WAKALA wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini, RITA, umewataka waumini wa Jumuiya ya Answar Sunna Tanzania wanaoshinikiza uongozi wa juu ya jumuiya hiyo ung'oke madarakani kutulia hadi watapotoa maamuzi yao mwishoni mwa mwezi huu.
Waumini hao wa Answar Sunna wanataka uongozi wao ung'oke kwa kukiuka katiba na kushindwa kuiendesha kwa mafanikio jumuiya yao inayotajwa ni taasisi kubwa ya pili nchini baada ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania, BAKWATA.
Meneja wa Ufilisi na Udhamini wa RITA, Linna Msanga Katema, aliiambia MICHARAZO kuwa, ofisi yao inatambua kuwepo kwa mgogoro ndani ya jumuiya hiyo baina ya waumini na uongozi wao na wanaendelea kuufanyia kazi.
Linna, alisema hatua waliyofikia katika kuutatua mgogoro huo ni vema waumini kupitia kamati yao maalum wakavuta subira ili waweze kutoa maamuzi mwishoni mwa mwezi huu baada ya kukutana na kupitia vielelezo vya pande hizo mbili.
Meneja huyo, alisema tofauti na hapo awali walipokuwa wakikosa ushirikiano toka kwa viongozi wanaolalamikiwa wakiwemo Baraza la Wadhamini na Amiri wa Jumuiya hiyo, Sheikh Juma Poli, sasa mambo ni shwari na ndio maana wanataka waumini watulie.
"Tumeshawaandikia barua kuomba watupe muda wa mwezi mmoja toka Julai 26 hadi Agosti 26, ili RITA tutoe maamuzi juu ya kinachoendelea baina ya pande hizo mbili, hivyo tunaomba waumini watulie haki itatendeka," alisema Linna.
Nao waumini hao waliofanya mkutano wao Jumapili iliyopita walitoa maamuzi ya kuvuta subiri ili kuona RITA itaamua nini, lakini wakisisitiza wanataka haki itendeke kwa manufaa ya jumuiya yao waliyodai inazidi kudumaa kutokana na uongozi uliopo.
Wakizungumza kwenye mkutano huo waumini hao waliutaka uongozi wa kamati yao inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Hamis Buguza na Katibu, Abdulhafidh Nahoda, kuendelea kufuatilia kujua RITA itaamua kitu gani na wao wameamua kuvumilia.
Mzozo wa waumini na uongozi wa jumuiya hiyo ulianza tangu mwaka juzi kutokana na madai ya ukiukwaji katiba ikiwemo kutoitishwa kwa mikutano kwa muda wa miaka 10, pamoja na kubinafsishwa mali za jumuiya hiyo bila waumini hao kushirikishwa.
Katibu wa Baraza la Wadhamini wa Jumuiya, Abdalla Lihumbi, alinukuliwa na gazeti hili wiki iliyopita akikiri uongozi wao kwenda kinyume akidai wanafanya mipango ya kupata suluhu kwa manufaa ya jumuiya yao iliyotambuliwa kitaifa mwaka 1992.
Mwisho
STRIKA

USILIKOSE

Monday, August 8, 2011
Simba Day ni leo Arusha, uhondo wapungua

KUHAMISHWA kwa tamasha la klabu ya Simba, 'Simba Day' kupelekwa jijini Arusha kumevuruga baadhi ya ratiba zilizokuwa zimepangwa, ingawa uongozi umesema kila kitu kipo sawa na kwamba leo watatambulisha rasmi kikosi chao kipya cha msimu huu jijini humo.
Tamasha hilo linalofanyika kwa mwaka wa tatu mfululizo, awali lilipangwa kufanyika jijini Dar es Salaam, lakini limekwama baada ya kukosekana muafaka wa malipo baina ya uongozi wa klabu hiyo na ule unaosimamia uwanja wa Taifa, na kulazimika kupelekwa Sheikh Amri Abeid.
Kutokana na kuhamishwa huko mkoani Arusha, baadhi ya mambo yaliyotarajiwa kufanyika leo kama pambano la timu za vijana za Simba na Azam U20 limefutwa na badala yake itachezwa mechi ya timu ya veterani ya Arusha dhidi ya viongozi wa Simba.
Kadhalika, bendi na vikundi vilivyokuwa vitumbuize katika tamasha hilo, pia vimeshindikana sawa na tukio la utoaji wa tuzo za wadau walioisaidia Simba kwa hali na mali, ambapo kesho watapewa wachache watakaobahatika kwenda jijini Arusha na wengine watatangazwa tu.
Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, aliiambia MICHARAZO, kuwa pamoja na hali iliyotokea iliyowatatiza kidogo, kila kitu kinatarajiwa kufanyika kwa ufanisi leo ambapo timu yao itakitambulisha rasmi kikosi chao kipya chenye wachezaji wapya wa kimataifa.
"Ni kweli kuhamishwa kwa tamasha hili toka Dar hadi Arusha kumevuruga baadhi ya mambo, lakini kila kitu kipo sawa na wakazi wa Arusha watarajie burudani ya kutosha kwani mambo yamerekebishwa, ili kufanikisha tamasha hilo," alisema Kamwaga.
Kamwaga, alisema kikosi chao tayari kipo jijini humo tangu Ijumaa kikijifua kabla ya leo kuvaana na Simba ya Uganda iliyotarajiwa kutua jana na kusafiri kwenda Arusha kwa ajili ya mechi hiyo ya kirafiki ya kimataifa.
Alisema kikosi chao kipo kamili ukiondoa Mwinyi Kazimoto anayeendelea kujiuguza majeraha yake aliyopata siku ya mechi ya fainali ya Kombe la Kagame kati ya Simba na Yanga, huku wachezaji wengine wawili, Ulimboka Mwakingwe na Amri Kiemba wakirejea toka majeruhi.
Kamwaga alisema watatumia tamasha hilo na hasa mechi yao na Simba ya Uganda kupima kikosi chao kabla ya kuvaana na Yanga wiki ijayo katika pambano la Ngao ya Jamii ikiwa ni uzinduzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Simba na Yanga zinatarajiwa kuvaana Agosti 17 katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, ikiwa ni wiki kadhaa tangu timu hizo kukutana kwenye fainali hizo za kombe la Kagame na Yanga kuibuka mshindi wa bao 1-0 lililofungwa na Mghana Kenneth Asamoah.
Mwisho
Villa Squad yahaha kusaka Mil 7.2 kuianza Ligi Kuu
UONGOZI wa klabu ya soka ya Villa Squad inahaha kusaka kiasi cha Sh. Milioni 7 kwa ajili ya kuiwezesha timu yao kwenda kuianda Ligi Kuu Tanzania Bara 2011-2012 ugenini Kanda ya Ziwa, huku aliyekuwa mlezi wao, Abdalla Bulembo akisisitiza kujiweka kando katika uongozi.
Villa iliyorejea kwenye ligi hiyo baada ya kushuka daraja mwaka 2008, imepangwa kuanza mechi zake kwa kucheza na Toto Afrika siku ya uzinduzi wa ligi hiyo Agosti 20 kabla ya kuivaa Kagera Sugar ndipo irejee Dar es Salaam kucheza mechi za nyumbani.
Habari za ndani za klabu hiyo zilizothibitishwa na uongozi wake zinasema kuwa, kwa bajeti ya haraka inayotakiwa kwa timu hiyo kwenda kucheza mechi hizo mbili za awali za Ligi Kuu inahitajika kiasi cha Sh. Milioni 7.2 ambazo klabu haijui itazipata wapi kwa sasa.
Katibu wa Villa, Masoud Yasin, alisema kinachowachanganya zaidi ni kuchelewa kutolewa kwa fedha toka kwa wadhamini ambazo kwa kawaida hupitia Shirikisho la Soka Tanzania, TFF na kutoa wito kwa wadau wa soka wa Dar es Salaam hasa wakazi wa Kinondoni kuwasaidia.
"Tunaomba wadau wa soka watusaidie ili Villa tuweze kuianza ligi kwa umakini kwani tuna hali mbaya ya kiuchumi, na hasa kuzisaka fedha hizo kwa ajili ya mechi hizo mbili za kanda ya Ziwa ambapo bajeti yake ni zaidi ya Sh. milioni saba," alisema katibu huyo.
Yasin, alisema hali yao kiuchumi ni mbaya na hawajui watafanyaje katika ushiriki wao hasa baada ya mlezi wao, Abdalla Bulembo kujiweka kando akikataa hata kuzishika nafasi ambazo zipo nje ya katiba yao kama pendekezo lililotolewa na Rais wa TFF, Leodger Tenga.
Tenga alitoa pendekezo hilo wakati akitatua sakata la kuenguliwa kwa Bulembo kuwania Uenyekiti wa Villa na kuibua mtafaruku kabla ya kutulizwa kwa uchaguzi huo kufanyika kwa kuachwa wazi nafasi zilizokosa wagombea wake ikiwemo hiyo ya Mwenyekiti.
