MICHARAZO MITUPU

KWA HABARI ZA BURUDANI, MICHEZO NA MATUKIO MBALIMBALI

STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 27, 2012

Cheka, Nyilawila kupimwa afya uzito kesho, kuvaana PTA J'mosi

Karama Nyilawila (kushoto) na Francis Cheka wanaotarajia kupima uzito na afya kesho kabla ya kuvaana katika pambano lao lwa kuwania ubingwa wa Mabara wa UBO litakalofanyika siku ya Jumamosi ukumbi wa PTA.

BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na  ICB na IBF-Afrika, Francis Cheka na aliyekuwa bingwa wa Dunia wa WBF, Karama Nyilawila wanatarajia kupima uzito na afya zao kesho tayari kwa pambano lao la Jumamosi kuwania ubingwa wa UBO-Mabara.
Mabondia hao wanatarajiwa kupambana katika pambano la uzani wa Super Middle la raundi 12 kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi.
Mratibu wa pambano hilo, Robert Ekerege wa Afrika Kabisa Entertainment, alisema Cheka na Nyilawila watapimwa uzito na afya zao sambamba na mabondia wengine watakaowasindikiza kwenye pambano lao kwenye ukumbi wa Mawela jijini Dar.
Ekerege, alisema kupimwa kwa afya na uzito wa mabondia hao ni kuashiria kuiva kwa pambano hilo la kimataifa litakalochezewa na mwamuzi toka Malawi.
"Tunatarajia kuwapima afya na uzito wao mabondia wote watakaopigana Jumamosi, karibu mabondia wote wameshatua Dar tayari kwa zoezi hilo litakaloanza kufanyika saa 5 asubuhi ili kujiweka tayari kwa mchezo huo utakaofanyika PTA," alisema.
Aliongeza kuwa, maandalizi ya ujumla wa pambano hilo la Cheka na Nyilawila ambalo ni la tatu kwao kukutana na yale ya utangulizi yamekamilika ikiwemo kubadilisha mgeni rasmi wa siku hiyo kutoka Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo , Amos Makalla hadi kuwa Kamanda wa Kanda Maalum Dar, Afande Suleiman Kova.
Ekerege alisema wamemkosa Waziri Makalla waliokuwa wamempanga awali kwa vile atakuwa safarini na hivyo kumpa jukumu la kumvika mshindi wa pambano hilo la kesho Mlezi wa mchezo wa ngumi nchini, Kamanda Kova aliyethibitisha kushiriki.
Aliongeza kuwa katika mapambano hayo bendi maarufu ya Mashukaa Band 'Wana Kibega' ndio watakaotoa burudani ukumbini.

Mwisho
Posted by Unknown at 10:40 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Arsenal, Man Utd, Liverpool zang'ara Kombe la Ligi

Mchezaji Ignasi Miquel akishangilia bao lake dhidi ya Coventry City
VIGOGO vya Ligi Kuu wa England, Arsenal, Manchester United, Liverpool na Tottenham Hotspurs usiku wa kuamkia zimefanya vema katika michuano ya Kombe la Ligi baada ya kutoa vipigo kwa wapinzani wao na kuvuka raundi nyingine.
Arsenal iliisasambua  Coventry City kwa mabao 6-1 kwenye pambano lililochezwa uwanja wa Emirates mjini London, wakati mahasimu wao Tottenham walipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Carlisle United ikiwa ugenini.
Manchester United wenyewe walipata ushindi wa mabao 2-1 wakiwa uwanja wa Old Trafford dhidi ya Newcastle United, wakati Liverpool ilitoka kupokea kichapo katika Ligi Kuu toka kwa wapinzani wao wa jadi Man United iliitafuna West Bromwich Albion kwa idadi kama hiyo ya mabao 2-1.
Mechi nyingine zilizochezwa jana WPR ilijikuta ikinyukwa nyumbani na Readind kwa mabao 3-2 na Norwich City iliilaza kwa bao 1-0 timu ya Doncaster Rovers.
Matokeo kamili ya mechi za michuano hiyo kwa siku ya jana ni kama ifuatavyo:
Norwich City 1-0 Doncaster Rovers
QPR 2-3 Reading
Arsenal 6-1 Coventry City
Celtic 2-1 Benfica
Manchester United 2-2 Newcastle
Carlisle United 0-3 Tottenham
West Brom 1-2 Liverpool
More: Scores | Fixtures | League Cup
 
Posted by Unknown at 10:34 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Coastal yatakata Mkwakwani, Toto ikiendeleza mdudu wa sare

 MABAO mawili toka kwa mshambuliaji nyota na mzoefu, Nsa Job na jingine la Daniel Lyanga jana yaliipaisha timu ya Coastal Union hadi nafasi ya pili mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuilaza Kagera Sugar goli 3-2.
Coastal  ilipata ushindi huo katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga ikiwa chini ya kocha wao wa makipa, Juma Pondamali na kulingana kila kitu na Azam waliokuwa wakiishikilia nafasi hiyo.
Huo ni ushindi wa pili kw atimu hiyo baada ya awali kufanya hivyo katika mechi ya fungua dimba la Ligi Kuu dhidi ya 'majirani' Mgambo Shooting kabla ya kutoka sare mbechi nyingine mbili.
Katika mfululizo wa ligi hiyo timu ya Toto Africans ya Mwanza imeendelea na mdudu wake wa sare baada ya jana kutoka suluhu ya bila kufungana na wenyeji wao Polisi Morogoro.
Hiyo ni sare ya nne kwa Toto Africans baada ya awali kufanya hivyo dhidi ya JKT Oljoro ilitoka sare ya 1-1, Azam 2-2 na kisha Mgambo Shooting mechi yao iliyopita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki kwa michezo kadhaa itakazozihusisha timu za Azam, Yanga na Simba ambazo kwa sasa zinawindana kwa ajili ya pambano lao litakalofanyika Jumatano ijayo jijini Dar. 

Posted by Unknown at 10:18 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wednesday, September 26, 2012

SHINDALO LA UCHORAJI KWA TAASISI ZA KIELIMU


Shindalo la Uchoraji Kwa Taasisi za Kielimu
Image Profession ikishirikiana na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa mara nyingine inatangaza kuanza kwa muhula mpya wa pili wa Shindano ya Uchoraji maalumu kwa Taasisi za elimu.
Shindano ambalo pia linajulikana Kama: Educational Drawing Competition au Image Profession Educational Drawing Competition, lina malengo ya kuibua vipaji katika fani ya uchoraji kwa kuzingatia uwekezaji kwa watoto na vijana.
Theme/Wazo kuu la mwaka huu: ART IMITATES LIFE au SANAA HUFUATISHA MAISHA
Makundi ya ushiriki
´ Chekechea,
´ Elimu ya Msingi,
´ Elimu ya Sekondari na  
´ Elimu  ya Juu
Kwa maelezo na taratibu za Shindano tembelea Facebook Page/Group “Tanzania Drawing Competition” au wasiliana na BASATA au
DRAWING COMPETITION – IMAGE PROFESSION,
P O BOX 92 DAR ES SALAAM.
SIMU: +255 222 664 740 / +255 713 484 040
/ +255 714 676 217 / +255 716 430 084
EMAIL: info@imageprofession.com
Posted by Unknown at 10:44 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Kamanda Kova ambadili Waziri Makalla pambano la Cheka, Nyilawila

Kamanda Kova
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, amembadili Naibu waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Amos Makalla katika kuwa mgeni rasmi wa pambano la kimataifa la kuwania ubingwa wa UBO, kati ya Francis Cheka na Karama Nyilawila.
Mratibu wa pambano hilo litakalofanyika siku ya Jumamosi kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam, Robert Ekerege aliiambia MICHARAZO kuwa, kumekuwa na mabadiliko ya mgeni rasmi badala ya Waziri Makalla sasa atakuwa Kova ambaye ni mlezi wa ngumi Tanzania.
Ekerege alisema Kova amechukua nafasi ya Makalla kutokana na waziri huyo kupangiwa safari nje ya nchi ambayo itafanyika wakati pambano la Cheka na Nyilawila likifanyika PTA.
Mratibu huyo alisema kutokana na udhuru huo wameona ni vema nafasi hiyo achukue mlezi wao wa ngumi, Kamanda KOva ambaye ameshaitikia wito huo wa kuwa mgeni rasmi ambapo ndiye atakayemvisha mkanda mshindi wa pambano hilo la uzani wa Supermiddle la raundi 12 litakalochezwa na mwamuzi toka Malawi.
"Kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, tumeamua kubadili mgeni rasmi wa pambano la jumamosi badala ya kuwa Waziri Makalla sasa ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, Waziri atakuwa safarini na hivyo hataweza kuhudhuria kama tulivyotangaza awali," alisema Ekerege.
Aliongeza, ugeni wa Kova katika pambano lao limewaongezea uhakika wa ulinzi wa kutosha siku ya mchezo huo ambao unawakutanisha Cheka na Nyilawila kwa mara ya tatu katika safari yao ya ngumi baina yao.
Ekerege alisema maandalizi mengine yanaendelea kama kawaida ambapo mabondia wote watakaopanda ulingoni wanatarajiwa kupima afya na uzito wao kesho kwenye ukumbi huo tayari kwa pambano la Jumamosi ambalo linadhaminiwa na kinywaji cha Coca Cola na kondomu za Dume na litapambwa na burudani toka kwa Mashujaa Band waliopania kuwachezesha wapenzi wa ngumi mtindo wao wa 'Kibega'.


Posted by Unknown at 10:02 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Manchester City hoi Kombe la Ligi, Chelsea yaua

Wachezaji wa Man City wakiwa hoi baada ya kujifunga moja ya mabao yaliyoizamisha jana mbele ya Aston Villa

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, imeanza vibaya msimu kwa kung'olewa   mapema kwenye michuano ya Kombe la Ligi baada ya kulazwa mabao 4-2 na Aston Villa, huku vinara wa ligi hiyo ya England, Chelsea ikitoa kichapo cha  mabao 6-0 kwa 'Mbweha'.
Kipigo hicho toka kwa Aston Villa, kimempa wakati mgumu kocha wa Man City, Roberto Mancini, kwani ni dalili za kushindwa kurejea mafanikio iliyopata msimu uliopita ilipotwaa taji la Ligi Kuu baada ya miaka 50.
Matokeo mengine ya mechi za jana za michuano hiyo ya Kombe la Ligi ni kama ifuatavyo;
Bradford iliinyuka Burton Abilion mabao 3-2 katika muda wa nyongeza, Chelsea  ilivuna ushindi wa mabao 6-0 kw Wolves, Crawley ilinyukwa mabao 3-2 na Swansea, Leeds United ikainyoa Everton magoli 2-1.


