STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Tanzania yapanda nafasi 6 Fifa, Uganda noma!

Wachezaji wa Taifa Stars katika moja ya mechi zao za kimataifa
TANZANIA imepanda kwa nafasi sita kwenye msimamo wa Orodha ya Viwango vya Soka vya Dunia, ikishika nafasi ya 126 kutoka ile ya 132 iliyoshikilia Desemba mwaka jana.
Kwa mujibu wa orodha mpya iliyotolewa leo Alhamisi, Uganda imeweka rekodi ya kushika nafasi ya 62 ikiwa nafasi ya juu zaidi kuwahi kushikwa na taifa hilo la Afrika Mashariki ikipanda nafasi moja juu. Desemba ilikuwa nafasi ya 63, huku Rwanda, Kenya, Burundi na Ethiopia zikiifuata nchi hiyo katika orodha hiyo kwa nchi za ukanda huo wa Afrika Mashariki.
Ivory Coast, Algeria zimeendelea kukomaa kwenye nafasi zao mbili za juu sawa na ilivyo kwa Ghana na Cape Verde kwa upande wa Afrika zikishika nafasi ya 19, 28, 33 na 39 duniani, huku Ubelgiji anapotaka kwenda kucheza soka la kulipwa nyota wa Afrika na Tanzania, Mbwana Samatta ikiendelea kuongoza orodha hiyo ya ubora dunia wakifuatiwa na Argentina, Hispania na Ujerumani katika nafasi nne Bora.

Top 10 ya Dunia:

1. Ubelgiji
2. Argentina
3 Hispania
4. Ujerumani
5. Chile
6. Brazili
7.Ureno
8. Colombia
9.England
10. Austria

Top 10 ya Afrika:

1. Ivory Coast
2. Algeria
3. Ghana
4. Cape Verde
5. Tunisia
6. Senegal
7. Congo
8. Guinea
9. Cameroon
10. Misri

Top 10 ya Cecafa:

1. Uganda
2. Rwanda
3. Kenya
4. Burundi
5. Ethiopia
6. Tanzania
7. Sudan
8. Sudan Kusini
9. Djibout
10. Eritrea

Wednesday, January 6, 2016

Simba yaongoza 1-0 dhidi ya URA, JKU yaifumua Jamhuri 3-0

KIPINDI cha pili cha pambano la michuano ya Kombe la Mapinduzi Kundi A limeanza kipindi cha pili sasa na Simba wanaongoza kwa bao 1-0.
Bao lao liliwekwa kimiani na Ibrahim Ajib, baada ya mabeki wa URA Uganda kuzembea kuokoa mpira langoni mwao na Ajib kufumua shuti lililotinga kimiani.
Pambano ni kali kweli kweli. Katika mchezo wa mapema jioni, JKU ilifumua Jamhuri Pemba kwa mabao 3-0.

Yanga wapewa Friends, Simba watupwa Moro Kombe la FA

Toto Africans wataumana na TP Lindanda, Pamba-Mwanza
African Lyon itakayoumana na Azam FC
Coastal Union

Mbeya City itatoka salama kwa Wenda FC
JKT Ruvu wanaoisubiri mshindi kati ya Lipuli na Kurugenzi Mafinga

Yanga itaifanyia nini Friends Rangers?
Kikosi cha Mgambo JKT

Azam wamepewa Lyon, watavuna nini
Simba wataifuatya Burkina Faso mjini Morogoro
 MICHUANO ya Michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mzunguko wa tatu inatarajiwa kuendelea Januari 12 na wikiendi ya Januari 23-27 kwa timu 32 kuchuana kuwania kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya michuano hiyo.
Timu 16 zinazoshiriki Ligi Kuu ya Bara zimeingia moja kwa moja mzunguko wa tatu ambapo Yanga yenyewe imepangwa kuumana na Friends Rangers, huku watani zao Simba wakipelekwa Morogoro kuvaana na Burkina Faso.
Timu nyingine 16 zilizofuzu kutoka raundi ya pili ni zile za Ligi Daraja la Kwanza na Daraja la Pili.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na TFF ni kwamba Jumamosi Januari 12, Majimaji itacheza dhidi ya JKT Mlale uwanja wa Majimaji mjini Songea, Januari 23 Pamba v Toto Africans uwanja wa CCM Kirumba, Ndanda FC v Mshikamano Nagwanda Sijaona Mtara, huku Burkinafaso wakiwakaribisha Simba SC katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Januari 24, Young Africans watacheza dhidi ya Friends Rangers uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Njombe Mji v Tanzania Prisons uwanja wa Amani Makambako, mjini Shinyanga Stand United watachuana dhidi ya Mwadui FC.
Mechi zingine ni Kagera Sugar v Rhino Rangers, Panone v Madini, Mtibwa Sugar v Abajalo, Lipuli/Kurugenzi v JKT Ruvu, Ashanti United v Azam FC, Africa Sports v Coastal Union, Geita Gold v Mgambo Shooting, Singida United v Mvuvuma na Wenda v Mbeya City.
Timu 15 zilizofuzu hatua ya tatu kutoka raundi ya pili ni Ashanti United, Friends Rangers, Panone, Geita Gold, Pamba, Mvuvuma, Burkinafaso, Rhino Rangers, Madini FC, JKT Mlale, Mshikamano FC, Njombe Mji, Wenda FC, Singida United, Abajalo huku mchezo mmoja kati ya Lipuli dhidi ya Kurugenzi ukichezwa leo Jumatano lakini ulishindwa kumalizika kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kuvunja mchezo dakika ya 23 na kesho Alhamisi utamaliza muda uliosalia ili kupata mshindi wa kufuzu raundi ya tatu.
Bingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) ataiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF CC) mwaka 2017.