Bulembo mwenyewe alipotafutwa na gazeti hili, alikiri ni kweli hana haja ya uongozi baada ya TFF kumwekea kauzibe, ingawa alisema anasikitika na hali inayoendelea na viongozi wa soka nchini kushindwa kuonyesha dhamira ya kweli ya kuinua mchezo huo kupitia klabu ndogo.
"Sitaki hata kusikia habari za kuongoza tena, maadam TFF iliamua kunikwamisha basi mie naendelea na shughuli zangu, ila sidhani kama viongozi wa soka nchini wanania ya kuinua mchezo huu," alisema Bulembo.
Villa ni miongoni mwa timu nne zilizopanda ligi kuu toka daraja la kwanza nyingine zikiwa ni JKT Oljoro Arusha, Coastal Union ya Tanga na Moro United ya Dar es Salaam na tayari TFF imeshatangaza ratiba ya kuanza kwa ligi hiyo Agosti 20 ikishirikisha jumla ya timu 14.
Mwisho
Villa iliyorejea kwenye ligi hiyo baada ya kushuka daraja mwaka 2008, imepangwa kuanza mechi zake kwa kucheza na Toto Afrika siku ya uzinduzi wa ligi hiyo Agosti 20 kabla ya kuivaa Kagera Sugar ndipo irejee Dar es Salaam kucheza mechi za nyumbani.
Habari za ndani za klabu hiyo zilizothibitishwa na uongozi wake zinasema kuwa, kwa bajeti ya haraka inayotakiwa kwa timu hiyo kwenda kucheza mechi hizo mbili za awali za Ligi Kuu inahitajika kiasi cha Sh. Milioni 7.2 ambazo klabu haijui itazipata wapi kwa sasa.
Katibu wa Villa, Masoud Yasin, alisema kinachowachanganya zaidi ni kuchelewa kutolewa kwa fedha toka kwa wadhamini ambazo kwa kawaida hupitia Shirikisho la Soka Tanzania, TFF na kutoa wito kwa wadau wa soka wa Dar es Salaam hasa wakazi wa Kinondoni kuwasaidia.
"Tunaomba wadau wa soka watusaidie ili Villa tuweze kuianza ligi kwa umakini kwani tuna hali mbaya ya kiuchumi, na hasa kuzisaka fedha hizo kwa ajili ya mechi hizo mbili za kanda ya Ziwa ambapo bajeti yake ni zaidi ya Sh. milioni saba," alisema katibu huyo.
Yasin, alisema hali yao kiuchumi ni mbaya na hawajui watafanyaje katika ushiriki wao hasa baada ya mlezi wao, Abdalla Bulembo kujiweka kando akikataa hata kuzishika nafasi ambazo zipo nje ya katiba yao kama pendekezo lililotolewa na Rais wa TFF, Leodger Tenga.
Tenga alitoa pendekezo hilo wakati akitatua sakata la kuenguliwa kwa Bulembo kuwania Uenyekiti wa Villa na kuibua mtafaruku kabla ya kutulizwa kwa uchaguzi huo kufanyika kwa kuachwa wazi nafasi zilizokosa wagombea wake ikiwemo hiyo ya Mwenyekiti.
Bulembo mwenyewe alipotafutwa na gazeti hili, alikiri ni kweli hana haja ya uongozi baada ya TFF kumwekea kauzibe, ingawa alisema anasikitika na hali inayoendelea na viongozi wa soka nchini kushindwa kuonyesha dhamira ya kweli ya kuinua mchezo huo kupitia klabu ndogo.
"Sitaki hata kusikia habari za kuongoza tena, maadam TFF iliamua kunikwamisha basi mie naendelea na shughuli zangu, ila sidhani kama viongozi wa soka nchini wanania ya kuinua mchezo huu," alisema Bulembo.
Villa ni miongoni mwa timu nne zilizopanda ligi kuu toka daraja la kwanza nyingine zikiwa ni JKT Oljoro Arusha, Coastal Union ya Tanga na Moro United ya Dar es Salaam na tayari TFF imeshatangaza ratiba ya kuanza kwa ligi hiyo Agosti 20 ikishirikisha jumla ya timu 14.
Mwisho
Ubalozi wa UAE wafuturisha waislam Dar
UBALOZI wa Nchi ya Falme za Kiarabu, UAE nchini kupitia taasisi ya kutoa huduma za kijamii ya Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan, umeamua kuwafuturisha waumini wa dini ya kiislam wa Msikiti wa Al Rahman wa Dar es Salaam kwa mwezi mzima wa mfungo wa Ramadhani.
Msaada huo wa futari unaoambatana na tende, ulianzwa kutolewa juzi jioni ambao mamia ya waumini wa msikiti huo walipata fursa ya kufuru chakula hicho kabla ya usiku kugawiwa tende zilizotolewa na ubalozi huo wa UAE.
Imamu wa Msikiti huo wa Al Rahman uliopo eneo la Kinondoni, Sheikh Abdullah Salim Bahssany, akiwahutubia waumini wake wakati wakigawiwa futari hiyo, alisema huo ni msaada toka ubalozi wa UAE na utakuwa ukitolewa hapo kila siku hadi mwezi mtukufu wa Ramadhani utakapomalizika mwishoni mwa mwezi huu.
Imamu huyo aliwaambia waumini hao kuwa wale waliokuwa na shaka na kupata futari katika funga zao, waondoe hofu kwani sasa watakuwa wakipata chakula hicho, huku akiushukuru ubalozi huo kwa ukarimu iliyouonyesha kwa waumini hao.
"Jamani futari mnayokula leo imetolewa na ubalozi wa nchi za Falme za Kiarabu na msaada huu utakuwa ukitolewa kwa mwezi mzima katika mfungo huu wa Ramadhani hivyo msiwe na hofu katika funga zenu,"alisema Sheikh Bahssany.
Baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam.
Mwisho
Msaada huo wa futari unaoambatana na tende, ulianzwa kutolewa juzi jioni ambao mamia ya waumini wa msikiti huo walipata fursa ya kufuru chakula hicho kabla ya usiku kugawiwa tende zilizotolewa na ubalozi huo wa UAE.
Imamu wa Msikiti huo wa Al Rahman uliopo eneo la Kinondoni, Sheikh Abdullah Salim Bahssany, akiwahutubia waumini wake wakati wakigawiwa futari hiyo, alisema huo ni msaada toka ubalozi wa UAE na utakuwa ukitolewa hapo kila siku hadi mwezi mtukufu wa Ramadhani utakapomalizika mwishoni mwa mwezi huu.
Imamu huyo aliwaambia waumini hao kuwa wale waliokuwa na shaka na kupata futari katika funga zao, waondoe hofu kwani sasa watakuwa wakipata chakula hicho, huku akiushukuru ubalozi huo kwa ukarimu iliyouonyesha kwa waumini hao.
"Jamani futari mnayokula leo imetolewa na ubalozi wa nchi za Falme za Kiarabu na msaada huu utakuwa ukitolewa kwa mwezi mzima katika mfungo huu wa Ramadhani hivyo msiwe na hofu katika funga zenu,"alisema Sheikh Bahssany.
Baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam.
Mwisho
Kondoo mwenye maandishi ya kiarabu azaliwa Kilimanjaro
Sunday, July 31, 2011
Uongozi wakana kumpa Nyagawa umeneja Simba

UONGOZI wa klabu ya soka ya Simba umekanusha taarifa kwamba umempa cheo cha umeneja kiungo wake iliyomtema kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania, Nico Nyagawa.
Nyagawa, aliyekuwa nahodha wa klabu hiyo ametemwa kwenye usajili wa kikosi kipya kitakachoitumikia timu hiyo msimu ujao, huku kukiwepo na taarifa kwamba kiungo huyo amekula shavu la kuteuliwa kuwa meneja wa timu hiyo.
Klabu ya Simba kupitria Afisa Habari wake, Ezekiel Kamwaga, alikanusha madai hayo ya kumpa Nyagawa umeneja, akisema cheo hicho bado kipo kwa King Abdallah Kibadeni, licha ya kukiri ni kweli wamemuacha mchezaji huyo kwa msimu ujao.
"Nyagawa hajapewa umeneja, ingawa ni kweli ametemwa kwenye orodha mpya ya kikosi cha Simba kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara," alisema Kamwaga.
Alisema kwa sasa uongozi wao unaangalia namna ya kumpa kazi nahodha wao huyo, kwa vile bado anaye mkataba na klabu hiyo hadi mwakani.
Alipoulizwa madai kwamba mchezaji huyo amekuwa akitaka kulipwa haki zake ili atimke zake kimoja Msimbazi, Kamwaga alisema hizo ni taarifa za uzushi kwa vile Nyagawa mwenyewe hajawahi kuueleza chochote uongozi juu ya jambo hilo hadi alipoongea na Sema Usikike.
"Hizo ni taarifa za uzushi tu, tulishazungumza na Nyagawa na ndio maana tunasema tupo katika mipango ya kumpa majukumu ndani ya Simba, " alisema.