Wachezaji wa Chelsea wakishangilia moja ya mabao yao katika mechi ya Kombe la Ligi jana usiku
Mechi nyingine Manchester City vs Aston Villa baada ya muda wa nyongeza 2-4,MK Dons ikalala mabao 2-0 kwa Sunderland, Preston iliangukia pua mbele ya Middlesbrough kwa kichapo cha mabao 3-1 na Southmpton ilivuna ushindi wa mabao 2-0 kwa Sheffied Wed, Swindon iliinyuka Burnley 3-1 na wagonga nyundo wa West Ham wakalala mabao 4-1 kwa Wigan.
Posted by Unknown at 9:50 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Mgunda afuata nyayo za Saintfiet atimuliwa Coastal Union

Hemed Suleiman 'Morocco' (kushoto) aliyetua Coastal Union
SIKU chake tangu klabu ya Yanga kumtimua kazi aliyekuwa kocha wake mkuu, Tom Saintfiet kutoka Ubelgoji, uongozi wa Coastal Union ya jijini Tanga umemtangaza, Hemed Suleiman 'Morocco' kuwa kocha mpya akichukua nafasi ya aliyekuwa kocha wao, Juma Mgunda.
Morocco, aliyekuwa akiinoa timu ya taifa ya Zanzibar, anatarajiwa kuiangalia Coastal ikicheza pambano  lao dhidi ya Kagera Sugar litakalofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani, chini ya kocha wa makipa, Juma Pondamali aliyekuwa ameachiwa timu baada ya Mgunda na msaidizi wake, Habib Kondo kutimuliwa.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini, uongozi wa Coastal ulifikia maamuzi hayo katika kikao kilichofanyika jana asubuhi na kwamba wamewatimua kufuatia kutoridhishwa na kiwango cha wachezaji wa timu hiyo licha ya kutofungwa mechi.
"Tayari wameshajulishwa maamuzi haya na Morocco atakuwa jukwaani kesho na ndiye atakayeongoza jahazi," alisema kiongozi mmoja wa juu wa timu hiyo.
Chanzo hicho kilisema kuwa katika mchezo wa leo, kocha wa makipa, Juma Pondamali ndiye atakayeiongoza timu hiyo na wanaamini mabadiliko yatazaa matunda.
Mgunda mwenyewe alinukuliwa jana akidai kuwa ameamua kujiondoa Coastal kwa nia njema na mapenzi mkubwa aliyonayo kwa timu hiyo aliyowahi kuichezea kwa mafanikio enzi zake za uchezaji.
Mgunda alisema aliona ni bora ajiondoe kutokana na shinikizo kubwa lililopo ndani ya Coastal ambayo imejiwekea malengo makubwa katika msimu huu wa ligi na kuwataka mashabiki na viongozi wa timu hiyo kumheshimu na kuyaheshimu maamuzi yake yaliyokuja wakati Coastal ikiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kutokana na kushinda mechi moja na kupata sare mechi mbili.
Posted by Unknown at 9:35 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Simba yaenda Zenji kuiwinda Yanga, Jangwani wakimbilia Bagamoyo








MABINGWA watetezi wa soka nchini Simba imeondoka jijini jana kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiwinda na pambano lao na watani zao Yanga litakalochezwa Jumatano ijayo.
Timu hizo mbili zinatarajiwa kukutana katika pambano la kwanza kwa msimu huu litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kurushwa 'live' na kituo cha Super Sport, huku Yanga ikiwa na deni kubwa la kipigo cha mabao 5-0 iliyopata katika pambano baiona yao lililofungia msimu uliopita.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu', alinukuliwa jana kuwa wachezaji wote 29 wa timu hiyo wameondoka na wanatarajia kurejea keshokutwa kwa ajili ya kuvaana na Prisons ya Mbeya kabla ya kurejea tena visiwani humo kuweka kambi hadi siku ya mchezo wao na Yanga.
Alisema kuwa wakiwa Zanzibar wataendelea kufanya mazoezi ya ufukweni na ya uwanjani na wanaamini kambi yao itazaa mafanikio kwa kushinda mechi hizo zinazowakabili.


Wakati Simba ikienda kujichimbia Zenji, watani zao walikuwa katika mchakato wa kuelekea mjii Bagamoyo kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo la watani zao na lile la Jumamosi ijayo itakapoumana na African Lyon.


Yanga imepania kulipa kisasi cha mabao hayo 5-0 iliyofungwa na Simba Mei 6, lakini pia wakiwa na deni la miaka zaidi ya 30 ya kipigo cha mabao 6-0 ilichopewa na Simba mwaka 1977.
Posted by Unknown at 9:25 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest



YANGA HATARINI KUSHUSHWA DARAJA - MADENI YA PAPIC NA NJOROGE YAWAPONZA FIFA

Kikosi cha Yanga kilichopo hatarini kiushushwa daraja
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah


Tumepokea barua kutoka Kitengo cha Sheria cha Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpirawa Miguu (FIFA) likitutaka tuitaarifu Yanga kuhusu mashtaka yaliyowasilishwa na kocha wazamani wa klabu ya Yanga, Kostadin Papic. Katika malalamiko yake, Papic anadai kuwa hajalipwa malimbikizo ya mshahara wake yanayofikia kiasi cha Dola 12,300 za Kimarekani. Katika barua yake, kocha huyo anadai kuwa alikuwa akiwasiliana na maofisa na viongozi wa Yanga, lakini hakupata ushirikiano na hivyo kuamua kwenda FIFA. TFF ilifanya juhudi za kuwasiliana na Yanga kuhusu malalamiko hayo ili kujaribu kumzuia kocha huyo asishtaki FIFA, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda.
Kama chombo kinachosimamia uendeshaji wa mpira wa miguu nchini, TFF imesikitishwa na habari hizo na inaiomba klabu ya Yanga kufanya kila jitihada kuhakikisha kuwa inawasilisha taarifa zote muhimu na nyaraka zinazohusiana na stahiki za kocha huyo ili kama ilishamalizana naye, sifa ya klabu ya Yanga isafishwe. Tayari barua imeshaandikwa kwa klabu ya Yanga kuitaka itekeleze utashi huo mapema iwezekanavyo.
Tukio hilo, si tu linachafua sifa ya klabu ya Yanga, bali soka ya Tanzania kwa ujumla kutokana na ukweli kwamba ikishadhihirika kuwa kuna tatizo la malipo ya makocha nchini, ni dhahiri kuwa itakuwa ni vigumu kwa klabu zetu na hata timu za taifa kupata makocha wazuri kutoka nje kwa kuwa watakuwa wamejengeka hofu ya kufanya kazi nchini.
Hili ni tukio la pili kwa Yanga baada ya mchezaji wake mwingine, John Njoroge kuishtaki klabu hiyo FIFA na kushinda kesi yake iliyoamuliwa mwezi Januari na Kitengo cha Usuluhishi wa Migogoro cha FIFA (DRC). Ushindi wa Njoroge unamaanisha kuwa iwapo Yanga itashindwa kutekeleza kumlipa mchezaji huyo kasi cha Sh milioni 17, inaweza kujikuta katika adhabu ambayo itatulazimisha tuishushe daraja; kuinyang’anya pointi kwa kiwango kitakachotajwa na FIFA; kuipiga faini au adhabu zote kwenda kwa pamoja. Tunaiomba Yanga itekeleze hukumu hiyo kwa wakati uliotajwa kwenye barua ya FIFA ili kuepuka hatua hizo.
Suala la Njoroge ni moja kati ya matukio mengi yanayohusu ukiukwaji wa taratibu za kuvunja mikataba yanayofanywa na klabu zetu. Kuna malalamiko ya wachezaji wengi dhidi ya klabu zao za zamani kuhusu kutolipwa stahiki zao. Hivyo TFF inatoa wito kwa klabu kujiepusha na vitendo hivyo kwa kuwa vinawanyima haki wachezaji, lakini pia vinachafua sifa ya nchi iwapo wachezaji wanachukua hatua za kwenda kwenye vyombo vya juu.
Tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari kuhusu kutimuliwa kwa sekretarieti nzima ya Yanga kutokana na kuonekana kuwa ina udhaifu. Taarifa hizo hazijaifikia rasmi TFF. Kiutaratibu, Yanga inatakiwa iwsasilishe majina ya maofisa watakaofanya kazi na TFF kwa sasa na itakapoajiri sekretarieti ya kudumu, basi itume barua nyingine ya kuwatambulisha watendaji wake.
Kama itakuwa imeitimua sekretarieti nzima, basi TFF inapokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa. Si nia ya TFF kutetea watendaji wazembe, lakini klabu hazina budi kufuatilia kwa karibu utendaji wa sekretarieti zao ili isije ikafikia wakati sekretarieti nzima inaondolewa kwa makosa ambayo yangeweza kusahihishwa kama kungekuwa na ufuatiliaji wa karibu. TFF imekuwa ikitoa mafunzo kwa watendaji wa klabu ili waweze kufanya kazi zao vizuri na kwa mintaarafu ya mpira wa miguu na hivyo kuondolewa kwa timu nzima kama hiyo kunamaanisha kuwa ni upotevu wa rasilimali ambayo imetumika kuwapa elimu ya kutenda kazi zao vizuri. TFF ilishafanya kozi ya Event Management kwa ajili ya watendaji wa klabu; semina ya kuangalia upya maazimio ya Bagamoyo kwa watendaji na viongozi na pia kozi ya utawala hivyo haipendi juhudi hizi zipotee kirahisi.
Angetile Osiah
KATIBU MKUU
Posted by Unknown at 9:05 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Monday, September 24, 2012

Vincent Barnabas akiri ligi ngumu msimu huu

Vincent Barnabas (kushoto) akiwa dimbani na timu ya taifa , Taifa Stars

WINGA machachari wa timu ya soka ya Mtibwa Sugar, Vincent Barnabas amesema matokeo ya mechi za awali za Ligi Kuu Tanzania Bara zimeonyesha jinsi gani msimu huu utakuwa na ligi ngumu isiyotabirika kirahisi.
Aidha nyota huyo aliyewahi kutamba na timu za Kagera Sugar, Yanga na African Lyon, ameitabiria klabu yake ya Mtibwa Sugar kufanya vema tofauti na msimu uliopita ilipomaliza ikiwa nafasi ya nne.
Akizungumza na MICHARAZO, Barnabas, alisema kwa mechi za raundi tatu zilizokwisha kucheza mpaka sasa inaonyesha wazi ligi ya msimu huu sio nyepesi kama watu walivyokuwa wakiifikiria.
Nyota huyo alisema kutokana na mwenendo wa ligi hiyo, ni vigumu kutabiri mapema nani anayeweza kuwa bingwa kwa vile ligi bado haijatulia.
"Sio siri msimu huu ligi imeanza kuonyesha ni ngumu kwa aina ya matokeo yaliyopatikana, naamini ugumu huu umetokana na klabu zote kujipanga vema na kusaidia kuongeza ushindani," alisema.
Juu ya Mtibwa ambayo ilianza kwa sare dhidi ya Polisi Moro kabla ya kuilaza Yanga mabao 3-0 na kuzimwa na Azam mwishoni mwa wiki kwa bao 1-0, winga huyo alisema anaamini itafanya vema msimu huu tofauti na ligi iliyopita.
"Kwa namna tulivyo, naamini tutafanya vema, licha ya ugumu unaoonekana kwenye ligi ya msimu huu, wachezaji tumejipanga kuipigania timu ili imalize msimu tukiwa katika nafasi bora zaidi ya msimu uliopita," alisema Barnabas.
Kwa matokeo ya mwishoni mwa wiki, Mtibwa imejikuta ikiachwa nafasi ya sita ya msimamo ikiwa na pointi nne sawa na ndugu zao za Kagera Sugar na Yanga iliyozinduka kwa kuilaza JKT Ruvu mabao 4-1, ikizizidi uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Mwisho
Posted by Unknown at 10:56 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Mashali, Sebyala kumkumuka Mwl Nyerere kwa masumbwi Dar