Ratiba kamili hii hapa:
Jan 12, 2016
MajiMaji v JKt Mlale -Majimaji Songea
 

Jan 23, 2016 
Pamba v Totyo Africans- CCM Kirumba, Mwanza
Burkina Faso v Simba- Jamhuri, Morogoro
Ndanda v Mshikamano- Nangwanda Sijaona, Mtwara
 

Jan 24, 2016
 Yanga v Friends Rangers- Taifa, Dar es Salaam.
Njombe Mji v Prisons-Mbeya- Amani, Makambako
Stand United v Mwadui- Kambarage Shinyanga
 

Jan 25, 2016
 Kagera Sugar v Rhino Rangers- Ali Hassan Mwinyi, Tabora
Panone v Madini- Ushirika, Moshi
 

Jan 26, 2016 
Mtibwa Sugar vAbajalo-Jamhuri, Morogoro
Lipuli/Kurugenzi v JKT Ruvu-Wambi, Mafinga
African Lyon v Azam-Karume, Dar es Salaam
African Sports v Coastal Union-Mkwakwani Tanga
Geita Gold Sports v Mgambo JKT- Nyankungu, Geita
 

Jan 27, 2016 
Singida Utd v Mvuvumwa- Namfua, Singida
 

Feb 10, 2016
Wenda v Mbeya City- Sokoine, Mbeya

Azam kutetea taji la Kagame visiwani Zanzibar

Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye na Rais wa Heshima wa Cecafa, Leodger Tenga
AZAM FC watatetea taji lao la Kombe la Kagame visiwani Zanzibar, baada ya Baraza la Vyama vya Soka kwa Nchi za Afrika Mashariki na Kati, CECAFA kutangaza tarehe ya michuano hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema leo la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) inatarajiwa kufanyika Julai – Agosti mwaka huu kisiwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye amesema pamoja na michuano ya klabu kufanyika  Zanzibar mwaka huu, pia wamejipanga kuendesha michuano ya U17 itakayofanyika Mei huko Uganda, michuano ya Soka kwa Wanawake (Uganda), Mashindano ya vijana chini ya miaka 20 (Burundi) huku michuano ya Chalenji 2016 imepangwa kufanyika nchini Sudan.
Mwishoni mwa wiki uongozi wa Kamati ya Utendaji wa CECAFA ulikutana nchini Sudan na kufanya kikao chake cha kwanza chini ya Rais Dk. Mutasim Ghafar ambaye pia ni Rais wa Chama cha Soka nchini Sudan (SFA).
Katika kikao hicho, CECAFA ilitangaza kumpa Leodgar Tenga Rais wa heshima wa Cecafa huku pia wakisaini makubaliano ya uendelezaji wa soka la vijana na Chama cha Soka cha Saudi Arabia (SAFF) kupitia kwa Rais wake Ahmed Alharbi.
Azam ndio mabingwa wa watetezi wa Kagame waliotwaa Agosti mwaka jana jijini Dar es salaam, wakati Uganda ndio watetezi wa Kombe la Chalenji.

Thursday, December 10, 2015

UHONDO WA LIGI KUU BARA UMERUDI TENA

Kagera Sugar
Azam

Mbeya City

Yanga

Africans Sports

Simba
UHONDO unarudi. Ndio ule uhondo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara unatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii wakati viwanja sita vitakavyowaka moto, gumzo zikiwa mechi nne tofauti zikiwamo za wapinzani wa jadi wa mikoa ya Tanga na Shinyanga.
Mjini Shinyanga Stand United itavaana na Mwadui, huku Mkwakwani kutakuwa na vita vya Wagosi Wa Kaya dhidi ya Wana Kimanumanu.
Hata hivyo mechi zinazotolewa macho ni za Jumamosi wakati watetezi Yanga watakapokuwa ugenini kwenye dimba la Mkwakwani kuvaana na Mgambo JKT, huku watani zao Simba watakuwa jijini Dar es Salaam kupepetana na vinara, Azam FC.
Ligi Kuu ilisimama kwa muda wa mwezi mmoja na ushei kupisha maandalizi na mechi za kimataifa za timu za taifa, Taifa Stars na Kilimanjaro Stars zilizokuwa zikishiriki michuano ya kuwania fainali za Kombe la Dunia na Kombe la Chalenji.
Yanga iliyoondoka asubuhi ya leo kwenda Tanga ikiwa na kiungo mshambuliaji wake mpya kutoka Niger, Issofou Boubakar Garba, ikiwa na pengo la nahodha wake, Nadir haroub 'cannavaro' aliye majeruhi na kukiwa na hatihati ya kumtuma Donald Ngoma aliyeumia mkono juzi mazoezi, ingawa ameandamana na timu hiyo.
Yanga yenye pointi 22 itavaana na Mgambo ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuitambia timu hiyo katika mechi yao ya msimu uliopita ilipoifunga mabao 2-0 siku chache tangu Maafande hao walipoitoa nishai Simba, lakini nahodha wa Mgambo, Fully Maganga ametamba kulipa kisasi.
Azam wanaoongoza msimamo ikiwa na pointi 25 itaikaribisha Simba kwenye dimba la Taifa, ikiwa na sura mpya kikosini akiwamo Haji Ugando na Novatus Lufuga waliosajiliwa katika dirisha dogo.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa kali kutokana na upinzani wa timu hizo hasa ikikumbukwa msimu uliopita walikuwa wakiwania nafasi nyuma ya Yanga na kusababisha kutuhumiana 'kuumiza'.
Mechi nyingine za wikiendi hii ni Mtibwa Sugar kuvaana na Mbeya City ugenini, Majimaji kuialika Toto Africans na Kagera Sugar kuikaribisha Ndanda na  watani wa jadi Stand Utd na Mwadui watamaliza udhia Kambarage Shinyanga.
JUmapili kutakuwa na mechi mbili ikiwamo ya Coastal Union dhidi ya watani zao wa jadi Africans Sports, huku timu zote zikiwa katika hali mbaya katika msimamo sawa na JKT Ruvu watakaokuwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam kuvaana na Prisons Mbeya.
Baada ya mechi hizo za wikiendi hii, Yanga itasalia Mkwakwani Tanga kucheza na Sports katika mechi ya kiporo siku ya Jumatano ambapo pia siku hiyo Azam itaikaribisha Mtibwa Sugar huku kiporo kingine cha Simba na Ndanda kitasubiri kuchezwa Januari Mosi mwakani.