Nyagawa aliyesajiliwa na Simba msimu wa 2005-2006 akitokea Mtibwa Sugar anatajwa kama mmoja wa wachezaji wenye nidhamu ya hali ya juu wa soka nchini, ingawa amekuwa na bahati mbaya ya kutoitwa mara kwa mara katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars.
Mwisho
Yanga yawatoa hofu mashabiki *Ni juu ya kutoweka kwa 'Diego'

UONGOZI wa klabu ya soka ya Yanga umewatoa hofu wanachama na mashabiki wake juu ya taarifa kwamba mshambuliaji wao nyota kutoka Uganda, Hamis Kizza 'Diego' ametoweka.
Kiza aliyeng'ara kwenye michuano ya Kombe la Kagame na kuibebesha taji mabingwa hao wa Tanzania Bara, ndiye aliyekuwa hajaripoti katika kambi ya timu hiyo inayojiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na mechi ya Ngao ya Hisani dhidi ya Simba.
Afisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu, alisema hakuna ukweli kuwa Kizza 'amepeperuka' Jangwani kama inavyovumishwa, ila nyota huyo alikuwa na matatizo ya kifamilia na kwamba angewasili mwishoni mwa wiki.
Sendeu, alisema kama mshambuliaji huyo asingekuwa mali yao jina lake lisingekuwa kwenyue orodha ya wachezaji wapya wa kikosi chao, pamoja na kuitumikia Yanga kwenye michuano ya Kombe la Kagame ambapo walifanikiwa kutwaa taji ikiwa ni mara yao ya nne tangu 1974.
"Ni kweli Kizza amechelewa kuja, lakini haina maana ndio kaingia mitini kama baadhi ya vyombo vya habari vinavyotaka kupotosha, tunadhani atawasili kabla ya Jumapili," alisema.
Aidha, Sendeu, alisema wameamua kukacha kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya timu za Coastal Union na Azam kutokana na walioziratibu kushindwa kufanya mawasiliano na uongozi wao kulingana na programu za benchi lao la ufundi.
"Hizo mechi tulikuwa tukizisikia tu redio na kwenye vyombo vingine vya habari, lakini uongozi haukuwa na taarifa nazo na ndio maana tumeamua kuachana nazo, kwani tunahisi kuna ujanja ujanja uliokuwa ukifanyika hasa mechi ya Coastal," alisema Sendeu.
Yanga wanaoendelea kujinoa jijini Dar chini ya makocha wake, Sam Timbe na Fred Felix 'Minziro' walitangaza kufuta mechi hizo zilizokuwa zichezwe mwishoni mwa wiki katika miji ya Tanga na Dar es Salaam.
Tamasha la Simba Day usipime!
BURUDANI mbalimbali za muziki na pambano la kirafiki la kimataifa litakaloihusisha wawakilishi wa Uganda kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika zinatarajiwa kupamba tamasha la soka la klabu ya Simba, 'Simba Day' litakalofanyika Agosti 8 jijini Dar es Salaam.
Wawakilishi hao wa Uganda, Simba Fc inayomilikiwa na Jeshi la nchi hiyo ndiyo watakaokuja kupamba tamasha hilo, ambalo pia litashuhudia timu ya Simba U23, ikikwaruzana na Azam katika kunogesha shamrashamra hizo.
Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, aliiambia MICHARAZO kuwa, tamasha lao litapambwa na burudani za muziki toka kwa bendi mbalimbali za muziki wa dansi na wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao hata hivyo hakuwataja.
Kamwaga alisema shamrashamra hizo za burudani ya muziki zitafuatiwa siku hiyo na utoaji wa tuzo za heshima kwa wadau wa Simba wakiwemo wachezaji, makocha na viongozi wa zamani walioisaidia klabu yao tangu ilipoanzishwa pamoja na wale wanaoisaidia sasa klabu hiyo.
"Karibu kila kitu kimekaa vema kwa sasa ikiwemo kuthibitishwa kwa Simba ya Uganda kuja nchini kucheza nasi katika tamasha hilo, ambalo kabla ya pambano hilo kutakuwa na burudani za muziki na pambano la timu za vijana za Simba na Azam," alisema Kamwaga.
"Mbali na burudani hizo pia tutatoa tuzo za heshima kwa wadau wetu katika namna ya kukumbuka na kushukuru mchango wao," alisema Kamwaga.
Kuhusu maandalizi yao ya mechi yao ya Ngao ya Hisani iliyoapngwa kucheza Agosti 17, Kamwaga alisema yanaendelea vema ikiwemo kikosi chao kuendelea kujifua kwa mazoezi pamoja na kucheza kadhaa za kirafiki visiwani Zanzibar.
Alisema wana imani kubwa ya kufanya vema kwenye pambano hilo dhidi ya Yanga pamoja na kwenye msimu mpya wa ligi kuu utakaoanza wiki moja baada ya pambano hilo la Ngao ya Hisani.
Simba ina deni la kulipa kisasi kwa Yanga iliyowafunga kwenye mechi kama hiyo msimu uliopita kwa mikwaju ya penati na kipigo ilichopata kwenye fainali za Kombe la Kagame lililochezwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam ambapo Mghana Kenneth Asamoah waliwaliza.
"Hatuna shaka na mechi zetu zijazo kutokana na maandalizi tuliyofanya huko Zanzibar," alisema Kamwaga aliyechukua nafasi hiyo hivi karibuni akimrithi, Clifford Ndimbo.
Mwisho
Kalapina ahubiri Uzalendo nchini
MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, Karama Masoud 'Kalapina' ametaka somo la uzalendo lifunzwe rasmi shuleni kwa nia ya kuwapika viongozi na wananchi watakaokuwa na uchungu wa kweli dhidi ya nchi yao kitu kinachoweza kupunguza ufisadi.
Kalapina, alisema somo hilo la uzalendo mbali na kusaidia kuondoa ufisadi, pia itawafanya hata wasanii kujipenda na kujithamini kwa kutanguliza utanzania kwanza tofauti na sasa kukosa kujiamini na kuendelea kuwatukuza wasanii wa kigeni na kushindwa kuwika kimataifa.
Akizungumza na blog hii mwishoni mwa wiki, Kalapina alisema mambo yanayoendelea nchini kuanzia kwa wananchi wa kawaida hadi viongozi na wanasiasa kuwa wabinafsi, wenye uchu na kutokuwa na uchungu wa nchi yao imetokana na kukosekana kwa somo la uzalendo.
"Nadhani watanzania tangu utotoni wakianza kufunzwa uzalendo na kujithamini wenyewe, vitendo vya ufisadi, uharamia na wasanii kupenda kuwaiga wasanii wa kimataifa badala ya kubuni kazi zao litaondoka na nchi itaenda vema," alisema.
Kalapina, alisema hata vitendo vya wanajamii kuwaibia kazi wasanii unatokana na ukosefu wa uzalendo na kuzidi kuwafanya wasanii kuendelea kuishi maisha ya dhiki kinyume na wenzao wa kimataifa wanaoongoza kwa utajiri kuliko hata viongozi wao wa serikali.
Kiongozi huyo wa kundi la muziki wa hip hop la Kikosi cha Mizinga, alisema hapendi hali ya mambo inayoendelea nchini kwa watanzania kuwa maskini wakati inafahamika nchi ina rasilimali zinazoweza kuwafanya waishi maisha ya kitajiri kuliko taifa lolote barani Afrika
Kalapina, alisema somo hilo la uzalendo mbali na kusaidia kuondoa ufisadi, pia itawafanya hata wasanii kujipenda na kujithamini kwa kutanguliza utanzania kwanza tofauti na sasa kukosa kujiamini na kuendelea kuwatukuza wasanii wa kigeni na kushindwa kuwika kimataifa.
Akizungumza na blog hii mwishoni mwa wiki, Kalapina alisema mambo yanayoendelea nchini kuanzia kwa wananchi wa kawaida hadi viongozi na wanasiasa kuwa wabinafsi, wenye uchu na kutokuwa na uchungu wa nchi yao imetokana na kukosekana kwa somo la uzalendo.
"Nadhani watanzania tangu utotoni wakianza kufunzwa uzalendo na kujithamini wenyewe, vitendo vya ufisadi, uharamia na wasanii kupenda kuwaiga wasanii wa kimataifa badala ya kubuni kazi zao litaondoka na nchi itaenda vema," alisema.
Kalapina, alisema hata vitendo vya wanajamii kuwaibia kazi wasanii unatokana na ukosefu wa uzalendo na kuzidi kuwafanya wasanii kuendelea kuishi maisha ya dhiki kinyume na wenzao wa kimataifa wanaoongoza kwa utajiri kuliko hata viongozi wao wa serikali.
Kiongozi huyo wa kundi la muziki wa hip hop la Kikosi cha Mizinga, alisema hapendi hali ya mambo inayoendelea nchini kwa watanzania kuwa maskini wakati inafahamika nchi ina rasilimali zinazoweza kuwafanya waishi maisha ya kitajiri kuliko taifa lolote barani Afrika
Coastal 'yamrudisha' Mwalala kwao
MSHAMBULIAJI mpya wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Ben Mwalala 'amerejeshwa' kwa nchini Kenya, baada ya timu yake iliyorejea Ligi Kuu Tanzania Bara, kuamua kupiga kambi ya kudumu nchini humo.
