana na kuiga sauti ya hayati Baba wa Taifa na kufanya kuchukua jina lake moja kwa moja ambapo kwa sasa popote uendapo uwezi kumwita kwa jina la Steve bali lazima useme Steve Nyerere
Kwa sasa ameingiza kazi yake mpya mtaani inayojulikana kwa jina la Before Wedding ambayo ipo mtaani ikisambazwa na kampuni ya Steps Entatainment ya jijini Dae rs salaam