Msimamo kamili wa ligi hiyo inayorejea tena ni huu hapa:
1. Azam                9   8   1   0   20 5  25
2. Yanga               9   7   2  0   22  5  23
3. Mtibwa Sugar    9   7   1    1   12  5  22
4. Simba               9   7  0   2   15  5  21
5. Stand Utd         10  6   1  3   11  4  19
6. Prisons             10  5  2   3   10 10 17
7. Mwadui Fc         10  4   3   3   11  10  15
8. Toto Africans     10  3   4   3   6  12  13
9. Mgambo           10  3   2   5   6   9   11
10. Majimaji          10  3   2   5   6   14  11
11. Mbeya City       10  2   3   5   8   9   9
12. Ndanda             9   1    5   3   6   8   8
13. Coastal Union  10  1    4   5   2   8   7
14.JKT Ruvu           10  1   2    7   6   16  5
15. Kagera Sugar    10 1    2   7    2   13  5
16. African Sports  9   1   0   8    1    11  3

Wafungaji:
9- Elias Maguli                      (Stand)
8- Donald Ngoma                (Yanga)
     Hamis Kiiza                      (Simba)
6-Kipre Tchetche                 (Azam)
5-Amissi Tambwe               (Yanga)
4-Fully Maganga            (Mgambo)
   Miraji Athuman                  (Toto)
   Shomary Kapombe          (Azam)
  Jeremiah Juma               (Prisons)
3-Atupele Green              (Ndanda)
   Ibrahim Ajibu                   (Simba)
   Jerry Tegete                  (Mwadui)
   John Bocco                        (Azam)
   Mohammed Mkopi       (Prisons)
   Paul Nonga                   (Mwadui)
   Raphael Alpha                (Mbeya)
   Said Bahanuzi               (Mtibwa)
   Simon Msuva                   (Yanga)
   Didier Kavumbagu          (Azam)
2-Shiva Kichuya                (Mtibwa)
   Malimi Busungu              (Yanga)
   Edward Christopher         (Toto)
   Ally Myovela                 (Prisons)
   Pastory Athanas              (Stand)
   Mohamed Ibrahim       (Mtibwa)
   Mussa Kindu               (JKT Ruvu)
   Samuel Kamuntu        (JKT Ruvu)
1- Farid Mussa                       (Azam)
   Frank Domayo                   (Azam)
   Peter Mapunda            (Majimaji)
   Rodgers Fred                 (Mtibwa)
   Paul Ngway                      (Kagera)
   Themi Felix                      (Mbeya)
   Allan Wanga                      (Azam)
   Jumanne Alfadhil           (Prisons)
   Joseph Mahundi             (Mbeya)
   David Kambole               (Mbeya)
   Justice Majabvi                (Simba)
    Vincent Barnabas          (Mtibwa)  
   Mbuyu Twite                    (Yanga)
   Stamili Mbonde           (Majimaji)
   Rashid Mandawa          (Mwadui)
   Thabani Kamusoko          (Yanga)
   Michael Aidan             (JKT Ruvu)
   Najim Magulu              (JKT Ruvu)
   Kenneth Masumbuko   (Kagera)
   Kiggy Makassy              (Ndanda)
   Salim Mbonde              (Mtibwa)
   Mudathir Yahya                (Azam)
   Hassan Materema          (Sports)
   Joseph Kimwaga             (Simba)
   Alex Kondo                   (Ndanda)
   Salim Kipanga                 (Sports)
   Fabian Gwanse             (Mwadui)
   John Kabanda        (Mbeya City)
   Juuko Murshid                (Simba)
   Ally Shomary                (Mtibwa)
   Hassan Hamis             (Majimaji)
   Ismail Mohammed       (Coastal)
   Geofrey Mlawa      (Mbeya City)
   Abuu Daud                 (Mgambo)
   Malik Ndeule               (Mwadui)
   Bakar Kigodeko          (Mwadui)
   Samir Luhaba              (Majimaji)
   Nassor Kapamba         (Coastal)
   Mohammed Hussen     (Simba)
   Ditram Nchimbi         (Majimaji)
   Seleman Kibuta          (Mtibwa)
   Deus Kaseke                  (Yanga)
   Jabir Aziz                    (Mwadui)
   Juma Abdul                    (Yanga)  

Straika wa Simba atwaa tuzo Kenya

Michael Olunga
MFUNGAJI Bora wa Kombe la Kagame, na Striaka anayemezewa mate na Simba, Michael Olunga ametwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL) katika sherehe za tuzo hizo zilizofanyika usiku wa jana Jumatano nchini humo.
Simba imekuwa ikimfukuzia Olunga tangu alipofanya vizuri na Gor Mahia katika michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika Tanzania Julai mwaka huu na Azam kutwaa ubingwa wa michuano hiyo.
Olunga amefanikiwa kutwaa tuzo hiyo baada ya kufunga mabao 19 na kuisadia Gor Mahia kutwaa ubingwa wa KPL.
Kiungo, Khalid Aucho wa Gor Mahia pia aliyekuwa akiwaniwa na Yanga alishika nafasi ya pili katika tuzo ya Kiungo Bora wa msimu.
Kipa Boniface Oluoch ambaye naye alikuwa akinyemelewa na Simba mwanzoni mwa msimu huu alifanikiwa pia kung'ara katika tuzo hizo kwa kuwatwaa tuzo ya Kipa Bora.
Olunga hata hivyo ametajwa kuwa mbioni kutua klabu ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL) ya Mamelodi Sundown ambayo awali ilikuwa ikimvizia Donald Ngoma wa Yanga ila ikampotezea.