Coastal iliyowahi kuwa mabingwa wa soka nchini mwaka 1988, imeamua kuweka kambi ya kudumu mjini Mombasa, kujiandaa na msimu mpya wa ligi utakaoanza mwezi ujao hali inayowafanya nyota wao wapya Mwalala na mkenya mwenzie Abubakar Husseni kurejea kwao.
Afisa Habari wa timu hiyo, Eddo Kumwembe, alisema uongozi wao umeamua kuweka kambi ya kudumu Kenya, ikicheza mechi kadhaa za kirafiki za kujipima nguvu kujiweka fiti kabla ya kuanza kwa mikikimikiki ya ligi iliyokuwa ianze rasmi Agosti 20.
Kumwembe, alisema awali walikuwa wamepanga kurejea kwa muda Tanzania kwa ajili ya kuja kucheza pambano la kirafiki na Yanga lililokuwa lichezwe jana, lakini kutokana na uongozi wa Jangwani 'kuchomoa' kucheza nao wameamua kusalia Kenya hadi msimu utakapoanza.
"Kutokana na Yanga kuchomoa kucheza na sisi, tumeamua kubaki Kenya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kwa kujipima nguvu na timu za huko," alisema.
Coastal inayonolewa na kocha Hafidh Badru, imefanya usajili unaoonekena wa kutisha kwa kuwajaza nyota wa kigeni kama Mwalala, Husseni na wanigeria wawili, Felix Amechi na Samuel Temi huku ikiwa na nyota wengine wa Tanzania akiwemo Aziz Salum Gilla aliyetoka Simba.
Mwisho
Coastal iliyowahi kuwa mabingwa wa soka nchini mwaka 1988, imeamua kuweka kambi ya kudumu mjini Mombasa, kujiandaa na msimu mpya wa ligi utakaoanza mwezi ujao hali inayowafanya nyota wao wapya Mwalala na mkenya mwenzie Abubakar Husseni kurejea kwao.
Afisa Habari wa timu hiyo, Eddo Kumwembe, alisema uongozi wao umeamua kuweka kambi ya kudumu Kenya, ikicheza mechi kadhaa za kirafiki za kujipima nguvu kujiweka fiti kabla ya kuanza kwa mikikimikiki ya ligi iliyokuwa ianze rasmi Agosti 20.
Kumwembe, alisema awali walikuwa wamepanga kurejea kwa muda Tanzania kwa ajili ya kuja kucheza pambano la kirafiki na Yanga lililokuwa lichezwe jana, lakini kutokana na uongozi wa Jangwani 'kuchomoa' kucheza nao wameamua kusalia Kenya hadi msimu utakapoanza.
"Kutokana na Yanga kuchomoa kucheza na sisi, tumeamua kubaki Kenya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kwa kujipima nguvu na timu za huko," alisema.
Coastal inayonolewa na kocha Hafidh Badru, imefanya usajili unaoonekena wa kutisha kwa kuwajaza nyota wa kigeni kama Mwalala, Husseni na wanigeria wawili, Felix Amechi na Samuel Temi huku ikiwa na nyota wengine wa Tanzania akiwemo Aziz Salum Gilla aliyetoka Simba.
Mwisho
Super D aachia DVD nyingine za kufunzia ngumi

KOCHA maarufu wa mchezo wa ngumi nchini, Rajab Mhamila 'Super D' aliyeamua kutumia njia ya DVD kuwafunza watu ngumi, ameachia kazi nyingne tatu mpya.
Kazi hizo tatu zinahusisha mapambano kadhaa ya nyota na mabingwa wa ngumi za kulipwa duniani, ziachiwa sokoni zaidi ya wiki moja sasa.
Akizungumza na MICHARAZO, Super D, alisema tofauti na kanda yake ya awali, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa 'clips' za michezo ya nyota wa dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.
Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa dunia akiwemo Manny Pacquiao, Floyd Maywather, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo pia zina michezo ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha Habib Kinyogoli.
"Katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na cd nyingine tatu tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundation," alisema.
Super D, ambaye ni kocha wa klabu ya ngumi ya Ashanti, alisema anaamini kupitia njia hiyo watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo.
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado vijana wenye vipaji vya ngumi wanaweza kujiunga na klabu zao za Ashanti na Amana kujifunza 'live' chini ya makocha Habib Kinyogoli, Kondo Nassor, yeye Super D na wengine wanaowanoa vijana mbalimbali.
Mwisho
Siujasaini kokote-Nsa Job
MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Yanga, Nsa Job, amedai hajasaini kokote hadi sasa licha ya jina lake kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa klabu ya Villa Squad.
Hata hivyo mchezaji huyo, alisema kama uongozi wa Villa utakaa nae mezani na kukubaliana juu ya masilahi atakubali kuichezea kwa vile imeonyesha nia ya kumhitaji.
Akizungumza na MICHARAZO, Job, aliyeachwa na Yanga msimu huu baada ya kuitumikia msimu uliopita akitokea Azam, alisema hakuna mazungumzo yoyote aliyofanya na Villa waka kusaini kuichezea klabu hiyo.
Alisema, mara alipoachwa na Yanga alikuwa kwenye mipango ya kwenda Sweden kucheza soka la kulipwa, hivyo hakuwahi kufanya mazungumzo na klabu yoyote, ila kama ni kweli Villa inamhitaji ataweza kuwasaidia wakielewana juu ya suala la masilahi.
"Sijasaini kokote ndugu yangu, sio Villa wala klabu nyingine niliyofanya nao mazungumzo, ila kama klabu hiyo inanitaka sioni tatizo kuichezea kama tutaelewana juu ya masilahi, si unajua soka ni ajira bwana," alisema Job.
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuzichezea Moro United na Simba, alisema hata kama atakubaliana na Villa kuichezea, bado mipango yake ya kwenda kucheza soka la kulipwa ipo pale pale kwani anaendelea kuwasiliana na wakala wake Nyupi Mwakitosa.
Job, alisema wakala huyo ambaye ni mchezaji wa zamani wa soka Tanzania mwenye uraia wa Sweden kwa sasa, amemhakikishia kumhangaikia kupata timu ya kwenda kufanya nanyo majaribio baada ya ile ya awali kushindwa kukubaliana nao baadhi ya mambo.
Mwisho
Pondamali awachanganya Villa Squad
UONGOZI wa klabu ya soka ya Villa Squad, umedai kuchanganywa na kitendo cha aliyekuwa kocha wao, Juma Pondamali kujiondoa kikosi, huku wakikanusha kumteua Rachel Mwiligwa kuwa msemaji mpya wa klabu yao.
Makamu Mwenyekiti wa Villa, Ramadhani Uledi, aliambia MICHARAZO juzi kuwa, kujiondoa kwa Pondamali kumewapa wakati mgumu kutokana na ukweli alikuwa sehemu ya mipango yao ya kuisaidia timu hiyo kwenye msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Uledi alisema kinachowachanganya zaidi ni hatua ya kocha huyo aliyekuwa pia Mkurugenzi wa Ufundi, kuondoka kimyakimya bila kuwaambia zaidi ya kusoma taarifa zake kwenye vyombo vya habari.
"Tumeshtushwa na kuchanganywa na Pondamali kujiondoa tukielekea kwenye mikikimikiki ya Ligi Kuu Tanzania Bara tuliyoirejea msimu huu, hatujui kitu gani kilichomkimbiza, ila kutakutana kujadili tuone tunafanyaje," alisema.
Uledi anayekaimu pia nafasi ya Mwenyekiti, ambayo ipo wazi baada ya TFF kusitisha kuwaniwa kwenye uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika Juni, mwaka huu, alisema pia sio kweli kama klabu yao imemteua Mwandishi Rachel Mwiligwa kuwa Msemaji wao, akisisitiza nafasi hiyo bado inashikiliwa na Idd Godigodi aliyetangaza kujiuzulu.
"Hatutateua msemaji mpya kwa kuwa nafasi hiyo na zile zinazotakiwa zitolewe kwa ajira rasmi, zitatangazwa baada ya kikao chetu, kwa maana hiyo Godigodi aliyetangaza kujiondoa baada ya kusoma taarifa za uteuzi wa Mwiligwa ataendelea na nafasi yake," alisema Uledi.
Mwenyekiti huyo aliongeza katika kikao chao watajadili suala la ushiriki wa timu yao katika msimu mpya wa ligi waliorejea baada ya kushuka msimu wa 2008-2009.
Villa Squad ni miongoni mwa timu nne 'mpya' zitakazocheza ligi ya msimu ujao iliyopangwa kuanza Agosti 20, zingine zikiwa ni JKT Oljoro, Coastal Union na Moro United.