Med Sebyala wa Uganda akiwa na taji lake la ubingwa wa Uganda
Thomas Mashali wa Tanzania akiwa na ubingwa wake wa TPBO


BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali anatarajia kuzidunda na Mganda Med Sebyala katika pambano la kuwania taji la Afrika Mashariki siku ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere.
Pambano hilo la uzati wa kati la raundi 10 limepangwa kufanyika Oktoba 14 kwenye ukumbi wa Friends Corner, Manzese Dar es Salaam.
Mratibu wa pambano hilo litakalosimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Regina Gwae alisema tayari wameshamalizana na mabondia hao kwa ajili ya pambano hilo la kimataifa.
Regina, alisema pambano hilo ni fursa nzuri kwa Mashali anayeshikilia ubingwa wa Taifa wa TPBO kujitangaza kimataifa iwapo atafanikiwa kumnyuka Sebyala.
“Huwezi kwenda nje kama ndani hufanyi vizuri na huwezi kwenda Ulaya, iwapo unashindwa kutamba  Afrika Mashariki, hivyo tumeona tumpe Mashali mchezo huu ili akifanya vyema aweze kuvuka mipaka ya sasa, "alisema Regina.
Regina alisema ana matumaini mpambano huo utakuwa mzuri na utakaovutia kutokana na ukweli mabondia wote wawili wana sifa zinazofanana waking'ara ndani ya nchi zao.
Alisema Sebyala ni mmoja wa bondia wazuri waliowasumbua baadhi ya nyota wa ngumi nchini kama Rashid Matumla na Francis Cheka aliowahi kuja kucheza nao hapa nchi  katika mechi za zisizo za ubingwa.
Mratibu huto aliwaomba wafadhili wajitokeze kwa ajili ya kudhamini mchezo huo unatarajiwa kuwa na mapambano ya utangulizi.

Mwisho
Posted by Unknown at 10:54 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Maugo kuwania ubingwa wa WBF Arusha

Bondia Mada Maugo

BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo anatarajiwa kupanda ulingoni mjini Arusha kuzichapa na Mustapha Katende kutoka Uganda katika pambano la kuwania ubingwa wa Mabara wa WBF.
Pambano hilo la uzani wa Super Middle la raundi 12 litafanyika Oktoba 28 kwenye ukumbi wa Triple A, jijini humo na kusindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki wa kizazi kipya.
Akizungumza na MICHARAZO leo asubuhi, Maugo alisema awali pambano hilo litakalosimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania, PST, lilikuwa limkutanishe na bondia toka Iran, Gavad Zohrenvard.
Maugo alisema hata hivyo bondia huyo wa Iran amepatwa na dharura na hivyo kupangiwa Mganda ili kuonyeshana nae kazi siku ya pambano hilo.
"Natarajia kupanda ulingoni Oktoba 28 kwenye ukumbi wa Triple A mjini Arusha kuzichapa na Mganda, Mustapha Katende, ambapo pia tutasindikizwa na michezo mbalimbali ya utangulizi," alisema.
Alitaja baadhi ya mabondia watakaowasindikiza siku hiyo ni Robert Mrosso wa Arusha atakayepigana na Selemani Said 'Tall' wa Dar na Abbas Ally wa Arusha dhidi ya Joseph Marwa wa Zanzibar.
Bondia huyo aliyepanda mara ya mwisho ulingoni April mwaka huu kuwania ubingwa wa IBF-Mabara dhidi ya Francis Cheka na kupigwa, alisema amejiandaa vya kutosha kuweza kunyakua taji hilo la WBF dhidi ya Mganda.
"Naendelea kujifua kwa ajili ya kuhakikisha natwaa taji hilo, sambamba na kusaidia kutoa hamasa kwa vijana wenye vipaji vya ngumi mkoani Arusha," alisema Maugo.

Mwisho
Posted by Unknown at 10:51 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

WAZIRI MAKALLA MGENI RASMI PAMBANO LA CHEKA< NYILAWILA

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Amos Makalla atakayekuwa mgeni rasmi katika pambano la ngumi la kuwania ubingwa wa UBO Mabara kati ya Francis Cheka na Karama Nyilawila


NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni Vijana na Michezo, Amos Makalla anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa pambano la kimataifa la kuwania ubingwa wa Mabara wa UBO kati ya mabondia Francis Cheka na Karama Nyilawila.
Pambano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam Septemba 29, na waratibu wa mchezo huo, kampuni ya Afrika Kabisa Entertainment wamesema Waziri Makalla ndiye atakayemvisha taji mshindi.
Promota Robert Ekerege, aliiambia MICHARAZO kwamba tayari amehakikishiwa na Waziri Makalla kuwa mgeni rasmi katika pambano hilo la Super Middle la raundi 12 amblo litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
"Mgeni rasmi katika pambano letu kati ya Cheka na Nyilawila atakuwa Naibu Waziri wa Michezo, Amos Makalla, na kila kitu kimekamilika katika maandalizi ya pambano hilo," alisema Ekerege.
Ekerege alisema mbali na Waziri Makalla, pia siku ya pambano hilo litahudhuriwa na Mlezi wa mchezo wa ngumi nchini, Suleiman Kova ambaye ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa, katika kunogesha pambano hilo mabondia kadhaa karibu 10 watapanda ulingoni kuwasindikiza akina Cheka kwa kucheza michezo ya raundi sita kila moja na wa watasindikiza na burudani toka Mashujaa Band.
"Mashujaa Band ndio watakaosindikiza michezo hiyo yote ambayo itakuwa na ulinzi wa kutosha ili kudhibiti vitendo vyote vya kihuni ambavyo vinaweza kutuharibia," alisema Ekerege.

Mwisho
Posted by Unknown at 10:50 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

VAN PERSIE AIZAMISHA LIVERPOOL, ARSENAL WAISHIKA MANCHESTER CITY, DEMBA BA HASHIKIKI...MILAN, INTER HOI!


LONDON, England
PENATI ya Robin van Persie kuelekea mwishoni mwa mechi iliipa Manchester United iliyocheza chini ya kiwango ushindi wa ugenini wa 2-1 dhidi ya wachezaji 10 wa Liverpool katika mechi yao iliyojaa hisia ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Anfield huku mabingwa watetezi, Manchester City wakishikiliwa kwa sare ya nyumbani ya 1-1 dhidi ya Arsenal leo.
Mholanzi Van Persie aliwahakikishia ushindi Man U wakati alipopiga penati ya shuti kali iliyomshinda kipa Pepe Reina kufuatia Glen Johnson kumuangusha Antonio Valencia.
Licha ya kucheza chini ya kiwango, Man U walipanda hadi katika nafasi ya pili katika msimamowa ligi wakiwa na pointi 12, wakizidiwa kwa pointi moja tu na vinara Chelsea.
Man City walipata sare ya tatu katika mechi zao tano za mwanzo wa msimu baada ya  Laurent Koscielny kuisawazishia Arsenal kwa bao la 'usiku' kufuatia goli la utangulizi la Joleon Lescott kuwapa wenyeji uongozi hadi mapumziko. Timu zote mbili hazijafungwa na kufikisha pointi tisa.
Tottenham Hotspur wamefikisha pointi nane baada ya Jermain Defoe kuwafungia bao la ushindi wa 2-1 dhidi ya Queens Park Rangers, ukiwa ni ushindi wa kwanza wa nyumbani wa Tottenham chini ya kocha Andre Villas-Boas.
Demba Ba alifunga bao pekee lililowapa Newcastle United ushindi wa 1-0 dhidi ya Norwich City inayonolewa na kocha wao wa zamani, Chris Hughton.
Hiyo ilikuwa ni mechi ya kwanza kwenye Uwanja wa Anfield tangu kutolewa kwa taarifa ya  Hillsborough iliyowasafisha mashabiki wa Liverpool ambao awali walikuwa wakilaumiwa kwa kusababisha vifo vya mashabiki 96 kwenye mechi yao ya nusu fainali ya Kombe la FA mwaka 1989.
Balaa kwa Liverpool lilianza katika dakika ya 39 wakati mchezaji wao Jonjo Shelvey alipotolewa nje kwa kadi nyekundu.
Hata hivyo, Liverpool walipata bao walilostahili baada ya kuanza kipindi cha pili kupitia shuti la Steven Gerrard, lakini Man U wakasawazisha dakika sita baadaye kupitia shuti la "upinde" la beki Rafael.
Bao la 'usiku' la Van Persie, ambalo ni la tano kwake msimu huu, limemuacha kocha Brendan Rodgers akikosa ushindi baada ya mechi tano za mwanzo wa msimu, ikiwa ni rekodi "mbovu" kabisa katika historia ya klabu hiyo kwenye Ligi Kuu ya England.
Posted by Unknown at 10:43 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Yanga kupokwa ushindi dhidi ya JKT Ruvu?

Kikosi cha timu ya Yanga

LICHA ya kuchekelea ushindi wa mabao 4-1 iliyopata dhidi ya JKT Ruvu, mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga huenda wakapokwa ushindi wao huo iliyopata juzi kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar iwapo itabainika wakikiuka kanuni za ligi juu ya idadi ya wachezaji wa kigeni kucheza mechi moja.
Yanga katika mechi yao na JKT iliwachezesha wachezaji wake wote watano wa kigeni, kitu kinachoelezwa ni kinyume na kanuni inayoruhusu klabu kuwatumia wachezaji wasiozidi watatu kucheza mechi moja ya ligi.
Katika pambano hilo la juzi Yanga iliwachezesha mapro wake wote akiwamo kipa Yew Berko, beki Mbuyu Twite, kiungo Haruna Niyonzima, mshambuliaji Didier Kavumbagu na winga Hamis Kiiza.
Micharazo, imedokezwa kwamba uongozi wa Simba tayari unajiandaa kuwasilisha barua ya kupinga kitendo kilichofanywa na watani zao za kuwatumia wachezaji wake hao wa kigeni katika mechi moja, ingawa tunaendelea kufuatilia kuona kama Yanga ilikiuka kanuni ya ligi kuhusu wachezaji au la...
Kama itakuwa imekiuka kuna uwezekano Yanga wakajikuta wakipokwa ushindi huo na kuzidi kuwasononesha baada ya kutoka kwenye machungu ya kushindwa kufurukuta katika mechi zao za awali ambapo ililazimishwa suluhu na Prisons Mbeya kabla ya kulala mabao 3-0 kwa Mtibwa Sugar.