Dk Magufuli atangaza Baraza lake la Mawaziri, Nape aula

http://cdn2.yatosha.com/wp-content/uploads/2015/12/jbb1.jpg
Rais Magufuli (kati) akitangaza baraza lake la mawaziri leo pembeni yake ni Makamu wa Rais, Samia Suluhu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEixVj-oa8o8h5mtB7qrIg9WGVDM6DXh5u6ZCW-onFLhTkXs-61vgU9X7eaqUoCx8GWrXRqX9ue_A7SEYgiDS6_ax4QIF8Nqf2St4KsqRNJI5bi4jLzfOrkAVdVHMOHWcl5fOJIS4j7gkR4/s640/NAPELAANA-620x400.jpg
Waziri Mteule wa Wizara ya Habari Michezo na Wasanii, Nape Nnauye
Na Tareeq Badru
HATIMAYE Rais Dk John Magufuli ametengua kitendawili cha muda mrefu juu ya sura ya Baraza lake la Mawaziri, baada ya mchana huu kulitangaza Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli ametangaza Baraza lenye watu 19, huku mawaziri wanne wa wizara nyeti ikiwamo ya Fedha na Mipango ikikosa watu wa kuzishikilia.
Jumla ya Wizara 18 zimeundwa na Dk Magufuli, huku akitangaza kufuta semina elekezi ambayo katika Utawala wa Awamu ya Nne ilikuwa kama fasheni kufanya. Dk Magufuli alisema uamuzi huo wa kufuta semina elekezi hiyo ina lengo la kuokoa Sh Bilioni 2 ambazo zingetumika na kusema ni bora zitapelekwa kwenye Elimu kusaidia kutatua tatizo la Madawati.
Baraza hilo jipya la Awamu ya Tano ina sura mchanganyiko ikiwamo wazoefu waliokuwa katika uongozi uliopita, wengine wapya na mmoja Prof Sospter Muhongo ambaye alikuwa gumzo katika sakata ya Escrow lililoibuliwa mwishoni mwa Bunge la 10. Wizara ya Habari, Michezo na wasanii imepewa Katibu Mwenezi na Itikadi wa CCM Bara, Nape Nnauye.


Baraza hilo jipya la Dk Magufuli lipo hivi:

Wizara ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora: George Simbachakene  na Angella Kairuki
Naibu: Seleman Jaffo
Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira: January Makamba
Naibu: Luhaga Mpina
Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu: Jenista Muhagama
Manaibu: Dk. Possy Abdallah na Anthony Mavunde.
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi: Mwigulu Nchemba
Naibu: William Ole Nasha
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano: Hajapatikana
Naibu: Inj. Edwin Ngonyani
Wizara ya Fedha na Mipango:Hajapatikana
Naibu: Ashantu Kizachi
Wizara ya Nishati na Madini: Prof. Sospter Muhongo.
Naibu: Medalled Karemaligo.
Wizara ya Katiba na Sheria: Dk. Harrison Mwakyembe
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Dk. Augustino Mahiga
Naibu: Dk. Susan Kolimba.
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa: Dk. Hussein Mwinyi
Wizara ya Mambo ya Ndani:Charles Kitwanga.
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi: William Lukuvi
Naibu: Angelina Mabula
Wizara ya Maliasili na Utalii: Hajapatikana.
Naibu: Inj. Ramol Makani
Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji: Charles Mwijage.
Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi: Hajapatikana
Naibu: Inj. Stella Manyanya
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Ummy Mwalim
Naibu: Dk. Hamis Kigwangala
Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo: Nape Nnauye
Naibu: Anastasia Wambura.
Wizara ya Maji na Umwagiliaji: Prof. Makame Mbarawa
Naibu:Inj. Isack Kamwela

Friday, September 11, 2015

Hapa Javu, kule Bahanuzi, hivi mnatokaje kwa Mtibwa Sugar?

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdEulqye6NB2gXsPi5nX52ruKNuZkwLExeKIBZx9YhfvRv9i-1GRUvXwcGWe-uVRRKZzgwsiMkZgmzbo80RFdgxlHnANAjRcCAnSAEfyBFFwRCrJPMxsv_FBRuFjUHKP11ERryy3d8XlE/s640/Javu.jpg
Hussein Javu
STRAIKA Hussein Javu, ameziangalia timu 15 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza kesho Jumamosi. Kisha akakiangalia kikosi cha Mtibwa Sugar atakachokichezea msimu huu kwa mkopo akitokea Yanga ambacho kimesafiri mpaka Shinyanga ili kuanza msimu wa ligi dhidi ya Stand United, kisha akatabasamu huku akisema 'lazima heshima itarudi safari hii'.
Javu aliyesajiliwa na Yanga misimu miwili iliyopita akitokea Manungu, alisema kukutana kwake tena na Said Bahanuzi 'Spiderman' na wakali wengine ndani ya Mtibwa kumempa uhakika wa kurejesha heshima yake na ya klabu hiyo kwa mjumla katika ligi hiyo ya msimu huu.
Mtibwa iliyoanza kwa kasi katika ligi ya msimu uliopita kabla ya kutetereka, itaanzia mechi zake ugenini kabla ya kurudi Manungu kuzisubiri Ndanda na Majimaji kisha kuikaribisha Yanga katika pambano litakalochezwa Sept 30 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
"Kwa mziki huu uliopo Manungu, sioni wa kuizuia Mtibwa kurejesha heshima yake msimu huu, ni kazi pevu lakini tumejiandaa kufanya makubwa, hasa kutokana na kurudi nyumbani chini ya kocha Mecky Maxime," alisema Javu.
Javu, Bahanuzi ni baadhi ya wachezaji wapya nane waliotua kwa Wakata Miwa hao kwa ajili ya kuunda kikosi cha msimu huu cha Mtibwa Sugar chenye wachezaji 28, wakiwamo 20 waliokuwa msimu uliopita.
Wengine nane wapya ni kipa Hussen Sharrif 'Casillas' na Issa Rashid 'Baba Ubaya' ambao nao wamerudisha majeshi nyumbani wakitokea Simba.