Mwisho
Makamu Mwenyekiti wa Villa, Ramadhani Uledi, aliambia MICHARAZO juzi kuwa, kujiondoa kwa Pondamali kumewapa wakati mgumu kutokana na ukweli alikuwa sehemu ya mipango yao ya kuisaidia timu hiyo kwenye msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Uledi alisema kinachowachanganya zaidi ni hatua ya kocha huyo aliyekuwa pia Mkurugenzi wa Ufundi, kuondoka kimyakimya bila kuwaambia zaidi ya kusoma taarifa zake kwenye vyombo vya habari.
"Tumeshtushwa na kuchanganywa na Pondamali kujiondoa tukielekea kwenye mikikimikiki ya Ligi Kuu Tanzania Bara tuliyoirejea msimu huu, hatujui kitu gani kilichomkimbiza, ila kutakutana kujadili tuone tunafanyaje," alisema.
Uledi anayekaimu pia nafasi ya Mwenyekiti, ambayo ipo wazi baada ya TFF kusitisha kuwaniwa kwenye uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika Juni, mwaka huu, alisema pia sio kweli kama klabu yao imemteua Mwandishi Rachel Mwiligwa kuwa Msemaji wao, akisisitiza nafasi hiyo bado inashikiliwa na Idd Godigodi aliyetangaza kujiuzulu.
"Hatutateua msemaji mpya kwa kuwa nafasi hiyo na zile zinazotakiwa zitolewe kwa ajira rasmi, zitatangazwa baada ya kikao chetu, kwa maana hiyo Godigodi aliyetangaza kujiondoa baada ya kusoma taarifa za uteuzi wa Mwiligwa ataendelea na nafasi yake," alisema Uledi.
Mwenyekiti huyo aliongeza katika kikao chao watajadili suala la ushiriki wa timu yao katika msimu mpya wa ligi waliorejea baada ya kushuka msimu wa 2008-2009.
Villa Squad ni miongoni mwa timu nne 'mpya' zitakazocheza ligi ya msimu ujao iliyopangwa kuanza Agosti 20, zingine zikiwa ni JKT Oljoro, Coastal Union na Moro United.
Mwisho
Waumini Answar Sunna wacharuka, watulizwa na RITA
WAUMINI wa Jumuiya ya Answar Sunna Tanzania wanaoshinikiza uongozi wa juu ya jumuiya hiyo hung'oke madarakani kwa kukiuka katiba, wametulizwa wakitakiwa kuwa na subira wakati ofisi wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini, RITA ukisubiri kutoa maamuzi juu ya mgogoro huo.
Wito huo umetolewa jana kwenye maazimio ya mkutano wa pamoja kati ya waumini hao na kamati yao maalum inayofuatilia mgogoro huo, uliofanyika kwenye msikiti uliopo makao makuu ya Answar Sunna, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kadhalika wito kama huo umetolewa na Meneja wa Ufilisi na Udhamini wa Rita, Linna Msanga Katema, alipozungumza na MICHARAZO akithibitisha ofisi yao imeomba ipewe muda wa mwezi mmoja kutoa majibu juu ya sakata linaloendelea kwenye jumuiya hiyo.
Meneja huyo alikiri kuwepo kwa mgogoro huo na kueleza tofauti na awali walipokuwa wakikosa ushirikiano toka kwa viongozi wanaolalamikiwa wakiwemo Baraza la Wadhamini na Amiri wa Jumuiya hiyo, Sheikh Juma Poli, sasa mambo ni shwari.
"Tumeshawaandikia barua kuomba watupe muda wa mwezi mmoja toka Julai 26 tuliowaandikia barua ili RITA tutoe maamuzi juu ya kinachoendelea baina ya pande hizo mbili, hivyo tunaomba waumini watulie haki itatendeka," alisema Katema.
Katika mkutano wao wa jana, waumini hao walionyesha kuwa na hasira ya kutaka viongozi wang'oke kwa kukiuka katika na kushindwa kuipeleka mbele jumuiya yao, kabla ya Mwenyekiti wa Kamati yao, Hamis Buguza kuwasihi wavute subira.
"Vuteni subira tusubiri maamuzi ya RITA ili kuona nini kitaamuliwa, ila lolote litakalotolewa tunawaahidi kuyaleta kwenu mjue kitu cha kufanya, ila kwa sasa ni mapema mno na Uislam unatufundisha kuwa na subira," alisema mwenyekiti huyo.
Kutokana na kauli ya Mwenyekiti pamoja na Katibu wao, Abdulhafidh Nahoda, waumini hao katika kutoa maazimio waliafiki kuvuta subira hadi maamuzi ya RITA yanayotarajiwa kutolewa Agosti 26, ili wajue la kufanya.
Hata hivyo walitoa angalizo kwa kudai kama kutakuwa na aina fulani ya upendeleo basi, watakachoamua wasije wakaamuliwa kwa madai wamechoka kuvumilia.
Mzozo wa waumini wa jumuiya hiyo na uongozi wao umeanza tangu mwaka juzi kutokana na madai viongozi wamekiuka katiba kwa kutoitisha mikutano kwa muda wa miaka 10, huku wakifanya maamuzi bila kuwashirikisha kama wanavyoelekezwa kwenye katika mama ya mwaka 1992.
Mwisho
Wito huo umetolewa jana kwenye maazimio ya mkutano wa pamoja kati ya waumini hao na kamati yao maalum inayofuatilia mgogoro huo, uliofanyika kwenye msikiti uliopo makao makuu ya Answar Sunna, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kadhalika wito kama huo umetolewa na Meneja wa Ufilisi na Udhamini wa Rita, Linna Msanga Katema, alipozungumza na MICHARAZO akithibitisha ofisi yao imeomba ipewe muda wa mwezi mmoja kutoa majibu juu ya sakata linaloendelea kwenye jumuiya hiyo.
Meneja huyo alikiri kuwepo kwa mgogoro huo na kueleza tofauti na awali walipokuwa wakikosa ushirikiano toka kwa viongozi wanaolalamikiwa wakiwemo Baraza la Wadhamini na Amiri wa Jumuiya hiyo, Sheikh Juma Poli, sasa mambo ni shwari.
"Tumeshawaandikia barua kuomba watupe muda wa mwezi mmoja toka Julai 26 tuliowaandikia barua ili RITA tutoe maamuzi juu ya kinachoendelea baina ya pande hizo mbili, hivyo tunaomba waumini watulie haki itatendeka," alisema Katema.
Katika mkutano wao wa jana, waumini hao walionyesha kuwa na hasira ya kutaka viongozi wang'oke kwa kukiuka katika na kushindwa kuipeleka mbele jumuiya yao, kabla ya Mwenyekiti wa Kamati yao, Hamis Buguza kuwasihi wavute subira.
"Vuteni subira tusubiri maamuzi ya RITA ili kuona nini kitaamuliwa, ila lolote litakalotolewa tunawaahidi kuyaleta kwenu mjue kitu cha kufanya, ila kwa sasa ni mapema mno na Uislam unatufundisha kuwa na subira," alisema mwenyekiti huyo.
Kutokana na kauli ya Mwenyekiti pamoja na Katibu wao, Abdulhafidh Nahoda, waumini hao katika kutoa maazimio waliafiki kuvuta subira hadi maamuzi ya RITA yanayotarajiwa kutolewa Agosti 26, ili wajue la kufanya.
Hata hivyo walitoa angalizo kwa kudai kama kutakuwa na aina fulani ya upendeleo basi, watakachoamua wasije wakaamuliwa kwa madai wamechoka kuvumilia.
Mzozo wa waumini wa jumuiya hiyo na uongozi wao umeanza tangu mwaka juzi kutokana na madai viongozi wamekiuka katiba kwa kutoitisha mikutano kwa muda wa miaka 10, huku wakifanya maamuzi bila kuwashirikisha kama wanavyoelekezwa kwenye katika mama ya mwaka 1992.
Mwisho
Saturday, July 30, 2011
Wednesday, July 27, 2011
Banka aishtaki Simba kwa TFF

KIUNGO Mohammed Banka ameishtaki klabu yake ya Simba kwa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, juu ya sakata lake la kutaka kupelekwa kucheza kwa mkopo katika timu ya Villa Squad bila ridhaa yake.
Banka, aliyeichezea Simba kwa mafanikio tangu ilipomsajili baada ya kutemwa na Yanga, msimu wa 2008-2009, alisema ameamua kuchukua maamuzi huo kutokana na kuona viongozi wa Simba wanamzungusha kuhusu suala la uhamisho wake.
Mwanasheria aliyepewa kazi ya kumpigania Banka, John Mallya, aliiambia MICHARAZO jana kuwa, wameandika barua Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, ili kuingilia kazi suala la mteja wao kabla ya hatua zingine za kisheria kufuata.
Mallya, alisema wameamua kuandika barua hiyo, TFF kutokana na kuona viongozi wa Simba wanakwepa kukutana kulimaliza suala la Banka, kutokana na wenyewe kukiuka mkabata baina yao na mchezaji huyo kama sheria zinavyoelekeza.
Alisema walikuwa katika mazungumzo mazuri na viongozi wa klabu hiyo, lakini juzi walipopanga kukutana ili kulimaliza suala hilo, wenzao walishindwa kutokea na kuona ni vema waombe msaada TFF, kabla ya kuangalia cha kufanya kumsaidia mteja wao.