Posted by Unknown at 10:38 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Simba yazidi kupaa Ligi Kuu Tanzania Bara

Amri Kiemba wa Simba ajijaribu kumtoka beki wa Ruvu katika pambano lao la jana
 
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba, wameendeleza wimbi la ushindi wa asilimia 100, baada ya kuibuika na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting, pambano lililochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Simba ilipata bao la kuongoza dakika ya 30, likiwekwa nyavuni na nyota wa kimataifa wa Zambia, Sunzu kwa kichwa maridadi akimalizia krosi iliyopigwa baada ya kazi nzuri ya kuwachambua mabeki iliyofanya na Said Nassor ‘Cholo’ aliyepanda kusaidia mashambulizi.

Dakika 38, Kiemba akawachachafya wachezaji wa Ruvu, kabla ya krosi yake kukosa mmaliziaji na kuishia mikononi mwa Benjamin Haule.

Simba iliendelea kushambulia ambapo katika dakika ya 44, beki Mau Bofu wa Ruvu alimwangusha Sunzu ndani ya 18 na mwamuzi Swai kuamuru ipigwe penati. Akuffor akabeba jukumu la kupiga tuta hilo, ambalo mlinda mlango Haule alipangua na kuwa kona tasa.

Hadi mapumziko, Simba ilitoka ikiongoza kwa bao hilo, huku mashabiki waliohudhuria mechi hiyo wakishuhudia maamuzi tata ya mwamuzi Swai, aliyeonekana dhahiri kutowajali vibendera wake Samwel Mpenzu na Godfrey Kihwili wote wa Arusha pindi wanapoashiria madhambi.

Kipindi cha pili kilianza kwa Ruvu kushambulia lango la Wekundu na kama si umakini mdogo miongoni mwa washambuliaji wake Paul Ndauka, Hussein Said na Hassan Dilunga aliyekuwa akipenya kirahisi safu ya ulinzi, wangeweza kupata mabao.

Sunzu akafanya shambuliazi kali dakika ya 55 lililotokana na jitihada binafsi akiwalima chenga mabeki, kabla ya Ruvu nao kurudi langoni mwa Simba na Dilunga (Hassani) nusura aipatie bao timu yake, kabla ya mawasiliano madogo na Abdulrahman Mussa kumgharimu.

Ruvu ikapata bao la kusawazisha mnamo dakika ya 78, lililowekwa nyavuni na mtokea benchi Seif Rashid, akitumia makosa ya beki Juma Nyoso wa Simba, aliyeshindwa kuondoa hatari langoni akiwa peke yake na kuukanyaga mpira huo na kuteleza, ambapo Seif aliunasa na kumchambua Juma Kaseja.

Daniel Akuffor akimtoka beki wa Ruvu Shooting


Wakati wengi wakimiani matokeo ya pambano hilo yangebaki kuwa ni sare ya bao 1-1, mtokea benchi wa Simba, Christopher Edward aliyeingia kuchukua nafasi ya Akuffor, akaipatia timu yake bao la pili dakika ya 87 kwa shuti na kuamsha mamia ya mashabiki wake jukwaani.
Posted by Unknown at 10:25 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Saturday, September 22, 2012

Minziro amrithi Saintfeit, Mwalusako arejeshwa Jangwani

Lawrance Mwalusako
KLABU ya soka ya Yanga imemrejesha madarakani Katibu Mkuu wao wa zamani, Lawrance Mwalusako na kumpa nafasi kocha msaidizi wa timu hiyo, Fred Felix Minziro kukaimu ukocha mkuu baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wake, Tom Saintfiet.
Taarifa zilizopatikana mapema leo leo asubuhi inasema kuwa, Mwalusako atakaimu nafasi ya ukatibu Mkuu iliyokuwa ikishikiliwa na Celestine Mwesigwe,huku Sekilojo Chambua akiteuliwa kuwa meneja wa timu na mtangazaji wa Cloud's, Abdul Mohammed akimrithi Louis Sendeu aliyekuwa amemaliza mkataba wa kuwa Afisa Habari wa Yanga.
Kutokana na mabadiliko hayo leo Yanga itashuka dimba la Taifa kuvaana na JKT Ruvu ikiwa chini ya safu mpya ya benchi lake la ufundi, Minziro akiongoza kama kaimu kocha Mkuu.
Fred Felix Minziro
Yanga haijashinda mechi zake mbili za awali ikianza na suluhu dhidi ya Prisons ya Mbeya kabla ya kubamizwa mabao 3-0 na Mtibwa Sugar.
Posted by Unknown at 12:49 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

  MECHI ZA ‘LIVE’ SUPER SPORTS LIGI KUU TANZANIA BARA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Septemba 21, 2012

MUDA WA MECHI ZA ‘LIVE’ SUPER WEEKEND
Mechi tano za Ligi Kuu ya Vodacom za Super Weekend katika mzunguko wa kwanza zitakazooneshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Super Sport zitaanza kati ya saa 1-.30 jioni na saa 1 kamili usiku.

Septemba 28 mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 1 kamili usiku. Mechi ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Septemba 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itaanza saa 11 kamili jioni.

Yanga na African Lyon zenyewe zitapambana Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni wakati Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar zitaoneshana kazi Oktoba 1 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.

Mechi ya mwisho katika Super Weekend itakuwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwakutanisha watani wa jadi Yanga na Simba, na itaanza kutimua vumbi saa 1 kamili usiku.

TWFA YATANGAZA KAMATI YA UCHAGUZI
Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) kimetangaza Kamati ya Uchaguzi yenye wajumbe watano kwa ajili ya uchaguzi wake unaotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu.

Kaimu Mwenyekiti wa TWFA, Margreth Mtaki amewaambia Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo kuwa kamati hiyo itaongozwa na Ombeni Zavala, na itarajia kutangaza mchakato wa uchaguzi huo Jumatatu (Septemba 24 mwaka huu).

Aliwataja wajumbe wengine wa kamati hiyo yenye jukumu la kuendesha uchaguzi wa chama hicho kuwa ni Rachel Masamu, Lloyd Nchunga, Nancy Mabula na Maneno Tamba.

Pia aliwataka wadau wa mpira wa miguu wa wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika TWFA mara Kamati ya Uchaguzi itakapoanza mchakato.

Wakati huo huo, uchaguzi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Kilimanjaro (KRFA) na Manyara (MARFA) unafanyika kesho (Septemba 22 mwaka huu).


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Posted by Unknown at 11:00 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Mpasuko wa kisiasa waibuka tena Zanzibar


Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar

 CHAMA cha Wananchi CUF kimesema kimegundua kuna viongozi wa SMZ  hawataki maridhiano yaliyozaa serikali ya Umoja wa Kitaifa, Novemba mwaka 2010.

Tamko hilo limetolewa na Mkurugenzi wa habari, Uenezi na mawasiliano ya umma wa CUF jana Salim Bimani Abdalla, kufuatia vurugu zilizotokea katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Bububu Septemba 16 mwaka huu.

Alisema kwamba chama hicho tayari kimewafahamu baadhi ya Viongozi kutoka CCM wanaopinga serikali ya Umoja wa kitaifa na tayari wanajitayarisha kuwashitakia kwa wananchi kupitia vyombo vya kutunga sheria Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BLW) na Bungeni.

Alisema kwamba hatua hiyo itasadia wananchi kuwatambua viongozi wenye kinyongo na mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ambayo yaliruhusu mfumo wa mpya wa serikali  ya pamoja.

“Kuna Viongozi  wa Serikali hawataki maridhiano yalioleta serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar tumewafahamu kupitia uchaguzi wa Bububu,”alisema Bimani.

Alieleza  kwamba vurugu za askari wa Vikosi kutumia nguvu kubwa ikiwemo kutisha watu kwa risasi za moto ni ushaidi wa kuwepo kuwepo viongozi ambao hawataki kubadilika na kumaliza siasa za uhasama visiwani humo.

Alisema kwamba hakutegemea vikosi vya SMZ  kutumia nguvu kubwa ikiwemo kutumia risasi za moto kupiga hewani wakati Vikosi hivyo vipo chini ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais (IKULU).

Aidha alisema kwamba katika kampeni za uchaguzi huo kuna viongozi wa CCM walitumia majukwaa vibaya ikiwemo kutoa lugha za matusi dhidi ya viongozi wa CUF wanaoshiriki kuunda serikali ya Umoja wa kitaifa.

Akizungumzia tuhuma hizo Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema tuhuma za CUF hazina msingi wowote na zimelenga kuficha ukweli na kuwadaganya wananchi.

Alisema kwamba chimbuko la vurugu katika uchaguzi huo limetokana na Viongozi wa CUF kupeleka  Vijana  3000 usiku wa kuamkia uchaguzi na kuwapa kazi ya kutisha watu ikiwemo kuhakiki wapiga kura waliokuwa wanajitokeza wakiwa katika magari kinyume na sheria ya uchaguzi.

Vuai alisema kwamba vijana  wa CUF walikuwa wakizuia watu kwenda kupiga kura hasa wafuasi wa CCM na kutoa vitisho kabla ya askari kuamua kuwatawanya katika maeneo ya vituo vya wapiga kura.

Vuai alisema kwamba wangalizi wa uchaguzi kutoka  CUF wakiwemo mawaziri baadhi yao walifanya kazi  kukagua kadi za  wapiga kura wakati sio majukumu yao.



Alisema kwamba sheria za uchaguzi zilianza kuvunjwa mapema na baadhi ya Mawaziri wa CUF kutokana na kutumia magari ya umma wakati wa kampeni na uchaguzi kinyume na sheria na misingi ya Utawala bora.

Alisema kwamba CCM ilitarajia kuwa CUF watafanya kampeni za kistarabu baada ya kumaliza tofauti za kisiasa tangu kuuda serikali ya pamoja, lakini wameshindwa kubadilika na kuendeleza siasa za chuki na uhasama kinyume na mataraji ya wananchi.

Vuai alisema kwamba katika uchaguzi huo watu wenye asili ya Pemba awakuhojiwa uhalali  wa kupiga kura tofauti na watu wenye asili ya  Bambi, Makunduchi au  Donge katika uchaguzi huo.

Vuai alisema akiwa kama  muasisi wa muafaka kutoka CCM anajuta kwa kupoteza muda kutafuta amani ya Zanzibar baada ya kuibuka wanasiasa wanaorudisha siasa za chuki na ubaguzi na kuvuruga amani na Umoja wa kitaifa.

Alisema kwamba CUF imeshindwa kufanya siasa za kistarabu ikiwemo kukemea vitendo vya kuhatarisha amani na umoja wa kitaifa vinavyoofanywa na Jumuiya ya Uamsho na mihadhara Zanzibar. (JUMIKI).