Lazima pachimbike Chanika, Ndonga zitapigwa hivi hivi!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEje2A78vXEe4Uo4cv-6s9mPx6Wq0Kif0wcoRpp930ZWk7OtAr3bMYet3LfivlK4JOjJVKxsPedLOpmffHtjd8sUlXJ6TL__ItbNw2pPa5ln6JBd4j88n55qMINxDsDLkfem7sagV3-nZwKR/s640/super+d+boxing+promotion.jpg
IWE isiwe ni lazima pachimbike Chanika, hii ni kutokana na mabondia Said Mbelwa na George Dimoso wanatarajiwa kupanda ulingoni ili kuzichapa katika pambano la kuwania Ubingwa wa Taifa wa ngumi za kulipwa.
Mabondia hao watazichapa siku ya Septemba 26 kwenye Ukumbi wa Butiama Villa Club, Chanika ambapo siku hiyo mashabiki wa soka hasa wa Simba na Yanga watakuwa wameshafahamukitu gani walichovuna kwenye pambano lao la  watani litakalofanyika kwenye Uwanja wa Taifa katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2015-2016.
Mratibu wa pambano hilo, Rajabu Mhamila 'Super D', alisema kuwa Mbelwa na Dimoso ambao tayari wapo kwenye kambi zao za maandalizi huku wakitambiana watazipiga katika pigano la raundi 10.
Super D alisema pambano hilo la uzito wa kati litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiliwemo la Seleman Zugo dhidi ya  Abdallah Luanje, Adam Ngange atakayeumana na Shaaban Mtengela.
Siku hiyo pia Said Uwezo ataonyesha uwezo wake dhidi ya Hassan Mgosi, Hamza Mchanjo yeye ataumana na Ally Maiyo katika mipambano tofauti isiyo ya ubingwa.
Super D alisema siku hiyo kutakuwa na uuzwaji wa DVD mpya za michezo kadhaa ya ngumi za kimataifa likiwamo pambano lililofunika mwaka huu wa 2015 kati ya Manny Pacquiao na Floyd Mayweather ambalo liliisha kwa Mmarekani Money Man kumchapa Man Pac

KUMEKUCHA LIGI KUU YA TANZANIA BARA 2015-2016

http://www.soka25east.com/wp-content/uploads/2015/08/image17.jpg
Watetezi Yanga
http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/07/Kikosi-cha-azam.jpg
Azam Fc washindi wa pili wa msimu uliopita
http://simbasports.co.tz/file/2015/08/simba-sports-club-212.jpg
Simba waliokamata nafasi ya tatu msimu uliopita
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/07/MBY-CITY.jpg
Mbeya City iliyokimbiwa na nyota wake wengi
VITA vya takriban miezi tisa vitakavyohusisha klabu 16 vinatarajiwa kuanza kesho Jumamosi wakati pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2015-2016 litakapofunguliwa rasmi.
Michezo saba itakayopigwa kwenye viwanja saba tofauti inatarajiwa kukata utepe wa ligi hiyo, kabla ya keshokutwa Jumapili kupigwa pambano la kukamilisha raundi ya kwanza litakalozikutanisha mabingwa watetezi, Yanga na mabingwa wa zamani Coastal Union ya Tanga.
Mechi za fungua dimba zitakazopigwa leo Jumamosi ni pamoja na lile la mabingwa wa Tanzania wa mwaka 1988 waliorejea Ligi Kuu baada ya miaka zaidi ya 20 itakayovaana na Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Simba haijaonja ushindi kwenye Uwanja huo tangu mwaka 2012 pale Patrick Mafisango alipofunga bao pekee na la ushindi wakati timu hiyo ikiizamisha Coastal Union kwa bao 1-0.
Mechi nyingine ni ile itakayozikutanisha Stand United dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Kambarage Shinyanga, Mwadui itakuwa wageni wa Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza na Majimaji Songea itaialika JKT Ruvu katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Ndanda watakuwa wenyeji wa maafande wa Mgambo JKT pale Nangwanda Sijaona, Mtwara, huku Azam itaikaribisha Prisons Mbeya Uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es Salaam na Mbeya City kuvaana na wakata Miwa wa Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.


Msimu wa 52
 Huu utakuwa ni msimu wa 52 tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo mnamo mwaka 1965 ikiwa na maana mwaka huu wa 2015 ni mwaka wa 50 tangu kuanza kwa michuano hiyo mikubwa nchini.
Klabu 16, nne zikiwa zilizopanda daraja na kurejea Ligi Kuu ya Bara na nyingine 12 zilizosalimika kwenye ligi iliyopita zitachuana kuwania taji hilo ambalo kwa sasa linashikiliwa na mabingwa wa kihistoria wa ligi hiyo, Yanga.
Yanga ndiyo klabu iliyotwaa mara nyingi ubingwa wa ligi hiyo tangu mwaka 1965, ikitwaa mara 25, huku wakifuatiwa kwa mbali na watani zao, Simba walionyakua mara 18.
Mtibwa Sugar ya Morogoro ndiyo klabu inayovisogelea vigogo hivyo ikiwa imeshinda ubingwa mara mbili mwaka 1999 na 2000, huku timu nyingine sita za Cosmo, Mseto, Pan Africans, Tukuyu Stars na Azam kila moja zikinyakua mara moja moja na kuhitimisha orodha ya mabingwa wa ligi.