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alikiri kupokewa kwa barua hiyo ya ombi la Banka kutaka shirikisho lao kuingilia kati na kudai itapelekwa kunakohusika kufanyiwa kazi.
"Ni kweli barua hiyo imefika kwetu, Banka akiomba TFF iingilie kati sakata lake la Simba," alisema Wambura.
Naye Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alikiri kuwepo kwa mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea baina ya pande hizo mbili, ingawa alisema alikuwa hajaipata nakala ya barua hiyo ya malalamiko ya Banka iliyopelekwa TFF.
"Hilo la kushtakiwa TFF, silijui kwani sijapata barua, pia siwezi kuliongelea kwa undani kwa vile lilikuwa linashughulikiwa na viongozi wa juu, ambao kwa bahati karibu wote wameenda Uturuki kushughulikia suala la ujenzi wa uwanja," alisema.
Banka, amekuwa akisisitiza kuwa kama Simba haimhitaji ni bora mlipe chake aangalie ustaarabu wake kuliko kumlazimisha kwenda Villa Sqaud iliyorejea ligi kuu msimu huu.
Mwisho
Bingwa wa Kick Boxing Kenya atua Bongo kuzipiga

BINGWA wa Kick Boxing kutoka Kenya, Rukia Kaselete ametua nchini tayari kwa ajili ya pambano lake dhidi ya Mtanzania Jamhuri Said, watakaosindikiza pambano la nani mkali kati ya Amour Zungu wa Zanzibar na Mchumia Tumbo wa Tanzania Bara.
Michezo hiyo iliyoandaliwa na Bingwa wa Dunia wa Kick Boxing anayeshikilia mikanda ya WKL na WKC, Japhet Kaseba inatarajiwa kucheza siku ya Jumamosi kwenye ukumbi wa DDC Keko, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Kaseba, alisema maandalizi ya michezo hiyo kwa wastani inaendelea vema ikiwemo mabondia wote kuwasili jijini akiwemo mkenya huyo atakayepigana na Jamhuri kusindikiza pambano la Zungu na mwenzake.
Kaseba alisema mabondia wote watakaoshiriki michezo hiyo ya Kick Boxing na Ngumi za Kulipwa wanatarajiwa kupimwa afya zao siku ya Ijumaa kwenye gym yake, iliyopo eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
"Kwa kweli kila kitu kinaenda vema ikiwemo mabondia wote kuwasili Dar tayari kwa ajili ya michezo hiyo ya Jumamosi, ambapo Amour Zungu atazipiga na Mchumia Tumbo katika pambano la kusaka mkali kati yao," alisema Kaseba.
Kaseba alisema mbali na pamoja ya pambano la Kaseleta na Jamhuri, siku hiyo pia kutakuwa na michezo mingine ya utangulizi ambapo wanadada Asha Abubakar wa Kisarawe na Fadhila Adam wa Dar wataonyeshana kazi kwenye kick boxing.
"Wengine watakaopigana siku hiyo ni kati ya Dragon Kaizum dhisi ya Faza Boy, Idd na Dragon Boy na Lion Heart ataonyeshana kazi na Begeje," alisema.
Aliongeza pambano la ngumi za kulipwa zitawakutanisha wakongwe wa mchezo huo, Ernest Bujiku dhidi ya Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo'.
Mwisho
Viongozi Simba waenda kumalizana na Waturuki
VIONGOZI wa klabu ya soka ya Simba wameondoka nchini juzi kuelekea Uturuki kwa ajili ya kwenda kumalizia taratibu za ujenzi wa uwanja wao mpya wa kisasa utakaojengwa eneo la Bunju, nje kidogo ya jijini la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa klabu hiyo, Ezekiel Kamwaga, viongozi walioondoka ni Mwenyekiti Ismail Aden Rage na Katibu wake, Evodius Mtawala.
Kamwaga alisema Rage na Mtawala waliondoka juzi kuelekea nchini humo kufanya mazungumzo ya mwisho na uongozi wa kampuni ya Petroland, ambayo ndiyo itakayoujenga uwanja huo utakaoingiza watazamaji wasiopungua 60,000.
"Viongozi wetu wawili wa juu wameondoka nchini jana, kwenda Uturuki kwa ajili ya kumalizana na watakaotujengea uwanja wetu wa kisasa utakaokuwa eneo la Bunju," alisema Kamwaga.
Afisa Habari huyo, alisema viongozi wao wameenda kuweka mambo sawa kabla ya wakandarasi hao kuja kuanza kazi yao na kuifanya Simba kufuata nyayo za klabu kubwa barani Afrika kama ASEC Memosa au Kaizer Chief zenye viwanja vikubwa vya kisasa.
Uwanja huo utakaokuwa wa kisasa na mkubwa kama ule wa Taifa, utaigharimu Simba kiasi cha Shilingi Bilioni 75 hadi utakapomalizika ukihusisha uwanja wa kuchezea, maduka, kumbi za mikutano na burudani, mbali na hoteli na kituo cha michezo.
Kwa hapa nchini ukiondoa Yanga yenye kuumiliki uwanja wa Kaunda, klabu nyingine yenye uwanja wake mwenyewe ni Azam iliyoujenga eneo la Chamanzi, Mbande nje kidogo ya jijini la Dar es Salaam ambao utaanza kutumika msimu mpya wa Ligi Kuu.
Mwisho
Simba yawaita DCMP Da kumjadili Mgosi
UONGOZI wa klabu ya soka ya Simba, umeutaka uongozi wa timu ya DC Motema Pembe ya DR Congo, kuja jijini Dar es Salaam kuzungumza nao ili waachiwe kiungo mshambuliaji, Mussa Hassani Mgosi vinginevyo imsahau kumpata.
Motema Pembe imeonyesha nia ya kumsajili Mgosi, isipokuwa inamtaka kama mchezaji huru, kitu kinachopingwa na uongozi wa Simba wenye mkataba bao ikidai kama ina ya dhati ya kumnasa mchezaji huyo wake wazungumze mezani waafikiane.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema klabu yao ipo tayari kumuacha Mgosi aende DCMP, ila kama uongozi wa klabu hiyo utakuja kuzungumza nao ili kumhamisha kwani ni mchezaji wao halali.
Kamwaga alisema Simba haina nia ya kumbania Mgosi, ila kwa hali ilivyo ni vigumu kwao kumtoa winga huyo bure wakati wana mkataba naye.
Kamwaga, alisema Simba itaona raha iwapo mchezaji huyo atajiunga na DCMP kama ilivyokuwa kwa akina Mbwana Samatta na Patrick Ochan walisajiliwa TP Mazembe, ila wenzake wanamtaka bure kitu kinachowafanya wamzuie hadi kieleweke.
"Kama kweli wana nia na Mgosi waje wazungumze nasi, Mgosi ana mkataba Simba na hivyo hatuwezi kumuachia bure," alisema.
Kamwaga, alisema tayari wameshaifahamisha TFF juu ya msimamo wao na wanasubiri kuona uongozi wa DCMP utafanya nini kuamua hatma ya Mgosi, ambaye jina lake lipo kwenye orodha ya usajili wa klabu ya Simba kwa msimu ujao wa ligi kuu Tanzania Bara.
Alisema kama mipango yake ya kwenda Congo itakwama, Mgosi ataendelea kuichezea timu yao kwa msimu ujao hadi atakapomaliza mkataba utakaoisha mwakani.
Katika hatua nyingine, Kamwaga alisema klabu yao inatarajiwa kuianika timu watakaocheza nao kwenye Tamasha la Siku ya Simba 'Simba Day' litakalofanyika Agosti 8 mwaka huu.
Kamwaga alisema klabu yao ilipeleka maombi kwa klabu tatu za nje ya nchi na leo wanatarajia kutangaza timu watakayocheza nao katika tamasha hilo
"Timu itakayotusindikiza kwenye Simba Day tutaitangaza kesho (leo) pia tutaanika kila kitu juu ya maandalizi ya tamasha hilo," alisema Kamwaga.
Mwisho
Talent Band kutambulisha mpya Sinza
BENDI ya muziki wa dansi ya Talent 'Wazee wa Kuchechemea' inatarajiwa kuvamia kitongoji cha Sinza ili kuitambulisha albamu yao mpya ya 'Shoka la Bucha'.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, aliambia MICHARAZO jana kuwa, onyesho hilo litafanyika kesho kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre (zamani Rufita) ambapo watatambulisha nyimbo zote zilizopo kwenye albamu hiyo mpya.
Jumbe, alisema onyesho hilo limeratibiwa na Mkurugenzi wa ukumbi huyo aliyemtaja kwa jina la Mamaa Joyce.
"Baada ya kuikamilisha albamu yetu mpya ya Shoka la Bucha, Talent Band, inatarajiwa kuitambulisha albamu hiyo katika onyesho maalum litakaloofanyika siku ya Alhamis kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre," alisema Jumbe.