Alisema Uamsho wamekuwa wakitoa lugha chafu dhidi ya Viongozi wa Kitaifa  na waasisi wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

“Najuta kupoteza muda wangu kutafuta muafaka wa amani ya Zanzibar wakati wezetu awataki kuacha siasa za chuki na uhasama,’alisema Vuai ambaye alikuwa Mjumbe wa kamati ya Muafaka.

Alisema kwamba akukuwa na sababu za msingi kwa viongozi wa CUF kuhakiki kadi za wapiga kura katika vituo wakati ndani ya chumba cha wapiga kura kuna mawakala wa vyama na orodha ya majina ya wapiga kura yakiwa na majina na picha za wahusika.

Katika uchaguzi huo mgombea wa CCM Hussen Ibrahim Makungu aliebuka mshindi kwa kumtagulia mgombea wa CUF Issa Khamis issa ambaye amegoma kusaini matokeo na kutangaza kupiga matokeo mahakama Kuu ya Zanzibar.

Mwisho


Posted by Unknown at 10:59 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

WAISLAM WAWAZIDI KETE POLISI WAANDAAMANA NA KUFANYA KONGAMANO DAR LICHA YA KUPIGWA MKWARA

JUMUIA NA TAASISI ZA KIISLAM TANZANIA WAKIWA KATIKA MAANDAMANO YA KUTOA TAMKO LA WAISLAM NCHINI DHIDI YA MAREKANI KURUHUSU KUTOLEWA FILAMU INAYOUKASHIFU MTUME MUHAMAD

JUMUIA NA TAASISI ZA KIISLAM TANZANIA WAKIWA KATIKA MAANDAMANO YA KUTOA TAMKO LA WAISLAM NCHINI DHIDI YA MAREKANI KURUHUSU KUTOLEWA FILAM INAYOUKASHIFU MTUME MUHAMMADI SAW

JUMUIA NA TAASISI ZA KIISLAM TANZANIA WAKIWA KATIKA MAANDAMANO YA KUTOA TAMKO LA WAISLAM NCHINI DHIDI YA MAREKANI KURUHUSU KUTOLEWA FILAM INAYOUKASHIFU MTUME MUHAMAD

waumini wa kiislam wakiwa katika kongamnao lao la kulaani Marekani kwa kuruhusu kutengenzwa kwa Filamu inayomkashfu Mtume Muhammad 'SAW' jana kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu, jijini Dar es Salaam

Umma wa Kiislam ukiwa kwenye kongamano lao lililofanyika jana jijini Dar

Umma wa Mtume Muhammad SAW, ukiwa kwenye kongamano lao la kulaani utengenezwaji wa filamu ya kumkshfu Mtume Muhammad SAW.
CHANZO:MZUKA WA FUNGO
Posted by Unknown at 10:59 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

IBF YAWATEUA MAKAMU WANNE WA RAIS KATIKA BARA LA AFRIKA, GHUBA ZA UARABU NA UAJEMI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAREHE 20/09/2012


Shirikisho la Ngumi la Kimataifa IBF limepanua wigo wake wa kusimamia na kuratibu ngumi katiuka bara lka Afrika, Mashariki ya kati, Ghuba ya Urarabu na Ghuba ya Uajemi. Katika miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa sana la vijana wengi kujiunga na ngumi na hivyo wengi kuhitaji huduma za shirikisho la IBF.
 
Ili kujiweka vizuri katika nafasi ya kutoa huduma nzuri inayotakikana, IBF imewateua Makamu wanne wa rais watakaomsaidia Raia wa Shirikisho hili Bwana Onesmo Ngowi.

Uteuzi huu umefuata mambo yafuatayo: Upendo wa wahusika wenyewe kwa mchezo wa ngumi, nafasi aliyonayo kwenye jamii, ukaribu wake na vijana, uwezo wake kielimu na michango yake kwa michezo.

Wafuatao wameteuliwa kuwa makamu wa Rais kuanzia mwisho wa mwezi huu:

Ayman Saad Bait-Saleem (Oman);

Makamu wa Rais,  Fedha
Ayman ni mhandisi mwenye shahada ya uzamili kutoka katika chuo kikuu cha Karolina ya Kusini (University of South Carolina, Colombia South Carolina, USA.) mwa nchi ya Marekani. Amefanya kazi kama Meneja Mkuu wa bandari ya Sultan Qaboos kwa miaka mingi, Meneja wa kampuni ya APL Moller Group ya Denmark nchini Oman, Kampuni ya Marekani ya ushauri wa Kihandisi na nyingine nyingi. Kwa sasa Ayman ni mfanyabishara mwenye kampuni nyingi nchini Oman mojawapo ikiwa ni AL SWAYNI SPORT SERVICES katika jiji la Muscat, Oman

William Steven Kallaghe

Makamu wa Rais, Utawala na Masoko
William ni msomi aliyebobea katika masuala ya Uchumi na Utawala na alisoma katika chuo kikuu cha Budapest, Hungary. Ana uzoefu mkubwa kwenye masuala ya uchumi na masoko na amefanya kazi na makampuni kadhaa kama Mkurugenzi Mkuu wa benki ya kiislamu ya NBC, Meneja Miradi wa benki ya CRDB, Meneja wa Masoko wa Kanda wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kabla ya kuhamishia ujuzi wake kama Mkurugenzi wa Masoko wa Benki ya NBC.

Henry Mann-Spain (Ghana)

Makamu wa Rais, Operations
Henry ni mfanyabishara aliyeboboea kwenye biashara mbalimbali na analimiki makampuni makubwa ya kutengeneza bidhaa za kilimo kama nguo na vyakula vya kugandishwa (Frozen Food).
Ana Shahada ya Uzamili wa Biashara (MBA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Harvard kilichopo katika jimbo la Massachusetts nchini Marekani. Henry amefanya kazi kwa miaka mingi na mashirika ya kimataifa yakiwamo UNHCR, ILO na UNDP.
Kwa sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Golden Crescent Ltd yanayojishughulisha na kutengeneza bidhaa kutoka kwenye mazao ya mifugo na kilimo nchini Ghana na kuyauza nchi za Ulaya, Marekani na Asia.


Louaa Debes (Misri)

Makamu wa Rais, Ubingwa na Viwango
Louaa ni mfanya biashara anayeishi katika jiji la cairo nchini Misri na ana uzoefu nkubwa kweney masuala ya biashara za kutengeneza nguo.
Louaa Debes amesoma biashara kwenye Chuo Kikuu cha Cairo na amefanya kazi na taasisi za serikali kabla ya kuanzisha shughuli za biashara. Debes anamiliki makampouni ya ulinzi, maduka makubwa (Super markets) pamoja na kamouni ya ukodishaji wa magari.

Imetolewa na:
Onesmo A.M. Ngowi

Rais
IBF katuka bara la Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba ya Uarabu na Uajemi.
(IBF President for Africa, Middle East, Arabian and Persian Gulfs)
Posted by Unknown at 10:41 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

99 BEAUTIFUL NAMES OF ALLAH

Sikiliza Redio

FREE LIVE RADIO ONLINE
Clouds FM
Listen to Clouds FM - FM 88.4 - Dar es Salaam

Grab radio widget | More radio
Free Live Radio Stations

LEO NI:

SASA NI

Blog Archive

  • ▼  2018 (47)
    • ▼  May (29)
      • ▼  May 06 (29)
        • Rostand anatunguliwa na kipa mwenzake
        • Waarabu wanapata penalti
        • Zimeongezwa dakika mbili
        • Dante ameumia
        • Pato anaingia kumpokea Makapu
        • Darfalou alimwa kadi naye
        • Juma Mahadhi apewa kadi
        • Rafael anatoka Abdul anaingia
        • Yanga inapigwa la tatu
        • Hassan Kessy anaupiga mwingi
        • Waarabu wameanza uhuni wao
        • Mopira umeanza
        • Timu zinarudi uwanjani
        • Takwimu za nusu ya kwanza
        • Ni mapumziko sasa
        • Imeongezwa dakika moja ya nyongeza
        • Yanga wanakosa bao
        • Pengo la Tshishimbi, Chirwa, Ajibu laonekana
        • Mambo bado magumu
        • Yanga inapata kona ya kwanza
        • Uwanja umeelemea kwa Yanga
        • Yanga chupuchupu tena
        • Yanga wanakoswa koswa
        • Dakika ya 15 mambo bado
        • Yanga yatanguliwa bao la mapema
        • Hiki ndicho kikosi cha Yanga kitakachoanza dhidi y...
        • Yanga yarahisishiwa kazi Kombe la Shirikisho Afrika
        • Simba hii ya Lechantre tema mate chini, Okwi motoooo!
        • Mkwera kamkalisha mtu kwa KO katika masumbwi
    • ►  April (2)
      • ►  Apr 29 (2)
    • ►  March (3)
      • ►  Mar 21 (2)
      • ►  Mar 17 (1)
    • ►  January (13)
      • ►  Jan 06 (5)
      • ►  Jan 05 (8)
  • ►  2017 (73)
    • ►  September (4)
      • ►  Sep 12 (4)
    • ►  April (7)
      • ►  Apr 13 (7)
    • ►  January (62)
      • ►  Jan 15 (9)
      • ►  Jan 13 (23)
      • ►  Jan 12 (8)
      • ►  Jan 09 (1)
      • ►  Jan 08 (8)
      • ►  Jan 06 (13)
  • ►  2016 (174)
    • ►  September (6)
      • ►  Sep 09 (6)
    • ►  August (7)
      • ►  Aug 19 (7)
    • ►  June (68)
      • ►  Jun 24 (9)
      • ►  Jun 23 (5)
      • ►  Jun 22 (8)
      • ►  Jun 15 (4)
      • ►  Jun 10 (6)
      • ►  Jun 09 (10)
      • ►  Jun 08 (9)
      • ►  Jun 03 (10)
      • ►  Jun 01 (7)
    • ►  May (53)
      • ►  May 30 (9)
      • ►  May 29 (2)
      • ►  May 28 (6)
      • ►  May 27 (10)
      • ►  May 22 (10)
      • ►  May 21 (5)
      • ►  May 20 (11)
    • ►  February (5)
      • ►  Feb 12 (5)
    • ►  January (35)
      • ►  Jan 10 (8)
      • ►  Jan 08 (12)
      • ►  Jan 07 (12)
      • ►  Jan 06 (3)
  • ►  2015 (459)
    • ►  December (3)
      • ►  Dec 10 (3)
    • ►  September (3)
      • ►  Sep 11 (3)
    • ►  August (28)
      • ►  Aug 22 (2)
      • ►  Aug 21 (4)
      • ►  Aug 19 (5)
      • ►  Aug 18 (4)
      • ►  Aug 15 (8)
      • ►  Aug 11 (3)
      • ►  Aug 03 (2)
    • ►  July (11)
      • ►  Jul 20 (4)
      • ►  Jul 11 (2)
      • ►  Jul 10 (5)
    • ►  June (26)
      • ►  Jun 26 (9)
      • ►  Jun 24 (2)
      • ►  Jun 22 (1)
      • ►  Jun 21 (4)
      • ►  Jun 17 (3)
      • ►  Jun 12 (7)
    • ►  May (25)
      • ►  May 18 (1)
      • ►  May 17 (8)
      • ►  May 15 (2)
      • ►  May 11 (4)
      • ►  May 10 (10)
    • ►  April (15)
      • ►  Apr 08 (5)
      • ►  Apr 06 (2)
      • ►  Apr 05 (1)
      • ►  Apr 03 (7)
    • ►  March (53)
      • ►  Mar 15 (6)
      • ►  Mar 09 (4)
      • ►  Mar 07 (7)
      • ►  Mar 06 (8)
      • ►  Mar 05 (7)
      • ►  Mar 04 (5)
      • ►  Mar 03 (5)
      • ►  Mar 02 (8)
      • ►  Mar 01 (3)
    • ►  February (163)
      • ►  Feb 28 (11)
      • ►  Feb 26 (9)
      • ►  Feb 25 (12)
      • ►  Feb 23 (7)
      • ►  Feb 22 (9)
      • ►  Feb 21 (3)
      • ►  Feb 20 (4)
      • ►  Feb 19 (4)
      • ►  Feb 18 (8)
      • ►  Feb 16 (6)
      • ►  Feb 15 (5)
      • ►  Feb 13 (9)
      • ►  Feb 12 (5)
      • ►  Feb 11 (3)
      • ►  Feb 09 (3)
      • ►  Feb 08 (10)
      • ►  Feb 07 (18)
      • ►  Feb 05 (6)
      • ►  Feb 04 (8)
      • ►  Feb 03 (12)
      • ►  Feb 02 (8)
      • ►  Feb 01 (3)
    • ►  January (132)
      • ►  Jan 31 (4)
      • ►  Jan 30 (14)
      • ►  Jan 28 (14)
      • ►  Jan 24 (10)
      • ►  Jan 21 (5)
      • ►  Jan 20 (6)
      • ►  Jan 18 (3)
      • ►  Jan 17 (2)
      • ►  Jan 12 (11)
      • ►  Jan 11 (4)
      • ►  Jan 10 (5)
      • ►  Jan 09 (8)
      • ►  Jan 05 (7)
      • ►  Jan 04 (17)
      • ►  Jan 03 (8)
      • ►  Jan 02 (14)
  • ►  2014 (1988)
    • ►  December (194)
      • ►  Dec 31 (4)
      • ►  Dec 30 (8)
      • ►  Dec 28 (10)
      • ►  Dec 25 (6)
      • ►  Dec 24 (5)
      • ►  Dec 23 (10)
      • ►  Dec 22 (8)
      • ►  Dec 21 (10)
      • ►  Dec 19 (20)
      • ►  Dec 18 (3)
      • ►  Dec 17 (5)
      • ►  Dec 16 (9)
      • ►  Dec 15 (3)
      • ►  Dec 14 (15)
      • ►  Dec 10 (2)
      • ►  Dec 09 (15)
      • ►  Dec 07 (9)
      • ►  Dec 06 (11)
      • ►  Dec 05 (10)
      • ►  Dec 04 (4)
      • ►  Dec 03 (2)
      • ►  Dec 02 (21)
      • ►  Dec 01 (4)
    • ►  November (112)
      • ►  Nov 30 (8)
      • ►  Nov 29 (3)
      • ►  Nov 27 (4)
      • ►  Nov 26 (11)
      • ►  Nov 11 (17)
      • ►  Nov 10 (1)
      • ►  Nov 09 (16)
      • ►  Nov 07 (6)
      • ►  Nov 06 (13)
      • ►  Nov 05 (6)
      • ►  Nov 04 (1)
      • ►  Nov 03 (13)
      • ►  Nov 02 (4)
      • ►  Nov 01 (9)
    • ►  October (184)
      • ►  Oct 31 (18)
      • ►  Oct 30 (5)
      • ►  Oct 29 (2)
      • ►  Oct 28 (3)
      • ►  Oct 27 (6)
      • ►  Oct 26 (9)
      • ►  Oct 25 (14)
      • ►  Oct 24 (6)
      • ►  Oct 23 (7)
      • ►  Oct 22 (10)
      • ►  Oct 21 (4)
      • ►  Oct 20 (15)
      • ►  Oct 18 (13)
      • ►  Oct 16 (9)
      • ►  Oct 15 (4)
      • ►  Oct 14 (7)
      • ►  Oct 13 (5)
      • ►  Oct 12 (5)
      • ►  Oct 07 (13)
      • ►  Oct 06 (4)
      • ►  Oct 05 (12)
      • ►  Oct 04 (13)
    • ►  September (222)
      • ►  Sep 29 (6)
      • ►  Sep 28 (7)
      • ►  Sep 27 (20)
      • ►  Sep 26 (1)
      • ►  Sep 25 (11)
      • ►  Sep 23 (9)
      • ►  Sep 21 (5)
      • ►  Sep 20 (9)
      • ►  Sep 19 (11)
      • ►  Sep 18 (1)
      • ►  Sep 14 (11)
      • ►  Sep 13 (12)
      • ►  Sep 12 (11)
      • ►  Sep 11 (4)
      • ►  Sep 10 (7)
      • ►  Sep 09 (11)
      • ►  Sep 08 (15)
      • ►  Sep 07 (17)
      • ►  Sep 06 (5)
      • ►  Sep 05 (11)
      • ►  Sep 04 (10)
      • ►  Sep 03 (12)
      • ►  Sep 02 (8)
      • ►  Sep 01 (8)
    • ►  August (167)
      • ►  Aug 31 (16)
      • ►  Aug 29 (9)
      • ►  Aug 28 (13)
      • ►  Aug 27 (22)
      • ►  Aug 26 (6)
      • ►  Aug 25 (16)
      • ►  Aug 24 (17)
      • ►  Aug 22 (9)
      • ►  Aug 21 (8)
      • ►  Aug 20 (1)
      • ►  Aug 17 (7)
      • ►  Aug 15 (13)
      • ►  Aug 14 (8)
      • ►  Aug 12 (3)
      • ►  Aug 04 (9)
      • ►  Aug 03 (10)
    • ►  July (81)
      • ►  Jul 23 (3)
      • ►  Jul 21 (5)
      • ►  Jul 19 (7)
      • ►  Jul 18 (11)
      • ►  Jul 17 (9)
      • ►  Jul 15 (6)
      • ►  Jul 14 (5)
      • ►  Jul 05 (8)
      • ►  Jul 04 (9)
      • ►  Jul 03 (5)
      • ►  Jul 01 (13)
    • ►  June (91)
      • ►  Jun 28 (5)
      • ►  Jun 24 (5)
      • ►  Jun 22 (8)
      • ►  Jun 20 (6)
      • ►  Jun 17 (9)
      • ►  Jun 15 (8)
      • ►  Jun 13 (5)
      • ►  Jun 12 (6)
      • ►  Jun 11 (6)
      • ►  Jun 10 (8)
      • ►  Jun 09 (6)
      • ►  Jun 06 (17)
      • ►  Jun 03 (2)
    • ►  May (70)
      • ►  May 28 (5)
      • ►  May 27 (10)
      • ►  May 16 (4)
      • ►  May 13 (10)
      • ►  May 09 (1)
      • ►  May 08 (20)
      • ►  May 06 (6)
      • ►  May 05 (3)
      • ►  May 04 (2)
      • ►  May 02 (6)
      • ►  May 01 (3)
    • ►  April (226)
      • ►  Apr 30 (5)
      • ►  Apr 29 (13)
      • ►  Apr 28 (6)
      • ►  Apr 27 (16)
      • ►  Apr 24 (12)
      • ►  Apr 23 (4)
      • ►  Apr 22 (13)
      • ►  Apr 21 (1)
      • ►  Apr 18 (4)
      • ►  Apr 17 (7)
      • ►  Apr 16 (2)
      • ►  Apr 15 (2)
      • ►  Apr 14 (11)
      • ►  Apr 13 (24)
      • ►  Apr 12 (5)
      • ►  Apr 11 (5)
      • ►  Apr 10 (8)
      • ►  Apr 09 (5)
      • ►  Apr 08 (10)
      • ►  Apr 07 (11)
      • ►  Apr 06 (14)
      • ►  Apr 05 (18)
      • ►  Apr 04 (4)
      • ►  Apr 03 (3)
      • ►  Apr 02 (9)
      • ►  Apr 01 (14)
    • ►  March (252)
      • ►  Mar 31 (2)
      • ►  Mar 30 (13)
      • ►  Mar 29 (13)
      • ►  Mar 28 (8)
      • ►  Mar 26 (6)
      • ►  Mar 25 (11)
      • ►  Mar 24 (6)
      • ►  Mar 23 (13)
      • ►  Mar 22 (9)
      • ►  Mar 20 (9)
      • ►  Mar 19 (9)
      • ►  Mar 18 (13)
      • ►  Mar 17 (6)
      • ►  Mar 16 (5)
      • ►  Mar 15 (10)
      • ►  Mar 12 (12)
      • ►  Mar 11 (9)
      • ►  Mar 10 (6)
      • ►  Mar 09 (15)
      • ►  Mar 08 (13)
      • ►  Mar 07 (2)
      • ►  Mar 06 (9)
      • ►  Mar 05 (6)
      • ►  Mar 04 (10)
      • ►  Mar 03 (9)
      • ►  Mar 02 (14)
      • ►  Mar 01 (14)
    • ►  February (204)
      • ►  Feb 27 (12)
      • ►  Feb 26 (10)
      • ►  Feb 25 (3)
      • ►  Feb 24 (10)
      • ►  Feb 23 (11)
      • ►  Feb 22 (8)
      • ►  Feb 21 (7)
      • ►  Feb 20 (5)
      • ►  Feb 19 (7)
      • ►  Feb 18 (11)
      • ►  Feb 16 (3)
      • ►  Feb 15 (11)
      • ►  Feb 14 (6)
      • ►  Feb 13 (14)
      • ►  Feb 12 (5)
      • ►  Feb 11 (7)
      • ►  Feb 10 (9)
      • ►  Feb 09 (10)
      • ►  Feb 08 (2)
      • ►  Feb 07 (15)
      • ►  Feb 06 (8)
      • ►  Feb 04 (8)
      • ►  Feb 02 (8)
      • ►  Feb 01 (14)
    • ►  January (185)
      • ►  Jan 31 (7)
      • ►  Jan 30 (11)
      • ►  Jan 29 (9)
      • ►  Jan 28 (9)
      • ►  Jan 27 (3)
      • ►  Jan 26 (8)
      • ►  Jan 25 (5)
      • ►  Jan 24 (11)
      • ►  Jan 23 (7)
      • ►  Jan 22 (4)
      • ►  Jan 21 (7)
      • ►  Jan 20 (3)
      • ►  Jan 19 (3)
      • ►  Jan 18 (12)
      • ►  Jan 17 (6)
      • ►  Jan 16 (1)
      • ►  Jan 15 (8)
      • ►  Jan 14 (12)
      • ►  Jan 13 (7)
      • ►  Jan 12 (14)
      • ►  Jan 11 (4)
      • ►  Jan 10 (2)
      • ►  Jan 09 (6)
      • ►  Jan 08 (3)
      • ►  Jan 07 (2)
      • ►  Jan 06 (7)
      • ►  Jan 03 (4)
      • ►  Jan 02 (6)
      • ►  Jan 01 (4)
  • ►  2013 (2402)
    • ►  December (166)
      • ►  Dec 30 (7)
      • ►  Dec 29 (3)
      • ►  Dec 27 (1)
      • ►  Dec 26 (8)
      • ►  Dec 25 (5)
      • ►  Dec 24 (2)
      • ►  Dec 23 (15)
      • ►  Dec 22 (8)
      • ►  Dec 21 (7)
      • ►  Dec 20 (12)
      • ►  Dec 19 (4)
      • ►  Dec 18 (9)
      • ►  Dec 17 (6)