Haina ugeni

 Majimaji-Songea, African Sports, Toto Africans na Mwadui Shinyanga ndizo klabu zilizopanda daraja msimu huu zikitokea katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL), ila ukweli ni kwamba hazina ugeni na ligi hiyo.
Kwa nyakati tofauti timu hizo zimeshaichezea ligi hiyo kabla ya baadhi kuzama kimoja kama ilivyokuwa kwa Mwadui iliyoshuka daraja mwaka 1986, Sports (1991) na Majimaji na Toto Africans zikipanda na kushuka kila zilipokuwa zikijisikia.
Kwa maana hiyo ligi ya msimu huu haina klabu ngeni za ligi hiyo, japo baadhi zimerejea kuichezea ikiwa imepita miaka mingi.
Ujio wa Mwadui na Sports na hata Majimaji unakumbusha enzi za Ligi Daraja la Kwanza ambapo klabu hizo zilijijengea jina kubwa kwa mafanikio iliyopata kwa nyakati tofauti kabla ya kupotea.
Zinakutana na klabu zilizolowea kwenye ligi hiyo kama Yanga, Simba, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar, Azam na JKT Ruvu ambazo tangu zianze kushiriki ligi hiyo kwa misimu tofauti hazijawahi kushuka daraja.
Mbali na klabu hizo ngangari, pia zitakumbana wakali wengine kama Coastal Union, Prisons-Mbeya, Stand United, Mgambo JKT, Mbeya City na Ndanda.

Mchuano 

Kama misimu mingine iliyopita, ligi ya safari hii inatarajiwa kuwa na mchuano mkali kati ya klabu shiriki na hata kwa wachezaji waliosajiliwa na klabu hizo. Inatarajiwa kuwepo kwa mchuano wa wachezaji wazawa na wale wa kigeni (mapro) sambamba na makocha kutunishiana misuli.
Jumla ya makiocha 16 wakuu, wakiwamo sita wa kigeni watakuwa na kazi ya kuthibitisha ubora wao katika msimu huu, sawa na itakavyokuwa kwa wachezaji mapro dhidi ya wazawa ambao msimu uliopita walifunika mwanzo mwisho kwa kunyakua tuzo karibu zote za VPL 2014-2015.
Simon Msuva aliweka rekodi ya kunyakua tuzo ya Mfungaji Bora akiwa na mabao yake 17 na pia tuzo ya Mchezaji Bora wa msimu, huku Kipa Bora akiwa ni Shaaban Kado na Kocha Bora ikienda kwa Mbwana Makata.
Je, wazawa wamezinduka na kuendelea kuwafunika mapro au ni nguvu ya soda tu baada ya misimu kadhaa ya kukimbizwa mchakamchaka na wachezaji wa kigeni waliotawala kila kona? Tusubiri, japo inatarajiwa msimu huu inatabiriwa kuibuka kwa nyota wapya ambao watafunika kutokana na vipaji vyao turufu ikiwabeba akina Geofrey Mwashiuya, Matheo Simon, Farid Mussa, Deus Kaseke, Malimi Busungu na wengineo.

Utabiri 

Kwa namna klabu zilizofanya usajili mzuri na kufanya maandalizi ya kutosha ni vigumu kutabiri moja kwa moja klabu zenye nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa msimu huu, lakini kwa kuangalia kikosi kimoja kimoja turufu inaziangukia timu za Yanga, Azam, Simba na Mwadui Shinyanga.
Hata hivyo kwa kuwa soka ni mchezo usiotabirika kirahisi siyo ajabu kuziona Stand United, JKT Ruvu, Majimaji, Coastal Union na Mtibwa Sugar zikichanua na kusumbua msimu huu.
Katika janga la kushuka daraja mwishoni mwa msimu kura inaziangukia Ndanda, Mgambo JKT, African Sports, Toto Africans na Prisons-Mbeya, kama hazitakaza buti na kupambana zitaenda na maji. Hii ni kwa sababu zilionekana kutojipanga kama klabu nyingine, japo siri ya mtungi...!
Zikikaa vibaya zinaweza kujikuta mwishoni mwa msimu zikifuata mkumbo wa Ruvu Shooting na Polisi Moro zilizoshuka msimu uliopita, pia zinapaswa kufahamu msimu huu timu tatu ndizo ambazo zitakazoteremka daraja hivyo zijipange kwelikweli. 


Ratiba:

Kesho Jumamosi:
Ndanda     v Mgambo JKT
African Sports v Simba
Majimaji    v JKT Ruvu
Azam         v Prisons
Stand Utd   v Mtibwa Sugar
Toto Africans   v Mwadui Fc
Mbeya City   v Kagera Sugar
 

Jumapili:
Yanga    v Coastal Union
 

Jumatano:
Yanga v Prisons
Mgambo JKT v Simba
Majimaji  v Kagera Sugar
Mbeya City v JKT Ruvu
Stand Utd  v Azam
Toto Africans v Mtibwa Sugar
Ndanda v Coastal Union
Alhamisi:

Mwadui FC v African Sports
 

Orodha ya Mabingwa tangu 1965-20151965- Sunderland (Simba)
1966- Sunderland (Simba)
1967- Cosmopolitan
1968- Yanga
1969- Yanga
1970- Yanga
1971- Yanga
1972- Yanga
1973- Simba
1974- Yanga
1975- Mseto
1976- Simba
1977- Simba
1978- Simba
1979- Simba
1980- Simba
1981- Yanga
1982- Pan Africans
1983- Yanga
1984- Simba
1985- Yanga
1986- Tukuyu Stars
1987- Yanga
1988- Coastal Union
1989- Yanga
1990- Simba
1991- Yanga
1992- Yanga
1993- Yanga
1994- Simba
1995- Simba
1996- Yanga
1997- Yanga
1998- Yanga
1999- Mtibwa Sugar
2000- Mtibwa Sugar
2001- Simba
2002- Yanga
2003- Simba
2004- Simba
2005- Yanga
2006- Yanga
2007- Simba
2007/08- Yanga
2000/09- Yanga
2009/10- Simba
2010/11- Yanga
2011/12- Simba
2012/13- Yanga
2013/14- Azam
2014/15- Yanga
2015/16   ???