Jumbe alizitaja nyimbo zitakazotambulishwa kwenye onyesho hilo kuwa ni Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu, Kilio cha Swahiba na zile za albamu yao ya kwanza ya Subiri Kidogo.
Naye mratibu wa onyesho hilo, Joyce alisema kila kitu kipo sawa na wanachosubiri ni kupata burudani toka kwa Talent.
Mwisho
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, aliambia MICHARAZO jana kuwa, onyesho hilo litafanyika kesho kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre (zamani Rufita) ambapo watatambulisha nyimbo zote zilizopo kwenye albamu hiyo mpya.
Jumbe, alisema onyesho hilo limeratibiwa na Mkurugenzi wa ukumbi huyo aliyemtaja kwa jina la Mamaa Joyce.
"Baada ya kuikamilisha albamu yetu mpya ya Shoka la Bucha, Talent Band, inatarajiwa kuitambulisha albamu hiyo katika onyesho maalum litakaloofanyika siku ya Alhamis kwenye ukumbi wa Nouvel Social Centre," alisema Jumbe.
Jumbe alizitaja nyimbo zitakazotambulishwa kwenye onyesho hilo kuwa ni Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu, Kilio cha Swahiba na zile za albamu yao ya kwanza ya Subiri Kidogo.
Naye mratibu wa onyesho hilo, Joyce alisema kila kitu kipo sawa na wanachosubiri ni kupata burudani toka kwa Talent.
Mwisho
Tamasha kubwa la sanaa kufanyika Moro
WASANII zaidi ya 100 wa mkoani Morogoro wanatarajia kufanya tamasha kubwa litakaloshirikisha sanaa za aina mbalimbali.
Mratibu wa tamasha hilo lililopewa jina la 'Wakali Concert', Athuman Mswagala 'Mahita' aliiambia Micharazokwa njia ya simu kutoka Morogoro kuwa tamasha hilo litafanyika Julai 30 katika ukumbi wa Vijana Social ulioko mjini hapa.
Mswagala, alisema lengo la tamasha hilo litakalowahusisha wasanii wa mkoa huo wa fani mbalimbali ni kufahamiana na kuibua vipaji vipya.
Alisema maandalizi kwa ajili ya tamasha hilo yanakwenda vizuri na kwamba kinachosubiriwa ni kufanyika kwa tamasha hilo.
Alisema katika tamasha hilo litakalokuwa likifanyika kila mwaka, wasanii watakaofanya vizuri watazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha taslimu.
"Kimsingi, maandaalizi yanakwenda vizuri na wasanii wengi wamethibitisha kushiriki hali ambayo naamini itakuwa burudani tosha kwa wakazi wa Morogoro" alisema.
Naye, mkurugenzi wa kampuni ya Katundu, wanaodhamini tamasha hilo, Mohamed Katundu, alisema kampuni yake imeamua kudhamini tamasha hilo kwa lengo la kusapoti wasanii wa Morogoro.
Katundu alisema hiyo ni moja ya mipango ya kampuni yake kuhakikisha wasanii mkoani hapa wanapata mafanikio makubwa kupitia sanaa mbalimbali.
Mratibu wa tamasha hilo lililopewa jina la 'Wakali Concert', Athuman Mswagala 'Mahita' aliiambia Micharazokwa njia ya simu kutoka Morogoro kuwa tamasha hilo litafanyika Julai 30 katika ukumbi wa Vijana Social ulioko mjini hapa.
Mswagala, alisema lengo la tamasha hilo litakalowahusisha wasanii wa mkoa huo wa fani mbalimbali ni kufahamiana na kuibua vipaji vipya.
Alisema maandalizi kwa ajili ya tamasha hilo yanakwenda vizuri na kwamba kinachosubiriwa ni kufanyika kwa tamasha hilo.
Alisema katika tamasha hilo litakalokuwa likifanyika kila mwaka, wasanii watakaofanya vizuri watazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha taslimu.
"Kimsingi, maandaalizi yanakwenda vizuri na wasanii wengi wamethibitisha kushiriki hali ambayo naamini itakuwa burudani tosha kwa wakazi wa Morogoro" alisema.
Naye, mkurugenzi wa kampuni ya Katundu, wanaodhamini tamasha hilo, Mohamed Katundu, alisema kampuni yake imeamua kudhamini tamasha hilo kwa lengo la kusapoti wasanii wa Morogoro.
Katundu alisema hiyo ni moja ya mipango ya kampuni yake kuhakikisha wasanii mkoani hapa wanapata mafanikio makubwa kupitia sanaa mbalimbali.
Saturday, July 16, 2011
Sunzu asaini mkataba wa miaka miwili
MSHAMBULIAJI wa Kimataifa kutoka Zambia, Felix Mumba Sunzu amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuichezea klabu ya soka ya Simba kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange Kaburu, aliuambia mtandao wa MICHARAZO jana usiku kwamba wameshamalizana na Sunzu na kwamba mchezaji huyo atarejea kwao wakati wakifanya taratibu za uhamisho wake wa kimataifa toka Al Hilal.
"Kila kitu kipo ok, baada ya mkutano mrefu baina yenu amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili kuwepo Simba," alisema Kaburu.
Kaburu hakupenda kueleza kwa undani mambo mengine waliyokubaliana na mchezaji huyo.
Kadhalika, Kaburu alikanusha taarifa kwamba wamemnyakua mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete akidai wanaheshimu mkataba uliopo baina ya Yanga na mchezaji huyo.
"Hizo ni taarifa za mtaani, ila si kweli, mtu ambaye tumemalizana nae ni Sunzu, huyo Tegete wala hatuna mpango nae," alisema.
Pia alisema sio kweli kama beki wao king'ang'anizi, Kelvin Yondan, amewakacha na kwenda Yanga kwa maelezo bado wana mkataba naye, pia kisheria Yanga wanapaswa waonane nao kama ni kweli walimtaka mchezaji huyo.
"taratibu zipo wazi, pia Yondan ana mkataba wa kuichezea Simba sasa ataendaje Yanga, hizi ni nyepesi nyepesi tu ila mchezaji huyo bado yupo Simba, alisema Kaburu.
Katiak hatua nyingine ni kwamba wachezaji wawili, Mohammed Banka na Athuman Idd 'Chuji' huenda wakaichezea Villa Squad kwa mkopo baada ya kuridhiana na Simba juu ya wachezaji hao wanaomudu nafasi ya kiungo.
Viongozi wa Villa waliuambia mtandao huu walikuwa wakimalizana na Simba, lakini hawakuweka kila kitu bayana wakidai watazungumza leo.
Friday, July 15, 2011
Twiga Stars kuanza na Ghana All African Games
SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF, imetangaza ratiba ya michuano ya soka kwa timu za wanawake zinazoshiriki michuano ya Afrika (All African Games) ambapo timu ya taifa ya Tanzania, Twiga Stars itaanza kibarua chake kwa kuumana na Ghana.
Michuano hiyo ya Afrika inatarajiwa kuanza kufanyika Septemba 3-18 kwenye mji wa Maputo, Msuimbiji, ambapo kwa mujibu wa ratiba hiyo ya CAF ni kwamba Twiga iliyopo kundi B itafungua dimba kwa kuumana na Ghana siku ya Septemba 5.
Timu zingine zilizopo katika kundi hilo ni Afrika Kusini na mabingwa wapya wa Kombe la COSAFA, Zimbabwe.
Ratiba hiyo ya CAF inaonyesha kuwa Twiga itashuka dimbani tena Septemba 8 kucheza na Afrika Kusini kabla ya kumaliza mechi zake, Septemba 11 kwa kucheza na Zimbabwe.
Twiga imejikuta kundi moja na timu hizo mbili ambazo ziliichachafya katika michuano ya Kombe la COSAFA, ambapo Afrika Kusini waliokuwa nao kundi moja waliwalaza bao 1-0 kabla ya Zimbabwe kuifunga kwenye mechi ya nusu fainali kwa mikwaju ya penati 4-2.
Timu zingine zitakazoshiriki michuano hiyo na zilizopangwa kundi A ni wenyeji Msumbiji, Cameroon, Algeria na Guinea, ambapo washindi wawili wa kwanza wa kila kundi ndizo zitakazosonga mbele kwa hatua ya nusu fainali.
Nigeria ndiyo waliokuwa mabingwa wa mwaka 2007, lakini hawakufanikiwa kufuzu
kwa michuano hiyo mwaka huu ambayo hufanyika kila baada ya miaka minne.
Wakati huo huo mikoa mitatu ya Dodoma, Mwanza na Ruvuma imeteuliwa kuwa vituo vya kuendeshea semina na mitihani ya utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wa daraja la pili na tatu inayotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kupitia Afisa Habari wake, Boniface Wambura, ni kwamba semina na mitihani hiyo itafanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia Agosti 2-5 katika vituo hivyo.
Taarifa hiyo inasema washiriki wa semina na mitihani hiyo watajitegemea kila kitu kuanzia gharama za usafiri, chakula na malazi, huku vyama vya soka vya mikoa ya Tanzania Bara vikihimizwa kuwakumbusha washiriki kuhudhuria semina na mafunzo hayo kwa faida yao.