      • ►  Dec 16 (7)
      • ►  Dec 14 (7)
      • ►  Dec 13 (8)
      • ►  Dec 12 (9)
      • ►  Dec 10 (8)
      • ►  Dec 07 (7)
      • ►  Dec 06 (9)
      • ►  Dec 05 (9)
      • ►  Dec 03 (6)
      • ►  Dec 02 (9)
    • ►  November (181)
      • ►  Nov 30 (14)
      • ►  Nov 29 (10)
      • ►  Nov 28 (5)
      • ►  Nov 27 (2)
      • ►  Nov 26 (9)
      • ►  Nov 25 (5)
      • ►  Nov 24 (1)
      • ►  Nov 23 (3)
      • ►  Nov 22 (3)
      • ►  Nov 21 (3)
      • ►  Nov 20 (8)
      • ►  Nov 18 (6)
      • ►  Nov 16 (9)
      • ►  Nov 15 (2)
      • ►  Nov 13 (3)
      • ►  Nov 12 (5)
      • ►  Nov 11 (7)
      • ►  Nov 10 (18)
      • ►  Nov 09 (18)
      • ►  Nov 07 (4)
      • ►  Nov 06 (9)
      • ►  Nov 05 (13)
      • ►  Nov 04 (7)
      • ►  Nov 03 (12)
      • ►  Nov 02 (1)
      • ►  Nov 01 (4)
    • ►  October (190)
      • ►  Oct 31 (10)
      • ►  Oct 30 (4)
      • ►  Oct 29 (2)
      • ►  Oct 28 (6)
      • ►  Oct 25 (5)
      • ►  Oct 24 (3)
      • ►  Oct 23 (3)
      • ►  Oct 22 (12)
      • ►  Oct 21 (7)
      • ►  Oct 20 (12)
      • ►  Oct 19 (11)
      • ►  Oct 18 (4)
      • ►  Oct 17 (1)
      • ►  Oct 16 (6)
      • ►  Oct 15 (16)
      • ►  Oct 14 (4)
      • ►  Oct 13 (6)
      • ►  Oct 12 (8)
      • ►  Oct 11 (2)
      • ►  Oct 10 (6)
      • ►  Oct 09 (6)
      • ►  Oct 08 (3)
      • ►  Oct 07 (7)
      • ►  Oct 06 (9)
      • ►  Oct 05 (11)
      • ►  Oct 04 (11)
      • ►  Oct 03 (7)
      • ►  Oct 02 (1)
      • ►  Oct 01 (7)
    • ►  September (204)
      • ►  Sep 30 (8)
      • ►  Sep 28 (8)
      • ►  Sep 27 (4)
      • ►  Sep 26 (16)
      • ►  Sep 25 (7)
      • ►  Sep 24 (12)
      • ►  Sep 23 (9)
      • ►  Sep 22 (11)
      • ►  Sep 21 (9)
      • ►  Sep 20 (9)
      • ►  Sep 19 (7)
      • ►  Sep 18 (2)
      • ►  Sep 17 (8)
      • ►  Sep 16 (7)
      • ►  Sep 15 (10)
      • ►  Sep 13 (20)
      • ►  Sep 12 (2)
      • ►  Sep 11 (6)
      • ►  Sep 10 (6)
      • ►  Sep 09 (2)
      • ►  Sep 08 (2)
      • ►  Sep 07 (2)
      • ►  Sep 06 (13)
      • ►  Sep 04 (1)
      • ►  Sep 03 (8)
      • ►  Sep 02 (6)
      • ►  Sep 01 (9)
    • ►  August (241)
      • ►  Aug 30 (4)
      • ►  Aug 29 (15)
      • ►  Aug 28 (6)
      • ►  Aug 27 (4)
      • ►  Aug 26 (7)
      • ►  Aug 25 (6)
      • ►  Aug 24 (3)
      • ►  Aug 23 (9)
      • ►  Aug 21 (10)
      • ►  Aug 20 (8)
      • ►  Aug 19 (9)
      • ►  Aug 17 (11)
      • ►  Aug 16 (9)
      • ►  Aug 15 (8)
      • ►  Aug 14 (6)
      • ►  Aug 13 (7)
      • ►  Aug 12 (4)
      • ►  Aug 11 (17)
      • ►  Aug 10 (11)
      • ►  Aug 09 (5)
      • ►  Aug 08 (9)
      • ►  Aug 07 (7)
      • ►  Aug 06 (9)
      • ►  Aug 05 (16)
      • ►  Aug 04 (11)
      • ►  Aug 03 (6)
      • ►  Aug 02 (18)
      • ►  Aug 01 (6)
    • ►  July (315)
      • ►  Jul 30 (8)
      • ►  Jul 29 (6)
      • ►  Jul 28 (11)
      • ►  Jul 27 (13)
      • ►  Jul 26 (9)
      • ►  Jul 25 (10)
      • ►  Jul 24 (12)
      • ►  Jul 23 (10)
      • ►  Jul 22 (13)
      • ►  Jul 21 (8)
      • ►  Jul 19 (10)
      • ►  Jul 18 (10)
      • ►  Jul 17 (13)
      • ►  Jul 16 (11)
      • ►  Jul 15 (13)
      • ►  Jul 14 (15)
      • ►  Jul 13 (7)
      • ►  Jul 12 (3)
      • ►  Jul 11 (16)
      • ►  Jul 10 (12)
      • ►  Jul 09 (15)
      • ►  Jul 08 (15)
      • ►  Jul 07 (8)
      • ►  Jul 06 (16)
      • ►  Jul 05 (6)
      • ►  Jul 04 (7)
      • ►  Jul 03 (10)
      • ►  Jul 02 (16)
      • ►  Jul 01 (12)
    • ►  June (253)
      • ►  Jun 30 (10)
      • ►  Jun 29 (5)
      • ►  Jun 28 (11)
      • ►  Jun 27 (14)
      • ►  Jun 26 (10)
      • ►  Jun 25 (14)
      • ►  Jun 24 (8)
      • ►  Jun 23 (10)
      • ►  Jun 21 (11)
      • ►  Jun 20 (8)
      • ►  Jun 19 (5)
      • ►  Jun 18 (9)
      • ►  Jun 17 (12)
      • ►  Jun 16 (10)
      • ►  Jun 15 (4)
      • ►  Jun 14 (12)
      • ►  Jun 13 (10)
      • ►  Jun 12 (10)
      • ►  Jun 11 (7)
      • ►  Jun 10 (17)
      • ►  Jun 08 (7)
      • ►  Jun 07 (8)
      • ►  Jun 06 (12)
      • ►  Jun 05 (7)
      • ►  Jun 03 (8)
      • ►  Jun 02 (10)
      • ►  Jun 01 (4)
    • ►  May (235)
      • ►  May 31 (8)
      • ►  May 30 (10)
      • ►  May 29 (3)
      • ►  May 28 (8)
      • ►  May 27 (4)
      • ►  May 26 (10)
      • ►  May 25 (2)
      • ►  May 24 (12)
      • ►  May 23 (9)
      • ►  May 22 (10)
      • ►  May 21 (14)
      • ►  May 20 (7)
      • ►  May 19 (4)
      • ►  May 18 (12)
      • ►  May 17 (7)
      • ►  May 16 (9)
      • ►  May 15 (5)
      • ►  May 14 (8)
      • ►  May 12 (8)
      • ►  May 11 (3)
      • ►  May 10 (6)
      • ►  May 09 (9)
      • ►  May 08 (10)
      • ►  May 07 (11)
      • ►  May 06 (13)
      • ►  May 04 (5)
      • ►  May 03 (12)
      • ►  May 02 (8)
      • ►  May 01 (8)
    • ►  April (183)
      • ►  Apr 30 (7)
      • ►  Apr 27 (9)
      • ►  Apr 25 (10)
      • ►  Apr 24 (8)
      • ►  Apr 23 (8)
      • ►  Apr 22 (12)
      • ►  Apr 21 (6)
      • ►  Apr 20 (2)
      • ►  Apr 19 (10)
      • ►  Apr 18 (7)
      • ►  Apr 17 (8)
      • ►  Apr 16 (13)
      • ►  Apr 15 (2)
      • ►  Apr 14 (5)
      • ►  Apr 13 (3)
      • ►  Apr 12 (7)
      • ►  Apr 11 (8)
      • ►  Apr 10 (7)
      • ►  Apr 09 (8)
      • ►  Apr 07 (3)
      • ►  Apr 06 (4)
      • ►  Apr 05 (2)
      • ►  Apr 04 (6)
      • ►  Apr 03 (10)
      • ►  Apr 02 (6)
      • ►  Apr 01 (12)
    • ►  March (195)
      • ►  Mar 31 (3)
      • ►  Mar 30 (9)
      • ►  Mar 29 (6)
      • ►  Mar 28 (3)
      • ►  Mar 27 (4)
      • ►  Mar 25 (10)
      • ►  Mar 22 (2)
      • ►  Mar 21 (10)
      • ►  Mar 20 (8)
      • ►  Mar 19 (10)
      • ►  Mar 18 (11)
      • ►  Mar 17 (9)
      • ►  Mar 16 (10)
      • ►  Mar 15 (12)
      • ►  Mar 14 (6)
      • ►  Mar 13 (4)
      • ►  Mar 12 (9)
      • ►  Mar 11 (4)
      • ►  Mar 10 (7)
      • ►  Mar 09 (3)
      • ►  Mar 08 (12)
      • ►  Mar 07 (7)
      • ►  Mar 06 (1)
      • ►  Mar 05 (5)
      • ►  Mar 04 (10)
      • ►  Mar 02 (7)
      • ►  Mar 01 (13)
    • ►  February (140)
      • ►  Feb 28 (4)
      • ►  Feb 27 (7)
      • ►  Feb 26 (10)
      • ►  Feb 25 (6)
      • ►  Feb 24 (5)
      • ►  Feb 23 (11)
      • ►  Feb 22 (8)
      • ►  Feb 21 (2)
      • ►  Feb 20 (1)
      • ►  Feb 18 (5)
      • ►  Feb 16 (10)
      • ►  Feb 15 (14)
      • ►  Feb 14 (1)
      • ►  Feb 13 (6)
      • ►  Feb 12 (10)
      • ►  Feb 11 (6)
      • ►  Feb 09 (8)
      • ►  Feb 05 (6)
      • ►  Feb 01 (20)
    • ►  January (99)
      • ►  Jan 31 (7)
      • ►  Jan 30 (12)
      • ►  Jan 24 (6)
      • ►  Jan 23 (8)
      • ►  Jan 18 (10)
      • ►  Jan 16 (5)
      • ►  Jan 15 (4)
      • ►  Jan 13 (6)
      • ►  Jan 12 (8)
      • ►  Jan 09 (8)
      • ►  Jan 08 (3)
      • ►  Jan 07 (7)
      • ►  Jan 05 (3)
      • ►  Jan 03 (7)
      • ►  Jan 01 (5)
  • ►  2012 (411)
    • ►  December (51)
      • ►  Dec 31 (9)
      • ►  Dec 29 (8)
      • ►  Dec 20 (3)
      • ►  Dec 19 (8)
      • ►  Dec 11 (5)
      • ►  Dec 10 (4)
      • ►  Dec 05 (5)
      • ►  Dec 04 (3)
      • ►  Dec 01 (6)
    • ►  November (48)
      • ►  Nov 29 (11)
      • ►  Nov 28 (10)
      • ►  Nov 27 (11)
      • ►  Nov 19 (10)
      • ►  Nov 17 (1)
      • ►  Nov 10 (5)
    • ►  October (23)
      • ►  Oct 29 (10)
      • ►  Oct 15 (3)
      • ►  Oct 14 (6)
      • ►  Oct 13 (4)
    • ►  September (94)
      • ►  Sep 30 (4)
      • ►  Sep 29 (8)
      • ►  Sep 28 (16)
      • ►  Sep 27 (3)
      • ►  Sep 26 (6)
      • ►  Sep 24 (7)
      • ►  Sep 22 (6)
      • ►  Sep 21 (12)
      • ►  Sep 20 (10)
      • ►  Sep 19 (8)
      • ►  Sep 17 (6)
      • ►  Sep 11 (3)
      • ►  Sep 05 (5)
    • ►  August (37)
      • ►  Aug 13 (1)
      • ►  Aug 12 (5)
      • ►  Aug 11 (10)
      • ►  Aug 08 (5)
      • ►  Aug 04 (2)
      • ►  Aug 03 (4)
      • ►  Aug 02 (5)
      • ►  Aug 01 (5)
    • ►  July (24)
      • ►  Jul 30 (9)
      • ►  Jul 29 (5)
      • ►  Jul 02 (2)
      • ►  Jul 01 (8)
    • ►  June (42)
      • ►  Jun 25 (5)
      • ►  Jun 19 (3)
      • ►  Jun 08 (1)
      • ►  Jun 07 (5)
      • ►  Jun 06 (8)
      • ►  Jun 04 (7)
      • ►  Jun 02 (3)
      • ►  Jun 01 (10)
    • ►  May (51)
      • ►  May 28 (5)
      • ►  May 25 (9)
      • ►  May 23 (5)
      • ►  May 22 (11)
      • ►  May 21 (9)
      • ►  May 19 (5)
      • ►  May 17 (7)
    • ►  April (15)
      • ►  Apr 20 (3)
      • ►  Apr 19 (8)
      • ►  Apr 07 (4)
    • ►  January (26)
      • ►  Jan 19 (3)
      • ►  Jan 18 (11)
      • ►  Jan 10 (3)
      • ►  Jan 06 (9)
  • ►  2011 (191)
    • ►  December (25)
      • ►  Dec 30 (12)
      • ►  Dec 27 (7)
      • ►  Dec 02 (6)
    • ►  November (17)
      • ►  Nov 18 (6)
      • ►  Nov 12 (11)
    • ►  October (6)
      • ►  Oct 20 (6)
    • ►  September (20)
      • ►  Sep 30 (11)
      • ►  Sep 26 (5)
      • ►  Sep 21 (1)
      • ►  Sep 13 (3)
    • ►  August (13)
      • ►  Aug 28 (2)
      • ►  Aug 27 (6)
      • ►  Aug 08 (5)
    • ►  July (30)
      • ►  Jul 31 (9)
      • ►  Jul 30 (1)
      • ►  Jul 27 (6)
      • ►  Jul 16 (1)
      • ►  Jul 15 (7)
      • ►  Jul 14 (4)
      • ►  Jul 09 (2)
    • ►  June (13)
      • ►  Jun 29 (1)
      • ►  Jun 26 (10)
      • ►  Jun 25 (2)
    • ►  April (23)
      • ►  Apr 25 (6)
      • ►  Apr 15 (17)
    • ►  March (20)
      • ►  Mar 12 (6)
      • ►  Mar 08 (3)
      • ►  Mar 04 (3)
      • ►  Mar 03 (6)
      • ►  Mar 02 (2)
    • ►  February (24)
      • ►  Feb 28 (2)
      • ►  Feb 26 (3)
      • ►  Feb 25 (3)
      • ►  Feb 24 (1)
      • ►  Feb 22 (3)
      • ►  Feb 19 (2)
      • ►  Feb 15 (1)
      • ►  Feb 12 (3)
      • ►  Feb 11 (1)
      • ►  Feb 04 (5)
  • ►  2010 (72)
    • ►  December (24)
      • ►  Dec 18 (3)
      • ►  Dec 16 (3)
      • ►  Dec 13 (2)
      • ►  Dec 10 (8)
      • ►  Dec 06 (6)
      • ►  Dec 05 (2)
    • ►  September (10)
      • ►  Sep 29 (3)
      • ►  Sep 23 (1)
      • ►  Sep 17 (2)
      • ►  Sep 10 (1)
      • ►  Sep 06 (1)
      • ►  Sep 05 (2)
    • ►  August (10)
      • ►  Aug 23 (4)
      • ►  Aug 22 (2)
      • ►  Aug 20 (1)
      • ►  Aug 03 (3)
    • ►  July (28)
      • ►  Jul 27 (5)
      • ►  Jul 23 (1)
      • ►  Jul 19 (15)
      • ►  Jul 10 (1)
      • ►  Jul 09 (2)
      • ►  Jul 07 (4)