Vinara
25-Yanga
18-Simba
2-Mtibwa
1-Cosmo, Mseto, Pan, Tukuyu, Coastal, Azam

Saturday, August 22, 2015

Nafasi nyingine kwa Manchester Utd EPL


http://strettynews.com/wp-content/uploads/2015/02/UnitedvPreston.jpg
Mashetani Wekundu ambao wamekuja kivingine msimu huu
Chelsea
Watetezi Chelsea wanaopepesuka
KIVUMBI cha Ligi Kuu England kinaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini mapema saa 8;30 mchana Mashetani Wekundu watakuwa wakisaka nafasi ya kurejea kileleni japo kwa sasa kadhaa wakati watakapovaana na vibonde Newcastle United kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Manchester United yenye pointi sita inaweza kuiengua Man City ambayo yenye itacheza kesho dhidi ya Everton kwa kufikisha pointi 9 kama itashinda huku ikiombea Leicester City ipoteze mchezo wake wa leo dhidi ya Tottenham Hotspur.
Ratiba kamili ya ligi hiyo kwa leo, kesho Jumapili na Jumatatu ambapo Arsenal itakuwa na kibarua kigumu cha kuibakaribisha Liverpool ipo hapo chini jionee mwenyewe;
Leo Jumamosi:
Manchester United     11 : 45    Newcastle United        
Crystal Palace     14 : 00    Aston Villa        
West Ham United     14 : 00    AFC Bournemouth        
Norwich City     14 : 00    Stoke City        
Sunderland     14 : 00    Swansea City        
Leicester City     14 : 00    Tottenham Hotspur        
Kesho Jumapili
West Bromwich Albion 12 : 30    Chelsea        
Everton     15 : 00    Manchester City        
Watford     15 : 00    Southampton        
Jumatatu
Arsenal     19 : 00    Liverpool

PATACHIMBIKA TAIFA, YANGA v AZAM NI SHEEDA!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjpjkGwXmOK250PzIJkj4gA7pkZ1mMpkKFXP2MG3mX3y_l3IHb7aHldzJdHcS2u-VTXyZldrrwgZtbd-yV0ndewKQDYjerOJ3aSNEVPxtJHCgeoHY8UgogGyJ-jYXVUU7COyj83XDERC6g/s1600/IMG_8065.JPG
Azam FC
Yanga
MABINGWA wa soka wa Tanzania, Yanga pamoja na Mabingwa wa Kombe la Kagame, Azam jioni ya leo wanatarajia kuonyeshana undava wakati zitakapokutana kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani.
Mchezo huo maalum kwa ajili ya kuzindua msimu mpya wa Ligi kuu ya Tanzania Bara utapigwa dimba la Taifa, huku timu zote zikitarajiwa kuwakosa baadhi ya nyota wake kutokana na matatizo mbalimbali.
Yanga ambao imeonyesha kuupania mchezo huo hasa baada ya kutolewa nishai na Azma kwenye robo fainali ya Kombe la Kagame, huenda isiwe na Amissi Tambwe aliyekuwa akisumbuliwa na Malaria, japo Donald Ngoma anaweza kucheza akitoka kuuguza maumivu ya nyonga.
Azam wenyewe wanaosaka ushindi wa kwanza wa mchezo huo wa Ngao ya Hisani na pia kujaribu kufuta uteja kwa wapinzani kila wakikitana kwenye pambano hilo inaweza kumkosa Kipre Tchetche.
Hata hivyo vikosi vyote chini ya makocha wao, Stewart Hall kwa Azam na Hans van Pluijm wa Yanga wamenukuliwa wakitamba kuwa leo itakuwa kazi tu, na kuzipa matumiani timu yao kushinda.
"Yanga ni wazuri na ni timu kubwa na unapocheza nao ni kama ina wachezaji 12 kutokana na mashabiki wanaoiunga mkono, lakini tupo tayari na vijana wanagu wana ari ya kushinda," alisema.
Pluijm alisema kuwa ameandaa vijana wake kwa ajili ya kazi moja ya kushinda Taifa, hasa baaada ya kuridhishwa na mabadiliko aliyoyaona kwa safu yake ya mbele wakiwa jijini Mbeya kwenye kambi.
Bila ya shaka mashabiki wa soka watapata uhondo katika mchezo huo utakaochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya baada ya refa wa awali, Israel Nkongo kupatwa na dharura ya kuugua na kuenguliwa.
Rekodi Azam Ngao ya Hisani:
2012: Simba 3-2 Azam
2013 Azam 0-1 Yanga
2014: Yanga 3-0 Azam
2015: Azam v Yanga???

Friday, August 21, 2015

3 zachemsha usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2015-2016

Stand United
Toto Africans
WAKATI dirisha la usajili kwa klabu vya Ligi Kuu nchini (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) likifungwa juzi klabu tatu za VPL vimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji katika muda uliopangwa.
 Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) alivitaja Klabu za Coastal Union ya Tanga, Stand United ya Shinyanga na Toto African ya jijini Mwanza kuwa zimeshindwa kuwasilisha usajili wao na kusema faini ni 500,000  kwa mchezaji mmoja hivyo klabu iliyochelewesha usajili au itakayobadili majina au kuongeza majina baada ya usajili kufungwa italazimika kulipia faini
“Usajili umefungwa jana (juzi) na timu tatu hazijawasilisha usajili wao hata wa mchezaji mmoja pamoja na TFF kuongeza muda wa usajili kwa wiki mbili”, alisema Kizunguto
Pia alisema si kwamba timu zingine zimefikisha idadi ya wachezaji wote kulingana na kanuni bali zingine zimesajili wachezaji 18, 24 hivyo hata wao endapo wataongeza watalipia faini.
Kizuguto alikumbusha timu ambazo zimesajili wachezaji wa kigeni kuwasilisha ada zao ili waweze kupata kbali cha kucheza ligi.
Awali TFF ilitoa muda wa wiki mbili kwa vilabu vyote nchini kukamilisha usajili, ambapo vilabu 13 vya ligi kuu vimeweza kukamilisha ndani ya wakati, klabu 24 vya ligi daraja la kwanza, klabu 24 ligi daraja la pili pia vimeweza kukamilisha usajili wao ndani ya muda uliopangwa.