Iliongeza kuwa semina na mitihani hiyo itatumika kuwapandisha daraja washiriki hao.
Hiyo ni semina ya pili kuandaliwa na TFF ndani ya kipindi kifupi ikiwa ni maandalizi na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwani karibu wiki moja sasa ilikuwa ikiendesha semina kama hiyo inayowahusisha waamuzi wa daraja la IA na IB iliyokuwa ikifanyika katika miji ya Mwanza na Dar es Salaam.
Semina na mitihani hiyo ilianza Julai 13 na inatarajiwa kufungwa leo Julai 16.
Michuano hiyo ya Afrika inatarajiwa kuanza kufanyika Septemba 3-18 kwenye mji wa Maputo, Msuimbiji, ambapo kwa mujibu wa ratiba hiyo ya CAF ni kwamba Twiga iliyopo kundi B itafungua dimba kwa kuumana na Ghana siku ya Septemba 5.
Timu zingine zilizopo katika kundi hilo ni Afrika Kusini na mabingwa wapya wa Kombe la COSAFA, Zimbabwe.
Ratiba hiyo ya CAF inaonyesha kuwa Twiga itashuka dimbani tena Septemba 8 kucheza na Afrika Kusini kabla ya kumaliza mechi zake, Septemba 11 kwa kucheza na Zimbabwe.
Twiga imejikuta kundi moja na timu hizo mbili ambazo ziliichachafya katika michuano ya Kombe la COSAFA, ambapo Afrika Kusini waliokuwa nao kundi moja waliwalaza bao 1-0 kabla ya Zimbabwe kuifunga kwenye mechi ya nusu fainali kwa mikwaju ya penati 4-2.
Timu zingine zitakazoshiriki michuano hiyo na zilizopangwa kundi A ni wenyeji Msumbiji, Cameroon, Algeria na Guinea, ambapo washindi wawili wa kwanza wa kila kundi ndizo zitakazosonga mbele kwa hatua ya nusu fainali.
Nigeria ndiyo waliokuwa mabingwa wa mwaka 2007, lakini hawakufanikiwa kufuzu
kwa michuano hiyo mwaka huu ambayo hufanyika kila baada ya miaka minne.
Wakati huo huo mikoa mitatu ya Dodoma, Mwanza na Ruvuma imeteuliwa kuwa vituo vya kuendeshea semina na mitihani ya utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wa daraja la pili na tatu inayotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kupitia Afisa Habari wake, Boniface Wambura, ni kwamba semina na mitihani hiyo itafanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia Agosti 2-5 katika vituo hivyo.
Taarifa hiyo inasema washiriki wa semina na mitihani hiyo watajitegemea kila kitu kuanzia gharama za usafiri, chakula na malazi, huku vyama vya soka vya mikoa ya Tanzania Bara vikihimizwa kuwakumbusha washiriki kuhudhuria semina na mafunzo hayo kwa faida yao.
Iliongeza kuwa semina na mitihani hiyo itatumika kuwapandisha daraja washiriki hao.
Hiyo ni semina ya pili kuandaliwa na TFF ndani ya kipindi kifupi ikiwa ni maandalizi na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwani karibu wiki moja sasa ilikuwa ikiendesha semina kama hiyo inayowahusisha waamuzi wa daraja la IA na IB iliyokuwa ikifanyika katika miji ya Mwanza na Dar es Salaam.
Semina na mitihani hiyo ilianza Julai 13 na inatarajiwa kufungwa leo Julai 16.
Stars kukipiga ughaibuni na Palestina, Jordan
KATIKA kujiweka fiti kabla ya kumaliza viporo vya michezo yake miwili iliyosalia ya kuwania kufuzu Fainali za Afrika za mwaka 2012, timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inatarajiwa kwenda Mashariki na Kati kucheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kuopitia Afisa Habari wake, Boniface Wambura inasema, Stars itaumana na timu za mataifa ya Palestina na Jordan mapema mwezi ujao.
Wambura alisema mechi ya kwanza ya timu hiyo inayoshikilia nafasi ya tatu katika kundi D lenye timu za Morocco, Afrika ya Kati na Algeria, itachezwa siku ya Agosti 10 katika mji wa Ramallah dhidi ya wenyeji wao Palestina.
Mechi ya Tanzania na Palestina itakuwa ni kama marudiano, kwani mapema mwaka huu timu hizo zilipepetana hapa nchini katika pambano jingine la kirafiki la kimataifa.
Katika mechi hiyo ilichezwa Februari 9 kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, Stars iliitambia Palestina kwa kuilaza bao 1-0, bado lililofungwa na winga mahiri, Mrisho Ngassa ambaye kwa sasa yupo Marekani kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Seattle Sounders inayoshiriki ligi ya Marekani, MLS.
Wambura aliongeza Stars itashuka tena dimbani Agosti 13 kupepetana na Jordan katika pambano litakalochezwa kwenye mji mkuu wa nchi hiyo ya Jordan, Amani.
Wambura alisema Stars itaondoka nchini Agosti 7 na kikosi cha timu hiyo kinatarajiwa kutajwa mara baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Jan Poulsen kurejea kutoka mapumziko nchini Denmark, mapema mwezi ujao.
Stars inahitaji ushindi katika mechi zake zilizosalia dhidi ya Algeria itakayochezwa nyumbani na ile ya mwisho dhidi ya Morocco, iwapo inataka kufuzu fainali hizo za Afrika zitakazofanyika mwakani katika nchi za Guinea ya Ikweta na Gabon.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kuopitia Afisa Habari wake, Boniface Wambura inasema, Stars itaumana na timu za mataifa ya Palestina na Jordan mapema mwezi ujao.
Wambura alisema mechi ya kwanza ya timu hiyo inayoshikilia nafasi ya tatu katika kundi D lenye timu za Morocco, Afrika ya Kati na Algeria, itachezwa siku ya Agosti 10 katika mji wa Ramallah dhidi ya wenyeji wao Palestina.
Mechi ya Tanzania na Palestina itakuwa ni kama marudiano, kwani mapema mwaka huu timu hizo zilipepetana hapa nchini katika pambano jingine la kirafiki la kimataifa.
Katika mechi hiyo ilichezwa Februari 9 kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, Stars iliitambia Palestina kwa kuilaza bao 1-0, bado lililofungwa na winga mahiri, Mrisho Ngassa ambaye kwa sasa yupo Marekani kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Seattle Sounders inayoshiriki ligi ya Marekani, MLS.
Wambura aliongeza Stars itashuka tena dimbani Agosti 13 kupepetana na Jordan katika pambano litakalochezwa kwenye mji mkuu wa nchi hiyo ya Jordan, Amani.
Wambura alisema Stars itaondoka nchini Agosti 7 na kikosi cha timu hiyo kinatarajiwa kutajwa mara baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Jan Poulsen kurejea kutoka mapumziko nchini Denmark, mapema mwezi ujao.
Stars inahitaji ushindi katika mechi zake zilizosalia dhidi ya Algeria itakayochezwa nyumbani na ile ya mwisho dhidi ya Morocco, iwapo inataka kufuzu fainali hizo za Afrika zitakazofanyika mwakani katika nchi za Guinea ya Ikweta na Gabon.
Hatimaye Sunzu atua Bongo
MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa timu ya Al Hilal ya Sudan, Felex Sunzu ametua nchini mapema leo tayari kufanya mazungumzo na klabu ya Simba ili kuichezea tyimu hiyo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2011-2012.
Sunzu alitua leo asubuhi akiambatana na mkewe na hadi wakati huu alikuwa akiendelea kufanya mazungumzo na uongozi wa Simba ili kuweza kumwaga wino wa kuichezea klabu hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu aliyempokea mshambuliaji huyo aliyeng'ara kwenye mihuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana akiichezea Zambia, iliyoalikwa amesema wakati wowote wataweka taarifa juu ya kumnasa rasmi mkali huyo.
Kwenye uwanja wa ndege, Sunzu ambaye alikuwa akitokea mapumzikoni nchini Nigeria, alisema amekuja nchini na kama atapata fursa ya kumalizana na Simba basi mashabiki wa timu hiyo watarajie makubwa kutoka kwake muhimu apewe ushirikiano.
Nyota huyo ambaye ameshindwa kuitumikia Al Hilal kwa kiwango stahiki kiasi cha klabu yake kutaka kumtoa kwa mkopo, alisema anazifahamu Simba na Yanga na anaimani atang'ara nchini kama ilivyo kwa mzambia mwenzake Davis Mwape aliyepo Yanga.
Simba inahaha kusaka mshambuliaji wa kuziba nafasi ya Mbwana Samatta aliyenunuliwa na TP Mazembe, ambayo Sunzu anaonekana kama 'muarubaini'wa tatizo la safu butu ya ushambuliaji ya timu hiyo iliyoshindwa kutwaa taji la Kagame kwa kulazwa na Yanga bao 1-0 katika mechi ya fainali baina yao iliyochezwa Jumapili iliyopita.
Subscribe to:
Posts (Atom)