BLOGS NYINGINE

  • HABARI MSETO BLOG
    PSSSF KUTOA HUDUMA, ELIMU MAONESHO YA NANENANE 2026 KATIKA KANDA TANO - AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw.Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenan...
    2 hours ago
  • BBCSwahili.com | Habari
    Trump afungua mlango wa mazungumzo na Iran - Iran bado haijatoa jibu kwa matamshi ya Trump. Trump amekuwa akisisitiza mara kwa mara kwamba mwisho wa vita kupitia mazungumzo uko karibu kufikiwa, lakini...
    5 hours ago
  • LENZI YA MICHEZO
    SERIKALI YAIWEKEA NGUVU SEKTA YA USALAMA, YAZINDUA MIRADI YA BILIONI 2.8 SONGWE - Serikali imeeleza kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kuimarisha vyombo vya ulinzi na usalama nchini kupitia utekelezaji wa maboresho makubwa ya ...
    19 hours ago
  • BIN ZUBEIRY
    YANGA SC YASAJILI CHIPUKIZI MWINGINE, NI HUSSEIN MIHAMBO WA MASHUJAA FC - KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji chipukizi, Hussein Juma Mihambo (19) kutoka Mashujaa FC kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao. Anakuwa mc...
    1 week ago
  • Mwanaspotimwanzo
    Kisa Simba, Yanga yamsimamisha mwanasheria wao - Simon alikaimu nafasi hiyo baada ya David Ruhago kufurushiwa virago.
    5 years ago
  • Mwananchimwanzo
    Magufuli awatuliza wabunge nafasi za uwaziri - Amesema hakuna haraka ya kuteua mawaziri kwa kuwa wengi wana sifa
    5 years ago
  • MLEKANI NEWS
    TAKUKURU Kubaini Mamluki Michezo Mei Mosi 2020 - *Wajumbe wa Kamati ya Michezo ya mashindano ya Mei Mosi wakiwa kwenye kikao cha Kwanza cha maandalizi ya michezo hiyo kilichofanyika mwishoni mwa wiki k...
    6 years ago
  • Burudan Mwanzo - Mwisho
    BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...
    6 years ago
  • Ustream Live Shows
    Wolf River Cam-New London - Wolf River Cam's New London location. See walleye, sturgeon, bass and many more types of fish. Viewers: 645,527
    7 years ago
  • Mzuka wa Fungo
    MSANII DIAMOND AZINDUA WIMBO WA COLOURS KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI - Cathbert Kajuna To:amichuzi,othmanmichuzi,MUHIDIN MICHUZI,Geofrey Adroph Bcc:fungoomar@yahoo.com May 15 at 6:00 AM Msanii Diamond akipagawisha mashabiki wa...
    8 years ago
  • Shaffih Dauda
    Kisa cha familia yenye “mkosi” zaidi katika soka, habari yao inasikitisha - Nou Camp ni kati ya sehemu ambayo kila mpenda soka angetamani kufiki, kwani nani asiyependa kumuona Messi na nani asiyependa kuona pasi nzuri zikipigwa na ...
    8 years ago
  • MASAI NYOTAMBOFU
    YALIYOJIRI: WATATU WABURUZWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUBEBA MABANGO YAKUMKASHIFU MH RAIS MAGUFULI - Jana wafuasi wa UKAWA walitiwa mbaroni baada ya kutoke mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe wa kumkashifu Mtukufu Mkuu san...
    10 years ago
  • ELIMU KWANZA TANZANIA
    Airtel yakabidhi Sh Mil 5 Tuzo za Mwanamakuka 2014 - Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi Mwenyekiti UWF na Mratibu wa Mradi wa Tuzo za Mwanamakuka Maryam Shamo wakati ...
    12 years ago
  • Soccerway.com
    -

FOLLOWERS

About Me

Unknown
View my complete profile

ZILIZOSOMWA SANA

  • Real Madrid 'yaua' Ulaya, Borrusia Dotmund yabanwa
  • Messi aichanganya Argentina adhabu ya FIFA
  • Viongozi DRFA warejea tena DRFA
Web Counter
WALIOTEMBELEA MPAKA SASA
Flag Counter

Tuliza akili zako kwa Game

BIASHARA NI MATANGAZO

WASILIANA NASI KWA MATANGAZO AU HABARI KUPITIA 0713-229787 au 0683-229787 ama email: kimwagaboy@yahoo.co.uk au wakuzataboy@yahoo.com
MICHARAZO MITUPU By BADRU KIMWAGA. Watermark theme. Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.