Mkwasa ataja majembe yake ya Uturuki, Dida aachwa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/06/Mkwasa-Stars.jpg
Kocha Mkwasa (kushoto) na Msaidizi wake, Hemed Morocco
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 22 atakaoondoka nao kuelekea Uturuki kupiga kambi ya kuiwinda Nigeria.
Wachezaji hao 22 wanatarajiwa kuondoka nchini Jumapili  usiku kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaochezwa Septemba 05, 2015. Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto, alisema kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa ametoa orodha ya wachezaji 22 watakaosafiri usiku wa jumapili. “Orodha ya wachezaji 22 imetoka katika kikosi kilichotangazwa wiki mbili zilizopita na Mkwasa ambapo walipata nafasi ya kufanya mazoezi kwa takribani wiki moja katika uwanja wa Karume”, alisema Kizuguto. Kizuguto alisema wachezaji wote waliochaguliwa kujiunga na timu ya Taifa wanapaswa kuripoti kambini Tansoma Hotel Jumapili saa 5 asubuhi kwa maandalizi ya mwisho ya safari hiyo. Wachezaji waliochaguliwa ni All Mustafa Aishi Manula, Said Mohamed, walinzi Shomari Kapombe, Abdi Banda, Mohamed Hussein, Hassan Isihaka, Juma Abdul, Haji Mngwali, Kelvin Yondani, Nadir Haroub. Wengine ni Mudathir Yahya, Himid Mao, Frank Domayo, Salum Telela, Deus Kaseke, Said Ndemla, John Bocco, Farid Musa, , Rashid Mandawa, Saimon Msuva, na Ibrahim Ajib. Taifa Stars kwa usafiri wa shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), na itafika jijini Istambul jumatatu asubuhi, ambapo itaelekea katika mji wa Kocael   kuweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Green Park Kartepe.

Man United wakatwa maini kwa Sadio Mane

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/05/16/16/28BDB01200000578-3084365-Southampton_s_Sadio_Mane_celebrates_the_first_of_the_first_half_-a-3_1431789411065.jpgKLABU ya Southampton imekiri kuwa Manchester United wanamuwania winga wao wa kimataifa wa Senegal Sadio Mane, lakini ikatamka wazi kwamba mkali huyo hauzwi ng'o.
Wiki iliyopita Southampton walikanusha taarifa za kupokea ofa yeyote kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23. Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21. 
Kutokana na hali hiyo United wameamua kuongeza nguvu zao katika kumsajili Mane kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi. Mane amefunga mabao 10 katika mechi 32 alizocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu -hat-trick kwa muda mfupi zaidi.
Hata hivyo mapema leo Ijumaa klabu hiyo ya Southampton imeweka bayana kwamba mchezaji huyo hauzwi hivyo Man United watafute pengine pa kupata mchezaji mpya.
Meneja wa The Saints, Ronald Koeman amefunguka kuwa mchezaji huyo hauzwi kwa bei yoyote.

Straika Msenegal atua Msimbazi, amtia tumbo joto Kiiza

Niang mwenye kofia akiwasili
Niang akipokea simu mara baada ya kuwasili kwenye hoteli aliyofikia jijini Dar es Salaam
Akiwaskiliana alipowasilia hotelin
KLABU ya Simba imezidi kujiimarisha baada ya mchana huu kumpokea straika kutoka Senegal, Papa Niang, ambaye anatarajiwa kupimwa Jumatatu wakati Simba ikiumana na Mwadui Shinyanga kabla ya kusainishwa mkataba wa kukipiga Msimbazi.
Niang ambaye ni mdogo wa nyota Mamadou Niang, mshambuliaji ambaye itachukua muda Watanzania kumsahau baada ya kuizamisha Taifa Stars kwa mabao 4 ametua akiambatana na meneja wake, Massouka Ekoko.
Ujio wa straika hutyo aliyekuwa akicheza soka la kulipwa El Salvador kunamaanisha kuwa kama mipango itaenda sawa basi kuna uwezakano wa dili la Mrundi Kevin Ndatisenga aliyeifungia Simba moja ya mabao mawili wakati wakiiua URA ya Uganda likafa.
Pia hata kibarua cha Hamis Kiiza 'Diego' ambaye ameanza kuwekewa zengwe huenda nacho kikaota nyasi, ili kutimiza idadi ya wachezaji saba wa kimataifa wanaohitajiwa na timu hiyo.
Mpaka sasa ina wachezaji sita wa kigeni ambao ni Justice Majabvi, Emiry Nibomana, Hamis Kiiza, Juuko Murshid na Simon Sserunkuma, huku pia ikiwa imetoa kwa mkopo Raphael Kiongera aliyepo KCB ya Kenya.
Wakati Niang akitua leo zipo taarifa kutoka Msimbazi kwamba straika mwingine mkali atatua siku yoyote kuanzia leo kumaliza na mabosi wa Simba, ikiwa ni mikakati ya kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa misimu mitatu hakijaonja ladha ya ubingwa wa Tanzania Bara.

Dondoo kuhusu Niang
Jina kamili: Papa Niang
Tarehe ya kuzaliwa: 5 Disemba, 1988 (miaka 26)
Mahali alipozaliwa: Matam Senegal
Urefu: Mita 1.81 
Nafasi anayocheza: Mshambuliaji
Klabu alizowahi kuzitumikia:
Kwasasa: Mchezaji huru
2005-2006: ASC Thies 
2007: FC OPA
2008: AC Oulu
2009-2012: FF Jaro
2013: FC Vostok
2013-2014: Al -Shabab SC
2014-2015: FC Mounana